Sababu zinazonifanya nisimpende Mungu

Sababu zinazonifanya nisimpende Mungu

4 Mnafanya dhihaka yenu juu ya nani? Mmepanua vinywa vyenu, na kutoa ndimi zenu? Je, ninyi si wana wa uasi, uzao wa uongo;

Isaya 57 :4

10 Ulikuwa umechoka kwa ajili ya urefu wa njia yako; lakini hukusema, Hapana matumaini; ulipata kuhuishwa nguvu zako; kwa sababu hiyo hukuugua.

Isaya 57 :10

11 Tena ni nani uliyemwogopa na kumhofu, hata ukasema uongo, wala hukunikumbuka mimi, wala kuweka hayo moyoni? Je! Mimi sikunyamaza tangu zamani, hata huniogopi?

Isaya 57 :11

12 Mimi nitatangaza haki yako, na matendo yako hayatakufaa.

Isaya 57 :12

13 Utakapolia, na wakuponye hao uliowakusanya; lakini upepo utawachukua; uvuvio tu utawachukulia mbali; lakini yeye anayenitumaini ataimiliki nchi, na kuurithi mlima wangu mtakatifu.

Isaya 57 :13

15 Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.

Isaya 57 :15

16 Kwa kuwa sitashindana na watu siku zote, wala sitakuwa na hasira siku zote; maana roho ingezimia mbele zangu, na hizo nafsi nilizozifanya.

Isaya 57 :16

17 Kwa sababu ya uovu wa kutamani kwake naliona hasira, nikampiga; nalificha uso wangu, nikaona ghadhabu; naye akaendelea kwa ukaidi, kuifuata njia ya moyo wake mwenyewe.

Isaya 57 :17

18 Nimeziona njia zake; nami nitamponya; nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia.

Isaya 57 :18

19 Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema Bwana; nami nitamponya.

Isaya 57 :19

20 Bali wabaya wanafanana na bahari iliyochafuka; maana haiwezi kutulia, na maji yake hutoa tope na takataka.

Isaya 57 :20

21 Hapana amani kwa wabaya; asema Mungu wangu.

Isaya 57 :21
 
Kama unasema hakuna aliyewahi kumwona wala kumjua Mungu, ni kwa nini watu wanamwabudu Mungu?
Kwani ibada ni nini Mkuu?

Kwa ufupi ibada ni kushika kanuni za asili ambazo kwazo ninaweza kuziita ndizo amri za Mungu.

Kuabudu sio kwenda kupoteza muda kanisani au misikitini. Sio kutoa Sadaka au Zaka kama watu wasemavyo. Kuabudu ni kushika kanuni za asili.

Kitabu cha Bibilia kilizingatia sana kanuni hizo. Hata waliokiandika walizizingatia sana. Mtu yeyote anayefuatana na nguvu ya asili lazima aonekane ananguvu na chanzo cha maarifa yote.

Kanuni zinazokufanya uishi ndio ibada. Kwa mfano kufanya kazi Kwa bidii. Kupumzika, Kula chakula Bora, kuwapenda wengine, kutunza mazingira n.k. ndio ibada.

Watu hudhani kwenda kanisani ndio kumjua Mungu lakini ni tofauti na hivyo.

Mungu anainekana kupitia nguvu ya asili, kazi na nguvu zake zinazihirishwa kupitia viumbe waonekanao na wasioonekana.

Mungu hajawahi kuonekana popote pale kwani Mungu yupo mahali pote Kwa ukamilifu wake. Mungu ni timeless yaani halimitiwi na wakati. Anaishi milele tangu milele. Mungu hana kesho wala Jana wenye Jana na kesho ni baadhi ya viumbe kama wanadamu ambao wanahesabu siku kutokana na uwepo wa Mianga yaani jua na mwezi.

Unahitaji kufikiri Kwa njia elfu moja katika ishu hizi. Vinginevyo utaishia kupotea katika mashaka yako Kwa kusema hakuna Mungu. Pia usikubali kupelekwa pelekwa na Watu wanaokutisha Kwa kuhoji. Sema katika kuhoji unapaswa uhoji kama mtu mwenye akili na si kama mtu aliyechanganyikiwa
 
Hapa umefanya Zambi mbili kwa mkupuo..

1.kumdhihaki mungu na kumdharau

2.umejaribu kushawishi watu wawe na mawazo kama yako.

Ushauri.....

Nenda kanisani ongea na mchungaji wako au s
Msikitini kwa shekh wako, upewe ushauri wa kisaikolojia
 
Duh! hivi vitu ndo vinachanganya zaidi. So what if uyo Sub God ndo akawa chanzo cha mafundisho hayo ya Jehanamu, shetani n.k , sisi binadamu sasa tunapaswa kuobey au tuishi tupendavyo. Just want to know your thoughts.
Wel,kama umeangalia vzur nmesema sub creations,sio sub God,..yan nkimaanisha uumbaji mdogo mdogo ,.na YES,huyu sub god(in a way ili uelewe vzur)ambaye ni bnadam,ni sisi inshort,.na ndio tunaoandika hiv vitab etc bible,quran etc,tuna introduce dini mbalimbali na madheheb,tunafanya fumbuzi mbali mbali za kisayansi kwa level yetu lakin n sio mbaya,hata the great creator mwenyew anajua kua i made these people to do wonders,sasa watu wanaofaham hii knowledge wanaifanya siri,na ule usem wa tumuumbe mtu kwa mfano wetu ni kwel,binadam akija jitambua yeye nan ,anakua na uwezo wa ki mungu kabsa,ingawa hawez mfikia the great creator,ndo maana ya kuumbwa kwa mfano wetu hyo,so bado bnadam hajajijua uwezo wake ila kadiri siku ziendavyo anajitambua,ndomana unaona kila siku mambo mapya yanavumbuliwa,technology etc,.mwanadam hutafuta na huchokonoa vtu ili apate mjua huyu great creator so results za hii jitihada ya kutafta ndo znatokea tafsiri nyiingi kuhusu huyu great creator,ndomana wachina wanatafsiri yao,wahindi wana yao,muslim wana yao,christians wana yao etc,..na vitabu hiv vinavyoitwa vitakatifu vmeandikwa na wanadam katka kutafta kuujua ukweli,so kuna stori nyingne za kwenye hiv vitab ni kwel na nyingne si kwel,ila ambazo si kwel ni nyiingi kuliko za kweli.yan vtab hiv hudokeza tuu,..mfano kimaandiko meng ilijulikana jua ndio inazunguka dunia bt si kweli,mfano tuu..historia ya mwanadam,hapa ndo kuna upotoshwaj mkubwa,kila race inajivutia upande wake,.ukienda kwa wachina watakwambia mungu ni mchina,wahind watakwambia mungu ni muhind,wazungu wanakuja na yao nao kua mungu ni mweupe kama wao etc,so stor hiz,kimaandiko dunia ina umri wa miaka 6000,..bt si kweli,..kitaalamu na kwa vithibitisho dunia ina aproximately miaka bil4.5,na hii ni proven,sio hypothesis..so mambo kama hayo..the great creator aliumba vitu ki sayansi,vika develope,mfano anaumba cell ina develope into tissue,organs had mmea kamili,ndomana wana sayans waki trace back uumbaji huja na majibu hayo kua viumbe vili develope frm one stage to another,ni vile vile kwenye vtu visivyo viumbe hai,mfano,maji,ni element moja na nyingne,ndio hvyo mungu/great creator aliumba,sayans yake si ya kitoto,ni sayans isiyoelezeka kwa urahis,na aliumba vtu to its best,yan sawia kabsa,..mfano naweza diriki sema the great creator aliumba dunia maalum kwa sis kuish,yan aliiumba to the best/maximum quality,..ila sis tunaendelea kufanya hiz sub creations na by our own will,wala haingilii yeye,so ukiona sjui mtoto anazaliwa kilema,or vifo or ajali or chochote,yeye hahusiki,ni sisi tunahusika,ni uumbaji wetu sis unaofanya haya so lawama ni yetu sis sio yake.yeye alishamalizaga zamaani..tena tambua,tusidhan sis na dunia yetu peke yetu ndo the only thing the great creator amefanya,..kuna vitu vikubwa zaaidi huko,kwenye galaxies na sayar nyingne ambazo ufaham wetu na sayans bado hazija fanikiwa kujua,so great creator anafanya huuge projects n hana mda wala haja et ya kuumba/kutengeneza dunia af awauwe na kuwachoma watu moto,hiz ni fikra na roho za kibinadam ndo znaandika mafundisho haya,creator hana akil za kibinadam,he is way past that..et akuskilizie utende dhambi kimtego mtego af aje akuchome moto,hzo ni fikra za bnadam tuu.
 
Sijaandika haya kwa nia ya kumdhihaki Mungu ila tu najarib kujua ukweli kuhusu yeye. Sina shida kuhusu uamuzi wa kutubu dhambi na kuokoka, ila tu kuna vitu kuhusu yeye inabidi nivijue, huenda nitaokoka. Coz mm kiukweli ni mtenda dhambi lyk I recklessly meddle with sin, hlf Nina moyo mgumu kweli ila I hope in the future nitapata majibu ya haya maswali enoah
Mungu ni mwema atakuokoa na utatoa ushuuda juu ya Wema wake na upendo wake kwako ukiijua kweli itakuweka huru nawe utakuwa huru kweli kweli, tatizo liko kwenye kukosa maarifa na kutokulijua neno,NEEMA ya Mungu na ishuke kwako kuijua kweli yake
 
Kwa Mara ya kwanza kusoma tred ya demons humu,hata humu kumbe mpoo?tubu siku zako za wisho zaja,
 
Kwani ibada ni nini Mkuu?

Kwa ufupi ibada ni kushika kanuni za asili ambazo kwazo ninaweza kuziita ndizo amri za Mungu.

Kuabudu sio kwenda kupoteza muda kanisani au misikitini. Sio kutoa Sadaka au Zaka kama watu wasemavyo. Kuabudu ni kushika kanuni za asili.

Kitabu cha Bibilia kilizingatia sana kanuni hizo. Hata waliokiandika walizizingatia sana. Mtu yeyote anayefuatana na nguvu ya asili lazima aonekane ananguvu na chanzo cha maarifa yote.

Kanuni zinazokufanya uishi ndio ibada. Kwa mfano kufanya kazi Kwa bidii. Kupumzika, Kula chakula Bora, kuwapenda wengine, kutunza mazingira n.k. ndio ibada.

Watu hudhani kwenda kanisani ndio kumjua Mungu lakini ni tofauti na hivyo.

Mungu anainekana kupitia nguvu ya asili, kazi na nguvu zake zinazihirishwa kupitia viumbe waonekanao na wasioonekana.

Mungu hajawahi kuonekana popote pale kwani Mungu yupo mahali pote Kwa ukamilifu wake. Mungu ni timeless yaani halimitiwi na wakati. Anaishi milele tangu milele. Mungu hana kesho wala Jana wenye Jana na kesho ni baadhi ya viumbe kama wanadamu ambao wanahesabu siku kutokana na uwepo wa Mianga yaani jua na mwezi.

Unahitaji kufikiri Kwa njia elfu moja katika ishu hizi. Vinginevyo utaishia kupotea katika mashaka yako Kwa kusema hakuna Mungu. Pia usikubali kupelekwa pelekwa na Watu wanaokutisha Kwa kuhoji. Sema katika kuhoji unapaswa uhoji kama mtu mwenye akili na si kama mtu aliyechanganyikiwa
Labda nikuulize tena.........Kwa kuwa umesema hakuna anayemjua wala kuwahi kumwona Mungu, je idea ya uwepo wa Mungu iliingiaje kwenye fikra za watu?
 
Inaonekana uko stressed muda huu (point yako ya sita) as if kuna jambo baya umefanya,linakuumiza,unalijutia

Kama iko hivyo kweli ni heri ukatubu kwa imani yako na kuamini sisi binadamu hakuna mkamilifu,wote tunamkosea Mungu

Kwa imani yangu nafahamu Mungu ni pendo na huwa hakusudii baya lolote litutokee
Sasa kama humpendi yeye manake hata ndani yako hakuna upendo

USHAURI
Usipende kumuongelea Mungu kiboya boya kama unawongelea wachumba zako huko

Hayo maswali # 1,2&3 nimeshindwa kuyajibu kwasababu sipo into dini kabisa
Leo nimekutana na pepo live huku,jamaa atambui uwepo wa mungu.
 
Adam hakujaribiwa na Shetani. Shetani angemfata Adam kuhusu kula lile tunda adamu angekataa. Akaona njia rahisi ni kumfuata Eva
 
Mkuu okoyoko Dunia ina mema na mabaya na kumejaa vitu vingi vya kuumiza,,,Ondoa wazo la ubaya kwa Mwenyezi na tafuta furaha katika maisha na ufurahi,,,Mimi mwenyewe huwa nina maswali mengi sana na huwa Sipendi yanipeleke mbali,,hakuna asie na dhambi...wengine tuna dhambi nyingi ila nipatapo mda na nikiwa na amani huwa Naenda church nivute hata hewa ya mle ndani tu.MUNGU anasema anawajua walio wake toka kuwekwa misingi ya ulimwengu,,,na kwa kuwa ni wake atawapick tu hata wakiwa guest,,bar au kwenye brothel,,,ndo maana wenye dhambi wengi wataona mwanga mwishoni na kutubu kama yule mwizi msalabani.Ishi maisha kwa kuyafurahia ukijua kila Siku imetoka kwa Mwenyezi nae ni mwingi wa rehema...Jisamehe nafsi yako na Mwombe MUNGU akupe ujasiri wa kumkaribia na kumshukuru maana hata yeye anajua sisi ni dhaifu na wenye kuhitaji msaada wake.
 
Labda nikuulize tena.........Kwa kuwa umesema hakuna anayemjua wala kuwahi kumwona Mungu, je idea ya uwepo wa Mungu iliingiaje kwenye fikra za watu?

Swali zuri Mkuu

Dhana ya kuwepo Kwa Mungu ni dhana kongwe iliyopitia misukosuko mingi.

Zipo njia mbalimbali ambazo ziliweza kuibua uwepo wa dhana ya uwepo wa Mungu.
Moja, Hadithi hasa Visakale ndio njia ambayo inatumiwa mpaka Leo. Musa kama Musa ambaye ni miongoni mwa Malegend wa imani za uwepo wa Mungu alipokea masimulizi(Visakale) vya mababu zake kabla hata hajafukuzwa Kwa farao.
Hivyo idea ya Mungu iliweza kurithishwa toka kizazi mpaka kizazi Kwa masimulizi.

Mbili, Maono na ndoto.
Wapo watu ambao waliweza kuona Maono ambayo mengine yalitoka Kwa Mungu(japo hakuna uthibitisho) ambao ndio walizidi kuboresha Yale masimulizi ya uwepo wa Mungu.

Hivyo ni kusema idea ya uwepo wa Mungu ilikuwepo kutokana na uhusiano uliokuwepo baina ya falme ya Binadamu na falme ya mbinguni. Ikumbukwe kuwa Malaika ni miongoni mwa Jamii za viumbe zinavyofanana na Wanadamu. Hivyo ni kusema palikuwa na ushirikiano baina ya pande hizi mbili. Malaika ni ngazi ya juu baada ya binadamu.

Shika kwenye akili yako hakuna kiumbe kilichowahi kumuona Mungu
 
Be careful my brother. No kweli jehanam aliumbiwa shetani kwa sababu ya uasi. Wafanyao uasi watashiriki hukumu na shetani. Tofauti ya binadamu na viumbe vingine ni utashi(reasoning).Hii ndiyo inakufanya umchukie Mungu, uone hayuko responsible.Utashi unampa binadamu fursa ya kuchagua. Mungu si dikteta. Hats mama Mungu anajua mahitaji yetu, anapenda tumwombe kwa kujenga hoja pia husamehe kwa ajili take mwenyewe I say a 43:25-26.
Mungu ameumba kwa kusudi lake. Ni kama vile seremala anavyotengeneza samani kwa mahitaji take, meza, kiti. Vinavyotengenezwa havina amri ya kutaka vitengenezwe vipi.
Mungu Ana Tabia ya wivu
 
Swali zuri Mkuu

Dhana ya kuwepo Kwa Mungu ni dhana kongwe iliyopitia misukosuko mingi.

Zipo njia mbalimbali ambazo ziliweza kuibua uwepo wa dhana ya uwepo wa Mungu.
Moja, Hadithi hasa Visakale ndio njia ambayo inatumiwa mpaka Leo. Musa kama Musa ambaye ni miongoni mwa Malegend wa imani za uwepo wa Mungu alipokea masimulizi(Visakale) vya mababu zake kabla hata hajafukuzwa Kwa farao.
Hivyo idea ya Mungu iliweza kurithishwa toka kizazi mpaka kizazi Kwa masimulizi.

Mbili, Maono na ndoto.
Wapo watu ambao waliweza kuona Maono ambayo mengine yalitoka Kwa Mungu(japo hakuna uthibitisho) ambao ndio walizidi kuboresha Yale masimulizi ya uwepo wa Mungu.

Hivyo ni kusema idea ya uwepo wa Mungu ilikuwepo kutokana na uhusiano uliokuwepo baina ya falme ya Binadamu na falme ya mbinguni. Ikumbukwe kuwa Malaika ni miongoni mwa Jamii za viumbe zinavyofanana na Wanadamu. Hivyo ni kusema palikuwa na ushirikiano baina ya pande hizi mbili. Malaika ni ngazi ya juu baada ya binadamu.

Shika kwenye akili yako hakuna kiumbe kilichowahi kumuona Mungu
Dhana nzima ni hallucination tupu.
 
Kuna maswali mengi kuhusu Mungu huwa najiuliza, mpaka SAA nyingine huwa namkasirikia Mungu (maybe nakufuru lakini acha iwe hivyo).Bcoz kwa ninavomuwazia Mungu ingekuwa ni heri nisingezaliwa.

1) Kama kweli Mungu ni upendo, kwanini aumbe jehanamu ya kutuchoma milele sisi tulio waovu (lyk for billions and trillions of years). Si heri angetumaliza tu kuliko kututesa milele? Kwenye shuhuda nyingine wakristo huenda motoni kwa dhambi moja tu ambayo hawakutubu. (I know hell was originally intended for the devil and his demons & not 4 humans)

2) Kwanini alimruhusu shetani kumjaribu Adam ikiwa alijua kuwa wanadamu wengi tutateseka duniani, tutaanguka maovuni, na atatutupa Jehanamu?

3) Kama Mungu anatuambia tukitenda dhambi na tusipomtii tutachomwa motoni, Je wakristo na waislamu (baadhi yetu) tutakuwa tunamtumikia Mungu kwasababu tunampenda na tunataka kumjua zaidi? au tutakuwa tunamtumikia kwasababu tunaogopa kwenda Jehanamu?

4) Mungu husema mawazo yake si kama ya kwetu, na njia zake zipo juu zaidi, nakubaliana na hilo. Maybe kutuchoma motoni it's in his nature, that's the way He is and we have to live with it.

5)All in all Mungu ana hekima kuliko mimi, coz ni muumba wa kila kitu. Maybe katika hekima yake yote, hii ndo decision bora aliokuja nayo. Labda ana reason nzuri behind all this ambayo mm siijui. Maybe Mungu mwenyewe akinijibu face 2 face, nitabadili mtazamo wangu kuhusu yeye.

6) Kingine kinachonikasirisha pia ni yeye kuruhusu mimi kuja hapa duniani, naona ni heri nguvu aliotumia kuniumba mimi angetumia kufanya kitu kingine, nachukia + najuta kuwa hapa duniani to see all this, dunia imejaa waovu (mm nikiwa mmoja wapo) pamoja na mateso ya kila namna.

Haya ndo mawazo yangu nimeamua ku-share nanyi, najua hata povu linitoke vipi it won't change the facts. Samahani kwa ntakaekuwa nimewakwaza humu jukwaani, naamini Mungu alishayajua mawazo yangu kuhusu yeye toka kitambo. So im just keeping it real.

Bila shaka umesoma bibilia kwa kiasi fulani na unaona kama yaliyoandikwa na maisha yanayoonekana ni kama mashariki na magharibi, na hivyo maswali mengi yanazaliwa na kiasi fulani unakosa majibu. nikupongeze sanaaa kwani hiyo ni njia nzuri ya kujifunza na kumjua Mungu.

Swali 1. a, Kimsingi mwandamu alivyoumbwa hawezi kufuta maagizo bila sheria au bila utaratibu, ndiyo maana pamoja na kuwa shule inakuletea maarifa lakini viboko na kufukuzana shule vipi.b, Lakini pia MUNGU hakuwaumba watu wake waishi duniani, bali waishi kwenye ufalme wake matayo 6.33, watu wengi wanaishi duniani na ndiyo maana ni vigumu kuishi kirahisi ndani ya maisha ya kiubinadamu.c Hatuumbwa kuishi kwa kuusikiliza mwili bali kuisikiliza roho kwa kuwa ndiyo yenye maagizo ya namna ya kuishi ukija kwenye ufalme, Roho ina blue print ya namna ya mtu kuishi kwenye ufalme na kuyafanya maisha rahisi mno, na hata hayo majibu ya maswali utajibiwa mwenyewe bila kuuliza.

Home work. 1,Jaribu kujua nini maana na tofauti ya kuishi duniani au ufalme kwa mujibu wa maandiko
2.Tofautisha matakwa ya mwili na roho katika kuishi na kutimiza mapenzi ya MUNGU
Swali 2. Kitu cha ajabu sanaaaa Ukiwa kwenye ufalme unanguvu kuliko shetani, hivyo kwa MUNGU shetani sio threat kwa Mtu wake, threat kubwa kwa mtu wa MUNGU ni dhambi na uovu na kutofuata sheria ya MUNGU. Hivyo kwa MUNGU hakuna threat ya shetani na jambo hili limetumika vibaya na kumpa shetani madaraka makubwa ambayo kimsingi hana kabisaaa, na ametumia udhaifu wa wanadamu kutojua nguvu yao ili kuwakandamiza, MUNGU anatushanga tunavyoangaika kwa kukosa maarifa.

Homework. Chunguza nguvu uliyonayo katika MUNGU, utagundua wewe ni unmovable machine kwenye ulimwengu wa roho, ukishajua then practise, utaanza kwa ugumu baadaye mwili na akili vitazoea.

Swali 3. Mara nyingi kupenda kitu huja baada ya kukifahamu vizuri, sheria zinaweza kuwepo ilikukuongeza kufahamu hcho kitu then ujikute kwenye pendo. Huwezi kumpenda MUNGU bila kumfahamu, tena bible inasema lazima uwe mwana ili uweze kumpenda, maana kumwabudu MUNGU lazima uwe rohoni nawe uwe roho ndiyo utamjua MUNGU, hivyo sheria nyingi zinajaribu kumfanya mwanadamu arudi rohoni kwani yeye hupenda kuwa mwilini jambo ambalo ni gumu kufahamu MUNGU.

Nitakupa mfano, Yesu anasema ili umpende MUNGU lazima mwili ufe katika dhambi, yaani ifike mahali unaichukia dhambi kama kinyesi, ukona mtu anatenda dhambi unaona kinyaa, hii inawezekana tu kwa mwili uliokufa,. Mwili ukifaa hauwezi kukumbuka face book, twitter wala chakula unakuwa umkufa unasubiri kuzikwa, kwa maana hiyohiyo ukifa katika dhambi huwezi kumbuka dhambi, na hapo roho inachukua uongozi wa mwili na kuifurahia sheria ya MUNGU na unajikuta unampenda MUNGU na kamawe huwezi mwachaaa, kama vile ilivyo ngumu kuacha kuvuta sigara ukiongozwa na mwili.

Ili jambo hili halitokee haliji mara moja unatumia nguvu kidogo kuachaa, then unajikuta unaanza kukoform na unaingia ndani kabisaaa. Lazima uombe sana, usome sana, na ujinyime sana mambo ya dunia ili kutengeneza shift ya mazingira ya dunia kwenda ufalme.
 
Sasa hii mada inaingia vipi katika ili jukwaa?

Wewe kama unajuta,juta peke yako. Sisi wengine tunafurahia uwepo wake.

Halleluya.
 
Back
Top Bottom