Huyu naye ni gt hivyo unapomjibu umjibu kwa reference za kibiblia maana inajitosheleza.
Mungu anasema hapendi hata mtu mmoja apotee bali wote waufikie uzima wa milele.......Tena anawaambia waisrael ambao hawakutii wakati ule akasema Ninawajaribu ili nipate kujua uthabiti wenu.
Imagine kwa watoto wako nyumbani kwako umewazaa ili baadaye uwatese?.Hapana unawapenda wote,unawatendea haki wote na wale wanaoumia ingawa ni wanao ni kwa sababu ya kukiuka,miongozo unayotoa kama baba laiti wangeifuata wasingeumia.
Ugumu wa mioyo yetu umetuingiza ktk mateso mengi duniani.Nchi nyingi duniani zinapigana vita wanauana kwa sababu tu ya ugumu wa mioyo yao (kutokutii kujua yaliyo mapenzi ya Mungu ili tuyafanye).
Mateso mengi ni zao la kutokutii miongozo mizuri.Mkinitii na kufuata amri zangu....mkifanya yaliyo mapenzi yangu hakika sitaangamiza nchi yenu.Kwa hiyo hapa utajua kuwa tumekosa utii mioyoni mwetu mbele za baba yetu(Mungu).
Anza mazoezi mema ya kufanya utii wewe umekiri kuwa ni muovu tayari kwa ishara hiyo tu wewe umeokoka maana Mungu anasema atakayenikana mbele za watu nami nitamkana......
Je wewe ukiwa baba wa nyumba unapenda watoto wako wakudharau?.Na kama hupendi unafanyaje kuleta nidhamu ktk nyumba yako?.Je unajisikiaje watoto wako wanapoishi kwa muongozo uutakao wewe?.Je hujawahi watisha wanao kuwa wakifanya jambo fulani baya watapatwa na balaa fulani (rejea hadithi za mafunzo kwa watoto) maishani mwao?.
Mungu ni upendo kwetu,Mungu ni upendo kwa wote,endelea kuamini uwepo wa Mungu hata kama ukifika ukamkosa huna hasara compared na kutokuamini uwepo wake then ukaenda ukamkuta.
Kwa maelezo yako naona hukufuru bali hii ndiyo njia yako sasa ya kumrudia Mungu na kushuhudia atakavyokubadilisha ili uwafundishe na wengine.
Nakutakia mubaraka mwema usome matayo 11:6.Imeandikwa anayo heri mtu yeyote asiye na mashaka nami asema bwana wa majeshi.Amina.