Sababu zinazonifanya nisimpende Mungu

Sababu zinazonifanya nisimpende Mungu

Mara hakuna Mungu mara tunanchukia Mungu...hivi unaanzaje kuchukia kitu kisichokuwepo.....
 
Je wa Africa tulikua na imani kabla ya Toleo hili la pili la kiimamani? Kama jibu ni ndio ni Wazi kua tulikua na MUNGU wetu. Wengi wanafikili kwamba Ukoroni ulikuja kuchukua, madini, pembe za Ndovu na kadhalika... Kumbe Mzungu alikuja "kupola... Kila kitu... Madini yetu Imani zetu..kuvuruga tamaduni zetu... Wao wanawafinyanga watoto wao kitawala Dunia.. Sisi Ufalme wa Bwelele Mbinguni ooo My God... Niishie hapa, kataa ukibwetele.
Huyo Mungu wa africa yupo wapi
 
Kama umekasirika nae tu basi haina shida nakupongeza tu kwa kutambua uwepo wake maana bila kuwepo yy usingemkasirikia lkn umekiri kama yupo
 
YEYE anakupenda mda wote.
Mzee wa Ukawa alikuja kugundua hivyo mwishoni kabisa mwa maisha yake na akamrudia Mungu, NAYE akampokea.
Basi na wewe iko siku utakuja kuujua Upendo wa Mungu kwako.

Time gonna tell you, if not.
 
Mwenye kuamini mungu na asiyeamini ni yupi muoga?
Mwoga ni yule asiyeamini uwepo wa Mungu.
Anajifariji kwamba, matendo yake maovu anayofanya kwa kujificha hayatajulikana, na pia hata adhibiwa kwayo, na tena hataki kuonywa, pia hataki kutii, yaani ana Kibri.
Nakadhalika.
 
Hakuna lolote yote haya unayoyaona huku diniani ni sababu za uasi wa binadamu toka mwanzo.
Adamu angetii masharti aliyoambiwa na Mungu leo ungekuta tunaishi paradise life.
Siyo kweli hili la Adam Mungu mwenyewe alilifahamu kuwa litakuwepo ni mipango ya kumfanya mwanadamu afanye maamuzi yake ataoona inafaa Mungu anajua kila kitu kilichopita na kijacho ndio maana sisi wanadamu ametupa Uhuru wa maamuzi huwa hatuna maelekezo tunaamua wenyewe.
Ila adamu hakutenda dhambi hii ni dhana ya mafundisho
 
Swali mujarabu mkuu. Yaani maelezo ya jamaa ni sawa tu na angeuliza ni kwa nini Adam hakuongeza uvumilivu kidogo. Jambo lililokuwa ndani ya uwezo wake pia.

Wazo la Mungu ni ukomo wa kufikiri. Ni namna tu ya kupata majibu rahisi kwa maswali magumu. Kila jambo lipo ndani ya uwezo wetu.

Hata kifo kimefanywa kuwa kigumu mno kueleweka. Watu wameweka dhana za roho na mwili, mambo ambayo hayapo katu.

Eti roho inaacha mwili. Hivi injini ya gari inaposhindwa kufanya kabisa na ukashindwa hata kuibadilisha na hivyo gari likashindwa kufanya kazi kabisa, tunasema nini kimeacha nini?

Kwa viumbe hai, kuna kuwepo au kutokuwepo. Hali ya mifumo ya kiumbe hai kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano ndio uwepo. Hali ya mifumo kushindwa kufanya kazi milele ni kutokuwepo (kufa). Ndio maana kiumbe huozaa na kupotea kabisa.
Mkuu nikusahihishe kidogo hapa shida ni uelewa wako mdogo.

Maisha yana mwendelezo huwa hayafiki mwisho kwanza kabisa huu mwili ukioza huanza maisha katika viumbe wengine huzaliwa (kuenguliwa) wadudu n.k na hii ndiyo hutupa picha halisi kuwa maisha huendelea Roho haifi inamwendelezo
 
Mkuu, nina mashaka na mazingira yaliyo kukuza napata wasiwasi kwa jinsi ulivyoanzisha mada ila nisaidie kujibu hili swari kama una uelewa nalo kama hautaweza usijibu maana hapa siyo Siasa tunautaka ukweli usio na mashaka juu ya nini kimeufanya Ulimwengu.

Uwepo wa nyota yetu ya Jua ni matokeo ya mlipuko wa Big bang na ili tupate uhakika tuangalie uhai wa nyota unapo koma (supernova) na zikaundwa nyota kutengeneza maisha mengine kutokana na kifo cha nyota 1, nyota moja ikifa huanzisha maisha ya Nyota nyingi zitakazo zaliwa na kuwa na sayari zake nyingine ktk mfumo wa kila nyota.

Maswari 2

1.Ulimwengu umepangiliwa kwa umakini kila Galax inajitegemea na nyota zake zina sayari zinazozunguka mabilioni na kila kimoja hupita njia yake bila kusababisha madhara kwa mwenzake je nguvu iliyofanya haya tuiiteje?

2.Ukirejea kuangalia matokeo ya uwepo wa Nyota yetu Jua na Sayari yenye uhai ya Dunia; jiulize hivi?
Mwanzo ulipotokea mlipuko jua letu likawepo hakukuwa na sayari lakini mavumbi ya hewa nzito yanayozunguka nguvu ya uvutani ktk Jua yalijiunda yakawa sayari na hizi Sayari zilipokea mwanga wa Jua wenye sumu Kali moja kwa moja na mwanzo vumbi lilikuwa lenye joto Kali lisiloweza kustawisha uhai wa asilia kwanza kuna Sumu ya miale ya Jua na kuna joto Kali kwa hiyo hakukuwa na uwezekano kiumbe chochote kinachoweza kuishi!
Je kilichoipoza Dunia yetu na kuitengenezea kiwambo cha hewa nzito kuchuja miale ya sumu ya jua isiingie duniani na kuweka hewa safi na kupanda uhai wa viumbe hai ni nini ni? Nguvu gani? Tuipe jina gani?
 
Kama Shetani yupo Basi hata Mungu yupo maana Alitupwa duniani baada ya kuasi Na ndio maana vita kati yake na Mungu ni kubwa ila haipiganwi isipokuwa kupitia mwanadamu.
Mungu yupo jamaa angu Na anaishi Ndani ya Jua sehemu isiyofikika Na kitu chochote kile.
1Timotheo 6-15.
 
Back
Top Bottom