Baadhi ya Watu wakipata chakula wakala wakashiba, basi hapo wameshakuwa wajanja.
wanabaki kutamba tu na kusema hawamjui au wanamchukia Mungu.
Wengi wao ni watoto wenye wazazi wanaojitoshereza kimapato.
Sisi tuliopitia maisha magumu tumeuona Mkono wa Mungu ukituokoa mara nyingi tu.
Tuliposhindwa kwenda kutibiwa kwenye hospitali za ghalama, kutokana na magonjwa sugu, Mungu aliingilia kati na kutuponya.
Tulipokosa chakula, Mungu alitulisha vyakula vya jalalani na hatukuugua matumbo.
Tulipofiwa na wazazi, Mungu alitulea mitaani hadi tukakua na kujitegemea maisha.
Tulipoonewa Mungu alitulinda na kupata haki yetu.
Tulipotaka kuuwawa na wenye nguvu, Mungu alizuia risasi zisitudhuru mwilini.
Tulipokosa mavazi na kutembea matako yakionekana, Mungu alituficha na uso wa aibu, tulienda shule hivyohivyo hadi tukahitimu na kufaulu.
Nakadhika nakadhalika nakadhalika nakadhalika.
Leo hii tunashuhudia kuwa Bila Upendo wa Mungu, sisi tusingekuwepo hapa tukiandika mada hizi.
Ni upendo wa Mungu uliotufikisha hapa tulipo.
Hongereni wenzetu ambao mlikuwa na nguvu ya kupata mahitaji yenu yoote kwa Pesa za wazazi wenu. Kwa vyeo vya walezi wenu.
Kwenu Mungu hana maana, hayupo, hana mchango wowote, sio chochote na mnasema kwa sasa mnamchukia.
Mnanguvu nyingi, mnajitegemea, mnajiweza kwa lolote.
Sisi bila Mungu hatuwezi chochote, hata kuamka asubuhi tunamtegemea Mungu, hata kutembea, hata kufumbua macho hatuwezi bila yeye kutupa nguvu.
Kwenu wenye nguvu Hakuna Mungu, kwetu sisi wanyonge Mungu yupo na ndio tegemeo letu.
Tunampenda sana sana sana, tunampenda mara Zilioni.
Asante Mungu kwa Upendo wako usio na mipaka, kwa kuwapenda watu wote, hata hao wanaosema wanakuchukia.