hatuongelei watu wanaookoka ili kuficha maovu, hao wapo, tena wengi tu. tunaongelea watu wanaookoka wakijua ya kwamba Yesu anawataka waokoke, wasipofanya hivyo hukumu iko juu yao, kwasababu hukumu ya kwaza kabisa juu ya mwanadamu siku ya mwisho ni hukumu ya kumkataa Yesu Kristo mwana wa Mungu aliye hai. kama wewe ukiokoka kwa kuficha maovu, hauko serious, utaaibika, na utapigwa tu na Mungu. juu ya huyo mchungaji unayemsema, ni mtu mmoja tu, ambaye kwanza si malaika hivyo uwe wa kwanza kurusha jiwe kama wewe pia haufanyi hivyo. simtetei, namaanisha kuwa mnaweza kuwa mko daraja moja tu na wewe unayemhukumu, wote towards jehanam. kuna walokole wengi wanaoona matunda ya kuwa na Mungu, na tunayafurahia. Mungu ni mwema siku zote. wachache ambao shetani anawaangusha, tunawaombea Mungu awasimamishe na tuendelee kumwabudu yeye katika roho na kweli. hatuwachukii na kuwaombea mabaya, kwasababu kama kufanya mambo mabaya ya aibu, hawatuaibishi sisi walokole wengine, wanamwaibisha Mungu na kulitukana Jina lake takatifu. hivyo ni Mungu mwenyewe atadili nao, sisi walokole wengine ambao tuko serious hiyo haituhusu, zaidi ya kuwaombea Mungu awakomboe na kuwasimamisha. na kwenu nyinyi ambao hamjaookoka, hukumu i karibu mlangoni, Bwana Yesu anakuja kulichukua kanisa lake pamoja na kuihukumu dunia hii iliyojaa uovu. dalili zinaonyesha yu malangoni, heri yeye yule anaezingatia kuyafua mavazi yake katika damu ya mwana kondoo, ili asipate aibu siku ile ambayo watu watalia na kusaga meno. hakuna faida yoyote mtu akiupata ulimwengu wote, utajiri wote, kila kitu unachofikiria kukifanya, halafu roho yako ikaishia jehanum milele, siku hiyo inakuja na i karibu mno. siku ambayo dunia ambayo ni tegemeo na kiburi cha wengi, itakunjwa kama karatasi, wenye hekima na wanajimu watalia na kusaga meno kwasababu aibu i mbele yao, na wale wenye kuongoza wengi kutenda mema, na wale waliomkiri na kumfuata Bwana Yesu, WATARUKARUKA KAMA NDAMA, kwasababu yule waliyemsubiri amekuja. HALELUYA to the lamb of God. Mungu na atusaidie.