Miss Halima
JF-Expert Member
- Aug 4, 2026
- 221
- 487
Mke wa nyota wa As Monaco Paul Pogba, Zulay Pogba amejitokeza hadharani kumtetea mume wake, na kukataa madai ya watu kwamba kiungo huyo mwenye umri wa miaka 33 anapaswa kustaafu soka na aliamua kurejea kucheza soka ili kutafuta fedha.
Kauli imekuja wakati Monaco ikiripotiwa kutaka kuvunja mkataba wa Pogba kufuatia mfululizo wa majeraha anayoyapitia tangu walipomsajili mchezaji huyo..
Paul pogba alifanikiwa kucheza mechi sita pekee msimu uliopita, huku akijaribu kuanza upya maisha yake ya soka baada ya kusimamishwa kwa muda mrefu kucheza soka kutokana na suala la matumizi ya dawa zilizopigwa marufuku.
Akiwa katika maandalizi ya msimu mpya Pogba ameripotiwa kusumbuliwa na tatizo la goti, Huku mashabiki na wachambuzi wakisema kwamba mwili wake hauwezi tena kuendelea kucheza soka la kiwango cha juu, Lakini mkewe alitoka na aliwajibu moja kwa moja wakosoaji hao..
“Kwa watu wote wanaosema Paul anapaswa kustaafu au kwamba amerudi kwenye soka kwa ajili ya pesa, napenda kuweka hili wazi, anayejua ni lini pogba atastaafu ni Mungu pekee.”
Kisha akaongeza,
“Na kwa wale wanaosema amerudi kwa ajili ya pesa, niaminini sisi tuko vizuri sana kifedha, namshukuru Mungu.”
Wanandoa hao, walifunga ndoa mwaka 2019 na wana watoto wawili wa kiume, Na wamepitia miaka kadhaa yenye changamoto nyingi nje ya uwanja.
Pogba aliwahi kuelezea kujiunga kwake na Monaco ni kama mwanzo mpya baada ya kile alichokiita “kipindi cha giza”, kilichohusisha kusimamishwa kwake na baadaye kuvunjwa kwa mkataba wake na Juventus mwishoni mwa mwaka 2024.
Kauli imekuja wakati Monaco ikiripotiwa kutaka kuvunja mkataba wa Pogba kufuatia mfululizo wa majeraha anayoyapitia tangu walipomsajili mchezaji huyo..
Paul pogba alifanikiwa kucheza mechi sita pekee msimu uliopita, huku akijaribu kuanza upya maisha yake ya soka baada ya kusimamishwa kwa muda mrefu kucheza soka kutokana na suala la matumizi ya dawa zilizopigwa marufuku.
Akiwa katika maandalizi ya msimu mpya Pogba ameripotiwa kusumbuliwa na tatizo la goti, Huku mashabiki na wachambuzi wakisema kwamba mwili wake hauwezi tena kuendelea kucheza soka la kiwango cha juu, Lakini mkewe alitoka na aliwajibu moja kwa moja wakosoaji hao..
“Kwa watu wote wanaosema Paul anapaswa kustaafu au kwamba amerudi kwenye soka kwa ajili ya pesa, napenda kuweka hili wazi, anayejua ni lini pogba atastaafu ni Mungu pekee.”
Kisha akaongeza,
“Na kwa wale wanaosema amerudi kwa ajili ya pesa, niaminini sisi tuko vizuri sana kifedha, namshukuru Mungu.”
Wanandoa hao, walifunga ndoa mwaka 2019 na wana watoto wawili wa kiume, Na wamepitia miaka kadhaa yenye changamoto nyingi nje ya uwanja.
Pogba aliwahi kuelezea kujiunga kwake na Monaco ni kama mwanzo mpya baada ya kile alichokiita “kipindi cha giza”, kilichohusisha kusimamishwa kwake na baadaye kuvunjwa kwa mkataba wake na Juventus mwishoni mwa mwaka 2024.