matunduizi
JF-Expert Member
- Aug 20, 2018
- 6,602
- 15,400
Utangulizi
Kaka watatu huko kusini mwa afrika wameapa kumpiga Mchungaji kila jumapili hadi atakapokubali Mimba aliyoikana ya Dada yao.https://www.faceofmalawi.com/2022/04/07/3-men-beat-pastor-for-impregnating-their-sister-and-denying-the-pregnancy-vows-to-continue-beating-him-every-sunday-until-he-accepts-the-pregnancy/
Hii imekuwa shida kubwa ya makasisi na viongozi wa kiroho.
Nimetafiti nimegundua hizi ndio sababu kuu.
1: Wanakuwa wamezungukwa Muda mwingi na wanawake
Wateja wakuu wa mambo ya Mungu huwa ni wakina mama. Hata Yesu walimzunguka lakini alikuwa na mipaka. Akiachana nao anaenda kukesha ila wengi wanalala na kuomba kidogo. Hapo Mtumishi utaangushwa.
2: Wana migogoro kwenye Ndoa zao
Hekima ya kushindwa kubalance ndoa na utume wanajikuta familia au Mke katelekezwa. Wafariji wakuu wanakuwa wana wa kike makanisani. Rahisi kuporwa hisia na kuzichepusha kwa wamama au wadada wanaomzunguka.
3: Ushauri nasaha
Katika maandiko hakuna Mtumishi eti amekaa chobisi/faragha anamshauri mwanamke kuhusu Ndoa na mapenzi. Hii hufanywa na wanasaikolojia wa duniani. Utafiti katika kitabu (Stop biblical counciling start Biblical ministering) anasema Asilimia 35 ya makansela wachungaji au wadunia huzini na hao wanaowakanseli. Unatakiwa kuomba, Na kufanya awe wa kiroho ili atatue matatizo yake na Yesu wake, sio wewe uanze kumchimba. Pia Ni dhambi kumshauri MTU mmoja faragha kwa jambo linalohusu watu wawili bila upande mwingine kuwepo. Utafanya maamuzi kwa taarifa za nusu uongo.
4: Shambulizi la Ngono
Wako watu wanatumwa kuwaangusha watumishi makusudi. Ni mkakati wa makusudi kuwablackmail au kuwapoza wale watumishi wa kweli. Hii hufanywa na majasusi wa kubwa kuwafunga viongozi wa kisiasa kwa kuwatengenezea skendo duniani. IInaitwa HONEY TRAP. Sio kila Mchungaji anazini kwa kupenda wengine wameangushwa.
5: KAFARA YA NGONO
Wale wachungaji feki ngono ni ibada. Ni sujudu kwa ibirisi ili kuongeza upako wa kuzimu. Huyu atazini na wajane, vibinti, wakongwe, wake za watu bila kukoma.
Mwisho
Ukisikia MTU anakuwa Mchungaji au Mtumishi wa Mungu Muombee sana. Angusho la kingono linanzunguka 24hrs7Days.
Ni hayo tu
Karibu kwa maoni zaidi na maswali.
Kaka watatu huko kusini mwa afrika wameapa kumpiga Mchungaji kila jumapili hadi atakapokubali Mimba aliyoikana ya Dada yao.https://www.faceofmalawi.com/2022/04/07/3-men-beat-pastor-for-impregnating-their-sister-and-denying-the-pregnancy-vows-to-continue-beating-him-every-sunday-until-he-accepts-the-pregnancy/
Hii imekuwa shida kubwa ya makasisi na viongozi wa kiroho.
Nimetafiti nimegundua hizi ndio sababu kuu.
1: Wanakuwa wamezungukwa Muda mwingi na wanawake
Wateja wakuu wa mambo ya Mungu huwa ni wakina mama. Hata Yesu walimzunguka lakini alikuwa na mipaka. Akiachana nao anaenda kukesha ila wengi wanalala na kuomba kidogo. Hapo Mtumishi utaangushwa.
2: Wana migogoro kwenye Ndoa zao
Hekima ya kushindwa kubalance ndoa na utume wanajikuta familia au Mke katelekezwa. Wafariji wakuu wanakuwa wana wa kike makanisani. Rahisi kuporwa hisia na kuzichepusha kwa wamama au wadada wanaomzunguka.
3: Ushauri nasaha
Katika maandiko hakuna Mtumishi eti amekaa chobisi/faragha anamshauri mwanamke kuhusu Ndoa na mapenzi. Hii hufanywa na wanasaikolojia wa duniani. Utafiti katika kitabu (Stop biblical counciling start Biblical ministering) anasema Asilimia 35 ya makansela wachungaji au wadunia huzini na hao wanaowakanseli. Unatakiwa kuomba, Na kufanya awe wa kiroho ili atatue matatizo yake na Yesu wake, sio wewe uanze kumchimba. Pia Ni dhambi kumshauri MTU mmoja faragha kwa jambo linalohusu watu wawili bila upande mwingine kuwepo. Utafanya maamuzi kwa taarifa za nusu uongo.
4: Shambulizi la Ngono
Wako watu wanatumwa kuwaangusha watumishi makusudi. Ni mkakati wa makusudi kuwablackmail au kuwapoza wale watumishi wa kweli. Hii hufanywa na majasusi wa kubwa kuwafunga viongozi wa kisiasa kwa kuwatengenezea skendo duniani. IInaitwa HONEY TRAP. Sio kila Mchungaji anazini kwa kupenda wengine wameangushwa.
5: KAFARA YA NGONO
Wale wachungaji feki ngono ni ibada. Ni sujudu kwa ibirisi ili kuongeza upako wa kuzimu. Huyu atazini na wajane, vibinti, wakongwe, wake za watu bila kukoma.
Mwisho
Ukisikia MTU anakuwa Mchungaji au Mtumishi wa Mungu Muombee sana. Angusho la kingono linanzunguka 24hrs7Days.
Ni hayo tu
Karibu kwa maoni zaidi na maswali.