Acheni kuita Wachungaji na Mapadre “Baba”

Yesu Anakuja

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
9,515
19,341
Leo nilikuwa najadili na mke wangu, tukafikia discussion moja, wanawake wengi sana wanapenda kuita wachungaji wao "baba yangu", wanawapa heshima kubwa kuliko hata ile wangewapa waume zao au baba zao. mchungaji au nabii au padre anainuliwa sana, anaonekana yeye ni mtu special sanaaaa, treatment anayostahili ni special sanaaaa, na yeye asipokuwa treated hivyo anachukia kwasababu anajiinua na kuona sio sawa na wengine. mimi na Mke wangu huwa tunapinga sana hili jambo. Yesu alikemea sana jambo hili baada ya kuona waalimu wa sheria na viongozi wa kwenye masinagogi wanapandisha mabega, wanapenda watu wawaite "mwalimu", baba n.k na wakipita hata masokoni au popote watu wawape recognition fulani ya special. na ndivyo ilivyo na siku hizi.

MATHAYO 23:9 INASEMA; Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni. Wala msiitwe viongozi, maana Kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo. Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu. Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa, na yeyote atakayejidhili atakwezwa.

Wachungaji, manabii, mitume, mapadre na mafather
, wengi huwa wanapenda sana recognition, wengine wamefikia hatua wanaamini wao ni baba wa kiroho wa mtu fulani as if wao wameokoa roho yake au labda walikuwa na uwezo wa option ya kuamua kumfanya aokoke au asiokoke. Enzi za Yesu alipokuwa katika mwili haya pia yalikuwepo, Mafarisayo na masadukayo na waalimu wa sheria walikuwa wanapenda sana recognition, Yesu akafuta icho cheo kwao, kilichokuwa kinawafanya wajiinue kujiona wapo bora kuliko wengine, ndio maana aliongea mstari huo hapo juu.

Wengine wanashindwa kuelewa, kwani Yesu alimaanisha tusiite biological parents baba? Au alimaanisha nini? JIBU: alimaanisha baba wa kiroho, kamwe usimfanye mchungaji wako, mwalimu, anayejiita nabii au mtume kuwa ni BABA yako, ukiangalia kwenye tv utaona watu wanampa sifa mchungaji ati “baba”, imefika mahali watu wanaita fulani ni baba yangu. Yesu alikataza hilo.

KUTOKA 20:12 anasema waheshimu baba yako na mama yako…, hapa alikuwa anaongelea baba na mama kimwili (biological), ila ukija kwenye mambo ya Mungu, acha kuita wachungaji au manabii wenu hao baba, kwasababu tunaye baba mmoja tu, aliye mbinguni, wala msiwaite waalimu kwa maana ya kuwainua wao. Hao hawana uwezo wowote kuwazaa kiroho, hata kama wamewahubiria wametumiwa kama vyombo tu ila anayewazaa kiroho ni Mungu, hao mnaowatukuza na kuwaita waalimu hawana uwezo wowote wa kufundisha na kubadilisha mioyo yenu, wajiite tu watumishi au vyombo vya Bwana, kwasababu hata wawe na uwezo mzuri namna gani kufundisha anayebadilisha roho ni Mungu wala sio uwezo wao wa kupangilia maneno. Mwenye kunielewa amenielewa, achene kutukuza watu. Na ninyi mnaotukuzwa msikubali kutukuzwa, achene anayestahili utukufu, Mungu wa mbinguni, apate utukufu wake wote, msiibe utukufu wake. Mungu awabarikini nyote muelewe hili.
 
Hakuna ubaya wowote kama anayeitwa hatachukua nafasi ya Mungu
huo mstari umeusoma lakini? MATHAYO 23:9 INASEMA; Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni. Wala msiitwe viongozi, maana Kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo. Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu. Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa, na yeyote atakayejidhili atakwezwa.

ni mchungaji gani, mwalimu gani aliyezoea kuitwa hivyo, fadha gani, aliyezoea kuitwa hivyo, ambaye atafurahi kama fulani anamwita hivyo na wewe haumwiti hivyo? na, mtu anayependa aitwe mwalimu, unafikiri kwa uwezo wake mwenyewe anaweza kufanya uelewe Neno la Mungu au ni Mungu ndiye anayekufundisha akimtumia yeye kama chombo tu? manake mwalimu hapo ni Mungu, sio icho chombo. unaletewa chakula kwa kutumia shahani halafu unaiinua sahani iliyotumika kuleta chakula badala ya mpishi na mmiliki wa ile sahani. pia, kiroho, hakuna mtu anamzaa mwingine, Yesu Kristo ndiye anatuzaa kiroho kwa Roho wake Mtakatifu. hatustahili kabisa kuitwa baba au mwalimu kiroho, ile yeye. na hakuna aliyewahi kustahili kuitwa hivyo ambaye hajawahi kuchukia au kujisikia vibaya kaam hataitwa hivo na wale waliozoea.
 
huo mstari umeusoma lakini? MATHAYO 23:9 INASEMA; Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni. Wala msiitwe viongozi, maana Kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo. Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu. Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa, na yeyote atakayejidhili atakwezwa.

ni mchungaji gani, mwalimu gani aliyezoea kuitwa hivyo, fadha gani, aliyezoea kuitwa hivyo, ambaye atafurahi kama fulani anamwita hivyo na wewe haumwiti hivyo? na, mtu anayependa aitwe mwalimu, unafikiri kwa uwezo wake mwenyewe anaweza kufanya uelewe Neno la Mungu au ni Mungu ndiye anayekufundisha akimtumia yeye kama chombo tu? manake mwalimu hapo ni Mungu, sio icho chombo. unaletewa chakula kwa kutumia shahani halafu unaiinua sahani iliyotumika kuleta chakula badala ya mpishi na mmiliki wa ile sahani. pia, kiroho, hakuna mtu anamzaa mwingine, Yesu Kristo ndiye anatuzaa kiroho kwa Roho wake Mtakatifu. hatustahili kabisa kuitwa baba au mwalimu kiroho, ile yeye. na hakuna aliyewahi kustahili kuitwa hivyo ambaye hajawahi kuchukia au kujisikia vibaya kaam hataitwa hivo na wale waliozoea.
‭1 Timotheo 1:18-19 BHN‬
[18] Mwanangu Timotheo, nakukabidhi amri hii kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Yatumie maneno hayo yawe silaha yako katika kupigana vita vizuri, [19] na ushike imani yako na dhamiri njema. Watu wengine hawakusikiliza dhamiri zao na hivyo wakaiharibu imani yao.

Nakukumbusha tu Timotheo hakuwa mtoto wa kimwili wa kuzaa kwa Paul.
 
‭1 Timotheo 1:18-19 BHN‬
[18] Mwanangu Timotheo, nakukabidhi amri hii kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Yatumie maneno hayo yawe silaha yako katika kupigana vita vizuri, [19] na ushike imani yako na dhamiri njema. Watu wengine hawakusikiliza dhamiri zao na hivyo wakaiharibu imani yao.

Nakukumbusha tu Timotheo hakuwa mtoto wa kimwili wa kuzaa kwa Paul.
ni wapi timotheo aliwahi kumwita paulo baba yake? lete na huo. kuita mtu mwanao ni kitu cha kawaida, hata ukikutana na mtu sokoni ambaye umri wake ni sawa na mtoto wako, mimi huwa nawaita mwanangu hujambo, that's normal. hata hivyo hili halina haja sana kubishana, cha mhimu kwa walioelewa, na wewe pia najua unaelewa kwamba, Yesu alikuwa anapinga watu wanaojiinua kama wazazi au waalimu wa wengine kiroho, bila kujua kuwa kimwili hao wanaweza kuwa hivyo, ila kiroho hakika baba ni Mungu tu, na mwalimu ni Mungu tu. kwasababu mchungaji au padre au yeyote hata ahubiri namna gani, mahubiri yake kama hayajasukumwa na Nguvu za Mungu yanakuwa hayana uwezo kubadilisha moyo wa mtu sasa kujisifu kwake kwamba yeye ndiye baba yake wa kiroho kunatoka wapi? anastahili vipi wakati kazi yote ya roho ameifanya Mungu mwenyewe? huko kupandisha mabega na kutaka watu wakurecognize hivyo ndiko Yesu alikataza na ni chukizo kwa Mungu kwasababu unakuwa unachukua utukufu wa Mungu. tofautisha mtu kukuita wewe baba au mwalimu, na wewe kumuita mtu mwanangu. angalia kama vinafanana. na unapofanya hayo, endelea kutafakari na MATHAYO 23:9 Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni. Wala msiitwe viongozi, maana Kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo. Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu. Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa, na yeyote atakayejidhili atakwezwa. na tueleze kama uondolewe kwenye Biblia au ubaki.

kuna watu hadi leo hii, wanamwita tb joshua baba yao kiroho, wengine wanamwita mwamposa, kuhani musa, na wengine wote hao, wanawaita aidha mwalimu wangu, au baba yangu. na wao wanatumia kofia hiyo kuwaamrisha chochote wakifanye wakiamini usipofanya unakuwa umekiuka mamlaka yao kama baba yako, wengine wanajifanya ukiondoka hata kanisani kwako kwasababu wao ni baba yako, hautafanikiwa, ni kama wanajiona wao wameshikilia tiketi yako ya uzima wa milele, na bila wao huwezi kufanikiwa kiroho wala kimwili.
 
Leo nilikuwa najadili na mke wangu, tukafikia discussion moja, wanawake wengi sana wanapenda kuita wachungaji wao "baba yangu", wanawapa heshima kubwa kuliko hata ile wangewapa waume zao au baba zao. mchungaji au nabii au padre anainuliwa sana, anaonekana yeye ni mtu special sanaaaa, treatment anayostahili ni special sanaaaa, na yeye asipokuwa treated hivyo anachukia kwasababu anajiinua na kuona sio sawa na wengine. mimi na Mke wangu huwa tunapinga sana hili jambo. Yesu alikemea sana jambo hili baada ya kuona waalimu wa sheria na viongozi wa kwenye masinagogi wanapandisha mabega, wanapenda watu wawaite "mwalimu", baba n.k na wakipita hata masokoni au popote watu wawape recognition fulani ya special. na ndivyo ilivyo na siku hizi.

MATHAYO 23:9 INASEMA; Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni. Wala msiitwe viongozi, maana Kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo. Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu. Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa, na yeyote atakayejidhili atakwezwa.

Wachungaji, manabii, mitume, mapadre na mafather
, wengi huwa wanapenda sana recognition, wengine wamefikia hatua wanaamini wao ni baba wa kiroho wa mtu fulani as if wao wameokoa roho yake au labda walikuwa na uwezo wa option ya kuamua kumfanya aokoke au asiokoke. Enzi za Yesu alipokuwa katika mwili haya pia yalikuwepo, Mafarisayo na masadukayo na waalimu wa sheria walikuwa wanapenda sana recognition, Yesu akafuta icho cheo kwao, kilichokuwa kinawafanya wajiinue kujiona wapo bora kuliko wengine, ndio maana aliongea mstari huo hapo juu.

Wengine wanashindwa kuelewa, kwani Yesu alimaanisha tusiite biological parents baba? Au alimaanisha nini? JIBU: alimaanisha baba wa kiroho, kamwe usimfanye mchungaji wako, mwalimu, anayejiita nabii au mtume kuwa ni BABA yako, ukiangalia kwenye tv utaona watu wanampa sifa mchungaji ati “baba”, imefika mahali watu wanaita fulani ni baba yangu. Yesu alikataza hilo.

KUTOKA 20:12 anasema waheshimu baba yako na mama yako…, hapa alikuwa anaongelea baba na mama kimwili (biological), ila ukija kwenye mambo ya Mungu, acha kuita wachungaji au manabii wenu hao baba, kwasababu tunaye baba mmoja tu, aliye mbinguni, wala msiwaite waalimu kwa maana ya kuwainua wao. Hao hawana uwezo wowote kuwazaa kiroho, hata kama wamewahubiria wametumiwa kama vyombo tu ila anayewazaa kiroho ni Mungu, hao mnaowatukuza na kuwaita waalimu hawana uwezo wowote wa kufundisha na kubadilisha mioyo yenu, wajiite tu watumishi au vyombo vya Bwana, kwasababu hata wawe na uwezo mzuri namna gani kufundisha anayebadilisha roho ni Mungu wala sio uwezo wao wa kupangilia maneno. Mwenye kunielewa amenielewa, achene kutukuza watu. Na ninyi mnaotukuzwa msikubali kutukuzwa, achene anayestahili utukufu, Mungu wa mbinguni, apate utukufu wake wote, msiibe utukufu wake. Mungu awabarikini nyote muelewe hili.
Ubarikiwe Sana uko sahihi kabisa
 
Back
Top Bottom