matunduizi
JF-Expert Member
- Aug 20, 2018
- 6,590
- 15,386
Karibu moja kwa moja,
Umasikini wa Kipato namaanisha kutokuwa na kipato cha kuendesha mambo yako na kibaki cha ziada kwa ajili ya kusaidia wahitaji. Utajiri wa kipato ni kinyume chake.
1: Unasikini ni matokeo ya Laana.
Torati 28 inataja laana za kujitenga na Mungu zote zinauhusiano na umasikini wa kipato. Umasikini wa kipato sio sifa ya ukiroho ni kitu cha kukikataa kwa maneno na vitendo.
2: Umasikini ni matokeo ya Uvivu wa kufikiri na kutenda. Mungu sio mvivu. Ni mchapakazi kwelikweli na Great thinker. Lazima unapomshinda Ibris tabia zako zifanane na za baba yako.
3: Umasikini unapoteza uwezo wako wa kuwasiliana na Mungu. Umasikini wa kipato utapelekea ulaji mbovu. Utakula ili usife, hautakula ili upate afya. Mfumo wako wa fahamu ndio njia anayotumia kuwasiliana na wewe. Sasa ukiwa duni kwa kutokula vizuri, uwezo wako wa kumsikiq Mungu unashuka.
4: Umasikini utakupunguzia uwezo wako wa kuabudu. Masikini hana Muda mwingi wa kuabudu. Muda wote anapambana na maisha. Tajiri wa kipato anaweza kuamua hata kufunga na kuomba week nzima na bado mambo yakaenda wakati masikini akithubutu kufanya hivyo atapoteza ajira, ataua familia na kudhalilika.
5: Umasikini unaleta aibu na fedheha. Tabia ya kuombaomba inashusha hadhi. Mtu wa Mungu kuwa mtu wa mizinga, kuvizia watu uwapige virungu, kunyenyekea matajiri ni kumdhalilisha Mungu.
6: Masikini wengi ni wajanjawajanja katika ibada. Ili ibada ikamilike lazima iwe na Maombi, Usomaji wa neno, Nyimbo na Sadaka. Kwenye sadaka hapo masikini ni walalamishi balaa, wengine wamekimbia kabisa ibada hiyo. Mungu aliposema usiende ibadani mikono mitupu alijua wanaokwenda ni matajiri wa vipato kwa maana wanapata na cha kutoa katika baraka anazowabariki.
Ili kutukumbusha aliamua Baba wa Imani Awe Ibrahimu sio Yuda Iskariote, Baba wa Uvumilivu na Ibada awe ni Bilionea Ayubu.
Ni hayo tu.
Umasikini wa Kipato namaanisha kutokuwa na kipato cha kuendesha mambo yako na kibaki cha ziada kwa ajili ya kusaidia wahitaji. Utajiri wa kipato ni kinyume chake.
1: Unasikini ni matokeo ya Laana.
Torati 28 inataja laana za kujitenga na Mungu zote zinauhusiano na umasikini wa kipato. Umasikini wa kipato sio sifa ya ukiroho ni kitu cha kukikataa kwa maneno na vitendo.
2: Umasikini ni matokeo ya Uvivu wa kufikiri na kutenda. Mungu sio mvivu. Ni mchapakazi kwelikweli na Great thinker. Lazima unapomshinda Ibris tabia zako zifanane na za baba yako.
3: Umasikini unapoteza uwezo wako wa kuwasiliana na Mungu. Umasikini wa kipato utapelekea ulaji mbovu. Utakula ili usife, hautakula ili upate afya. Mfumo wako wa fahamu ndio njia anayotumia kuwasiliana na wewe. Sasa ukiwa duni kwa kutokula vizuri, uwezo wako wa kumsikiq Mungu unashuka.
4: Umasikini utakupunguzia uwezo wako wa kuabudu. Masikini hana Muda mwingi wa kuabudu. Muda wote anapambana na maisha. Tajiri wa kipato anaweza kuamua hata kufunga na kuomba week nzima na bado mambo yakaenda wakati masikini akithubutu kufanya hivyo atapoteza ajira, ataua familia na kudhalilika.
5: Umasikini unaleta aibu na fedheha. Tabia ya kuombaomba inashusha hadhi. Mtu wa Mungu kuwa mtu wa mizinga, kuvizia watu uwapige virungu, kunyenyekea matajiri ni kumdhalilisha Mungu.
6: Masikini wengi ni wajanjawajanja katika ibada. Ili ibada ikamilike lazima iwe na Maombi, Usomaji wa neno, Nyimbo na Sadaka. Kwenye sadaka hapo masikini ni walalamishi balaa, wengine wamekimbia kabisa ibada hiyo. Mungu aliposema usiende ibadani mikono mitupu alijua wanaokwenda ni matajiri wa vipato kwa maana wanapata na cha kutoa katika baraka anazowabariki.
Ili kutukumbusha aliamua Baba wa Imani Awe Ibrahimu sio Yuda Iskariote, Baba wa Uvumilivu na Ibada awe ni Bilionea Ayubu.
Ni hayo tu.