Rudi nyumbani, kumenoga - by TTCL

Rudi nyumbani, kumenoga - by TTCL

Niliacha kutumia Internet ya TTCL mwaka 2008 kutokana na kero zao. Hata hivyo, naamini kero hizo kwa miaka hii hazi-exist manake wakati ule tulikuwa tunatumia dial up modem!

Siku mahali nguzo ikidondoka; hesabu unakaa hata mwezi bila huduma unless uwe kwenye line ya kishua na sio hizi zetu za Uswahilini!

But guess what? Speed niliyokuwa naipata 2008 bado Tigo hawajaifikia kwenye eneo langu hii 2018.

Tatizo kubwa labda kwenye bei zao! Ni wazito sana ku-respond kwenye price war. Wenzao wakiona ushindani umekuwa mkubwa; faster wanatumia pricing weapon ku-win soko! Wasiposhusha bei ya vifurushi basi haraka sana watazindua kifurushi kipya ambacho ni more competitive!

X akizindua kifurushi kipya leo; Y ana-counterattack kesho yake huku TTCL wakibaki pale pale wanapiga usingizi!

Matokeo yake, unaweza kukuta leo hii TTCL ndie mwenye cheapest bundles in the market! Lakin baada ya muda, anakuwa ndie mwenye most expensive bundles in the market na wanabaki hivyo kwa miezi kadhaa kama sio mwaka!

Kinachofuata hapo ni wateja wake kutupa modem kwenye droo na kuhamia kwenye bundle nafuu!

Tena kuna cku hapa niliuliza ikiwa bei za hawa jamaa ni hadi ziwe approved kule juu!

Kama ndivyo, basi wabadilike na kuipa Sales Department uhuru wa kutosha utakaowawezesha kupambana na industry monsters ambao wapo very aggressive sokoni!

TTCL wakiachiwa wajidai na wakapata aggressive sales management team; hawa akina Vodacom cjui Tigo na wenzao wote lazima waombe poo!!
Point natamani kandamba angeona haya madini
 
TTCL wanakula data haraka sana kuliko motandao mingine nilinunua bundle la shs 15000. Nikapata 5GB mchana na 25GB usiku huwezi amani ndani ya siku nne sikuwa na bundle.
Nikaapa sinta tumia ttcl tena.
Siyo kweli Mimi nimtumiaji mzuri Sana wa bundle,huwa na nunua gb 7 kwa elfu 5 na sijawahii kosa kuingia you tube, Instagram,jamii forum na Soma emails daily bundle linaenda moderate kwa speed ya uhakika
 
Point natamani kandamba angeona haya madini
Wanayajua sana tu tatizo lao kufanya ni kuendesha business as usual!!

Nilishawahi kuwaomba kazi hawa jamaa na proposal juu on how I can deliver in sales and customer service!!

Nadhani ile proposal kama haikufungiwa maandazi basi ilitupwa in a dustbin!!

Kwahiyo wanajua sana sema basi tu!! Moja ya mambo ambayo hadi sasa serikali hawajafanikiwa japo nusu, ni ku-inflict corporate culture in government institutions! Kusipokuwa na corporate culture, there will be no business oriented minds! If no business oriented minds; huwezi kupambana na wenzako!!
 
Siyo kweli Mimi nimtumiaji mzuri Sana wa bundle,huwa na nunua gb 7 kwa elfu 5 na sijawahii kosa kuingia you tube, Instagram,jamii forum na Soma emails daily bundle linaenda moderate kwa speed ya uhakika

GB 7 kwa 5000 ni kifurushi cha siku au wiki? mi natumia cha GB 3 kwa 2000 cha wiki
 
Back
Top Bottom