Boss la DP World
JF-Expert Member
- Dec 12, 2021
- 1,997
- 7,552
Morogoro kwasasa si mkoa salama, vitendo vya uporaji kwa kutumia bodaboda vimeongezeka, vikundi vya uhalifu vinasumbua sana katika baadhi ya mitaa na kufanya raia waishi kwa hofu.
Cha ajabu jeshi la polisi limeweka jitihada kubwa kupambana na bajaji, yaani ikifika saa 1 jioni, polisi wenye silaha zamoto huanza kukamata bajaji na kuzipiga faini ya laki 2 kwa kisingizio kuwa haziruhusiwi kuingia mjini.
Cha ajabu ni kwamba ifikapo sa 1 jioni daladala karibu zote huwa zimepaki japo idadi kubwa ya raia bado wanakuwa mjini hivyo vijana wa bajaji hutumia fursa hiyo kujipatia mkate wa kila siku.
Juzi Boss la DP World nilikuwa najaza mafuta (full tank) kwenye sheli moja mjini morogoro, ghafla nikaona purukushani bajaji moja imekosa mwelekeo kumbe askari kaingiza mkono kuizima ili waikamate.
Baada ya kumkamata yule kijana wakampiga kisha gari ikaja wakamchukua, polisi mmoja akawa anaendesha bajaji kuelekea kituoni. Binafsi nilijua labda ni mhalifu nikataka kulipongeza jeshi la polisi kwa kazi mujarab
Kuja kufuatilia naambiwa ni zoezi la ukamataji bajaj na baada ya kufuatilia kwa kina nikabaini ni agizo toka kwa RPC ili kuongeza makusanyo yatokanayo na faini (ubunifu wa kipumbavu kabisa)
BILA SHAKA HUYU RPC AMETUMWA NA MAKONDA KUFANYA HAYA ILI KUTEKELEZA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI.
BAJAJ MOROGORO, MAKONDA AKIFIKA KWENU MUULIZENI KWANINI ANAWAFANYIA HIVYO?
Cha ajabu jeshi la polisi limeweka jitihada kubwa kupambana na bajaji, yaani ikifika saa 1 jioni, polisi wenye silaha zamoto huanza kukamata bajaji na kuzipiga faini ya laki 2 kwa kisingizio kuwa haziruhusiwi kuingia mjini.
Cha ajabu ni kwamba ifikapo sa 1 jioni daladala karibu zote huwa zimepaki japo idadi kubwa ya raia bado wanakuwa mjini hivyo vijana wa bajaji hutumia fursa hiyo kujipatia mkate wa kila siku.
Juzi Boss la DP World nilikuwa najaza mafuta (full tank) kwenye sheli moja mjini morogoro, ghafla nikaona purukushani bajaji moja imekosa mwelekeo kumbe askari kaingiza mkono kuizima ili waikamate.
Baada ya kumkamata yule kijana wakampiga kisha gari ikaja wakamchukua, polisi mmoja akawa anaendesha bajaji kuelekea kituoni. Binafsi nilijua labda ni mhalifu nikataka kulipongeza jeshi la polisi kwa kazi mujarab
Kuja kufuatilia naambiwa ni zoezi la ukamataji bajaj na baada ya kufuatilia kwa kina nikabaini ni agizo toka kwa RPC ili kuongeza makusanyo yatokanayo na faini (ubunifu wa kipumbavu kabisa)
BILA SHAKA HUYU RPC AMETUMWA NA MAKONDA KUFANYA HAYA ILI KUTEKELEZA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI.
BAJAJ MOROGORO, MAKONDA AKIFIKA KWENU MUULIZENI KWANINI ANAWAFANYIA HIVYO?