Rostam Aziz aachia ngazi CCM

Sikushangaa sana kusikia kutoka kwake kuwa amejiuzuru kwa sababu ya kutoathiri biashara yake. Hapo sasa ndo watanzania akili kumkichwa kwa maana ya kwamba yeye alikuwa anaiba na kuwakandamiza watanzania na hakuona hilo kuwa tatizo kwake na lilipokuja kugusa biashara yake basi hapo ndo kope za macho yake alizozigandisha kwa sumaku akaamua kuinasua sumaku na kuona kuwa kuna haja ya kuachia ngazi. To hell he has to go no matter what...naungana na wale wanaosema kwa serikali makini yenye kumbukumbu na yenye kuwajibika huyo jamaa from the time he resigned alitakuwa kukamatwa na kufikishwa kwa pilato fasta. Ila kwa sababu ni serikali ya watu wasioona, wasio na kumbukumbu, irresponsible kama kiongozi wao mkuu, basi atatukuzwa na kukumbukwa kama mfalme na hautapita muda mara unasikia kuwa amekuwa ni mfano wa kuigwa na ameonesha siasa komavu. Hilo atalianza Kikwete walai kabisa na watachukua hatua yake hii kuwa kama changa la macho la kuwaeleza wananchi wenye akili mgando kuwa CCM sasa ni safi na wale waliotuhumiwa wameondoka ilihari chama kizima kimeoza na kinanuka misili ya panya aliyefia ufunguni mwa kitanda.
 
Movie/sinema ndio inaanza,believe me...mwisho wa movie ccm kuchapana fimbo na kuvunjika..time will tell.
 
Amechukua uamzi wa busara maana kila kukicha amekuwa akisemwa hili mara lile ilimradi tu adui zake wametaka kusema, ilipaswa na kuachana na hata chama chenyewe kwani kwa chama kilipofika huwezi kunishawishi kwamba kimepoteza mvuto kwa sababu ya mapacha watatu, ni zaidi ya hapo ccm inapaswa kufanya utafiti wa kutosha
 
Tahadhari, Rostam ndio kascore goli la ushindi, ila watu wanafurahi kama vile RACHEL ndio wamefungwa. Huu mkakati wa kuwavua gamba utaishia KUWASAFISHA mapacha 3. Kumbukeni maneno Rostam aliyomwambid Membe, watatumia mbinu zile zile [walizotumia 2005 kumuingiza kikwete madarakani], kuhakikisha kuwa wanatimiza malengo yao. Wataunda MTANDAO MPYA NJE WAKIWA NJE YA CC na NEC... Ndio wameanza utekelezaji wa mkakati wao. 2014 mtawaona hawa watu kuwa ni mashujaa, mtasema akina Sita waliwaonea 2011
 
Mkuu not assumptions kwenye uongozi na hizi kazi za madaraka you need to be squeaky clean.., harufu yoyote ya rushwa na ufisadi he/she needs to step down na akajaribu kazi nyingine..., try umachinga, barmaid au biashara for all I care. Hapa hatutaki tukushike na ngozi ndio tujue umeiba.., !!!!

if one person calls you a chicken you say maybe they are crazy,
if two people calls you a chicken you start wondering, maybe am a chicken...
if 3 people say you are a chicken you better start laying some eggs...


Kama kila mtu anasema wewe ni Fisadi.... Sure as Hell wewe ni Fisadi


Legal cause is a complex topic, which there is no need nor time to examine here. However, I want to distinguish between that which causes the motivation or intent for committing the act and that which causes the result or harm of the act--namely, the act itself. The former is largely a matter for subjective proof involving the state of mind of the actor; whereas the latter, the act itself and its consequences, is a matter of objective proof. But then again, I wonder if you agree with my earlier question of whether you believe in presumption of innocence or not.




Huu ni ushindi kwa wapambanaji dhidi ya UFISADI (bila kujali chama). Hakuna cha mahakama wala cha nini, mtindo ni mmoja wa magamba kujidondosha yenyewe. Huyu bwana alikuwa ni chief architect wa EPA pamoja na wajukuu zake: KAGODA na MEREMETA ambao walichangia ushindi wa kishindo wa Mhe Dkt Dkt Dkt JK wa 2005. Baadaye akawa chie engineer wa DOWANS binti RICHMOND ambayo imechangia hiki KIZA tunachokishuhudia leo hii. Huyu bwana atapata jahanamu yake hapa hapa duniani!!!

you remind me of the Dark ages and i think you probably belive in this:

war-is-peace-freedom-is-slavery-ignorance-is-strength1.jpg



Kujiuzulu haitoshi, na pesa yetu arudishe!

Hii sinema ndio kwanza inaanza; cdm kaeni mkao wa kula mfadhili anakuja huyo! Najua baada ya hapa ni kufanyiziana mbele kwa mbele, wale waheshimiwa wabunge waliofika hapo walipo kwa msaada wa huyu bwana mkubwa, jitukezeni mhesabiwe ili tumpeleke huyu bepari mbele ya sheria.

we need evidence.....




Ha ha! You say so because you know (CCM) as the accuser have no guts of taking him to court. Your doing good job defending him legally, but you can not change his image (especially politically) to the society, unless he put his effort to do so. If what your saying was applicable in Tanzania no one would bother to burn those vibakas in the street (take matters on their hand). So, although your trying hard to defend him legally here, I doubt if it is worth the effort. I should also remind you; you are in "Jukwaa la Siasa" and not "Jukwaa la Sheria" so that being said your playing soccer in a basketball field.

This type of argument is called an argumentum ad ignorantiam in the logic textbooks, usually translated as the argument from ignorance, or as the appeal to ignorance. Sometimes it is also called lack-of-knowledge inference, negative evidence, or negative proof.

btw

do you believe in presumption of innocence or not?






Yeah, quite true bcoz hakuna mwanaume katika serikali mwenye balls za kumpeleka mahakamani. serekali yote iko fukoni!!!

Actually they don't have evidence to do so
 
Mwanangu Azizi we Jembe nimekukubali, uamuzi wako unaonyesha kweli we ni dume, wasikutishe hao wahuni na Mafisad wa Kichaga wa Chadema wamejaa maneno mengi ukiwachunguza zaidi utagundua fikra na matendo yao yapo kujinufaisha wao kama wachaga na sio jamii ya Tz. Wanaigunga tutakukumbuka sana kwa michango yako ndani na nnje ya Igunga. We gona mic u R Azizi.
Hizo ni Gutter politics kama za Nape
 
[h=4]Topic Information[/h]There are currently 1564 users browsing this thread. (261 members and 1303 guests)



nadhani you guys need a commercial break...

NK1_0002.jpg
 
Lakini, si angeweza kuyasema haya katika paragraph tatu tu. Nimejitahidi kusoma risala nzima naona zimejaa sifa tu za mazuri aliyowafanyia watu wa Igunga, na Watanzania kwa ujumla, lakini hajasema mabaya yeyote aliyoyafanya.
 
Naangalia saivi usiku wa habari, tbc bila chenga, rostam aziz ametangaza kujvua gamba

nawakilisha
 
waliotufikisha kwenye matatizo ya umeme ndiyo hawa,ukijadiri umeme lazma umemgusaa Rostam.Tujadili umeme wakti tumeishazoea giza.Nafikiri watu wana machungu ya kujadili nduli na si tatizo.tutajadili ummeme ijumaa kwani ngereja atawasilisha bajeti ya nishati na madini. mwana magamba yeyote ukigusia la Rostam kubwaga manyanga analeta story tofauti
 
Lakini, si angeweza kuyasema haya katika paragraph tatu tu. Nimejitahidi kusoma risala nzima naona zimejaa sifa tu za mazuri aliyowafanyia watu wa Igunga, na Watanzania kwa ujumla, lakini hajasema mabaya yeyote aliyoyafanya.

huyu katufilisi kaka, kutuibia na kagoda yake,dowans,n.k sihitaji hata kusikia mazuri yake. Jambazi huyu.
 
Kwa upande mmoja inaonekana Rostam Aziz ni "sacrificial lamb". Inabidi tufikirie kapata hasara gani kwa kujiuzulu? Bado ni tajiri mkubwa. Bado ana connections za kisiasa na access kwa viongozi wakuu wa nchi. Inawezekana kapewa kitu mpaka aka kubali kujiuzulu. Kapata hasara gani kwa kuachia nyadhifa hizo? Kiukweli ni haja pata hasara yoyote.

Kwa upande wa pili hili ni jambo la kihistoria. Tunaweza kusema ni kiongozi wa kwanza kujiuzulu kutokana na public pressure. Nani alitegemea "untouchable" kama Rostam Aziz angejiuzulu? Pia hii ina wapa CCM jeuri ya kuongea. Watasema zile siku 90 zimeisha na magamba yameanza kujivua. CCM itatumia hii kama fursa ya kipropaganda kwamba kweli wapo serious.

Ila swali la muhimu zaidi kujiuliza ni je is this too little to late? Je bado wanaweza kuinusuru chama? Kujiuzulu RA kunaisaidia vipi CCM kwa sasa? Time will tell.
 
Naangalia saivi usiku wa habari, tbc bila chenga, rostam aziz ametangaza kujvua gamba

nawakilisha
mkuu wewe uko nchi gani? habari ipo humu tangu kumekucha wewe ndiyo unakurupuka saa hizi!! ajabu sana,,, japo ungesoma vichwa tu vya habari hapa usingeandika hii.
 
Rostam Aziz said:
Mara tu baada ya kumalizika kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ambacho kilichagua wajumbe wapya wa Kamati Kuu na kuidhinisha uundwaji wa Sekretarieti mpya, dhana ya kujivua gamba ambayo naamini Mwenyekiti wetu aliianzisha kwa nia njema ilianza kuenezwa ikichukua tafsiri na mwelekeo tofauti na ule wa awali.

Wajumbe wawili wa Sekretarieti,
Naibu Katibu Mkuu (Tanzania Bara), Mhe. John Chiligati, na Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi, Mhe. Nape Nnauye, walisikika wakitangaza kwamba Halmashauri Kuu ya Taifa ilikuwa imefikia uamuzi wa kuwapa siku tisini wale walioitwa watuhumiwa wanaokabiliwa na tuhuma za ufisadi ndani ya chama kujitoa katika nafasi zao za uongozi vinginevyo watafukuzwa na chama.

Wazee wangu, baada ya kushinikizwa sana na vyombo vya habari wawataje kwa majina wanasiasa waliokuwa wakituhumiwa kwa ufisadi ambao ni wajumbe wa NEC na ambao wanapaswa kujiuzulu nyadhifa zao, wajumbe hao wa Sekretarieti walikwenda mbele zaidi.

Baada ya awali kuwaeleza waandishi wa habari kwamba majina ya watuhumiwa hao yalikuwa yakifahamika kutokana na kuhusishwa katika kashfa tofauti kama zile za Richmond, EPA na ununuzi wa rada, mwishoni viongozi hao walikaririwa wakiyataja majina ya wanasiasa watatu kuwa ndiyo ambao walikuwa wakilengwa na maamuzi hayo.

Wazee wangu, nilishangazwa na kushitushwa na namna porojo na fitina za kisiasa zilivyofinyangwa kwa mara nyingine tena baada ya kusikia jina la mbunge wenu ambaye ni mimi, likitajwa kuwa miongoni mwa yale matatu ya viongozi waliokuwa wakitakiwa eti kupima wenyewe na kisha kuchukua uamuzi wa kujiuzulu nafasi zao za uongozi ndani ya NEC katika kipindi cha siku tisini.

Niliseme hili mapema. Mshangao na mshituko wangu haukusababishwa na kutajwa kwa jina langu, la hasha, bali namna uamuzi halisi wa NEC na hususani dhana nzima ya ‘kujivua gamba’
ilivyoweza kupindishwa na wajanja wachache na kisha kuendeshwa kwa maslahi binafsi ya kikundi fulani cha watu.

Kwa wenye uelewa hii inaitwa Self explanatory ! Nape, soma katikati ya msitari la sivyo utajikuta ligi unayocheza inakuzidi uwezo na vema urudi kichangani ubahatishe chandimu. Rostamu kaweka mezani je, mnataka nini zaidi - kutafuniwa ?

Mnamkumbuka Lowassa wakati akijiuzulu Februari, 2008 ? Kama tatizo ni Uwaziri Mkuu haya ! Akabaki mwanachama mwaminifu na mwaka 2010 akagombea Ubunge kupitia CCM, akapigwa jeki na swahiba wake JK na akashinda kwa kishindo.

Rostamu naye anadai atabaki kuwa mwanachama mwaminifu wa CCM, case closed au ? Kama wana ubavu si wamvue uanachama ? Kweli wajinga ndio waliwao na huko CCM ni maskani yao hasa. Unavua gamba unabaki nalo, sasa umefanya nini !
 
Back
Top Bottom