Rostam Aziz aachia ngazi CCM

Rostam Aziz aachia ngazi CCM

Hapo penye blue sidhani kama was necessary. Unakiabisha hata chama cha Rostam alichokipenda mpaka kuamua kuvua nyadhifa zote lakini kubaki na kadi ya chama. Labda ni kukumbushe tu kuna wachaga muhimu sana ndani ya CCM akiongozwa na mzee Kisima (mshauri mkuu wa chama), Salakana, Mama Mkapa, Waziri Chami, Mama Sumaye, Mama Nsilo Swai etc sijui na wao je wako kujinufaisha wao kama wachaga na sio jamii nzima? Au hili panga la ukabila linakata upande mmoja tu. Hivi kwa lugha hizi za Nape & Co CCM inahitaji kweli majimbo ya Kilimanjaro miaka ijayo?

umewasau waziri Agrey Mwanri na Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Beno Malisa
 
once again jf has proven 2 be reliable source. cause b4 we had alot of dought about dis.


Mkuu ina maana bado ulikuwa Tomaso wa kuamini JF kuwa ni highly reliable and timely source of information?
 
TBC imeonyesha kwa sehemu uamuzi mgumu uliochukuwa na Rostam wa kujivua gamba mh kweli gamba lilikuwa gumu kiasi cha kuanzakuangua kilio mbele ya wapiga kura wake, Tbc wataonyesha habari hiyo ifikapo saa 4 usiku leo,
 
Moods naomba mu i treat hii thread independently.
Kuna Mama mmoja nafahamiana nae,anafanya Kazi CCM (nAFASI KUBWA TU),anasema (Tetesi) kuwa RA kashaanza KUuuza vitu vyake na kuna habar za chini chini kuwa anataka kula zake kona kwenda kusikojulikana.
Ntaendelea kuwa update
 
Tetesi zilizopo mtaani kwa sasa ni kwamba wazee wa ccm wametumwa kumshawishi bwana Rostamu Azizi ili aweze kulejea ktk nafasi ya ubunge kwani wanadai akiondoka ktk ubunge itawapa wakati mgumu sana wana ccm ktk uchaguzi huo mdogo

tusubili lisemwalo lipo na kama halipo laja
 
Nimesoma nimeona jamaa kaachia ni sawa tu lakini najua hii timing anatafutwa Lowasa .Hapa kuna jambo kinakuja but nashangaa wao wanawasafisha Bungeni na huku nje wana wavaa .Rostam hajapokea barua ya kumwambia ajiondoe kashikwa na hasira za kutukanwa na Nape .Hao watu 3 hakuna aliye pewa barua hadi sasa .So CCM wana nini la kuringia ? Wacha aachie na zaidi aende mahakamani .Tunakata kuona kesi ina unguruma .Sifa apewe Chadema si CCM.This is a list of shame so CCM wanasema wameshinda kitu gani ? Only Chadema maana ndiyo waliothubutu .
 
Tatu, nilishangazwa na kushitushwa na ujasiri ambao umekuwa ukioneshwa na baadhi ya viongozi wetu wapya wa Sekretarieti wanaolitaja jina langu na kulihusisha na kile wanachokiita ufisadi ambao hata ukweli wa kimazingira na kihistoria ukiachilia mbali ushahidi wa wazi umeshathibitisha kwamba ni porojo za kisiasa zilizotokana na makovu na matarajio ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 na ule ujao wa 2015.

Napenda kuliweka hili sawa sawa. Uamuzi wangu wa kuachia nafasi zangu zote za uongozi nilizopata kwa tiketi ya CCM haukutokana na wala haumaanishi kukubaliana na shinikizo lililopotoshwa kuhusu azma ya utekelezaji wa dhana ya kujivua gamba, la hasha, bali dhamira ya dhati ya kuachana na siasa hizi uchwara (gutter politics) na kutumia muda wangu kushughulika na biashara zangu.

Aidha, nimefikia uamuzi huo lengo likiwa ni kuwajengea heshima na imani machoni mwa wanachama na wananchi wengine, viongozi wangu ambao na
amini baada ya mimi kujitoa watapata fursa ya kutafakari upya changamoto nyingine mbadala zinazowakabili ambazo msingi wake ni dhamana kubwa walizo nazo za kukiongoza chama chetu na nchi yetu kupitia Serikali yake.
Wakati nachukua uamuzi huu, natambua vyema kwamba, watatokea watu ndani ya chama chetu na nje ambao watafanya kila juhudi kupotosha au kupindisha ukweli kuhusu hatima yangu ya kisiasa baada ya kujiweka kando na kujipa mimi mwenyewe na chama changu fursa ya kutafakari kwa kina majaaliwa yangu na ya nchi yangu katika siku zijazo.


Maswali ni mengi kuliko majibu na hizo siasa za Uchwara ndani ya CCM!!! Tuamini hivi hivi tu kuwa hajapewa barua ya kumtaka ajiviue gamba kabla hajashughulikiwa? Kwa nini ameamua sasa na sio wakati ule alipopigiwa sana kelele? ana hofu ya nini huyu jamaa? Nini kinafuatia kama ameza kuona kuna uchwara ndani ya chama chake mwenyewe ?
 
Vichwa vya JF hivi, hawa wote wamechangia hii habari pasipo kuisoma vizuri ingawa habari inaelezea vyema juu ya yeye kuachia Ubunge hawa bado wanauliza juu ya swali hilo hilo?!
Mkuu ukisikia ''KUKURUPUKA'' ndio huko, wanadandia tu treni bila kujua linatoka wapi linaenda wapi, na hiyo taarifa imeandikwa Kiswahili....ingekua KIINGLISHI??? ......ila nahisi uchangiaji ungepungua coz nani angekua tayali kuonekana KAYUMBA, tena mie ningejibanza na dikshonari yangu kutafsiri, ya kujibu au kuchangia ningeDESA kwa nani??....hahaha!
 
Kazi hii aliianza Slaa miaka kadhaa nyuma .Yeye alikuja Jangwani na List of shame na ndiyo inayo waumiza hawa CCM .Leo hata barua hawajampa barua but kaona maji yako shingoni kajiondoa mwenyewe .CCM wanatangaza ushindi kweli wana akili hawa ?
 
GREAT THINKERS wakiwa cornered,uwezo wa kufikiri hupungua na uanza kupiga blah blah kama the man in the streets-what else can expliain hii MOB JUSTICE inayoendelea kwenye hii thread
 
JK ni nahodha wa meli aayetegema upepo badala ya yeye kuongoza.

Haya mambo yasingetokea kama JK angewaambia wanamagamba wenzake kishakaji kuwa kaeni pembeni. 2010. Sasa aibu na adha ya kujiuzulu inazidi kuipa nyingi point CDM na vyama vya upinzani.

JK na CCM wanapiga deki nyumba kwa kutumia matope.

Vile vile JK is not in control au kwa sbabau anazojua yeye hataki kuonekana yeye ni naodha. wa hii meli inapelekwa na upepo
 
Maswali ni mengi kuliko majibu na hizo siasa za Uchwara ndani ya CCM!!! Tuamini hivi hivi tu kuwa hajapewa barua ya kumtaka ajiviue gamba kabla hajashughulikiwa? Kwa nini ameamua sasa na sio wakati ule alipopigiwa sana kelele? ana hofu ya nini huyu jamaa? Nini kinafuatia kama ameza kuona kuna uchwara ndani ya chama chake mwenyewe ?


Hivi wandugu hamsomi hiyo hotuba vizuri? Kwa kifupi makampuni ambayo ana hisa nayo yalishamwambia kuwa kuchafuliwa kwake kunashusha uaminifu na mapato ya makampuni hayo na kwamba kama hayuko tayari kujivua gamba basi hisa zake zote zitauzwa ili kunusuru mustakabari wa makampuni hayo yakiwemo yale ya nje ya nchi
 
Folks,

1. Do not copy the whole speech when quoting or responding to one part of the speech. Just copy or quote what you want to respond to. All members have an equal access to the full speech in the first post.

2. Do not copy the names of the members visiting the thread, be it one or 1000; all members have the same access to see the names and the number of people visiting the thread.

If you somebody contravene the above he/she will face a ban - no explanation will be given. We have to consider that quite a good number of our members visit the site through mobile devices.

For Admin.
Umeeleweka, however kuna wengine utawahukumu kwa kutosoma post yako au kutofungua page ya post hii kwa sababu si kila mtu anafungua pg zote au anasoma post zote, lakini umeeleweka.
 
Hongera rostam kwa kuonesha njia,huo ndio uamuzi wa busara,nchi yetu ingepiga hatua kama tungekua na utaratibu wakuachia ngazi kama huu,
 
Yangu macho...nataka kuuona mwisho wa hao wanaoitwa magamba na msitakabali mpya wa ccm. EL naye atafuata nini? si nasikia wameamriwa kujivua magamba
 
Back
Top Bottom