Rostam Aziz aachia ngazi CCM

Rostam Aziz aachia ngazi CCM

Nimeisoma Hotuba ya Rostam na kuitafakari vizuri sana hatma ya maamuzi yake...
Bila shaka yaonyesha kazi nzuri imefanywa na Uongozi mpya ambao kwa mchezo wa Kibongo wamemzunguka Rostam na wenzake. Hongera Chiligati na Nnauye, hakika leo nimewaaminia kwa kazi yenu kutokana na kauli za Rostam kushangazwa na maamuzi ya uongozi mpya wa chama.

Sina uhakika kama aloyasema yote ni ya kweli lakini kama kweli amejiuzuru bila kupenda na kamalizia kwa maneno haya:- Napenda kuliweka hili sawa sawa. Uamuzi wangu wa kuachia nafasi zangu zote za uongozi nilizopata kwa tiketi ya CCM haukutokana na wala haumaanishi kukubaliana na shinikizo lililopotoshwa kuhusu azma ya utekelezaji wa dhana ya kujivua gamba, la hasha, bali dhamira ya dhati ya kuachana na siasa hizi uchwara (gutter politics) na kutumia muda wangu kushughulika na biashara zangu.


Hapa ndipo napomalizia na kusema JK kweli msanii maana kawazunguka Boyz 2Men, na mwisho wa siku kawaondoa wote na kabakia pekee mjengoni. Lakini kwa kumtahadharisha tu afahamu kwamba kazi ya kummaliza yeye kama wale waliotangulia na kuandika historia mpya nchini NDIO INAANZA RASMI!. Nyoka kujivua gamba sii hoja, sumu yake inabakia palepale. Hivyo, ukitaka kumuua nyoka lenga kichwa! na waganga wa kienyeji wanasema - Sumu ya nyoka hutibiwa na magamba yake!.
What next! yangu machoo....

Mkandara maneno hayo mazito na hakika yanakuja ila unapoyatoatoa hapa jf unayakwamisha maana yana maslahi kwa taifa.
 
Ndugu zangu this is for the great thinkers lakini mbona tunafanya vitu kama vya watoto wa std 1, hebu angalieni vema quote ya para ya pili Rostam amejivua nyadhifa zote za kisiasa pamoja na Ubunge wa jimbo la Igunga. hebu tuwe makini katika issues kwa kuzisoma na kuzielewa vema.
natumaini nimeeleweka. Let us wait and see for others....................
 
Afadhali labda sasa New Habari corporation wataanza kuandika issues za maana wataachana na gutter politics.
 
Huyu bwana kaachia ngazi chamani na ccm kama changa la moto jamani, huyu jamaa kajipanga kututafuna zaidi kama nchi bila kelele za kufatwa fatwa na vyombo vya habari au ccm wenzake.
My take na angalizo muhimu sana kufatilia:
  • Sasa ndo tutaliwa ipasavyo na huyu bwana kama hatua za kumkamata na kumfungulia mashtaka hazitafanywa
  • Naomba ufanyike ufatiliaji kama ile hela ya tozo la dowans imeshalipwa kwani yawezekana huyu jamaa kashapewa chake
  • Kashfa zote zinazomhusu huyu jamaa sasa ndo wakati muafaka wa kuanza ku deal nazo kwani hana wa kumkingia kifua
  • Kuna jamaa mkenya anaitwa Stanley alikuwa anazungumzwa sana wakati wa dowans, kwa taarifa yenu tu huyu Stanley mkenya sasa hivi ni Executive director wa Symbion (iliyokuwa dowans).........
  • This is food for your thought guys, work on it!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kwa upande mmoja inaonekana Rostam Aziz ni "sacrificial lamb". Inabidi tufikirie kapata hasara gani kwa kujiuzulu? Bado ni tajiri mkubwa. Bado ana connections za kisiasa na access kwa viongozi wakuu wa nchi. Inawezekana kapewa kitu mpaka aka kubali kujiuzulu. Kapata hasara gani kwa kuachia nyadhifa hizo? Kiukweli ni haja pata hasara yoyote.

Kwa upande wa pili hili ni jambo la kihistoria. Tunaweza kusema ni kiongozi wa kwanza kujiuzulu kutokana na public pressure. Nani alitegemea "untouchable" kama Rostam Aziz angejiuzulu? Pia hii ina wapa CCM jeuri ya kuongea. Watasema zile siku 90 zimeisha na magamba yameanza kujivua. CCM itatumia hii kama fursa ya kipropaganda kwamba kweli wapo serious.

Ila swali la muhimu zaidi kujiuliza ni je is this too little to late? Je bado wanaweza kuinusuru chama? Kujiuzulu RA kunaisaidia vipi CCM kwa sasa? Time will tell.
Wewe umeangalia upande mmoja tu wa faida hujaangalia kuwa kwenye biashara yeyote huwa kuna hasara, isome tena barua yake read between the lines utaona ana kinyongo na watu fulani na hicho kinyongo ndio upande ambao hujauona.
 
hv kwa watanzania wa leo na wanavyo ona mambo yanayo fanywa na chadema bungeni kweli wanaweza kuipa ccm chance ya kulishika jimbo la igunga tena? Chadema mjipange vyema kuchukua jimbo akuna lisilowezekana
 
Jamaaa anadai anaachia na ubunge sijui kama inawezekana kwa akina magamba,hapa kuna mchezo mchafu unapangwa kuwapoteza wadanganyika! Naamini hivi coz hii siyo kawaida kwa mtu kuachia ubunge tena akitoka chama cha magamba,hii haiwezekani!
 
Huyu bwana kaachia ngazi chamani na ccm kama changa la moto jamani, huyu jamaa kajipanga kututafuna zaidi kama nchi bila kelele za kufatwa fatwa na vyombo vya habari au ccm wenzake.
My take na angalizo muhimu sana kufatilia:
  • Sasa ndo tutaliwa ipasavyo na huyu bwana kama hatua za kumkamata na kumfungulia mashtaka hazitafanywa
  • Naomba ufanyike ufatiliaji kama ile hela ya tozo la dowans imeshalipwa kwani yawezekana huyu jamaa kashapewa chake
  • Kashfa zote zinazomhusu huyu jamaa sasa ndo wakati muafaka wa kuanza ku deal nazo kwani hana wa kumkingia kifua
  • Kuna jamaa mkenya anaitwa Stanley alikuwa anazungumzwa sana wakati wa dowans, kwa taarifa yenu tu huyu Stanley mkenya sasa hivi ni Executive director wa Symbion (iliyokuwa dowans).........
  • This is food for your thought guys, work on it!!!!!!!!!!!!!!!!!

Hii inawezekana kabisa,dili la kuuza Dowans limetiki,kakamata Billion 90,hata ingekuwa shetani angejiuzulu! Ukijumuisha na pesa za mauzo ya Dowans lazima anapesa kama akina Beckam,huku akijua mbwa wetu wote koko hana wasiwasi wa maisha tena!
 
Jamani someni vizuri, mbona ametangaza kuachia ujumbe wa NEC, ubunge pamoja na nyadhifa zoote alizozipata kupitia CCM bali atabaki na kadi tu kama mwanachama wa CCM........
 
Thanks MMKJ nilikuwa sijawahi sikia sauti ya Rostam! Kumbe jamaa kiswahili kinapanda vizuri tu!
 
kidumu chama cha mapinduzi,,,,,,,,,,,haibu yenu,mnajua kushumu lakin midomo inanuka.haya kurupukeni na lingine sasa 2015 CCM OYEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE
 
Huyo sisi tunaye tu hata angejivua ngozi amekula chetu lazima arudishe!!
 
Yeye ni mfanya biashara wa ndani na nje huivyo anataka kuendelea na biashara zake. Ni zipi hizo?? Si huyu ambaye hamna hata chembe ya jina lake brela? Anafanya biashara kimiujiza?
 
Back
Top Bottom