Riwaya: Ufukwe wa Madagascar

Riwaya: Ufukwe wa Madagascar

Akhsante mwamba!

Hapa nasubiri nijue Amanda na wenzake walifanyaje baada ya kukuta gari lao halipo!

Mwandishi angekuwa anatupa na matukio ya upande wa pili badala ya kuegemea upande mmoja tu

Sio vizuri tukaja kushtuka Amanda anakutana na tibba kwenye mission bila kuambiwa alitoka tokaje huko mtoni!


Otherwise story imesimama, Hongera sana kwa mtunzi!
 
RIWAYA: UFUKWE WA MADAGASCAR
SEHEMU: 36
Mtunzi:Kelvin Mponda

...akishuka kwenye ile lifti atoke kisha nikaingia mle ndani na kubonyeza kitufe ukutani nikiiamuru ile lifti inifikishe ghorofa ya tano ya lile jengo. Mlango ulipojifunga ile lifti ikaanza kupanda juu na wakati ule mawazo mengi yakawa yakipita kichwani mwangu.
Nilianza kwa kukumbuka mambo yote yaliyojili tangu siku ile ya kwanza nilipoondoka jijini Dar es Salaam nchini Tanzania kuja pale Bujumbura nchini Burundi. Kisha nikamkumbuka yule msichana mrembo wa ajabu aitwaye Amanda niliyesafiri naye kutoka jijini Kigali nchini Rwanda namna alivyonisaliti kwa wale wanajeshi na kugeuka mwiba mchungu katika safari yangu. Nikiwa katikati ya mawazo yale nikamkumbuka Hidaya kabla ya mawazo yangu kuhamia tena kwa yule mtu aliyejitambulisha kwangu kwa jina la Jean-Baptiste Nibizi muda mfupi kabla ya kuuwawa kwa risasi kwenye ukingo wa ule mto mkubwa kando ya daraja la barabara ielekeayo mbali na jiji la Bujumbura.
Hatimaye mawazo yangu yakahamia nyumbani kwa Balozi Adam Mwambapa muda mfupi uliopita nikikumbuka namna nilivyopambana na lile jitu hatari na hatimaye kuchomoka na ushindi mwembamba katika pambano la kukata na shoka. Mwishowe mawazo yangu yakahamia kwa yule kijana mfanyakazi wa nyumbani kwa Balozi Adam Mwambapa aliyejitambulisha kwangu kwa jina la Sundi. Kitendo cha kumkumbuka Sundi kikayapelekea mawazo yangu yaweke nanga kwenye mjadala mzito juu ya Padri Aloysius Kanyameza.
Kitendo cha ile lifti kugota haraka kikayarudisha mawazo yangu mle ndani na hapo nikashtukia kuwa tayari nilikuwa nimefika kwenye ghorofa ya tano ya lile jengo la New Parador Residence. Mlango wa kile chumba cha lifti ulipofunguka nikalitengeneza vizuri koti langu na kutoka nje.
Sasa nilikuwa nimetokezea kwenye korido pana iliyomezwa na utulivu wa aina yake. Korido ile ilikuwa ikipakana na milango mingi ya vyumba kwa upande wa kushoto na kulia. Nikasimama kidogo nikiichunguza korido ile kwa utulivu. Katikati ya ile korido kulikuwa na kitufe kikubwa chekundu cha kengele ya hatari pembeni ya mtungi mkubwa wa gesi ya kuzimia moto wa dharura. Kwenye dari ya korido ile kulikuwa na taa ndefu za tubelight za mtindo wa kupendeza zilizokuwa zikiangaza mwanga wa wastani katikati ya korido ile na hivyo kuyafanya mandhari yale tulivu yapendeze. Lile jengo lilikuwa kubwa hivyo na ile korido nayo ilikuwa ndefu kiasi kwamba sikuweza kuona mwisho wake vizuri.
Hatimaye nikaanza kutembea taratibu nikiichunguza kwa makini milango yote iliyokuwa ikitazamana na ile korido. Juu ya ile milango kulikuwa na vibao vidogo vya rangi ya kijivu vilivyokuwa na utambulisho wa namba ya chumba husika. Nikaendelea kutembea taratibu kwa utulivu huku nikiyatembeza macho yangu huku na kule kutazama zile namba milangoni. Haikuwa hadi pale nilipofika katikati ya korido ile upande wa kulia ndiyo nikauona mlango wenye kibao kilichochongwa vizuri namba 302.
Kwa sekunde kadhaa nikasimama nikiutazama mlango ule kwa makini. Jambo moja lilinishangaza kidogo huku nikijiuliza kama kweli ule mlango ulikuwa ni wa kuelekea ofisini kwa meneja wa ile hoteli kwa nini hapakuwa na utambulisho wowote pale mlangoni unaoelezea kuwa ile ni ofisi ya meneja wa ile hoteli?. Huku nikiendelea kujiuliza kwa nini ofisi ya meneja wa hoteli kubwa kama ile iwekwe ghorofa ya tano ya lile jengo badala ya kuwekwa ghorofa ya chini ambapo ndiyo ingelikuwa rahisi zaidi kufikiwa na wateja wanaohitaji huduma. Nikaendelea kujiuliza pasipo kupata majibu hata hivyo muda haukuwa rafiki kwangu hivyo hatimaye nikausogelea ule mlango na kubofya kitufe kidogo cha kingele kilichokuwa kando yake.
Ulipita muda mrefu pasipo mwitikio wowote wa kutoka ndani ya kile chumba na hali ile ikanisukuma nisogee tena pale mlangoni na kubofya kile kitufe cha kengele. Mara moja tu kengele ile ilipoanza kuita tena mara nikauona ule mlango ukifunguliwa taratibu na mbele yangu akasimama mwanaume mmoja mfupi mwenye sura ya umbo duara, macho makubwa, pua ya kibantu na mdomo wenye kingo pana uliozungukwa na ndevu zilizokatiwa vizuri. Mwanaume mfupi na mnene mwenye kitambi cha ukwasi huku amevaa suti ya kodrai ya rangi ya udongo, shati la rangi ya kijivu na tai nyeusi shingoni. Nilipomchunguza vizuri mtu yule nikaridhika kuwa alifaa kuitwa meneja wa hoteli ile kwa namna ya haiba yake. Tabasamu hafifu la kirafiki likaanza kuumbika usoni na hapo yule mtu akavunja ukimya akinikaribisha na nilipomtazama nikagundua kuwa umri wake haukwenda mbali zaidi ya miaka arobaini.
“Bien venu Monsieur et tu as de la chance, parceque je me préparer a quitté le bureau”. Karibu sana ndugu, tena una bahati sana maana ndiyo nilikuwa najiandaa kufunga ofisi. Yule mtu akanikaribisha kiungwana na wakati nikiingia mle ndani akanipa mkono na tabia yake ile ya ukarimu ikawa imenivutia sana. Ule mlango nyuma yangu ukafungwa.
“Merci beaucoup”. Ahsante sana. Nikaitikia kwa furaha huku nikipiga hatua zinazopwaya ndani ya ofisi ile ngeni kabisa machoni mwangu huku taratibu nikiyatembeza macho yangu kutazama mandhari ya ile ofisi.
Ilikuwa ofisi kubwa yenye mandhari tulivu ya kuvutia. Upande wa kulia kulikuwa na kiti kikubwa cha sofa nyuma ya meza kubwa ya ofisini yenye majalada mengi yaliyopangwa moja juu ya lingine, bendera ndogo ya mezani ya taifa la Burundi, kidau cha wino, mhuri, kompyuta moja ya mezani na simu ya mezani pembeni yake. Kando ya ile meza kulikuwa na kabati kubwa la mbao lenye nyaraka za kiofisi kando ya sefu moja ya chuma.
Nikaendelea kuyatembeza macho yangu taratibu mle ndani na kwa kufanya vile upande wa pili wa ile ofisi nikaliona dirisha kubwa ukutani likiwa limefunikwa kwa mapazia mawili marefu. Upande wa kushoto wa ile ofisi kulikuwa na seti moja ya makochi mazuri ya sofa nyuma ya meza fupi ya kioo yenye ua zuri juu yake na pembeni ya makochi yale ukutani kulitundikwa runinga pana flat screen iliyofungwa sistimu ya nzuri mziki. Nilipotazama kwenye kona moja iliyokuwa upande wa kushoto wa ile ofisi nikauona mlango na hapo nikahisi kuwa ule ulikuwa ni mlango wa kuelekea sehemu ya maliwato ya ile ofisi ingawa sikuwa na hakika ya moja kwa moja hata hivyo ule mlango ulikuwa umefungwa. Ofisi ilikuwa nzuri na yenye mandhari ya kisasa yaliyonogeshwa na hewa nzuri ya kiyoyozi kilichokuwa mle ndani. Sakafuni kulikuwa na zulia zuri la rangi ya chanikiwiti lenye manyoya laini ya kupendeza. Nilipochunguza vizuri kando ya dirisha kubwa la mle ndani nikakiona kipoza maji.
“Sʾil vous plais, assaiez-vous”. Tafadhali karibu uketi. Yule meneja wa hoteli akanikaribisha niketi kwenye kochi moja la mle ndani baada ya kuniona nikisitasita huku yeye akizunguka na kwenda kuketi kwenye kile kiti cha ofisini kilichokuwa nyuma ya ile meza yake ya utukufu.
“Merci”. Ahsante. Nikashukuru na kwenda kuketi kwenye kochi moja la sofa la mle ndani lililokuwa karibu na ile meza ya ofisini. Kitambo kifupi cha ukimya kikapita huku nikiutumia muda wangu kuyazoea vizuri mandhari yale na hali ile ya ukimya ilipokuwa mbioni kushika hatamu nikavunja ukimya baada ya kukohoa kidogo kusafisha koo langu.
“Jʾai besoin de voir le directeur de cet hôtel, sans doute cʾest toi”. Nahitaji kuonana na meneja wa hii hoteli, bila shaka ndiyo wewe. Nikaongea kwa utulivu huku nikimtazama yule mtu mfupi mbele ya kile kiti cha ofisi.
“Cʾest moi”. Ndiyo mimi. Yule mtu akaitikia kwa utulivu pasina mashaka yoyote kisha akakohoa kidogo kusafisha koo lake kabla ya kuendelea.
“Je mʾappelle Monsieur Vital Desire Habonimana, le directeur de cet hôtel. Quel est votre nom?. Naitwa ndugu Vital Desire Habonimana, meneja wa hoteli hii. Jina lako nani?. Yule mtu mfupi akamaliza kujitambulisha huku akinikodolea macho nami nikakohoa kidogo kabla ya kuvunja ukimya.
“Je mʾappelle James Lusungu Iʾofficié de Iʾembassade de Tanzanie ici à Bujumbura. Je vous savoir si le jour avant hier notre ambassadeur a arrivé ici à Iʾhôtel partucipé à la reunion”. Naitwa James Lusungu, afisa wa ubalozi wa Tanzania hapa Bujumbura. Nataka kufahamu kama juzi balozi wetu alifika hapa hotelini kwako kuhudhuria mkutano”. Nikadanganya kwa kujiamini huku nikimtazama yule mtu kwa makini. Kitambo kifupi cha ukimya kikapita huku yule mtu mfupi akinitazama kwa utulivu kama anayefikiria jambo fulani pasipo kuonesha tashwishwi yoyote usoni mwake halafu baada ya kuitazama saa yake ya mkononi akavunja tena ukimya.
“Pourquoi ne pas rentre au bureau et demande cette question aupès de votre ambassadeur?”. Kwa nini usirudi ofisini na kumuuliza Balozi wako swali hilo?. Maelezo ya yule mtu yakanishangaza na haraka nikagundua kuwa kulikuwa na namna fulani ya jeuri katika maelezo yake tofauti kabisa na wakati ule alipokuwa akinikaribisha mle ndani muda mfupi uliopita. Hata hivyo kwa kuwa tayari nilikuwa ndani ya ofisi yake tena nikiwa na haja yangu binafsi nikaamua kujipa uvumilivu huku nikilazimisha tabasamu la kirafiki usoni mwangu.
“Notre ambassadeur maintenant il est en voyage vers Dar es Salaam Tanzania”. Balozi wetu sasa hivi yuko safarini anaelekea Dar es Salaam Tanzania. Nikaongea kwa kujiamini huku nikidanganya na hapo yule mtu mfupi akaangua kicheko cha ghafla kilichonishangaza na kuniacha kwenye mduwao wa aina yake. Kicheko kile kilipofika ukomo yule mtu akaongea kwa utulivu kama mtu aliyefyatukwa na akili kichwani.
“Un homme adulte comme toi, tu nʾas pas honte de tromper?”. Mtu mzima kama wewe hivi huoni aibu kudanganya?.
Maelezo ya yule mtu mfupi meneja wa hoteli ile yakanipelekea nihisi kuwa huwenda nilikuwa nikifahamika vizuri na mtu yule kuliko vile nilivyokuwa nikidhani. Hata hivyo nikapiga moyo konde na kumeza funda kubwa la mate kuitowesha hofu moyoni mwangu huku dalili zikiashiria kuwa mambo hayakuwa shwari tena mle ndani.
“Donc toi, tu connais là où est Iʾembassadeur Adam Mwambapa?’’. Kwa hiyo wewe unafahamu mahali alipo Balozi Adam Mwambapa?. Nikamuuliza yule mtu kwa jazba kidogo. Yule mtu akacheka tena huku akijishika kidevu chake kifahari kabla ya kuniuliza.
“Tu veus savoir là où est votre embassadeur ou tu veus savoir si le jour avant hier il a partucipé à la reunion ici à Iʾhôtel?”. Unataka kufahamu mahali alipo balozi wako au unataka kufahamu kama juzi alihudhuria mkutano hapa hotelini?.
“Les tout” Vyote. Nikamjibu kwa jazba.
“Ne te trompes pas camarade en pensant quʾ on est te connait pas qui tu es”. Usijidanganye komredi ukidhani kuwa hatukufahamu vizuri kuwa wewe ni nani”. Yule mtu mfupi akaniambia huku akiangua kicheko hafifu cha dhihaka.
“Je ne comprends pas, tu parles quoi?”. Mbona sikuelewi unaongea nini?. Nikamuuliza yule mtu kwa hasira za kudhihakiwa.
“Bien venu camarade jʾai pensé que tu sera encore malin et echaper à cet obstacle”. Karibu sana komredi nilidhani kuwa mara hii ungekuwa mwerevu kuruka kiunzi hiki. Sauti kavu ya kiume kutoka nyuma yangu ikazungumza kwa utulivu hali iliyonishtua na kunipelekea nigeuke haraka kutazama nyuma yangu na kwa kufanya vile nikajikuta nikitazamana na mdomo wa bastola yenye uchu aina ya Type 64 Silenced iliyofungwa kiwambo maalum cha kuzuia sauti. Moyo wangu ukapiga kite kwa nguvu kisha kijasho chepesi kikaanza kunitoka sehemu mbalimbali mwili wangu.
Sasa nilikuwa na hakika kuwa nilikuwa nimejiingiza kwenye himaya ya adui pasipo kujua na pale ndiyo nikafahamu kwanini yule mtu mfupi mbele yangu aliyejinadi kuwa ni meneja wa ile hoteli alikuwa akiongea kwa kujiamini sana ule muda mfupi uliopita. Jambo la kushangaza zaidi ni kuwa ile bastola nyuma yangu ilikuwa imeshikwa na yule kijana wa mapokezi ya ile hoteli aliyekuwa akifuta glasi kwa kile kitaulo kidogo wakati ule nilipokuwa nikiingia kwenye ile hoteli kati ya wale vijana wawili wahudumu wa ile hoteli waliokuwa ile sehemu ya mapokezi kule chini. Yule kijana aliyenishikia bastola nyuma yangu bado alikuwa katika sare zake za kazi huku usoni akitengeneza tabasamu jepesi la ushindi wenye dhihaka na kejeli.
Kwa kweli sikuwa nimetarajia kabisa kuwa vijana wale niliowakuta kule sehemu ya mapokezi ya ile hoteli kuwa walikuwa ni mamluki waliopandikizwa eneo lile kwa ajili ya kufanikisha mpango wa kuninasa. Mara moja nikakumbuka namna vijana wale walivyokuwa wakitazamana wakati nilipokuwa nikizungumza nao kule chini sehemu ya mapokezi ya ile hoteli na hapo nikagundua kuwa kumbe kulikuwa na jambo lililokuwa likiendelea baina yao dhidi yangu.
Hata hivyo sikuweza kuelewa ni kwa namna gani yule kijana aliyenishikia bastola nyuma yangu alikuwa amefanikiwa kuingia mle ndani pasipo kufanya kelele yoyote ya kunishtua. Hisia zangu zikanitanabaisha kuwa nilikuwa nimekutana na watu hatari na professional katika harakati za kijasusi. Nikapiga moyo konde na kumeza funda kubwa la mate kuupoteza mshtuko mkubwa usoni mwangu kisha nikageuka na kumtazama yule mtu mfupi mbele yangu aliyejinadi kwangu kuwa ndiye meneja wa ile hoteli kisha nikavunja ukimya.
“Quelle obstacle?”. Kiunzi gani?. Nikauliza kwa kujiamini ingawa haraka niligundua kuwa sauti yangu ilikuwa imeanza kupwaya. Swali langu likaibua kicheko kingine cha ghafla kwa wale watu ingawa sikuweza kufahamu hasa ni kitu gani kikubwa katika swali lile kilichowapelekea wale watu waangue kicheko cha ghafla vile kama makahaba waliohongwa bia kaunta. Kicheko kile kilipokoma yule mtu mfupi mbele yangu akavunja ukimya na kuanza kuongea huku akinitazama kwa makini na nilipoyachunguza macho yake nikagundua kuwa hayakuwa na huruma hata kidogo.
“Premier jʾaimerais tʾappelle Tibba Ganza, et non tes noms de massonge les quels tu utilises pour depasser les frontierres de nos pays”. Kwanza ningependa kukutambua kama Tibba Ganza na siyo hayo majina yako ya uongo unayoyatumia kwa ujanja kuvuka mipaka ya nchi zetu. Yule mtu mbele yangu akaongea kwa hakika huku akionekana kuwa na taarifa nyingi juu ya nyendo zangu hali iliyonipelekea nihisi kuwa wale watu walikuwa na ushirika mmoja na Amanda. Hivyo sikuwa tena na shaka kuwa hata taarifa zangu walikuwa wamezipata kutoka kwake...ITAENDELEA
 
RIWAYA: UFUKWE WA MADAGASCAR
SEHEMU: 37
Mtunzi:Kelvin Mponda

“Si tu nʾas pas des reponses, alors laisser moi partir”. Kama huna majibu basi wacha mimi niondoke. Nikamwambia yule mtu mfupi mbele yangu huku nikifahamu fika kuwa tayari usalama wangu ulikuwa mashakani na hivyo nilipaswa kuwa makini sana na watu wale. Nikaanza kusimama nikitaka kuondoka hata hivyo sikufanikiwa kwani yule kijana nyuma yangu akanizaba makofi mawili ya nguvu kichwani kisha akamalizia kwa kunitandika ngumi moja ya mbavuni iliyonirudisha chini niendelee keti pale kwenye lile kochi kwa mkono wake mmoja uliokomaa kama mbao ya mninga.
“Resté comme ça toi singe et nʾose pas de bouger”. Tulia hivyo hivyo wewe tumbili na usidhubutu kujitikisa. Yule kijana mwenye sare za mhudumu wa hoteli ile nyuma yangu akanionya na kwa kweli maumivu ya kile kipigo chake yalikuwa makali mno mwilini. Masikio yangu yakawa yakisikia sauti kali ya mvumo huku maumivu ya mbavu zangu yakinifanya niheme juu juu. Tukio lile likampelekea yule mtu mbele yangu aangue tena kicheko cha dhihaka kilichosindikizwa na mluzi mwepesi. Hatimaye nikamuona yule mtu mfupi akiingiza mkono wake mfukoni na kuchukua sigara kutoka katika pakiti. Alipoitia ile sigara mdomoni akajiwashia kwa kibiriti chake cha gesi na kuvuta mapafu kadhaa na kisha kuupuliza moshi wake angani tukio lililoonekana kumfurahisha sana. Hatimaye akuvunja ukimya.
“Ne te trompe pas camarade tu vas nullpart. Nous etions etrer dʾattendre cette chance pour lontemps et on ne peut pas le laisser faire encore’’. Usijidanganye komredi kwani huwendi popote. Tumekuwa tukiisubiri hii bahati kwa muda mrefu na hatuwezi kuichezea tena.
“Qui etes-vous et vous avez quel problème avec moi?”. Ninyi ni akina nani na mna shida gani na mimi?. Nikawauliza wale watu kwa jazba na hapo nikamsikia yule mtu mfupi mbele yangu akinijibu kwa msisitizo.
“Cʾest mieu de ne pas nous connaître”. Ni afadhali usitufahamu.
“Je pense que vous avez la confision”. Nahisi mmechanganyikiwa. Nikawaambia wale watu kwa hasira na kabla sijamaliza kuongea yule kijana nyuma yangu akanitandika ngumi mbili za mgongo zilizonipelekea nihisi maradhi ya kichomi cha mbavu. Kwa kweli nilisikia maumivu makali mno yaliyonipelekea niheme ovyo huku yule kijana nyuma yangu akanivua lile koti langu na kuanza kunipekua. Alipomaliza akawa amefanikiwa kuipata ile bastola yangu iliyokuwa mafichoni tukio lile likampelekea atabasamu kabla ya kunizaba kofi moja la nguvu usoni kiasi cha kunifanya nione maruweruwe mbele yangu.
“Tu as parvenu à nous echapé deux fois, mais cʾest ne pas ce tour”. Ulifanikiwa kututoroka mara mbili lakini siyo sasa hivi. Yule kijana nyuma yangu akanionya huku akinisukasuka ovyo kwa mkono wake shingoni na kwa kweli kitendo kile kiliniudhi sana hata hivyo nilijipa uvumilivu.
“Dis nous camarade, où arrive votre travail?”. Tuambie komredi kazi yako imefikia wapi?. Yule mtu mfupi mbele yangu akaniuliza huku akikungʾuta majivu ya sigara yake kwenye kibakuli kidogo cha majivu ya sigara kilichokuwa juu ya ile meza ya ofisini.
“Vous mʾavez donné quelle travail ou bien vous avez la confision?” Kazi gani mliyonipa au mmechanganyikiwa?. Nikamuuliza yule mtu mfupi mbele yangu huku hasira zimenipanda na kwa kweli utulivu wa nafsi ulishapotea kabisa moyoni mwangu. Muda uleule mara nikamuona yule mtu mfupi aliyeketi kwenye kile kiti cha ofisini mbele yangu akisogeza kile kiti nyuma na kusimama kisha akapiga hatua zake hafifu kunikaribia pale kwenye kochi nilipoketi. Alipofika akanipulizia moshi wake wa sigara usoni kisha ghafla akanitandika ngumi mbili za tumbo huku akitabasamu kama hayawani. Maumivu makali yakasambaa mwilini mwangu na nilipomtazama usoni yule mtu nikaliona tabasamu lake la kinyama namna lilivyochanua.
“Dis nous quʾest ce que tu es venu faire ici au Burundi?”. Tuambie umefuata nini hapa nchini Burundi?.
Tukio lile likanipelekea nimkate jicho kali la hasira yule mtu huku nikitamani kusimama na kumtia adabu. Hata hivyo nafsi yangu ilinionya pale nilipoukumbuka ule mdomo wa bastola nyuma yangu namna ulivyokuwa ukitazamana na kisogo changu kwa uchu. Hivyo nikaamua kujipa utulivu.
“Soyez vigilant je pense que vous avez la confision et la personne que vous cherchez cʾest ne pas moi’’. Hebu kuweni makini nahisi mmejichanganya na mtu mnayemtafuta siyo mimi. Nikawaambia wale watu huku lengo langu likiwa ni kuzidi kuununua muda, kujitoa hatiani lakini vilevile kuipa akili yangu utulivu katika kufikiria nini cha kufanya ili kujinasua katika mtego ule.
“Dʾaccord, parceque tu ne veu pas nous dire de ta volonté, alors nous allons tʾa mainer là où on va tʾobliger de parler”. Okay, kwa kuwa hutaki kutuambia kwa hiari yako basi tunakupeleka sehemu utakayolazimishwa kutuambia. Yule mtu mfupi mbele yangu akaniambia kwa dhihaka.
“Où est-ce que vous mʾamainer?”. Mnanipeleka wapi?. Nikamuuliza yule mtu mfupi kwa shauku.
“Attends, dans peu de temps tu vas voir”. Subiri muda siyo mrefu utaona. Yule mtu mfupi mbele yangu akiniambia huku akiirekebisha vizuri tai yake shingoni na kupitia maelezo yake nikafahamu kuwa alikuwa akimaanisha alichokuwa akikiongea. Sikutaka kuendelea kusubiri kwani nilifahamu fika nini ambacho kingefuatia baada ya pale. Hivyo kufumba na kufumbua nikageuka kwa pigo moja makini la kareti lililoipokonya vizuri bastola ya yule kijana nyuma yangu huku nikitupa teke farasi maridadi nyuma yangu lililomtupa vibaya yule kijana nyuma yangu kwenye ile meza ya ofisini na kumbwaga kama gunia. Yule kijana akanitukana tusi zito huku akinilaani kwa shambulizi lile makini la kushtukiza.
Nikawahi kujitupa kando ya lile kochi hata hivyo yule kijana nyuma yangu hakunipa nafasi ya kujipanga badala yake akawahi kunichapa teke zito la kifuani lililonitupa ukutani na kunisababishia maumivu makali mno. Hata hivyo nilipoanguka tu chini nikawahi kusimama haraka na kujipanga. Pigo la pili la teke la yule kijana lilipokuja nikawahi kuliona hivyo nikalipangua kama mchezo kwa mikono yangu miwili kisha kwa nguvu zangu zote nikamsukumia yule kijana kwenye lile kabati la mle ofisini. Yule kijana hakuwa na namna ya kujitetea hivyo akajikuta akiparamia lile kabati kama kipofu na hatimaye kuanguka nalo sakafuni na hivyo kusababisha droo za lile kabati kufunguka na nyaraka zote za mle ndani kutawanyika ovyo.
Yule mtu mfupi kuona vile akawahi kutumbukiza mkono wake kwenye koti lale la suti kuchukua bastola ili anilenge. Kuona vile nikawahi kujitupa kwenye lile kochi la sofa la mle ndani kisha nikabinuka nalo na kulifanya kama ngao ya kujikinga na risasi za yule mtu mfupi huku nikitafuta namna ya kujiweka mbali na hatari ile.
Zile risasi za yule mtu mfupi zikawa zikinikosakosa na nilipoona hatari inazidi kunikaribia nikanyanyuka na lile kochi mzegamzega nikimfuata yule mtu mfupi aliyejinadi kwangu kuwa ndiye meneja wa ile hoteli. Hata hivyo haraka niligundua kuwa yule mtu mfupi hakuelekea kuwa meneja wa ile hoteli kwani alionekana kuwa makini zaidi kwenye mapigano baada ya kulikwepa lile kochi kama mchezo kwa kuruka hewani huku amechanua msamba wa nguvu jambo ambalo kamwe sikuwa nimelitarajia kutokana na ufupi wake. Hata hivyo sikumsubiri yule mtu mfupi amalizie mbwembwe zake hivyo alipotua chini tu nikawa tayari nimemfikia na kumsindikiza kwa pigo matata la teke lililomtupa chini huku akipiga yowe la hofu.
Hata hivyo furaha yangu haikukamilika kwani wakati nilipokuwa nikigeuka nikajikuta nikitandikwa teke moja la shingo na yule kijana mwenye sare za mhudumu wa ile hoteli. Maumivu makali yakasambaa mwilini huku nikipepesuka ovyo kurudi nyuma kama bondia aliyepigwa konde zito la kichwani na mpinzani wake. Nilipokuwa mbioni kutafuta mhimili wa kusimama yule kijana akaniwahi kwa kunitandika pigo lingine la teke la kifuani liitwalo Hook kick lililonilevya vibaya baada ya kujipigiza ukutani huku maumivu makali yakisambaa mwilini kama niliyetupiwa tofali gumu za zege.
Pigo lile likawa limempelekea yule kijana mwenye sare za mhudumu wa ile hoteli anogewe na mafanikio yale hivyo haraka akinifikia na kutupa mapigo matatu ya Kung-fu ambayo niliyaona vizuri na kuyakwepa kwa ulaini kama upepo. Pigo lake la tatu shingoni kwangu nikalipangua na hapo nikapata nafasi nzuri ya kutupa ngumi mbili kwenye koo lake kisha nikamchapa mapigo matatu makini yaliyotia udhaifu mkubwa tumboni mwake na kumsababishia kichefuchefu cha ghafla. Kisha nikamalizia kwa kumchapa teke moja matata la korodani lililompelekea abweke kama mbwa koko huku akupepesuka kama mlevi na kuanguka chini.
Yule mtu mfupi aliyejinadi kwangu kuwa ndiye meneja wa ile hoteli kuona vile akawahi kuiokota bastola yake sakafuni kule ilipoangukia hata hivyo hakufanikiwa kwani niliwahi kulishika pindo la lile zulia dogo alilokanyaga ambalo lilikuwa katikati ya ile ofisi. Kisha nikalivuta lile zulia kwa nguvu na hivyo kumchota yule mtu mfupi mtama mzuri wa aina yake uliyompaisha hewani kama bwege na alipotua chini akafikia juu ya ile meza fupi ya kioo na kuvunjika mkono. Ile meza ikavunjika vipande vipande huku yule mtu mfupi akipiga yowe kali la maumivu.
Yule kijana mwenye sare za mhudumu wa ile hoteli alikuwa tayari ameshakusanya nguvu za kutosha hivyo kuona vile akaokota lile koti langu na kunirushia kichwani pale nilipokuwa huku akinifuata kwa kasi ya ajabu. Haraka nikajua kuwa lengo lake lilikuwa ni kunifunika kwa hila na lile koti ili hatimaye apate nafasi nzuri ya kunishambulia. Hata hivyo niliwahi kuishtukia mapema hila ile hivyo nikawahi kulinasa lile koti hewani kwa mguu wangu wa kushoto kisha nikalizungusha kwa kasi na kumtupia yule kijana ambapo lilimfikia vizuri na kumziba usoni. Yule kijana alipokuwa akihangaika kulitoa lile koti usoni nikawa tayari nimemfikia hata hivyo alikuwa mpambanaji mwenye ujuzi wa hali ya juu kwani japokuwa alikuwa haoni mbele yake lakini alijitahidi kwa kila namna kuyazuia vyema mapigo yangu akianzia kichwani, kifuani na tumboni. Hatimaye akafanikiwa kuliondoa lile koti usoni mwake na kulitupa kando.
Sasa tukawa tukipambana kwa mapigano ya ana kwa ana huku kila mmoja akijitahidi kumsoma vizuri mwenzake. Pigo moja la yule kijana sikuliona mapema hivyo lilitua vibaya tumboni mwangu na kwa kuwa sikuwa nimejiandaa maumivu yake yakanifanya nihisi kutaka kutapika. Pigo lake la pili la kareti likatua shingoni mwangu na hapo sekunde kadhaa nikahisi kukatika kwa mawasiliano kati ya shingo yangu na sehemu nyingine za mwili wangu.
Haraka nikarudi nyuma na kuishika shingo yangu nikiigeuza geuza huku na kule hadi pale niliporidhika kuwa ilikuwa imerudi mahala pake ndiyo nikajipanga. Pigo la tatu la teke liliponijia nikawahi kuinama kidogo na kuliacha likikata upepo angani bila mafanikio na hapo nikageuka kwa hasira na kumchapa yule kijana ngumi tatu makini za mgongoni. Alipogeuka nikamuwahi kwa kichwa makini kilichoupasua vibaya mwamba wa pua yake na kumtupa nyuma huku damu nyingi ikianza kumtoka puani. Yule kijana akiishika pua yake kwa maumivu makali mno huku akitukana kila aina ya matusi na alipoona hali inazidi kuwa mbaya haraka akachomoa kisu chake cha mkunjo kutoka mafichoni. Hivyo wakati nilipokuwa nikimkaribia bila kujua pigo lake moja likanichana begani na kupelekea damu nyingi ianze kunitoka kwenye lile jeraha.
Mchezo wa visu japokuwa nilikuwa nikiumudu vizuri lakini kamwe sikuupenda kwani kosa moja la kutokwepa vizuri shambulio lilikuwa likileta matokeo yenye athari mbaya kwa mhanga. Pigo lingine lilipokuja nikajitahidi kulikwepa hata hivyo nilichelewa kidogo kwani kile kisu kilinichana vibaya mkononi na kunisababishia jeraha lingine linalovuja damu. Yule mwenzake mfupi alikuwa tayari amepata nguvu mpya hivyo akasimama na kunifuata kwa kasi huku akipega makelele kama mwehu. Hata hivyo hakunifikia kwani alipokuwa akinikaribia nikamrudisha kule alipotoka kwa teke moja makini la kinyume nyume lililomtupa kwenye ile meza kubwa ya ofisini na kubinuka vibaya.
Pigo lingine la yule kijana liliponijia nikawahi kulipangua kwa nguvu zote na hapo kile kisu mkononi kikamponyoka na kurukia hewani. Ilikuwa nafasi nzuri kwani nilijirusha hewani na kukiwahi kile kisu kabla hakijatua kisha nilipoanguka chini nikajiviringisha haraka mbali na eneo lile kwa mtindo wa kininja halafu kwa wepesi wa ajabu nikakizungusha kile kisu na kukitupa kwa yule kijana mwenye sare za mhudumu wa ile hoteli. Yule kijana akajitahidi kukikwepa kile kisu bila mafanikio.
Shabaha yangu ilikuwa makini sana kwani kile kisu kilisafiri angani na hatimaye kupenya kwenye tumbo la yule kijana huku sehemu tu ya mpini wake ikibaki nje. Yule kijana akapiga yowe kali la hofu hata hivyo alikuwa na roho ngumu kama paka kwani badala yake akasimama kwa ghadhabu huku akikichomoa kile kisu tumboni mwake na kuanza kunifuata kwa hasira kama zombi. Kweli nilishangazwa sana na tukio lile kwani yule kijana hakuelekea kujionea huruma hata kidogo kutokana na damu nyingi iliyokuwa ikimtoka kwenye lile jeraha tumboni mwake.
Haraka nilipogeuka kumtazama yule mtu mfupi aliyejinadi kwangu kuwa ndiyo meneja wa ile hoteli nikamuona kuwa alishaikamata vyema bastola yake na kuanza kuielekezea kwangu. Sikuwa na mashaka yoyote kuwa endapo mtu yule angevuta kilimi cha ile bastola asingenikosa hata kama angekuwa mzembe wa shabaha kwa kiasi gani.
Nikiwa tayari nimeiona hatari ile sikutaka kutoa nafasi hivyo nikasubiri kidogo yule kijana anifikie kisha nikamkwepa kidogo na kumsindikiza kwa teke maridadi kuelekea kwa yule mtu mfupi. Bila shaka yoyote mahesabu yangu yalikuwa makini kwani wakati yule kijana akitupwa kwa pigo langu upande ule na yule mtu mfupi aliyejinadi kwangu kuwa ndiye meneja wa ile hoteli naye akawa tayari amefyatua risasi pasipo kuwa makini.
Kufumba na kufumbua nikamuona yule kijana akitupwa hewani kwani risasi za yule mtu mfupi zilikuwa tayari zimefanikiwa kulifumania vizuri pafu lake la upande wa kushoto. Nikamsikia yule kijana akipiga yowe hafifu la maumivu na alipotua chini akatikisa kidogo na kutulia sakafuni huku roho yake ikiwa mbali na mwili...ITAENDELEA
 
RIWAYA: UFUKWE WA MADAGASCAR
SEHEMU: 38
Mtunzi:Kelvin Mponda

Wakati yule mtu mfupi aliyejinadi kwangu kuwa ni meneja wa ile hoteli akiwa ameshikwa butwaa kwa kitendo cha kumuua mwenziwe mimi nikawahi kujitupa kando ya eneo lile karibu na lile kochi la mle ofisini lilipokuwa limeangukia lile koti langu jeusi la mvua. Kisha nikaupenyeza mkono wangu kwenye mfuko wa koti lile na kuchomoa bastola na mara hii sikutaka kupoteza muda. Hivyo risasi moja niliyoiruhusu kufanya safari ikasafiri kwa shabaha makini na kukisambaratisha vibaya kiganja cha mkono cha yule mtu mfupi na hapo ile bastola ikamponyoka mkononi huku akiwa ameingiwa na hofu kuu. Ndani ya sekunde chache tayari nikawa nimemfikia yule mtu pale alipokuwa amesimama huku akiwa anaweweseka ovyo kwa hofu ya maumivu kama mwehu.
Yule mtu mfupi kuona vile akawahi kujihami kwa kurusha teke hata hivyo lilikuwa pigo dhaifu kwani niliwahi kulidaka kisha nikamchota mtama maridadi kupitia mguu wake mmoja uliosalia chini. Pigo lile likampelekea yule mtu atue chini kwa matako na kupiga yowe kali la maumivu huku akiponyokwa na tusi zito mdomoni. Alipotaka kuinuka akajikuta akitazamana na mdomo wa bastola yangu mkononi. Hofu iliyomuingia ikamrudisha chini taratibu huku akiona aibu kunitazama usoni.
“Qui etes-vous?”. Wewe ni nani?. Nikamuuliza yule mtu kwa hasira.
“Leonidas Ndikumagenge”. Yule mtu akajitambulisha kwa hofu.
“Vouz aves quel problème avec moi?”. Mna shida gani na mimi?. Nikamuuliza yule mtu hata hivyo hakunijibu badala yake akainamisha kichwa chake chini. Sikumkawiza badala yake nikamzaba makofi mawili ya nguvu kumuweka sawa kabla ya kumuuliza tena.
“Vous etes envoyer par qui?”. Mmetumwa na nani?. Nikamkwida tai yake shingoni yule mtu na kumuuliza huku akiugulia maumivu ya ule mkono wake uliovunjika na kile kiganja chake nilichokisambaratisha kwa risasi.
“Je ne sais pas”. Sifahamu. Yule mtu mfupi akinijibu kwa mkato na hapo nikamzaba tena kofi la usoni lililompelekea azidi kuona maruweruwe huku akiendelea kuugulia maumivu. Nikazidi kumkwida shingo yake kwa ile tai huku nikiendelea kumuuliza.
“Vous etes à combien dans ce battument?”. Mpo wangapi kwenye hili jengo?.
“Nous sommes trois”. Tuko watatu. Yule mtu mfupi akanijibu kwa hofu na hapo nikamtazama kidogo huku nikitafakari juu ya lile jibu lake. Hatimaye nafsi yangu ikajiridhisha kuwa huwenda mtu yule alikuwa akizungumza ukweli pale nilipowakumbuka wale vijana wawili walionikaribisha kule mapokezi ambao mmoja wapo ndiye yule niliyetoka kupambana naye muda mfupi uliopita mle ndani. Hatimaye nikayapeleka tena macho yangu kumtazama Yule mtu mfupi pale chini.
“Tu sais quoi consernant le Pretre Aloysius Kanyameza?”. Unafahamu nini kuhusu Padri Aloysius Kanyameza?. Nikamuuliza tena yule mtu mfupi huku nikiusukasuka ovyo ule mkono wake uliovunjika.
“Je ne sais rien, et je ne lui conais même pas”. Sifahamu chochote na wala simjui. Yule mtu mfupi akaongea kwa tabu huku akilalama kwa maumivu makali ya majeraha yake mikononi. Nilifahamu fika kuwa alikuwa akinidanganya kupitia jibu lake hata hivyo katika mazingira yale sikuona kama alikuwa tayari kuzungumza ukweli wowote. Kitambo kifupi cha ukimya kikapita mle ndani huku nikifikiria nini cha kufanya na nilipokuwa katika hali ile yule mtu akavunja tena ukimya akiongea kwa shida.
“Nʾesaye pas de fuire tu ne vas pas arrivé loin, parceque nos gents sont partout”. Usijaribu kutoroka hutofika mbali kwani watu wetu wapo kila mahali. Nikamsikiliza vizuri yule mtu na hapo nikagundua kuwa alikuwa akijitahidi kuniogopesha kuwa bado sikupaswa kuitwa mshindi katika vita ile. Hata hivyo nikalipuuza onyo lake kumtupia swali lingine.
“Où est Iʾautres?”. Yule mwenzako yuko wapi?.
“II est dans votre vehicule là dehors il vous attend”. Yupo kwenye gari lako kule chini nje ya hoteli anakusubiri. Maelekezo ya yule mtu mfupi yakanipelekea nishikwe na mshangao. Kumbe wale vijana wawili niliyowakuta pale mapokezi kule chini kwenye ile hoteli walikuwa mamluki waliopandikizwa katika namna ya kuhakikisha kuwa ninakamatwa mapema kabla sijafika mbali katika harakati zangu. Hivyo yule kijana mwingine wa pale mapokezi alikuwa ameenda kunivizia kwenye gari langu ili ikitokea kuwa nimewatoroka mwenzake aweze kunimaliza kiulaini. Mawazo yale yakapelekea tabasamu jepesi kuumbika usoni mwangu.
“Comment sʾappelle lʾautre”. Anaitwa nani?.
“Il sʾappelle Blaise”. Anaitwa Blaise Tugiramahoro. Yule mtu mfupi akanijibu kwa uoga na nilipomkata jicho la hadhari akanyoosha maelezo.
“II sʾappelle Blaise Tungiramahoro’’. Anaitwa Blaise Tugiramahoro.
Nikamsikiliza yule mtu kwa utulivu na wakati nilipokuwa nikijiandaa kumuuliza swali lingine mara ghafla nikasikia ile kengele ya nje ya mlango wa kile chumba ikilia. Nilipoyatega vizuri masikio yangu ile kengele ikanitanabaisha kwa nje ya kile chumba mlangoni kulikuwa na mtu aliyekuwa akihitaji kuingia mle ndani. Haraka nikayarudisha tena macho yangu kumtazama yule mtu mfupi mateka wangu na sikuona kama angekuwa na taarifa zozote nyingine muhimu za kunisaidia. Hivyo nikainyanyua bastola yangu mkononi na kabla yule mtu hajazungumza alichotaka kuniambia risasi zangu mbili tayari zilikuwa mwilini mwake. Risasi moja kwenye moyo kifuani mwake na risasi nyingine shingoni pasipo kelele yoyote mle ndani kwani bastola yangu ilikuwa imefungwa kiwambo maalum cha kuzuia sauti.
Muda mfupi uliofuata nikawa tayari nimeufikia ule mlango wa kile chumba na kabla ya kuufungua nikainama na kuchungulia kwenye tundu la funguo kwenye kitasa cha ule mlango. Nilichokiona kule nje ya ule mlango kikanitahadharisha kuwa mambo hayakuwa shwari. Mwanaume fulani aliyevaa sare za mhudumu wa ile hoteli alikuwa amesimama nje ya ule mlango wa kile chumba. Sura yake, kiwiliwili wala sehemu yake ya chini sikuweza kuiona kutokana na udogo wa lile tundu la funguo pale mlangoni. Hata hivyo mtu yule mkononi alikuwa ameshika sinia lenye chupa moja ya mvinyo mwekundu wa kifaransa Château Lascombes na glasi moja ndefu yenye karatasi nyeupe ya tishu ndani yake. Nilipozidi kuchungulia vizuri nikashtukia kuwa chini ya lile sinia yule mtu alikuwa ameshika bastola.
Sasa sikuwa na shaka tena kuwa hatari ilikuwa mlangoni. Hata hivyo niliwaza kuwa kuendelea kusubiri zaidi pasipo kufungua ule mlango kungeweza kumpelekea yule mtu aliyesimama pale mlangoni kuingiwa na wasiwasi na hivyo kutafuta namna nyingine ya kunikabili. Hivyo haraka nikaichomeka bastola yangu nyuma kiunoni na kuufungua taratibu ule mlango huku tabasamu la kirafiki likiwa usoni mwangu. Yule mtu aliyekuwa akibisha hodi nje ya ule mlango haraka nilipomchunguza nikamkumbuka kuwa alikuwa ni yule kijana mwingine kati ya wale vijana wawili walionikaribisha vizuri muda mfupi uliopita kule chini ya ile hoteli sehemu ya mapokezi. Ambaye yule mtu mfupi aliyejinadi kwangu kuwa ndiye meneja wa ile hoteli ambaye sasa alikuwa marehemu mle ndani alikuwa amemnasibu kwa jina la Blaise Tigiramahoro. Alikuwa ni yule kijana aliyesemekana kunisubiri kwa kunivizia kwenye gari langu kule nje chini ya ile hoteli.
“Oh! bien venue monsieur”. Oh! karibu sana ndugu. Nikamkaribisha yule kijana kwa utulivu huku usoni nikiwa nimeumba tabasamu la kirafiki. Hata hivyo haraka niliweza kuuona mshtuko mkubwa usoni kwa yule kijana kiasi cha kumpelekea asite kuingia mle ndani. Lakini tabasamu na macho yangu vikamshawishi aingie na huku nikizidi kuufungua zaidi ule mlango wakati huo nikijitahidi kuuegemea ule mlango. Yule kijana ikabidi anitazame kidogo huku usoni mwake akilazimisha tabasamu ingawa nilipomchunguza vizuri nikafahamu kuwa macho yake hayakwendana kabisa na lile tabasamu lake badala yake alionekana kujawa na wasiwasi mwingi. Hata hivyo akajikaza na kuniitikia kwa utulivu ingawa sauti yake ilipwaya kidogo.
“Merci beaucoup!”. Ahsante sana!. Yule kijana akaitikia huku akiingia mle ndani kwa tahadhari na sinia lake mkononi. Sikuwa na muda wa kupoteza hivyo mara baada ya yule kijana kuingia mle ndani haraka nikaufunga ule mlango nyuma yake. Hata hivyo yule kijana alikuwa amejiandaa kwani mara tu alipoingia mle ndani haraka akalitua lile sinia chini na kugeuka huku akiwa na bastola yake mkononi.
Nikiwa nimejiandaa kwa tukio lile sikutaka kumpa nafasi ya kuonesha umahili wake yule kijana hivyo kabla hajamalizia vizuri kuielekeza bastola yake kwangu tayari nilikuwa nimegeuka na kuvuta kilimi cha bastola yangu mkononi. Risasi yangu moja ikatoboa pafu lake la kulia huku risasi nyingine ikiacha tundu dogo linalovuja damu nyingi kwenye moyo wake. Yule kijana akapiga mweleka wa nguvu na alipoanguka chini akatikisika kidogo na kutulia.
Muda haukuwa rafiki tena kwangu kwani nilifahamu fika kuwa muda siyo mrefu washirika wa watu wale wangeweza kuhisi kilichowasibu wenzao kwenye kile chumba na hivyo kufika mle ndani haraka jambo ambalo kamwe sikupenda litokee kabla sijatoka kwenye kile chumba cha ile ofisi na hatimaye kutokomea mbali kabisa na lile eneo.
Hivyo nilianza kwa kupitisha upekuzi wa haraka mle ndani. Kupitia zile nyaraka za kiofisi zilizokuwa kwenye kabati la mle ndani na droo za ile meza kubwa ya ofisini niliweza kugundua kuwa meneja wa ile hoteli alikuwa haitwi jina la Vital Desire Habonimana kama yule mtu mfupi alivyojinadi pale awali. Meneja wa ile hoteli alikuwa akifahamika kwa jina la ndugu Alain Basuzuguye.
Hatimaye nilimaliza kufanya upekuzi katika zile nyaraka za kiofisi kwenye lile kabati na zile droo za ile meza ya ofisini pasipo kupata kitu kingine chochote cha maana. Hivyo nikahamishia upekuzi wangu kwenye ile miili ya wale watu niliyopambana nao na kuwaangamiza mle ndani. Kitu kilichonishangaza kama siyo kunishtua ni kuwa katika mavazi ya wale watu niligundua vitu vidogo vyeusi mfano wa vifungo vilivyonasishwa vizuri kwenye kosi za mashati yao. Nilipoendelea kuchunguza haraka nikagundua kuwa vile vidude vilikuwa ni vifaa pandikizi vya mawasiliano ya kijasusi viitwavyo UHF-Voice Transmitters vinavyoweza kunasa mazungumzo ya watu waliopo ndani ya umbali wa futi thelathini na tano na kuyasafirisha mawimbi ya maongezi hayo katika umbali usiopungua mita mia tatu au sawa na urefu wa viwanja vitatu vya mpira wa miguu.
Nikavitazama vifaa vile vya mawasiliano kwa utulivu huku mawazo mengi yakipita kichwani mwangu. Kwa namna moja au nyingine nilikuwa na kila sababu ya kuamini kuwa maongezi kati yangu na wale watu mle ndani yalikuwa yamesikika na mtu au watu fulani waliokuwa ndani ya lile jengo la hoteli au mbali na ile hoteli sehemu fulani ambayo sikuifahamu. Nilipozidi kuwaza nikaja na hitimisho kuwa kulikuwa na uwezekano mkubwa kuwa mtu au watu hao waliokuwa wakifuatilia maongezi yale baada ya kupoteza mawasiliano na wenzao wa mle ndani sasa wangekuwa katika jitihada kubwa za kukifikia kile chumba cha ile ofisi ya meneja wa ile hoteli kama siyo kulifikia lile jengo la hoteli ikiwa ni sehemu ya mkakati wao katika kuhakikisha kuwa sitoroki na kuwaacha solemba.
Nilifahamu hatari ambayo ingenifikia endapo ningeendelea kupoteza muda wangu ndani ya kile chumba. Hivyo haraka nikavitupa sakafuni vile vifaa vidogo vya mawasiliano ya kijasusi kutoka katika miili ya wale watu na kuvikanyaga kwa buti zangu ngumu miguuni nikivisaga kuviharibu. Kisha haraka nikasogea kwenye dirisha la ile ofisi na kusogeza pazia kando nikitazama kule chini nje ya lile jengo. Kwa kufanya vile nikashikwa na mstuko kidogo. Chini ya lile jengo usawa wa dirisha la ile ofisi nikawaona wanaume watatu waliovaa sare za kijeshi wakioneshana kwa vidole vyao katika kile chumba cha ofisi nilichokuwa ndani yake. Tukio lile kwangu ilikuwa ni ishara mbaya hivyo haraka nikalirudishia vizuri lile pazia pale dirishani huku moyo wangu ukiwa umeanza kupoteza utulivu. Haraka nikaelekea kwenye ule mlango wa mle ndani kuelekea kile chumba cha maliwato. Nilipofika nikaufungua ule mlango kwa tahadhari bastola yangu ikiwa mkononi katika namna ya kuchunguza usalama wa mle ndani. Sikuona kitu chochote cha maana hivyo nikaufunga ule mlango huku akili yangu ikianza kufanya kazi ya ziada katika kufikiria ni kwa namna gani ningeweza kulitoroka lile jengo pasipo kukabiliana na upinzani mwingine mbele yangu.
Nikiwa katika ile hali kuendelea kufikiria mara nikawa nimepata wazo. Haraka nikaisogelea maiti ya yule kijana wa mwisho kupambana naye mle ndani kisha nikaanza kumvua zile sare za mhudumu wa ile hoteli upesi. Nilipomaliza nikazivaa nguo zile haraka juu ya nguo zangu ingawa zilikuwa na mabaka ya damu hata hivyo nilijitahidi kuzitengeneza kwa kila namna katika namna ya kuondoa viashiria vya haraka vya kutiliwa mashaka na mtu yeyote ambaye angenitazama juu juu. Nilipomaliza nikalichukua lile koti langu la mvua na kulikunja vizuri kisha nikalichukua lile sinia lenye ile chupa ya kinywaji na glasi nikilibeba kwa uangalifu. Baada ya kujihisi nimeuvaa vyema muonekano wa mhudumu wa ile hoteli nikaivua kofia yangu kichwani na kuikunjia ndani ya lile koti nililolishikilia vizuri chini ya lile sinia. Bila kupoteza muda nikavaa kofia ya mhudumu wa ile hoteli na kuitengeneza vizuri kichwani mwangu. Niliporidhika vizuri na muonekano wangu nikafungua mlango wa kile chumba na kutoka huku nikiiweka vizuri ile chupa ya ule mvinyo juu ya lile sinia ili kuficha yale madoa ya damu yaliyokuwa kifuani kwenye lile vazi la mhudumu wa ile hoteli nililolivaa.
Nilipotoka nje ya kile chumba nikashika uelekeo wa upande wa kulia nikielekea mwisho wa ile korido sehemu kulipokuwa na ngazi za kushukia chini ya lile jengo. Sikutaka kutumia lifti kushuka chini ya lile jengo kwa kuanzia ghorofa ile kwani kufanya vile ningetengeneza ushahidi wa wazi kwa mtu yeyote aliyekuwa akinifuatilia. Hivyo nilipofika mwisho wa ile korido nikaanza kushuka zile ngazi kwa haraka nikielekea chini kwenye ghorofa ya nne ya lile jengo. Wakati nilipokuwa nikishuka zile ngazi nikakutana na wanaume wawili waliovaa suti nadhifu nyeusi wakipanda zile ngazi kwa pupa na nilipowatazama haraka nikawatambua kuwa hawakuwa watu wa kawaida kutokana na muonekano wao. Wakati nikipishana na watu wale hawakusalimiana na mimi badala yake nikawaona haraka wakiipeleka mikono yao kwenye mifuko ya makoti yao ya suti huku wakinitazama kwa macho ya mashaka. Hata hivyo haraka nilibadili dhamira yao kwa kuwasalimia vizuri huku nikitabasamu. Wale wanaume hawakuitikia salamu yangu badala yake wakanipita na kuendelea na safari yao huku...ITAENDELEA
 
Dah kiongozi unatisha sana....endelea kutupa uhondo tafadhali.
 
Mwambaaaaaa itika wito basi Arosto huku
Nmefika
Mwambaaaaa

mwamba we hatari

Mkuu tupia kitu

Mwamba sema chochote,lini tena?

Pamoja mkuu

Shukran Mwamba

Dah kiongozi unatisha sana....endelea kutupa uhondo tafadhali.

MWAMBAAA big up sana

Daah, hatari sana.
Shusha vitu mkuu majasusi tupo hapa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom