Riwaya: Siri

Riwaya: Siri

SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 7: EPISODE 1
KAMPALA – UGANDA
Saa tatu za asubuhi
televisheni ya taifa ya Uganda
ilikatisha vipindi vilivyokuwa
vinaendelea na kujiunga na
matangazo ya moja kwa moja
kutoka katika kambi kubwa ya
kijeshi iliyoko nje kidogo ya jiji
la Kampala ambako Rais wa
Uganda Jenerali Akiki
Rwamirama alitarajiwa
kulihutubia taifa kutokea katika
kambi hiyo.
Msafara wa Jenerali Akiki
uliwasili katika kambi hiyo
kubwa akapokewa na mkuu wa
majeshi wa Uganda,wimbo wa
Taifa ukapigwa halafu mkuu
wa majeshi akazungumza
machache na kumkaribisha Rais
azungumze na wanajeshi
waliokuwa na hamu ya
kumsikiliza na kupitia kwao
taifa zima liweze kupata
ujumbe.Jenerali Akiki akaelekea
katika mimbari iliyoandaliwa
na kuwasalimu wanajeshi
ambao waliitika kwa sauti
kubwa akatabasamu na
kuendelea
“Mheshimiwa waziri wa
ulinzi,mkuu wa
majeshi,makamanda wote wa
vikosi na wote mlioko hapa
itifaki ikiwa imezingatiwa”
akanyamaza na kuwatazama
wanajeshi halafu akaendelea
“Awali ya yote napenda
kwa niaba ya serikali yangu na
wananchi wa Uganda kuchukua
nafasi hii kuwapa pole nyingi
ndugu zetu wa Tanzania,Congo
na Rwanda kwa tukio baya
lililotokea usiku wa jana jijini
Dar es salaam la mlipuko wa
bomu,tukio ambalo
lilisababisha watu wengi
kuuawa na miongoni mwao ni
wake za marais wa
Tanzania,jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo na
Rwanda waliokuwa
wamekwenda nchini Tanzania
kuhudhuria mkutano mkubwa
wa wake za marais
ulioandaliwa na mke wa Rais
wa Tanzania.Tunawapa pole
sana wote waliofiwa na
tunawahAkikishia kwamba
ndugu zao wa Uganda tuko
pamoja nao kwani huu ni msiba
wa Afrika Mashariki.Shambulio
lile ni la kinyama kabisa na
tunalilaani kwa nguvu zetu
zote” akanyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Nadhani mpaka sasa wengi
wenu tayari mmekwisha
itazama video iliyoanza
kusambaa toka jana usiku
ambayo inamuonyesha mtu
anayejulikana kama James
Kasai akitamba kuhusika katika
tukio lile la mauaji akishirikiana
na kikundi cha kigaidi cha
IS.Huyu James Kasai ni kiongozi
wa kikundi cha waasi ambaye
amekuwa akiendesha
mapambano na serikali ya
Congo kwa muda mrefu na
baada ya kutimuliwa kutoka
nchini Jamhuri ya kidemokrasia
ya Congo inadaiwa alikimbilia
katika misitu iliyoko Kaskazini
mwa nchi yetu.Nchi za Rwanda
na Congo zimekuwa
zikitulaumu sisi kwamba
tunamuhifadhi James Kasai
lakini ukweli ni kwamba hatuna
uhakika wa uwepo wake katika
misitu yetu kama
inavyodaiwa.Toka shutuma
hizo zilipoanza,tumefanya
operesheni za kijeshi zaidi ya
mara mbili kumsaka James
Kasai lakini hatujafanikiwa
kumpata huko mahala
wanakodai
amejificha.Tunaamini James
Kasai atakuwa bado amejificha
katika misitu ya Congo na si
nchini Uganda kama
inavyodaiwa” akanyamaza tena
kidogo kisha akaendelea
Kuanzia saa tisa za usiku
wa kuamkia leo,ndege za kivita
za Rwanda zimeingia katika
anga letu na kufanya
mashambulizi katika vijiji
vilivyoko kandoni mwa misitu
ya Kaskazini mwa nchi
yetu.Bado hatujapata idadi
kamili ya watu waliouawa lakini
uharibifu uliofanyika ni
mkubwa.Mashambulizi hayo
yamefanywa kwa kisingizio cha
kumtafuta James Kasai.Vikosi
vyetu mahiri vya Anga
vilifanikuwa kuziangusha ndege
vita mbili za jeshi la Rwanda
zilizoingia katika anga letu kwa
lengo la kufanya
mashambulio.Kitendo hiki ni
cha kichokozi na serikali ya
Uganda kamwe haiwezi
kukivumilia ! akasema kwa
ukali Rais Akiki na wanajeshi
wakashangilia
“Narudia tena kwamba
kitendo hiki kilichofanywa na
serikali ya Rwanda
kutuvamia,kufanya
mashambulio na kuua watu
wetu katu serikali
ninayoiongoza haiwezi
kukivumilia !! akasema kwa
ukali na kunyamaza
akawatazama wanajeshi halafu
akaendelea
“Kwa muda mrefu sasa
Rwanda wamekuwa
wakiendesha chokochoko dhidi
ya nchi yetu lakini tumekaa
kimya hatujawajibu chochote
na sasa wameamua kutuvamia
na kutushambulia.Ninasema
kwa mara ya tatu hiki
walichokifanya ni uchokozi wa
wazi na hatuwezi kuukubali
uchokozi huu ukaendelea.Tuko
tayari kupambana na taifa
lolote lile liwe kubwa au dogo
ambalo litathubutu
kutuchokoza hivyo basi tayari
nimemuelekeza mkuu wa
majeshi aweke vikosi vyetu
vyote vya jeshi katika utayari
wa vita na vikosi vingine
vitangulie katika mpaka wetu
na Rwanda.Tunataka kutoa
ujumbe kwa dunia kwamba
Uganda si mahala pa kufanyia
majaribio ya kijeshi.Ukiingiza
pua yako Uganda tutakukata
hadi miguu.Damu ya watu
waliouawa bila hatia haiwezi
kumwagika bure lazima tulipe
na tukomeshe uovu huu
uliofanywa na Rwanda !
akasema Rais Akiki na
wanajeshi wakamshangilia kwa
nguvu
“Kwa wananchi wa Uganda
nawaomba muwe watulivu na
muendelee na shughuli zenu
kama kawaida.Jeshi lenu lenye
wanajeshi walio na ari kubwa
ya kuitetea nchi yao liko imara
kuwalinda dhidi ya adui yeyote
kutoka nje anayetishia amani na
usalama wenu na ndiyo maana
jana usiku liliweza kuzima
mashambulio ya ndege za jeshi
za Rwanda na kuangusha ndege
mbili.Hatutaishia katika
kuangusha ndege mbili tu la
hasha,tunataka tuende mbali
zaidi na kumfundisha adabu
huyu mvamizi wetu ! Jenerali
Akiki akaendelea kushangiliwa
kwa nguvu
Narudia tena kuwaomba
ndugu zangu tusimame pamoja
katika hili na kupinga aina
yoyote ya uvamizi kwa taifa
letu.Mimi na serikali
ninayoiongoza ambao tulikula
kiapo cha kuilinda mipaka ya
nchi yetu nawaahidi kwamba
tutapamba na yeyote hadi tone
la mwisho la damu yetu katika
kuilinda nchi yetu.Jambo la
mwisho ambalo nataka
kuwasisitiza wananchi wa
Uganda fuatilieni sana vyombo
vya habari kwani kila hatua
tutakayoichuikua tutakuwa
tukiwajulisha
Ahsanteni
Mungu Ibariki Uganda
Jenerali Akiki akamaliza
hotuba yake fupi kisha
akaongozwa na mkuu wa
majeshi kuelekea sehemu
ambako kikao cha faragha
kingefanyika kati ya Rais na
makamanda wa vikosi mbali
mbali vya jeshi.Kikao hicho
kilidumu kwa saa mbili kisha
Rais akaondoka akiwa katika
ulinzi mkali sana kurejea
ikulu.Akiwa njiani akapigiwa
simu na mke wake aliyekuwepo
jijini Dar es salaam.
“Hallow” akasema Jenerali
Akiki
“Hallo mpenzi habari za
huko.Nilikuwa naitazama
hotuba yako” akasema Dr
Natukunda Rwamirama mke wa
Rais wa Uganda
“Unasemaje kuhusu hotuba
ile? Huko Dar es salaam
wanaiongeleaje? Akauliza
Jenerali Akiki huku
akitabasamu
“Watu wana hofu kwamba
kwa hotuba ile uliyoitoa
leo,kuna uwezekano mkubwa
kukazuka vita baina ya Uganda
na Rwanda” akasema Dr
Natukunda
“Uwezekano ni mkubwa
sana.Katu hatuwezi kuvumilia
kitendo ilichokifanya serikali ya
Rwanda.Wametuvamia na
kutushambulia hatuwezi kukaa
kimya lazima tujibu.Ninaapa
kuifanyia Rwanda kitu kibaya
sana ! akasema Jenerali Akiki
“Lakini mume wangu sioni
sababu ya kuanzisha vita na
Rwanda”
“Umefurahia Rwanda
ilichokifanya? Wamevamia
wakafanya mashambulio na
kuua watu wetu.Hilo ni jambo
zuri?akauliza Jenerali Akiki kwa
sauti ya ukali kidogo.
“Si jambo zuri walilolifanya
lakini Rwanda walikuwa na
sababu ya kufanya
vile.Wanafahamu kwamba
tunamuhifadhi James Kasai na
kwa muda mrefu wamekuwa
wakilalamikia jambo hili kwani
wakati akiendesha mapambano
yake nchini Congo James Kasai
aliua wanyarwanda wengi
pia.Rwanda wamekuwa
wakishinikiza tumfukuze au
tumkamate James lakini
tumekuwa tukikanusha kwa
nguvu kwamba James Kasai
hayupo Uganda.Unadhani
Rwanda hawajui kama James
yupo Uganda na sisi tumempa
hifadhi?Wanajua na ndiyo
maana wakafanya operesheni
ile ili waweze kumuondoa wao
wenyewe baada ya sisi
kuendelea
kumkumbatia.Mpenzi wangu
kwa hiki alichokifanya James
sidhani kama kuna ulazima wa
kuendelea kumpa hifadhi na
kumtetea.Ni wakati wa kumtaka
aondoe vikosi
vyake.Tukiendelea kumuhifadhi
yeye na kundi lake
atatusababishia matatizo
makubwa sana.Namlaumu sana
mdogo wangu kwa kukubali
kuolewa na mwanaume kama
Yule ambaye hana hata chembe
ya ubinadamu” akasema Dr
Natukunda.Jenerali Akiki
akavuta pumzi ndefu halafu
akauliza
“Mke wangu hilo suala ni
gumu kidogo.Japo James
amefanya kitendo hicho lakini
hatuwezi kumuondoa kwa
haraka namna hiyo.Wewe
mwenyewe unafahamu namna
tunavyofaidika na huyu
mt……….” Akasema Jenerali
Akiki na mke wake akamkatisha
“Mume wangu niko hapa
Dar es salaam nimeshuhudia
kile alichokifanya ni kitendo cha
kinyama sana.James hafai
kabisa na sasa ameharibu zaidi
baada ya kujiunga na magaidi
wa IS.Tumuondoe haraka kwani
huko tunakoelekea atakuja
kutushambulia hata sisi
wenyewe” akasema Dr
Natukunda
“Sawa nimekuelewa vipi
kuhusu safari ya kurudi?
Akauliza Jenerali Akiki
“Nimeahirisha kidogo ili
nishiriki miili ya marehemu
ndipo niondoke.Hawa
waliouawa walikuwa marafiki
zangu.Millen Kelelo alikuwa ni
rafiki yangu sana na siwezi
kuondoka Tanzania bila
kumuaga.Mkutano tuliokuja
kuhudhuria haupo tena hivyo
baada tu ya kuaga miili ya
marehemu nitaanza safari ya
kurejea Uganda”akasema Dr
Natukunda
“Vipi kuhusu usalama
wako?
“Usalama hapa ni mkubwa
usiwe na wasiwasi” akasema
“Sawa hAkikisha baada tu
ya zoezi hilo kukamilika basi
unarejea nyumbani mara moja”
akasema Jenerali Akiki na
kukata simu
“Nadhani Natukunda yuko
sahihi ni wakati wa James
kuondoa vikosi vyake katika
ardhi ya Uganda.Tumekuwa
tukimfadhili katika mapambano
yake na serikali ya Congo na sisi
tumekuwa tukifaidika kwa
kupata madini na rasilimali
nyingine kupitia kwake hivyo
yeye ataendelea kubaki hapa
Uganda lakini vikosi vyake
lazima viondoke.Nitawasiliana
naye ili aweze kuondoa kimya
kimya vikosi vyake kwa muda
huu ambapo hali ya hewa
imechafuka.Baadae hali
itakapotulia
atavirejesha.Kuhusu Rwanda
lazima niwafundishe
adabu.Nitawachapa kuanzia
mpakani hadi mji wao mkuu wa
Kigali.” Akawaza Jenerali Akiki
Alipofika ikulu moja kwa
moja akaelekea chumbani
kwake akachukua simu ya
satelaiti na kumpigia James
Kasai
“Mheshimiwa
Rais”akasema James Kasai
baada ya kupokea simu
“James habari yako”
“Mheshimiwa Rais naamini
simu hii umenipigia kuhusiana
na kile kilichotokea Dar es
salaam jana”akasema James
Kasai
“James kwa nini ulifanya
vile? Kwa nini hukunijulisha
kama kuna shambulio
unalipanga nchini Tanzania?
Akauliza Jenerali Akiki kwa
ukali
“Mheshimiwa Rais …….”
Akasema James lakini Jenerali
Akiki akamkatisha
“Nisikilize James.Kwa
sababu ya kile ulichokifanya
hivi sasa tunajiandaa kuingia
katika vita na Rwanda.Usiku wa
kuamkia leo ndege za vita za
Rwanda zimevamia ardhi yetu
na kufanya mashambulio katika
vijiji vilivyo kandoni mwa
misitu yetu.Wamefanya hivyo ili
kulipiza kisasi kwa kile
ulichokifanya kumuua mke wa
Rais wa Rwanda,balozi pamoja
na raia wengine.Rwanda
wanafahamu kwamba unapewa
hifadhi na Uganda lakini na hii
imekuwa ni sababu ya
kutokuelewana nao kwa muda
mrefu.Ulichokifanya jana
kimefanya mahusiano yetu
kuwa magumu zaidi.Tayari
nimepeleka vikosi vya jeshi
katika mpaka wetu na
Rwanda,tuko tayari kwa
vita.Katika hili sintarudi nyuma
lazima niishikishe adabu
Rwanda.Sifahamu kuhusu
Congo na Tanzania wao
watachukua hatua gani kwani
toka lilipotokea shambulio lile
sijaweza kuwasiliana na
viongozi wake.Rais wa Congo
hatuna mahusiano mazuri lakini
Rais wa Tanzania hakupokea
simu yangu nilipompigia.James
kwa hiki ulichokifanya ambacho
sasa kinakwenda kuigharimu
nchi yetu nimefikia maamuzi ya
kukutaka uondoe vikosi vyako
nchini Uganda.Tumekuhifadhi
kwa muda wa kutosha sasa ni
wakati wa kuondoa vikosi
kwenda kutafuta hifadhi
sehemu nyingine Uganda si
sehemu salama tena kwa vikosi
vyako.Pale hali itakapotulia
utavirejea tena lakini wewe
utaendelea kubaki hapa hapa
Uganda” akasema Jenerali Akiki
na James akashusha pumzi
“Mheshimiwa Rais
nafahamu nilich………”
“James hakuna tena
mjadala katika suala hili tayari
nimekwisha fanya maamuzi
hivyo anza kuandaa vikosi kwa
ajili ya kuondoka.Utajua
mwenyewe utavipeleka wapi
aidha Congo au Sudan lakini
nakupa siku mbili uwe tayari
umeondoa vikosi vyako katika
ardhi ya Uganda.Nadhani
umenielewa James si kwamba
ninakufukuza bali ni kwa ajili ya
usalama wa watu wako”
akasema Jenerali Akiki
“Nimekuelewa mheshimiwa
Rais”
“Sawa.Nasubiri
utekelezaji.Kama kutakuwa na
tatizo lolote au utahitaji msaada
nijulishe tafadhali”akasema
Jenerali Akiki na kukata simu
DAR ES SALAAM – TANZANIA
Ndege ya Patrice Eyenga
Rais wa jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo ilitua
katika uwanja wa ndege wa
kimataifa wa Julius Nyerere
jijini Dar es salaam.Waziri wa
mambo ya nje ya nchi
alikuwepo uwanjani pale
kumpokea kisha wakaelekea
ikulu ambako alikutana na Rais
Dr Fabian Kelelo
“Pole sana Patrice”
akasema Dr Fabian baada ya
kumpokea Patrice Eyenga ikulu
“Dr Fabian bado sijaamini
mpaka sasa kama kweli mke
wangu Rebeca amefariki dunia”
akasema Patrice Eyenga
“Ni ngumu kuamini Patrice
lakini ni kweli Rebeca na Millen
wamefariki dunia.Hata mimi
iliniwia ugumu kuamini
nikalazimika kwenda hospitali
jana usiku kuthibitisha na kweli
wamefariki”akasema Dr
Fabian.Patrice Kelelo
alichanganyikiwa.Alisimama na
kwenda kusimama
dirishani.Akatoa kitambaa
akafuta machozi
“Nimeumia sana Dr
Fabian.Rebeca alikuwa ni kila
kitu kwangu.Nisingeweza
kufika hapa nilipofika leo kama
si yeye.Amekuwa ni taa yangu
inayoniongoza.Dah ..! Ninakosa
hata neno la kusema” akasema
Patrice Eyenga
“Patrice inaumiza
mno.Tukio hili ni la kinyama
sana”akasema Dr Fabian
“Dr Fabian tukio hili
limetokeaje?Hakukuwa na
ulinzi wa kutosha?akauliza
Patrice
“Ulinzi ulikuwa wa kutosha
sana” akajibu Dr Fabian
“Kama kulikuwa na ulinzi
wa kutosha magaidi hao
waliwezaje kupenya na kufanya
shambulio? Akauliza Patrice
“Hilo ndilo ambalo vyombo
vyetu vya uchunguzi
vinalifanyia kazi kujua namna
magaidi hao walivyoweza
kupenya na kuingia nyumbani
kwa balozi wakatekeleza
shambulio lle.Pale uchunguzi
utakapokuwa umekamilika
tutajua nini hasa kilitokea,lakini
kiulinzi tulikuwa tumejiandaa
sana” akasema Dr Fabian.
“Kama ningejua Rebeca
wangu anakuja kufa
nisingemruhusu laini sikuwa na
wasiwasi wowote na usalama
wake ndiyo maana
nikamruhusu aje” akasema kwa
uchungu Patrice
“Patrice lazima tumpate
huyu mtu James Kasai.Kwa
namna yoyote ile lazima
apatikane na alipe kwa hiki
alichotufanyia ! akasema Dr
Fabian
“James Kasai ! akasema
Patrice huku akiuma meno kwa
hasira
“James Kasai bazazi
mkubwa Yule ameniulia mke
wangu.Ninaapa sintafumba
jicho hadi nihAkikishe ametiwa
nguvuni ! akasema Patrice
Eyenga
Wakati mazungumzo
yakiendelea Dr Fabian
akajulishwa kwamba Rais
Benjamin Ntezimana wa
Rwanda tayari ametua katika
uwanja wa ndege wa Julius
Nyerere na alikuwa njiani
kuelekea ikulu
“Rais Benjamin tayari
ametua na muda wowote
atafika hapa”Dr Fabian
akamweleza Patrice Eyenga
“Benjamin naye anakuja?!
akauliza Patrice kwa hamaki
“Patrice nafahamu wewe na
Benjamin hamtazamani
machoni lakini kwa wakati huu
wekeni pembeni tofauti
zenu.Huu ni wakati ambao
mnapaswa kuonyesha
mshikamano mkubwa sana na
kuunganisha nguvu kupambana
na adui yetu mkubwa.Suala hili
ni zaidi ya tunavyofikiria.James
Kasai katika video yake
amesema kwamba ametekeleza
tukio lile kwa ajili ya kulipiza
kisasi kwako lakini kwa namna
ninavyolitazama tukio hilo ni
zaidi ya kulipiza kisasi”
“Dr Fabian kuna jambo
lolote ambalo unalifahamu
kuhusiana na tukio lile na
hujanieleza?akauliza Patrice
“Bado ni mapema sana
kusema chochote Patrice lakini
kwa namna ninavyolitazama
suala hili lilivyopangwa
nalazimika kuamini kwamba ni
zaidi ya kulipiza kisasi kwa
Rebeca” akasema Dr Fabian na
kunyamaza kidogo halafu
akasema
“Millen alinifuata siku moja
akanieleza kwamba balozi wa
DRC Germinus Mapupu
alimfuata ofisini kwake na
kumueleza kuwa anataka
kuwakutanisha wake za marais
wa Congo na Rwanda kwa
chakula watakapokuwa hapa
nchini kuhudhuria mkutano wa
wake za marais wa dunia na
akamuomba naye ahudhurie na
amualike pia na mke wa Rais
wa Rwanda kwani asingeweza
kukataa mwaliko wake.Mimi
nilimuunga mkono kwa suala
lile zuri na kumuahidi kumpa
ushirikiano mkubwa.Kila mara
alikuwa akinipa taarifa za
maendeleo ya mpango huo na
mimi nilivikabidhi vyombo vya
usalama kuhAkikisha ulinzi
unaimarishwa.Hadi siku ya
tukio niliwasiliana na watu wa
usalama na wakanihAkikishia
kwamba usalama
umeimarishwa lakini usiku
nikapewa taarifa kwamba
mabomu matatu yamelipuka na
mke wangu amefariki dunia”
akasema Dr Fabian na
kuinamisha kichwa chini
“Ningejua kama anakuja
Tanzania kuuawa
nisingemruhusu aje ! akasema
Patrice
“Hakuna aliyejua kama
tukio lile lingetokea.Wote
tuliamini tuko salama na ndiyo
maana nilimruhusu hata mke
wangu kwenda” akasema Dr
Fabian
Wakati wakiendelea na
maongezi wakajulishwa
kwamba Rais Benjamin
Ntezimana tayari alikuwa
amewasili ikulu.Dr Fabian
akatoka kwenda kumpokea
akamkaribisha ndani
wakazungumza faragha kwa
dakika ishirini halafu wakawa
na kikao cha pamoja kati ya
marais watatu kutoka
Tanzania,Rwanda na jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 7: EPISODE 2
Melanie Davis aliwasili
katika makazi ya Gosu Gosu na
kumkuta akimsubiri kwani
alimpigia simu mapema sana na
kumtaka asiende kazini siku ile
atakuwa na mazungumzo naye
muhimu.
“Karibu sana malaika
wangu” akasema Gosu Gosu
baada ya Melanie kuwasili
“Gosu Gosu mpenzi wangu
nafahamu tuna mengi ya
kuzungumza lakini unafahamu
kabla ya kitu chochote nini
ninahitaji” akasema Melanie na
Gosu Gosu hakutaka
mazungumzo zaidi akamfuata
pale sofani akambusu na
kumuinua akambeba kuelekea
chumbani.Mle chumbani
hakukuwa na kupoteza muda
mtanange ukaanza mara
moja.Gosu Gosu ambaye
alikuwa na pumzi kama farasi
alikwenda mizunguko miwili
bila kuchoka na kumpuuza
Melanie aliyekuwa akimuomba
Gosu Gosu wapumzike kwani
alikwisha fika kilele zaidi ya
mara tatu.
“Leo ulikuwa umenipania
sana” akasema Melanie huku
akimpiga Gosu Gosu kijikofi
kidogo na wote wakaangua
kicheko
“Sote tulikuwa
tumekamiana sana siku ya leo
ndiyo maana mchuano ulikuwa
mkali sana.Unawezaje kwenda
mizunguko miwili bila
kuchoka?Kuna kitu unatumia
cha kukuongezea nguvu?
Akauliza Melanie na Gosu Gosu
akaangua kicheko
“Situmii chochote cha
kuniongezea nguvu.Ninakula
vizuri na kuutunza mwili wangu
kwa mazoezi ndiyo maana nina
uwezo mkubwa namna
hii.Kama usingepiga kelele
ningeendelea hadi mzunguko
wa tatu” akasema Gosu Gosu na
wote wakaangua kicheko
“Nakupenda sana Gosu
Gosu.Sijui nikuelezaje ili ujue
namna ninavyokupenda”
akasema Melanie
“Nafahamu Melanie namna
unavyonipenda.Mimi pia
nakupenda zaidi ya
ninavyoweza kukueleza”
akajibu Gosu Gosu na kumbusu
Melanie
“Ule mpango wa kulipiza
kisasi ulifanikiwa vizuri
sana.Hongera” akasema Gosu
Gosu na Melanie akatoa
tabasamu
“Mpango wangu
umekwenda vizuri sana.Lengo
lilikuwa ni kumuua Rebeca
peke yake lakini ilishindikana
kumuua mwenyewe bila wale
wenzake”
“Ni tukio kubwa na baya
zaidi kuwahi kutokea katika
ukanda huu wa Afrika
Mashariki kwa wake watatu wa
marais kuuawa katika
shambulio moja.Naamini
uchunguzi mkubwa
utafanyika.Nina wasiwasi sitaki
uingie katika matatizo mpenzi
wangu” akasema Gosu Gosu
Melanie akatabasamu na
kusema
“Relax my Gosu
Gosu.Hawana tena haja ya
kufanya uchunguzi wakati
aliyefanya shambulio lile tayari
wanamfahamu.Unadhani kwa
nini tulimfuata James Kasai?Ni
kwa sababu ya jambo hili.Hivi
sasa nguvu yote inaelekezwa
kumtafuta yeye”
“Ni vipi kama James
akikamatwa na akakutaja
kwamba unashirikiana
naye?Gosu Gosu akauliza
“Kwanza si rahisi
kukamatwa na pili hata kama
akikamatwa na kunitaja mimi
sijali kwani nilichokuwa
nakitaka kimetimia.Hivi sasa
Patrice Eyenga yuko katika
majonzi makubwa sana.Moyo
wake unakatwa taratibu na kisu
kikali.Patrice atakufa taratibu
sana kwa mateso anayoyapata
kwa kifo hiki cha mke wake”
akasema Melanie huku
akitabasamu
“Vipi kuhusu IS kuhusika
katika shambulio lile?
“IS ?
“Ndiyo.Hawa ni magaidi
ambao James amekiri
kushirikiana nao”
“Gosu Gosu usiwe na wasi
wasi wowote tafadhali.Mimi
ninayemtambua ni James Kasai
na si IS.Kama yeye
anashirikiana na magaidi ni juu
yake.Gosu Gosu wewe ni
mwanajeshi na hupaswi kuwa
na wasiwasi wowote” akasema
Melanie
“Lazima niwe na wasiwasi
kwa sababu sitaki uingie katika
matatizo” akasema Gosu Gosu
“Tuachane na hayo Gosu
Gosu kwani leo ni siku ya furaha
sana kwa kufanikiwa kulipiza
kisasi kwa Patrice Eyenga”
akasema Melanie huku
Akikichezea kifua cha Gosu
Gosu
“Gosu Gosu uliwahi
kunitamkia kwamba uko tayari
kufanya chochote kwa ajili
yangu”
“Ndiyo Melanie.Niko tayari
kufanya chochote kwa ajili
yako”
“Ahsante sana Gosu
Gosu.Kuna mtu nahitaji
kumuondoa pia”
“Niambie ni nani huyo mtu
nikamtoe roho yake hata sasa
hivi? Akauliza Gosu Gosu
“Hayuko hapa
Tanzania.Yuko Paris Ufaransa”
akasema Melanie na Gosu Gosu
akashusha pumzi na
kumuangalia
“Ni nani huyo mtu na
amefanya nini?akauliza Gosu
Gosu
“Usitake kujua amefanya
nini.Mtu yeyote ambaye
ninataka kumuondoa duniani
fahamu kwamba amenifanyia
jambo zito hivyo hata huyu
ambaye nataka kumtanguliza
huko waendako wafu
amenifanyia jambo baya
kabisa.Ninachotaka kujua ni je
uko tayari kunisaidia? Akauliza
Melanie huku akitabasamu
“Melanie nadhani jibu
tayari unalo kwamba mimi niko
tayari muda wowote ule
kufanya chochote kwa ajili
yako.Nielekeze mahala
anakopatikana mtu huyo na
mimi nitakwenda kumtoa roho
yake” akasema Gosu Gosu.
“That’s my Gosu Gosu”
akasema Melanie na
kumbusu.Nitakupa taarifa zake
zote baadae ila anza kufanya
maandalizi kwani unatakiwa
kesho kutwa uondoke kuelekea
Paris”
“Hakuna tatizo
Melanie.Nitaanza maandalizi
mara moja na nitakwenda
kumtoa uhai wake huyo mtu
unayemtaka.Kuanzia sasa
usihangaike tena kwenda kwa
akina James Kasai au
kwingineko.Kama unataka
kumuondoa mtu uhai niambie
mimi nitatekeleza” akasema
Gosu Gosu
“Nakupenda Gosu Gosu na
sitaki kukuingiza katika hatari
ndiyo maana ninawatumia watu
kama akina James Kasai katika
mipango yangu ya kulipiza
kisasi.” akasema Melanie huku
akitabasamu
“Ni watu wangapi ambao
bado wako katika orodha ya
wale ambao unataka
kuwaondoa duniani? Gosu Gosu
akauliza
“Sina orodha bali nina watu
wachache tu ambao nataka
walipe uovu wao wakimalizika
hao nitakuwa nimewatendea
haki wazazi wangu kwani
niliwaahidi kuwalipia kisasi”
akasema Melanie.Baada ya
dakika chache wakaingia tena
katika mzunguko mwingine wa
tatu halafu Melanie akaondoka
kuelekea nyumbani kwake
akamuacha GosuGosu
akijiandaa kwenda
kushughulikia safari ya
kuelekea Paris.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 7: EPISODE 3
Kikao cha faragha baina ya
marais wa Tanzania,Rwanda na
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo kilichochukua saa tatu
kilimalizika halafu marais wote
watatu wakajitokeza mbele ya
waandishi wa habari waliokuwa
wamekusanyika ikulu
wakisubiri kikao kile kimalizike
ili wapate walau neno kutoka
kwa marais wale.Toka
lilipotokea shambulio lile baya
Rais wa Tanzania Dr Fabian
hakuwa amezungumza
lolote.Vituo karibu vyote vya
matangazo vilikatisha
matangazo yao na kujiunga
moja kwa moja ikulu kusikiliza
hotuba ya Rais.
Ndani ya ukumbi watu
wote wakasimama baada ya
marais kuingia.Mkurugenzi wa
mawasiliano ya Rais
hakupoteza muda
akamkaribisha moja kwa moja
Rais Dr Fabian aweze kusema
neno kwa niaba ya marais
wenzake wa Rwanda na
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo.
“Poleni sana ndugu
waandishi wa habari kwa
kutusubiri muda
mrefu.Tulikuwa na kikao kizito
kidogo ndiyo maana
tumechelewa” akasema Dr
Fabian halafu akaitazama
karatasi yake na kuendelea
“Ndugu wanahabari awali
ya yote nipende kuwashukusu
sana kwa kufika kwenu kwa
wingi.Nimeelezwa kwamba
wengi wenu mmefika hapa toka
asubuhi lakini hamjakata tamaa
kusubiri ili kuwapelekea
watanzania taarifa” akasema Dr
Fabian na kunyamaza kidogo
halafu akaendelea
“Ndugu zangu siku ya jana
nchi yetu na jumuiya ya Afrika
Mashariki imepata pigo
kubwa.Watu wasio na hata
chembe ya huruma wamefanya
shambulio ambalo limepelekea
mauaji ya watu hamsini na saba
kupoteza maisha na miongoni
mwao ni wake za marais wa
Rwanda,jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo na mke
wangu mimi,pia mabalozi wa
Rwanda na jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo wao
wanaoziwakilisha nchi zao hapa
nchini pamoja na familia zao
wamepoteza maisha.Hili ni
moja ya tukio baya kabisa.
Tukio hilo lilitokea
nyumbani kwa balozi wa
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo ndugu Germinus Mapupu
ambapo walikuwa
wamehudhuria hafla ya chakula
cha jioni ambacho balozi
Germinus Mapupu alikuwa
amekiandaa kwa ajili ya bi
Rebeca Muyenga mke wa Rais
wa Congo na Agatha Ntezimana
mke wa Rais wa Rwanda.Lengo
kubwa la kuandaa chakula
hicho lilikuwa ni
kuwakutanisha pamoja wake
hao za marais ikiwa ni katika
jitihada za kuondoa tofauti
zao.Kama mnavyofahamu kwa
muda sasa nchi za Rwanda na
Congo hazina maelewano
mazuri na balozi Mapupu
alitaka kutumia fursa hii
ambayo wake hao za marais
wote wanakutana hapa Dar es
salaam kwa ajili ya kuanza
mchakato wa kutafuta
maelewano baina ya nchi zao
lakini lengo lake hilo jema
halikuweza kufanikiwa kwani
wote waliuawa.Ni ukatili
mkubwa sana ambao
haukubaliki.
Baada ya tukio lile la mauaji
hayo ya kinyama mtu anayejiita
James Kasai alijitokeza na
kusambaza video akidai
kuhusika katika shambulio hilo
akishirikiana na kikundi cha
kigaidi cha IS ambacho kwa
miaka ya karibuni kimekuwa
kikijiimarisha sana katika bara
la Afrika hususan ukanda huu
wa Afrika Mashariki.Si mara ya
kwanza kwa kikundi cha IS
kufanya shambulio katika nchi
yetu.Watanzania bado
hawajasahau kitendo
walichokifanya IS miaka
michache iliyopita pale
walipoteka wanafunzi na
kuwachinja kama kuku na sasa
wamerejea tena” Dr Fabian
akanyamaza kwa sekunde
chache halafu akasema
Huyu mtu anayeitwa James
Kasai ni nani? Akauliza Dr
Fabian na kunyamaza akameza
mate
“James Kasai anatokea
nchini Jamhuri ya kidemokrasia
ya Congo na anaongoza kikundi
cha waasi ambao kwa miaka
zaidi ya kumi wamekuwa
wakipigana na
serikali.Alipoingia madarakani
Rais Patrice Eyenga aliwaita
mezani viongozi wa makundi
yote ya serikali ambayo kwa
miaka mingi yalikuwa
yakipigana na serikali kwa
lengola kutafuta amani lakini ni
James Kasai pekee ambaye
alikataa kushiriki katika
majadiliano ya kuleta amani ya
Congo na aligoma kuweka
silaha chini hivyo akafurushwa
na jeshi la Congo na inaaminika
alikimbilia katika misitu ya
Kaskazini mwa Uganda na sasa
ameamua kushirikiana na
kikundi cha kigaidi cha IS na
kufanya shambulio baya katika
ardhi yetu.James Kasai
amekuwa ni tishio kubwa si
kwa Tanzania tu bali kwa
jumuiya nzima ya Afrika
Mashariki na hatuwezi
kumuacha akaendelea kuwa
tishio kwa nchi zetu lazima
uovu wake ufike mwisho
Mimi na wenzangu marais
wa Rwanda na jamhuri ya
kidemokrasi ya Congo
tumekuwa na kikao kizito cha
faragha na katika kikao hicho
tumeazimia kuunganisha nguvu
kuhAkikisha tunampata James
Kasai akiwa mzima au
amekufa.Kila nchi itatoa kikosi
cha wanajeshi na tutaunda
kikosi kimoja ambacho
kitakuwa na silaha na zana kali
za kivita ambacho kitakwenda
kumsaka James Kasai kokote
aliko.Kitapanda milima na
mabonde,kitavuka mito na
bahari,misitu na nyika na
kuhAkikisha James Kasai
anatikana akiwa mzima au
mfu.Narudia tena tutapanda
milima na mabonde,tutavupa
mito na bahari,misitu na nyika
tukimsaka James Kasai na
lazima tumpate akiwa mzima au
amekufa.
Tunaamini James Kasai
yuko katika misitu iliyo
Kaskazini mwa Uganda na
tunaamini serikali ya Uganda
wanalifahamu hilo lakini
wamekuwa wakimkingia kifua
hivyo basi tunaitaka serikali ya
Uganda ihAkikishe
inashirikiana na kikosi ambacho
kitaundwa kwa ajili ya
kumtafuta James Kasai.Mtu
huyu mkatili asiye na hata
chembe ya ubinadamu yuko
ndani ya jumuiya ya Afrika
Mashariki na kwa mujibu wa
taratibu za jumuiya ya Afrika
Mashariki kunapotokea kitisho
chochote katika mojawapo ya
nchi wanachama basi nchi
nyingine zote wanachama
hujitolea vikosi vya jeshi
ambavyo vitakwenda
kupambana kuhAkikisha
kwamba nchi hiyo inakuwa
salama.James Kasai ni hatari si
kwa jamhuri ya kidemokrasia
ya Congo pekee bali kwa
jumuiya nzima ya Afrika
Mashariki hivyo nchi
wanachama zinatakiwa
kuunganisha nguvu kupambana
na adui huyu na ninawaahidi
wana Afrika mashariki
tutamfutilia mbali James
Kasai.Siku zake zinahesabika”
Dr Fabia akanyamaza baada
ya mpambe wake kumsogelea
na kumpa kijikaratasi
kilichosomeka
“Miili iko tayari kuelekea
uwanja wa ndege”
Dr Fabian akakisoma
kijikaratasi kile halafu
akaendelea na hotuba yake
Narejea tena kuwapeni pole
wana jumuiya ya Afrika
Mashariki kwa msiba huu mzito
uliotupata.Mimi nikiwa
mwenyekiti wa jumuiya hii
ninawahAkikishia kwa
kushirikiana na wenzangu
tutahAkikisha jumuiya yetu
inakuwa salama.TutahAkikisha
hakuna tena kitisho chochote
cha namna hii na watu kama
hawa wanaondolewa haraka
sana katika jumuiya yetu pale tu
wanapoibuka.
Mungu ibariki Afrika
Mashariki
Ahsanteni kwa kunisikiliza
Dr Fabian akamaliza hotuba
yake fupi na hakukuwa na
nafasi yoyote ya kuuliza
maswali.Akawaongoza wale
maraisi wenzake kutoka ndani
ya ukumbi ule wakaelekea nje
ambako magari yalikuwa
yameandaliwa na kwa pamoja
wakaondoka kuelekea uwanja
wa ndege wa Julius Nyerere
ambako miili ya marehemu
ilikuwa inapelekwa tayari kwa
kusafirishwa kuelekea katika
nchi zao.
Msafara wa marais watatu
uliwasili katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Julius
Nyerere ambako kuliandaliwa
shughuli maalum kwa ajili ya
kuaga miili ya marehemu kabla
ya kusafirishwa.Marais
walichukua nafasi zao
wakindelea kusubiri miili
iwasili.Watu walikuwa wengi
wakiwa wamekaa kwa utulivu
mkubwa na simanzi katika
mahema huku kwaya ikiwa
jukwaani ikiimba kuwafariji
.Ulinzi ulikuwa mkali mno eneo
lote la uwanja wa ndege.
Dakika chache baada ya
marais kuwasili pale uwanja wa
ndege wa Julus Nyerere magari
yaliyobeba majeneza yenye
miili ya marehemu yakawasili
na kufuata utaratibu majeneza
yakashushwa na
kupangwa.Viongozi wa dini
waliokuwepo mahala pale
wakapewa nafasi ya mwanzo ya
kuwaombea
marehemu.Hakukuwa na
hotuba yoyote iliyopangwa
kutolewa pale uwanjani hivyo
baada ya viongozi wa dini
kuwaombea marehemu
likafuata zoezi dogo la kuaga
miili ya
marehemu.Waliopangwa kuaga
miili ile pale uwanjani ni
wafanyakazi wa balozi za
Rwanda na jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo vile vile
raia wa nchi hizo wanaoishi
hapa nchini.Kulikuwepo vile
vile na kundi la wake za marais
walikuwa wamefika nchini
kuhudhuria mkutano wa wake
za marais ulioandaliwa na mke
wa Rais wa Tanzania marehemu
Millen Kelelo.Majeneza
hayakufunguliwa bali watu
walipita mbele yake kutoa
heshima za mwisho kwa
marehemu.Wakati zoezi
likiendelea,taratibu ndege mbili
za jeshi zilianza kusogea na
kujipanga vizuri.Zoezi la kutoa
heshima za mwisho kwa miili
ile ya marehemu lilimalizika na
wanajeshi wakasogea
wakabeba jeneza lenye mwili
wa marehemu Agatha
Ntezimana mke wa Rais wa
Rwanda wakaupeleka katika
ndege ya jeshi,ukafuatia mwili
wa balozi wa Rwanda na mke
wake pamoja na watu wengine
wa kutoka Rwanda waliouawa
katika shambulio.Lango la
ndege likafungwa na ndege
ikaondoka.Kikosi kingine cha
askari wakabeba jeneza lenye
mwili wa marehemu Rebeca
Eyenga mke wa Rais Patrice
Eyenga wa jamhuri ya
kidemokrasia na kuupakia
katika ndege ikafuatia miili ya
balozi Germinus Mapupu na
mingine ya watu kutoka
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo waliouawa katika
shambulio.Lango la ndege
likafungwa na ndege ikapaa
kuelekea Kinshasa.Lilikuwa ni
tukio lililoleta simanzi
kubwa.Dakika tatu baada ya
ndege za jeshi kuondoka,ndege
ya Rais Patrice Eyenga ikasogea
akakumbatiana na Dr Fabian
Kelelo pamoja na Rais Benjamin
Ntezimana kisha akaelekea
katika ndege yake ambayo
haikuchukua muda ikapaa na
kuondoka.Baada ya muda mfupi
ndege ya Rais Benjamin nayo
ikasogea akaagana na Dr Fabian
akapanda ndegeni naye
akaondoka kuelekea Kigali.
Rais Dr Fabian Kelelo
akaenda kuwasalimu
wanakwaya waliofika pale
kuwafarijji
waombolezaji,akasalimiana pia
na viongozi wa dini,akaagana na
baadhi ya wake za marais
waliokuwa wamekuja
kuhudhuria mkutano wa wake
za marais kisha akaondoka pale
uwanjani kurejea ikulu
“James Kasai ! akawaza Dr
Fabian akiwa garini.Jina hili
lilipita kichwani kwake kila
mara na kumfanya akunje sura
kwa hasira
“Bazazi huyu nitamfundisha
adabu.Hiki alichokifanya atalipa
kwa gharama kubwa sana”
akawaza na kuchukua simu
akazitafuta namba za simu za
Rais wa Uganda akampigia na
kuelezwa kwamba yuko katika
kikao muhimu
“Huyu ndiye ambaye
amemuhifadhi James Kasai
nchini Uganda japokuwa
amekuwa akikanusha vikali
kufanya hivyo lakini ukweli
tunao kwamba James Kasai
yuko nchini Uganda na sintajali
kama mimi na yeye ni
marafiki,tunakwenda kuvamia
Uganda kumtafuta James
Kasai.Sijali kitakachotokea
kama ni vita niko tayari
kuingiza nchi vitani lakini
lazima James apatikane”
akawaza Dr Fabian ambaye
sura yake ilitawaliwa na
majonzi makubwa.
Alipokaribia kufika ikulu
simu yake ikaita alikuwa ni
Jenerali Akiki Rwamirama Rais
wa Uganda.Dr Fabiana
akaitazama simu ile kwa hasira
kisha akaipokea
“Hallow mheshimiwa Rais”
akasema Dr Fabian
“Dr Fabian nimeikosa simu
yako nilikuwa katika kikao
muhimu”
“Mheshimiwa naomba
nikupigie simu baada ya dakika
tano” akasema Dr Fabian na
kukata simu.Gari lilifika ikulu
akashuka na kuelekea
chumbani kwake akachukua
simu na kuvuta pumzi ndefu
kisha akampigia Jenerali Akiki
“Dr Fabian habari yako.Pole
sana kwa tukio lililotokea.Mara
tu nilipopata taarifa za tukio lile
nilikupigia simu kukupa pole
lakini simu yangu
haikupokelewa.Kwa niaba ya
wananchi wa Uganda ninakupa
pole sana kwa tukio
lililotokea.Tuko pamoja na
msiba huu ni wetu sote.Pole
sana mheshimiwa Rais”
akasema Jenerali Akiki na sura
ya Dr Fabina ikajikunja kwa
hasira
“Jenerali Akiki hauko
pamoja na sisi na
usinidanganye kwamba msiba
huu umekugusa!
“Kwa nini unasema hivyo
mheshimiwa Rais? Sisi ni
ndugu.Uganda na Tanzania tuna
mahusiano ya kindugu hivyo
msiba huu ni msiba wa
Tanzania ni msiba wa Uganda
na ni msiba wa Afrika
mashariki.Uganda tunalia kama
mnavyolia watanzania Congo na
Rwanda” akasema Jenerali
Akiki
“Kama kweli msiba huu
umekugusa nataka unieleze
mahala alipo James Kasai !
akasema Dr Fabian
“James Kasai?
“Ndiyo.Humfahamu?
“Ninamfahamu James Kasai
lakini hayupo Uganda !
“Usinidanganye Jenerali
Akiki.James Kasai yuko Uganda
na umempa hifadhi”
“Hilo si kweli Dr
Fabian.James Kasai hayupo
nchini Uganda.Taarifa
nilizonazo ni kwamba James
Kasai amejificha katika misitu
ya Congo.Tafadhali usiziamini
taarifa zinazotolewa na Congo
na Rwanda wakidai kwamba
James Kasai yuko Uganda”
“Jenerali Akiki,tunao
ushahidi wa kutosha kwamba
James yuko nchini Uganda na
kwa kuwa hutaki kuweka wazi
mahala alipo,sisi tunaandaa
kikosi ambacho kitaingia katika
misitu ya Uganda kuendesha
operesheni ya kumsaka.Itakuwa
ni operesheni kubwa kuwahi
kufanywa na vikosi vya afrika
mashariki.Tutapita msitu kwa
msitu hadi tuhAkikishe James
Kasai anapatikana akiwa mzima
au mfu ! akasema Dr Fabian
ambaye uso wake ulionyesha
hakuhitaji masihara.Zilipita
sekunde kadhaa Jenerali Akiki
akasema
“Usiku wa kuamkia
jana,ndege za jeshi la Rwanda
zilivamia anga letu na kufanya
mashambulizi katika vijiji
vilivyopo kandoni mwa misitu
iliyopo Kaskazini ambako
wanadai James Kasai
amejificha.Katika mashambulio
hayo watu tisa waliuawa na
vijiji kadhaa kharibiwa
vibaya.Vikosi vya jeshi letu la
anga vilifanikiwa kuangusha
ndege mbili za Rwanda
zilizoingia katika anga letu kwa
lengo la kufanya mashambulizi”
akanyamaza kidogo na
kuendelea
“Asubuhi ya leo
nimezugumza na vikosi vya
jeshi na nimeagiza vikosi vyote
vya jeshi vikae katka utayari wa
vita.Tayari nimepeleka vikosi
katika mpaka wetu na Rwanda
na muda wowote vikosi
vitaingia Rwanda kulipiza kisasi
kwa kile ambacho tunakiita ni
uchokozi mkubwa.Rwanda
wametuvamia na kuua watu
wetu bila hata kuwa na uhakika
kama kweli James Kasai yupo
nchini Uganda.Kitendo kile
hakivumiliki na hakiwezi
kuachwa hivi hivi lazima
tuchukue hatua kali ndiyo
maana nataka niifanye nchi ya
Rwanda kama mfano kwa wale
wengine wote ambao wanataka
kufanyia mchezo
Uganda.Naomba nikuweke wazi
Dr Fabian kwa kuwa wewe
ndiye mwenyekiti wa jumuiya
ya Afrika Mashariki kwamba
ninajiandaa kuingia katika vita
na Rwanda na nchi nyingine
yoyote ambayo itathubutu
kuvamia Uganda” akasema
Jenerali Akiki
“Jenereali Akiki tafadhal
usithubutu kufanya hicho
unachotaka
kukifanya.Ukithubutu kuivamia
kijeshi Rwanda basi nchi zote za
Afrika mashariki zitamuunga
mkono Rwanda”
“Hilo haliniogopeshi Dr
Fabian.Umekwisha nihAkikishia
kwamba mmekutana Dar es
salaam na marais wa Rwanda
na Congo na tayari mmepanga
kuivamia Uganda.Ninawaonya
msithubutu kufanya
hivyo.Msithubutu kamwe
kutuma wanajeshi wenu nchini
Uganda kwani hawatafika
kokote nitawafyekelea
mbali.Jeshi langu limekwisha
jiandaa na liko tayari kwa
vita.Siogopi kama
mtaunganisha nguvu lakini
nataka kukuhAkikishia jambo
moja kwamba jeshi langu linao
uwezo wa kupambana na
majeshi yenu yote.Nakuonya Dr
Fabian usiingize nchi yako
vitani utajutia uamuzi
wako.Jeshi la Uganda la sasa si
lile la Iddi Amin mliyemchakaza
wakati ule.Hili ni jeshi jipya
ambalo lina uwezo wa
kupambana na majeshi ya nchi
yoyote.Ninawakaribisha
wanajeshi wenu lakini chimbeni
makaburi ya kutosha kwani
hakuna atakayerejea nyumbani
salama.Hakuna ambaye
atavamia ardhi ya Uganda
akatoka akiwa salama.Hivi si
vitisho nazungumza ukweli na
kama hamuamini
ninachokisema basi subirini
muone kile kitakachotokea
nchini Rwanda ! akasema
Jenerali Akiki na kukata simu
“Aaagh !! akasema kwa
hasira Dr Fabian
“Hakuna nchi yoyote ndani
ya Afrika Mashariki inayoweza
kuitisha Tanzania kijeshi.Akiki
akitaka kupigana na Tanzania
utakuwa ndio mwisho
wake.Tutatuma kwanza kikosi
cha umoja kwenda kumtafuta
James Kasai na kama
ikionekana upo ulazima basi
nitalituma jeshi la wananchi
kwenda Uganda lakini
operesheni kama hii ni
ndogo.Kikosi kidogo tu
kitakwenda kikishirikiana na
vikosi vingine kutoka Rwanda
na Congo” akawaza Dr Fabian
na simu yake ikaita akajulishwa
kuwa anahitajika katika kamati
ya maandalizi
KAMPALA – UGANDA
Baada ya kumaliza
mazungumzo na Dr
Fabian,Jenerali Akiki akampigia
simu James Kasai
“Mheshimiwa Rais”
akasema James Kasai
“James nimekupigia
tena.Nimetoka kuzungumza na
Rais wa Tanzania muda mfupi
uliopita na mazungumzo yetu
hayakwenda vizuri.Kwa mara
ya kwanza tumefokeana na
kutoleana vitisho vya
kushambuliana kijeshi.Jambo
lingine ni kwamba marais wa
Congo na Rwanda wote
wamekutana nchini Tanzania
na kwa pamoja wamekubaliana
kuunda kikosi ambacho
kitafanya operesheni ya kijeshi
kukusaka.Hivi tuzungumzavyo
tayari maandalizi ya kikosi
hicho yameanza na pale
kitakapokuwa tayari kitatumwa
Uganda.Wanafahamu mahala
vilipo vikosi vyako hivyo kwa
usalama wao nakuomba
uviondoe ili kikosi hicho
kitakapofika wakute tayari
wamekwisha ondoka” akasema
Jenerali Akiki
“Nimekuelewa mheshimiwa
Rais na tayari maandalizi
yamekwisha anza ya
kuondoka.Nategemea usiku wa
leo vijana wataanza
safari.Nitakujulisha pale
watakapokuwa wameanza
kuondoka”
“Vizuri sana.Endapo kuna
msaada wowote utauhitaji
usisite kunijulisha mara moja
nitakusaidia” akasema Jenerali
Akiki
“Nashukuru sana
mheshimiwa Rais kwa kila
kitu.Pale nitakapokuwa na
uhitaji wa chochote basi
nitakujulisha” akasema James
Kasai na kuagana na Rais.
“Pamoja na umuhimu wake
kwetu lakini James Kasai
ameniingiza katika matatizo
makubwa sana.Amevuruga
mahusiano yetu mazuri na nchi
nyingine za Afrika Mashariki na
hadi tumefikia hatua ya
kutishiana kijeshi.Sikupenda
kabisa kulumbana na Rais wa
Tanzania ambao wamekuwa ni
ndugu zetu kwa miaka mingi
lakini imelazimu kufanya hivyo
kwa ajili ya kumlinda
James.Sitaki kuingia katika vita
na Tanzania kwani ina jeshi
bora mno…” akawaza Jenerali
Akiki na kukuna kichwa.
“Kwa sasa mambo
yamekwisha haribika
nimekwisha tunisha misuli
hivyo sitakiwi kulegea.Natakiwa
kuendelea kutunisha misuli ili
kuonyesha kweli nimedhamiria
kupigana na jeshi la nchi yoyote
ambayo itathubutu kuvuka
mpaka na kuingia Uganda.Kwa
nchi ya Rwanda lazima niipe
onyo ili siku nyingine wasirudie
kitendo walichokifanya cha
kuvuka mpaka na kushambulia
Uganda” akawaza Jenerali Akiki
na kumpigia simu waziri wa
mambo ya nje wa Uganda
akamtaka awarejeshe
nyumbani mabalozi wa Uganda
walioko katika nchi za Rwanda
na jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo na vile vile akamtaka
awaelekeze mabalozi
wanaoziwakilisha nchi hizo
nchini Uganda waondoke
haraka sana Uganda ndani ya
saa ishirini na nne.
DAR ES SALAAM – TANZANIA
Ilikaribia saa moja za jioni
jijini Dar es salaam muda
ambao Melanie Davis alikuwa
akijiandaa kwenda nyumbani
kwa Gosu Gosu kwani
waliahidiana kukutana jioni ya
siku ile kwa ajili ya
mazungumzo.Akiwa chumbani
kwake akijiandaa simu yake
ikaita akatazama mpigaji
alikuwa ni katibu wake muhtasi
Frimina
“Mina unasemaje?akauliza
Melanie
“Madam kuna tatizo”
akasema Frimina na Melanie
akastuka kidogo
“Kuna tatizo gani? akauliza
“Nimepata taarifa muda si
mrefu kwamba Gosu Gosu
amepigwa risasi”
“Gosu Gosu ! Oh my God !
Melanie akastuka sana na
kuangusha kifaa alichokuwa
amekishika mkononi
“Madam Melanie ! akaita
Frimina
“Mina kuna kitu kimoja tu
ambacho nataka kukisikia
kutoka kwako.Is he okay?
“Nimeambiwa kwamba
amekimbizwa hospitali na hali
yake ni mbaya sana”
“Yuko hospitali
gani?akauliza Melanie
“Nimeambiwa amepelekwa
hospitali kuu ya Mtodora”
akasema Frimina na Melanie
akahisi miguu yake inaisha
nguvu akakaa kitandani.
“Gosu Gosu jamani !
akasema Melanie.Hakupoteza
muda akachukua mkoba wake
na kutoka mbio akamfuata
Joyce akamtaka ampeleke
katika hospitali ya Mtodora
“Gosu Gosu tafadhali
naomba usiniache.Bado
ninakuhitaji sana katika maisha
yangu.Una umuhimu mkubwa”
akawaza Melanie huku machozi
yakimporomoka
“Ni nani hawa waliompiga
risasi Gosu Gosu na kwa nini?
Akaendelea kujiuliza maswali.
“Endapo Gosu Gosu
akifariki dunia litakuwa ni pigo
lingine kubwa kwa upande
wangu.Ni mtu ninayemtegemea
kwa mambo mengi.Kama si
yeye nisingeweza kuonana na
James Kasai.Ni yeye ambaye
kila wakati anaifanya akili
yangu ikae sawa.Ni mtu
muhimu sana katika maisha
yangu” akaendelea kuwaza
huku gari likiwa katika mwendo
mkali kuelekea hospitali.Mara
kwa mara alivua miwani na
kufuta machozi
“Gosu Gosu kupigwa risasi
imetonesha kidonda
changu.Kitendo hiki
kimenikumbusha machungu ya
wazazi wangu.” akawaza na
kuendelea kufuta machozi
Walifika katika hospitali ya
Mtodora na Melanie akashuka
na kukimbia hadi katika jengo
la mapokezi akajitambulisha
kuwa ndugu yake amepigwa
risasi na ameletwa pale
hospitali.
“Kuna wagongwa kadhaa
wamepokelewa hapa hospitali
jioni hii wakiwa na majeraha ya
sirasi.Ndugu yako anaitwa
nani?akauliza muuguzi wa
mapoezi
“Gosu Gosu”akatamka
Melanie na Yule muuguzi
akatazama katika kompyuta
yake
“Papi Gosu Gosu” akasema
Yule muuguzi
“Ndiyo”
“Mgonjwa wako yuko hapa
hospitali lakini kwa sasa
ameingizwa katika chumba cha
upasuaji” akasema Yule
muuguzi na kumuelekeza
Melanie kilipo chumba cha
upasuaji kisha kwa haraka
akiwa na Joyce wakaelekea
huko.
Mlango wa chumba cha
upasuaji ulikuwa umefungwa
na hakuruhusiwa mtu
asiyehusika kuingia ndani ya
chumba kile hivyo kuwalazimu
akina Melanie kusubiri nje.
“Ee Mungu naomba
umponye Gosu Gosu” hii ndiyo
kauli ambayo Melanie alibaki
anaitamka kimoyo
moyo.Alishindwa kukaa
akanyanyuka na kuanza
kuzunguka zunguka
“Madam Melanie kaa
upumzike tafadhali.Hatujui
upasuaji huo utachukua muda
gan..” akasema Joyce na mara
mlango ukafunguliwa akatoka
muuguzi mmoja aliyevaa
mavazi ya kijani Melanie
akamkimbilia
“Dada samahani” akasema
Melanie na Yule muuguzi
akasimama
“Ndugu yangu ameingizwa
humu kufanyiwa upasuaji
amepigwa risasi vipi hal….”
“Bado yuko kwenye
upasuaji.Endeleeni kusubiri
hadi upasuaji ukimalizika
mtajulishwa kila kitu” akasema
Yule mwanadada na kuendelea
na safari
“Madam Melanie kaa utulie
utachoka sana ukiendelea
kusimama.Yawezekana
upasuaji ukachukua muda
mrefu” akasema Joyce
“Nashindwa kukaa
Joyce.Ninapata wakati mgumu
sana” akajibu Melanie na
kuchukua simu akampigia
Frimina
“Frimina tayari niko hapa
hospitali lakini Gosu Gosu
ameingizwa katika chumba cha
upasuaji niko hapa na Joyce
tunasubiri upasuaji
umalizike.Nataka uniambie
tukio hili limetokea wapi?
“Gosu Gosu leo hakuwepo
kazini kwa siku nzima lakini
jioni ya leo alikuja ofisini kwake
kuna vitu alikuja kuchukua
akaniaga kwamba atakuwa na
safari ya Paris kesho
kutwa.Muda mfupi baada ya
kuondoka nikapigiwa simu na
walinzi kwamba Gosu Gosu
amepigwa risasi wakati
akijiandaa kuingia barabara
kuu.Inadaiwa kwamba
walijitokeza watu wawili
waliokuwa na pikipiki kubwa
wote wakiwa wamevaa mavazi
meusi na kofia ngumu kichwani
hivyo sura zao hazikuweza
kuonekana.Mmoja aliyekuwa
nyuma alikuwa na bunduki
ndogo akaanza kulimiminia
risasi gari la Gosu Gosu huku
mwenzake akimimina risasi juu
kuzuia watu wasisogee eneo lile
na baada ya kuhAkikisha
kwamba wamemimina risasi za
kutosha wakaondoka na hakuna
mpaka sasa aliyewatambua
watu hao ni akina nani”
akasema Frimina
“Dah ! akasema Melanie na
kushika kiuno
“Ahsante
Frimina.Nitaendelea
kuwasiliana nawe kuhusiana na
kile kinachoendelea hapa”
akasema Melanie na kukata
simu
“Ni nani hawa
waliomshambulia Gosu
Gosu?Nini walikuwa
wanakihitaji kutoka
kwake?Nadhani hawa jamaa
lengo lao lilikuwa ni kumuua tu”
akaendelea kuwaza
Walikaa pale nje kwa muda
wa saa tano ndipo alipotoka
daktari na kuwapa taarifa
“Poleni sana kwa
kusubiri.Tumefanya upasuaji
wa kuondoa risasi mwilini mwa
mgonjwa wenu.Jumla alikuwa
amepigwa risasi kumi na mbili
katika sehemu mbali mbali za
mwili wake.Risasi mbili
alipigwa katika bega la
kulia,risasi moja katika kiganja
cha mkono wa kulia,saba katika
sehemu ya juu ya paja,na mbili
sehemu ya chini ya mguu wa
kulia.Inaonekana mshambuliaji
alikuwa upande wa kulia kwani
ndio hasa
ulioshambuliwa.Risasi nyingine
zaidi ya kumi hazikuweza
kuingia mwilini mwake kwa
kuwa alikuwa amevaa fulana
isiyopenya risasi na bila fulana
hiyo asingeweza kuwa hai hadi
sasa kwani inaonekana
washambuliaji hao walikuwa na
lengo la kuua kabisa.Kwa sasa
atapelekwa katika chumba cha
uangalizi maalum huku
tukiangalia hali yake kwa
ukaribu zaidi” akasema daktari
“Daktari nakushukuru sana
kwa kazi kubwa mliyoifanya
lakini naomba ufanye kila lililo
ndani ya uwezo wako
kuhAkikisha ndugu yangu
anapona na kama utaona kuna
ulazima wa kumpeleka nje ya
nchi basi usisite kunishauri
hivyo daktari nakuomba sana”
akasema Melanie huku michirizi
ya machozi ikionekana machoni
pake
“Usijali mama.Ni kazi yetu
kuhAkikisha tunaokoa maisha
ya kila mgonjwa anayeletwa
hapa hospitali.Nakuahidi
kufanya kila lililo ndani ya
uwezo wangu kuhAkikisha
mgonjwa wako
anapona”akasema Melanie na
kuelekeza macho mlangoni
ambako mlango mkubwa
ulifunguliwa na kitanda
kikatolewa kikisukumwa na
wauguzi.Juu ya kitanda kile
alikuwa amelala Gosu Gosu
akiwa hana fahamu.Melanie na
Joyce wakawafuata wauguzi
wale hadi katika chumba cha
uangalizi maalum ambako akina
Melanie hawakuruhusiwa
kuingia kwa usiku ule
“Madam hakuna
tunachoendelea kukifanya hapa
twende nyumbani ukapumzike
kisha tutakuja tena kesho
alfajiri kujua maendeleo ya
mgonjwa.Kama kutakuwa na
mabadiliko yoyote wauguzi
wapo watatujulisha” akasema
Joyce
“Ni kweli Joyce.Twende
tukapumzike” akasema
Melanie.Joyce akazungumza na
wauguzi na kuwataka
wawajulishe endapo kutakuwa
na mabadiliko yoyote kwa
mgonjwa.
Waliondoka pale hospitali
huku kichwa cha Melanie
kikiwa kizito kwa mawazo
akijiuliza ni nani waliofanya
tukio lile na kwa nini Gosu Gosu
amepigwa risasi?
“Joyce twende nyumbani
kwa Gosu Gosu.Nataka
nikazungumze na mtumishi
wake wa ndani” akasema
Melanie na Joyce akaendesha
gari hadi nyumbani kwa Gosu
Gosu.Walinzi wote walikuwa
wakimfahamu hivyo
wakamkaribisha ndani na
kumuamsha mtumishi wa ndani
wa Gosu Gosu kama Melanie
alivyokuwa ameelekeza.
“Karibu sana mama
Melanie” akasema Yule
mtumishi ambaye alionekana
kutofahamu chochote
kilichokuwa kimetokea
“Ahsante nashukuru”
akasema Melanie
“Mama chumbani kwa kaka
kuko wazi kama unataka
kwenda lakini yeye bado
hajarudi hadi mida hii” akasema
Yule mtumishi
“Lucy hilo ndilo hasa
lililonileta hapa”akasema
Melanie na kunyamaza kidogo
“Nimetokea hospitali.Gosu
Gosu amepatwa na matatizo”
“Matatizo gani?akauliza
Lucy kwa mstuko
“Amepigwa risasi na watu
wasiojulikana” akasema
Melanie na Lucy akaangua kilio
“Tafadhali usilie Lucy.Gosu
Gosu hajafa lakini hali yake si
nzuri yuko katika chumba cha
uangalizi maalum baada ya
kufanyiwa upasuaji wa kuondoa
risasi alizokuwa amepigwa”
akasema Melanie na kumlazimu
Joyce kumbembeleza Lucy
anyamaze
“Nimekuja hapa kukupa
taarifa hizo kwani niliamini
bado hujazipata hata hivyo
kuna jambo nataka unisaidie
kulifahamu”
“Jambo gani?
“Nataka kujua kama kuna
mtu yeyote wa karibu wa Gosu
Gosu unayemfahamu aidha
ndugu au rafiki” akasema
Melane na Lucy akamtazama
kwa wasi wasi mkubwa.
“Usihofu Lucy Gosu Gosu ni
mzima” akasema Melanie baada
ya kuutambua wasiwasi
mkubwa aliokuwa nao Lucy
“Rafiki yake mkubwa
ambaye ninamfahamu anaitwa
Austin”
“Austin?
“Ndiyo”
“Anaishi wapi huyo Austin?
“Sifahamu anaishi wapi
lakini ninazo namba zake za
simu kama ukitaka kuwasiliana
naye” akasema Lucy na kwenda
chumbani akachukua simu yake
na kumpa Melanie namba za
simu za Austin akaziandika
katika simu yake akampigia
“Hallow” ikasema sauti ya
upande wa pili baada ya
kupokea simu
“Hallow Austin” akasema
Melanie
“Nani mwenzangu?
Akauliza Austin kwa mshangao
kidogo
“Naitwa Melanie
Davis.Unamfahamu Papi Gosu
Gosu?
“Ndiyo ni rafiki yangu.Kuna
nini? Akauliza Austin
“Naomba nikujulishe
kwamba Gosu Gosu amepatwa
na matatizo”
“Matatizo gani?
“Amepigwa risasi na watu
wasiojulikana jioni ya leo”
“Tafadhali
usinitanie”akasema Austin
“Si utani ni kitu cha kweli
kabisa.Alikimbizwa hospitali
amefanyiwa upasuaji na kwa
sasa amewekwa katika chumba
cha uangalizi maalum.Nimetoka
huko sasa hivi”akasema Melanie
“Wewe uko wapi hivi sasa”
akauliza Austin’
“Kwa sasa niko hapa
nyumbani kwake na mfanyakazi
wake Lucy ndiye aliyenipa
namba zako”
“Ahsante sana kwa taarifa
hii.Ninaelekea hospitali sasa
hivi” akasema Austin na
Melanie akakata simu akaagana
na Lucy wakaondoka kurejea
nyumbani.
Alipofika nyumbani kwake
akapitiliza moja kwa moja
chumbani akautupa mkoba
sofani “Kichwa kinaniuma
sana” akawaza Melanie na
kwenda kuchukua chupa ya
mvinyo akaenda kuketi sofani
na kuanza kunywa.Mara
akasikia mlio fulani ukitoka
katika mojawapo ya simu
yake.Ulikuwa ni mlio wa
kumfahamisha kwamba
kwamba kuna mtu alimpigia
simu lakini akamkosa.Akainuka
akaenda kuzitazama simu zake
na mojawapo ya simu
iliyopigwa ni ya Devotha.
“Devotha anataka nini
?Amepiga simu mara sita !
akawaza na kuamua kumpigia
“Hallo Devotha” akasema
Melanie baada ya simu yake
kupokelewa
“Hallo Melanie.How’s Gosu
Gosu?akauliza Devotha kwa
sauti yenye kicheko kidogo
ndani yake
“Gosu Gosu?
“Ndiyo anaendeleaje?Is he
dead? Akauliza Devotha na
Melanie akawa kimya huku
akihema haraka haraka.Sura
yake ilibadilika
“Sikiliza Melanie” akasema
Devotha
“Usihangaike kuumiza
kichwa chako nani waliompiga
risasi Gosu Gosu?My people
did” akasema Devotha
“What?! You wanted to kill
him?Why Devotha ?! akauliza
Melanie kwa uchungu
“Nilitaka kumuua kabla
hajaniua” akasema
Devotha.Melanie akastuka sana
kwa kauli ile ya Devotha
“Kwa nini unasema hivyo?
Akauliza Melanie
“Melanie Davis bado u
mchanga sana katika mambo
haya hivyo siku zote usitake
kushindana na wakubwa
zako.Ulidhani sintajua kama
umemtuma Gosu Gosu aje Paris
kuniua? Akauliza Devotha na
Melanie akawa kimya
“Nafahamu mipango yako
yote ninafuatilia kila
unachokifanya
Melanie.Ninafahamu Gosu Gosu
alikuwa aondoke kesho kuja
Paris kuniua.Ulifikiria nini
kumtuma Gosu Gosu aje kuniua
Melanie?Do you think it’s easy
to kill someone like me?
Akauliza Devotha huku akitoa
kicheko
“Bahati yake Yule jamaa
ana maisha marefu kama paka
lakini ule ni ujumbe kwamba
hata wewe ninaweza
nikakumaliza muda wowote
ninaotaka hivyo nataka uende
katika mstari tunaotaka
sisi.Nikikuelekeza fanya jambo
Fulani tekeleza na ukitaka
kwenda kinyume chake
matokeo yake hayatakuwa
mazuri.Hili ni onyo la mwisho
kwako na ukithubutu tena
kutaka kufanya mambo
unavyotaka wewe nitakuondoa
haraka bila kusita na
kumuweka mtu
mwingine.Umenisikia
Melanie?akauliza
Devotha.Melanie alikuwa
anatetemeka kwa ndani.
“Melanie umenielewa?
“Nimekuelewa”
“Good.Prepare yourself for
the next mission” akasema
Devotha na kukata simu.
“Oh my God ! akasema
Melanie na kuvuta pumzi ndefu
akaitupa simu kitandani
“Is this real or I’m
dreaming?akajiuliza
“Devotha amefahamuje
kama nimepanga mipango na
Gosu Gosu ya kwenda
kumuua?Kwa vyovyote vile
lazima kuna namna ambayo
amesikia mazungumzo
yetu.Hakuna mwingine ambaye
nimemueleza jambo hili zaidi ya
Gosu Gosu pekee.Nadhani ipo
namna ambayo hawa watu
wamefanya ili kuwawezesha
kufuatilia kila ninachokifanya
na kusikia kila
ninachokizungumza.Naamini
hivyo kwa sababu sifahamu
Devotha alifahamu vipi kuhusu
mimi kumfuata James Kasai?
Niliporejea kutoka Uganda
alinipigia na kunieleza kwamba
anafahamu nimetoka kuonana
na James Kasai.Nilijiuliza sana
amefahamu vipi sikupata jibu
lakini sasa nimefahamu.Swali
ninalojiuliza ni je kitu gani
wameniwekea ambacho
kinawafanya waweze
kunifuatilia kila
ninachokifanya? Kipo kitu
wameniwekea ambacho lazima
nikifahamu kwani bila
kukifahamu hakuna mpango
wangu utakaofanikiwa”
akawaza Melanie
Zaidi ya saa moja Melanie
alikuwa amekaa sofani akiwaza
namna Devotha anavyoweza
kunasa mazungumzo yake
akashindwa kupata jibu
“Kuna teknolojia kubwa
imetumika hapa na kufahamu
walichokifanya itanilazimu
nifanye majaribio
kadhaa.Kwanza nitahama hiki
chumba na kuhamia katika
chumba kingine ambacho
nitaweka kila kitu
kipya.Nitanunua kila kitu kipya
kuanzia mavazi hadi urembo.Hii
mikufu,heleni zote nitaziacha
sintazivaa tena yawezekana
kuna kifaa wameniwekea
ambacho kukibain itanichukua
muda mrefu.Nitaweka mfumo
mpya wa ulinzi katika chumba
change nitakachohamia ili
asiweze kuingia mtu mwingine
wakati sipo”akawaza Melanie
na kulala
RIYADH – SAUDI ARABIA
“Abu Zalawi unaonekana
kuguswa sana na tukio
lililotokea Tanzania.Umekuwa
unalifuatilia kwa karibu sana”
akasema Najma wakiwa
sebuleni ndani ya jumba lao
kubwa wakitazama runinga
huku Mathew akibadilisha
chaneli mbalimbali kutafuta
taarifa za kina za tukio
lile.Ulipita muda kidogo
Mathew akasema
“Fedha zile ulizosaini Dubai
kumtumia James Kasai ndizo
zimesababisha mauaji haya”
“Ni kweli.Tulipokwenda
Dubai nilisaini mkataba wa
kumtumia fedha James Kasai
ambaye ameingia mashirikiano
na kikundi cha IS.Usiniambie
umeguswa na kilichotokea
wakati nawe umewahi kuwa
gaidi na hizi ndizo zilikuwa
shughuli zenu kuua watu”
akasema Najma
“Uko sahihi nimepitia huko
katika ugaidi lakini kwa sasa
ninaanza kuondoka huko
taratibu”
“Usijali Abu Zalawi sisi kazi
yetu ni kutoa fedha kwa IS na
wanachokwenda kukifanya sisi
hakituhusu” akasema Najma
“Lakini ni ufadhili huu wa
fedha kwa vikundi vya kigaidi
ndiyo sababu inayomfanya
Habiba Jawad atafutwe sana na
mashirika makubwa ya kijasusi
duniani.Anatafutwa na
Mossad,CIA n.k. Kwa nini
tusiachane na mambo haya ya
kufadhili ugaidi tukaendelea na
maisha yetu ya kawaida?
Hatutakuwa na maisha ya
furaha na amani kama
tutaendelea na mambo haya ya
kufadhili ugaidi” akasema
Mathew akionekana kuumizwa
na kile kilichotokea Tanzania
“Abu Zalawi usiwe na hofu
sisi tuko salama”akajibu Najma
“Hatuko salama
Najma.Hujui ni namna gani
Habiba Jawad anatafutwa na
mataifa makubwa ambayo
yanaongoza katika kupiga vita
ugaidi duniani hasa Marekani
na Israel.Sikuwa nimekueleza
jambo hili lakini haikuwa rahisi
kuufikisha mwili wa seif Jawad
hapa.Majasusi wa Mossad
waliuwekea kifaa maalum cha
kuufuatilia kufahamu mahala
ulipo wakiamini kwamba
unaweza ukawasaidia kufika
kwa Habiba Jawad.Kwa bahati
nzuri niliweza kukigundua kifaa
hicho na kukiondoa.Kama
nisingeweza kukigundua mama
angekuwa katika matatizo
makubwa na yeye akiingia
katika matatizo sisi sote
mnakuwa kwenye
matatizo.Ninadhani ni wakati
wa mama Habiba kuachana na
mambo haya ya kufadhili ugaidi
akajielekeza katika biashara
zake” akasema Mathew Najma
akabaki kimya
“Najma mimi nilikuwa gaidi
na katika harakati zangu
nimekwisha ua watu wengi.Si
siku nyingi sana nililipua bomu
katika kituo cha treni jijini
Jerusalem na katika shambulio
lile watu wengi walipoteza
maisha.Baada ya kunusurika
katika mashambulio ya Israel
nilijiuliza nini sababu ya
kuendelea kuua watu?
Nimekuwa nikisoma
mafundisho mbali mbali ya dini
yetu na nimegundua kwamba
nilikuwa ninafanya kosa kubwa
kutumia kigezo cha dini
kuendesha mambo ya
kigaidi.Dini yetu ni dini safi na
hairuhusu ugaidi.Uislamu si
ugaidi bali wapo magaidi ndani
ya Uislamu.Binafsi nimeama
kuachana na mambo yale ya
ugaidi na kumcha mwenyezi
Mungu Subhanahu wa
ta’ala.Naamini hata wewe
ndicho kitu unachokitaka kwani
nakumbuka siku ile tukiwa
Dubai ulistuka sana baada ya
kuuona mgongo wangu na
ukanihAkikishia kwamba
maisha yale yamekwisha”
akasema Mathew
“Abu Zalawi hayo yote
uliyoyasema ninayafahamu na
ninatamani sana kutoka katika
maisha haya niishi maisha ya
kawaida ya amani.Hata mimi
sifurahii kufadhili ugaidi na kila
ninaposikia kundi Fulani la
kigaidi ambalo tunalifadhili
fedha limefanya shambulio
moyo wangu huumia sana
kwani katika mauaji hayo wapo
watoto,wanawake,wapo
waislamu na wasio
waislamu.Lakini mikono yangu
imefungwa na siwezi kufanya
chochote.Ninafuata maelekezo
ya mama.Kwa sasa mimi ndiye
ambaye amekuwa akinituma
sehemu mbali mbali
kumuwakilisha katika shughuli
zake mbali mbali na mikataba
mingi ya fedha mimi ndiyo
husaini badala yake”
“Ahsante sana Najma kwa
maneno hayo ambayo nilihitaji
sana kuyasikia.Lakini umewahi
kukaa na mama yako ukajaribu
kuzungumza naye kuhusiana na
athari za kufadhili ugaidi?
“Hapana sijawahi
kuzungumza naye
chochote.Kuna mambo ambayo
siwezi kuzungumza naye na
mojawapo ni suala hilo.Ni
mama yangu lakini Habiba
Jawad anatisha na akikasirika
wanasema huwa ni mbaya sana
ingawa sijawahi kumuona
akiwa amekasirika.Nasikia kuna
mambo ambayo ameyapiga
marufuku kuyazungumzia na
hilo ni kubwa ambalo hataki
lizungumzwe na neno la Habiba
Jawad ni amri” akasema Najma
“Nitazungumza naye kesho
juu ya suala hili” akasema
Mathew na Najma akamtazama
kwa mshangao
“Unataka kwenda
kuzungumza naye jambo hili?
“Ndiyo nitazungumza naye”
“Utaanzaje Abu
Zalawi?akauliza Najma
“Usihofu nitazungumza
naye kesho.Nitamfuata
nyumbani kwake” akasema
Mathew na Najma akaonyesha
wasiwasi kidogo
“Mbona unaonyesha hofu
Najma?
“Usimfuate nyumbani
kwake.Hapendi kufuatwa
kwake na kama ana jambo la
kukueleza basi atakuita yeye
mwenyewe.Labda umsubiri
atakapotoka kwenda kupata
kifungua kinywa ndipo uombe
kuzungumza naye lakini
usimfuate katika nyumba yake
ya kulala” akasema Najma
“Hujawahi kuingia katika
nyumba yake?
“Nimeingia mara nyingi
lakini pale tu yeye mwenyewe
aliponiita kwenda kuzungumza
au kunipa maagizo mbali mbali”
“Kwa nini hapendi watu
waingie ndani ya nyumba
yake?Kuna siri yoyote
anaificha?
“Mama yangu ni mtu
mwenye siri nyingi nadhani
ndiyo maana anachunga sana
watu kuingia ndani mwake.Kwa
mfano ofisi yake ipo ndani ya
jumba lake lakini hakuna
anayefahamu iko sehemu gani
bali yeye peke yake.Nasikia
kuna handaki ambalo anaweza
akajificha na kukaa humo hata
miaka mitano bila kutoka nje
lakini hakuna anayefahamu
mahala lilipo wala mlango wa
kuingilia.Kuna mtu mmoja tu
anayefahamu mengi kuhusu
jumba lile la mama naye ni bi
Nasrat Jazer.Huyu ninaambiwa
amekuwa mtumishi wa ndani
wa mama toka akiwa msichana
na hadi sasa amekuwa
mzee.Huyu ndiye ambaye
mama anamuamini sana kati na
ndiye pekee ambaye anaweza
akaingia na kutoka muda
wowote ndani ya jumba la
Habiba Jawad” akasema Najma
“Naj nakushukuru sana kwa
maelezo haya uliyonipa lakini
kesho nitamtafuta Habiba
nizungumze naye.Najua
haitakuwa rahisi kunielewa
lakini nitajaribu” akasema
Mathew akazima runinga na
kuelekea chumbani kulala.
“Nimeumizwa sana na tukio
lile la kigaidi nchini
Tanzania.Nilishuhudia wakati
fedha zikisainiwa ambazo
zimekwenda kumfadhili James
Kasai ambaye ametekeleza
shambulio lile.Kuua wake
watatu wa marais kwa mara
moja pamoja na mabalozi nini
hasa kusudio lake?Huyu James
anatokea jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo na
inasemekana anaishi nchini
Uganda kwa nini akashambulia
Tanzania ambayo kwa miaka
mingi imekuwa ni mhifadhi
mkuu wa wakimbizi wengi
kutoka nchini Congo?
Wanajeshi wa Tanzania
wamemwaga damu yao nchini
Congo wakiipigania amani ya
Congo kwa nini leo huyu mtu
mmoja aibuke na kufanya
mauaji yale makubwa?Au hii ni
mipango ya Habiba Jawad
kulipiza kisasi kwa kifo cha
mwanae Edger Kaka? Nadhani
ndilo hasa lilikuwa lengo lake
kumfadhili James Kasai fedha
nyingi ili aweze kufanya
shambulio lile.Nimeumizwa
sana na kitendo kile na ninaapa
lile litakuwa ni tukio la
mwisho.Sintakubali tena kundi
lolote la kigaidi kushambulia
Tanzania.Kesho nakwenda
kuzungumza na Habiba Jawad
anieleze ukweli kama
shambulio lile ni yeye ndiye
aliyelipanga na nini kusudio
lake?Nadhani uvumilivu
unaanza kunishinda siwezi tena
kuendelea kuvumilia kuona
ugaidi ukiendelea wakati ninao
uwezo wa kuzuia.Niko tayari
kupoteza maisha lakini niwe
nimemuua Habiba Jawad.Yule
mama bado hajanifahamu
vyema mimi ni kiumbe wa aina
gani” akawaza Mathew
DAR ES SALAAM – TANZANIA
Saa kumi na mbili za
asubuhi juu ya alama ilimkuta
tayari Melanie amewasili
hospitali ya Mtodora kwenda
kumtazama Gosu
Gosu.Alichokikuta hospitali pale
kilimmaliza nguvu.Hali ya Gosu
Gosu ilibadilika usiku na
kulazimika kumuwekea
mashine ya kumsaidia
kupumua.Melanie
hakuruhusiwa kuingia ndani
bali alimuona Gosu Gosu kupitia
kioo kikubwa.
“Maskini Gosu Gosu mpenzi
wangu usiniache.Tafadhali
usiondoke na kuniacha peke
yangu ! Melanie akawaza huku
akimtazama Gosu Gosu kupitia
kioo.Mara akashikwa bega na
kugeuka
“Habari yako dada” jamaa
mmoja mwenye mwili
uliojengeka
akamsalimu.Melanie hakuwa
akimfahamu yule jamaa.Akafuta
machozi na kusema
“Nzuri habari yako”
“Naitwa Austin January ni
rafiki wa karibu wa Gosu
Gosu.Natumai wewe ndiye
uliyenipigia simu jana usiku
kunijulisha masahibu haya
yaliyompata mwenzetu”
akasema Austin
“Ndiyo ni mimi.Naitwa
Melanie Davis”
“Melanie pole sana.Ni mara
ya kwanza tunaonana je wewe
ni ndugu yake? Akauliza Austin
“Gosu Gosu ni mchumba
wangu” akasema Melanie na
Austin akastuka kidogo halafu
akatabasamu
“Nafurahi
kukufahamu.Mimi ni rafiki yake
mkubwa” akasema Austin
“Nilifika jana nyumbani
kwake baada ya kutoka hapa
hospitali nikamuuliza mtumishi
wake wa ndani kama
anamfahamu rafiki au ndugu wa
karibu wa Gosu Gosu akanipa
namba zako nikakupigia”
akasema Melanie
“Gosu Gosu ana asili ya
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo lakini kwa sasa ni Raia
wa Tanzania.Hana ndugu
ninaye mfahamu huku Tanzania
na toka nilipokutana naye mimi
ndiye nimekuwa ndugu
yake.Nilikutanishwa naye na
mtu mmoja ambaye sasa ni
marehemu anaitwa Mathew
Mulumbi na toka wakati huo
tumekuwa watu wa karibu
mno.Nashukuru kwa kunipa
taarifa.Nataka kufahamu tukio
hili limetokeaje?
“Kwa mujibu wa taarifa
nilizopewa ni kwamba Gosu
Gosu alikuwa anatoka ofisini
kwake jana jioni na wakati
akisubiri kuingia barabara kuu
wakatokea watu wakiwa katika
piki piki na mmoja aliyekaa
nyuma alikuwa na bunduki
akaanza kumimina risasi katika
gari la Gosu Gosu.Mimi nilipewa
taarifa hizo na katibu wangu
muhtasi ndipo nikaja moja kwa
moja hospitali kujua maendeleo
yake” akasema Melanie
“Nimejaribu kupiga simu
polisi kufuatilia kama kuna mtu
yeyote aliyepatikana lakini
mpaka sasa hawajampata mtu
yeyote uchunguzi unaendelea”
akasema Austin na ukimya
ukapita.
“Nimejiuliza sana sababu ya
Gosu Gosu kushambuliwa
nimekosa jibu.Ninawaza je ni
sababu za kibiashara au ni
kulipiza kisasi? Akauliza Austin
“Nadhani tutapata jibu pale
jeshi la polisi
watakapokamilisha uchunguzi
wao na kuwapata watu
waliofanya shambulio hili”
akasema Melanie
“Nakuahidi Melanie mtu
huyu lazima atapatikana.Iwe
mvua au jua lazima atapatikana.
Kwa sasa tuendelee
kumuombea Gosu Gosu aweze
kupona.Hali yake si nzuri na
kwa mujibu wa daktari
niliyezungumza naye amenipa
ukweli kwamba hali hii
aliyonayo sasa kupona ni
hamsini kwa hamsini hivyo
tujiandae kwa lolote
litakalotokea” akasema Austin
na Melanie akaangua kilio
“Gosu Gosu wangu jamani
!!!
Austin akamnyamazisha
“Tafadhali Melanie jizuie
kumwaga chozi.Kwa sasa
tunahitaji sana kuwa
majasiri.Gosu Gosu anatuhitaji
sana” akasema Austin na
Melanie akafuta machozi.Austin
akamshika bega na kusema
“Sikiliza
Melanie.Ninamfahamu Gosu
Gosu ni mpambanaji.He’ll fight
this.Believe me Gosu Gosu will
fight this !
“Austin najua unajaribu
kunipa moyo lakini hali haisi ya
Gosu Gosu
inaonekana.Uwezekano wa
kupona ni mdogo sana.Oh
jamani mimi !!
“Melanie eneo hili halihitaji
kelele ! Austin akawa mkali
“Jitahidi kujizuia kumwaga
machozi eneo hili.Ndugu za
Gosu Gosu ni sisi wawili pekee
hivyo basi ninahitaji
kushirikiana na mtu mwenye
ujasiri.Kama hautakuwa na
ujasiri tafadhali kaa nyumbani
usifike hapa ! akasema Austin
“Samahani nimekuelewa
Austin”
“Good.Sasa nenda
nyumbani kapumzike mimi
nitaendelea kukaa hapa na
kama kuna chochote kitatokea
nitakujulisha”akasema Austin
na kumshika mkono Melanie
akamsindikiza hadi katika gari
lake ambamo alikuwemo Joyce
dereva wake
“Melanie kuwa jasiri,Gosu
Gosu atapambana na
atapona.Ninamfahamu vyema
ni mpambanaji” akasema Austin
na kuagana na Melanie
akaondoka
“Dah ! Gosu Gosu amemtoa
wapi Yule mtoto?Halafu mbona
hajanieleza chochote kama
tayari ana mchumba?Siku hizi
ameanza kuniweka mbali katika
masuala yake ndiyo maana hata
suala hili hakutaka
kunishirikisha.Hata hivyo
anastahili kupongezwa kwa
kumpata mwanamke mzuri
kama yule” akawaza Austin na
kurejea ndani.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 7: EPISODE 4
Saa kumi na mbili za alfajiri
Rais wa Tanzania Dr Fabian
Kelelo alitaarifiwa kwamba Dr
Evans rais mstaafu tayari
alikuwa amewasili ikulu.Dr
Fabian akatoka kwenda
kukutana naye akamkaribisha
katika chumba cha
mazungumzo ya faragha.
“Ahsante sana kwa
kukubali kuonana nami asubuhi
hii Dr Fabian kwani bila kuwahi
asubuhi hii sidhani kama
tutaweza kuonana hapo baadae
na kuzungumza” akasema Dr
Evans
“Mzee nakushukuru sana
kwa kufika.Toka tukio lile
lilipotokea nimekusahau
kabisa.Uliponipigia simu alfajiri
ya leo ndipo
nikakukumbuka.Ahsante sana
kwa kuja kuniona mzee wangu
nakuhitaji sana kwa wakati
kama huu” akasema Dr Fabian
“Pole sana Dr Fabian.Hata
mimi nilijua kijana wangu
lazima atanihitaji sana kwa
wakati huu” akasema Dr Evans
ukimya mfupi ukapita
“Mzee ulisema una jambo la
msingi unataka kunieleza”
akasema Dr Fabian
“Ni kweli kuna jambo
ambalo ninataka kukueleza
linalohusiana na hiki
kilichotokea”
“Nakusikiliza
mzee”akasema Dr Fabian
“Nimetafakari sana kuhusu
tukio lile na kuna jambo moja
limenijia akilini.Ninadhani tukio
lile ni la kulipiza kisasi”
“Kulipiza kisasi
gani?akauliza Dr Fabian
akionyesha mshangao kidogo
“Miezi michache iliyopita
ukishirikiana na Patrice Eyenga
mlituma timu ya watu ikawaua
Lucy Muganza na mume wake
na baada ya hapo kukatokea
tena matuko tukio ya mauaji
akauawa balozi wa umoja wa
ulaya halafu ghafla kukawa
shwari.Nimetafakari sana
sababu za James Kasai kufanya
shambulio lile tena ndani ya
ardhi ya Tanzania lakini sababu
alizotoa haziniingii akilini.Kama
angekuwa na nia ya kulipiza
kisasi kwa Rais Patrice Eyenga
angekwisha fanya hivyo muda
mrefu lakini kwa nini asubiri
hadi sasa? James Kasai hana
ugomvi wowote na Tanzania
lakini ukichunguza kwa undani
sana tukio lile lilivyopangwa
utagundua kwamba liliwalenga
sana mkeo Millen na Rebeca
Eyenga ambao ni wake za
marais waliopanga mauaji ya
Lucy Muganza”akasema Dr
Evans na Dr Fabian akaonekana
kuzama katika mawazo
akakunja sura na kusema
“Dr Evans kuna picha
Fulani nimeanza kuipata
kufuatia maelezo
yako.Nakumbuka wiki iliyopita
Millen alinieleza kwamba
alifuatwa ofisini kwake na
balozi wa jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo
Germinus Mapupu akamueleza
kuwa anataka kuwaleta pamoja
wake za marais wa Rwanda na
Congo hivyo ataandaa chakula
maalum cha usiku na akamtaka
Millen amsaidie kumleta mezani
Agatha Ntezimana mke wa Rais
wa Rwanda.Tulifurahi kwa
jitihada hizo za balozi kutumia
mkutano ule kutafuta suluhu ya
mgogoro unaofukuta baina ya
nchi zao mbili na Millen
alikubali kusaidia
kuwapatanisha wake za marais
hao.Kama mauaji yale yalikuwa
ni ya kulipiza kisasi basi lazima
balozi Germinus Mapupu
alitumiwa katika kuandaa
mpango ule wa kuwaleta
mezani Rebeca na Agatha.Swali
linakuja nani waliokuwa nyuma
ya mpango huo? Ninaamini
kama balozi Germinus
angefahamu kuwa mpango ule
utasababisha mauaji
asingethubutu kushiriki”
“Exactly !! akasema Dr
Evans
“Nadhani umeanza
kunielewa
ninachokimaanisha.Balozi
Germinus Mapupu aliandaa
hafla ile kwa kujua kwamba ni
jambo jema ambalo litasaidia
kuleta amani katika nchi zao na
hakujua kama mpango ule
ulikuwa na lengo
lingine.Umeuliza swali zuri nani
yuko nyuma ya mpango ule?
Kama unakumbuka Lucy
Muganza alikuwa anatumiwa na
umoja wa Ulaya na hasa hasa
nchi ya Ufaransa na kazi zake
kubwa alizotakiwa kufanya ni
kwanza kuvuruga jumuiya ya
Afrika Mashariki na pili kuleta
machafuko nchini
Congo.Ukilitazama kwa kina
jambo hili utagundua kwamba
kinachotokea sasa kina mlengo
kama ule wa kuisambaratisha
jumuiya ya Afrika
Mashariki.Vita inanukia kati ya
Rwanda na Uganda.Rwanda
wameshambulia maeneo ya
Uganda na kuua watu na
Uganda wameandaa vikosi vyao
kwa ajili ya vita.Rwanda nao
wamekwisha weka tayari vikosi
vyao kukabiliana na yeyote
atakayethuibutu kuvamia ardhi
yao.Jamhuri ya kidemokrasa ya
Congo imeweka vikosi vyake
katika utayari na imepeleka
vikosi vingine katika mpaka
wake na Uganda.Tayari Uganda
imewataka mabalozi wake
walioko katika nchi za Rwanda
na Congo warejee nyumbani
mara moja na imewatimua
mabalozi wa nchi hizo walioko
Uganda.Ukiacha hayo wewe na
nchi za Rwanda na Congo
mnaandaa kikosi cha pamoja
ambacho kitafanya operesheni
ya kumsaka James Kasai.Kikosi
hicho kitavamia misitu ya
Kaskazini mwa Uganda
inakodaiwa James Kasai
amejificha na Uganda haiko
tayari kwa kikosi hicho kuvamia
ardhi yake itafanya
mashambulizi na huo utakuwa
ni mwanzo wa vita.Rwanda na
Congo zitavamia Uganda na
hapo hakutakuwa tena na
jumuiya ya Afrika
Mashariki.Fabian mmeingia
katika mtego na
mmenasa.Mlifanya maamuzi
bila kutulia na kutafakari.Sasa
basi tujiulize nani ambao
wanataka jumuiya ya Afrika
Mashariki ivunjike?Nani
wanataka machafuko yarejee
nchini jamhuri ya kidemokrasia
ya Congo?Jibu ni umoja wa
Ulaya na si nchi zote za umoja
wa Ulaya bali Ufaransa ambayo
imejificha chini ya kivuli cha
umoja wa ulaya.Unanielewa
lakini Dr Fabian?
“Mzee ninakuelewa vizuri
sana”
“Ahsante kwa kunielewa
lakini hayo ni mawazo yangu tu
sijamanisha kwamba ndiyo
ukweli wenyewe”
“Mzee umenifumbua macho
yangu na nimepata mwangaza
mkubwa kwa haya
uliyonieleza.Sikuwa
nimeyafikiria kabisa.Sasa
unanishauri nifanye nini mzee
wangu?
“Ninakushauri ufanye
uchunguzi wa siri sana kujua
nani walio nyuma ya mpango
ule wa marehemu balozi
Mapupu kuandaa chakula na
kuwaita wake za
marais.Hakuwa peke yake
lazima wapo watu
waliomshawish kuandaa
mpango ule wakidai ni mpango
wa amani.Pili sitisha mipango
yote ya kutaka kuivamia
Uganda kijeshi kwa kigezo cha
kumtafuta James Kasai”
“Mzee mtu huyu ni muuaji
na ameweka wazi kwamba
mashambulio yataendelea na
kibaya zaidi huyu mtu tayari
anashirikiana na kundi la
kigaidi la IS.Hatuwezi
kumuacha akendelea kufanya
atakavyo na kuua watu….” Dr
Fabian akasema kwa ukali
“Dr Fabian nisikilize na
unielewe.Huu ni mtego
mmetegewa na tayari
mmenasa.Mkithubutu kutumia
nguvu za kijeshi mtaitumbukiza
jumuiya ya Afrika mashariki
katika machafuko makubwa na
pale machafuko hayo
yatakapomalizika hakutakuwa
tena na jumuiya ya Afrika
mashariki.Kila nchi itajikuta
peke yake na hicho ndicho
maadui zenu
wanachokihitaji.Uchumi wa
nchi za Afrika Mashariki
utayumba sana.Dr Fabian
nakusihi sana usikubali kutumia
njia za kijeshi katika jambo hili”
akasema Dr Evans
“James Kasai ni mtu hatari
ana jeshi lake tutawezaje
kumpata bila ya kutumia nguvu
za kijeshi?akauliza Dr Fabian
“Inatakiwa ifanyike
operesheni ya kimya
kimya.Tengeneza kikosi cha siri
ambacho kitafanya kazi hiyo ya
kumsaka James Kasai kwa siri
kubwa na hatimaye watamtia
nguvuni.Tunacho kikosi cha
jeshi kinachojihusisha na
operesheni maalum
kinachoongozwa na Austin
January,kitumie kikosi hicho
wana uwezo mkubwa wa
kumpata James Kasai” akasema
Dr Evans
“James Kasai yuko kati kati
ya kundi la waasi na wana
silaha kali.Kikosi chetu ni
kidogo ukilinganisha na kundi
kubwa la waasi tena
wanaomiliki silaha nzito
nzito.Tutakwenda kuwapoteza
vijana wetu” akasema Dr Fabian
“Kikosi kile maalum kabisa
kilianza wakati wa uongozi
wangu unadhani kwa nini
nilikianzisha kikosi kama kile?
Ni kwa ajili ya operesheni kama
hizi.Kikosi kile kina watu mahiri
sana ambao wamepitia mafunzo
ya hali ya juu mno.Wanao
uwezo mkubwa wa kupigana
kwenye hali zote iwe
majini,ardhini,msituni jangwani
n.k.Ni kikosi chenye watu
wachache kutokana na gharama
kubwa ya mafunzo kwa
mwanajeshi
mmoja.NakuhAkikishia Dr
Fabian ukitumia kikosi hiki
utafanikiwa kumpata James
Kasai”akasema Dr Evans na Dr
Fabian akashusha pumzi.
“Mzee umenipa ushauri
mzuri sana lakini nina wasi
wasi kwamba ushauri huu
umechelewa kwani tayari
mipango imekwisha andaliwa
na baadae leo vikosi kutoka
Rwanda na jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo
vitawasili kwa ajili ya kuungana
na kile cha Tanzania kwa
mazoezi ya wiki moja kisha
wataelekea Uganda kumtafuta
James Kasai”
“Dr Fabian ninajua una
hasira za kuondokewa na
mkeo.Si wewe peke yako bali
hata wenzako wa Rwanda na
Congo nao pia wana hasira
ndiyo maana nyote kwa pamoja
mmekubaliana kirahisi sana
kutuma kikosi cha jeshi
kuvamia Uganda kumsaka
James Kasai bila kupima athari
za kile mnachotaka
kukifanya.Unapokalia kiti cha
urais hupaswi
kukurupuka.Unapaswa kuwa na
subira.Kila jambo linapotokea
jitahidi kwanza kufanya tafakari
ya kina kabla ya kutoa
maamuzi.Naweza kusema
kwamba mmekurupuka sana
katika maamuzi yenu ya kuunda
kikosi cha pamoja mkasahau
hata kuwashirikisha
wanachama wengine wa
jumuiya ya Afrika mashariki.Ni
vipi kama wanachama hao
wengine hawatakubaliana na
hatua mnazozichukua? Dr
Fabian ninaiona jumuiya ya
Afrika Mashariki
iliyogawanyika vipande vipande
na mbaya zaidi jumuiya
inakwenda kusambaratika
ikiwa katika mikono
yako.Utaandikwa katika vitabu
vya historia kwamba ulichangia
kwa jumuiya ya Afrika
Mashariki kuvunjika na
utasomwa kwa vizazi hadi
vizazi.Tafadhali usiruhusu
jambo hili litokee katika
utawala wako.Fanya maamuzi
magumu ambayo yatainusuru
jumuiya” akasema Dr Evans na
Dr Fabian akainamisha kichwa
akiwaza
“Dr Fabian kilichonileta
kwako asubuhi hii ni
kuwasilisha mawazo yangu na
ushauri lakini ninakuachia
wewe mwenyewe kila kitu
utapima na kuona kama yanafaa
na utaangalia namna ya
kuyafanyia kazi.Ahsante sana
kwa kunisikiliza mheshimiwa
Rais na kwa mara nyingine tena
pole sana” akasema Dr Evans
huku akisimama
“Mzee nakushukuru sana
kwa kuja kuniona na kunipa
mawazo mazuri.Naomba nipe
muda nitafakari nini cha
kufanya lakini nakuahidi
mawazo haya mazuri lazima
nitayafanyia kazi”
“Ahsante sana Dr
Fabian.Sasa ninaweza
kuondoka” akasema Dr Evans
na Rais akamsindikiza hadi
katika gari lake akaondoka.
“Aliyoyasema Dr Evans
yanaweza kuwa na
ukweli.Ukilitazama kwa kina
tukio lile kuna uwezekano
mkubwa sana likawa na
malengo ya kulipiza kisasi na
kwa upande mwingine ukawa
ni mwendelezo wa kile
alichotakiwa kukifanya Lucy
Muganza yaani kusambaratisha
jumuiya ya Afrika
mashariki.Ushauri wa Dr Evans
kuhusu kutotumia nguvu za
kijeshi kumsaka James Kasai ni
mzuri na ukilitazama jambo hili
kwa kina ni kweli jumuiya ya
Afrika Mashariki inaelekea
kusambaratika.Jana Rwanda
imeshambulia Uganda na hivi
sasa kila nchi inaandaa vikosi
vyake vya jeshi tayari kwa
vita.Ni kweli yataibuka
machafuko makubwa sana
katika eneo hili la afrika
mashariki kama juhudi za
haraka zisipochukuliwa.Suala
hili lipo katika mikono yangu
kwa sasa na ndiye
nitakayeamua juu ya uhai wa hii
jumuiya.Je nisimamishe
operesheni ya kijeshi ambayo
tumepanga kuifanya kumtafuta
James Kasai?akajiuliza Dr
Fabian
“Endapo tutasimamisha
operesheni ya kijeshi
tunayoiandaa kwa ajili ya
kumsaka James Kasai Rais wa
Uganda atajaa kiburi na atajiona
mkubwa kuliko nchi zote za
Afrika Mashariki.Anaweza
akavamia nchi yoyote kwa
kujua kwamba hakuna nchi
inayoweza kuitisha
Uganda.Lazima achapwe kidogo
kupewa fundisho ingawa
ushauri wa Dr Evans nao ni
mzuri lakini dah ! sijui nifanye
nini.I think I need to talk to
Austin” akawaza na kuchukua
simu akazitafuta namba za
Austin
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 7: EPISODE 5
Austin akiwa nje ya chumba
alimolazwa Gosu Gosu mara
simu yake ikaita akaitoa
mfukoni kutazama mpigaji
alikuwa ni Dr Fabian Kelelo
Rais wa jamhuri ya muungano
wa Tanzania.Akastuka kwani ni
muda umepita hawakuwa
wamewasiliana
“Mheshimiwa Rais”
akasema Austin
“Austin habari yako”
“Nzuri kabisa mheshimiwa
Rais”
“Austin samahani kwa
usumbufu asubuhi hii”
“Bila samahani
mheshimiwa Rais.Kwanza pole
sana mzee kwa msiba mzito
uliokupata”
“Ahante sana.Austin
nakuhitaji mara moja hapa
ikulu” akasema Dr Evans
“Mheshimiwa Rais
utanisamehe sintaweza kufika
hapo kwa wakati niko hapa
hospitali ya Mtodora toka jana
usiku mmoja wa rafiki yangu
ambaye nimeshirikiana naye
katika misheni mbali mbali
amepigwa risasi jana jioni”
“Ooh Pole sana.Ni nani
huyo?
“Ni Gosu Gosu mheshimiwa
Rais” akasema Austin
“Ulikuwa naye katika ile
misheni ya Lucy?
“Ndiyo mheshimiwa Rais”
“Vipi hali yake?
“Hali yake si nzuri
mheshimiwa Rais.Kwa mujibu
wa madaktari chochote
kinaweza kutokea”
“Dah ! hili ni pigo kubwa
sana.Nitazungumza na daktari
mkuu wa hapo hospitali ili
kuweka uzito mkubwa katika
kumuhudumia.Kuna kingine
chochote ambacho unadhani
ninaweza kusaidia?
“Hapana mheshimiwa Rais
pale nitakapokuwa na chochote
ninachohitaji nitakujulisha”
akasema Austin
“Sawa Austin basi endelea
kukaa hapo hapo hospitali
kumuhudumia mgonjwa na
chochote kitakachojiri
utanijulisha.Austin tafadhali
kuweni makini sana.Chukueni
kila aina ya tahadhari kuanzia
sasa”
“Sawa mheshimiwa rais”
akajibu Austin na Dr Evans
akakata simu.
“Huyo jamaa aliyepigwa
risasi alishiriki katika mauaji ya
Lucy Muganza.Yawezekana Dr
Evans yuko sahihi kwamba
haya ni matukio ya kulipiza
kisasi” akawaza Dr Evans na
kumpigia simu Edwin Mbeko
mkuu wa idara ya siri ya
usalama wa ndani wa nchi
akamtaka afike ikulu mara moja
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 7: EPISODE 6
Edwin Mbeko aliwasili
ikulu kwa haraka kama
alivyotakiwa na
Rais,akapokewa na kupelekwa
katika chumba cha
mazungumzo ya faragha.
“Edwin habari za asubuhi”
“Nzuri mzee shikamoo”
“Marahaba.Edwin nina
ratiba ndefu sana siku ya leo na
nisingeweza kupata nafasi ya
kuzungumza nawe baadae
ndiyo maana nimekuita hapa
asubuhi hii ili nikupe
maelekezo” akasema Dr Evans
“Niko tayari mkuu kupokea
maelekezo” akasema Edwin
“Tutazungumza kwa kirefu
tutakapopata muda kuhusiana
na kilichotokea lakini kwa sasa
kuna jambo nataka wewe na
idara yako
mlichunguze.Marehemu balozi
Germinus Mapupu aliandaa
hafla ya chakula cha jioni
nyumbani kwake kwa ajili ya
wake za marais wa Rwanda na
Congo,nataka kufahamu
alishirikiana na nani kuandaa
hafla ile? Nina uhakika hakuwa
peke yake hivyo tukimfahamu
ambaye alisaidiana naye
kuandaa tutakuwa na sehemu
nzuri ya kuanzia uchunguzi
wetu.Nataka idara yako
ijielekeze katika suala
hilo.Masuala mengine
yatashughulikiwa na idara za
polisi na vyombo
vingine.Tumeni kila uwezo mlio
nao kuhAkikisha mnajua mtu au
watu ambao walishirikiana na
balozi Mapupu” akasema Dr
Fabian
“Sawa mheshimiwa Rais
tutalifanyia kazi suala hilo”
“Nitazungumza nawe tena
jioni ya leo nataka hadi muda
huo tayari kuwe kuna chochote
mmekipata” akasema Dr
Fabian na kuagana na Edwin.
Baada ya kutoka ikulu
Edwin Mbeko alikwenda moja
kwa moja ofisini
kwake.Alifunga ofisi yake kwa
funguo ili mtu mwingine
asiweze kuingia ndani kisha
akampigia simu Devotha
“Edwin Mbeko” akasema
Devotha baada ya kupokea simu
“Devotha habari za muda
huu”
“Nzuri kabisa.Kuna taarifa
gani asubuhi hii?akauliza
Devotha
“Nimetoka ikulu muda
mfupi uliopita kuzungumza na
Rais wa Jamhuri ya muungano
wa Tanzania”
“Amekuambia nini?
“Ametoa maelekezo kwa
idara yangu tuchunguze tujue
balozi Mapupu alishirikiana na
nani katika kuandaa hafla ile ya
chakula cha jioni”
“Tayari ameanza kuwa na
wasiwasi kwamba kuna mtu au
watu walio nyuma ya balozi
Mapupu.Edwin hAkikisha
Melanie hajulikani kama ni yeye
aliyefadhili hafla ile” akasema
Devotha
“Tumekwisha lifanya hilo
madam na tayari tumekwisha
futa mawasiliano yote ya balozi
Mapupu na Melanie hivyo usiwe
na wasi wasi wowote
tunamlinda Melanie kwa kila
uwezo tulio nao” akasema
Edwin
“Good.Kuna jambo lingine
hAkikisha Melanie hafahamu
kama vijana wako ndio
waliompiga risasi Gosu
Gosu.Akijua mambo yanaweza
kuwa mabaya” akasema
Devotha
“Hawezi kujua chochote
lakini kuna kitu Fulani
kimetokea ambacho kinanipa
wasiwasi kidogo.Nmejulishwa
asubuhi na timu wanaomfuatili
Melanie kwamba mawasiliano
yamekatika na hawawezi
kumpata Melanie.Inaonekana
amegundua kuhusu zile saa
zake tulizozibadilisha ambazo
tumeziwekea vifaa maalum
kama ulivyoelekeza pamoja na
zile simu zake na hajavitumia
kabisa leo”akasema Edwin
Mbeko
“Ni mimi ndiye niliyefanya
kosa nilimwambia kwamba
ninafuatilia kila
anachokifanya.Sikutakiwa
kumueleza jambo hilo.Nadhani
ametafuta ni namna gani
tumeweza kufuatilia
mazungumzo yake na Gosu
Gosu na akagundua
tumemuwekea vifaa katika saa
zake na kuna mchezo
umefanyika katika simu yake
ndiyo maana leo hajavitumia
kabisa vifaa hivyo.Kitu cha
msingi ni kuwalinda wale
wadada wawili nyumbani
kwake akigundua kwamba
tuliwatumia kufanya mchezo
huo atawafanyia kitu
kibaya.Melanie amebadilika
sana anahitaji ” akasema
Devotha
“Nimekuelewa
madam.Nitafanya kama
ulivyoelekeza” akasema Edwin
Mbeko na kumuaga Devotha
RIYADH – SAUDI ARABIA
Saa moja za asubuhi simu
ya Najma ikaita akainuka na
kuichukua.
“Mama anapiga” akasema
na kuipokea wakasalimiana
halafu Habiba akasema
“Nawataka kwangu asubuhi
hii kwa ajili ya kifungua
kinywa” akasema Habiba na
Najma akabaki ameduwaa
“Najma umenisikia?
Akauliza Habiba
“Nimekusikia
mama.Nitamjulisha Abu”
akasema Najma na Habiba
akakata simu
“Kuna nini?akauliza
Mathew baada ya kuona uso wa
Najma ukiwa na mabadiliko
“Mama anataka twende
nyumbani kwake kupata
kifungua kinywa” akasema
Najma
“Ni kama vile alijua kuwa
ninahitaji kuzungumza naye”
akasema Mathew Najma
akaamka na kwenda maliwato
“Huyu Habiba Jawad ni
mwanamke wa aina gani?
Amefahamu vipi kama
ninahitaji kuonana naye siku ya
leo?Anazidi kunishangaza na
kuna nyakati najikuta
nikiingiwa na hofu.Yawezekana
anatumia nguvu za giza si
bure.Ni jana tulikuwa
tunajadiliana namna ya kuweza
kuzungumza naye halafu
asubuhi ya leo anatukaribisha
kwake.Hii ni ajabu kwa kweli”
akawaza Mathew akainuka na
kukaa kitandani
“Mpenzi unamuwaza
Habiba Jawad?akauliza Najma
baada ya kumkuta Mathew
akiwa amekaa kitandani
akiwaza
“Nimeshangaa kidogo
kwani ni jana tulikuwa
tunajadiliana namna ya
kuzungumza naye na leo
asubuhi anatualika nyumbani
kwake”
“Usimuwaze Habiba ndivyo
alivyo.Tumekwisha mzoea.Ana
uwezo mkubwa wa kuhisi mtu
unawaza kitu gani.Tulale kidogo
kabla ya kuelekea kwa Habiba”
akasema Najma huku
akimkumbatia Mathew
“Ninatamani hata sasa
nimfuate Habiba nyumbani
kwake.Sijapata usingizi usiku
wa leo nikiwaza kuhusu
shambulo la Tanzania.IS
wamefanya mauaji ya kikatili
sana wakisaidiana na James
Kasai.Kinachoniumiza zaidi
nilishuhudia utiaji saini wa
mabilioni ya fedha ambayo
alipewa James Kasai kuimarisha
kikosi chake cha waasi.IS
wanataka kujiimarisha katika
eneo la Afrika Mashariki na
kati,wanataka kujenga kambi
kubwa ya mafunzo ya kigaidi
nchini Congo na magaidi hao
watasambazwa sehemu
mbalimbali duniani kuua watu
wasio na hatia.I won’t let that
happen..!
“Abu mpenzi ! akaita Najma
kwa sauti laini na kumstua
Mathew toka mawazoni
“Uko mbali sana
kimawazo.Nini kinakusumbua?
“Najaribu kujipanga namna
nitakavyozungumza na Habiba”
akasema Mathew na Najma
akacheka
“Liweke kando jambo hilo
nakuhitaji” akasema Najma na
Mathew akaelewa alichotakiwa
kukifanya akampa Najma haki
yake ya asubuhi.
Baada ya kipute cha
asubuhi wakaingia bafuni kuoga
kisha wakajiandaa wa ajili ya
kwenda kupata kifungua
kinywa nyumbani kwa Habiba
Jawad.Walipokuwa tayari
wakatoka na kutembea
kuelekea katika jumba la
Habiba.Himaya ya Habiba
ilikuwa na majumba nane
makubwa ya ghorofa na jumba
lake lilikuwa katikati ya
majumba yote.Zilikuwepo pia
nyumba nyingine ndogo ndogo
kumi na tano.Katika Himaya hii
Habiba aliishi na watumishi
wake,wasaidizi wake wa
karibu,walinzi na sasa
waliongezeka Mathew na
Najma.Mwanae Abu Dahir
alikuwa na makazi yake sehemu
nyingine ambako huko nako
Habiba alikuwa na nyumba
yake ambayo hufikia kama
akiamua kwenda kumtembelea
mwanae.
Kutoka katika nyumba yao
hadi nyumbani kwa Habiba
hakukuwa na umbali na
kulitengenezwa njia nzuri sana
za kutembea kwa miguu kutoka
jengo moja hadi jingine.Walifika
katika nyumba ya Habiba
wakakaribishwa ndani na
mmoja wa watumishi wa ndani
wa Habiba.Ilikua ni mara ya
kwanza kwa Mathew kuingia
ndani ya jumba la Habiba
Jawad.
“Uzuri wake ni kama lile
jumba la Jaber kule Jordan
lakini tofauti ni kwamba Habiba
hajaweka viti vya dhahabu
kama Yule jamaa kule Jordan”
akawaza Mathew wakiwa
sebuleni wakimsubiri
Habiba.Baada ya dakika chache
Habiba akatokea Mathew na
Najma wakasimama na
kumsalimu kwa adabu.
“Karibuni sana
wanangu.Abu Zalawi ni mara
yako ya kwanza kuingia
hapa.Umelizoea lile jengo
lingine ambalo tumekuwa
tukikutana mara kwa mara kwa
chakula na maongezi lakini hili
ndilo jengo langu binafsi hata
akina Najma ni nadra sana
kuingia humu” akasema Habiba
“Nashukuru sana mama
kwa kutukaribisha” akasema
Mathew kisha Habiba
akawachukua hadi katika
chumba maalum kwa ajili yam
lo wa asubuhi pekee.Kulikuwa
na meza yenye viti sita ambayo
ilishehenezwa vyakula vya aina
mbalimbali.Habiba
akawakaribisha mezani
wakapata kifungua
kinywa.Baada ya kumaliza
Habiba akasema
“Najma ninamuhitaji Abu
Zalawi nina mazungumzo
naye.Tutakapomaliza
mazungumzo yetu atakuja
nyumbani” akasema Habiba na
Najma akaondoka akamuacha
Mathew pale nyumbani kwa
Habiba
“Abu Zalawi kwa mara
nyingine tena karibu sana hapa
nyumbani kwangu.Wewe ni
mmoja wa watu wachache sana
ambao wamewahi
kukaribishwa ndani ya nyumba
hii” akasema Habiba na
kumtaka Mathew amfuate.
Ni jumba lililokuwa na
vyumba na kona nyingi na
hatimaye wakafika katika
mlango sehemu ambako
walikutana na ukuta wa rangi
nyeupe.Taa nyeundu ikawaka
na sauti ikasikika ikimtaka
Habiba atamke jina lake.
“Voice recognized”
ikasikika sauti baada ya Habiba
kutamka jina lake na mara
vikasikika vyuma vikilia na
sehemu ya ukuta ikajifungua
“Abu Zalawi karibu sana
katika makazi yangu” akasema
Habib akimuongoza Mathew
kuingia katika sebule nzuri sana
yenye uzuri wa ajabu
“Kumbe Habiba anayo
sebule nyingine nzuri kushinda
ile niliyoiona kule chini”
akawaza Mathew alipoingia
katika sebule ile nzuri na kubwa
Habiba akaboyeza kidude
Fulani ukutani na mlango
ukajifunga.
“Karibu sana Mathew
Mulumbi.Hapa tuko huru
kuzungumza kitu chochote bila
kuhofia mtu yeyote” akasema
Habiba
“Sikujua kama una sebule
nyingine nzuri namna hii
mama.Ahsante kwa
kunikaribisha”akasema Mathew
“Nimekuleta hapa ili
tuzungumze kwa uhuru.Leo
nataka tuzungumze kwa
Kiswahili kwani hakuna
anayetusikia” akanyamaza
kidogo halafu akasema
“Mathew kwa siku nzima ya
jana haukuwa katika hali yako
ya kawaida.Hii ilisababishwa na
tukio lililotokea Tanzania
ambalo IS wametajwa
kuhusika.Nikiutazama uso
wako una maswali zaidi ya elfu
moja ya kuniuliza lakini kuna
kitu ambacho nataka
ukifahamu” Habiba akanyamaza
akamtazma Mathew na
kuendelea
“Nilikutuma uongozane na
Najma kwenda Dubai kwa
makusudi kabisa na nilitaka
ushuhudie James Kasai
akifadhiliwa fedha.Sikutaka
ufanye chochote bali uwe
shuhuda tu.Uliporejea uliniuliza
swali kwa nini nilitaka
ushuhudie jambo lile? Akasema
Habiba na kukaa kimya tena
“Mathew nimewahi
kukutamkia zaidi ya mara moja
kwamba ninakupenda na
nimekuchagua kutoka katika
kundi la mamilioni ya
watu.Usinielewe vibaya
ninakupenda kama mwanangu
na ndiyo maana nimediriki
kukupa mali zote ambazo
alistahili Seif.Pembeni ya hilo
kuna jambo lingine
kubwa.Niliwahi kukudokeza na
leo ninarejea tena kwamba
ninataka uchukue nafasi yangu”
akanyamaza akatazama chini
“Nilipokueleza jambo hili
ulistuka sana ukajibu kwamba
huwezi kuwa mfadhili wa
magaidi.Leo tena narejea
kusema kwamba wewe ndiye
ambaye nimekuchagua ushike
nafasi yangu.Kwa nini
ninakuandaa wewe? Ni kwa
sababu unaweza ukafanya kile
ninachotaka ukifanye.Kuna siri
ambazo nitakueleaza ambazo
hakuna anayezifahamu hata
watoto na wasaidizi wangu wa
karibu” akasema Habiba
“Siri ya kwanza ambayo
nataka uifahamu ni kwamba I’m
dying”
“You are dying?akauliza
Mathew
“Yes I’m dying.Kwa sasa
naomba nisikueleze chochote
lakini fahamu kwamba
ninakufa.Hii ni siri yangu
kubwa ambayo sijamueleza mtu
yeyote wa karibu na hata
wanangu hawajui.Ninajua una
kifua cha kuficha siri hivyo
iweke kifani kwako siri
hii.Hapaswi mtu yeyote
kuifahamu.Umenielewa
Mathew?akauliza Habiba Jawad.
“Nimekuelewa mama
lakini…
“Hicho unachotaka kuuliza
siku nyingine nitakueleza.Najua
unataka nikufafanulie kauli
yangu kwamba ninakufa lakini
muda bado utafahamu hapo
baadae” akasema Habiba
“Mama umenistua sana”
“Usistuke Mathew.Lengo
lako la kunitafuta llikuwa ni
kuniua na pale nitakapokuwa
nimekufa basi misheni yako
itakuwa imetimia.Habiba jawad
atakuwa amekufa na ugaidi
utakuwa umekomeshwa
duniani” akasema Habiba na
kucheka
“Mama ni kweli malengo
yangu yalikuwa ni kukuua
lakini baada ya kufanikiwa
kuonana nawe ana kwa ana
mtazamo wangu ulibadilika
kabisa.Tazama niko hapa sasa
nimeoa mwanao na nimeingia
katika orodha ya watoto
wako…” akasema Mathew na
Habiba akatoa kicheko kidogo
“Mathew Mulumbi
ninakupenda sana” akasema na
kuendelea kucheka
“Ninakufahamu Mathew
Mulumbi zaidi ya vile
ujuavyo.Nafahamu pamoja na
yale yote ambayo nimekufanyia
lakini bado akili yako inawaza
siku moja utaniua na kuondoka
hapa na misheni yako itakuwa
imekamilika”
“Hapana si hivyo mama”
akasema Mathew
“Huwezi kunidangnya
Mathew ninajua.Ninakuomba
ondoa mawazo hayo.Kama
nilivyokwambia kwamba hapa
ndipo mahala unapotakiwa
kuwepo.Hapa ni nyumbani
kwako.Una misheni kubwa sana
zaidi ya ile ya kuniua hivyo
endelea kufuata maelekezo
yangu.Tuachane na hilo turejee
nchini Tanzania” akasema
Habiba
“James Kasai amefanya
shambulio kubwa ambalo
limepelekea vifo vya watu zaidi
ya hamsini kwa mujibu wa
taarifa niliyonayo.Huyu James
Kasai ni nani?Kwa nini
ametekeleza shambulio
lile?akauliza Habiba Jawad
“James Kasai anaongoza
kikundi cha waasi ambao kwa
muda mrefu wamekuwa
wakipambana na jeshi la
serikali ya jamhuri ya
kidemokrasiaya Congo.Kwa
muda wa miaka mingi
kumekuwa na vita isiyokwisha
nchini Congo na kwa kiasi
kikubwa vita hiyo imekuwa
ikisababshwa na nguvu kubwa
kutoka nje ya nchi hiyo.Zipo
nchi za Ulaya ambazo
zimekuwa zikifadhili makundi
mbali mbali ya waasi ili
kuanzisha mapigano na serikali
ya Congo kwa maslahi yao.Hii
ndiyo sababu utaona
kumekuwa na makundi mengi
ya waasi yakiibuka mara kwa
mara.Kwa miongo kadhaa
wananchi wa Congo wamekuwa
wakiishi katika machafuko hadi
pale Patrice Eyenga aliposhinda
urais na kuwaita mezani
viongozi wote wa makundi ya
waasi wakazungumza na
kukubaliana kumaliza tofauti
zao.Ni James Kasai pekee
ambaye hakuwa tayari kuweka
silaha chini hivyo akafurushwa
na majeshi ya serikali
akakimbilia nchini
Uganda.James Kasai hakuwa
amefadhiliwa na mataifa ya
Ulaya kama ilivyokuwa kwa
makundi mengine mengi ya
waaasi baliyeye alikuwa
akifadhiliwa na moja wapo ya
nchi jirani na jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo na
ndiyo maana aliweza kumiliki
silaha nzito nzito na kufanikiwa
kushika sehemu kubwa ya
Congo hasa miji ile yenye utajiri
mkubwa wa madini.Nchi
iliyomfadhili ilikuwa ikifaidika
kwa kiasi kikubwa cha madini
kilichoibwa kutoka katika
migodi mikubwa” akasema
Habiba na kumtazama Mathew
aliyekuwa kimya akimsikiliza
“Watu wengi wanadhani
kwamba vikundi vya waasi
nchini Congo vilikuwa
vikifadhiliwa na mataifa ya nje
pekee lakini hawajui kama zipo
nchi jirani ambazo zilikuwa
zikifadhili vikundi vya waasi
nchini Congo.Baada ya
kufurushwa kutoka
Congo,James Kasai alikimbilia
Uganda ambako amepewa
hifadhi na serikali ya Uganda
katika misiti ya Kaskazini mwa
Uganda.Nchi iliyokuwa
inamfadhili James Kasai haitoi
ufadhili tena hivyo kumfanya
awe katika hali mbaya kifedha
na hapo ndipo IS walipoingia.IS
wanataka kupanua mtandao
wao na kujiimarisha barani
Afrika.Wanatafuta sehemu ya
kujenga kambi kubwa ya
mafunzo ya kigaidi na wakaona
katika misitu mikubwa ya
Congo kunafaa sana kujenga
kambi yao hivyo basi wakaenda
kuzungumza na James Kasai
wakataka kuingia naye
makubaliano ya masharikiano
ili aweze kuwasaidia waweze
kujenga kambi kubwa ya
mafunzo nchini Congo.James
alikubali kushirikiana na IS kwa
sharti la kulipwa kiasi kikubwa
cha fedha na silaha.Huo ndio ule
mkataba ulioushuhudia Dubai”
akasema Habiba na kunyama
kidogo halafu akaendelea
“Kuingia madarakani kwa
Rais Patrice Eyenga kulikuwa
na athari kubwa hasa kwa
mataifa yale ambayo yalikuwa
yananufaika kupitia migogoro
ya Congo na hii ikasababisha
nchi hizo kutafuta njia za
kuwarejesha tena kuendelea
kuchuma rasilimali za Congo na
njia pekee ambayo ingeweza
kuwasaidia kurejea tena nchini
Congo ni kwa kuanzisha
machafuko.Ukatengenezwa
mpango wa kumuondoa Patrice
Eyenga madarakani kwa kupitia
uchaguzi mkuu
uliopita.Aliandaliwa mtu
anaitwa Lucy Muganza ili aweze
kuchuana na Patrice Eyenga
katika uchaguzi mkuu.Huyu
Lucy Eyenga alikuwa ni
mfanyabiashara bilionea
aliyependwa sana nchini
Congo.Kwa bahati mbaya Lucy
hakuweza kufika katika
uchaguzi mkuu kwani aliuawa
yeye na mumewe nchini
Tanzania” akanyamaza kidogo
na kusema
“Ninajaribu kukupa historia
hii kwa sababu najua
huifahamu kwani wakati haya
yote yakitokea wewe hukuwa
na habari”
“Ni kweli mama mambo
haya ni mara ya kwanza
ninayasikia kutoka kwako
sikuwa nikiyafahamu” akasema
Mathew
“Mataifa haya makubwa
yakiongozwa na nchi ya
Ufaransa wana mpango pia wa
kuisambaratisha jumuiya ya
Afrika Mashariki.Kwa nini
wanataka kuisambaratisha
jumuiya hii? Jibu ni kutokana na
uimara wake.Bila kuivunja
vipande vipande jumuiya hii
itawawia ugumu kuweza
kuanzisha machafuko nchini
Congo kwani kwa sasa tayari
Congo ni mwanachama wa
jumuiya hiyo na kwa taratibu
zilivyo za jumuiya hiyo endapo
kutatokea nchi au kikundi
chochote toka ndani au nje ya
jumuia ya Afrika Mashariki
kikatishia amani ya mojawapo
ya nchi mwanachama basi nchi
zote za jumuiya zitaungana
pamoja na kuunda jeshi moja
ambalo litakwenda kuisaidia
nchi hiyo.Jumuiya ikivunjika
Congo itabaki peke yake na hata
pale machafuko yatakapotokea
basi hakuna nchi
itakayoisaidia.Shambulio lile la
James Kasai lina malengo hayo
pia ya kuanzisha machafuko
yatakayopelekea jumuiya ya
Afrika Mashariki
kusambaratika.Kama
umefuatilia vyombo vya habari
ni kwamba vikosi vya anga vya
nchi ya Rwanda vilivamia katika
misitu ya Kaskazini mwa
Uganda ambako inaaminika
James Kasai amejificha na
kushambulia vijiji kadhaa na
kuua watu.Rais wa Uganda
ametangaza kwamba kitendo
kile cha Rwanda ni cha
kichokozi na ni tangazo la
vita.Vikosi vya Uganda
vimesogezwa katika mpaka
wake na Rwanda tayari
kuishambulia Rwanda.Nchi ya
Rwanda nayo imeapa kila risasi
moja itakayorushwa katika
upande wake zitarejea risasi
elfu moja.Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo nayo
imesogeza vikosi vyake katika
mpaka wake na Uganda.Nchi
tatu za Tanzania Rwanda na
Congo zimeunda kikosi kimoja
cha jeshi kwa ajili ya kwenda
kufanya operesheni ya kijeshi
nchini Uganda na serikali ya
Uganda imeapa kukifyekelea
mbali kikosi hicho.Tayari
Uganda imewarejesha
nyumbani mabalozi wake
kutoka nchi za Rwanda na
Congo.Kwa ujumla hali ya
Afrika Mashariki ni tete na
endapo hakutachukuliwa juhudi
za haraka jumuiya ya Afrika
mashariki itavunjika vipande
vipande na hicho ndicho
wakubwa hao
wanachokitafuta.Kuna mpango
mkubwa sana umeandaliwa wa
kuivuruga Afrika Mashariki na
tayari mambo
yameanza.Naamini mambo
yakiendelea kama yalivyo kwa
muda wa wiki moja
hakutakuwa tena na jumuiya ya
Afrika Mashariki” akanyamaza
Habiba na kumtazama Mathew
halafu akatabasamu
“Kama kawaida yako
nikikutazama ninaona maswali
zaidi ya elfu moja katika sura
yako lakini sitaki leo uniulize
swali lolote” akasema Habiba na
kunyamaza tena halafu
akamkazia macho Mathew na
kusema
“Mathew Mulumbi
ninakutuma uende Tanzania”
“Tanzania?Mathew akauliza
kwa mshangao
“Ndiyo nataka uende
Tanzania.Unakwenda kwa
misheni maalum” akasema
Habiba na Mathew akashusha
pumzi
“Najua umestuka lakini
nakuomba usistuke.Nataka
urudi nyumbani Tanzania kwa
ajili ya misheni maalum
nitakayokutuma mimi” akasema
Habiba
“Niko tayari mama.Misheni
gani unanituma
Tanzania?akauliza Mathew.
“Unakwenda kuikomboa
Afrika mashariki.Nataka
ukamuue James Kasai na vile
vile kuung’oa mzizi wa IS nchini
Tanzania na Afrika Mashariki na
kati.Si operesheni nyepesi lakini
ndiyo itakayoinusuru Afrika
Mashariki.James Kasai ana
nguvu kubwa hivi sasa na kama
asipodhibitiwa ataleta maafa
makubwa sana katika Afrika
mashariki hivyo unakwenda
kummaliza” akanyamaza na
kumtazama Mathew
“Naona kuna jambo
limekukaba koo unataka
kulisema”
“Mama Habiba mimi sina
tatizo kabisa na misheni hii
unayonituma na ninakuahidi
kuitekeleza kwa ukamilifu
mkubwa sana lakini swali langu
kwako umeonyesha kuguswa
na kile alichokifanya James
Kasai lakini ametekeleza tukio
lile kwa kutumia fedha
zako.Kwa nini ulikubali
kumfadhili mtu ambaye
ulifahamu fika ni muuaji na
anakwenda kuua watu wasio na
hatia? Kwa nini umemuacha
akatekeleza shambulio lile baya
hadi sasa Afrika Mashariki
inataka kusambaratika ndipo
unaamua auawe? Kwa nini ..oh
my God ! akasema Mathew na
kushika kichwa kwa mikono
yake
“You still have so much to
learn my son” akasema Habiba
“Umekuwa unaniambia
maneno hayo kila wakati
kwamba bado kuna mengi
natakiwa kujifunza.Wapi
nikajifunze hayo unayosema
natakiwa kujifunza?akauliza
Mathew
“You don’t
understand……”akasema
Habiba na Mathew akamkatisha
“Make me understand then!
akasema kwa ukali na
kusimama.Habiba akamtazama
kwa macho makali kisha
akasema
“Sit down !
Mathew akaketi
“Nilikuonya na leo tena
ninarudia kukuonYa likiwa ni
onyo la mwisho kwamba
unapozungumza nami chunga
sana ulimi wako.Usirudie tena
kusimama na kuninyooshea
kidole.Umenisikia Mathew?!
Akauliza Habiba kwa ukali
“Samahani mama”
“Ninafahamu unauchukia
ugaidi na karibu nusu ya maisha
yako umekuwa ukipambana na
magaidi lakini vita ya ugaidi si
rahisi kama unavyodhani ndiyo
maana ninakuambia kwamba
kaa jifunze.Unadhani hakuna
mwingine ambaye ninaweza
kumuweka katika nafasi
yako?Wako wengi
sana.Mamilioni ya majasusi
lakini nimeamua kukuchagua
wewe miongoni mwao hivyo
tafadhali fuata kile
ninachokuelekeza ! akasema
Habiba kwa ukali
“Sawa mama
nimekuelewa.Samahani sana”
akasema Mathew
“Unakwenda Tanzania kwa
kazi moja tu ya kumuua James
Kasai vile vile kuung’oa mzizi
wa IS afrika Mashariki.Hii si
misheni nyepesi lakini nitakupa
kila aina ya msaada
kuhAkikisha unafanikiwa.Ukiwa
Dar es salaam nitakupa
maelekezo yote ya mahala alipo
James Kasai na vile vile
kuhusiana na mtandao wa
IS.Utaanza kwanza na James
Kasai halafu utamalizia na
IS.Sikupangii namna
utakavyoendesha operesheni
yako lakini usimweleze mtu
yeyote kuhusu mahala
ulipokuwa na kuhusu
mimi.Narudia usimueleze
chochote mtu yeyote kuhusu
yale uliyoyapitia toka kutekwa
na Mossad hadi kufika kwangu
kwani kama nilivyokueleza
jambo hili ni siri yangu nawe”
akanyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Utaondoka toka hapa hadi
Cairo Misri kwa kutumia hati ya
kusafiria ya Abu Al Zalawi raia
wa Saudia Arabia na kutoka
Misri utapanda ndege ya moja
kwa moja kuelekea
Tanzania.Kila kitu kwa ajili ya
safari hiyo kimekwisha
andaliwa na muda wako wa
kukaa katika eneo la Afrika
Mashariki ni siku
thelathini.Utakapomaliza
misheni yako utatoweka na
asifahamu mtu yeyote
umeelekea wapi.Utarejea hapa
kuja kuendelea na kile ambacho
nimekuleta hapa
ukifanye.Nitakupa maelekezo
namna ya kuweza kuondoka
Tanzania bila mtu yeyote kujua
umeelekea wapi” akasema
Habiba
“Mama kwa mara nyingine
tena ninakuomba samahani
kwa kukukwaza hata hivyo
kuna kitu nataka kuuliza kama
utaniruhusu”
“Uliza usihofu” akasema
Habiba
“Kwa nini umeguswa na
Afrika mashariki hadi ukanitaka
nikamuue mmoja wa washirika
wako?akauliza Mathew na
Habiba akatabasamu
“Ni kwa sababu sitaki eneo
unakotoka liingie katika
machafuko ndiyo maana nataka
ukahAkikishe unamaliza hatari
yoyote inayoweza kusababisha
mvurugano afrika
Mashariki.Nimefanya hivi
kutokana na mapenzi makubwa
uliyo nayo kwa nchi
yako.Umepitia magumu mengi
yote ni kwa ajili ya nchi yako
Tanzania na kwa kuwa
ninakupenda kama kijana
wangu sitaki kukuona ukiumia
kwa sababu ya kile
kinachotokea katika nchi yako
ndiyo maana nataka ukamalize
hatari hiyo inayoikabili nchi
yako na pale utakapohAkikisha
iko salama basi utarejea hapa
kuendelea na misheni
nyingine.Naamini sasa umeanza
kunielewa kwa nini
nilikwambia kwamba hapa
ndipo mahala unapotakiwa
uwepo” akasema Habiba
“Kweli mama nimeanza
kukuelewa kwa nini uliniambia
vile na ninashukuru sana kwa
kunipa fursa ya kwenda
kuipigania nchi yangu na
kuokoa jumuiya ya Afrika
mashariki isivunjike hata hivyo
bado ninajiuliza namna
nitakavyoweza kupambana na
James Kasai ambaye ana kikosi
kikubwa chenye zana nzito za
vita na mimi nikiwa peke yangu
au na watu wangu wachache
ambao nitawateua wanisaidie
katika operesheni yangu”
“Kuna siri ambayo wengi
hawaifahamu kuhusu James
Kasai.Huyu mtu haishi porini
kama watu
wanavyodhani.James Kasai
anaishi jijini Kampala tena
maisha ya kifahari
sana.Tanzania,Rwanda na
Congo zinaandaa kikosi kwa
ajili ya kwenda kuvamia misitu
kumsaka James lakini
hawatafanikiwa kumpata.James
haishi msituni anaishi
Kampala.Utakapofika Dar es
salaam ndipo nitakapokupa
maelekezo kuhusiana na
mahala alipo James.Hii ni siri
ninakupa ambayo hata wakuu
wa nchi za Afrika Mashariki
hawaijui” akasema Habiba
“Mama mambo haya yote
unayafahamu vipi?akauliza
Mathew
“Narejea tena ile kauli
yangu tulia ujifunze.Utafahamu
mambo mengi sana kama ukiwa
mvumilivu na utanishukuru
badala ya kunichukia” akasema
Habiba
“Kitu kingine,Najma
asifahamu chochote kama
unakwenda
Tanzania.Utamweleza
nimekutuma kazi nchini
Misri.Ukifika Tanzania lazima
utakutana na ndugu jamaa na
marafiki zako na mkeo Peniela
lazima atapata habari kwamba
uko hai lakini siku zote muweke
Najma mbele kwani
anakupenda sana na furaha
yake iko kwako.Nadhani
umenielewa Mathew”
“Nimekuelewa
mama.Ninakushukuru kwa
mara nyingine tena kwa fursa
hii uliyonipa ya kwenda
kuisaidia nchi yangu.Sasa
nimeanza kukuelewa
ulivyosema kwamba uko tofauti
na watu wanavyodhani.Ahsante
kwa kunipa nafasi ya
kukufahamu japo kidogo”
akasema Mathew na
mazungumzo yakaishia pale
Habiba akamtoa Mathew mle
ndani akamruhusu aondoke.
“Mtu niliyekula kiapo cha
kumuua pale nitakapomtia
machoni leo hii ndiye amegeuka
msaada kwa nchi
yangu.Imenishangaza sana
sikutegemea kama Habiba
Jawad angeweza kufanya kitu
kama hiki alichokifanya.Japo
kuna maswali mengi ambayo
ningependa kumuuliza lakini
ngoja nikafanye kama
alivyonitaka.Ninamshukuru
hata kwa hiki kidogo
alichonisaidia kwa nchi yangu”
akawaza Mathew akielekea
nyumbani kwake baada ya
kuondoka kwa Habiba Jawad
“Hatimaye ninarejea tena
nyumbani.Natamani ningekuwa
na mbawa nipae hata sasa hivi
kwa furaha niliyonayo ya
kwenda tena nyumbani lakini
siendi kustarehe.Ninakwenda
katika misheni ambayo si
misheni rahisi.Ninakwenda
kumuua James Kasai mmoja wa
watu hatari kabisa katika Afrika
Mashariki.Haitakuwa
operesheni nyepesi kama
alivyosema Habiba.James Kasai
ni mtu aliyejizatiti sana kiulinzi
na mbaya zaidi ni kwamba
anahifadhiwa na serikali ya
Uganda hivyo maficho yake si
mahala ambapo panaweza
kuingilika kirahisi hata hivyo
nitahAkikisha ninamtia
mikononi na kumuua.Habiba
amenishangaza pia aliposema
kwamba anataka nikaung’oe
mzizi wa IS nchini Tanzania na
Afrika mashariki.Hiki ni kikundi
ambacho amekuwa anakifadhili
fedha kwa nini leo hii anataka
nikaung’oe mzizi wake
Tanzania?akajiuliza Mathew
“Nisiumize kichwa changu
kwa mawazo ninachotakiwa ni
kuanza kujipanga namna
nitakavyotekeleza operesheni
hii muhimu sana.Nahitaji
kutafuta watu watakaonisaidia
katika operesheni hiyo.Kwa
namna yoyote ile namuhitaji
sana Gosu Gosu.Yule ni
mwanajeshi asiyeogopa
chochote.Sifahamu nitampata
wapi,nitajua nikifika
Tanzania.Ninamuhitaji vile vile
Ruby.Huyu naye sifahamu
nitampata wapi lakini
nitakapofika Tanzania nitajua”
akasimama baada ya picha
fulani kumjia akilini
“Austin January ! akawaza
na sura yake ikabadilika
“Ni mtu ambaye anaweza
kuwa muhimu sana anaweza
akanisaidia mno lakini sifahamu
kama naye alinusurika usiku ule
tuliposhambuliwa na kikosi cha
Mossad.Lilikuwa ni shambulio
baya sana.Haya yote nitayajua
nikifika Dar es salaam” akawaza
na kumkumbuka Peniela
“Peniela mke wangu na
watoto wangu.Sijui watakuwa
katika hali gani pale
watakaposikia kwamba niko
hai.Dah ! kweli mambo
yamevurugika sana lakini kila
kitu kitakwenda kujulikana
huko huko mbele ya safari”
akawaza Mathew
DAR ES SALAAM – TANZANIA
Saa tano za asubuhi mwili
wa Millen Kelelo mke wa Rais
wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania uliwasili katika
viwanja vya ikulu kwa ajili ya
kuagwa kabla ya kusafirishwa
kwenda nyumbani kwao
Tukuyu Mbeya kwa
mazishi.Watu walikuwa ni
wengi na ulinzi ulikuwa mkali
sana.Kila aliyepita alikaguliwa
na mitambo maalum
kuhAkikisha hakuna anayeingia
na silaha au kitu chochote cha
hatari.
Vilio vilisikika pale mwili
wa Millen ulipokuwa
unashushwa garini na
kupelekwa ndani ambako
wanafamilia walipewa nafasi ya
kwanza ya kuuaga mwili wa
mpendwa wao kabla ya
waombolezaji wengine.Ni
wazazi na Dr Fabian pekee
walioruhusiwa kuuona mwili
wa Millen kwa mara ya mwisho
kwani ulikuwa umeharibika
sana.Jeneza likafunguliwa na Dr
Fabian akalisogelea machozi
yakamporomoka
“Oooh Millen kwa nini
umekufa kifo kibaya namna
hii?Umewakosea nini hawa
watu hadi wakuue kikatili
namna hii?Endapo ningefahamu
kama unakwenda kufa kifo cha
namna hii nisingekuruhusu
uende.Nani atabaki mshauri
wangu?Maisha yangu
yatakuwaje bila wewe Millen?
Sijawahi lia machozi mengi
namna hii katika maisha yangu
ninakuahidi wale wote
waliofanya kitendo hiki
watalipa kwa gharama kubwa
sana.Ninaapa mmoja baada ya
mwingine lazima watalipa
ukatili huu waliokufanyia.Kwa
heri Millen tutakutana huko
kwa muumba wetu kwani wote
safari yetu ni moja” Dr Fabian
aliyaongea maneno haya
kimoyo moyo akimuaga mke
wake kipenzi Millen
Kelelo.Alipotoka wakafuata
wazazi kisha jeneza likafungwa
wengine walitoa heshima zao za
mwisho wakati jeneza
limefungwa.
Wakati wanafamilia
wakiendelea kuuaga mwili wa
Millen,Dr Fabian akajulishwa
kwamba Rais wa Kenya tayari
ametua uwanja wa ndege na
alikuwa njiani kuelekea ikulu
kushiriki katika zoezi lile la
kuuaga mwili wa Millen.Dr
Fabian akatoka nje akachukua
simu na kumpigia Patrice
Eyenga.
“Patrice nimetoka
kuutazama mwili wa Millen
sasa hivi.Kilichofanyika
kilikuwa ni unyama uliovuka
mipaka.Huyu mwanaharamu
James Kasai lazima apatikane
kwa namna yoyote ile.Sijali
kama tutaingia vitani na Uganda
au vipi lakini lazima apatikane
akiwa mzima au
amekufa.Kitendo alichokifanya
hakivumiliki” akasema Dr
Fabian
“Dr Fabian hivi
tunavyozungumza kikosi kwa
ajili ya operesheni ya kumsaka
James Kasai kiko uwanjani
wakijiandaa kuondoka kuja
Tanzania kuungana na wenzao”
“Safi sana Patrice.Tayari
maandalizi yamekamilika kwa
ajili ya kikosi hicho”
“Ahsante sana Dr Fabian
tutaendelea kuwasiliana”
akasema Patrice wakaagana na
kukata simu
“Nilikwisha anza kufikiria
kuachana na mpango wa
kutumia kikosi cha jeshi
kumsaka James Kasai lakini
baada ya kuona ukatili
aliomfanyia mke wangu
nimeamua kuendelea na
maandalizi ya kikosi cha jeshi
cha pamoja.Hawezi akafanya
ukatili wa namna hii halafu
akaachwa hai.Jenerali Akiki ni
rafiki yangu sana,Uganda ni
ndugu zetu lakini katika hili
ninaweka kila kitu pembeni na
nitapeleka kikosi kwenda
kumsaka James Kasai hata
kama Uganda hataki jambo
hilo.Tayari Jenerali Akiki
amekwisha dai kwamba
kupeleka kikosi maalum
kumtafuta James Kasai ni
kitendo cha uvamizi na
ameahidi kujibu lakini
akithubutu kuua hata
mwanajeshi mmoja ataiona
nguvu yangu.Nitamchapa
vibaya sana na hata kumuondoa
madarakani” Dr Evans
akatolewa mawazoni baada ya
kujulishwa kwamba tayari
wanafamilia na ndugu wa
karibu wamekwisha maliza
zoezi la kutoa heshima za
mwisho kwa mwili wa
marehemu.Akarejea ndani na
kushauriana jambo na wasaidizi
wake pamoja na mkuu wa
kamati ya maandalizi ya
shughuli ile.Wakati
wakijadiliana akajulishwa
kwamba rais wa Kenya David
Njoroge alikuwa
amewasili.Akatoka kwenda
kumpokea akamkaribisha ndani
wakawa na mazungumzo ya
faragha ya dakika chache
“Pole sana Dr Fabian kwa
kilichotokea” akasema Rais
David
“Ahsante sana
David.Ahsante sana kwa kuja
kunifariji”
“Nilikuwa na ziara ya
kwenda Afrika Kusini lakini
imenibidi kuahirisha ili kuja
kuungana nawe katika wakati
huu mgumu.Mke wangu yeye
nimemtuma aende Rwanda
akaniwakilishe na makamu
wangu wa Rais amekwenda
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo.Msiba huu ni mkubwa.Si
msiba wenu peke yenu ni msiba
wa wana afrika mashariki wote”
akasema David
“Kilichofanyika ni ukatili
uliovuka mipaka ya
ubinadamu.Ni kitendo ambacho
hakiwezi kuvumilika hata
kidogo ! akasema Dr Fabian
“Dr Fabian pamoja na kuwa
katika wakati mgumu sana
lakini kuna jambo ambalo
ninataka kuzungumza nawe”
“Jambo gani David?
“Ni kuhusu hatua
unazotaka kuchukua kuhusu
mtu ambaye anadaiwa kuhusika
katika shambulio hili James
Kasai.Nimejulishwa kwamba
mmekubaliana na marais wa
Rwanda na Congo kuunda
kikosi kimoja kitakachokwenda
Uganda kufanya operesheni ya
kumsaka na kumtia nguvuni
James Kasai”
“Ni kweli
David.Tumekubaliana kuunda
kikosi ambacho kitakwenda
Uganda kuhAkikisha James
Kasai anapatikana.Hivi
tunavyozungumza kikosi cha
kutoka Congo kiko uwanja wa
ndege kikijiandaa kuja Tanzania
kuungana na vikosi vya
Tanzania na Rwanda.Watafanya
mazoezi ya pamoja ya wiki moja
kisha wataelekea katika misitu
ya Kaskazini mwa Uganda
ambako ndiko aliko James Kasai
na wataendesha operesheni ya
kijeshi hadi watakapompata
James.Safari hii hatapona
lazima atiwe nguvuni” akasema
Dr Fabian
“Dr Fabian umekwisha
wasiliana na Rais wa Uganda
ukamjulisha kuhusu mpango
huo?akauliza David
“Nimezungumza naye lakini
hatukuelewana na Jenerali
Akiki akadiriki kunitolea
vitisho.Kwa nini anamkingia
kifua James Kasai?Kwa nini
hataki kutoa ushirikiano?Mimi
na wenzangu tumekwisha amua
kwamba Jenerali Akiki akubali
au akatae lazima tuingie Uganda
kumsaka James Kasai na kama
akithubutu kuua hata
mwanajeshi mmoja kutoka
katika kikosi hicho kama
alivyoahidi atakiona cha
moto,nitamchakaza ! akasema
Dr Fabian
“Dr Fabian nimekuja
kukushauri ndugu yangu
simamisha kwanza shughuli
zozote za kijeshi mnazotaka
kuzifanya nchini Uganda ili
tujaribu kutafuta suluhu kwa
njia ya mazungumzo.Kabla
sijapanda ndege kuja huku
nimepewa taarifa kwamba
vikosi vya Uganda na Rwanda
vilikuwa vinashambuliana
mpakani.Kwa ujumla hali si
shwari na kuna hatari kubwa
eneo zima la Afrika Mashariki
likaingia katika machafuko.Kila
nchi imeweka vikosi vyake
katika utayari wa vita na tayari
Uganda imekwisha waondoa
mabalozi wake katika nchi za
Rwanda na Congo hii inaashiria
tayari kuna uhasama mkubwa
sana baina ya nchi zetu.Kitendo
cha kutumia nguvu za kijeshi
kitakuwa ni kama kuongeza
mafuta kwenye
moto.Kitazidisha
mzozo.Nashauri hatua zozote za
kijeshi dhidi ya Uganda
zisimamishwe kwanza na
tuwashawishi Rwanda na
Congo warejeshe majeshi yao
nyuma ili yafanyike
mazungumzo na kupata suluhu
ya jambo hili”
“David ahsante sana kwa
kuguswa na jambo hili lakini
naomba nikuhAkikishie
kwamba mimi na wenzangu
tumekwisha azimia kwamba
kwa namna yoyote ile lazima
James Kasai apatikane na ili
kumpata lazima tutumie nguvu
za kijeshi.James tayari
amekuwa hatari kwa nchi zetu
na tukimuacha atakuwa na
madhara makubwa mno.Tayari
amekwisha fanya ukatili
mkubwa sana huko Congo hadi
kufikia hatua ya kufunguliwa
mashtaka katika mahakama ya
uhalifu wa kivita.Hatuwezi
kumuacha akaendelea lazima
tummalize na mwisho wake
umewadia.Hatutarudi nyuma
katika maamuzi haya na kama
Uganda hawatatuunga mkono
katika suala hili sisi tutaendelea
na operesheni hadi tuhAkikishe
James Kasai
amepatikana.Endapo Jenerali
Akiki ataamua kuanzisha vita
sisi tuko tayari na
tutamchakaza vibaya sana”
akasema Dr Fabian na
kunyanyuka
“Mheshimiwa Rais nadhani
tutaendelea na mazungumzo
badae leo tuna ratiba ndefu
sana.Baada ya kumaliza
shughuli za hapa tunatarajia
kuelekea jijini Mbeya kwa ajili
ya mazishi siku ya kesho”
“Ahsante sana Dr Fabian
kwa kunipa dakika hizi chache
tukazungumza.Nakuomba
ukipata nafasi yatafakari hayo
niliyokueleza.Ni wewe ambaye
unaweza ukainusuru jumuiya
yetu isiingie katika machafuko”
akasema David
“Ahsante kwa ushauri
David nitauzingatia” akasema
Dr Fabian kisha wakatoka
kwenda kuendelea na ratiba
nyingine.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 7: EPISODE 7
Melanie Davis hakutoka
katika chumba chake alikuwa
anafuatilia katika runinga
shughuli ya kuuaga mwili wa
marehemu Millen Kelelo mke
wa Rais wa jamhuri ya uungano
wa Tanzania.Pembeni ya
kitanda chake alikuwa na simu
yake ambayo aliitumia
kuwasiliana na Austin juu ya
maendeleo ya GosuGosu.Kwa
mujibu wa taarifa ya Austin
hadi mchana ule bado hali ya
Gosu Gosu haikuwa nzuri.
“Ninaogopa hadi kwenda
hospitali kumtazama Gosu Gosu
kwani ni mimi ambaye
nimesababisha haya yote
yakamtokea.Kama
nisingemtuma akamuue
Devotha haya yote
yasingemtokea.This isn’t over
Devotha.Mimi nawe
tutapambana.Ulifanikiwa mara
ya kwanza sintakupa nafasi ya
kufanikiwa mara ya
pili..”akatolewa mawazoni na
mlio wa simu akaichukua
kutazama mpigaji alikuwa ni
Devotha na sura yake
ikajikunja.
“Huyu shetani ninamuwaza
kumbe naye ananiwaza !
akawaza Melanie huku
akiitazama simu kwa hasira
halafu akaipokea
“Hallo”akasema
“Melanie samahani sana
kwa maneno niliyokutamkia
mara ya mwsho
tulipozungumza simuni.Kuna
maneno ambayo niliyatam…….”
“Devotha hayo yamekwisha
pita nieleze sababu ya kunipigia
simu” akasema Melanie na
kumkatisha Devotha
“Melanie kutokana na
matokeo mazuri ya kile
ulichokifanya ndiyo maana
nimetangulia kwa kukuomba
samahani kwa yale
niliyokutamkia.Pokea salamu
nyingi za pongezi kutoka kwa
Rais Michael
Weren.Anakupongeza kwa hiki
ulichokifanya ambacho ndicho
hasa tulichokuwa tunakitaka na
ndicho tulikutuma
ukakifanye.Japokuwa ulifanya
kwa kutumia njia unazozijua
wewe lakini matokeo yake
ndiyo yale ambayo tulikuwa
tukiyatafuta.Kutokana na
matokeo haya makubwa
kuanzia sasa mashirikiano yako
na James Kasai yamebarikiwa
na unaweza ukaendelea.Hakuna
atakayehoji kama James
anashirikiana na magaidi ama
vipi lakini tunachohitaji sisi ni
mipango yetu iende vyema kwa
hiyo uko huru Melanie
kushirikiana na yeyote ili mradi
uhAkikishe kwamba
mashirikiano hayo hayatakuwa
na athari kwetu” akanyamaza
kidogo halafu akaendelea
“Jambo la pili ni kwamba
baada ya kumaliza awamu ya
kwanza sasa unaingia katika
awamu ya pili ambayo ni
kumuondoa Rais Patrice Eyenga
wa Congo.Jumuiya ya Afrika
mashariki haina muda mrefu
itasambaratika hivyo
tunaelekeza macho yetu nchini
Congo.Lazima tumuondoe Rais
Patrice Eyenga.Hivyo basi fanya
mazungumzo na James Kasai
muone namna jambo hilo
linavyoweza
kutekelezeka.Kama kuna
chochote ambacho James Kasai
atahitaji sisi tuko tayari
kumpatia” akasema
Devotha,Melanie akashusha
pumzi ndefu na ukimya mfupi
ukapita kisha Devotha akauliza
“Umenielewa Melanie
nilichokwambia?
“Nimekuelewa Devotha
nitalifanyia kazi” akasema
Melanie
“Good.Naomba tuweke
tofauti zetu pembeni na
tumalize salama misheni
yetu”akasema Devotha
“Lakini hii haina maana
kwamba nimekusamehe kwa
kitendo ulichokifanya cha
kutaka kumuua Gosu Gosu !
akasema Melanie
“Kama nisingemuwahi
angeniua mimi.Ninamfahamu
Gosu Gosu vizuri.Kwa nini lakini
ukataka kuniua Melanie?Kitu
gani kibaya kimesababisha
unichukie kiasi
hiki?Tusichukiane tafadhali
hadi kufikia hatua ya kutaka
kuuana.Mimi nawe ni kitu
kimoja” akasema Devotha
“Lazima nikuue shetani
wewe ! akawaza Melanie
“Sawa Devotha naomba na
wewe usirudie tena kunikaripia
kama mtoto mdogo”
“Nimekuelewa Melanie na
samahani sana.Haitajirudia
tena.Tukiachana na hayo
nimezungumza na Edwin
Mbeko anasema amepewa
jukumu na Rais la kuchunguza
nani waliokuwa wakishirikiana
na balozi Germinus Mapupu
katika kuandaa hafla ile ya
chakula cha usiku kwa wake za
marais.Usihofu kila kitu iko safi
kwani hawataweza kugundua
chochote kuhusu wewe”
akasema Devotha na kuagana
na Melanie
“Wenyewe wameanza
kunikubali kwa jambo
nililolifanya.Devotha leo hii
amekuwa mdogo kama
nini.Ameona mwenyewe mimi
si mtu wa kufanyia
mchezo.Baada ya mafanikio
makubwa sasa wanataka niende
mbali zaia nimuue Patrice
Eyenga.Ninakubaliana nao kwa
kuwa Patrice Eyenga ni mmoja
watu waliomo katika orodha ya
wale ninaohitaji kuondoa roho
zao.Alishiriki katika mauaji ya
wazazi wangu hivyo hakuna
msamaha lazima
aondoke.Baada ya Patrice
Eyenga atafuata Rais wa
Tanzania Dr Fabian na Devotha
ajiandae.Pale
nitakapohAkikisha wale wote
waliohusika katika kuwaua
wazazi wangu wameondoka
duniani ndipo nitakapoanza
kuyapanga upya maisha
yangu.Kwa sasa akili yangu yote
naielekeza katika kulipiza
kisasi” akawaza Melanie
akainuka na kuchukua glasi
yenye mvinyo mkali
“Nitazungumza na James
Kasai na tutapanga namna
tutakavyoweza kumuondoa
Patrice Eyenga.Kama tumeweza
kumuondoa mke wake
hatutashindwa kumuondoa
Patrice Eyenga lakini huu ni
mpango mkubwa sana ambao
lazima upangwe kwa ustadi
mkubwa mno.Ngoja niwasiliane
naye sasa hivi bila kuchelewa
nione ataniambia nini” akawaza
Melanie na kuchukua simu
ambayo huutumia kuwsiliana
na James akampigia
“Habari yako Melanie”
akasema James Kasai baada ya
kupokea simu
“Nzuri James habari yako”
“Hamsini kwa hamsini
siwezi kusema nzuri au
mbaya.Unasemaje Melanie
kwani muda huu si wa
kuzungumza simuni na
nimepokea simu yako kwa
kuwa ni mtu muhimu sana
kwangu”
“James samahani kwa
usumbufu na ahsante kwa
kupokea simu yangu.James
nahitaji kuzunguza nawe pale
utakapokuwa na nafasi.Nina
jambo kubwa na la muhimu la
kujadiliana” akasema Melanie
“Jambo gani
Melanie?Unaweza ukanigusia
japo kwa ufupi nione uzito
wake kama tunaweza
kuzungumza sasa hivi au hadi
tupate nafasi ya kutosha.Kuwa
huru usiogope” akasema James
Kasai
“Baada ya awamu ya
kwanza kuwa na mafanikio
makubwa sasa nataka kuingia
katika awamu ya pili nayo ni
kumuua Patrice Eyenga”
akasema Melanie na James
Kasai akawa kimya kwa muda
“James ! akaita Melanie
“Melanie suala lako ni zuri
na zito sana hatuwezi
kulizungumza simuni.Tafadhali
njoo Uganda.Nitampa
maelekezo Eddie Okello
atawasiliana na Gosu Gosu”
“Gosu Gosu alipatwa na
matatizo alipigwa risasi yuko
katika hali mbaya sana”
akasema Melanie
“Gosu Gosu amepigwa
risasi?
“Ndiyo amepigwa risasi na
watu wasiofahamika”
“Pole sana.Namuombea
apone haraka sana.Basi Eddie
atawasiliana nawe moja kwa
moja na kukupa maelekezo”
akasema James na kuagana na
Melanie
“Gosu Gosu kupigwa risasi
kunawastua watu
wengi.Namshukuru Yule rafiki
yake Austin ambaye amenipa
moyo kwamba Gosu Gosu
atapona.Yule jamaa Austin
ndiye Yule ambaye Devotha
alinieleza nikae naye mbali?
Nakumbuka alinitajia majina
kadhaa na mojawapo ni hili la
Austin.Itanilazimu nifanye
uchunguzi nijue kama ni yeye
kweli ili niweze kumuepuka
haraka sana.Baadae jioni ya leo
nitakwenda hospitali.Hata
hivyo he’s very handsome”
akawaza na kutabasamu kidogo
akachukua glasi yenye kinywaji
akanywa
“Afrika Mashariki nywele
zimewasimama kwa tukio lile
dogo la kuuawa kwa wake za
marais sasa wasubiri mengine
makubwa ambapo wataondoka
Patrice Eyenga na swahiba
wake Dr Fabian.Kama kuna rais
mwingine ambaye alishiriki
kupanga mauaji ya wazazi
wangu naye pia ajiandae”
akanywa mvinyo
“Sikutegemea kama katika
maisha yangu nitakuwa mkatili
namna hii.Lakini wakati
mwingine walimwengu ndio
wanaosababisha watu wakawa
makatili”
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 7: EPISODE 8
Bado hali ya Gosu Gosu
iliendelea kuwa tete.Austin
January hakubanduka hospitali
akifuatilia kwa karibu sana hali
ya Gosu Gosu akihofia
yawezekana waliotaka kumuua
wangeweza kumfuata pale
hospitali.Akiwa ametulia nje
akitafakari mara akawaona
watu wawili wakijana
walipofika karibu akamtambua
mmoja wao alikuwa ni Melanie
Davis.Akasimama
“Melanie” akasema Austin
na kumpa mkono Melanie
“Austin” akasema Melanie
na Austin akawakaribisha
katika viti wakaketi
“Usingesumbuka kuja huku
usiku huu ungepiga tu simu
kuulizia maendeleo ya
mgonjwa” akasema Austin
“Austin hujui tu hali gani
ninapitia kwa sasa kwa tukio
hili la Gosu Gosu
kushambuliwa.Nashindwa kula
wala kunywa.Natamani nikae
hapa hospitali nikimtazama
mpenzi wangu muda wote.Gosu
Gosu ni kila kitu kwangu”
akasema Melanie na kuchukua
kitambaa akafuta machozi
“Nyamaza kulia
Melanie.Kama nilivyokueleza
awali kwamba Gosu Gosu ni
jasiri na atashinda vita hii ya
kupigania maisha yake”
akasema Austin
“Austin najua hayo ni
maneno ya kunipa moyo lakini
ukweli halisi ni kwamba Gosu
Gosu hatapona” akasema
Melanie na kuanza tena kulia na
kuangusha kichwa chake
mapajani mwa Austin ambaye
alimuinua na kumpiga piga
mgongoni
“Melanie usilie
tafadhali.Gosu Gosu anatuhitaji
sana sisi muda huu tuwe
majasiri.NinakuhAkikishia
kwamba Gosu Gosu
atapona.Naomba uniamini”
akasema Austin. Na Melanie
akafuta machozi
“Kuwa jasiri Melanie.Gosu
Gosu atapona
ninakuhAkikishia” akasema
Austin.Joyce aliyekuwa
amefuatana na Melanie
akainuka kama vile
anazungumza na simu akaenda
kusimama pembeni.
“Austin nakushukuru sana
kwa kuacha shughuli zako na
kuja kushinda hapa na mgonjwa
usiku na mchana” akasema
Melanie
“Kama nilivyokueleza Gosu
Gosu ni ndugu yangu hivyo niko
tayari kuacha kila kitu kwa ajili
yake” akasema Austin
“Unafanya kazi gani Austin?
“Mimi ni mfanya biashara”
“Biashara gani?
“Ninafanya biashara ya
kuuza magari”
“Ouh vizuri sana.Magari ya
aina gani unauza?Unaweza
kunielekeza lilipo duka lako nije
kutembelea?
“Mimi sina duka la magari
bali biashara yangu ni kuingiza
gari mbili au tatu natafuta
wateja ninawauzia kisha
naagiza nyingine au wakati
mwingine watu wanaohitaji
magari wamekuwa wakinitumia
sana mimi kuwaagizia magari
nje ya nchi” akasema Austin
“Kwa nini usifungue duka
lako mwenyewe la kuuza
magari kuliko kuagiza gari moja
moja?
“Mtaji wangu bado mdogo
ndiyo maana ninafanya hivyo
lakini pale mtaji wangu
utakapokuwa mkubwa nina
mpango wa kufungua duka”
akasema Austin na ukimya
ukapita
“Nitakapohitaji gari
nitakuja kukuona.Mimi ni
mpenzi sana wa magari ya
kifahari”
“Usijali pale utakapohitaji
njoo unione nitakusaidia kupata
gari la ndoto yako” akasema
Austin na Melanie akaomba
akamuone Gosu Gosu.Austin
akazungumza na muuguzi
Melanie akavishwa mavazi
maalum na kuingizwa ndani ya
chumba alimo Gosu Gosu
aliyekuwa akipumua kwa
msaada wa mashine
Melanie alitumia dakika
zaidi ya kumi ndani ya chumba
kile cha Gosu Gosu kisha
akatoka huku machozi
yakimtiririka
“Austin I need to go
home.Ninahisi kama kichwa
change kinataka kupasuka
baada ya kumuona Gosu Gosu
akiwa katika hali
ile.Tutaendelea
kuwasiliana.Kesho sintafika
hapa hospitali nitakuwa na
safari ya muhimu sana.Hata
hivyo nitajitahidi kuwasiliana
nawe kujua maendeleo”
akasema Melanie na Austin
akawasindikiza hadi katika gari
lao wakaondoka
“Umefanikiwa kuipata
picha ya Austin?Melanie
akamuuliza Joyce
“Ndiyo
madam.Nimefanikiwa kumpiga
picha kadhaa bila yeye
kutambua”
“Good” akasema Melanie na
kuchukua simu ya Joyce
akazitazama zile picha za Austin
ambazo Joyce alimpiga bila yeye
kujua.
“He’s such a handsome
guy.Ameanza kunivutia.Kama
Gosu Gosu hatapona basi
nitakuwa na huyu Austin.Ana
sura nzuri,umbo zuri
anapangilia maneno yake
wakati wa kuongea na
anajali.Hata hivyo natakiwa
kuthibitsha kama kweli ni yeye
yule ambaye Devotha alinionya
nikae naye mbali” akawaza na
kuzihamisha zile picha kutoka
katika simu ya Joyce kwenda
katika simu yake halafu
akamtumia Devotha akimuuliza
kama Yule ndiye Austin
aliyemuonya akae naye mbali
“Kaa mbali sana na huyu
mtu.Usimpe nafasi
akakufahamu wewe ni
nani.Huyu ndiye mmoja wa
wale niliokukanya usiwe karibu
nao” Devotha akamjibu Melanie
“Pamoja na onyo hili la
Devotha lakini tayari Austin
amekwisha nivutia
sana.Nitamsogeza karibu.If he’s
a killer like Gosu Gosu He’ll be
killing for me.Hakuna
mwanaume katika dunia hii
anayeweza kusema hapana kwa
Melanie” akawaza Melanie na
kutabasamu
Muda mdupi baada ya akina
Melanie kuondoka pale
hospitali,Rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania
akampigia simu Austin
“Habari yako Austin”
akauliza Dr Fabian
“Nzuri kabisa mheshimiwa
Rais”
“Vipi maendeleo ya
mwenzako?
“Hali yake bado si nzuri
hata kidogo”
“Tunaweza kumsafirisha
kumpeleka nje ya nchi?
“Nimewauliza madaktari
wamesema kwamba kwa hali
yake hii haitawezekana.Kwa
sasa anapumua kwa msaada wa
mashine”
“Sawa Austin utaendelea
kunijulisha kile kitakachokuwa
kinaendelea hapo
hospitali.Kesho tutamzika mke
wangu kisha nitarejea Dar es
salaam nitafik hapo hospitali
kumtazama mwenzako.Ulisema
anaitwa nani?
“Papi Gosu Gosu”
“Sawa nitafika hapo
kumtazama Gosu Gosu.Bado
naendelea kusisitiza umakini
sana kwani hatujui
waliomshambulia Gosu Gosu
walikuwa na malengo gani”
akasema Dr Fabian
“Ninachukua tahadhari
kubwa mheshimiwa Rais ndiyo
maana sijabanduka hapa
hospitali nikihofia pengine
waliofanya kitendo hiki wakijua
bado yuko hai wanaweza
wakamfuata hapa hospitali”
“Austin nakutakia usiku
mwema.Tutaonana kesho”
“Ahsante sana mheshimiwa
Rais” akasema Austin na Rais
akakata simu
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 7: EPISODE 9
Afrika Mashariki iliamshwa
na taarifa za vikosi vya Uganda
na Rwanda kushambuliana
usiku kucha katika mpaka wa
nchi zao.Wakati hayo yakijiri
katika mpaka wa Uganda na
Rwanda,nchini Tanzania kikosi
maalum cha jeshi
kilichojumuisha wanajeshi
kutoka nchi za Tanzania
Rwanda na Congo kilikwisha
kutana na kuanza mazoezi ya
pamoja kabla ya kuelekea
nchini Uganda kumsaka James
Kasai.
Pamoja na hali hiyo tete
iliyozikumba baadhi ya nchi za
Afrika Mashariki bado biashara
kati ya Tanzania na Uganda
ziliendelea kama kawaida.Safari
za ndege ziliendelea vile vile
safari za treni na mafuta
yaliendelea kusafirishwa kama
kawaida kutoka Uganda
kwenda Tanzania.
Katika uwanja wa ndege wa
Julius Nyerere,Melanie Davis
alikuwa mmoja wa abiria
waliokuwa ndani ya ndege ya
shirika la ndege la Tanzania
ikielekea jijini Kampala
Uganda.Taratibu ndege ikaanza
kuondoka kisha ikashika kasi na
kupaa kuelekea Kampala.
Iliwachukua muda wa saa
tatu na dakika thelathini
kuwasili katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Entebbe
nchini Uganda.Hali ilikuwa
shwari kabisa na hakukuwa na
kitisho chochote kwa abiria
japokuwa ulinzi ulikuwa mkali
mno uwanjani pale .
Melanie na abiria wengine
wakashuka ndegeni na kwenda
kukamilisha taratibu za
uhamiaji kisha wakaruhusiwa
kuingia Uganda.Eddie Okello
alikuwepo uwanjani kumpokea
Melanie
“Melanie karibu tena kwa
mara nyingine Uganda”
akasema Eddie baada ya
kumpokea Melanie
“Ahsante Eddie nashukuru”
akasema Melanie na Eddie
akamuongoza katika gari lake la
kifahari wakaondoka pale
uwanjani
“Nataka kujua maendeleo
ya Gosu Gosu”akasema Eddie
“Hali yake si nzuri kama
nilivyokueleza simuni.Mpaka
sasa anapumua 0kwa msaada
wa mashine.Madaktari
wanasema kwa hali aliyofikia ni
hamsini kwa hamsini na loloet
linaweza kutokea hivyo tuzidi
kumuombea”
“Nimemfahamu Gosu Gosu
kwa miaka mingi toka tukiwa
wadogo msituni.Ni mpiganaji
asiyekata tamaa na nina
uhakika atapambana kwa ajili
ya maisha yake na wale
anaowapenda” akasema Eddie
“Yawezekana kweli Gosu
Gosu akapona kwani huyu ni
mtu wa pili sasa anatamka
hivyo.Namuombea apone bado
ninamuhitaji”akawaza Melanie
“Nani lakini
waliomshambulia Gosu
Gosu?Tayari
wamepatikana?akauliza Eddie
“Mpaka sasa haijulikani
bado nani waliomshambulia na
hajakamatwa mtu yeyote
kuhusiana na tukio lile”
“Ilikuwa ni bahati watu hao
walimuwahi kwani kama
wangempa upenyo kidogo
wasingefanikiwa.Ninamfahamu
Gosu Gosu ana uwezo mkubwa
wa kucheza na silaha na
alikuwa akishika silaha sote
tulikuwa tunaingiwa hofu
kwani hubadilika na kuwa mtu
mwingine kabisa”akasema
Eddie
“Kwa bahati mbaya siku
alipopigwa risasi hakuwa na
silaha yoyote
garini.Alichokumbuka ni fulana
ya kuzuia risasi ambayo huwa
haachi kuivaa kila mara.Hiyo
ndo iliyomsaidia kwani alipigwa
risasi nyingi tumboni .Bila
fulana ile hivi sasa tyari
tungekwisha
mzika.Waliomshambulia
walikusudia kumuua kabisa”
Akasema Melanie
“Tuzidi kumuombea apone
haraka” akasema Eddie
“Kampala kunaonekana
shwari kabisa kama vile hakuna
kitisho chochote cha usalama”
Akauliza Melanie
“Kampala kuko
shwari.Shughuli zinaendelea
kama kawaida na hakuna
kitisho chochote cha
usalama.Mapigano
yanaripotiwa kuendelea huko
mpakani lakini huku hakuna
chochote” akajibu Eddie na
kupunguza mwendo kidogo
halafu akaendelea
“Hawa mataifa wanaotaka
kuungana kumtafuta James
wanajisumbua bure
hawataweza kumpata James
hata wafanye nini badala yake
wanawapeleka wanajeshi wao
kwenda kuuawa” akasema
Eddie.Melanie alikuwa kimya
kabisa akimsikiliza.Eddie
alipoona Melanie haongei
chochote akaweka mziki na
safari ikaendelea bila
mazungumzo yoyote hadi
walipofika katika barabara
moja nzuri iliyopandwa maua
mazuri pembezoni.Baada ya
muda wakafika katika geti
lililokuwa linalindwa na askari
wenye silaha.Eddie akashusha
kioo na kusalimiana na kiongozi
wa askari wale ambaye
aliamuru geti lifunguliwe na
gari la Eddie likaingia
ndani.Eddie akamfungulia
mlango Melanie akashuka na
kushangaa kwa madhari nzuri
aliyoiona.Kulikuwa na jumba
kubwa zuri sana Eddie
akamkaribisha ndani
akamtambulisha kwa
wahudumu wanne wa jumba
lile ambao walikuwa wamevaa
sare maalum.Mwanamama
mmoja ambaye alionekana
ndiye msimamizi mkuu wa
jumba lile akawaongoza
Melanie na Eddie kuelekea
katika chumba cha mapumziko
“Melanie karibu sana.Hapa
ni sehemu salama kabisa usiwe
na hofu” akasema Eddie
“Hapa ni wapi?Mbona
kunalindwa na polisi?akauliza
Melanie
“Hii ni nyumba ya
wageni”akajibu Eddie na
kunywa kinywaji kidogo
walichoandaliwa
“Nyumba gani ya wageni
inalindwa na askari wenye
silaha?akauliza Melanie
akionekana kuwa na hofu
kidogo
“Hii ni nyumba ambayo
wageni maalum wa Rais wa
Uganda hufikia ndiyo maana
unaona inalindwa na askari
wenye silaha”
“Wageni wa Rais?Melanie
akashangaa
“Ndiyo hii ni nyumba ya
kufikia wageni maalum wa rais”
“Mimi si mgeni wa
Rais.Mimi nimekuja kuonana na
James Kasai na sina mahusiano
yoyote na Rais.Au amenileta
hapa kwa sababu za kiusalama?
Akauliza Melanie
“Sifahamu chochote
Melanie lakini yeye malekezo
niliyopewa ni kukuchukua na
kukuleta hapa na mimi
ninatekeleza maelekezo hayo”
“Yuko wapi James?akauliza
Melanie
“Siwezi kujibu swali hilo”
akasema Eddie na kusimama
“Melanie nimekufikisha
mahala nilipoelekezwa mimi
ninaondoka ninakwenda
kuendelea na shughuli zangu
tutaonana tena” akasema Eddie
“Sasa nitaonana vipi na
James?Melanie akauliza
“Usihofu Melanie.James
utaonana naye.Kuwa na amani”
akajibu Eddie na kuondoka
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 7: EPISODE 10
Saa moja za jioni zilifika
gari mbili na kumchukua
Melanie na kuondoka
naye.Hakujua alikuwa
anapelekwa wapi lakini moyoni
alikuwa akiamini yuko
salama.Gari zile mbili baada ya
mizunguko kadhaa ya jiji la
Kampala ambalo Melanie
hakuwa akiifahamu vyema
hatimaye wakawasili katika
jumba moja lililokuwa likiwaka
taa nyingi.Hakukuwa na mlinzi
yoyote nje na mara tu
walipokaribia geti likafunguka
wakaingia ndani.Wale jamaa
waliokuwa wamevaa suti
nyeusi wakashuka mmoja wao
akamfungulia Melanie mlango
wa gari akashuka.Kutoka ndani
ya ile nyumba akatoka jamaa
mmoja ambaye alikuwa
amevalia suti nzuri ya rangi ya
kijivu akampokea Melanie
“Karibu sana Melanie
akasema Yule jamaa na
kumshika Melanie mkono
akamsaidia kupanda ngazi
kuelekea ndani ya jumba lile
zuri.Walipanda ngazi kuelekea
ghorofani hadi katika mlango
mmoja uliokuwa na walinzi
wawili wenye silaha
wakafunguliwa mlango
wakapita na kulifuata korido
ambalo lilikuwa na walinzi
kadhaa wenye
bunduki.Wakaukuta tena
mlango mwingine ukafunguliwa
wakaingia na kujikuta ndani ya
chumba kikubwa kizuri.James
Kasai alikuwa ametulia sofani
akivuta sigara huku mbele yake
kukiwa na chupa kadhaa za
pombe kali.
“Melanie Davis” akasema
James alipomuona Melanie
akasimama wakakumbatana
kisha akamuelekeza sehemu ya
kukaa
“Karibu sana
Melanie.Nimefurahi kukuona
tena japo umekuja wakati
ambao nimekuwa na heka heka
nyingi” akasema James
“Ahsante James na
samahani kwa kuja kwa wakati
kama huu”
“Usijali Melanie wewe ni
mtu muhimu sana kwangu
hivyo nimeahirisha kila kitu
kwa sababu yako.Kama
unavyojua baada ya tukio lile la
juzi kule Dar es salaam baadhi
ya nchi zimeapa kunisaka hadi
wanikamate.Wengine
wamediriki kufanya
mashambulio katika vijiji
vinavyozunguka misitu
mikubwa wakiamini nimejificha
humo.Nchi ya Uganda kwa sasa
imeingia katika mgogoro
mkubwa na majirani zake na
tayari wamekwisha anza
kushambuliana kwa hali hiyo
basi nimeamua kuondoa vikosi
vyangu kutoka Uganda na
tunaelekea jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo kwenda
kuanza rasmi mapambano na
serikali ya Congo.Kwa heshima
yako nimewaacha vijana wangu
wakiendelea na zoezi hilo la
kuhama na mimi nimekuja hapa
kukutana nawe.Karibu na jisikie
nyumbani”
“James utanisamehe sana
kwa kukuingiza katika matatizo
haya makubwa”akasema
Melanie
“Hapana
Melanie.Hujaniingiza katika
matatizo yoyote bali haya ndiyo
maisha yamgu na tumekwisha
yazoea.Nilihitaji sana kufanya
tukio kama lile ili kutuma
salamu kwa Patrice Eyenga
kwamba nipo na
ninakuja.Karibu Melanie
tufurahie kinywaji” akasema
James na kumiminia Melanie
kinywaji katika glasi.
“Mipango inakwenda
vyema kama ulivyokuwa
unataka.Kama hali ikiendelea
hivi ilivyo sasa basi jumuya ya
Afrika Mashariki itabaki
historia.Hivi sasa kuna
mvurugano mkubwa sana kila
nchi ndani ya jumuiya
haielewani na nyingine”
akasema James Kasai ambaye
kama kawaida yake alikuwa
amevaa fulana ya kukatwa
mikono huku mabega yake
yaliyojaa michoro mingi yakiwa
wazi.Shingoni alivaa mikufu ya
thamani kubwa.Vidole vyake
vote vya mikono vilichafuliwa
na pete za thamani kubwa sana
“Nashukuru kwa mipango
inakwenda vyema.Baada ya
mpango wetu ule wa kwanza
kufanikiwa nimekuja tena
kwako kuomba msaada wako”
akasema Melanie
“Karibu” akasema James
“Kama nilivyokueleza
simuni jana kwamba mpango
wangu unaofuata ni kumuua
Rais Patrice Eyenga.Huyu na
mwenzake wa Tanzania ndio
waliopanga mauaji ya wazazi
wangu. Sifahamu nitawezaje
kulitekeleza hilo ndiyo maana
nimekuja hapa kwako kuomba
msaada” akasema
Melanie.James akaitupa sigara
aliyokuwa anaivuta katika
chombo kilichokuwa mezani
halafu akachukua sigara
nyingine kubwa akaiwasha
akavuta.Ulipita ukimya wa
dakika tatu kisha akasema
“Melanie
Davis.Ulichokitamka ni kitu
kikubwa sana ambacho
sikuwahi kufikiria kama
unaweza ukakitamka.Kinazidi
uwezo wako” akasema na
kuvuta sigara ile kubwa
“Pamoja na ukubwa wake
lakini nimelipokea wazo lako
kwa mikono miwili kwa sababu
ni kitu ambacho ninakihitaji
sana japo kwa bahati mbaya
hata mimi mwenyewe sifahamu
nitaweza kumuua vipi
Patrice.Lakini kwa kuwa tayari
wazo liko mezani lazima
tutafute namna ya kuweza
kumuondoa Rais Patrice
Eyenga.Kuna mtu mmoja tu
ambaye anaweza akatusaidia
ambaye tunakwenda kuonana
naye usiku wa leo.Naomba
unisubiri hapa nikajiandae
kwani mtu tunayekwenda
kuonana naye ni mtu mzito”
akasema James Kasai na
kunyanyuka akaondoka.Baada
ya dakika kumi akatoka akiwa
amevaa suti nzuri rangi nyeusi
iliyomkaa vyema
“Wow ! kumbe huyu jamaa
akivaa suti anapendeza sana.Ni
mara ya kwanza ninamuona
akiwa amevaa suti nimezoea
kumuona akiwa katika mavazi
yake ya kijeshi” akawaza
Melanie
“Melanie sasa tunaweza
kuondoka”akasema James
akamshika mkono Melanie
wakashuka ngazi hadi nje
ambako kulikuwa
kumeandaliwa magari yapatayo
manne yote aina ya marcedece
benz rangi nyeusi
wakafunguliwa milango na
kuingia katika mojawapo ya
gari kisha msafara ule wa
magari ukaondoka.
“Melanie tunakwenda
kuonana na mtu mzito sana
hivyo tutamueleza ukweli wote
bila kumficha hata kitu kimoja
kuhusu wewe” akasema James
“Sawa James” akasema
Melanie
“Vipi maendeleo ya Gosu
Gosu?akauliza James
“Bado hali yake si
nzuri.Tumuombee kwani lolote
linaweza kutokea” akasema
Melanie na safari
ikaendelea.Taratibu walianza
kuliacha jiji la Kampala na
kufuata barabara iliyokuwa
imepandwa miti pembeni.Baada
ya mwendo wa dakika ishirini
wakazikuta taa kandoni mwa
barabara na kwa mbali kidogo
ulionekana mji Fulani
mdogo.Mara mwendo wa
magari ukapungua walikuwa
katika kizuizi,kulikuwa na
wanajeshi wenye silaha zaidi ya
kumi.Magari yote yakakaguliwa
halafu yakaruhusiwa
kupita.Baada ya dakika tano
wakakuta tena kizuizi kingine
na mtu aliyekuwa katika gari la
mbele kabisa akashuka
akazungumza na wale maafisa
wa jeshi na hapo magari
yakakaguliwa tena kisha
yakaruhusiwa kuendelea na
safari.Walikwenda kwa
mwendo wa dakika kumi
wakakutana na kizuizi kingine
wakakaguliwa tena na kisha
wanajeshi sita wakaingia katika
gari na kuyaongoza magari yale
wakafuata barabara ya upande
wa kushoto.Walikuwa ndani ya
kambi ya jeshi.Ulinzi ulikuwa
mkali sana ndani ya kambi
ile.Melanie aliingiwa na hofu
Baada ya mwendo wa
dakika kadhaa wakipita katika
barabara iliyokuwa kandoni
mwa kambi ile wakakuta geti
lililokuwa na ulinzi mkali
sana.Geti likafunguliwa magari
yale yakaingia ndani.James
Kasai hakuwa na hata chembe
ya wasi wasi.Walielekea katika
jumba moja kubwa la rangi
nyeupe.Magari yakasimama na
milango ya gari walimopanda
James na Melanie ikafunguliwa
James akamtaka Melanie
washuke walikuwa wamefika
safari yao.Mtu mmoja aliyevalia
nguo za kijeshi aliyechafuka
vyeo mabegani akampokea
James na kumsalimu Melanie
halafu akawaongoza kuingia
ndani ya jumba lile
zuri.Waliingia katika sebule
nzuri na kumkuta mtu mmoja
aliyevaa mavazi ya kijeshi
akiwa anazungumza na simu
akiwa amegeukia dirishani Yule
mwanajeshi aliyewapokea
akawaelekeza sehemu za
kukaa.Melanie alihisi miguu
yake inamuisha nguvu baada ya
Yule mtu aliyekuwa
akizungumza na simu kugeuka
na kuwatazama.Alikuwa ni Rais
wa Uganda Jenerali Akiki
Rwamirama.
“Rais wa Uganda !!
akashangaa
“Karibuni sana.James Kasai
karibu”akasema Jenerali Akiki
akasalimiana na James huku
Melanie akiwa amesimama.Rais
Akiki akamgeukia Melanie
“Anaitwa Melanie
Davis”James akamtambulisha
Melanie kwa Rais
“Melanie karibu
sana.Nimefurahi kukutana
nawe” akasema Jenerali Akiki
“Melanie huyu ni Rais wa
Uganda.Anaitwa Jenerali Akiki
Busingye Rwamirama” akasema
James Kasai
“Karibuni sana.Nadhani
kabla ya yote tukapate kwanza
chakula kilichokwisha
andaliwa.Uliponiambia unakuja
na mgeni muhimu kwa
mazungumzo niliandaa kabisa
chakula kwa ajili yake” akasema
Jenerali Akiki kisha
akaongozana na akina James
kuelekea katika chumba cha
chakula akawakaribisha mezani
wakapata chakula
“Mama yuko wapi?akauliza
James Kasai ambaye alionekana
kuzungumza na Jenerali Akiki
kama mtu wake wa karibu sana
“Mama amesafiri
amekwenda nje ya nchi
kupumzika na familia hadi hapo
upepo mbaya unaovuma sasa
hivi utakapotulia.Unajua
yanapotokea mambo kama haya
yanayoendelea hivi sasa familia
huwa ya kwanza kulengwa
ndiyo maana nimewaondoa
kuwapeleka nje kupumzika hadi
pale mambo yatakapokuwa
shwari basi watarejea.Vipi zoezi
linakwendaje?
“Zoezi linakwenda vyema
na hivi tuzungumzavyo tayari
kila kitu kimekwisha hamishwa
na usiku wa leo vijana wanafika
Congo na kuanza kujenga
kambi”
“Good” akasema Jenerali
Akiki wakaendelea kupata
chakula.Walipomaliza kula
chakula Jenerali Akiki
akawachukua hadi katika
sehemu ya mazungumzo
“Sasa tunaweza kuendelea
na mazungumzo yetu.Melanie
Karibu sana.Umekuwa kimya
muda mrefu yawezekana ni
mazingira yanakuogopesha
lakini nakusihi usiogope.Hapa
ni sehemu salama kabisa na
ndiyo maana unaona niko
hapa.Nyumba hii ni maalum
kwa ajili ya Rais pale
kunapokuwa na kitisho
chochote cha usalama.Hali ya
kiusalama kwa sasa si nzuri
sana ndiyo maana nimeletwa
hapa” akasema Jenerali Akiki.
“Sina hofu yoyote
mheshimiwa Rais baada ya
kukuta Amani imetawala na
watu wanaendelea na shughuli
zao kama kawaida” akasema
Melanie
“Uganda ni shwari tofauti
na taarifa za habari za vyombo
vya magharibi ambao
wamekuwa wakikuza taarifa
kwamba eneo zima la Afrika
Mashariki halikaliki.Wewe
mwenyewe umeshuhudia watu
wakiendelea na maisha yao ya
kila siku bila hofu yoyote na
hivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa
Tanzania.Sikatai kwamba
hakuna kitisho cha amani lakini
hali si kama wanavyotangaza
hawa jamaa.Sisi kama nchi
lazima tujihami dhidi ya kitisho
chochote kutoka nchi
yoyote.Kumekuwa na mfululizo
wa majibizano ya risasi na
mabomu kuanzia jana usiku
katika mpaka wetu na
Rwanda.Watu wengi hawaelewi
mgogoro wetu na Rwanda
haujaanza kwa sababu ya tukio
la juzi bali ni wa siku nyingi
lakini baada ya tukio la juzi
Rwanda wamepata sababu ya
kutaka kuanzisha vita
nasi.Nimekwisha waonya
kwamba nitaichakaza ile
nchi.Nimejipa siku chache za
kuona mwenendo wao na kama
watakuwa bado wanataka
kupigana nasi nitaipiga ile nchi
vibaya mno.Ni nchi ndogo
ambayo haiwezi kuniumiza
kichwa changu.Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo
halikadhalika tumekuwa na
mzozo nao wa muda mrefu na
wote wanataka kuitumia nafasi
hii kupigana nasi.Tanzania
hatujawahi kuwa na ugomvi
nao ni ndugu zetu.Ni hasira tu
za Dr Fabian lakini naamini
washauri wake watamshauri
vyema.Naamini sisi na Tanzania
katu hatutaweza kupigana
ndiyo maana utaona Tanzania
haijapeleka vikosi vyake vya
jeshi katika mpaka wake na
Uganda kwa ajili ya
vita.Ninaamini hata kile kikosi
cha umoja wanachokiunda
Tanzania walishawishiwa na
hawa marais wa Rwanda na
Congo.Kwa ujumla ugomvi wetu
mkubwa ni sisi na Rwanda na
Congo ndiyo maana nimeamua
kuwaita nyumbani mabalozi
wangu na kuwafurusha
mabalozi wao,sitaki mchezo”
akasema Jenerali Akiki.
“Tuachane na hayo.James
karibu.Nieleze kile
kilichotukutanisha hapa usiku
wa leo” akasema Jenerali
Akiki.James Kasai akarekebisha
tai yake na kusema
“Mheshimiwa Rais kuna
jambo kubwa ambalo limenileta
kwako usiku wa leo” akasema
na kunyamaza kidogo
“Mheshimiwa Rais nadhani
unamkumbuka Lucy Muganza”
akasema James
“Ndiyo ninamfahamu.Lucy
Muganza alikuwa ni rafiki wa
familia yangu.Yeye na mke
wangu walisoma pamoja hivyo
walikuwa na ukaribu
mkubwa.Kila nilipopata safari
ya kwenda Paris Lucy na
mumewe walinikaribisha katika
makazi yao Paris na Lucy
alinipikia chakula yeye
mwenyewe kwa mikono
yake.Hakutaka chakula changu
kipikwe na wapishi
wengine.Kwa ujumla naweza
kusema Lucy alikuwa ni kama
ndugu yetu.Tulishibana
sana.Wiki mbili kabla ya
kuuawa walikuwa na
mazungumzo na mke wangu
kuhusiana na kuanzisha
kampuni ya kutengeneza taulo
za kike hapa Uganda na
alimuahidi kwamba anakwenda
katika uchaguzi na pale
uchaguzi utakapomalizika basi
watalijadili suala hilo lakini kwa
bahati mbaya alikatishwa
maisha yake kikatili” akasema
Jenerali Akiki
“Japo hakuna ushahidi wa
moja kwa moja uliopatikana
kuhusiana na waliomuua Lucy
na mumewe lakini tunafahamu
mauji yale yalipangwa na
Tanzania na jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo.Hakuna
kitu cha kuficha Congo na
Tanzania walipanga mauaji
yale.Tunafahamu kwamba
Patrice Eyenga na Dr Fabian
Kelelo ndio wahusika wakuu wa
mauaji yale” akanyamaza
kidogo na kuwasha sigara
halafu akaendelea
“Nakumbuka tulimaliza
mkutano wa kawaida wa
jumuiya ya Afrika mashariki na
Rais Fabian akachukua
uenyekiti na katika mkutano
huo tuliikaribisha rasmi
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo kama mwanachama
mpya.Kikao kilipomalizika Rais
Patrice na Dr Fabian walikuwa
na mazungumzo marefu ya siri
na wiki moja baadae Lucy
akauawa nchini
Tanzania.Patrice alikuwa na
wasiwasi kama angegombea na
Lucy lazima angeshindwa
uchaguzi ndiyo maana
akapanga njama za kumuua.Ni
ukweli ulio wazi kwamba kama
Lucy angeshiriki katika
uchaguzi ule angeshinda kwa
namna anavyokubalika nchini
Congo.Kama Lucy angeshinda
uchaguzi mashirikiano yetu
yangekuwa makubwa sana na
niliahidi kumpa ushirikiano
mkubwa sana katika uongozi
wake.Kwa bahati mbaya
mambo hayakuwa kama
yalivyokusudiwa.Kuna wakati
naichukia sana siasa.Kama
isingekuwa siasa basi hivi sasa
Lucy angekuwa mzima kabisa”
akasema Jenerali Akiki na
kuvuta sigara
“Mheshimiwa Rais”
akasema James
“Aliyeko mbele
yako,Melanie Davis ni binti wa
Lucy na Laurent Muganza
ambaye jina lake halisi ni
Theresia Muganza” akasema
James.Nusura sigara aliyoshika
Jenerali Akiki imponyoke kwa
mstuko alioupata.Akamtazama
Melanie kwa mshangao
mkubwa
“Huyu ndiye Theresa
Muganza mtoto wa Lucy?
Akauliza Jenerali Akiki
“Ndiyo mheshimiwa Rais”
akasema James
“Hapana si yeye.Nimekuwa
karibu na familia ya Muganza
ninawafahamu wote
ninamfahamu Theresia
Muganza na hata picha zao
ninazo lakini huyu hafanani
kabisa na Theresia ! akasema
Jenerali Akiki huku akiendelea
kumtazama Melanie.James
akamfanyioa ishara Melanie
aendelee
“Nakumbuka mama
alinipigia simu jioni
iliyotangulia siku ya kuuawa
kwake akaniambia kwamba
kesho yake watakuja Dar es
salaam kunichukua
tunakwenda wote Kinshasa kwa
ajili ya sherehe za mama
kutambulishwa kama mgombea
uchaguzi kupitia chama cha
upinzani cha CDP.Nilikataa
kwenda Kinshasa nikamweleza
mama kwamba wao waende
peke yao kwani nilikuwa
najiandaa kwa mitihani,lakini
alisisitiza kwamba lazima
twende wote kama
familia.Kesho yake alitua katika
uwanja wa ndege wa Julius
Nyerere nikawapokea.Walihitaji
kupumzika kidogo Dar es
salaam kabla ya kuelekea
Kinshasa hivyo tukaondoka
uwanja wa ndege kuelekea
katika nyumba niliyokuwa
ninaishi.Tukiwa njiani ndipo
lilipotokea lile shambulio.”
Akanyamaza kidogo na
kutazama chini.Baada ya muda
akaendelea
“Baba na mama wote
walifariki pale pale kwa risasi
na mimi nikapigwa risasi ya
kifua nikakimbizwa hospitali
nikafanyiwa upasuaji na baadae
nikahamishiwa Paris kwa
matibabu zaidi. Mazishi ya
wazazi wangu niliyashuhudia
kupitia runinga.Nilitibiwa kwa
siri hadi nilipopata nafuu.Siku
moja alikuja kunitembelea Rais
wa Ufaransa Michael Weren na
ndipo akanieleza kila kitu
kuhusiana na chanzo cha
kuuawa wazazi wangu” Melanie
akanyamaza tena kidogo halafu
akamtazama Rais Akiki na
kuendelea
“Rais Michael Weren
alinieleza mambo mengi namna
rasilimali za Congo
zinavyochotwa na watu
wachache.Alinieleza kwamba
walihitaji mtu ambaye
angeweza kusimamia rasilimali
za Congo ziwanufaishe watu wa
Congo na ndipo wakamshawishi
mama yangu aweze kugombea
urais kupitia chama cha CDP na
akakubali kwa bahati mbaya
hakufikia malengo yake
akauawa.Nilielezwa mambo
mengi na mwisho Rais Michael
akanitaka nivae viatu vya mama
yaani niyaendeleze yale ambayo
mama alitakiwa kuyakamilisha
akimaanisha kuikomboa nchi
yangu ya Congo kutoka katika
makucha ya
wanyonyaji.Nilikuwa na hasira
na watu waliomuua mama
hivyo nikakubali na ndipo
ulipoanza mkakati wa
kuniandaa.Jambo la kwanza
nililofanyiwa lilikuwa ni
kubadili mwonekano
wangu.Ililetwa timu ya
madaktari bingwa wa upasuaji
wa plastiki wakanifanyia
upasuaji mwonekano wangu
ukabadilika na kuwa hivi
ninavyoonekana sasa.Baada ya
hapo nikatumwa Afrika
Mashariki kwa ajili ya kuja
kuendelea na kazi ambayo
mama alitakiwa kuifanya yaani
kuikomboa Congo kutoka katika
makucha ya wanyonyaji”
akasema Melanie na Jenerali
Akiki akawasha sigara nyingine
akavuta
“Kwa hiyo mheshimiwa
Rais mimi ndiye Theresa
Muganza mtoto wa Lucy na
Laurent Muganza” akasema
Melanie
“Nimekuelewa
Melanie.Huna haja ya kuelezea
zaidi” akasema Jenerali Akiki na
kuvuta mkupuo mkubwa wa
sigara akapuliza moshi
“Lini hawa jamaa
watatuacha huru? Miaka mingi
wametutawala wametufanyia
kila aina ya udhalilishaji
tumekuwa watumwa
wao,wametuchapa
viboko,wamechukua kila aina
ya mali waliyotaka lakini bado
hata kidogo tulichobaki nacho
wanakitaka.Nina hasira sana na
haya mataifa ya magharibi”
akasema na kupuliza moshi
“Sikujua kama Ufaransa
ndio waliomshawishi Theresia
Muganza kuingia katika siasa
kwa maslahi yao huku
wakimdanganya kwamba
anakwenda kuikomboa
Congo.Kwa miaka nenda miaka
rudi nchi hizi kubwa
wamekuwa wakifadhili
makundi ya waasi ambao
wamekuwa wakipigana vita
isiyokwisha kwa maslahi yao
wenyewe.Wote tunalitambua
hilo.Hata wakongomani
wanalitambua hilo ndiyo maana
mimi niliamua kumuunga
mkono James Kasai ambaye
hakuwa chini ya nchi yoyote ya
Ulaya na mapambano yake
yalikuwa ni kuikomboa Congo
kutoka katika makucha ya
mabeberu.Alikuwa akipambana
kwa maslahi ya kweli ya
wakongomani.Huyu ndiye
pekee ambaye anaweza
akairejesha Congo katika
mikono ya wakongomani na
wakafaidika na rasilimali zao
lakini wengine wote wanaodai
kutaka kuikomboa Congo ni
vibaraka wa mataifa
makubwa.Mabeberu hao
wamemshtaki James katika
mahakama ya uhalifu wa kivita
na hivi sasa anatafutwa lakini
nimeapa kumpigania James
hadi mwisho kwani amejitolea
kupambana kuikomboa
Congo.Kwa nini Lucy alikubali
kudanganywa na hawa watu?
Akauliza Jenerali Akiki
“Kama haitoshi bado
wanataka kumtumia tena na
mwanae.Melanie hawa watu
wamekuingiza katika hatari
kubwa sana kwa ajili ya maslahi
yao wenyewe ! akafoka Jenerali
Akiki
“Ninafahamu mheshimiwa
Rais” akasema Melanie na
Jenerali Akiki akavua kofia
akaiweka mezani na
kumtazama Melanie kwa macho
makali
“Mheshimiwa Rais”
akasema Melanie
“Ninafahamu
wanachokitaka hawa watu
ambao wamenituma kuja
huku.Wanadai kwamba
ninachokifanya ni kwa ajili ya
kuikomboa Congo wakati
kumbe kuna mambo
wanayatafuta.Ninafahamu
mheshimiwa Rais kwamba
wanataka kunitumia kwa
maslahi yao na waliponituma
nilikubali kwa kuwa nilikuwa
tayari na mipango yangu
mingine”
“Mipango ipi uliyo nayo
Melanie?akauliza Jenerali Akiki
“Mpango wa kwanza ni
kulipiza kisasi kwa wale wote
waliohusika katika vifo vya
wazazi wangu na ndiyo maana
nilimfuata James Kasai anisaidie
katika mpango wangu wa
kulipiza kisasi.Nilianza kwanza
na wake za marais Dr Fabian na
Patrice Eyenga” akasema
Melanie
“Ulifanya vizuri sana
Melanie na sikulaumu kwa
ulichokifanya.Kitendo
walichokifanya wale jamaa ni
kibaya sana na hakikubaliki na
wanastahili adhabu
kali.Ninakuunga mkono kwa
ulichokifanya japo kimezua
mtafaruku mkubwa lakini
jambo kubwa ni kwamba hawa
wakatili lazima nao wapate
mateso makali” akasema
Jenerali Akiki
“Mheshimiwa Rais”
akasema James
“Baada ya kile kilichotokea
Dar es salaam,Melanie alinipigia
simu akaniambia kwamba
anataka kuingia katika awamu
ya pili ya mpango wake
akaniambia kwamba safari hii
anataka kumuua Patrice
Eyenga” akanyamaza baada ya
sura ya Jenerali Akiki
kuonyesha mstuko kidogo
“Kumuua Patrice
Eyenga?akauliza Jenerali Akiki
“Ndiyo mheshimiwa
Rais.Ninataka kumuua Patrice
Eyenga na nikitoka hapo
nitahamia Tanzania nataka
kumuua pia Dr Fabian
Kelelo.Hawa ndio waliowaua
wazazi wangu na katika
mpango wangu lazima nao
niwaondoe” akasema Melanie
“Aliponieleza jambo hilo”
James akaendelea
“Nilishindwa kumpa jibu la
moja kwa moja nikamtaka aje
Kampala tuzungumze kwani
hata mimi jambo hili liko juu ya
uwezo wangu.Kwa hiyo
mheshimiwa Rais tumekuja
hapa kwako kwa suala
hilo.Melanie anataka Patrice
Eyenga auawe” akasema James
Kasai na Jenerali Akiki akainuka
akaenda dirishani akafunua
pazia akachungulia nje halafu
akaenda kuegemea
meza.Akainamisha kichwa
akatafakari kisha akasema
“Melanie kwanza kabisa
ninashukuru sana kukutana
nawe.Nilikuwa najiuliza sana
mahala alipo Theresa Muganza
na hatimaye
umenifikia.Ninashukuru sana
James kwa kumleta mwanangu
huyu.Kwa ukaribu niliokuwa
nao na wazazi wako wewe ni
sawa na mwanangu”akasema
Jenerali Akiki
“Ahsante sana mheshimiwa
Rais” akasema Melanie
“Naomba nikuhAkikishie
kwamba ninakuunga mkono
kwa mpango wako wa kulipiza
kisasi kwa wale wote
waliofanya unyama mkubwa wa
kuwaua wazazi wako.Hata
hivyo mpango wa kumuua
Patrice Eyenga huu ni mpango
mkubwa sana na hauwezi
ukatekelezeka kwa haraka
kama unavyodhani.Kumuua
Rais wa nchi hata kama ni
ndogo si mpango mdogo.Ni
jambo zito na gumu sana hasa
kwa nyakati hizi ambapo ulinzi
kwa marais wengi umekuwa
mkali mno.Kwa miaka ya
zamani ilikuwa rahisi kidogo na
ndiyo maana marais wengi
waliuawa lakini kwa miaka ya
sasa marais ni watu
wanaolindwa mno.Nadra sana
kusikia Rais wa nchi Fulani
ameuawa zama hizi” akasema
Jenerali Akiki na kunyamaza
kwa muda
“Hata hivyo mpango huu
wa kumuondoa Patrice Eyenga
si mbaya.Ni mpango mzuri
kwani huyu naye amekuwa ni
kibaraka wa baadhi ya mataifa
ya makubwa.Alisaidiwa na
Marekani kuingia madarakani
na alipoingia tu ikulu
akayafukuza makampuni
mengine yote makubwa kutoka
mataifa ya Ulaya yaliyokuwa
yamewekeza katika sekta ya
madini na sasa sekta ya madini
nchini Cogo inashikwa na
makampuni ya
kimarekani.Japokuwa hakuna
vita nchini Congo kwa sasa
lakini bado sehemu kubwa ya
mali inazidi kuchotwa na
wageni hawa kufuatia mikataba
mibovu inayowapa nafasi
wawekezaji wa kimarekani
kufaidika na rasilimali za Congo
kuliko wazawa hivyo bado nchi
ya Congo haijampata mtu yule
ambaye atakuwa mzalendo wa
kweli na atahAkikisha rasilimali
zote ambazo Mungu amewapa
wakongo zinawanufaisha kuliko
kwenda kuyanufaisha mataifa
makubwa ya kigeni”
akanyamaza tena akafikiri
kidogo halafu akasema
“Mtu pekee ambaye
ninaamini ana uchungu na nchi
ya Congo na ambaye anaweza
akasimamia rasilimali za Congo
ili ziwanufaishe wananchi wa
Congo ni James Kasai.Sina
mashaka naye hata kidogo
kwani ninafahamu harakati
zake toka enzi za baba yake
ambaye aliuawa na vikosi vya
serikali ya Congo” akanyamaza
akamtazama Melanie na
kusema
“Melanie mimi niko tayari
kuungana nanyi katika mpango
huu endapo tutakubaliana
kwamba baada ya mauaji hayo
James Kasai ndiye
atakayechukua nafasi ya Rais
wa Jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo” akasema Jenerali Akiki
na James Kasai akatabasamu
“Mheshimiwa Rais mimi
ninachokihitaji ni kuwamaliza
wale wote ambao waliwaua
wazazi wangu.Hata hivyo kifo
cha Patrice Eyenga ni kitu
ambacho mataifa ya Ulaya hasa
Ufaransa watakifurahia sana
kwani kitawapa nafasi ya
kuweza kurejea tena nchini
Congo”
“Usihofu Melanie.Hakuna
nchi ambayo itasogeza pua yake
Congo.James Kasai akichukua
urais wa Congo atawafurusha
wawekezaji wote na mali zote
za Congo zitamilikiwa na
wazawa.Kupitia madini hayo
watoto watasoma shule
bure,huduma za afya zitaboreka
ujenzi wa miundo mbinu
utafanyika na mambo mengine
mengi”
“Mheshimiwa Rais jambo
hili ndilo ambalo nimekuwa
nikilipigania kwa miaka mingi
hivyo nadhani ni wakati sasa
umefika wa kuibadili historia ya
Congo” akasema James Kasai
“Nakubaliana nawe
James.Wakati umefika wa
kufanya ukombozi wa kweli
kwa nchi ya Congo.Mimi
nitashirikiana nanyi katika
mpango huo hata hivyo
tambueni kwamba mpango huu
utatugharimu fedha nyingi mno
kuutekeleza” akasema Jenerali
Akiki
“Kuhusu pesa mimi
nitagharamia mheshimiwa
Rais.Kiasi chochote
kitakachohitajika mimi nitatoa”
akasema Melanie na Jenerali
Akiki akamtazama
“Niachieni suala hili
nilifanyie kazi halafu nitawaita
na kuwapa
mrejesho.Nitazungumza
kwanza na mkuu wa majeshi wa
Congo ambaye nina undugu
naye.Nitamdokeza suala hili
kisha tutajadiliana namna
tutakavyoweza kumuondoa
Patrice Eyenga.Hatuwezi
kutekeleza mpango huu sisi
wenyewe bila kushirikiana na
watu wa ndani ya serikali ya
Congo” akasema Jenerali Akiki
Kikao kilimalizika saa saba
za usiku kwa jenerali Akiki
kulibeba suala lile na kuwaahidi
kuwapa mrejesho siku
inayofuata.Melanie na James
Kasai wakaondoka katika
makazi yale ya Rais yaliyomo
ndani ya kambi ya jeshi.
DAR ES SALAAM – TANZANIA
Nahodha wa meli kubwa ya
mizigo alitoa maelekezo na meli
ile ikasimama.Ilikaribia sana
kufika katika bandari ya Dar es
salaam.
“Annabel sasa
umefika.Hatuwezi kwenda
nawe hadi bandarini.Vijana
wangu watakupeleka hadi
ufukweni kisha baada ya hapo
utajua mwenyewe
utakavyoendelea”akasema
Nahodha wa meli ile ambayo
Ruby alisafiri nayo kutokea
bandari ya Le havre nchini
Ufaransa.Wafanyakazi wengine
wote wa meli ile walikusanyika
pamoja kwa ajili ya kumuaga
Ruby ambaye kwa kwa muda
wote wa safari alikuwa ni kama
mwenzao.Walimzoea sana
kwani alikuwa ni mwanamke
pekee melini hivyo
walihAkikisha wanamtunza
kwa kila namna ili aweze kufika
salama Tanzania
“Kaka zangu sina neno zuri
la kuwashukuru kwa wema
wenu mkubwa na ukarimu wa
ajabu sana
mlionifanyia.Ahsanteni sana
kwa kila kitu.Nimefurahi mno
kuwa nanyi kwa muda huu
wote wa safari hadi kufika
hapa.Nimefurahi kuwafahamu
na katika maisha yangu
sintaweza kuwasahau
kamwe.Ninyi nyote mtakuwa
ndani ya moyo wangu hadi siku
ninaingia kaburini” akasema
Ruby na makofi yakapigwa.
“Naomba niwashukuru kwa
ujumla wenu kwani nikisema
nimshukuru mmoja mmoja
muda haunitoshi hivyo
naombeni mpokee sana
shukrani zangu za dhati
kabisa.Nitaendelea kuwaombea
ili msafiri salama kurejea
nyumbani na tutazidi
kuwasiliana.Mtakapokuja tena
Tanzania aidha mmoja mmoja
kwa matembezi au kikazi kama
hivi msiache kunitafuta na
nitakuwa mwenyeji wenu”
akasema Ruby na
kuwakumbatia kuwaaga
mmoja mmoja halafu
akasindikizwa na nahodha hadi
katika boti ile ndogo ambayo
ilikuwa na watu wanne
ikashushwa majini kisha
ikawashwa na kuondoka
kuelekea ufukweni.
Walimfikisha Ruby
ufukweni wakaagana na
kuondoka akaanza kutembea
taratibu.Hakujua alikuwa
sehemu gani kwani jiji la Dar es
slaam hakulifahamu
vyema.Aliiona kwa mbali
barabara na magari yakipita
akaanza kuelekea huko.Wakati
akitembea mara akakutana na
vijana waliokuwa wamekaa
kikundi jumla yao wakiwa
sita.Wote wakatimua mbio
walipomuona akacheka kwa
namna walivyotimua mbio
“Wamestuka kuniona hapa
usiku huu.Wanadhani mimi ni
mzimu” akawaza Ruby huku
akiendelea kupiga
hatua.Alikuwa na begi lake la
mgongoni na pochi ndogo
ambayo alikuwa ameweka
fedha na vifaa vingine vidogo
vidogo.Suruali yake alikuwa
ameikunja hadi magotini
akavaa fulana ndefu ambayo
iliificha bastora aliyokuwa
ameichomeka katika suruali.
“Dar es salaam jiji
lisilolala.Nikifika barabarani
nitajua nielekee wapi” akawaza
Ruby huku akiongeza hatua
kuelekea barabarani.
Hatimaye baada ya
kutembea kwa dakika kadhaa
akaifikia barabara.Magari
yalikuwa mengi barabarani
akatembea barabara akiwa
hana wasiwasi wowote wa
kukutana na vibaka kwani
alikuwa na bastora
kiunoni.Alivuka barabara na
kuingia upande wa pili
akatembea hadi katika mtaa
mmoja akamkuta mlinzi
anayelinda duka akamuuliza
mahala anakoweza kupata teksi
akamuelekeza na Ruby akafuata
maelekezo ya Yule mzee
akajikuta ametokea katika
klabu moja ya usiku.Kulikuwa
na magari mengi yameegeshwa
na watu wengine walikuwa
wamekaa nje kulikokuwa na
sehemu nzuri za kukaa
wakipata kinywaji.Ruby
akamfuata mlinzi mmoja
aliyekuwa amevaa sare zenye
rangi nyekundu na nyeusi
akiwa na rungu akamsalimu na
kumuuliza mahala anakoweza
kupata taksi.Mlinzi yule
akamuelekeza mahala
zinakoegeshwa taksi
Madereva taksi
walimchangamkia sana
walipomuona,Ruby akachagua
gari moja zuri akamtaka dereva
ampeleke katika hoteli nzuri
isiyo ya ghali sana lakini yenye
usalama wa kutosha.
“Umetokea wapi
dada?akauliza Yule dereva taksi
ambaye alionekana kulifahamu
vyema jiji
“Hapa hapa Dar”akajibu
Ruby kwa ufupi akionekana
kutotaka mazungumzo yoyote
na yule dereva
“Dar es salaam ni
kubwa.Sehemu gani ya Dar
unatokea? Akauliza Yule dereva
na Ruby akakasirika
“Stop asking
questions.Drive ! akasema Ruby
kwa sauti kali kidogo
“Samahani dada.Ni kawaida
yetu sisi madereva
kuwachangamkia wageni”
akasema Yule dereva na safari
ikaendelea kimya kimya
Dereva taksi akafungua
droo ya gari na kumpatia Ruby
vipeperushi sita vya mahoteli
mbali mbali
“Huwa tunatembea na
vipererushi hivi kwa ajili ya
wateja wetu hasa wanaotoka
nje ya Dar es salaam au nje ya
nchi.Tazama kama kuna hoteli
itakayokupendeza kati ya hizo”
akasema Yule dereva na Ruby
akachukua vile vipeperushi
akavipitia
“Nipeleke Hotel Marcelino”
akasema Ruby
Mazungumzo yalikuwa
machache sana garini hadi
walipofika hoteli Marcellino
“Hapa ni sehemu nzuri na
salama naamini patakufaa”
akasema yule dereva huku
akiegesha gari maegesho.Ruby
akafungua ule mkoba wake
mdogo akampa Yule dereva
dola kadhaa za kimarekani
kama nauli kwani hakuwa na
fedha ya Tanzania.Yule dereva
akatoa tabasamu kubwa sana
“Sister kama utahitaji
dereva mwaminifu
anayeifahamu kila sehemu ya
jiji usiache kunitafuta” akasema
Yule dereva na kumpatia Ruby
kadi yake ya
biashara.Wakaagana na Ruby
akaingia ndani ya hoteli
akapokewa vizuri sana na
wahudumu wachangamfu na
kuchukua chumba kizuri
kilichokuwa ghorofa ya
sita.Alikodisha chumba kwa
muda wa siku mbili na kulipa
kwa kutumia dola za
kimarekani
“Ahsante Mungu
umenifikisha salama
Tanzania.Haikuwa safari rahisi
lakini umenisimamia toka
mwanzo hadi sasa.Naamini una
kusudi na mimi ndiyo maana
ukaniepusha na mitego yote
iliyotegwa ili nife.Ee baba
nimerudi nyumbani,nimekuja
kuitumikia nchi
yangu.Nakuomba uniongoze
niweze kuitumikia nchi yangu
kwa kila uwezo ulionijalia”Ruby
akaomba mara tu baada ya
kuingia chumbani.
“Sasa nimeingia Dar es
salaam.Mtu wa kwanza
kumtafuta ni Rais Dr Fabian
ambaye natakiwa kumjulisha
kwamba tayari
nimefika.Ningefurahi sana kama
kipenzi changu Mathew
Mulumbi angekuwepo furaha
yangu ingekamilika.Hata hivyo
kwa kuwa tayari nimefika
salama Dar es salaam nitatafuta
ukweli juu ya kifo chake.Lazima
nijue alikufaje na kama
ikiwezekana kujua alizikwa
wapi na kupata masalia
yake.Lakini kuna kitu ndani ya
nafsi yangu kinakataa kabisa
kuamini kuhusu kifo cha
Mathew.Kwa vile tayari niko
hapa nitaujua ukweli kwa sasa
nishughulikie kwanza
mawasiliano na Rais” akawaza
Ruby na kuingia bafuni kuoga
kisha akakaa sofani akaishika
kompyuta yake akataka
kuiwasha akasita
“Ngoja nisiiwashe kwanza
wale jamaa kule Uingereza
wanaweza wakaiona kwani
bado ilikuwa imeunganishwa na
mtandao wao.Kuna vitu
natakiwa kuvifanya lakini hadi
pale nitakapokuwa na
kompyuta nyingine pembeni”
akawaza Ruby na kuchukua
kitabu chake cha kumbu kumbu
akazitafuta namba za simu za
Rais Dr Fabian akapiga simu
mapokezi na kuomba huduma
ya simu binafsi.Baada ya dakika
chache akapigiwa simu na
kujulishwa kwamba anaweza
akapiga namba yoyote ya simu
anayoitaka.Akampigia Dr
Fabian.Simu ikaita na
kupokelewa.
“Hallow” ikasema sauti ya
upande wa pili ambayo Ruby
aliitambua mara moja ni ya Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais”
akasema Ruby
“Nazungumza na nani?Dr
Fabian akauliza
“Unazungumza na Ruby”
“Ruby?
“Ndiyo.Ruby Rafael
Magalla”
“Oh my God ! Ruby.Uko
wapi? Akauliza Dr Fabian
“Tayari nimeingia Dar es
salaam usiku huu”
“Thank you Lord” akasema
Dr Fabian na kushusha pumzi
“Uko salama kabisa?
“Ndiyo mzee niko salama
kabisa” akajibu Ruby
“Ruby nashukuru sana
umefika salama.Mimi kwa sasa
siko Dar es salaam niko
Mbeya.Nadhani ulipata taarifa
za tukio lililotokea juzi”
“Tukio gani mheshimiwa
Rais?
“Hujapata taarifa za tukio
lililotokea juzi?
“Hapana mzee.Sikuwa
nafuatilia habari zozote
nilijiweka nje kabisa ya dunia”
“Kuna tukio limetokea hivi
majuzi hapo Dar es salaam na
watu kadhaa walifariki
akiwamo mke wangu.Kesho
tutamzika Tukuyu Mbeya kisha
nitarejea Dar es salaam.Nitakuja
kuzungumza nawe mara
nitakaporejea”
“Pole sana mheshimiwa
Rais”
“Ahsante sana.Nataka
kufahamu mahala ulipofikia”
akasema Dr Fabian na Ruby
akamfahamisha hoteli alikofikia
chumba na jina analotumia la
Annabel.
“Dakika chache zijazo
watakuja wasaidizi wangu hapo
hotelini watakuchukua na
kukupeleka sehemu
salama.Wewe ni mtu muhimu
sana.Jiandae muda si mrefu
watakuja kukuchukua”
“Ahsante sana mheshimiwa
Rais”
“Ahsante sana Ruby kwa
kujitahidi hadi umeweza kufika
salama.Nilikuwa na wasiwasi
mkubwa kama ungeweza kufika
salama.Kesho tutazungumza
kwa kirefu zaidi nitakaporejea”
akasema Dr Fabiana na kuagana
na Ruby
“Ahsante Mungu kwa
kuendelea kuninyooshea
mambo yangu.Huyu ndiye hasa
niliyetakiwa kuwasiliana naye
kabla ya yote na kumfahamisha
kwamba niko Dar es
salaam.Amesema kuna tukio
limetokea hivi majuzi ni tukio
gani hilo hadi mke wake
akafariki dunia? Nitajua hiyo
kesho tutakapoonana.Natamani
kuwasilianana Gosu Gosu
kumjulisha kwamba niko Dar es
salaam lakini ngoja kwanza
nisubiri atafahamu hapo baadae
nitakapokuwa nimetulia”
akawaza Ruby huku akipakia
vitu katika begi lake
Dakika kumi na tano zilipita
toka alipozungumza na Rais
mlango wa chumba chake
ukagongwa.Akaishika bastora
yake halafu akasogea taratibu
mlangoni na kuufungua kwa
tahadhari kubwa.Kulikuwa na
watu wapatao wanne
“Annabel?akauliza mmoja
wa wale jamaa
“Ndiyo”
“Tumepewa maagizo na
mzee tuje tukuchukue.Mizigo
yako iko wapi?akauliza Yule
jamaa huku akiingia mle
chumbani mwa Ruby
“Sina mizigo zaidi ya hili
begi dogo”akasema Ruby na
mmoja wa wale jamaa
akalibeba begi lile wakatoka
hadi mapokezi ambako Ruby
alirudisha chumba na
kuongozana na wale jamaa hadi
nje ambako kulikuwa na magari
matatu ya rangi nyeusi.
Ruby alipelekwa hadi
katika nyumba moja nzuri sana
na kukaribishwa katika chumba
kikubwa na kizuri.
“Hapa sasa naweza kulala
usingizi mzuri.Sina hofu
yoyote”akawaza Ruby akiwa
kitandani
RIYADH – SAUDI ARABIA
Kumepambazua tena jijini
Riyadh.Saa mbili za asubuhi
tayari Mathew Mulumbi
alikwisha wasili katika uwanja
wa ndege wa kimataifa wa
mfalme Khalid jijini
Riyadh.Alikuwa ameongozana
na mkewe Najma ambaye
waliagana na Mathew akaenda
kukamilisha taratibu halafu
akaenda sehemu ya kusubiria
ndege.Muda ulipofika waliingia
ndegeni na safari ikaanza
kuelekea Cairo Misri
Ilikuwa ni safari ya saa
mbili kutoka Riyadh hadi Cairo
Misri.Kutokea pale Mathew
alitakiwa kuondoka na ndege ya
shirika la ndege la Misri
kuelekea Tanzania ambayo
ilikuwa inaondoka Cairo saa
kumi za jioni.
DAR ES SALAAM – TANZANIA
Ni kama vile Ruby alifumba
macho na kufumbua akajikuta
tayari imekwisha fika
asubuhi.Akatoka kitandani na
kwenda kufunua pazia
akatazama nje.Kulikuwa na
madhari ya kuvutia
mno.kulikuwa na uwanja
mkubwa uliokuwa na nyasi
nzuri za kijani.Kulikuwa pia na
bwawa kubwa la kuogelea
“Hapa ni wapi? Ni hoteli au
ni wapi?Mbona pazuri namna
hii?Nyumba nzuri,mandhari
safi,ulinzi wa
kutosha.Namshukuru sana Rais
kwa kunileta hapa.Nimelala
usingizi mzuri sana leo nikiwa
na uhakika niko salama” Ruby
akageuka baada ya mlio wa
simu kusikika akaenda mezani
akaichukua na kupokea
“Hallow” akasema
“Ruby habari yako”akasema
mtu wa upande wa pili na Ruby
akaitambua sauti
“Mheshimiwa Rais”
akasema Ruby
“Umeamkaje Ruby?
“Nimeamka salama kabisa”
“Nafurahi kusikia
hivyo.Nimekupigia kujua
maendeleo yako.Unahudumiwa
vizuri?
“Ndiyo mheshimiwa
Rais.Ninahudumiwa vyema”
“Sawa Ruby endelea
kupumzika nitarejea jioni
tutaonana.Kama kuna sehemu
yoyote unataka kwenda
wasaidizi wangu hapo
watakupeleka.Kuwa huru jisikie
nyumbani” akasema Dr Fabian
“Nashukuru sana
mheshimiwa Rais” akasema
Ruby na Rais akakata simu
“Sasa baada ya kuwa na
uhakika kuwa niko salama
natakiwa kuanza
maandalizi.Mua wote niliokaa
ndani ya meli safarini kuja huku
nilisahau kabisa kuupendezesha
mwi…” akatolewa mawazoni
baada ya kengele ya mlango
kulia akaenda kuufungua
akakutana na mwanamama
mmoja mnene.
“Shikamoo mama” akasema
Ruby
“Marahaba mwanangu
hujambo?
“Sijambo.Karibu mama”
“Ahsante.Naitwa mama
Adelina.Mimi ndiye muangalizi
mkuu wa nyumba hii.Sikuwepo
jana usiku ulipofika nilikuwa
Mbeya msibani lakini alfajiri ya
leo Rais amenirejesha Dar es
salaam kwa helkopta ili nije
nihAkikishe unapata huduma
nzuri.Karibu sana jisikie
nyumbani”akasema Yule mama
na Ruby akatabasamu
“Nashukuru sana mama”
akasema Ruby kisha
wakazungumza kidogo na
mama Adelina akamuacha Ruby
ajiandae.Alipojiandaa alikuta
gari liko tayari linamsubiri
akaondoka kwenda kufanya
manunuzi ya vitu mbali mbali
hasa nguo na vipodozi
UGANDA
Saa kumi na moja za jioni
helkopta iliyombeba mkuu wa
majeshi wa jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo iliwasili
katika kambi ya muda
iliyowekwa na vikosi vya Congo
katika mpaka wake na
Uganda.Wanajeshi hawakuwa
na taarifa zozote za mkuu wa
majeshi kuwatembelea kule
mpakani.
Helkopta aina ya UH – 60
Black Hawk ya jeshi la anga la
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo ilitua katika kambi ya
muda.Mlango ukafunguliwa
akashuka Jenerali Jean Paul
Mutombo mkuu wa majeshi ya
Congo.Alipokewa na mkuu wa
kikosi kile kilichopiga kambi
mpakani kisha akamuongoza
hadi katika ofisi ya muda
ambako akapewa taarifa fupi ya
maendeleo ya kambi toka
walipofika. Kisha
akazungushwa katika kambi ile
akaikagua halafu akazungumza
na wanajeshi akawataka wawe
tayari muda wowote
kupambana na adui yeyote
atakayetishia amani na utulivu
wa nchi yao.
Baada ya kuzungumza na
wanajeshi na kuwapa moyo
Jenerali Mutombo akaagana na
maafisa wa jeshi akaingia katika
helkopta,akawapa maelekezo
marubani waelekee upande wa
Uganda.Marubani wale walitii
amri kisha helkopta ikapaa na
kuondoka pale kambini.Ndani
ya helkopta alikuwepo Jenerali
Mutombo,mlinzi wake na
marubani wawili.Jenerali
Mutombo aliwapa maelekezo
marubani wake sehemu ya
kuelekea na baada ya dakika
arobaini wakawasili katika
uwanja mkubwa uliokuwa
katikati ya msitu.Pembeni ya
uwanja ule kulikuwa na
helkopta moja na wanajeshi
kadhaa wakiwa wameizunguka
kuilinda.Helkopta ya Paul
Mutombo ikatua ikatua katika
uwanja ule,akashuka na
kupokewa na jamaa wawili
waliovaa suti
nzuri,wakasalimiana kwa
furaha wakionekana ni watu
wanaofahamiana sana.Jenerali
akawataka mlinzi wake na wale
marubani wamsubiri akaelekea
ndani ya nyumba nzuri ya rangi
nyeupe.Aliingia ndani hadi
katika sebule nzuri ambako
alimkuta Rais wa Uganda
Jenerali Akiki.Wakasalimiana
kwa furaha kisha
akamkaribisha katika chumba
kingine kwa ajili ya
mazungumzo
“Jenerali Mutombo ahsante
sana kwa kufika” akasema
Jenerali Akiki
“Nisingeweza kukataa
mwito wako mheshimiwa
Rais.Nimetoka kukagua vikosi
vilivyoko mpakani ndipo nikaja
hapa” akasema Jenerali
Mutombo
“Vipi maendeleo ya vijana?
“Vijana wanaendelea
vizuri,wako tayari
kukuchakaza” akasema Jenerali
Mutombo na wote wakaangua
kicheko kikubwa sana
“Uganda na Congo hatuwezi
kupigana hata siku moja.Najua
wengi hasa nchi za magharibi
wanasubiri sana jambo hilo
litokee lakini nakuhAkikishia
katu hatutapigana.Imekuwa ni
kawaida yetu kutunishiana
misuli ila hatutaweza kupigana”
akasema Jenerali Akiki
“Ni kweli mheshimiwa Rais
kupigana ni kitu ambacho
hakiwezi kutokea lakini hata
hivyo Yule jamaa James Kasai
alifanya jambo baya kabisa
kumuua mke wa Rais Patrice
ndiyo maana amekasirika na
kusogeza majeshi
mpakani.Asingefanya vile haya
yote yasingetokea” akasema
Jenerali Mutombo
“Umeongea jambo zuri na
hapo ndipo sehemu nzuri ya
kuanzia mazungumzo yetu
Jenerali Mutombo” akasema
Jenerali Akiki na kubonyeza
kitufe chini ya meza na sekunde
chache mlango ukafunguliwa
akaingia mmoja wa walinzi
wake na kupiga saluti
“Mvinyo tafadhali” akasema
Jenerali Akiki na chupa tatu za
mvinyo zikaletwa haraka sana
akamkaribisha Jenerali
Mutombo
“Mvinyo safi wa Uganda
huu.Siku hizi hatuagizi mvinyo
toka nje tunatengeneza mvinyo
hapahapa Uganda” akasema
Rais Akiki
“Ni hatua nzuri.Ni mvinyo
safi kabisa”
“Sasa tuendelee na
mazungumzo yetu” akasema
Jenerali Akiki na kunywa funda
la mvinyo
“Uligusia kuhusu kile
alichokifanya James
Kasai.Nakubaliana nawe
kwamba hakufanya jambo zuri
na amesababisha hali ya amani
kuchafuka katika eneo lote la
Afrika Mashariki hata hivyo
kuna jambo fulani ambalo
nataka kukufahamisha”
akasema Jenerali Akiki na
kunyamaza kidogo kisha
akaendelea
“Unakumbuka miezi
michache iliyopita aliuawa Lucy
na mumewe Laurent Muganza
nchini Tanzania”
“Ndiyo nakumbuka
mheshimiwa rais” akasema
Jenerali Mutombo
“Mpaka sasa hakuna ripoti
yoyote inayoeleweka kuhusiana
na mauaji yale.Serikali ya
Tanzania inadaiwa kwamba
waliotekeleza mauaji yale
walikuwa ni majambazi na wote
waliuawa lakini ukweli hauko
hivyo.Mauaji yale
yalipangwa.Patrice Eyenga na
Dr Fabian Kelelo ndio
waliopanga mauaji yale na
walimuua Lucy kwa hofu ya
Patrice kushindwa katika
uchaguzi kama angegombea na
Lucy ambaye alikuwa
anakubalika sana nchini Congo”
akasema Jenerali Akiki
“Wengi tulihisi hivyo
mauaji yale yalikuwa ya kisiasa”
akasema Jenerali Mutombo
“Ndiyo.Walijitahidi
kujipanga vizuri ili Lucy auawe
nchini Tanzania na serikali ya
Congo isihusishwe katika
mauaji yale.Wauaji walipewa
maelekezo ya kuiteketeza
familia nzima lakini kwa bahati
mbaya mtoto wa Lucy aitwaye
Theresa Muganza alinusurika”
“Tulielezwa hivyo lakini
kitu cha kushangaza ni kwamba
hadi sasa hakuna anayejua
Theresa yuko wapi na hali yake
inaendeleaje.Tuna wasiwasi
naye atakuwa ameuawa kimya
kimya” akasema Jenerali
Mutombo.Rais Akiki akanywa
mvinyo kidogo na kusema
“Theresa Muganza yuko
hai,amerejea Afrika mashariki
na amekuja hapa Uganda
kuonana nami.Amekuja kulipiza
kisasi kwa wale wote
walioshiriki katika mauaji ya
wazazi wake.Amekuja na nguvu
kubwa na kile kilichotokea juzi
nchini Tanzania yeye ndiye
yuko nyuma yake”
“Theresa ndiye aliyefanya
tukio lile? Anashirikiana na
James Kasai? akauliza Jenerali
Mutombo
“Theresa Muganza ndiye
aliye nyuma ya tukio lile na
mengi yatakayofuata.Amekuja
kulipiza kisasi kama
nilivyokwambia.Ameanza na
wake za marais Patrice Eyenga
na Dr Fabian na sasa amekuja
na mpango mkubwa zaidi”
Jenerali Akiki akanyamaza na
kumtazama Jenerali Mutombo
“Amekuja na mpango
upi?akauliza
“Anataka kumuua Patrice
Eyenga.Nimekuita hapa ili
tujadili suala hili” akasema
Jenerali Akiki.Mutombo
akamtazama kwa muda halafu
akashusha pumzi
“Tafadhali niambie
unachokizungumza hapa ni
utani”
“Si utani Mutombo ni
ukweli mtupu na
ninamaanisha.Niko upande wa
Theresa na ninataka kumsaidia
kumuua Patrice
Eyenga.Alifanya ukatili mkubwa
sana kumuua Lucy”
Ulipita tena muda kidogo
halafu Jenerali Mutombo
akasema
“Hivi sasa Congo hawajui
kama nimekuja hapa kukutana
nawe ni siri yangu na walinzi
wangu.Endapo itajulikana
nitaonekana msaliti kwa
taifa.Nimekuja hapa kwa kuwa
ninakuheshimu sana
mheshimiwa.UKiacha
mahusiano yetu ya kindugu
,umekuwa mwalimu wangu
kijeshi na nimefika hapa
nilipofika kwa sababu yako
lakini pamoja na hayo
sikutegemea kama umeniita
hapa kunieleza ujinga kama
huu” akasema Jenerali
Mutombo huku akisimama
“Tafadhali jenerali
Mutombo kaa unisikilize kile
ninachotaka kukueleza.Nipe
dakika kumi tu kisha
utaondoka”akasema Jenerali
Akiki na Mutombo akaketi.Rais
Akiki akachomoa mkebe na
kutoa sigara moja kubwa
akaiwasha na kuchukua
nyingine.
“Cigar ?akasema na
kumrushia Jenerali Mutombo
kisha wote wakavuta sigara
kidogo halafu Rais Akiki
akasema
“Jenerali Mutombo naomba
ufahamu kwamba maafisa
wengi wa jeshi la Congo
wamepita katika jeshi la Uganda
na nimewafundisha mimi hivyo
ninafahamu kila
kinachoendelea ndani ya jeshi
lenu.Ninafahamu wewe na
maafisa kadhaa mmeandaa
mpango wenu wa mapinduzi
mnataka kumuondoa Rais
Patrice madarakani na sababu
kuu ya kutaka kufanya
mapinduzi ni kutokana na
kuikomesha biashara ya silaha
ambayo iliwanufaisha sana
wewe na maafisa wengine wa
jeshi.Mlikuwa mkiwauzia silaha
makundi ya waasi lakini kwa
sasa hakuna tena biashara hiyo
kwa sababu hakuna
uasi.Ninafahamu kuna nchi
moja kubwa ambayo
inatengeneza silaha na ndiyo
inafadhili mpango wenu wa
kumuua Patrice Eyenga ili
machafuko yatokee na
muendelee na biashara ya
kuuza silaha.Ni mengi
ninayafahamu lakini sitaki
kuyasema hapa kwa sababu ya
muda.Nikosoe kama ninasema
uongo” akasema Jenerali Akiki
na Mutombo hakujibu kitu.
“Ukimya huo unaonyesha
kwamba ninachokisema ni cha
kweli” akasema Jenerali Akiki
na kuvuta sigara yake kubwa
“Jenerali Mutombo
nimekuita hapa kukujulisha
kwamba ninataka kuungana
nanyi katika mpango wenu wa
kumuua Patrice Eyenga”
akasema Jenerali Akiki na
ukimya ukapita huku sigara
zikiendelea kutoa moshi
“Mheshimiwa Rais ni kweli
tunao mpango huo wa
mapinduzi lakini wewe kwa
nini unataka kujiunga nasi?
Akauliza Mutombo
“Lucy Muganza alikuwa
rafiki yangu na nimekasirishwa
sana na kitendo alichokifanya
Patrice Eyenga cha
kumuua.Yule ni mtu mkatili
sana na amekwisha waua watu
wengi kimya kimya hasa
mahasimu wake
kisiasa.Hatuwezi kumuacha
huyu mtu aendelee kuua watu
kimya kimya.Unadhani
akifahamu kuhusu mpango
wenu wa mapinduzi mtabaki
salama?Hakuna atakayebaki
salama nyote mtauawa lakini
kama mtashirikiana nami
endapo kutatokea chochote
basi mtakuwa na sehemu ya
kukimbilia.Nitawapa hifadhi
nchini Uganda.Paul ni wakati
sasa wa kuleta mabadiliko ya
kweli nchini Congo.Ni wakati
wa wakongomani kunufaika na
mali zao.Hilo litawezekana pale
tu Rais Patrice Eyenga
atakapoondolewa madarakani”
akasema Rais Akiki halafu
akaiweka sigara yake katika
kisahani cha kuwekea majivu
“Paul nchi za nje
zimekwisha nufaika vya
kutosha na nchi ya Congo.Ni
wakati wa kusema hapana.Ni
wakati wa kuendesha
mapambano kwa manufaa ya
wakongo.Wakati wa
kutangulizwa na mataifa ya nje
kumwaga damu ya wakongo
umekwisha.Msikubali tena
kuwa vibaraka wa mataifa ya
kigeni”
“Umesema Theresia
Muganza amekuja kulipiza
kisasi nani wanaompa nguvu ya
kuweza kufanya haya
yote?akauliza Paul Mutombo
“Theresia anaungwa mkono
na Ufaransa na ndio
waliomuwezesha hadi akafika
hapa alipofika”akajibu Jenerali
Akiki
“Kama anaungwa mkono na
Ufaransa kwa nini basi
akamtumia James Kasai
kutekeleza shambulio lile la Dar
es salaam?Akauliza Jenerali
Mutombo
“Ufaransa hawataki
kujulikana kama wanahusika na
kile kitakachotokea Congo
ndiyo maana wanataka
kuwatumia waafrika wenyewe
ili hata pale mambo
yatakapoharibika wao
wasihusishwe na lolote hivyo
basi wao wanamuwezesha
Theresia kifedha ili aweze
kutengeneza mtandao wa
kumuwezesha kufanikisha
mipango yao.Katika harakati
zake za kutafuta namna ya
kulipiza kisasi Theresa alijikuta
akifika kwa James Kasai na
ndiye aliyemsaidia kutekeleza
shambulio lile la Dar es salaam”
“Mheshimiwa Rais,Theresia
anatakiwa akae mbali kabisa na
James Kasai.Hana sifa nzuri na
anatafutwa kila kona.Kama
haitoshi tayari amegeuza kundi
lake kuwa la
kigaidi.Anashirikiana na
magaidi wa IS.Huyu mtu hafai
hata kidogo kuungwa mkono
na…”
“Jeneral Mutombo”
akasema Rais Akiki na
kumkatisha Mutombo
“Katika mpango wa
mapinduzi James Kasai naye
anapaswa kushiriki” akasema
Akiki na Mutombo akamtazama
kwa macho makali
“Mheshimiwa Rais hilo ni
jambo lisilowezekana.James
Kasai hawezi kushirikiana
nasi!”
“Baada ya kumuondoa
Patrice Eyenga James Kasai
anatakiwa apate nafasi ndani ya
serikali mpya itakayoundwa
tena nafasi ya juu ya
uongozi.Hilo ni jambo moja
ambalo lazima
tukubaliane”akasema Jenerali
Akiki na kumfanya Jenerali
Mutombo kuangua kicheko
kikubwa halafu akasimama
“Ahsante mheshimiwa rais
kwa kunipotezea muda
wangu.Nahitaji kurejea Congo”
akasema Mutombo
“Jenerali Mutombo kaa
chini tafadhali tuendelee na
mazungumzo ! akasema Rais
Akiki
“Ahsante kwa mvinyo safi
mheshimiwa rais” akasema
Jenerali Mutombo na kuanza
kupiga hatua kuelekea
mlangoni
“Fikiria kuhusu familia
yako Jenerali Mutombo !
akasema Rais Akiki na Jenerali
Mutombo akasimama akageuka
na kumfuata Akiki
“Usijaribu kucheza na
familia yangu Jenerali
Akiki.Kabla hujafikiria yangu
hebu fikiria kwanza familia
yako uliyoipeleka mafichoni nje
ya nchi ! akasema Jenerali
Mutombo na Akiki akatabasamu
“Kaa chini tuendelee na
maongezi yetu” akasema Akiki
na Mutombo akaketi
“Tafadhali naomba iwe
mwanzo na mwisho kuihusisha
familia yangu katika jambo
hili.Ukithubutu kuigusa familia
yangu na wewe ya kwako
hakuna atakayesalimika !
akasma Paul Mutombo
“Tusifike huko Jenerali
Mutombo.Tuko hapa kujadili
jambo lenye maslahi makubwa
kwa nchi ya Congo”
“Mheshimiwa Rais
umenistua uliposema kwamba
James Kasai anatakiwa
kupatiwa nafasi ndani ya
serikali itakayoundwa baada ya
mapinduzi kufanyika”akasema
Paul
“Sikiliza Paul.Ushiriki wa
James Kasai katika suala hili ni
muhimu sana.Yeye ndiye
atakayemuua Rais Patrice
Eyenga.Jeshi la Congo
halitahusishwa katika lawama
yoyote ya kumuua Patrice
Eyenga.Mzigo wote ataubeba
James Kasai na mara tu
itakapotangazwa kwamba Rais
Patrice amefariki jeshi
litatangaza kushika nchi”
akasema Jenerali Akiki
“Mpaka hapo kidogo
ninakuelewana na mpango huo
ni mzuri lakini tatizo liko hapo
kwa James Kasai.Japo tunaweza
kumtumia katika mpangowetu
lakini si mtumzuri kushirikiana
naye na hapaswi kupewa nafasi
ndani ya serikali kwa sababu
ndiye atajulikana na dunia
nzima kuwa amemuua Rais
Patrice.Tutakuwa ni watu wa
ajabu sana kama tutampa
madaraka mtu aliyemuua
Rais.Mtu huyu tayari
anajulikana ni gaidi na kwa
namna yoyote ile hapaswi
kushika nafasi yoyote ya
madaraka” akasema Jenerali
Mutombo na kumtazama Rais
Akiki
“Fikiria wewe mwenyewe
mheshimiwa Rais jambo
hili.Tutachekwa na hata ndege
wa angani kumpa James
madaraka yoyote ndani ya
serikali mtu ambaye dunia
nzima inamjua ni gaidi na
amekwisha fanya ukatili
mkubwa sana”
“Unalolisema Jenerali
Mutombo ni jambo la
kweli.James Kasai ameharibu
sana kushirikiana na magaidi
wa IS.Juhudi zote alizozifanya
kwa miaka mingi kupambana
kwa maslahi ya Congo
zimeharibiwa na kitendo chake
cha kujiunga na magaidi wa
IS.Hata hivyo tunamuhitaji
katika mpango huu na kama
akishirikiana nasi hatuwezi
kumuacha hivi hivi lazima naye
afaidike na mapinduzi hayo”
akasema Jenerali Akiki
“Mheshimiwa Rais nashauri
kila mmoja akatafakari zaidi
jambo hili na tuwe tena na
kikao kingine ambacho kitatupa
mwangaza zaidi.Umekuwa ni
mwanzo mzuri.Naomba
tukutane tena baada ya siku
tatu tuendelee na mjadala huu”
akasema Jenerali Mutombo
“Sawa Jenerali Mutombo
nakubaliana nawe Tukutane
tena baada ya muda
huo.Tafadhali tujitahidi
kulitafakari kwa kina suala hili
ili tutakapokutana tuweze
kuzungumza lugha moja halafu
tuanze mchakato rasmi”
akasema Jenerali Akiki na
kuagana na Jenerali Mutombo
akaondoka
“Jenerali Mutombo yuko
sahihi kuhusu James Kasai.Ni
ukweli ulio wazi aliharibu sana
harakati zake pale alipojiunga
na kikundi cha kigaidi cha
IS.Sifa yake ilibadilika kutoka
mpambanaji hadi
gaidi.Haitawezekana kumpa
madaraka ndani ya serikali pale
yatakapofanyika
mapinduzi.Nitazungumza naye
na kumfahamisha kwamba
suala la urais halitawezekana
tena” akawaza Jenerali Akiki
- MELANIE DAVIS
AMEANZA MIPANGO YA
KUMUUA RAIS PATRICE
EYENGA KATIKA
HARAKATI ZAKE ZA
KULIPA KISASI KWA
WALE WALIOUA WAZAZI
WAKE JE MPANGO HUU
UTAFANIKIWA?
- RUBY TAYARI
AMEWASILI DAR ES
SALAAM SALAMA KWA
AJILI YA KUONGOZA
IDARA YA SIRI YA
USALAMA WA NDANI
WA NCHI KAMA
ALIVYOOMBWA NA RAIS
- MATHEW MULUMBI
YUKO NJIANI AKIELEKEA
TANZANIA KATIKA
MISHENI YA KUMUUA
JAMES KASAI JE
ATAFANIKIWA?
- MPENZI MSOMAJI
USIKOSE SEHEMU IJAYO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom