Riwaya: Siri

Riwaya: Siri

Ila Tafadhal tuongezee idadi za episode....Umeahid mbili umetupia moja dyuuu kwel haya ni Mateso bila Chuki
 
SIRI

Episode 25
Mtunzi Patrick CK

kilichokuwa na vifaa mbali
mbali.Ndani ya chumba kile
kulikuwa na mlango mwingine
akaingiza namba ukafunguka
akaingia katika chumba
ambacho kulikuwa na lifti
akaingia na kuelekea chini
akashuka na kuelekeza jicho
lake katika mlango uliokuwa
mbele yake ukafunguka
akaingia ndani ya chumba
kikubwa cha maabara.Kabla ya
kuingia katika maabara
akaingia katika kichumba
kidogo akavaa mavazi maalum
halafu akaanza kazi. **************
Saa moja za jioni Dr Olivia
akatoka ofisini kwake akaingia
garini na kuondoka.Alihisi
uchovu alikuwa amefanya kazi
kwa muda wa siku nzima
“Mwili umechoka natamani
nifike nyumbani haraka
nikapumzike.Zoezi limekwenda
vyema na ninatumai kesho
kupata majibu.Akili yangu
itatulia baada ya kupata majibu
ya kipimo kile na baada ya hapo
nitajua nini kitaendelea”
akawaza Dr Olivia Alipofika nyumbani kwake
akakuta kuna gari la kifahari
limeegeshwa nje akastuka
“Gari la nani hili? Sina miadi
na mtu yeyote kuja kwangu leo
na sipendi kukaribisha wageni
nyumbani kwangu hasa
usiku”akawaza
“Yawezekana ni baba
amekuja lakini baba hii si
kawada yake.Kama angekuwa
na shida na mimi angenijulisha
tuonane na hana mazoea ya
kuja kwangu bila taarifa”
akawaza Dr Olivia akachukua
mkoba na mafaili yake akashuka garini.Mtumishi wake
wa ndani akatoka haraka kwa
ajili ya kumpokea mizigo
“Lucy hili gari la
nani?Nimekwisha wapa
maelekezo msipokee mgeni
yeyote bila ruhusa yangu kwa
nini mmekiuka maelekezo
yangu? akauliza Dr Olivia
akionekana kuwa mkali kidogo
“Samahani dada ni yule
rafiki yako aliyekurudisha jana
hapa nyumbani ndiye yuko
ndani” akajibu Lucy huku
akipokea mizigo “Rafiki yangu gani?akauliza
Dr Olivia
“Yule aliyekurudisha jana
usiku anaitwa Mathew”
“Oh my Gosh
Mathew!!akasema Dr Olivia na
kushusha pumzi
“Ndiyo dada.Alipokuja
alizuiliwa getini akaomba
niitwe nikaenda nikamueleza
kwamba haupo akasema
atakusubiri.Sikuwa na wasi
wasi naye kwa kuwa jana
ulikuwa naye nikajua ni rafiki
yako.Nilitaka nikujulishe
akasema nisifanye hivyo kwani anataka akufanyie
surprise.Samahani sana dada
sintarudia tena” akasema Lucy
na Dr Olivia akatabasamu
“Usijali Lucy huyu hana
tatizo lakini siku nyingine
usirudie kukaribisha mtu bila
ruhusa yangu.Unapaswa
kuniuliza kwanza kabla
hujafanya maamuzi yoyote”
akasema Dr Olivia na kuingia
“Hello Mr Bilionea”
akasema Dr Olivia alipoingia
sebuleni
“Hello Olivia”akasema
Mathew na kusimama wakashikana mikono Dr Olivia
akajitupa sofani
“Pole sana Olivia.Samahani
kwa kuja bila taarifa lakini jana
hatukuachana
vyema.Nilikuacha ukiwa
umelala haujitambui kwa
kinywaji na sikuwa na namba
yako ya simu ndiyo maana
nimekuja leo ili kujua
unaendeleaje.Nisamehe sana
kwa uvamizi huu” akasema
Mathew
“Usijali Mathew lakini
wakati mwingine
kufanya hivi I don’t like
suprises” akasema Dr Olivia
“It wont happen again”
akasema Mathew
“Karibu sana
Mathew.Ninashukuru jana
ulinifikisha nyumbani
salama.Kama ningeendesha gari
mwenyewe nisingefika salama”
akasema Dr Olivia
“Niliona hali uliyokuwa
nayo ndiyo maana nikaamua
kukuleta nyumbani.Olivia
ninashukuru nimekuona na
kuhakikisha uko salama sasa
ninaweza kuondoka” “Acha kunitania
Mathew.Yaani umepoteza muda
wako wote kunisubiri halafu
nimefika tu unaondoka?
Umekuja kwangu wewe ni
mgeni wangu.Tupate chakula na
maongezi kisha utakwenda
kwako.Unakimbilia wapi wakati
mkeo hayupo ?Au una miadi na
mwanamke leo?akauliza Dr
Olivia
“Hapana sina miadi na mtu
yeyote.Ninakuona umechoka
sana ninataka kukupa nafasi ya
kupumzika” “Hayo ni mawazo yako
mimi sijasema kama
nimechoka.Wait for me
ninakuja baada ya muda mfupi”
akasema Dr Olivia na kupanda
chumbani kwake akaingia
bafuni kuoga na kisha oga
akachukua kompyuta yake na
kumpigia simu Habiba
Jawad.Mawasiliano yao
yamekuwa ni katika mtandao
“Olivia” akasema Habiba
Jawad baada ya kupokea simu
“Madam Habiba habari za
huko? “Tunaendelea vyema vipi
wewe unaendeleaje?
“Ninaendelea vyema
pia.Madam nimekupigia
kukujulisha kwamba jana
nimefika salama na usiku wa
jana nikaanza kazi.Nilifanikiwa
kupata baadhi ya sampuli
kutoka katika kaburi lile la
Edger”
“Wow ! kazi nzuri sana
Olivia.Wepesi wako
umenishangaza sana” akasema
Habiba
“Usijali madam” “Nini kinaendelea baada ya
kuzipata sampuli hizo? Lini
tutegemee majibu ya vipimo?
“Tutegemee kesho
madam.Maabara ile ina uwezo
mkubwa sana na inaweza kutoa
majibu ya vipimo vya vinasaba
kwa siku moja hadi mbili hivyo
tutegemee kesho kupata
majibu”
“Olivia sijui niseme
nini.Nina furaha kubwa na vile
vile nina hofu” akasema Habiba
“Madam habiba sote tuna
hofu kubwa kwani majibu
yatakayopatikana yatatupa picha kamili kuhusu Edger
kama kweli ni mzima au
amefariki dunia” akasema Dr
Olivia
“Dr Olivia tafadhali naomba
uhakikishe kipimo hicho
kimefanyika kwa uhakika
mkubwa sana kwani lengo hasa
la kujenga kituo hicho ni kwa
ajili ya kufanya uchunguzi huo
kwa hiyo kesho ndipo tutajua
kama uamuzi wa ujenzi wa
kituo hicho ulikuwa wa
manufaa” akasema Dr Olivia
“Usihofu Madam
Habiba.Niko makini sana na suala hili na majibu
yatakayopatikana yatakuwa na
uhakika.NImeshughulikia suala
hili mimi mwenyewe” akasema
Dr Olivia
“Ahsante sana Olivia.Mimi
na familia yangu tunasubiri
majibu kutoka kwako kwa
hamu kubwa ili tujue nini
kifuate” akasema Habiba
“Tuombe Mungu majibu
yawe mazuri” akasema Dr
Olivia
“Olivia kila la heri vile vile
endelea kuwa makini sana hasa
kwa wakati huu.Usimuamini mtu yeyote yule.Majibu
yatakapotoka kesho tutaangalia
namna ya kufanya ili uwe na
ulinzi.Tafadhali tuwasiliane
tena kesho” akasema Habiba na
kukata simu.Dr Olivia
akashusha pumzi
“Olivia ..Olivia..Olivia..!!
akasema Dr Olivia akiwa
ameweka mikono kichwani.
“Olivia ninakwenda
kupotea hivi hivi nikiona.Kwa
nini lakini nimekubali kufanya
kazi na hawa watu ?akajiuliza
“I’m not with them.I’m
doing this for Edger! Majibu yakipatikana mimi na wao
hatutakuwa na mahusiano tena
na ikiwezekana hata kituo chao
nitawaachia”akawaza na
kuingiwa na woga
“Nikienda kinyume na
matakwa yao wataniua na
familia yangu.Nifanye
nini?akajiuliza
“I’m confused.Nashukuru
Mathew amekuja atanisaidia
kuyaondoa mawazo haya na
kukiweka sawa kichwa changu”
akasema Dr Olivia na kushuka
sebuleni. “Samahani kwa kukuweka
muda mrefu Mathew ”akasema
Olivia
“Usijali Olivia” akajibu
Mathew
“Mathew nakushukuru
umekuja.I real needed someone
to talk to.The house is big and
boring,ninapotoka kazini
nimechoka ninakosa mtu wa
kuongea naye ndiyo maana
ninaamua kwenda klabu
kupoteza mawazo” akasema Dr
Olivia na Mathew akatabasamu
“Tupate chakula kwanza I
feel hungry !! akasema Dr Olivia na kumuongoza Mathew katika
chumba cha chakula.
Baada ya kupata chakula
wakaelekea katika chumba
maalum cha
kupumzikia.Kulikuwa na sofa
nzuri sana na luninga kubwa
ukutani.Katika ukuta mwingine
kulikuwa na kioo kikubwa
ambaco ndanoi yake maji
yalikuwa yanamwagika na
kutoa sauti nzuri huku muziki
wa ala ukisikika kwa
mbali.Kilikuwa ni chumba cha
kipekee kabisa “Ninapotaka kupumzika
huwa ninakuja humu”akasema
Dr OIivia na kumkaribisha
Mathew halafu akafungua
kabati na kutoa chupa zaidi ya
nane za whisky.
“Mathew let’s have some
fun.Hakuna haja ya kwenda
klabu tunaweza kufurahi hata
hapa nyumbani.Kwa ufupi jana
nilifurahi sana kupata kampani
yako.Wewe ni mtu ambaye kila
mtu angependa kutoka
naye.Unajua namna ya
kumfanya mtu afurahi na
asijihisi mpweke.Mathew mkeo ana bahati sana.U wa kipekee
mno” akasema Dr Olivia
“Olivia nashukuru.Kitu
ulichokihisi kwangu nami
ndicho nilichokihisi
kwako.Nilifurahi sana kuwa
nawe jana.Nilikuwa nimeboreka
na nilitaka kuondoka lakini
baada ya kukutana nawe
nilijikuta nikitamani kuendelea
kuwa nawe hadi tukajikuta
tukikaribia kufika
asubuhi”akasema Mathew na
wote wakaangua kicheko
“Let’s have fun Mathew”
akasema Dr Olivia wakaanza kupata kinywaji.Uwepo wa
Mathew ulimpa faraja kubwa
sana Dr Olivia.Walizungumza
mambo mengi na Dr Olivia
alionekana kuzidiwa kwa
kinywaji akainuka na kumfuata
Mathew sofani.
“Mathew why are you
here?akauliza Dr Olivia.Mathew
akatabasamu akamtazama na
kusema
“Nadhani nilikueleza
kwamba nilikuja hapa kwa ajili
kujua maendeleo yako kwani
jana nilikuacha katika hali
ambayo haikuwa nzuri” “Are you sure Mathew?
“Olivia mbona una wasi
wasi na mimi?Nimefanya vibaya
kuja kukujulia hali?akauliza
Mathew
“Hapana Mathew hujafanya
vibaya.Ninataka kujua hasa nini
kimekuleta kwangu hadi
ukaamua kunisubiri? Akauliza
tena Olivia
“Olivia tayari umezidiwa na
kinywaji nadhani ni wakati wa
mimi kuondoka nikuache
ukapumzike” akasema Mathew
“C’mon Mathew you came
here to have fun so let’s have fun” akasema Olivia akimshika
mkono Mathew
“Usihofu leo tuko nyumbani
hata kama ukizidiwa na kilevi
basi utalala hapa hadi
asubuhi.Mathew samahani
kama swali nililokuuliza
limekukera lakini ninataka
niufahamu ukweli.Kama hauko
tayari kunieleza ukweli ngoja
mimi nikueleze ukweli”
akasema Dr Olivia na kunywa
funda moja la kinywaji
“I saw the way you were
looking at me yesterday.I see
love in your eyes.You like me”akasema Dr Olivia na
kumsogelea zaidi Mathew
“Mathew mimi nina tatizo
moja nalo ni kusema
ukweli.Hata kama unakwepa
kunieleza ukweli lakini
ninakuona
machoni,ninaitazama midomo
yako you like me.You came here
for me.You need me”akasema
Dr Olivia
“Olivia nimekuja hapa
kuk……”akasema Mathew
lakinbi Dr Olivia akamzuia
“Tatizo la wanaume wengi
hamtaki kuwa wazi hata pale mnapoelezwa ukweli.Mathew
ulichokifanya si kitu kibaya
kwani hata mimi nilijiuliza sana
ni namna gani ningeweza
kukupata tena.Ninafurahi kuwa
karibu yako.Ninajihisi furaha na
amani nikiwa karibu
yako.Natamani niwe karibu
yako muda wote.Unanifanya
nifurahi,nitabasamu.Mathew
naamini hautanielewa vibaya
kwa hiki nitakachokueleza
lakini mimi na wewe nataka
tujuane zaidi nataka tuwe
karibu zaidi and for tonight I’m
going to …” Dr Olivia hakumalizia sentensi yake
mikono yenye nguvu ya
Mathew ikamvuta na
kumkumbatia kwa nguvu
akaanza kumporomoshea
mabusu mfululizo.Dr Olivia
naye akajibu kwa busu,taa ya
kijani ikawaka na safari
ikaanzia hapo.Chumba cha
mapumziko kiligeuka sayari ya
mahaba.Walihama kutoka sofa
moja hadi lingine.
“Mathew this is not the
right place.Twende chumbani
kwangu” akasema Dr Olivia
wakatoka mle katika chumba cha mapumziko wakapanda
ghorofani chumbani kwa Dr
Olivia.Wote wawili mahaba
yalikwisha wazidi hivyo
walipofika tu chumbani
hakukuwa na maongezi Mathew
akamshika Dr Olivia na
kumuangusha kitandani
ukaanza mtanange wa kukata
na shoka
“Mathew thank you so
much.I needed this.It’s been a
while” akasema Dr Olivia na
Mathew
akatabasamu.Walimaliza
mzunguko mmoja “Ahsante pia nawe.Naomba
nikiri kwamba ni kweli
nilikufuata hapa nyumbani na
na kilichonileta hapa ni
hiki.Olivia nilipokuona jana
ulinisisimua sana.Nilivutiwa
sana nawe na ninaomba tuwe
na ukaribu mkubwa zaidi”
akasema Mathew
“Nilikuona toka jana
nikayasoma mawazo yako na
nilipokuona hapa leo
sikushangaa nilijua
kilichokuleta na mimi nilikuwa
nakihitaji sana.Mathew naomba
tafadhali usinifikirie vibaya kwa sababu imekuwa rahisi mno
kwangu kujiachia kwako na
sijui imenitokeaje.Mimi ni
mwanamke mgumu sana na
ndiyo maana mpaka leo hii
sijabahatika kuwa na rafiki wa
kiume lakini wewe tumekutana
jana tu na leo hii nipo juu ya
kifua chako.Imenitokea hivyo
na nisingejitendea haki kama
ningekuacha
ukaondoka.Ningejilaumu sana
Mathew” akasema Dr
Olivia.Mathew akaupeleka
mkono katika nywele laini za Dr
Olivia akazichezea na kusema “Olivia katu siwezi
nikakuchukulia rahisi
rahisi.Nitakuheshimu sana na
urafiki wetu nitaupa thamani
kubwa,na ningependa urafiki
wetu uendelee zaidi na zaidi
japokuwa nina familia lakini
haiwezi kuwa kigezo cha
kukuumiza wewe”
“Mathew ninakuhitaji sana
hasa kwa wakati huu.Naomba
usimame na mimi.Ninahitaji
mno mtu wa kunishika mkono
naomba uwe karibu nami japo
kwa muda huu ambao
utakuwepo hapa Dar es salaam.Nimejikuta nikipata
nguvu mpya na tumaini toka
jana nilipokutana
nawe.Sifahamu kwa nini
ninajishi namna hii yawezekana
Mathew kuna kizizi unakitumia”
akasema Dr Olivia na wote
wakaangua kicheko.
“Natania Mathew siamini
kabisa katika mambo hayo
japokuwa wapo
wanaoamini”akasema Dr Olivia
“Dr Olivia nadhani ni
wakati wangu wa kuondoka
nikuache upumzike” “Hapana Mathew leo utalala
hapa hapa utaondoka
asubuhi.You are single and I’m
single shida iko wapi?Kuwa na
amani hapa ni sehemu salama
kabisa.Nakuhitaji usiku wa leo
Mathew.Please stay” akasema
Dr Olivia.Mathew akamtazama
machoni na kusema
“Uko sahihi Olivia.Sina
sababu ya kukimbia kwani niko
peke yangu.Tuufanye usiku
wetu uwe wa kipekee” akasema
Mathew
“Thank you Mathew.Thank
you so much.We need champagne to celebrate our
new beginning ” akasema Dr
Olivia na kuvaa nguo akatoka
mle chumbani akaenda
kuchukua vinywaji.
****************
Saa kumi na mbili za
asubuhi Mathew aliamka
akaoga na kuagana na Dr Olivia
akaondoka zake.
“Ninaapa sijawahi kuwa na
usiku mzuri kama jana.Mathew
ni mwanaume wa pekee
kabisa.Sifahamu imenitokeaje lakini kwake nimejikuta nikiwa
mrahisi mno lakini sijakosea
kwani ananisaidia sana kupita
katika kipindi hiki kigumu
ninachopitia.Nikiwa naye
ninakuwa na amani sana na
tabasamu usoni lakini nikiwa
peke yangu ninajiona kama vile
ninaelekea kwenye kitanzi cha
kuninyonga” akawaza Dr Olivia
baada ya Mathew kuondoka
“Ngoja nimuweke kando
Mathew nijielekeze katika
jukumu kubwa nililo nalo.Siku
ya leo ni siku ya kipekee kabisa
kwani ukweli unakwenda
kujulikana kama Edger kaka
alikufa katika ile ajali au bado
mzima.I’m so scared” akawaza
Dr Olivia akakaa kitandani
akionekana kuwa na mawazo
mengi.Akainuka na kuendelea
kujiandaa.
Alifika ofisini kwake saa
nne za asubuhi na kabla ya
kufanya shughuli yoyote
alijiegemeza kitini
“Ninaogopa kuufahamu
ukweli.Nina wasi wasi maisha
yangu yanaweza yakabadilika
kuanzia siku ya leo.Hii ni siku ngumu sana kwangu” akawaza
Dr Olivia
Alikaa kitini kwa zaidi ya
dakika kumi akiwaza halafu
akainuka
“Sipaswi kuogopa.Natakiwa
kuufahamu ukweli” akasema Dr
Olivia na kuvaa koti lake jeupe
akaelekea katika maabara
maalum
Ilipofika saa kumi na moja
jioni Dr Olivia tayari alikuwa na
majibu.Mwili ulimtetemeka
baada ya majibu kuonyesha
kwamba mwili ule haukuwa wa
Edger.Machozi yakamtoka “He’s alive..!He’s not dead !
akasema Dr Olivia.Alikuwa peke
yake ndani ya maabara ile
kubwa.
“Haya mambo nimekuwa
nikiyaona katika filamu na
sikujua kama siku moja
nitayashuhudia kwa maco
yangu.Kila mtu anajua kwamba
Edger amekufa.Oh my God
where is he?akajiuliza
Ni wazi Dr Olivia alikuwa
katika wakati mgumu sana
baada ya kupata majibu yale.
“Habiba alikuwa sahihi
kuamini Edger hajafa.Naniwaliofanya mchezo
ule na kwa nini?Naamini
waliofanya mchezo ule ni watu
wataalamu mno kwani
walifanikiwa kumuaminisha
kila mtu kwamba Edger
amefariki.Kama Habiba
asingeingiwa na shaka ukweli
usingeweza kujulikana lakini
sasa ukweli umejulikana Edger
hajafa na kinachofuata ni
kutafuta mahala alipo” Akawaza
Dr Olivia akatoka mle maabara
akarejea ofisinikwake na
kumpigia simu Habiba Jawad
kupitia kompyuta yake “Dr Olivia naamini simu hii
ina habari njema” akasema
Habiba
“Madam Habiba tayari
ninayo majibu hapa” akasema
Dr Olivia na Habiba Jawad
akavuta pumzi ndefu
“Nimesubiri kwa muda
mrefu kuufahamu ukweli lakini
sasa majibu yamepatikana
ninapata hofu kuyapokea”
akasema Habiba
“Usiogope Madam
Habiba.Kuwa jasiri na uyapokee
majibu” akasema Dr Olivia “Haya nipe majibu Olivia”
akasema Habiba na kufumba
macho.
“Madam niliingia mimi
mwenyewe katika kaburi lile la
Edger na kuchukua sampuli za
mabaki nilizozihitaji na
nimefanya kipimo mimi
mwenyewe kwa usahihi
mkubwa na majibu yaliyotoka
ni …..” akasita kidogo
“Nieleze Olivia unazidi
kuniweka roho juu”akasema
habiba
“Majibu yanaonyesha
kwamba mwili uliozikwa katika lile kaburi si mwili wa Edger ”
akasema Dr Olivia na Habiba
akafunika uso kwa viganja
vyake vya mikono.Akakaa
kimya kwa dakika mbili na
alipotoa viganja vile uso wake
ulikuwa umeloa machozi.
“Ahsante
Mungu.Nimesubiri kwa muda
mrefu sana kuupata ukweli
huu.Imenigharimu muda na
fedha nyingi kuufahamu
ukwelikwamba mwanangu Seif
hajafa bali yuko hai.Olivia sijui
nikushukuruje kwa jambo hili
kubwa ulilolifanya” akasema Habiba akiendelea kumwaga
machozi ya furaha.
“Madam Habiba baada ya
kuufahamu ukweli kwamba
Edger hajafa nini
kinafuata?akauliza Dr Olivia
“Kinachofuata baada ya
kuufahamu ukweli huu ni
kuanza kumtafuta kila kona ya
dunia kwani mpaka sasa bado
hatujui mahala alipo na nani
anamshikilia.Olivia
ninakushukuru mno na
ninaomba nikuache ili nikutane
na watuwangu nizifikishe
taarifa hizi njema kabisa.Nitawasiliana nawe
baadae” akasema Habiba na
kumuaga Olivia
“Mimi mwenyewe sitaki
kuendelea kukaa hapa kichwa
changu kimevurugika
kabisa.Majibuhaya
yaliyopatikana yamezidi
kunichanganya na kuniongezea
hofu.Nani waliofanya jambo lile
la kuidanganya dunia kwamba
Edger amefariki dunia?Edger
yuko wapi?Watu hao
walifahamu kwamba Edger ni
mshirika wa IS ndiyo maana
wakamteka na kutunga kifo chake? Nitaendelea kujuta
kumfahamu Edger kwa ajili
yake nimejikuta nikiingia katika
ulimwengu wa magaidi ambao
wamenibana katika kona na
sijui nifanye nini,sijui
nimweleze nani jambo hili
ambalo linaelekea kunipa
uchizi.Ninayaona maisha yangu
yakielekea shimoni kwani
naamini ikosiku nitajulikana
kuwa ninashirikiana na
magaidi.Kila ninapowaza jambo
hili ninazidi kuchanganyikiwa”
akawaza Dr Olivia. “Ninamshukuru Mungu
ameniona na kuniletea
Mathew.Ni wakati kama huu
ninamuhitaji sana mtu kama
yule ambaye hunipa nguvu ya
kusimama.Ninahisi
amani,furaha na nguvu nikiwa
naye” akawaza Dr Olivia na
mara gari ziliposimama katika
taa za barabarani akachukua
simu akazitafuta namba za
Mathew akampigia
“Dr Olivia” akasema
Mathew
“Mathew uko wapi mida
hii?akauliza “Nimetoka kazini muda si
mrefu ninaelekea
nyumbani.Wewe uko
wapi?akauliza Mathew
“Mathew kama hutajali
tunaweza kukutana nyumbani
kwangu?akauliza Dr Olivia
“Kuna tatizo lolote Dr
Olivia?akauliza Mathew baada
ya kugundua utofauti katika
sauti ya Dr Olivia
“Ninakuhitaji Mathew”
“Usijali Olivia,ninakwenda
nyumbani kwangu kisha
nitakuja kwako,nisubiri hapo
tafadhali”akasema Mathew “Ahsante sana Mathew”
akasema Dr Olivia na kukata
simu
“I real need someone like
Mathew today.Nahitajimtu wa
kunipa nguvu kwa sababu
mambo yanayonikabili ni
mazito” akawaza Dr Olivia
Alifika nyumbani kwake na
kujilaza kitandani kichwa
kilikuwa kizito
“Nimeingia kwenye
ulimwengu wa magaidi na sijui
namna ya
kutoka.Nimeikamilisha kazi yao
na sitaki kuendelea kushirikiana nao tena hawa
jamaa lazima nitafute namna ya
kuwakwepa.Hata hivyo duniahii
ina maajabu sana.Mwili ule
ambao watu wote tuliamini
ulikuwa wa Edger ni wa nani?
Haya aya mambo ni magumu
sana na sitakikuendelea
kuumiza kichwa changu zaidi”
akawaza Dr Olivia na kuingia
bafuni kuoga kisha akajilaza
kitandani akimsubiri Mathew.
Saa moja na nusu Mathew
akafika nyumbani kwa Dr Olivia
ambaye alifurahi sana kumuona
akamkumbatia kwa nguvu “Mathew nimefurahi sana
umekuja.Kila nikuonapo
ninapata nguvu” akasema Dr
Olivia na kumuongoza Mathew
wakaenda kukaa nje sehemu
maalum ya kupumzikia,Olivia
akaleta chupa kadhaa za
mvinyo
“Olivia toka tumefahamiana
juzi umekuwa unatumia sana
kinywaji.Inaonekana kuna
jambo linakusumbua na
unataka kuliondoa kichwani
kwako kwa kutumia
kilevi.Unaweza ukanieleza una
tatizo gani Olivia?You can trust me,Im here for you” akasema
Mathew
“Sina tatizo lolote Mathew
nahitaji tu
kufurahi.Ninaonekana kama
nina tatizo
linanisumbua?akauliza Dr
Olivia
“Ninajua kumsoma mtu
hasa ambaye ana jambo
linamsumbua na japokuwa
hutaki kuniweka wazi lakini
naamini kwamba
unalotatizo.Nataka nikuelekeze
kitu Dr Olivia,siku zote kama
una tatizo usilitatue kwa
kunywa pombe.Njia hiyo
kamwe haitakusaidia kutatua
tatizo lako.Sikulazimishi
unieleze tatizo lako kwanini
muda mfupi tu umepita toka
tumefahamiana lakini kama
hutajali unaweza ukaniamini na
kunieleza kinachokusumbua”
akasema Mathew.
“Mathew hayoni mawazo
yako,sina tatizo lolote
linalonisumbua” akasema Dr
Olivia huku akichukua chupa ya
mvinyo na kutaka kuimimina
katika glasi Mathew akamzuia “Olivia hakuna kutumia
mvinyo leo.Today let’s have fun
without alcohol.Kamauna tatizo
tulitatue bila kutumia kilevi
chochote” akasema Mathew
“Mathew sina tatizo lolote
linanisumbua.Tutumie mvinyo
tafadhali”akasema Dr Olivia
“Hapana Olivia.Leo hakuna
kutumia mvinyo.Si mazoea
mazuri kutumia mvinyo kila
siku.Tuzungumze na kama
kunakitu ambacho kinatufanya
tufurahi basi tufanye lakini si
kugeuza mvinyo sehemu ya
maisha yetu” “C’mon Mathew siwezi
kuwa kawaida kama sintatumia
hata mvinyo kidogo” akasema
Dr Olivia
“Hap…………” Mathew
akanyamaza baada ya simu ya
Dr Olivia kuita.Akatazama
mpigaji na sura yake
ikabadilika.
“Is there any problem
Olivia?akauliza Mathew
“Mathew I have to take this
call” akasema Dr Oliviana
kuelekea ndani.
“Hallow madam Habiba”
akasema Dr Olivia baada ya kuipokea simu ile ambayo
ilipigwa kupitia mtandao wa
skype.
“Dr Olivia nimefikisha
majibu yale kwa wenzangu na
wote wamefurahi sana kwamba
zile hisia zetu kuhusu Edger
kuwa hai ni sahihi
kabisa.Kinachofuata sasa ni
hatua ya tatu ambayo ni
kumtafuta Edger yuko
wapi.Katika hatua hii ya tatu
utakuwa ukiwasiliana na Sayid
Omar yeye ndiye
niliyemkabidhi jukumu lote la
kuhakikisha Edger anajulikana yuko wapi na anapatikana kwa
gharama zozote zile.Olivia
ninakushukuru sanakwa jambo
kubwa ulilolifanya la kuamua
kushirikiana nasi naomba
uendelee kuwa nasi na
ninakuahidi kwamba lazima
Edger atapatikana kwa gharama
zozote.Ninachokusisitiza Olivia
ni usiri.Endelea kuitunza siri
uliyoifahamu hata kama
itakulazimu kuhatarisha maisha
yako lakini siri uliyoifahamu
katu usifumbue mdomo na
kumweleza mtu yeyote”
akasema Habiba “Madam Habiba
tumekwisha wekamakubaliano
na ninaomba makubaliano yetu
muyazingatie na mara tu baada
ya Edger kupatikana utakuwa ni
mwisho wetu mtaniacha
niendelee na maisha yangu”
“Usiogope tutalizingata hilo
Olivia.Mimi ni mtu
ninayeheshimu sana
makubaliano.Naomba sasa
uzungumze na Sayid Omar na
atakupa maelekezo” akasema
Habiba Jawad na katika simu
akatokea mtu mmoja mwenye
kipara na miwani “Hallow Olivia.Naitwa sayid
Omar na kama alivyokuelekeza
Habiba katika awamuhii ya tatu
utakuwa na mimi.Katika awamu
ya kwanza ulikuwa na Abu
dahir,awamu ya pili ukawa na
Habiba na sasa ni awamu ya
tatu ambayo utakuwa na
mimi.Awamu hii imegawanyika
katika sehemu mbili.Sehemu ya
kwanza ni kufahamu nani
waliomchukua Edger na yuko
wapi.Sehemu ya pili itakua ni
kumchukua mahala
alipo.Mpaka sasa hatuna
uhakika ni nani waliofanya mchezo ule na kumchukua
Edger.Nipe muda hadi kesho
asubuhi kwa saa za kwenu
Tanzania nitakupigia simu na
kukueleza ni wapi tunahisi yupo
Edger” akasema Sayid Omar na
kuagana na Dr Olivia ambaye
alihisi miguu inamuisha nguvu
akakaa kitandani
“Ee Mungu kwa nini
umeniacha nikaingia katika
mtihani huu? Nimeingia katika
himaya ya magaidi,himaya ya
watu makatili,wauaji na sioni
mlango wa kutokea.Nionyeshe
njia ee Mungu niweze kujitoa katika mikono ya watu hawa”
akaomba Dr Olivia akilengwa na
machozi
“Kama watafanikiwa
kumpata Edger utakuwa ni
mwisho wa mahusiano yangu
naye.Sitaki kuwa na ukaribu
wowote na hawa magaidi”
akawaza Dr Olivia na
kukumbuka kwamba alimuacha
Mathew peke yake akatoka na
kurejea mahala alipokuwa
Mathew
“Mathew tafadhali naomba
uniruhusu ninywe glasi hata
moja tu ya mvinyo ili kichwa
changu kikae sawa.Bila kupata
mvinyo nahisi kichwa changu
kitapasuka” akasema Dr
Olivia.Mathew akamtazama na
kuchukua chupa akamimina
mvinyo katika glasi.Olivia
akaishika glasi ile na kunywa
pombe yote iliyokuwemo.
“Oh my God !! akasema Dr
Olivia
“Olivia nieleze tatizo lako
tafadhali.You can trust me”
akasema Mathew.Dr Olivia
akainamisha kichwa akazama
mawazoni “Olivia mimi ni rafiki yako
na kama tumeamua kuwa
marafiki hakuna haja ya
kufichana kama una jambo
kubwa nieleze tafadhali
yawezekana nikawa na msaada
kwa tatizo lako” akasema
Mathew.
“Hata kama nikikueleza
Mathew hautaweza
kunielewa”akasema Dr Olivia
“Usiogope Olivia nieleze
nitakuelewa” akasema Mathew
“Nina tatizo kubwa sana
Mathew na ninahitaji msaada wa Mungu pekee kulitatua”
akasema Dr Olivia
“Olivia pole sana kwa tatizo
ulilonalo lakini bado naendelea
kukusisitiza unieleze tatizo lako
kwani yawezekana Mungu
amenituma kwako ili niwe
msaada wa tatizo ulilo
nalo.Usiogope Olivia hata kama
tatizo ni kubwa kiasi gani
nieleze na mimi nitakuelewa”
akasema Mathew.Dr Olivia
akafikiri kidogo na kusema
“Hapana Mathew siwezi
kukueleza.Tatizo nililo nalo nitalikabili mimi mwenyewe na
kulimaliza”akasema Dr Olivia
“Olivia kuna maana gani ya
kuwa marafiki kama hatuwezi
kushirikishana matatizo
tunayopitia?Urafiki maana yake
ni kushirikishana kila tatizo na
kusaidiana.Kama rafiki yako
niko tayari kukusaidia katika
matatizo yote uliyonayo”
akasema Mathew
“Mathew sitaki kukuingiza
katika matatizo.Nitakabiliana
nao mimi mwenyewe” akasema
Dr Olivia “Utakabiliana na akina
nani? Are you in trouble with
some people? akauliza Mathew
“Mathew umenichanganya
hadi nimejikuta nikitamka kitu
ambacho sikupaswa
kukitamka”akasema Dr Olivia
“Niambie ukweli Olivia uko
katika matatizo na watu gani?
Dr Olivia akainamisha
kichwa akafikiri halafu akasema
“Mathew sipendi
kukushirikisha katika tatizo
langu lakini kwa kuwa
umesisitiza nitakueleza kwa ufupi tu.Ni kweli nina tatizo na
watu Fulani”
“Matatizo gani? Ni akina
nani?Mathew akauliza
“Usihofu Mathew ni jambo
ambalo ninaweza kulimaliza na
ninajitahidi kulimaliza.Endapo
nikishindwa kulitatua na
kuhitaji msaada
nitakujulisha.Naomba nisiingie
kwa ndani zaidi” akasema Dr
Olivia
“Nimekuelewa Dr Olivia na
ninakuomba kama ulivyoahidi
kwamba endapo utashindwa kutatua tatizo lako mimi niko
hapa tayari kukusaidia”
“Ahsante
Mathew.Nikishindwa
nitakutafuta” akasema Dr Olivia
“Olivia umeahdi kunitafuta
pale utakapohitaji msaada
wangu lakini mimi ninapenda
kukupa msaada mdogo sana”
“Msaada upi Mathew?
“Nitakupa namba ambazo
unatakiwa uziweke kichwani na
utazitumia pale tu unapokuwa
matatizoni.Ukipiga namba hizo
zitaniwezesha mimi kujua pale
unapokuwa na matatizo.Narudia tena kukupa
angalizo kwamba namba hizi si
za kutumia hovyo hadi pale
utakapokuwa umepata
matatizo.Namba hizo ni kirusi
ambacho kinaweza kuchota
taarifa kwa haraka na
kunijulisha mahala ulipo na
mimi nikatafuta msaada namna
ya kukusaoid” akasema Mathew
“Umewahi kusomea mambo
haya ya teknolojia?Kirusi hicho
kinakusaidia nini
Mathew?akauliza Dr Olivia
“Nina utaalamu kidogo wa
haya masuala.Kirusi hiki
kinanisaidia kwa familia yangu
kujua kama wako katika
hatari.Kuna wakati mwanangu
mmoja aliwahi kutekwa ndipo
nilipoamua kutumia njia hii
kujua kama wako kwenye
matatizo”akasema Mathew na
kumtajia Dr Olivia namba zile
akazihifadhi kisha wakaendelea
na maongezi mengine.walipata
chakula cha usiku na ilipofika
saa tano Mathew akaaga ili
aondoke lakini Dr Olivia akawa
na ombi
“Mathew naomba
usinichoke tafadhali.Ninaomba na usiku wa leo uupitishe hapa
kwangu.Ninakuhitaji sana
Mathew” akasema Dr
Olivia.Haikuwa rahisi kwa
Mathew kukataa.
 
SIRI
Episode 26
Mtunzi. Patrick CK

Dr Olivia Themba
aliyaelekza macho yake katika
saa kubwa ya ukutani
akiangalia namna mishale
inavyopishana.Ilikaribia saa
mbili za asubuhi muda ambao
Sayid Omar aliahidi kumpigia
simu kumpa taarifa zakuhusiana na mahala alipo
Edger kaka na mipango ya
kumchomoa kutoka mahala
anaposhikiliwa.
“Nilitamani sana kujua
ukweli kuhusu Edger Kaka
lakini sasa baada ya kuufahamu
ukweli nimeingiwa na hofu
kub..” Olivia akatolewa
mawazoni baada ya simu kuita
katika kompyuta yake.Mpigaji
alikuwa ni Sayid
Omar.Akashusha pumzi na
kuipokea
“Hallo Sayid” “Habari za asubuhi Dr
Olivia”
“Habari nzuri kabisa Sayid”
akajibu Dr Olivia
“Dr Olivia nimekupigia
kama
nilivyokuahidi.Tumejitahidi
sana kuchunguza lakini mpaka
sasa bado hatujui Edger yuko
wapi na nani anamshikilia,lakini
uchunguzi wetu kuna viashiria
kwamba yawezekana Edger
akawepo nchini
Tanzania.Tunahisi hivyo
kutokana na mpango ule wa
kumteka namna ulivyoratibiwa.Isingewezekana
kufanyika jambo kama lile bila
serikali kuwa na
taarifa.Ukilitazama tukio lile
kwa undani zaidi utaona
kwamba lazima serikali ya
Tanzania wana mkono
wake.Tunahisi kwamba Mossad
waliwapa taarifa serikali ya
Tanzania na wakaratibu
mpango ule kwa pamoja hivyo
sehemu ya kuanza kumtafuta
Edger na kufahamu mahala
alipo ni Tanzania” akasema “Sayid mna uhakika
kwamba Edger yuko hapa
Tanzania?akauliza Dr Olivia
“Hatuna uhakika mkubwa
lakini tunahisi hivyo.Tukio lile
la kutengeneza kifo chake
lilitengenezwa kitaalamu sana
na tunaamini lazima serikali ya
Tanzania ilishirikiana na Israel
hivyo Tanzania ni sehemu nzuri
kuanzia uchunguzi wa kujua
mahala Edger alipo.Kuna
uwezekano mkubwa akawepo
hapo hapo nchini amefungwa
mahala Fulani akihojiwa.Zoezi letu litaanzia nchini Tanzania”
akasema Sayid
“Sayid,Tanzania ni
kubwa.Mmejipanga kuanzia
wapi uchunguzi huo?akauliza
Dr Olivia
“Ili kufanikisha operesheni
kubwa kama ile lazima mkuu
wa nchi awe anafahamu kila
kitu na atoe idhini ya kufanya
kwake”
“Una maanisha rais?
akauliza Dr Olivia
“Ndiy😵peresheni kubwa
kama ile haiwezi kufanyika bila
ya rais kufahamu.Nina uhakika mkubwa kwamba rais
anafahamu kuhusu jambo hili
na anafahamu alipo Edger hivyo
basi uchunguzi wetu utaanzia
kwa rais wa jamhuri ya
muungano wa
Tanzania”akanyamaza kwa
muda halafu akaendelea
“Olivia tumegundua
kwamba rais ana mtoto wake
anayesoma katika shule moja ya
kimataifa hapo Dar es
salaam.Tunataka kumtumia
huyo ili kumlazimisha rais
atueleze kile kitu kuhusu Edger” akasema Sayid na kumstua
Olivia
“Mnataka kumtumia mtoto
wa rais?
“Ndiyo tunataka kumtumia
mtoto wa rais ili kumfanya baba
yake atusikilize na aturejeshee
au kutueleza mahala alipo
Edger”akajibu Sayid
“Sayid kabla ya kufanya
lolote nashauri muwe kwanza
na uhakika mkubwa kwamba
serikali ya Tanzania inafahamu
kuhusu suala hilo la
Edger.Mkifanya mambo bila
uchunguzi mtajikuta mkiumiza watu wengine ambao hawana
kosa lolote kama huyo mtoto
wa rais”akasema Dr Olivia
“Usiogope Dr Olivia,tayari
tunao uhakika mkubwa
kwamba serikali ya Tanzania
wanahusika katika suala hili na
lazima rais anafahamu mahala
alipo Edger na yeye ndiye
atakayetupa mwangaza wote
wa mahala alipo” akasema
Sayid na Dr Olivia akashusha
pumzi
“Mpango tulioupanga
umekaa namna hii.Kupitia kituo
chako cha utafiti utatengeneza kirusi ambacho tutakitumia
katika mpango huu.Tunataka
kirusi hicho kiwe cha aina yake
na ambacho kinaweza
kumuathiri binadamu na
kumuua.Kirusi hicho kiwe na
uwezo wa kuua kwa kuanzia
siku saba na isizidi siku kumi na
mbili.Baada ya kutengeneza
kirusi hicho utatengeneza pia
kinga yake.Tutamchoma mtoto
wa rais sindano yenye kirusi
hicho na atakapoanza kuumwa
tutamjulisha rais kwamba
mwanae amechomwa sindano
yenye kirusi hatari na hapo tutamtaka amuachie huru Edger
ili tuweze kuokoa uhai wa
mwanae.Unauonaje mpango
huo?akauliza Sayid.Dr Olivia
akabaki kimya akimtazama
Sayid kupitia kompyuta yake
“Dr Olivia” akaita Sayid
baada ya kuona Dr Olivia akiwa
kimya sana
“Sayid naomba ufahamu
jambo jambo moja”
“Jambo gani Olivia?
“Nilipokutana na Habiba
Jawad mama yake Edger na
alinieleza mambo mazito
kwamba ninyi ni washirika wa IS na hata Edger naye ni
mshirika wa mtandao
huo.Niliogopa mno na sikutaka
kuendelea kushirikiana naye
lakini aliniomba sana nimsaidie
aweze kumpata
mwanae.Nilikubali kumsaidia
kwa sharti kwamba baada ya
Edger kupatikana sintaendelea
kushirikiana nanyi tena na
kwamba Edger akipatikana
aondoke nchini Tanzania na
wala asijihusishe tena na
masuala yoyote ya
kisiasa.Nimefanya kila
lililowezekana na ukweli umebainika kwamba Edger
yuko hai kaziyangu imeishia
hapo.Jambo unaloniambia
nilifanye kwamba nitengeneze
kirusi ambacho mtakitumia
katika mpango wa kumtafuta
Edger limenishanganza na
siwezi kufanya kitu kama
hicho.Nimekwisha wasaidia
mmempata uhakika kwamba
Edger yuko hai
imetosha”akasema Dr Olivia
“Olivia sina sababu ya
kuzungumza maneno mengi
lakini kwa ufupi tu ni kwamba
wewe ni mwenzetu.Toka ulipokubali kushirikiana na Abu
dahir tayari ulikubali kuwa
mwenzetu” akasema Sayid na
Dr Olivia akamkatisha haraka
“Mimi si mwenzenu.Mimi si
IS.Mimi si gaidi !! Akasema Dr
Olivia kwa ukali
“Dr Olivia sahihi yako ipo
katika vitabu vyetu hivyo
tunakuhesabu ni mwenzetu na
huo ni ukweli ambao hauwezi
kuuepuka.Utaendelea kupokea
maagizo na maelekezo kutoka
kwetu.Wewe ni mtu muhimu
kwetu na hatutakusumbua hadi
pale tutakapokuwa na uhitaji na msaada wako na kwa sasa
tunahitaji sana msaada wako ili
tuweze kumpata Edger hivyo
andaa mipango ya kutengeneza
kirusi hicho kama
nilivyokuelekeza.Atakuja
mtaalamu mwingine wa
masuala hayo ya utengenezaji
wa virusi utashirikiana
naye.Umenielewa Dr
OIivia?akauliza Sayid Omar
“Sayid nataka kwanza
tuweke sawa jambo hili.Mimi si
mmoja wenu.Mimi si
IS.Mlinishirikisha katika
shughuli zenu bila mimi kujua hivyo msinihesabu kama
mwenzenu.Kama daktari
ninayetambua wajibu wangu
nilijitolea kuokoa maisha ya
Edger hivyo sitaki jambo jema
nililolifanya ligeuke shubiri
kwangu.Msinifanye nijutie
kitendo nilichokifanya cha
kuokoa uhai wa Edger”
akasema Dr Olivia na machozi
yakimtoka
“Dr Olivia samahani sana
kwa maneno
niliyoyatamka.Siku zote
tunakupa heshima kubwa na ya
kipekee kabisa kwani bila wewe hivi sasa Edger angekwisha
fariki.Pamoja na yote
uliyoyafanya lakini bado Edger
yuko katika hatari maisha yake
bado yako hatarini hivyo kile
ulichokifanya cha kuokoa
maisha yake bado kinaendelea
na tunahitaji sana msaada
wako.Lakini Olivia hayo yote
hayaondoi ukweli kwamba
umekwisha zifahamu siri zetu
na umekula kiapo cha
kutokufungua mdomo kusema
chochote kuhusiana na yale
uliyoyagundua hivyo wewe
tayari ni mwenzetu lakini kama nilivyokueleza tutakutumia pale
tu ambapo tutakuwa na uhitaji
na msaada wako na kama
hatuhitaji msaada wako
hatutakuwa na shida nawe
utaendelea na maisha yako
kama kawaida.Kuwa mmoja
wetu ni fursa ambayo
itakuwezesha Dr Olivia kuingia
katika ulimwengu wa watu
wazito wenye nguvu na
mabilionea.Kuna fursa nyingi
zinakuja kupitia sisi.Olivia
utakuwa mwanamke mwenye
nguvu,tajiri,na hakuna ajuaye
kwani siku moja unaweza ukashika nafasi ya juu ya
uongozi.Hupendi siku moja
kuwa rais wa kwanza
mwanamke?Hupendi siku moja
uongoze watu zaidi ya milioni
hamsini?Hutaki jina lako
kuingia katika vitabu vya
historia ya nchi na dunia?
Akauliza Sayid na Dr Olivia
akabaki kimya
“Kimya hicho kinanifanya
niamini kwamba uko
tayari.Olivia tuna mipango
mikubwa sana juu yako.Endelea
kuwa mtulivu na ufuate
maelekezo yetu tutakayokueleza na utafika
mbali sana.Ninakuhakikishia
kwamba hautajutia
kushirikiana nasi” akasema
Sayid
“Sayid suala hili linakuwa
gumu kwangu kwa sababu rais
ambaye tunataka kumtumia
mtoto wake kumshinikiza
atueleze mahala alipo Edger,ni
rafiki mkubwa wa baba yangu
na mimi ninamuita baba.Mtoto
wake Coletha ninafahamiana
naye ananiita dada.Sisi ni zaidi
ya marafiki bali tunaishi kama
ndugu hivyo sitaki kuwa sehemu ya kuitesa familia hii ya
rais” akasema Dr Olivia
“Dr Olivia sisi tunapokuwa
katika kutimiza malengo
hatuangalii kuhusu ndugu
zetu.Kama italazimu
kuwaumiza ndugu zetu ili
kufanikisha shughuli yoyote
muhimu tunafanya hivyo bila
kusita hivyo basi suala la wewe
kuwa na ukaribu na familia ya
rais halina nafasi kwetu.Mpango
wetu lazima utekelezwe.Kuna
wakati ambao lazima tufanye
maamuzi magumu” akasema
Sayid “Sayid hapana siwezi
kufanya jambo kama hilo.Siwezi
kuiumiza familia ya rais ambayo
ni sawa na familia
yangu.Coletha ni mdogo wangu
na siwezi kutengeneza kitu
ambacho kitahatarisha uhai
wake.Nashauri mtafute namna
nyingine ya kufanya kumtafuta
Edger na si kuitumia familia ya
rais kwani mkiumiza familia hii
mtakuwa mnaniumiza mimi
pia.Nawasihi mkae tena mfikirie
kwa undani namna nyingine ya
kufanya” akasema Dr Olivia “Olivia nilikueleza muda
mfupi uliopia kwamba wewe ni
mtu muhimu sana kwetu na
tuna mipango mikubwa juu
yako lakini unanishangaza kwa
namna unavyofanya jambo hili
liwe gumu.Unanifanya nitamke
kitu ambacho sikuwa nimetaka
kukisema.Nafsi yangu inaniuma
kusema hivi lakini Dr Olivia
imefika wakati ambao
itakulazimu kuchagua aidha
familia yako au familia ya rais”
akasema Sayid na kumstua Dr
Olivia “Una maanisha nini
Sayid?akauliza Dr Olivia
“Namaanisha kwamba
itakulazimu kuchagua familia
moja aidha familia yako au
familia ya rais kwani kama
hautakuwa tayari kutekeleza
mpango huu hatutakuwa na njia
nyingine zaidi ya kuishikilia
familia yako hadi pale
utakapokuwa tayari kufanya
kile ulichoelekezwa” akasema
Sayid na Dr Olivia akastuka
sana
“Sayid ninakuomba sana
familia yangu isihusishwe kwa namna yoyote na mambo
yangu.Hawafahamu chochote
kuhusiana na yale
ninayoyafanya hivyo naomba
msiwahusishe kwa namna
yoyote ile” akasema Dr Olivia
“Olivia familia yako
itaendelea kuwa salama endapo
utakuwa mvumilivu na
kutekeleza yale
tutakayokuelekeza kuyafanya
hivyo nakuomba sana yapokee
maelekezo yangu na ukubali
kuyafanyia kazi lakini kama
utakwenda kinyume nasi lazima
tukuadhibu kwa kuishikilia familia yako na
ninakuhakikishia endapo
tukifanya hivyo itakuwa vigumu
sana kuwaona tena.Sikutaka
kuyasema hayo Dr Olivia na
sitaki tufikie huko kwani sisi ni
washirika na tuna mipango
mingi mizuri kwako ambayo
itategemea sana ushirikiano
wako kwetu hivyo Dr Olivia
ninakuomba sana tusaidie
katika hili.Tumuokoe Edger na
tuendelee na mipango mizuri
tuliyonayo.Huyo binti wa rais
ambaye unamuhofia hatutaki
kumuua bali tunataka kumtumia kwa ajili ya
kumshinikiza rais atueleze
mahala aliko Edger” akasema
Sayid.Dr Olivia
alichanganyikiwa.
“Dr Olivia” akaita Sayid.Dr
Olivia akafuta machozi na
kusema
“Sayid tafadhali naomba
msiiguse familia yangu
nitafanya hicho mnachotaka
nikifanye” akasema Dr Olivia
“Safi sana Olivia.Ahsante
kwa maamuzi hayo mazuri
ninakuhakikishia kwamba
hautajutia maamuzi hayo.Ninataka sasa uanze
kufanya maandalizi ya
kutengeneza kirusi hicho na
nitamtuma mtaalamu mwingine
aje akusaidie katika hilo zoezi
“Hapana sihitaji mtu yeyote
wa kunisaidia.Nitaifanya kazi
hiyo mimi mwenyewe” akasema
Dr Olivia
“Una hakika hutaki mtu wa
kukusaidia Dr Olivia?akauliza
sayid
“Sihitaji mtu wa kusaidiana
naye.Nitaifanya kazi hii mimi
mwenyewe” “Sawa Olivia.Unaweza
ukaniambia itachukua muda
gani kutengeneza kirusi hicho?
“Sina hakika itachukua
muda gani hadi hapo
nitakapoanza kazi hiyo.Nipe
muda wa kufanya utafiti kujua
ni aina gani ya kirusi
kinahitajika” akasema Dr Olivia
“Sawa Olivia tutaendelea
kuwasiliana mara kwa mara
kujua maendeleo ya mpango
huo lakini naomba jambo hili
lisichukue muda mrefu sana
kwani hatujui Edger yuko
katika hali gani huko aliko” akasema Sayid na kuagana na
Dr Olivia
“Nitaendelea kujuta kila
wakati kumfahamu na
kumsaidia Edger.Wema na
juhudi zangu vimegeuka
shubiri.Nimejiingiza katika
mtego nimenasa na siwezi tena
kutoka.Familia yangu nayo
imeingizwa katika suala hili na
sasa wako katika hatari
wanatishiwa kuuawa endapo
sintafanya wanavyotaka.I won’t
let that happen to my
family.Wazazi na ndugu zangu
hawafahamu kama nina mahusiano na watu wa
IS.Hakuna ajuaye kama hata
fedha za kituo kile ambacho kila
mmoja anajua ni changu
zimetoka kwao.Ee Mungu
naomba unitoe katika shimo hili
la moto nilimojitumbukiza”
akawaza Dr Olivia akitoa
machozi
“Sijui itakuaje pindi wazazi
wangu wakifahamu kwamba
ninashirikiana na
magaidi.Nitafanya nini
mimi?akaendelea kujiuliza
maswali “Sina ujanja IS
wameniweka kwenye kona
lazima nifanye wanachokitaka
ili familia yangu waendelee
kuwa salama.Lakini nitaendelea
kuwa sehemu yao hadi
lini?Nitaendelea kufanya kazi
zao hadi lini? Akajiuliza na
kukumbuka maneno ya Sayid
Omar.
“Olivia utakuwa
mwanamke mwenye
nguvu,tajiri,na hakuna ajuaye
kwani siku moja unaweza
ukashika nafasi ya juu ya
uongozi.Hupendi siku moja kuwa rais wa kwanza
mwanamke?Hupendi siku moja
uongoze watu zaidi ya milioni
hamsini?Hutaki jina lako
kuingia katika vitabu vya
historia ya nchi na dunia?
“Nilikubaliana na Habiba
Jawad kwamba kwa namna
yoyote ile Edger akipatikana
hataendelea na shughuli za
siasa hapa nchini.Tulikubaliana
kwamba mipango ya kumtaka
Edger awanie urais wa
Tanzania ifutwe na sasa
wameanza kunifikiria mimi
kunifanya niwe rais wa Tanzania.Hawa watu tayari
wanao mtandao mkubwa hapa
nchini na kwa uwezo wao
mkubwa wa kifedha walio nao
wanaweza wakalifanikisha hilo
walitakalo.Kama waliweza
kumtengeneza Edger Kaka
akawa ni mmoja wa watu
maarufu kabisa na ambaye
ilibaki kidogo tu angeshika
madaraka ya urais
hawashindwi kunifanya mimi
kuwa rais wa Tanzania”
akawaza Dr Olivia na kwa mbali
akatabasamu “Hakuna mtu katika dunia
hii asiyependa kuwa mtu
mkubwa.Hakuna anayeweza
kukataa kushika madaraka ya
urais na kwa kuwa watu hawa
tayari wamekwisha anza
kunifikiria kwa hilo lazima
watahakikisha wanalifanikisha
na siwezi kusema hapana kwani
wanatumia kigezo cha
kuiteketeza familia
yangu.Wanazidi kunichanganya
hawa watu ngoja kwanza
niachane na masuala hayo
nijielekeze katika hili kubwa la
kutengeneza kirusi” akawaza Dr Olivia na kwenda katika
chumba chake cha kusomea
kilichojaa vitabu akachagua
vitabu anavyovihitaji na
kuviweka mezani akaanza
kupitia kimoja baada ya
kingine.Alizima kabisa simu
yake ili asipate bughudha
yoyote.Kwa siku nzima Dr
Olivia alishinda katika chumba
chake cha kusomea akipitia
vitabu na machapisho mbali
mbali alivyoamini vingemsaidia
katika kile alichotaka kukifanya.
MIEZI MITATU BAADAE
 
SIRI
Episode 27

Mtunzi. Patrick CK

Kwa muda wa miezi mitano
Dr Olivia Themba aliweka
pembeni kazi zake zote
akajielekeza katika jukumu
moja tu la kutengeneza kirusi
ambacho kingetumika katika
mpango wa kumtafuta
Edger.Olivia alifanikiwa
kutengeneza kirusi SAB104
ambacho alikifanyia majaribio
kwa Sokwe na kilionyesha
mafanikio kama alivyokuwa
amekusudia.
Akiwa nyumbani kwake
usiku akampigia simu Sayid ambaye wamekuwa
wakiwasiliana mara kwa mara
“Olivia habari za
huko?akauliza Sayid
“Huku kwema kabisa.Sayid
nimekupigia simu kukujulisha
kwamba rasmi sasa kirusi kiko
tayari.Jina la kirusi hicho ni
SAB104 kina uwezo wa kuua
ndani ya siku kumi na nne kama
mgonjwa hatakuwa amepata
matibabu.Dalili za maambukizi
ya kirusi hiki huanza kujitokeza
siku moja tu baada ya kuingia
mwilini.Mgonjwa huanza kuhisi mwili umechoka na usingizi wa
mara kwa mara.Ndani ya …”
“Olivia subiri kidogo”
akasema sayid na kumkatisha
Dr Olivia
“Hizo ni habari njema sana
ambazo nimekuwa nasubiri
kuzisikia kwa muda
mrefu.Nataka unielezee kwa
kituo kuhusiana na kirusi hicho
ili na mimi nikielewe kiundani”
akasema sayid na Dr Olivia
akamueleza kwa undani
kuhusiana na kirusi kile.
“Kazi nzuri sana umeifanya
Dr Olivia ni kazi ambayo itamfurahisha kila mtu lakini
kuna kitu kimoja ambacho
nataka kifanyike.Umenieleza
kwamba kirusi hicho
umekifanyia majaribio kwa
sokwe.Nataka kirusi hicho
kifanyiwe majaribio kwa
binadamu” akasema Sayid
“Hakuna haja ya kufanya
majaribio kwa
binadamu.Majaribio
niliyoyafanya ka Sokwe
yanatosha sana” akasema Dr
Olivia
“Olivia hatutaki
kubahatisha.Umefanya kazi kubwa na nzuri hivyo lazima
tuwe na uhakika wa kile
tunachotaka kukifanya hivyo
atakuja mu wetu ambaye ni
mtaalamu wa masuala hayo
kuthibitisha kirusi hicho kama
kinaweza kufanya kazi
tunayoitaka.Atakuja mtu kesho
kuchukua kirusi hicho ili
tukifanyie majaribio kuona
uwezo wake” akasema Sayid
“Sayid mnataka kukijaribu
wapi kirusi hicho? Nina
wasiwasi kinaweza kusambaa
na kuleta janga kubwa”akauliza Dr Olivia akionekana kuwa na
wasiwasi
“Usiwe na wasiwasi Dr
Olivia.Tutakujulisha pale
majaribio yatakapokuwa
yamekamilika.Mpokee mtu
atakayekuja kesho kuchukua
kirusi hicho”akasema Sayid.
“sayid sidhani kama hilo ni
jambo zuri.Kirusi hiki
nimekwisha kifanyia majaribio
na nina uhakika nacho”
akasema Olivia
“Usihofu Olivia tunataka
kujiridhisha kuhusu uwezo wake” akasema sayid na kukata
simu.
BAADA YA SIKU 1O
Tayari zimekwisha pita siku
kumi toka kirusi SAB104
kilipochukuliwa kwa ajili ya
kwenda kufanyiwa majaribio na
akina Sayid.Dr Olivia akiwa
ofisini kwake akapigiwa simu
na Sayid
“Habari yako
Sayid”akasema Dr Olivia
“Habari nzuri kabisa Olivia” “Kuna habari gani
mpya?akauliza Dr Olivia
“Olivia itakulazimu kwenda
nchini jamhuri ya kidemokrasia
ya Congo kesho kutwa”akasema
Sayid
“Nikafanye nini
huko?akauliza Dr Olivia
akishangaa
“Ukifika Kinshasa utafikia
hotel Zoela moja kati ya hoteli
kubwa kabisa jijini
Kinshasa.Chumba chako ni PS
3.Hotelini hapo utakutana na
mtu anaitwa Seif Almuhsin
ambaye atakuwa katika chumba PS1.Hivi ni vyumba vyenye
hadhi ya rais hivyo usihofu
usalama wako”
“Seif almuhsin ni nani?Kwa
nini nikaonane naye
Kinshasa?akauliza Dr Olivia
“Usiulize maswali mengi
Olivia,anza kufanya maandalizi
ya kwenda Kinshasa na kila kitu
utakifahamu huko.Tiketi yako
yako ya ndege italetwa ofisini
kwako kesho asubuhi” akasema
Sayid na kuagana na Dr Olivia
“Nikafanye nini
Kinshasa?Huyu Seif Almuhsin ni
nani?Mbona sijawahi kumsikia wakimtaja? Akajiuliza Dr Olivia
bila kupata majibu.
KINSHASA – SIKU MBILI
BAADAE
Saa kumi na mbili za jioni
Dr Olivia aliwasili katika uwanja
wa ndege wa kimataifa jijini
Kinshasa.Uwanjani hapo
alipokewa na mtu maalum na
moja kwa moja akapelekwa
Hotel Zoela ambako
alipokelewa na kupelekwa moja
kwa moja katika chumba chake
ambacho kilikwisha andaliwa.Kilikuwa ni chumba
kikubwa chenye hadhi ya
chumba cha rais.Dr Olivia
hakushanganzwa na uzuri wa
chumba kile kwani uzuri wa
chumba chake ni mara mbili
zaidi ya chumba hiki.Akaoga na
kujilaza kitandani kwa ajili ya
kujiandaa kukutana na Seif
Almuhsin.
“Mpaka sasa sielewi sababu
ya kuja Kinshasa.Huyu Seif
Almuhsin ni nani? Akajiuliza Dr
Olivia
“Siamini kama leo nimefikia
hatua hii.Nilikuwa nayasoma mambo haya katika magazeti na
kutazama katika luninga namna
kikundi cha IS kinavyosumbua
dunia kwa kufanya mauaji ya
kinyama sehemu mbali mbali
lakini leo hii ninakaa nao meza
moja na kupanga mipango
mbali mbali.Ni vipi endapo
dunia itafahamu kwamba
ninashirikiana na
IS?Nitawaeleza nini familia
yangu kuhusu suala hili
wanielewe? Dah ! inaniumiza
sana kuona maisha yangu
yakiharibika
nikijiona.Nimesoma sana lakini elimu yangu yote imeshindwa
kuwa na manufaa kwa jamii
yangu bali ninaitumia
kuwasaidia hawa magaidi.Kuna
wakati ninajiuliza kwa nini
nisiitaarifu serikali kuhusu
suala hili lakini ninaingiwa na
hofu kwani mtandao wa hawa
jamaa ni mkubwa na kwa
kufanya hivyo nitaendelea
kujiweka katika hatari kubwa
kwani lazima wataniua mimi na
familia yangu.Ngoja niendelee
kufanya vile wanavyotaka lakini
lazima nitafute njia ya kujitoa
katika mtandao huu” akawaza Dr Olivia na kutolewa
mawazoni baada ya muhudumu
kugonga mlango.Dr Olivia
akaenda kuufungua mlango na
muhudumu akampatia
kijikaratasi chenye ujumbe
ukimuelekeza meza
iliyoandaliwa maalum kwa ajili
ya chakula cha
usiku.Hakupoteza muda
akaanza kujiandaa.Baada ya
kujiandaa akatoka na kuelekea
katika ukumbi wa chakula
akakaa katika meza
aliyoelekezwa.Muhudumu akafika na kumuhudumia
kinywaji.
“Halow Olivia” sauti
ikamstua Olivia aliyekuwa
katika mawazo mengi.Mtu
mmoja aliyevaa suti nyeupe
akavuta kiti na kukaa.Bila
kutambulishwa Dr Olivia akajua
yule ndiye Seif
Almuhsin,akamtazama kwa
sekunde kadhaa na kuuliza
“Seif Almuhsin? Akauliza
Olivia na yule jamaa
akamungalia Olivia huku
akitabasamu “U mrembo sana
Olivia.Nimefurahi kukutana
nawe ana kwa ana” akasema
Seif
Wahudumu wakafika na
kuandaa meza.
“Olivia sura yako
inaonyesha wasiwasi
mkubwa”akasema Seif
“Hayo ni mawazo yako Seif
sina wasi wasi wowote”
akasema Olivia
Walipata chakula na
kuzungumza mambo mengi na
kisha Seif akamtaka waondoke
waende katika chumba chake “Olivia karibu sana kuwa na
amani usiwe na hofu yoyote,uko
salama” akasema Seif baada ya
kuingia chumbani.
“Seif nimeelekezwa nije
Kinshasa kukutana nawe lakini
sijaambiwa sababu ya kuja
hapa.Nataka kufahamu
tafadhali kwa nini niko
hapa?akauliza Dr Olivia
“Dr Olivia uko hapa kwa
ajili ya kushuhudia mafanikio
kazi yako.Kama unakumbuka
alikuja mtu kuchukua kirusi
kile kwa ajili ya kukifanyia
majaribio ambayo yalikuja kufanywa nchini Congo.Watu
wawili walichukuliwa na
kuchomwa sindano yenye virusi
hivyo na wakahifadhiwa
sehemu tukawafuatilia kwa
makini sana toka siku ya
kwanza walipopata maambukizi
ya virusi hivyo” akasema Seif na
sura ya Olivia ikaonyesha wasi
wasi
Seif akawasha kompyuta
yake kisha akawasiliana na mtu
Fulani akamtaka amuonyeshe
picha ya mtu wa kwanza na
baada ya muda Dr Olivia
akamshuhudia mtu aliyelala chini akiwa anatokwa na damu
puani na mdomoni alikuwa
katika hali mbaya sana.Dr Olivia
akastuka sana
“Huyu ni mtu wa kwanza
ambaye muda wowote atafariki
dunia” akasema Seif na
kumtaka yule jamaa
amuonyeshe mtu wa pili
“Huyu ni mtu wa pili
ambaye hali yake ilikuwa
mbaya lakini baada ya kuanza
kutumia dawa uliyotengeneza
ya kupambana na virusi wale
hali yake imebadilika na
anaendelea vyema lakini kama asingetumia dawa ile hali yake
ingekuwa mbaya kama yule mtu
wa kwanza” akasema Seif
“Seif sitaki kuangalia picha
hizi ziondoe tafadhali” akasema
Dr Olivia akigeuza shingo
kutazama upande
mwingine.Seif akatoa
maelekezo watu wale wawili
wote wauawe kwani hawana
kazi nao tena
“Sasa rasmi nimeingia
katika ulimwengu wa mauaji”
akawaza Dr Olivia akitetemeka
kwa ndani “Olivia hiki
ulichokishuhudia ni matokeo ya
kile
ulichokitengeneza.Nathubutu
kukwambia kwamba huu
ulikuwa ni mtihani mkubwa
kwako na umefaulu kwa alama
za juu sana” akasema Seif
“Kwa hiyo
hamkuniamini?akauliza Dr
Olivia
“Dr Olivia ni kawaida yetu
kuwa na uhakika wa kila
tunachokifanya hivyo
ilitulazimu kufanya majaribio
ya kirusi kile kuthibitisha uwezo wake na sasa baada ya
kuthibitisha uwezo wake
tunaweza kukitumia katika
mpango wetu.Tayari maandalizi
yamekamilika na usiku huu
mtoto wa rais atachomwa
sindano yenye kirusi na baada
ya siku mbili tutamtaka rais
atuonyeshe mahala alipo
Edger.Usihofu mipango
inakwenda vizuri.Siku si nyingi
tutafahamu mahala alipo Edger”
akasema Seif almuhsin
“Ni vipi kama rais atakataa
kutoa ushirikiano? Ni vipi kama akigoma kufuata maelekezo
atakayopewa?akauliza Dr Olivia
“Dr Olivia unaonekana una
wasi wasi mwingi.Usiwe na
hofu tafadhali,tuna uhakika na
kile tunachotaka kukifanya.Kwa
namna yoyote ile rais lazima
atatekeleza kile tunachokitaka”
akasema Seif
“Lazima niwe na wasiwasi
kwani Coletha ni mdogo wangu
familia zetu ni marafiki kwa
muda mrefu,sitaki binti yule
apoteze maisha”
“Dr Olivia
usihofu.Hatapoteza maisha.lazima rais atatekeleza
kile tunachokitaka ndani ya
muda atakaopewa na kama
akishindwa kutekeleza maagizo
basi hakuna namna mwanae
atapoteza maisha.Olivia hii ni
vita ya haki hivyo basi kupoteza
ndugu katika mapambano ni
jambo la kawaida.Sisi hatuogopi
kufa au kuua.Olivia umekwisha
ingia katika ulimwengu wetu
hivyo mambo kama haya
unapaswa kuyaozea.IS si watu
watu wabaya kama
inavyodhaniwa lakini sisi
tunaendesha mapambano kwa ajili ya kudai haki na katika
kudai haki wakati mwingine
tunalazimika kuua kwani hata
hao maadui zetu nao
wanatuua.Mabomu yenye tani
nyingi yanaangushwa katika
kambi zetu kila uchao na kuua
watu wetu hivyo na sisi lazima
tujibu”
“Hakuna kitu
mtakachonieleza kikanifanya
nikubali kuungana nanyi.Niko
nanyi kwa shinikizo na ondoeni
katika vichwa vyenu kwamba
mimi ni mwenzenu.Katu siwezi
kuwa sehemu yenu” akasema Dr Olivia na kumfanya Seif
aangue kicheko
“Olivia wewe ni mwenzetu
tayari na muda utafika ambapo
utakiri kwa ulimi wako kwamba
ni mwenzetu.Wewe una
umuhimu mkubwa sana kwetu
Olivia na kuna mipango mingi
mikubwa juu yako ambayo
naamini tayari
umekwishajulishwa hivyo
endelea kuwa mtulivu na
mvumilivu” akasema Seif
ARUSHA - TANZANIA
Mkutano wa wazalishaji
wakubwa wa bidhaa za maziwa
katika nchi za Afrika Mashariki
ulikuwa unaendelea katika
hoteli moja kubwa jijini
Arusha.Wazalishaji hawa
walikutana ili kujadili namna ya
kutatua changamoto kadhaa
wanazokutana nazo katika
sekta yao ya maziwa.Mathew
Mulumbi ambaye naye
anamiliki kiwanda cha
kutengeneza maziwa ya unga
alikuwa ni miongoni mwa
washiriki wa mkutano huo Wakati mkutano
ukiendelea bangili ya dhahabu
aliyokuwa ameivaa Mathew
ikatoa mlio na taa ndogo
nyekundu ikawaka
mfulululizo.Mathew akastuka
na kuitazama bangili ile halafu
katika kompyuta yake iliyokua
mezani ukaingia ujumbe
akaifunika kompyuta yake na
kutoka akaelekea maliwato
akatoa simu yake na kuangalia
ujumbe ulioingia akastuka
“Dr Olivia!! She’s in trouble
“Akasema kwa mshangao Akapiga simu ya Olivia
lakini haikuwa
ikipatikana.Haraka haraka
akatoka maliwato akaenda
kukusanya vifaa vyake na bila
kuaga mtu akatoka katika
chumba cha mkutano
akachukua taksi akarejea
hotelini alikofikia.Haraka
haraka akaifungua kompyuta
yake kuutazama ujumbe ule
ulioingia “Ramani
inanionyesha kwamba taarifa
imetumwa kutoka sehemu
fulani Kigamboni.Olivia yuko
Kigamboni I must help her” akawaza Mathew akiangalia
ramani iliyoonekana katika
kompyuta yake na sehemu
Fulani katika ramani ile
kulikuwa na mduara
mwekundu ikionyesha ndipo
mahala taarifa ilikotoka.
“Olivia yuko katika
matatizo gani? Kwa muda wa
miezi kadhaa sasa toka
tumefahamiana Olivia hayuko
kawaida anaonekana kuna
jambo kubwa
linamsumbua.Nimejaribu
kumuuliza mara kwa mara
kutaka kujua tatizo lake lakini amekuwa mgumu
kunieleza.Natakiwa kurejea Dar
es salaam haraka sana
kumsaidia” akawaza Mathew na
kupiga simu ofisi za shirika la
ndege la Tanzania kujua kama
kuna ndege yoyote
inayoondoka muda mfupi ujao
kuelekea Dar es
salaam.Alitaarifiwa kwamba ipo
ndege ambayo itaondoka ndani
ya saa moja kutoka muda ule
kuelekea Dar es salaam,akakata
tiketi na hakutaka kupoteza
muda akaanza kukusanya vifaa
vyake kwa ajili ya kuondoka.Wakati akipakia vifaa
vyake sandukuni simu yake
ikaita alikuwa ni rafiki yake
Gibson.
“Gibson mambo
vipi?akauliza Mathew
“Mambo poa Mathew
habari za Arusha?
“Huku kwema lakini
ninajiandaa kurejea Dar es
salaam”
“Mkutano umemalizika?
“Hapana bado lakini kuna
dharura imetokea na
kunilazimu niondoke kabla
mkutano haujamalizika” “Mathew tayari umekwisha
pata taarifa?akauliza Gibso
“Taarifa zipi Gibson?
“Hujapata taarifa
zozote?Hujaingia katika
mitandao ya kijamii kuona
kilichotokea?
“Toka asubuhi nilikuwa
katika mkutano na sijapata
muda wa kujua nini
kinaendelea.Nijuze tafadhali”
akasema Mathew
“Nilidhani safari yako ya
ghafla ni baada ya kupata
taarifa za kilichotokea” “Sifahamu chochote
Gibson.Nini kimetokea?
“Ni kuhusu yule rafiki yako
Dr OIivia.Mapema leo
ametekwa nyara na watu
wasiojulikana wakati akiingia
nyumbani kwake akitokea
uwanja wa ndege.Mpaka sasa
bado hajapatikana.Hiyo ndiyo
habari kubwa ya leo” akasema
Gibson
“Olivia ametekwa?Mathew
akashangaa
“Ndiyo ametekwa.Ni taarifa
kubwa sana nikajua nawe tayari
unafahamu” “Sifahamu kama Olivia
ametekwa wewe ndiye wa
kwanza kunijuza.Gibson
ahsante sana kwa taarifa hizi
tutazungumza zaidi nikirejea
Dar es salaam baadae jioni’
akasema Mathew na kukata
simu
“Kumbe Olivia ametekwa
nyara !! Nani hao waliomteka
nyara?akawaza Mathew na
kuingia katika mitandao ya
kijamii kufuatilia taarifa
zile.Alihisi mwili wote
ukimsisimka baada ya kusoma taarifa mbali mbali namna tukio
lile lilivyotokea.
“Kwa taarifa
zinavyoelezea,tukio hili la
utekaji wa Olivia limefanywa
kitaalamu mno na waliofanya
hivi si watu wa mzaha ni watu
wenye uwezo
mkubwa.Walikuwa
wamejipanga vyema
kuhakikisha kwamba mpango
wao unafanikiwa” akawaza
Mathew
“Nini sababu ya Olivia
kutekwa? Watekaji hao ni watu
wanaotaka kujipatia fedha au kuna suala lingine?Kwa haraka
haraka namna tukio lilivyotokea
siamini kama watu hao
wamemteka Olivia kwa sababu
ya fedha lazima kuna sababu
kubwa.Nilifanya vyema kumpa
program ile ya kunijulisha pindi
anapokuwa katika hatari.Olivia
ni mtu wangu wa karibu sana
siwezi kukubali akawa katika
hatari nitalibeba jukumu la
kumtafuta kuhakikisha
anapatikana.Ninarejea Dar es
salaam na jiji
litatikisika.Watekaji hao
wamekosea sana kumteka mtu wangu wa karibu” akawaza
Mathew na kupakia mizigo yake
kisha akachukua gari la hoteli
akaelekea uwanja wa ndege
tayari kurejea Dar es salaam.
MPENZI MSOMAJI
* BILA KUTARAJIA DR OLIVIA
ANAJIKUTA AKIINGIA KATIKA
MIKONO YA KIKUNDI CHA IS
NA ANAKUBALI KUFUATA
MAELEKEZO YAO ILI WAZAZI
NA FAMILIA YAKE WAWE
SALAMA.ATAFANIKIWA
KUJITOA KATIKA MIKONO YA
IS?
 
Hii story ni hatari kwakweli, na alivoingia mathew sulumbi dah !! Speechless kwakweli , can't wait kwa episode zijazo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom