Riwaya: Siri

Riwaya: Siri

SIRI
episode 28
Mtunzi.Patrick CK

ENDELEA………………………….
DAR ES SALAAM
MathewMulumbi aliwasili
katika uwanja wa kimataifa wa
Julius Nyerere Dar es salaam
akitokea jijini Arusha.Alitoka
ndani ya uwanja na kupokewa
na dereva wake safari ya
kuelekea nyumbani ikaanza “Tukio gani limetokea hapa
jijini leo?Mathewakamuuliza
dereva wake kana kwamba
hajui chochote kilichotokea
“Kumetokea tukio la utekaji
leo.Yule rafiki yako Dr Olivia
ametekwa nyara na watu
wasiojulikana.Hujapata taarifa
hizo mpaka muda huu?akauliza
Athuman dereva wa Mathew
“Tayari ninazo taarifa hizo
nilitaka nipate uhakika kama
taarifa hizo ni za kweli.Kuna
taarifa zozote mpaka sasa kama
amepatikana? “Mpaka sasa hakuna taarifa
zozote zilizotolewa kama
amepatikana lakini naamini
bado hajapatikana kwani kama
angekuwa amepatikana
ingekwisha tangazwa” akasema
Athumani.Ukapita ukimya
Mathewakauliza
“Athumani wewe
unazunguka sehemu mbali
mbali na unasikia mengi,kwa
tetesi ulizozisikia huko mtaani
nini yaweza kuwa sababu ya
kutekwa kwake?akauliza
Mathew “Mkuu kwa kweli mpaka
sasa hakuna anayejua nini
sababu ya Olivia kutekwa.Kila
mtu anaongea la kwake.Wengi
wanaamini kwamba watekaji
wamefanya hivyo kwa ajili ya
kutaka fedha kwani Dr Olivia ni
mtoto wa bilionea na hata yeye
mwenyewe ana mafanikio
makubwa.Kikubwa kilichopo
mtaani ni hicho kwamba
watekaji lengo lao ni kujipatia
fedha.Michezo kama hii ya
kuteka watu na kudai fedha
haikuwepo nchini kwetu
imeibuka ghafla na kushika kasi.Wafanya biashara
wakubwa na matajiri wako
kwenye hatari kubwaya
kutekwa na kulazimishwa kutoa
fedha nyingi ili kuachiwa
huru.Serikali inatakiwa
kudhibiti mchezo huu
usiendelee kwani unaleta hofu
kubwa hasa kwa wafanya
biashara wakubwa.Leo katekwa
Dr Olivia kesho atakuwa nani?
Hofu kubwa imetanda” akasema
Athumani
“Uko sahihi Athumani
kwamba michezo kama hii ya
utekaji haijazoeleka hapa nchini kwetu.Ni wajibu wa wananchi
kushirikiana na serikali
kudhibiti matukio kama haya
yanayoanza kushika kasi hapa
nchini.Wananchi wanatakiwa
kutoa ushirikiano mkubwa kwa
jeshi la polisi kila pale
wanapokuwa na
taarifa.Michezo kama hii ya
utekaji hufanywa na watu
kutoka nje wakisaidiwa na watu
wachache wa ndani” akasema
Mathewa safari ikaendelea
kimya kimya
“Wamekosea sana hawa
jamaa kumteka Olivia.Hawakujua kama Olivia
ni mtu wangu wa
karibu?Nitahakikisha ninaingia
katika mapambano na kumuooa
Olivia kwa gharama zozote”
akawaza Mathew
“Lakini nini hasa sababu ya
kumteka Olivia? Wanahitaji
fedha? Nahisi lengo lao ni hilo la
kujipatia fedha lakini papo hapo
kuna kitu ndani mwangu
kinakataa kwamba lengo la
watekaji ni kujipatia
fedha.Nahisi kuna kitu zaidi ya
fedha.Toka nilipokutana na
Olivia nimehisi ana tatizo
linamsumbua na nilipomdadisi
alikiri kweli ana tatizo na watu
Fulani ambao hakutaka
kuwataja.Je ni watu hao ndio
walimteka nyara? Kama ni wao
nini hasa tatizo lao? Je
wamehitilafiana katika
biashara? Kama ndiyo ni
biashara gani anaifanya Olivia?
Hajawahi kunieleza kama ana
biashara nyingine tofauti na
kumiliki kituo kile cha utafiti wa
magonjwa lakini naamini
hawezi kukosa biashara.Maisha
ya Olivia yametawaliwa na usiri
mwingi hapendi kuweka wazi maisha yake ndiyo maana
linapotokea tatizo kama hili
tunashindwa wapi tuanzie
kumtafuta.Hata hivyo nitafanya
uchunguzi na ukweli
utabainika” akawaza Mathew
Tayari kiza kilikwisha ingia
alipofika nyumbani
kwake.Akaenda chumbani
kwake na kukaa kitandani
akatafakari namna
atakavyoufanya uchunguzi ule.
“Tayari ninafahamu mahala
alipo Olivia lakini siwezi
kwenda huko kwa
kukurupuka.Natakiwa kujipanga vyema kwani
watekaji ni watu
waliojiandaa.Kabla ya kufanya
lolote natakiwa kwanza
nikaonane na wazazi wa Olivia
kujua kinachoendelea hadi
sasa.Yawezekana Olivia
amepatikana au yawezekana
tayari watekaji wamewasiliana
nao na kudai kiasi cha
fedha.Vile vile natakiwa
kuwaeleza azma yangu ya
kumtafuta Olivia na wao
waridhie na kunipa ruhusa ya
kulichunguza jambo hili.Siwezi
kukurupuka na kuanza kuchunguza bila kupata ridhaa
yao” akawaza Mathewna
kufungua kasiki lililkuwa
chumbani kwake akatoa
bastora akaiweka katika koti na
kuondoka.Hakuhitaji dereva
usiku huu aliondoka peke yake.
“Nimewaza sana kuhusu
sababu ya kutekwa Olivia lakini
bado sijapata jibu.Sababu
kwamba watekaji wanataka
fedha hainingii kabisa
akilini.Mgogoro aliowahi
kunidokeza waweza ukawa ni
sababu pia lakini kuna kitu
wengi wanakisahau kuna sababu ya kimapenzi pia.Hii
inawezekana ni mojawapo ya
sababu pia.Yawezekana kuna
kigogo mmoja anayemtaka
lakini Olivia amekataa kumpa
nafasi hivyo akaamua kutumia
nguvu.Nikikutana na wazazi
wake ninaweza kupata mwanga
zaidi kwani wao wanamfahamu
vyema kuliko mimi” Akawaza
akiwa garini akielekea
nyumbani wazazi wa Olivia
Alifika eneo la Mikindani
akautafuta mtaa wa
Themba.Kutokana na umaarufu
wake na namna alivyojitolea kusaidia jamii inayomzunguka
wakazi wa eneo la Mikindani
waliamua kumzawadia Agrey
Themba mtaa ambao waliuita
mtaa wa
Themba.Mathewaliuliza ilipo
nyumba ya bilionea Themba
akaelekezwa akapunguza
mwendo baada ya kulikaribia
geti.Ulinzi ulikuwa mkali eneo
lile.Gari la
Mathewlikasimamishwa na
walinzi waliokuwa wanalinda
geti la kuingilia ndani kwa
mlinzi mmoja
akamfuata.Mathewakashusha kioo akasalimia naye na mlinzi
yule akamtaka ajitambulishe
yeye ni nani
“Naitwa Mathewni rafiki wa
Olivia nimekuja kuonana na
wazazi wake”akasema Mathew
“watu hawaruhusiwi
kuingia ndani labda kwa miadi
maalum hata kama ni ndugu”
akasema yule mlinzi
“Sina miadi ya kuonana na
wazazi wa Olivia lakini mimi ni
mwanafamilia ni mchumba wa
Olivia”akasema Mathewyule
mlinzi akamtazama kwa makini “Kaka usiwe na hofu mimi
ni mwanafamilia,nimetoka
safari Arusha jioni hii nikapata
taarifa za tukio lililotokea
nikaona nije moja kwa moja
nyumbani” akasema
Mathewambaye alikuwa ndani
ya gari la kifahari sana hivyo
mlinzi yule akaruhusu geti
lifunguliwe na Mathewakaingia
ndani.Ilikuwa ni mara yake ya
kwanza kuingia katika jumba
lile kubwa.Magari kadhaa ya
kifahari yaliyopata matano
yalikuwa yameegeshwa.Kijana
mmoja ambaye alionekana ndiye mpokeaji wa wageni
akamuelekeza sehemu ya
kuegesha
magari,Mathewakashuka
akapokewa na yule kijana
akamkaribisha na kumuongoza
kuelekea sebuleni ambako
kulikuwa na watu
kadhaa.Mathewakawasalimu
wote aliowakuta mle
ndani.Alimfahamu Agrey
Themba ingawa hawakuwa
marafiki.Pembeni yake alikaa
mwanamama ambaye kwa
haraka Mathewakamtambua
kuwa alikuwa mama yake Olivia kwa namna
walivyofanana.Muhudumu
akafika haraka na
kumuhudumia
Mathewkinywaji.
Dakika tano baada ya
Mathewkuingia mle sebuleni
wale wageni waliokuwamo
wakaaga na kuondoka,Agrey
akawasindikiza na pale sebuleni
akabaki mama yake Olivia
“Karibu sana baba”akasema
bi Lucy Themba mama yake
Olivia “Nashukuru mama.Pole
sana kwa tatizo lililotokea”
akasema Mathew
“Tunashukuru baba.Dunia
hii imekuwa na watu makatili
sana.Siku hizi ubinadamu
umetoweka.Watu wanatenda
matendo ya kinyama mchana
wa jua bila kuogopa.Mambo
haya sijui yanatokea
wapi.Yanataka kupoteza amani
tuliyo nayo Tanzania” akasema
bi Lucy
“Ni kweli mama mambo
haya ni mageni kabisa katika
nchi yetu.Watanzania tumezoea amani na hatujazoea kusikia
matukio kama haya ya kuteka
watu tena mchana wa
jua.Mambo kama haya
yanatokea sana katika nchi za
wenzetu lakini taratibu
yameanza kutokea na hapa
kwetu pia.Serikali kupitia
vyombo vyake wanapaswa
kudhibiti hali hii isiendelee
kwani kama matukio ya namna
hi yakiendelea yanaweza kuzua
hofu kubwa hasa kwa wafanya
biashara ambao ndio walengwa
wakubwa” akasema Mathew na Agrey Themba akarejea mle
sebuleni
“Kijana karibu
sana.Samahani hatukusalimiana
vyema wakati ulipoingia”
akasema Agrey na kumpa
mkono Mathew
“Karibu sana” akasema
Agrey
“Nimekaribia mzee.Poleni
sana na tukio la leo”akasema
Mathew
“Tumekwisha poa kijana
wangu.Ni jambo ambalo
limetuacha katika simanzi
kubwa”akasema Agrey huku akimtazama Mathewkwa
makini sana
“U mgeni kabisa machoni
kwangu.Tumewahi kuonana
sehemu fulani? Naomba
unikumbushe tafadhali kwani
uzee umekwisha piga hodi na
kuna nyakati ninasahau”
akasema Agrey
“Mzee mimi nakufahamu ila
wewe sidhani kama
unanifahamu.Ninaitwa
MathewMulumbi ni
mfanyabia………….” Kabla
Mathewhajaendelea Agrey
akamkatisha“MathewMulumbi hili si
jina geni kwangu.Wewe ndiye
mwenye kiwanda cha
kutengeneza maziwa cha Masai
Milk?
“Ndiyo mimi mzee” akajibu
Mathew
“Nimefurahi kukutana
nawe Mathewkaribu
sana.Ninamiliki shule kadhaa
hapa jijini dare s salaam
ambazo hupata huduma ya
maziwa kutoka kiwandani
kwako.Niliambiwa kiwanda kile
kinamilikiwa na kijana mmoja
anaitwa Mathewlakini sikuwahi kukutia machoni.Niliambiwa
ukiacha kiwanda kile unazo pia
biashara nyingine kubwa
kubwa.” akasema Agrey
“Ndiyo mzee.Nina biashara
nyingine mbali mbali,viwanda
mashamba nk”
“Hongera sana
Mathew.Nimefurahi
nimekutana nawe leo ingawa
tumekutana katika wakati kama
huu wa matatizo.Naamini pale
tatizo hili litakapokuwa
limemalizika tutapata wasaa
mzuri wa kukutana na
kuzungumza mambo mengi hususan masuala yetu ya
kibiashara”akasema Agrey
“Ahsante sana
mzee,nitafurahi sana kupata
wasaa wa kuzungumza nawe
mambo mengi na kupata
mawazo mengi zaidi ya
biashara” akasema
Mathewukimya mfupi ukaputa
Mathewakasema
“Mzee na mama
mtanisamehe kwa kuja bila
taarifa lakini nimekuja
kuwapeni pole kwa tukio
lililotokea leo.Nilikuwa katika
mkutano Arusha ndipo nilipopata taarifa za kutekwa
Olivia hivyo ikanilazimu
kukatisha mkutano na kurejea
Dar es salaam.Dr Olivia ni rafiki
yangu.Nimefahamiana naye
miezi kadhaa iliyopita na
amekuwa rafiki yangu mkubwa
ndiyo maana nilipopata taarifa
za kutekwa kwake
nimelazimika kuja mara moja
kuungana na familia yake katika
wakati huu mgumu vile vile
kusaidia katika
kumtafuta”akasema Mathew
“Mathewninakushukuru
sana kwa kuguswa na suala hili.Wewe ni rafiki wa kweli na
kwa hili ulilolionyesha la
kuacha shughuli zako zote na
kuja kuungana nasi kutufariji
katika wakati huu mgumu
limetugusa sana.Kwa nini Olivia
hajawahi kututambulisha
kwetu? Wewe unapaswa kuwa
sehemu ya familia yetu.Olivia
anao marafiki wengi lakini
hakuna aliyeonyesha kuguswa
kama wewe” akasema Agrey
“Mzee mpaka sasa kuna
taarifa zozote zimepatikana
kujua mahala alipo
Olivia?akauliza Mathew “Nimekuwa na mawasiliano
ya karibu sana na rais,mkuu wa
jeshi la polisi nchini na hao
wote tunawasiliana kila mara
na hadi nilipowasiliana nao
kama dakika ishirini zilizopita
bado Olivia hakuwa
amepatikana.Jeshi la polisi
linaendelea na juhudi zake na
hakuna kulala hadi wahakikishe
Olivia anapatikana.Rais
amekwisha toa maelekezo kwa
jeshi la polisi wahakikishe
wanatumia kila uwezo walio
nao kumtafuta Olivia na
kumpata.Ninaamini mpaka kesho asubuhi tunaweza
tukawa na taarifa nyingine
nzuri lakini taarifa tuliyonayo
hadi muda huu bado Olivia
hajapatikana” akasema
Agrey.Ukapita ukimya wa
sekunde kadhaa halafu
Mathewakasema
“Mzee samahani tunaweza
kuzungumza faragha kidogo?
“Sawa hakuna tatizo”
akasema Agrey akamchukua
Mathewwakatoka nje ya
nyumba wakaelekea katika
bustani ambako kulikuwa na
sehemu za kukaa kupumzika “Nakusikiliza Mathew”
Akasema Agrey
“Mzee nitakuchukulia muda
wako kidogo lakini nataka
nipate picha ya namna tukio lile
lilivyotokea.Mimi sijabahatika
kufika eneo la tukio kama
nilivyokueleza kwamba
nilikuwa Arusha.Naamini
utakuwa umefika eneo la tukio
na utakuwa umeshuhudia
namna tukio
lilivyotokea.Nataka kufahamu
mazingira ya namna tukio lile
lilivyotokea kwani nimesoma tu
mtandaoni na sijapata picha halisi” akasema Mathew.Agrey
akamtazama Mathewkidogo na
kusema
“Niliwasiliana na Olivia
asubuhi ya leo akiwa jijini
Kinshasa na akanieleza kwamba
atarejea leo nyumbani.Alirejea
salama na tukio la kutekwa
limetokea wakati akijiandaa
kuingia ndani ya nyumba yake
akitokea uwanja wa ndege.Kwa
siku za karibuni Olivia aliamua
kuwa na walinzi kwa kuwa
wewe ni mtu wake wa karibu
nadhani umekwisha waona
akiwa nao sehemu mbali
mbali.Aliamua kuwa na walinzi
baada ya kuwa na wasi wasi na
usalama wake hivyo alipotoka
uwanja wa ndege alikuwa na
magari mawili moja alikuwamo
yeye na mlinzi wake mmoja
pamoja na dereva na lingine
walikuwemo walinzi wake
wengine.Kwa mujibu wa
mashuhuda ni kwamba magari
yalipokaribia katika geti la
nyumba ya Olivia ilitokea
helkopta na mtu mmoja
akajitokeza katika helkopta ile
akiwa na bunduki kubwa na
kuanza kumimina risasi katika magari yale na dereva wa gari la
Olivia akapigwa risasi akafa
pale pale na gari la Olivia
likaenda kugonga ukuta.Walinzi
wake nao waliuawa
wote.Taarifa kutoka kwa mlinzi
wa getini ambaye alijificha
wakati tukio lile linatokea
alisema kwamba zilitokea gari
mbili kwa kasi na kumchukua
Olivia wakaondoka naye.Jeshi la
polisi walijaribu kufuatilia picha
za kamera za ulinzi lakini
hawakuweza kuwatambua watu
wale kwani walikuwa
wamefunika nyuso zao na vile vile gari zote mbili zilikuwa na
namba zinazofanana.Helkopta
ile imepatikana imekutwa
imetelekezwa sehemu nje ya jiji
na dereva wake amekutwa
ameuawa yeye na familia yake
inaonekana helkopta ile iliibwa
na watekaji wakaitumia kisha
wakaitelekeza.Hapo ndipo
walipofikia jeshi la polisi na
uchunguzi unaendelea”
akasema Agrey
“Pole sana mzee wangu.Hili
linaonekana ni tukio
lililopangwa kitaalamu
sana.Kuna mtu yeyote ambaye anashikiliwa hadi sasa kufuatia
tukio hilo?akauliza Mathew
“Kwa taarifa nilizozipata ni
kwamba hadi sasa watu zaidi ya
ishirini wanashikiliwa na jeshi
la polisi vile vile watumishi
wote wa nyumbani kwa Olivia
nao pia wanashikiliwa na jeshi
la polisi kwa
mahojiano.Mtandao uliofanya
tukio hili unaonekana ni mrefu
ndiyo maana idadi hiyo kubwa
ya watu inashikiliwa ndani ya
kipindi kifupi” akasema Agrey
na gari Fulani likaingia
wakashuka watu wawili Agrey akamuomba Mathewamsubiri
akawapokee wageni wale
atarejea.Agrey akaenda
kuwapokea wageni wake na
kuwakaribisha ndani baada ya
muda mfupi akarejea
“Samahani kwa kukuacha
mwenyewe Mathew,mgeni yule
ni naibu waziri wa mambo ya
nje amekuja kutupa pole,ni
rafiki yangu sana.Tuendelee na
mazungumzo yetu” akasema
Agrey
“Mzee nimeomba
tuzungumze faragha kuna suala
la muhimu sana la kujadiliana mimi na wewe na sikupenda
mtu mwingine alifahamu’
akasema Mathew
“Ni suala gani
Mathew?akauliza Agrey.
“Hakuna anayefahamu
sababu ya Olivia kutekwa lakini
wengi tunaamini yawezekana
watekaji wanataka fedha kwani
mchezo wa namna hii upo
katika nchi mbali mbali na mara
watekaji wanapomteka mtu
hupiga simu kwa familia yake
wakidai kiasi kikubwa cha
fedha.Hamjapigiwa simu na mtu yeyote msiyemfahamu?akauliza
Mathew
“Hata sisi tunaamini hivyo
kwamba watekaji hao
yawezekana lengo lao ni
kujipatia fedha lakini mpaka
sasa hawajapiga simu na
hatujapokea simu yoyote
ambayo hatuifahamu” akajibu
Edger
“Kama lengo lao ni fedha
basi watapiga simu na
watakapopiga watatoa vitisho
kwamba msiwasiliane na jeshi
la polisi” “Tumekwisha eleweshwa
tayari na jeshi la polisi
kuhusiana na suala hilo na
watakapopiga tutawasiliana na
polisi haraka sana” akasema
Agrey
“Hata hivyo umakini
mkubwa unatakiwa kwani watu
hawa ni hatari na wamejipanga
vyema hivyo kosa moja hata
dogo linaweza kuweka uhai wa
Olivia mashakani” akasema
Mathew
“Unaniogopesha
Mathew.Unashauri wakinipigia simu kutaka fedha nisiwasiliane
na polisi?akauliza Agrey
“Sina maana kwamba
usiwasiliane na jeshi la polisi
lakini umakini mkubwa sana
unatakiwa.Hata polisi
wasipokuwa makini mnaweza
mkapoteza fedha na Olivia
msimpate.Tuachane na hilo
kuna suala la pili ambalo nataka
tuzungumze” akasema
Mathewna kunyamaza kidogo
kisha akasema
“Nimefahamiana na Olivia
miezi kadhaa iliyopita na
tumekuwa marafiki wa karibu sana.Katika ukaribu wetu
nimekugundua kwamba Olivia
alikuwa na tatizo
linalomsumbua na siku moja
niliwahi kumuomba anieleze
tatizo lake lakini alinieleza kwa
kifupi kwamba ana matatizo na
watu Fulani.Nilimtaka anieleze
ni tatizo gani na watu hao ni
akina nani lakini hakutaka
kuliongelea suala hilo.Hali hiyo
imeendelea kwa muda mrefu na
baada ya tukio la leo nimeanza
kupata picha kwamba
yawezekana watu hao ambao
alinidokeza kwamba ana matatizo nao watakuwa na
mahusiano na kutekwa
kwake.Nimekuja kwako
kufahamu je hakuwahi
kukueleza chochote wewe au
mama kuhusiana na tatizo
lililokuwa linamsumbua?
Akauliza Mathew.Agrey
akafikiri kidogo na kusema
“Ni mara ya kwanza
ninasikia kutoka kwako
kwamba Olivia alikuwa na
tatizo linamsumbua.Kwa tabia
yake Olivia ni mtu msiri sana ni
nadra kuweka wazi tatizo
linalomsumbua.Akikueleza tatizo lake basi limemshinda
kulitatua na anahitaji
msaada.Anaamini sana katika
kutatua matatizo yake yeye
mwenyewe bila kuomba
msaada.Kutokana na wote kuwa
na shughuli nyingi,mimi naye
tumekuwa tukionana mara
chache na hata tunapoonana
hajawahi kunieleza kama ana
tatizo linamsumbua.Ni watu
gani hao aliokuwa katika
mgogoro nao? Inawezekana
kabisa wakawa wanahusika
katika tukio la leo kama
unavyosema” akasema Agrey.
 
SIRI
Episode 29

Mtunzi.Patrick CK

“Ngoja nikamuulize mama
yake yawezekana amewahi
kumueleza chochote kuhusiana
na tatizo lake” akasema Agrey
“Hakuna sababu ya
kumsumbua mama.Naamini
hajamweleza kwani kama
angekuwa anafahamu chochote
angekwisha kwambia” akasema
Mathewna ukimya mfupi
ukapita halafu Mathewakasema
“Mzee ninaomba nikueleze
jambo kubwa ambalo limenileta
hapa lakini naomba jambo hilo
libaki kati yetu”
“Nakusikia Mathew” “Mimi nimewahi kufanya
kazi katika idara ya ujasusi
lakini kwa sasa nimeachana na
shughuli hizo na ninaendelea na
biashara zangu lakini kuna
nyakati hulazimika kurejea tena
katika kazi yangu hiyo ya
zamani pale linapotokea jambo
ambalo linanilazimu niwepo
kulishughulikia.Mara nyingi
nimekuwa nikiombwa na
serikali kushughulikia masuala
Fulani pale penye ulazima na
siwezi kukataa kwani nina
mapenzi makubwa na nchi
yangu” akasema Mathew.Agrey Themba akamuangalia kwa
macho yaliyojaa mshangao
mkubwa
“Wewe ni
mpelelezi?akauliza Agrey
“Ndiyo.Nimewahi kuifanya
kazi hiyo lakini kwa sasa
ninafanya shughuli zangu
binafsi”akasema
MathewMulumbi
“Nimeshangaa sana
Mathewsikutegemea kabisa
bilionea kama wewe unaweza
kuwa mpelelezi” akasema Agrey
“Niliwahi kufanya kazi hiyo
zamani lakini kwa sasa nimekwisha achana nao
ninajishughulisha na biashara
zangu kama nilivyokueleza
awali.Mzee Themba,Olivia ni
rafiki yangu mkubwa na kwa
sababu yake nimeamua
kutumia ujuzi wangu nilio nao
katika masuala haya ya
uchunguzi kumtafuta na
kuhakikisha ninampata”
akasema Mathew
“Mathewahsante sana kwa
kujitolea kutumia ujuzi wako
kumtafuta mwanangu lakini
suala hili tayari liko katika
mikono ya jeshi la polisi na wanatumia kila nguvu
waliyonayo kuhakikisha
wanampata Olivia.Ninashauri
kama unalo jambo lolote
linaloweza kusaidia kupatikana
kwa Olivia liwasilishe kwa jeshi
la polisi walifanyie kazi kwani
wao wana nguvu kubwa na
mtandao mrefu.Hata hivyo
nakushukuru sana Mathewkwa
moyo wako wa kujitolea kwa
ajili ya Olivia”akasema Agrey
Themba
“Mzee,kwa uzoefu wangu
nimegundua watekaji hawa ni
watu waliojiandaa na hawajakurupuka.Wanafahamu
Olivia ni mwanao,wanafahamu
ukaribu wako na rais na
wanajua kabisa kwamba
kutokana na ukaribu huo nguvu
itakayotumika kumtafuta Olivia
ni kubwa hivyo wamejiandaa
vyema kukabiliana na nguvu
yoyote
itakayotumika.Ukifuatilia
namna walivyomchukua Olivia
ndipo utagundua kwamba watu
hawa si watu wa kufanyia
mzaha na operesheni hii
hawakukurupuka wamejipanga
vyema.Operesheni kama hizi hufanywa na watu wenye
utaalamu mkubwa hasa
majasusi pale wanapomuhitaji
mtu Fulani muhimu.Nimefanya
kazi katika idara ya ujasusi
nikiwa tegemeo hivyo mambo
kama haya ninayafahamu
vyema na ndiyo maana
nimejitolea kumtafuta Olivia
kwani nina uhakika mkubwa wa
kumpata kwa kuwa
ninazifahamu mbinu zote za
kijasusi”akasema Mathew.Agrey
akafikiri kwa muda na kusema
“Mathewmaneno yako
yanazidi kunipa woga kuhusu mwanangu kama huko aliko
atakuwa salama ninatamani
sana kukupa jukumu hili la
kumtafuta mwanangu lakini
tayari polisi wanaendelea na
uchunguzi na hatuwezi kuwa na
timu mbili za uchunguzi kwa
wakati mmoja.Polisi wana
mtandao mkubwa sana na
wanaweza wakampata Olivia
kwa haraka zaidi kuliko ukiwa
peke yako.Ushauri wangu
Mathewnitakuunganisha na
mkuu wa jeshi la polisi
uzungumze naye na kama kuna
kitu chochote ambacho unadhani kinaweza kusaidia
katika uchunguzi utawaeleza na
wao watakifanyia kazi.Kwa sasa
jeshi la polisi wanatafuta sana
taarifa zozote ambazo zinaweza
kusaidia kumpata Olivia wewe
unaweza kuwa mtu muhimu
sana kwao” akasema Agrey
“Mzee suala hili la la Olivia
ni pan asana na ninakuomba
usilichukulie krahisi.Hatuwezi
kuwaachia jeshi la polisi peke
yao na ndiyo maana nimeamua
kusaidia uchunguzi kwa
kutumia uzoefu nilio nao lakini kwa mbinu zangu ninazozijua”
akasema Mathew
“Mathewnimekuelewa sana
kijana wangu lakini hofu yangu
ni kwamba nikikuruhusu
ufanye uchunguzi wako peke
yako unaweza ukaingiliana na
jeshi la polisi na kumuweka
Olivia katika hatari zaidi ndiyo
maana nikashauri kwamba
uungane na jeshi la polisi au
kama una taarifa zenye msaada
basi wape polisi.Binafsi bado
nina imani kubwa na jeshi la
polisi kwamba watampata
Olivia ndani ya muda mfupi kwani nguvu waliyoanza nayo
ni kubwa” akasema
Agrey.Mathewakamtazama
Agrey na kusema
“Olivia ametekwa saa tano
asubuhi,tayari giza limeingia na
hakuna taarifa yoyote yenye
kutia matumaini kuhusu mahala
aliko Olivia.Mzee nafahamu
juhudi kubwa zinafanyika
kumtafuta Olivia lakini bado
haitoshi.Nguvu zaidi inahitajika
na ninaomba ridhaa yenu ili na
mimi nitoe msaada wangu”
akasema Mathew “Mathewbado imani yangu
ni kubwa kwa jeshi la polisi
kwamba watampata
Olivia.Wamekwisha jipanga
vyema kabisa na kwa mipango
yao namna walivyonieleza
wanakwenda vizuri.Kupitia
tukio hili la Olivia jeshi la polisi
wanataka kuchimba hadi mzizi
wa mtandao huu wa watekaji
hapa nchini na kuusafisha
kabisa.Mathewnadhani hatuna
cha kuzungumza zaidi nina
wageni wananisubiri
ndani.Kama utakuwa tayari
kushirikiana na jeshi la polisi basi utanijulisha ili
nikuunganishe na viongozi wa
polisi” akasema Agrey Themba
na kumpa mkono
Mathewakimuaga
“Mzee ni vipi nikikueleza
kwamba tayari ninafahamu
mahala alipo Olivia? akauliza
Mathew
“What?!! Agrey akapatwa
na mstuko mkubwa.
“Mzee nisikilize vizuri”
akasema Mathewhuku Agrey
akimtazama kwa macho yenye
woga “Baada ya Olivia
kunidokeza kwamba ana
matatizo na watu fulani
niliingiwa hofu kuhusu maisha
yake na nilichokifanya nilimpa
namba Fulani nikamtaka
azipige namba hizo pindi
anapokuwa katika
matatizo.Namba hizo ni za
program maalum ambayo
ninaitumia kwa ajili ya usalama
wa familia yangu.Nikiwa
mkutanoni Arusha nilipata
ujumbe ukinijulisha kuwa
namba ile imepigwa nikatazama
ni nani amepiga nikagundua ni Olivia.Programu ikanionyesha
hadi mahala ambapo namba
hiyo ilipigwa na ninaamini
ndipo alipo Olivia”akasema
Mathew
“Jesus Christ !! akasema
Agrey.Mathewakamtaka
waelekee katika gari lake
akachukua kompyuta na
kumuonyesha Agrey
“Namba zile nilizompa
Olivia zilipigwa hapa kwenye
huu mduara mwekundu
ambako ramani hii
inatuonyesha kwamba ni
sehemu fulani Kigamboni”akasema
Mathew.Agrey akaitazama
ramani ile kwa makini huku
midomo ikimtetemeka
“Ma.mma…Mathewunachok
isema ni cha kweli?akauliza
“Ndiyo mzee ni kitu cha
kweli kabisa.Nimerejea kutoka
Arusha kwa sababu nina
uhakika wa kumpata
Olivia.Ninayo sehemu ya
kuanzia kumtafuta Olivia.Kabla
sijaenda mahala hapo niliona ni
vyema nikafika kwanza hapa
kuzungumza nanyi na
kuwaeleza mipango yangu kuhusiana na kumpata
Olivia.Mzee ninaomba
mniruhusu nikamtafute
Olivia.Ninawaahidi ninao uwezo
mkubwa wa kumpata kwa
haraka” akasema Mathew
“Nadhani mama yake naye
anatakiwa kulifahamu suala
hili” akasema Agrey na
kumpigia simu mke wake
akamtaka awafuate pale
bustanini ambaye alifika mara
moja.
“Lucy utatusamehe tulitoka
nje kuna suala nyeti sana
tulikuwa tunazungumza.Mathewameniel
eza jambo zito sana” akasema
Agrey
“Ni jambo gani?akauliza
Lucy
“Mathewhebu mueleze mke
wangu naye asikie”akasema
Agrey,Mathewakamueleza kila
kitu alichomueleza Agrey,Lucy
akaanza kumwaga machozi
“Lucy usilie
tafadhali.Nimekuita hapa ili
tushirikiane katika kutoa
maamuzi nini
kifanyike.Mathewamenieleza
historia yake amewahi kufanya kazi katika idara ya ujasusi na
ameomba atusaidie katika
kumtafuta Olivia.Nilisita
kumruhusu afanye hivyo kwa
kuwa tayari jeshi la polisi
wanalishughulia hili suala hivyo
nikaogopa kusitokee mgongano
katika uchunguzi” akasema
Agrey
“Agrey are you out of your
mind? Mtoto wetu ametekwa na
watu wasiojulikana na hatujui
mpaka sasa hivi yuko
wapi.Amekuja mtu mwenye
taarifa nyeti kama hii ambayo
inaweza ikasaidia kumpata mwanetu halafu hutaki kumpa
ushirikiano!! Akafoka Lucy
“Lucy si kwamba sitaki
kumpa ushirikiano ninaogopa
kuleta mgongano kwani tayari
jeshi la polisi wanalishughulikia
suala hili.Nimekuita hapa ili
tujadiliane tuone nini cha
kufanya” akasema Agrey
“Agrey hupaswi kuweka
mjadala katika suala hili.Kwa
hapa tulipofika tunahitaji
msaada wa kila aina kumpata
Olivia.Hata kama jeshi la polisi
wanaendelea na uchunguzi
bado haizuii na sisi kuendelea na jitihada nyingine za
kumtafuta Olivia.Hatuwezi
kukaa na kulitegemea jeshi la
polisi peke yake.We need to do
something! Mungu amemleta
huyu kijana ambaye ameacha
shughuli zake zote na kuamua
kutusaidia kumtafuta
Olivia,lazima tumpe ushirikiano
mkubwa” akasema Lucy
“Mathewtunakusikiliza
wewe una ushauri
gani?akauliza Agrey
“Kilichonileta hapa
kuzungumza nanyi ni kuomba
mnipe ruhusa ya kumtafuta Olivia.Nina uhakika mkubwa
nitampata.Ninao uzoefu
mkubwa sana katika masuala
haya ndiyo maana nina uhakika
wa kumpata Olivia na tayari
ninayosehemu ya
kuanzia.Naombeni wazee
wangu mnikubalie niweze
kumtafuta Olivia.Ninakuondoa
hofu mzee wangu kwamba
uchunguzi wangu hautaweza
kuleta mgongano wowote au
kuingilia uchunguzi wa jeshi la
polisi.Ningeweza kufanya
uchunguzi huu kimya kimya
bila kumtaarifu mtu yeyote lakini nimeona haitakuwa
vyema kufanya hivyo bila
kupata Baraka zenu.Nafahamu
si jambo jepesi,ni jambo la
hatari sana lakini niko tayari
kulifanya na nitahakikisha
Olivia anapatikana” akasema
Mathew
“Mathewninatamani sana
kusema nenda kamtafute Olivia
lakini ninasita kukutuma uende
huko peke yako
Mathew.Nashauri taarifa hii
tuwape jeshi la polisi
wakaifanyie kazi,wao wana nguvu kubwa kuliko ukiwa
peke yako”akasema Agrey
“Mzee laiti ungenifahamu
hata kidogo usingekuwa na
hofu nami.Ninapoamua kuingia
katika kazi hizi siogopi
kitu.Hata hao waliomteka Olivia
kama wananifahamu na
wakasikia kwamba
MathewMulumbi anajiandaa
kumsaka Olivia mioyo yao
itabadili mapigo wataingiwa na
hofu kubwa kwa sababu
wanajua ziraili ameanza kazi
yake.Siogopi chochote mzee
wangu kwa ajili ya Olivia.Ninaomba mnipe ruhusa
niende nikaanze kazi usiku huu”
akasema Mathew
“Mathewhakuna mjadala
katika suala hili.Tunahitaji sana
msaada wako kumtafuta
Olivia.Ninakupa Baraka zote
kijana wangu nenda kamtafute
Olivia.Tumia kila aina ya uwezo
ulio nao kuhakikisha unasaidia
kumpata mwanangu” akasema
Lucy Themba mama yake
Olivia.Agrey Themba alitaka
kusema kitu mke wake
akamzuia “Agrey nimekwisha toa
Baraka zangu Mathewakasaidie
kumtafuta Olivia sitaki maelezo
zaidi.Mathewunaweza kwenda
baba kama kuna tatizo lolote
utalipata chukua namba yangu
hii ya simu utawasiliana
nami.Mimi ndiye nina uchungu
mkubwa kwa mwanangu
kupotea hivyo siwezi kukataa
msaada wako Mathew”
akasema Lucy Themba na
kumpatia Mathewnamba zake
za simu
“Mzee ninaondoka
tutaendelea kuwasiliana.Kila nitakachokipata nitawasiliana
nanyi” akasema Mathewna
kupiga hatua ndefu hadi katika
gari lake akaondoka
“Lucy sijafurahishywa na
hiki ulichokifanya” akasema
Agrey baada ya
Mathewkuondoka
“Sihitaji mjadala wowote
katika suala hili Agrey na kama
umechukia mimi sijali kwani
ninachohitaji ni mwanangu
apatikane.Kijana amekuja na
anazo taarifa zinazoweza
kusaidia kupatikana kwa Olivia
kwa nini tusimpe nafasi ya kusaidia na isitoshe ni
mpelelezi anazo mbinu nyingi
za kuweza kusaidia kumpata
Olivia.Kwa nini unakuwa na
wasi wasi katika suala
hili?Nashindwa kukuelewa
Agrey” akasema Lucy
“Lucy wote tuna uchungu
mkubwa kwa tukio la leo lakini
tunapaswa tuwe makini sana
katika hatua tunazozichukua
kwani nyingine zinaweza
kusababisha madhara badala ya
kuwa msaada kwetu.Jeshi la
polisi hivi sasa wako kazini
wakimtafuta Olivia.Wanakwamba lazima mwanao
atapatikana.Msihi pia Lucy
asiwe na wasi wasi,jeshi la
polisi wako kazini na
wanaendelea kufanya kila
waliwezalo kuhakikisha
kwamba wanampata
Olivia.Mimi bado siamini kama
jeshi la polisi wanaweza
wakashindwa kumpata
Olivia.Mtandao wao ni mkubwa
sana na nguvu kubwa kwa sasa
wameielekeza katika suala hili
hivyo ninawatoa wasiwasi
kwamba Olivia lazima
atapatikana.Tuendelee kushikamana.Kama mtapata
taarifa zozote zinazoweza
kusaidia katika uchunguzi huu
tuzifikishe haraka kwa jeshi la
polisi ili zifanyiwe
kazi”akasema Dr Evans
“Nimekuelewa Evans na
ninakushukuru sana kwa
kuweka uzito mkubwa katika
suala hili.Nina imani kubwa na
jeshi la polisi chini ya
maelekezo yako kwamba Olivia
atapatikana” akasema Agrey
“Agrey nitaendelea
kuwasiliana nawe na
kukujulisha kila nitakachokuwa ninakipata kutoka kwa jeshi la
polisi” akasema Dr Evans
wakaagana
“Agrey amenistua sana.Hili
suala la Olivia litanipasua moyo
wangu” akawaza Dr Evans na
kuweka mkono kifuani mahala
unakokaa moyo.Mapigo ya
moyo wake yalibadilika na
kwenda kwa kasi kubwa.
“Siri imegundulika”
akawaza
“Yote ambayo huyo
Mathewamemueleza Agrey ni
ya kweli kabisa.Ni kweli Olivia
yuko kitalu 7 Kigamboni.Maelezo
niliyoyapata kutoka kwa
Devotha ni kwamba walimtaka
Olivia awape namba za Sayid
Omar ambaye amekuwa
akiwasiliana naye mara kwa
mara na akawapa namba zile
ambazo walipozipiga mfumo
wote ukajifunga.Kompyuta zote
zikazima na hakuna
kilichoendelea hadi sasa.Kumbe
namba zile Olivia alipewa na
Mathew.Who is this
MathewMulumbi?akajiuliza Dr
Evans “Kwa kuwa tayari
amekwisha fahamu mahala
alipo Olivia hatua za haraka
sana zinatakiwa kuchukuliwa
ama sivyo mpango wetu
utaharibika.Kwanza kabisa
Olivia anatakiwa aondolewe
haraka sana mahala pale na
jambo la pili ni kuhakikisha
kwamba huyo
Mathewanapatikana kwa
sababu tayari ni mtu hatari
kwetu.Hiki ni kirusi hatari
ambacho kinatakiwa
kudhibitiwa haraka mno”
akawaza Dr Evans na kuzitafuta namba za simu za Devotha
Adolph akampigia
“Mr president” akasema
Devotha
“Devotha uko wapi?
“Niko hapa kitalu 7
mheshimiwa rais”
“Devotha we have a big
problem”akasema DrEvans
“Tatizo gani mheshimiwa
rais?
“Nitakueleza lakini kwa
sasa kuna mambo nataka
ufanye kwa haraka.Kwanza
kabisa nataka Twiga atolewe
kitalu 7 na apelekwe kitalu 2 ambako ni salama
zaidi”akasema Dr Evans
“Kuna tatizo gani
mheshimiwa rais?Kwa nini
tumuhamishe?akauliza Devotha
“Nisikilize Devotha na
utekeleze kile
ninachokuagiza.Hakikisha sasa
hivi Twiga anaondolewa hapo
kitalu 7 na kupelekwa kitalu
2.Peleka timu P3 unit hapo
kitalu 7 wakalinde na
wahakikishe kwamba hakuna
mtu yeyote anayeingia mle
ndani.Yeyote atakayekaribia
eneo hilo akamatwe haraka sana.Nataka kila kitu
kiondolewe hapo kitalu 7 na
nyumba ibaki tupu.Tekeleza
hayo yote haraka
sana.Nitaonana nawe usiku huu
kukueleza kuna nini
kinaendelea”akasema Dr Evans
na kukata simu
“Natakiwa kuonana na
daktari wangu naona
mabadiliko makubwa ya
kiafya.Hili suala la Olivia
limeniletea matatizo makubwa”
akawaza Dr Evans na jina la
Mathewlikamjia kichwani
“Who is this guy !! Is he real
or a ghost? Huyu amekuja
kuharibu kila kitu na anatakiwa
adhibitiwe haraka sana kabla
hajaharibu kila kitu.Kwa
maelezo aliyonipa Agrey
inaonekana Mathewanafahamu
alipo Olivia lakini hajui
anashikiliwa na akina nani
ndiyo maana anataka
kuchunguza.Naomba iwe hivyo
asifahamu chochote” akawaza
Dr Evans na kuchukua simu
akazitafuta namba za
mkurugenzi wa idara ya ujasusi
akampigia “Mheshimiwa rais”akasema
mkurugenzi wa idara ya ujasusi
baada ya kupokea simu ya rais
“Jacob habari za usiku huu”
“Nzuri kabisa mheshimiwa
rais”
“Jacob nahitaji
msaada.Nataka upitie katika
kumbu kumbu za watu
waliowahi kufanya kazi katika
idara yako na angalia kama
kuna mtu anaitwa
MathewMulumbi” akasema Dr
Evans “Sawa mheshimiwa
rais.Unahitaji jibu kwa usiku
huu?
“Now ! akasema Dr Evans
kwa saui ya juu
“I need the answer now!!
Akasisitiza
“Naomba dakika chache
mheshimiwa rais” akasema
Jacob silele mkurugenzi wa
idara ya ujasusi
Baada ya dakika tatu Jacob
akapiga simu
“Niambie Jacob”
“Mheshimiwa rais
nimezipata taarifa hizo.Ni kweli kuna mtu aliwahi kufanya kazi
katika idara yetu ya ujasusi
anaitwa MathewMulumbi”
akasema Jacob.Dr Evans
akashusha pumzi akatafakari
kwa sekunde chache na kusema
“Nataka unitumie faili lenye
taarifa zake sasa hivi katika
barua pepe yangu sasa hivi”
akasema Dr Evans
“Sawa mheshimiwa
rais”akasema Jacob
“Damn ! akasema Dr Evans
kwa hasira.Tayari walikwisha
ingia ikulu gari likasimama
akashuka haraka haraka na kuelekea ndani moja kwa moja
katika ofisi yake ndogo
akawasha kompyuta yake na
kuanza kulipitia faili
alilotumiwa lenye taarifa za
MathewMulumbi.Kadiri
alivyoendelea kusoma taarifa za
MathewMulumbi ndivyo
alivyoendelea kuhisi
baridi.Alimaliza kulipitia faili
lile akajiegemeza kitini.Kichwa
kilibeba mzigo wa mawazo.
“MathewMulumbi !!
akasema
“Taarifa zake zinatisha.Ni
mmoja kati ya majasusi mahiri kabisa kuwahi kutokea nchini
mwetu.Nimepitia misheni zote
alizozifanya na zote
amezikamilisha vyema kwa
umahiri mkubwa sana.Mambo
yaliyomo katika faili hili ni
mazito kabisa” akawaza Dr
Evans
“Imeibuka vita mpya.Huyu
mtu aliyejitokeza naweza
kusema ni jeshi la mtu mmoja
kutokana na uwezo wake
mkubwa.Tunatakiwa
kupambana naye kwa umakini
mkubwa sana kwani huyu
jamaa amekusudia kumtafuta Olivia na anaweza akampata
kutokana na uwezo mkubwa
alio nao” akawaza Dr Evans na
kumpigia simu Devotha
“Devotha zoezi
linakwendaje?akauliza
“Kwa sasa tunamuondoa
Twiga hapa kitalu 7 kuelekea
kitalu 2 na tayari timu P3 Unit
wako njiani wanakuja hapa
kuimarisha ulinzi kama
ulivyoelekeza” akasema
Devotha
“Good.Naomba baada ya
kutoka kitalu 2 njoo hapa ikulu
moja kwa moja kuna masuala muhimu sana ya kuzungumza”
akasema Dr Evans na kukata
simu
“Hili suala la Olivia linazidi
kuwa kubwa.Kabla hatujapata
majibu kutoka kwa Olivia
kuhusiana na ukaribu wake na
kikundi cha IS ambao ameibuka
MathewMulumbi ambaye ni
tatizo kubwa
pia.Mathewamedhamiria
kumkomboa Olivia kutoka
katika mikono ya watekaji na
tayari anafahamu mahala
alipo.Je anafahamu kama ni
serikali ndio tunaomshikilia Olivia?Anafahamu kama Olivia
ana ukaribu na watu wa IS?
Naye pia ni mmoja wao? Dr
Evans akajiuliza maswali
“Nashukuru kwa Agrey
kunipa taarifa mapema
kuhusiana na Mathewna baada
ya kufahamu uwepo wake
kinachofuata sasa ni
kupambana naye.Hatampata
Olivia tena kwani mahala
alikopelekwa si rahisi
kupafikia.Wakati tukiendelea na
suala la Olivia tutaendelea pia
kushughulika naye.Tutaelekeza
nguvu kubwa kumsaka na kuhakikisha
anapatikana.Hawezi kunishinda
mtu mmoja” akawaza Dr Evans.
 
Prezidaa apatwa na maumivu ya kichwa baada ya kupitia wasifu wa Mathew......Hatare sanaaaaa
 
#kwa yoyote alyechoxhwa na aroxto ya riwaya ya siri aje PM then me ntamtumia whtxp yote fo free km me nlvyotumiwa much thanks tu #shunie,#baba swalehe,#Mbududa
#kaz kwenu !!!
Shukrani sana mkuu umeniondolea arosto
 
jaribu kua attach je nayo haifanyi kaz??
pole kwa arosto mama,kama unaweza nichek pm nikutumie mana ww mara nying ukiwa nayo huwa unalusha mzigo fulu..so nahsi unaweza kuibadili huko kuleta hapa wadau wasome..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom