Riwaya: Siri

Riwaya: Siri

SIRI
Episode 21
Mtunzi. Patrick CK

TANZANIA
Rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania
alilazimika kukatisha ratiba ya
shughuli zake zote jijini Dar es
salaam baada ya kupata taarifa
za mlipuko uliotokea jijini
Dodoma na kumuua waziri
mkuu.Muda mfupi kabla ya
kupokea taarifa ile ya kuuawa
kwa waziri mkuu,rais alipokea
taarifa kutoka kwa mkuu wa
jeshi la polisi nchini akimjulisha
kuhusu mauaji ya mkubwa
Donald Nkebo aliyekutwa
ameuawa kwa kupigwa risasi
katika nyumba moja yeye
pamoja na watu wengine
watano.Taarifa ya kuuawa
Donald Nkebo ilimstua mno rais
kwani ni mtu aliyekuwa
anamtegemea sana katika
kufanikisha mipango ya
kuwamaliza wapinzani wake
kisiasa.Rais alimuagiza mkuu
wa jeshi la polisi nchini
kuhakikisha kwamba analiagiza
jeshi lake kufanya kila
linalowezekana kuwapata watu
waliofanya mauaji yale ya
Donald Nkebo na vijana wake.Akiwa bado katika
mstuko mkubwa wa kuuawa
Donald Nkebo rais alizidi
kutikiswa baada ya kupewa
taarifa ya waziri mkuu kuuawa
katika mlipuko.Ilikuwa ni
taarifa mbaya sana kuipokea
kwa siku ile.Mara tu baada ya
kupata taarifa zile alilazimika
kuitisha kwa haraka kikao cha
baraza kuu la usalama la
taifa.Kikao kile kiliwajumuisha
yeye rais,makamu wa rais,rais
wa Zanzibar ambaye alifika kwa
haraka baada ya kupewa mwito
wa kuwepo kwa kikao kile,alikuwepo pia makamu wa
rais wa Zanzibar vile vile
walikuwepo wakuu wote wa
vyombo vya ulinzi na usalama
wa nchi.
“Ndugu zangu
ninawashukuru sana kwa
kufika kwenu kwa haraka mara
tu baada ya kupokea
mwito.Kabla ya yote ninapenda
tusimame kwa dakika moja
tuwakumbuke wenzetu
waliopoteza maisha katika
mashambulio yaliyotokea leo
jijini Dodoma na katika mauaji
mengine yaliyotokea hapa Dar es salaam” akasema Dr Evans
kisha wote wakasimama
kuwaombea marehemu wote
waliofariki katika mashambulio
yale mawili.
“Ndugu viongozi wenzangu
sijui nianzie wapi,lakini naomba
nikiri kwamba nimetikiswa”
akasema rais na kunayamza
kidogo
“Nilipigiwa simu na mkuu
wa jeshi la polisi alfajiri ya leo
akanipa taarifa kwamba mmoja
wa wafanya biashara wakubwa
hapa nchini Donald Nkebo
amekutwa katika nyumba Fulani ameuawa pamoja na
watu wengine watano.Donald ni
mtu anayefahamika sana hapa
nchini ni mmoja wa wawekezaji
wakubwa ana viwanda vyake
kadhaa na biashara nyingine
kubwa kubwa na vile vile ni
mmoja kati ya wafadhili
wakubwa wa chama
chetu.Binafsi ni mtu ambaye
ninamfahamu na kumheshimu
sana hasa kutokana na mchango
wake mkubwa katika uchumi
wetu.Mazingira ya kifo chake
yalinistua sana na nikampa
maelekezo mkuu wa jeshi la polisi kuhakikisha watu
waliofanya mauaji hayo
wanapatikana.Mpaka sasa kuna
chochote ambacho
kimepatikana kuhusiana na
mauaji hayo?akauliza Dr Evans.
“Mkuu,mara tu baada ya
jeshi la polisi kupata taarifa za
mauaji yale na kuyathibitisha
nilikutaarifu na ukanipa
maelekezo,tayari tumekwisha
fungua jalada la uchunguzi na
vijana wako kazini wakiendelea
na kazi.Mimi mwenyewe baada
ya kupokea taarifa hiyo
niliondoka na kwenda eneo la tukio kuthibitisha kwani Donald
ni mtu niliyekuwa
nikifahamiana naye sana
tulikutana tukiwa chuo kikuu
cha Dar es salaam na toka hapo
tumeendelea kuwa marafiki
wakubwa.Mheshimiwa rais
tunaendelea kuchunguza
nyumba ile yalimofanyika
mauaji kujua shughuli gani
zilizokuwa zinaendelea kwani
kumekutwa vifaa mbali mbali
vya mawasiliano na inaonekana
kulikuwa na kompyuta kadhaa
lakini zote
zimeondolewa.Inaonekana baada ya kutekeleza mauaji yale
wauaji waliondoka na
kompyuta zote zipatazo
kumi.Tunahisi kuna kitu katika
hizo kompyuta ndiyo maana
zikachukuliwa na wauaji.Vile
vile wauaji walichukua simu
zote za watu waliowaua.Donald
amekutwa akiwa ameuawa
ndani ya gari akiwa amevaa
mavazi ya kulalia,inaonekana
aliondoka nyumbani kwake na
kwenda katika nyumba ile usiku
hivyo tunataka kujua
mahusiano yake na wale watu
waliouawa.Mheshimiwa rais timu maalum kutoka makao
makuu iko kazini hivi sasa na
nitakutaarifu kila pale
nitakapopata taarifa yoyote
kutoka kwao” akasema inspekta
jenerali wa polisi
“Kabla taarifa hiyo
niliyopokea kutoka kwa IGP
haijapoa nikapokea tena taarifa
nyingine ya kifo cha waziri
mkuu..” akasema Dr Evans na
kuinamisha kichwa
“I’m sorry,kifo cha waziri
mkuu kimeniumiza mno”
akasema Dr Evans naukimya
ukatawala ndani ya chumba kile.Kila mmoja alikuwa na uso
wenye simanzi.
“Wakuu wote wa vyombo
vya usalama mko hapa nataka
kujua nini kimetokea Dodoma
hadi bomu likategwa katika
ofisi ya waziri mkuu na
kumuua.Mmekwisha wajua
watu waliofanya tukio hilo ni
akina nani?akauliza Dr Evans na
kuwatazama wakuu wale wa
vyombo vya usalama
“Inspekta jenerali tuanze na
wewe.Jeshi la polisi ndio
wanaolinda ofisi zote kuu za
serikali.Imewezekanaje watu wakaingia na kutega bomu
wakati jengo lile lina ulinzi saa
ishirini na nne bila polisi
kugundua?Askari wako
walikuwa wapi?akauliza Dr
Evans kwa sauti kali kidogo
“Mheshimiwa rais ni kweli
jengo la ofisi ya waziri mkuu
linalindwa na askari polisi kwa
saa ishirini na nne na
kilichotokea kimetustua hata
sisi ngazi za juu na tumejiuliza
swali hilo hilo imewezekanaje
hawa watu wakapenya na
kutega mabomu katika geti la
ofisi ya waziri mkuu ambako kuna ulinzi wa saa ishirini na
nne?Askari wetu walikuwa
wapi? Mheshimiwa rais ni
mapema sana kupata majibu ya
maswali haya kwani uchunguzi
ndiyo kwanza umeanza,tayari
timu maalum ya makachero
mahiri kabisa ndani ya jeshi la
polisi wamekwisha tua jijini
Dodoma na tayari wameanza
uchunguzi kuhusiana na tukio
hili na mimi mwenyewe baada
ya kumalizika kwa kikao hiki
ninakwenda Dodoma kujua nini
hasa kilichotokea na
nitahakikisha ndani ya muda mfupi tunapata majibu”
akasema Inspekta jenerali wa
polisi.Ukimya ukapita tena
halafu Dr Evans akasema
“Idara ya kupambana na
ugaidi ni kazi yenu kudhibiti
matukio kama haya ya
ugaidi,mlikuwa wapi na kuacha
shambulio hili likatokea?
Shambulio kama hili si la
kupangwa kwa siku
moja,lazima limechukua muda
kuandaliwa.Ninyi kama idara
yenye jukumu la kuzuia mambo
kama haya yasitokee hamkuwa
na viashiria vyovyote vilivyowaonyesha kwamba
shambulio kama hili linaweza
kutokea?Mmeshindwaje
kubaini jambo kama hili
kutokea hasa katika sehemu
nyeti kama ofisi ya waziri
mkuu?akauliza Dr Evans kwa
ukali
“Mheshimiwa rais”
akasema Genevieve Nelson
mkuu wa idara ya kupambana
na ugaidi.
“Idara yangu haikuwa na
taarifa zozote za kuweza
kutokea kwa shambulio
lile.Tayari idara yangu imekwisha ingia kazini
kuwatafuta wale wote
waliofanya tukio hili
tukishirikiana na vyombo
vingine.Timu ya watu nane
tayari wamekwisha wasili jijini
Dodoma.Nina uhakika mkubwa
kwamba hadi kufika mchana wa
leo tutakuwa tumepata jibu zuri
la nani waliofanya shambulio
hilo”akasema Genevieve
“Kwa idara hii muhimu
sana kushindwa kubaini
kuwepo kwa shambulio hili ni
udhaifu mkubwa sana.Najiuliza
kama leo wameweza kutega bomu katika ofisi ya waziri
mkuu bila chombo chochote
kung’amua je watashindwa
kuingia na kutega bomu
ikulu?Kuna umuhimu gani wa
kuwa na idara ya kudhibiti
ugaidi ikiwa magaidi wanawza
kupenya hata katika ofisi nyeti
za serikali na kufanya
mashambulio?akauliza Dr
Evans kwa ukali akiwatazama
wakuu wale wa vyombo vya
usalama
“CDF kuna nini upande
wako? Akauliza Dr Evans
“Baada ya kupata taarifa za
tukio hilo nimeelekeza timu ya
wataalamu wa mabomu ifike
haraka sana eneo la tukio na
tayari wako eneo la tukio
wakisaidiana na wataalamu
kutoka jeshi la polisi kukusanya
kila kitu kwa ajili ya uchunguzi
kubaini ni bomu la aina gani
lililotumika na limetengenezwa
wapi.” akasema mkuu wa
majeshi.Ilimchukua Dr Evans
dakika chache za kutafakari
kisha akasema
“7 Agosti 1998 tulionja
adha ya mashambulio ya kigaidi baada ya ubalozi wa marekani
hapa nchini kulipuliwa.Watu 11
walipoteza maisha na wengine
85 walijeruhiwa.Leo kwa mara
ya pili tena magaidi
wanatushambulia na safari hii
wakimlenga kiongozi mkubwa
kabisa wa serikali ambaye ni
waziri mkuu wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania.Hili ni
jambo lisilokubalika na
linaumiza sana.Damu ya watu
hawa imepotea bila hatia
yoyote.Nataka vyombo vyote
vya ulinzi na usalama nchi hii
mshirikiane na muhakikishe kwamba watu hawa waliofanya
unyama wa namna hii
wanapatikana haraka sana na
watueleze nini sababu ya
kufanya hivi.Wametuchokoza
na hatuwezi kukaa
kimya.Yeyote aliyetuchokoza
lazima apate majibu yake.Awe
ni mtu,kikundi cha watu au taifa
lazima ajulikane na apate stahili
yake kwa unyama huu
waliotufanyia.Nataka tutume
ujumbe kwa dunia kwamba
Tanzania si sehemu salama kwa
magaidi na wale wote wenye
kufikiria kufanya mashambulio katika ardhi yetu wasithubutu
kufanya hivyo tena.Kwa kuwa
bado ni mapema sana na hatuna
taarifa zozote za nani
wamefanya shambuliohili
nataka tukutane tena hapa saa
kumi na moja jioni na mpaka
wakati huo kila mmoja aje hapa
akiwa na taarifa idara yake
imefikia wapi katika
kuwatambua magaidi
waliofanya unyama huu kwenye
ardhi yetu” akasema Dr Evans
na wajumbe wa kikao kile
wakatawanyika na kuwaacha
Dr Evans,makamu wa rais na rais wa Zanzibar katika
mazungumzo mazito
MAZISHI YA KITAIFA - BAADA
YA SIKU 3
Uwanja wa Uhuru jijini Dar
es salaam ulifurika pomoni
katika mazishi ya kitaifa ya
waziri mkuu wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania
aliyefariki katika mlipuko wa
bomu jijini Dodoma.Viongozi
kutoka nchi mbali mbali za
Afrika waliwasili kuhudhuria
mazishi yale ya kitaifa.Rais wa jamhuri ya muunganoi wa
Tanzania Dr Evans akiwa na
mke wake waliwasili katika
uwanja wa taifa tayari
kuwaongoza watanzania katika
shughuli ile.Dakika chache
baada ya rais kuwasili,mwili wa
waziri mkuu ukaingizwa
uwanjani kwa ajili ya kuagwa.
Viongozi wa dini
walifungua shughuli ile kwa
kusoma dua kisha zikafuata
salamu kutoka kwa wakuu
mbali mbali wa nchi
waliohudhuria mazishi yale na
hatimaye ukafika wakati ambao rais wa jamhuri ya muungano
wa Tanzania akapewa nafasi ya
kuhutubia hadhira ile kubwa ya
watanzania waliofika kumuaga
waziri mkuu.
“Ndugu watanzania na
wageni wetu mliotoka katika
mataifa jirani kuja kuungana
nasi katika mazishi haya ya
kitaifa,awali ya yote napenda
kumshukuru mwenyezi Mungu
mwingi wa rehema
kutukutanisha hapa sote siku ya
leo katika shughuli hii ya
kumuaga mpendwa wetu
mheshimiwa waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania” Dr Evansa
akanyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Dakika thelathini kabla ya
uhai wake kukatishwa
kikatili,nilizungumza naye na
nikampa maelekezo katika
mambo kadhaa na nilimuahidi
kwamba mwisho wa wiki
tungekutana jijini Dodoma.Nusu
saa baada ya kuzungumza naye
nilipewa taarifa za kifo
chake,nilipatwa na mstuko
ambao siwezi kuuelezea.Kifo
hiki kimenigusa sana mimi binafsi,watanzania wote kwa
ujumla na wapenda amani kote
duniani.Nimepokea salamu za
rambi rambi kutoka kwa
mataifa mengi duniani wote
wakiguswa na msiba huu
mkubwa,nawashukuru sana
nyote mliotufariji katika wakati
huu mgumu” rais akanyamaza
tena kidogo na kuendelea
“Hakuna maneno mazuri ya
kumuelezea mpendwa wetu
huyu kwani hakuna
asiyefahamu utendaji wake wa
kazi.Binafsi amekuwa msaada
mkubwa sana kwangu na
serikali
ninayoiongoza.Amekuwa
msimamizi mzuri wa shughuli
zote za serikali kwa umakini na
weledi mkubwa sana.Muda
hautoshi kumuelezea mpendwa
wetu huyu itoshe tu kusema
kwamba utendaji wake wa kazi
ulitukuka na tumempoteza mtu
muhimu mno.
Kutokana na utendaji kazi
wake uliotukuka na uadilifu
usio na kifani,alitengeneza
maadui wengi wa ndani na nje
ya nchi hasa wafujaji wa fedha
za serikali,mafisadi na wahujumu uchumi.Hakusita
kukemea ubadhirifu na
kuchukua hatua stahiki kila pale
alipoubaini.Maadui hawa
aliowatengeneza hawakuona
namna nyingine ya kupambana
naye zaidi ya kuitoa roho
yake.Walichokifanya ni unyama
uliopitiliza na
haukubaliki.Ninatuma salamu
kwa wale wote waliofanya
kitendo hiki,awe ni mtu,kikundi
cha watu wa ndani au nje ya
nchi siku zenu
zinahesabika.Mmetuchokoza na
sasa ni wakati wetu wa kujibu mapigo na majibu yetu
hayatakuwa
madogo.Tutawasaka magaidi
hawa kila sehemu,iwe
ardhini,majini au hata
angani,hawana sehemu ya
kujificha.Hakuna jiwe libaki juu
ya lingine wote walioshiriki
uovu huu watapata stahili yao”
akasema Dr Evans kwa
msisitizo mkubwa
Wakati mazishi ya kitaifa
yakiendelea katika uwanja wa
uhuru jijini Dar es salaam,katika
uwanja wa ndege wa Julius
Nyerere ndege ya shirika la ndege la Ethiopia ikitokea Tel
Aviv kupitia Addis Ababa ilitua
na abiria kuanza kushuka.Ndani
ya ndege hii walishuka majasusi
watano kutoka shirika la ujasusi
la Israel Mossad.Majasusi hawa
walikuja nchini kwa ajili ya
kutekeleza operesheni maalum
ya kumteka Edger kaka.Tayari
walikwishapata taarifa kwamba
Edger kaka alikuwa na mipango
ya kurejea nchini siku ya
mazishi ya waziri mkuu ili
aweze kuwahi mazishi hayo
kwani waziri mkuu alikuwa ni
mmoja wa watu aliowaheshimu sana.Waliwahi kufika nchini
kabla ya ndege aliyopanda
Edger Kaka na Olivia ambayo
ililazimika kuchelewa kuondoka
nchini Israel kwa sababu za
kiufundi.Ukweli ni kwamba
hakukuwa na hitilafu yoyote
katika ndege hiyo bali ulikuwa
ni mpango maalum wa Mossad
ili Edger achelewe kufika nchini
Tanzania na kufika Dar es
salaam usiku ili mpango wa
kumteka uweze kutekelezwa
kama ulivyopangwa.
Majasusi wale baada ya
kukamilisha taratibu za
uhamiaji na kuruhusiwa kuingia
nchini kila mmoja alipokelewa
na mtu maalum kutoka ubalozi
na kumpeleka katika nyumba
anakoishi afisa mmoja wa
ubalozi ambako ndiko mipango
yote ya operesheni ile ilikuwa
inafanyika.Siku mbili zilizopita
majasusi wengine watatu
waliwasili nchini kimya kimya
kwa ajili ya kuandaa operesheni
hiyo ya siri wakisaidiwa na
maafisa wa ubalozi wa Israel
nchini Tanzania.
Baada ya kuhakikisha kila
mmoja wao ameingia nchini salama na hakukuwa na tatizo
lolote bila kupoteza muda kikao
kikaanza
“Poleni kwa safari na
karibuni Tanzania” akasema
Gershom Rabin mkuu wa
operesheni ile.
“Kwa siku tatu tulizokaa
hapa tumekuwa na kazi kubwa
ya kuhakikisha tunaandaa
operesheni kubwa ya aina yake
ambayo itatuwezesha kumpata
Edger kaka na kuiacha serikali
ya Tanzania ikiamini kwamba
Edger kaka amefariki katika
ajali ya gari.Mpaka sasa mipango yote inakwenda
vyema.Nimekuwa na
mawasiliano na mawasiliano na
watu wetu Noam na Yosef
ambao wako ndani ya ndege
aliyopanda Edger na
wamenihakikishia kwamba
Edger bado yuko ndegeni
nimewasiliana pia na marubani
wa ndege hiyo
wamenihakikishia kwamba
ndege itaingia Dar es salaam saa
sita za usiku leo hivyo
operesheni yetu bado
inaendelea vizuri kama tulivyoipanga” akasema
Gershom
“Hapa mbele yetu kuna
ramani” akasema Gershon na
kuisogelea ramani ile.
“Hii ni barabara ambayo
inatoka uwanja wa ndege wa
Julius Nyerere kuja
mjini.Shughuli yetu itafanyikia
eneo hili hapa lenye mduara
mwekundu.Ni kilometa kadhaa
kutoka uwanja wa ndege na
tumechagua eneo hili kwa kuwa
hatutaki tukio lifanyike kati kati
ya jiji ambako kwa nyakati hizo
bado linaweza kuvuta watu.Ilan na Moshe mtakuwa katika
uwanja wa ndege wa Julius
Nyerere kumsubiri Edger kisha
mtawapokea Noam na Yosef
halafu mtalifuata kwa nyuma
gari atakalopanda Edger huku
mkiendeleza kuwasiliana
nasi.Sina haja ya
kuwakumbusha nini mnapaswa
kufanya kila mmoja anafahamu
sehemu yake ni ipi na
tumekwisha fanya mazoezi ya
kutosha hivyo kilichobaki ni
utekelezaji tu.Kikubwa
ninachowasisitiza ni umakini
mkubwa sana kwani operesheni hii ni ya siri na serikali ya
Tanzania haifahamu
chochote.Kosa moja hata dogo
linaweza kutuletea matatizo
makubwa hivyo epukeni
kufanya kosa.Mwisho kabisa
kumbukeni kunaweza kutokea
mabadiliko katika operesheni
hii hivyo kila mmoja awe
makini katika kumlinda
mwenzake” akasema Gershom
kisha wakaendelea na
majadiliano kuhusiana na
operesheni ile.
 
SIRI
episode 22
Mtunzi. Patrick CK

*******************
Ndege ya shirika la ndege la
Ethiopia ambayo ilipaswa
kuingia nchini saa sita za
mchana iliwasili katika uwanja
wa kimataifa wa Julius Nyerere
saa sita za usiu.Hii ilitokana na
sababu za kiufundi zlizotajwa
kujitokeza na kuilazimu ndege
ile kuchelewa.Ndani ya ndege
hii ndimo alimokuwamo Edger
kaka pamoja na Olivia
Themba.Edger alichagua
kupanda ndege hii ili awahi
kufika Dar es salaam na kuhudhuria mazishi ya kitaifa
ya waziri mkuu vile vile lakini
lengo lake halikufanikiwa
kutokana na mpango wa shirika
la ujasusi la Israel Mossad
kuichelesha ndege ile ili
waweze kutekeleza operesheni
yao.
Ndani ya ndege aliyopanda
Edger Noan na Yosef majasusi
kutoka Mossad walikuwa
wanamfuatilia kila
anachiokifanya huku
wakiendelea kuwasiliana na
wenzao walioko tayari jijni Dar
es salaam. “Welcome home Olivia”
akasema Edger baada ya ndege
kutua.Dr Olivia akatabasamu
“Welcome home Edger”
akasema Olivia
“Olivia nafahamu baada ya
kushuka ndegeni kila mmoja
ataenda uelekeo wake japo
ningetamani sana tungepata
walau hata dakika kumi za
kuwa pamoja kabla ya
kuachana ili niweze
kukushukuru tena kwa yote
uliyonifanyia.Nimekwisha
kushukuru sana lakini bado
haitoshi nitaendelea kukushukuru tena na tena kwa
yale uliyonifanyia kwani siwezi
kuyalipa kwa fedha zaidi ya
kuendelea kukushukuru.Kwa
muda huu mfupi tuliokuwa
pamoja umekuwa mtu wangu
wa karibu sana na ninajihisi
vibaya kuachana nawe
leo”akasema Edger.Dr Olivia
akamshika mkono na kusema
“Edger hupaswi kuendelea
kunishukuru mimi bali
mshukuru sana Mungu ambaye
alinitumia mimi kuyaokoa
maisha yako.Sifa na utukufu
mrejee yeye ambaye amekupa tena nafasi
nyingine.Ninakuahidi kwamba
huu hautakuwa mwisho wa
kuonana.Bado nitandelea
kuonana nawe mara kwa mara
kujua maendeleo
yako.”akasema Dr Olivia
“What about dinner
tomorrow?akauliza Edger.Olivia
akatabasamu na kusema
“Sawa hakuna tatizo katika
hilo”
“Thank you
Olivia.Nitakupigia simu
kukujulisha ni saa ngapi na
wapi tukutane kwa ajili ya chakula cha usiku” akasema
Edger
“Ahsante Edger.Ni wakati
wa kushuka sasa” akasema
Olivia
“Olivia nimekumbuka
kitu,kesho nitakwenda kuwapa
pole wazazi wa Judy utapenda
kuambatana nami?Ni vyema
kama tutakwenda sote kwani
Judy alikuja Israel kwa ajili ya
kuniuguza hivyo lazima
nikawape pole wazazi wake
kwa kifo cha mtoto wao”
“Usijali tutakwenda
wote.Tutawasiliana asubuhi tujue tutakutana wapi” akasema
Olivia akachukua mkoba wake
mdogo na kuelekea mlangoni na
nyuma yake alimfuata Edger
Kaka wakashuka ndegeni bila
kujua kama nyuma yao kuna
majasusi wanawafuatilia.
Edger na Olivia
walikamilisha taratibu za
uwanjani na kuingia nchini.Nje
ya uwanja Edger alipokewa na
rafiki yake mkubwa ambaye pia
ni katibu wake Stanley pia
walikuwepo viongozi wa chama
cha Democratic na watu
wengine kadhaa.Haikuwa imetangazwa kama Edger Kaka
angerejea nchini na lengo kuu la
kuweka siri ujio wake ni ili
awashangaze watu kwa kufika
ghafla ndani ya uwanja wa
uhuru hivyo ni watu wachache
waliofahamu kuhusu kurejea
kwake na kufika uwanjani
kumpokea.
“Karibu tena nyumbani
Edger” akasema Stanley kisha
akamtambulisha Edger kwa
viongozi wa juu wa chama cha
Democratic aliokuwa nao pale
uwanjani .Wakati Edger
akiendelea kusalimiana na viongozi wa chama cha
Democratic waliofika
kumpokea,Dr Olivia alikuwa
anasalimiana na familia yake
waliofika pale kumpokea
wakiongozwa na baba yake
bilionea Aggrey
Themba.Ilikuwa ni furaha
kubwa sana kwao kwa mtoto
wao kurejea nchini salama
“Olivia tunamshukuru sana
Mungu umerejea
salama”akasema Agrey
“Hata mimi ninashukuru
sana kurejea tena nyumbani
salama na kuwaoneni tena familia yangu.Nilikuwa
nawakumbuka kila dakika”
akasema Olivia halafu
akawachukua familia yake
akaenda kuwatambulisha kwa
Edger ambaye alifurahi sana
kukutana nao na Aggrey
akaahidi kumkaribisha rasmi
Edger nyumbani kwao kwa ajili
ya kufahamiana
zaidi.Hakukuwa tena na muda
wa kupoteza uwanjani pale
Edger akaongozwa katika gari
lililoandaliwa kumchukua na
viongozi wale wa chama cha
democratic wakaingia katika magari yao kisha msafara wa
magari matatu ukaondoka pale
uwanjani.Olivia na familia yake
nao wakaingia katika gari lao na
kuondoka.Majasusi Noam na
Yosef waliokuwa wanamfuatilia
Edger toka Israel wakaungana
na majasusi wenzao wawili
waliofika pale uwanjani
kuwapokea wakaingia garini na
kuondoka kuufuata msafara wa
Edger.
Hakukuwa na magari katika
barabara ya kutoka uwanja wa
ndege hivyo mwendo wa
magari ya msafara wa Edger ulikuwa mkali.Kilometa tano
kutoka uwanja wa ndege wa
Julius Nyerere gari lililokuwa
limetangulia mbele ya msafara
ule wa Edger lilikutana uso kwa
uso na lori la mafuta lililopoteza
uelekeo na kishindo kikubwa
kikasikika.Gari la pili ambalo
ndilo alimokuwa amepanda
Edger likagonga kwa nyuma
gari lile la kwanza lililogongwa
na lori la mafuta.Dereva wa gari
la tatu naye alishindwa kulizuia
gari lake akagonga kwa nyuma
gari la Edger.Ilikuwa ni ajali
mbaya. Mara tu baada ya ajali ile
kutokea majasusi wanne kutoka
katika gari lililokuwa
linaufuatilia kwa nyuma
msafara ule wa Edger
wakashuka kama umeme na
kulifuata gari la Edger.Kwa kasi
ya aina yake wakaufungua
mlango na kumkuta Edger
akiwa amepoteza fahamu na
alikuwa anavuja damu katika
paji la uso.Kulikuwa pia na watu
wengine wawili waliokuwamo
ndani ya lile gari na mmoja wao
alikuwa anagugumia kwa
maumivu.Edger akatolewa haraka haraka na kukimbizwa
katika gari lingine lililokuwa
linalifuata lile lori la mafuta kwa
nyuma kisha ukatolewa mwili
kutoka katika ile gari
ukavishwa pete za Edger
pamoja na mkufu wa dhahabu
wenye kidani chenye herufi E
kisha mwili ule ukakimbizwa
katika gari alimokuwamo
Edger.Wakati zoezi la
kubadilisha mwili ule
likifanyika kwa kasi majasusi
wengine walikuwa katika zoezi
la kumtoa dereva wa lori la
mafuta lililosababisha ajali ambaye alikuwa amebanwa
miguu.Gorshem kiongozi wa
opersheni ile akaitwa haraka
kushuhudia namna dereva yule
alivyobanwa miguu
“Amebanwa sana na hatuna
muda wa kuendelea
kumnasua,tumuacheni
tuondoke” akaelekeza na kisha
tanki la mafuta likafunguliwa na
mafuta yakaanza
kusambaa,kifaa Fulani
kikategwa na
Majasusi wote wakakimbilia
katika gari lao wakaondoka. Magari machache
yaliyokuwa yanatoka uwanja
wa ndege usiku ule yalilazimika
kusimama kutokana na ajali
ile.Gari la akina Olivia nalo
likalazimika kusimama baada
ya kukuta magari mengine
yamesimama na wakajulishwa
kwamba kuna ajali kubwa
imetokea mbele na magari
hayawezi kupita.Mara ghafla
ukatokea mlipuko mkubwa.Gari
lile la mafuta na magari
mengine yaliyokuwa karibu
yakafunikwa na moto mkubwa. Baada ya kukamilisha zoezi
la kumtwaa Edger timu ya
majasusi ikaelekea moja kwa
moja sehemu Fulani kandoni
mwa bahari ya Hindi
kulikokuwa na boti mbili.Pale
walikuta kuna gari nyingine
mbili na haraka haraka Edger
akashushwa kutoka ndani ya
gari akaingizwa katika
boti.Katika boti ile pia kulikuwa
na familia ya dereva wa lile lori
lililosabisha ajali na lengo
lilikuwa ni kumuhamisha
dereva yule na familia yake na
kuwapeleka kuishi nchini Israel.Majasusi wale wakaagana
na maafisa wa ubalozi
waliowasindikiza wakaingia
katika boti na kuondoka kwa
kasi kubwa.Boti zile mbili
zilikwenda kwa kasi kubwa
hadi mataa ya jiji ya dar es
salaam yalipoanza kuonekana
kama nyota ndipo walipoikuta
meli kubwa na Edger
akashushwa kutoka katika ile
boti akaingizwa melini akaanza
kupatiwa huduma.Gershon
kiongozi wa operesheni ile
akakutana na watu wake katika
mojawapo ya ofisi “Ninawapongeza kwa kazi
kubwa na nzuri mliyoifanya
le😵peresheni imekuwa na
mafanikio makubwa sana na
imekwenda kama tulivyokuwa
tumeipanga japo nasikitika
kwamba hatukuweza kuondoka
na dereva yule kama
tulivyokuwa tumekubaliana
naye kwani kwa namna
alivyokuwa amebanwa
ingetuchukua muda kumnasua
na sisi hatukuwa na muda
lakini tunayo familia yake
ambayo nitahakikisha
wanakuwa katika mikono salama na watatunzwa kwa
maisha yao yote.Hatujampoteza
mtu yeyote katika operesheni
hii na haya ni mafanikio
makubwa sana
kwetu.Operesheni hii ni
muhimu sana katika vita dhidi
ya magaidi ambao wamekuwa
wakiendelea kuua watu wetu
kila uchao.Kupitia mtu huyu
tutafahamu mambo mengi sana
kuhusiana na mtandao wa IS”
akasema Gorshen.
Jijini Dar es salaam magari
ya zimamoto kutoka uwanja wa
ndege wa Julius Nyerere yalifika kwa haraka sana eneo la tukio
na kuanza kuuzima moto ule
mkubwa uliokuwa unawaka na
iliwachukua zaidi ya nusu saa
kuuzima moto ule mkubwa.Ni
mwenyekiti pekee wa chama
cha Democratic aliyenusurika
katika ajali ile kwani yeye
alikuwa katika gari la tatu na
baada ya ajali ile kutokea
alifanikiwa kutoka salama na
kuanza kukimbia kama mtu
aliyechanganyikiwa huku
akipiga kelele za kuomba
msaada.Ulipotokea moto ule
mkubwa yeye hakuwepo eneo lile alikuwa katika gari moja
lililokuwa limesimama mbali
kidogo akiomba msaada wa
kuwaokoa wenzake waliopata
ajali akiwemo mbunge Edger
Kaka.
Moto ulizimwa na miili
ikatolewa katika magari ikiwa
imeungua vibaya sana.Askari
polisi walifika haraka sana na
kulifunga eneo lile ili kuzuia
umati watu wasilisogelee eneo
lile.Taarifa za kutokea kwa ile
ajali zilianza kusambaa katika
mitandao ya kijamii kama moto
wa nyika na watu wakaanza kufika eneo lile hasa baada ya
taarifa hizo kueleza kuwa
mbunge Edger Kaka ni
miongoni mwa wanaodaiwa
kufariki katika ajali hiyo mbaya.
Miili ya watu waliokuwemo
katika magari yale yaliyoungua
moto ikaanza kutolewa na
haikuwa rahisi kutambulika
kwani walikuwa wameungua
vibaya sana.Mwili ambao
ulidaiwa kuwa wa Edger
uliweza kutambuliwa kwa kuwa
ulikuwa na mkufu wenye kidani
chenye herufi E pamoja na pete
za kidoleni zote zikiwa na herufi E ikiwa ni herufi ya kwanza ya
jina lake.Miili yote ilichukuliwa
na kupelekwa hospitali
kuhifadhiwa.
Olivia Themba ambaye
ndiye aliyekuwa na Edger
nchini Israel alimuomba baba
yake amkimbize hospitali
ilikopelekwa miili ya marehemu
ili kuhakiki kama taarifa zile za
Edger kufariki katika ajali ile ni
za kweli.Huku akimwaga
machozi mengi aliweza
kuutambua mwili wa Edger
kutokana na mkufu ule
aliokuwa amevaa wenye kidani chenye herufi E pamoja na pete
za mkononi.Aliwahakikishia
watu kwamba mwili ule ni wa
Edger Kaka kwani mkufu ule
alikuwa ameuvaa toka wakiwa
Israel.Taarifa za kifo cha Edger
zililistua taifa
BAADA YA MIAKA MIWILI

Tayari imekwisha pita
miaka miwili toka lilipotokea
shambulio la bomu jijini
Dodoma lililomuua waziri mkuu
wa Tanzania na watu wengine
kadhaa.Kwa kipindi hiki chote cha miaka miwili bado vyombo
vya uchunguzi havikuwa
vimefanikiwa kuwapata watu
waliofanya shambulio lile la
kigaidi.katika kipindi hicho cha
miaka miwili ,uchaguzi mkuu
wa rais na wabunge ulifanyika
na Dr Evans Mwaluba
akashinda uchaguzi huo kwa
kura nyingi kwani hakupata
upinzani mkubwa.Watu pekee
aliokuwa akiwahofia ni Damian
Mwamba na Edger kaka ambao
wote walifariki dunia.
Kifo cha Edger kaka bado
kiliendelea kuzua maswali mengi namna
kilivyotokea.Kulikuwa na
maswalimengi yaliyokosa
majibu kuhusiana na ajali ile
lakini kilichowashangaza zaidi
watu ni na hata wachunguzi wa
ajali ile ni kupotea kwa familia
ya dereva wa lori lililosababisha
ajali ambayo haikujulikana
mahala ilipo.
Ni siku ya jumanne Dr
Olivia Themba akiendelea na
majukumu yake ya
kazi,akapewa taarifa kwamba
ana mgeni wake.Alipomaliza
kuzungumza na mgonjwa akaenda katika sehemu ya
mapumziko kwa madaktari na
kuagiza mgeni wake apelekwe
kule.Kijana mmoja nadhifu
aliyevaa suti nzuri ya kijivu
akajitokeza na kumfuata Dr
Olivia ambaye alimtazama
kijana hakuwa akimfahamu
“Hallo” akasema Dr Olivia
kijana yule akavua miwani
aliyokuwa amevaa
akatabasamu
“Hallow Dr Olivia habari
yako” akasema yule jamaa “Habari yangu
nzuri”akajibu Dr Olivia huku
naye akitabasamu.
“Dr Olivia naamini ni mara
yetu ya kwanza kuonana”
akasema yule jamaa
“Sina kumbukumbu kama
tumewahi kuonana hapo kabla
lakini mwenzangu unaonekana
kunifahamu vizuri” akasema Dr
Olivia
“Naitwa Oscar Benard ni
meneja wa Loll’s Hotel”akasema
Oscar
“Loll’s Hotel ninaifahamu”
akasema Olivia “Unakaribishwa sana Dr
Olivia kutembelea hoteli yetu
kupumzika na kupata chakula”
akasema Oscar
“Nafurahi kukufahamu
Oscar,nikusaidie nini?akauliza
Dr Olivia
“Nimekuja hapa kuonana
nawe kwa shida mahsusi
kabisa”
“Karibu” akasema Olivia
“Katika hoteli yangu
amekuja mgeni toka nje ya nchi
ni tajiri na amekuja maalum
kwa ajili ya kuonana nawe” akasema na Dr Olivia
akaonyesha mstuko
“Amekuja kuonana na
mimi? Ni nani huyo?Akauliza
“Ndiyo amekuja kuonana
nawe.Amenipa maelezo mafupi
tu kwamba yeye ni ndugu wa
Edger kaka hivyo anahitaji
kukuona kuna mambo anataka
kuzungumza nawe
yanayomuhusu Edger”akasema
Oscar
“Ndugu wa Edger kaka?Dr
Olivia akashangaa
“Ndiyo anasema yeye ni
ndugu wa Edger Kaka” “Anaitwa nani huyo mtu na
ametokea wapi? akauliza Dr
Olivia akionekana kuwa na wasi
wasi
“Dr Olivia kazi yangu mimi
ilikuwa kufikisha ujumbe
kwako kwamba kuna ndugu wa
Edger Kaka amekuja na
anahitaji kuzungumza nawe
kuna jambo muhimu
sana.Ninasubiri jibu kama uko
tayari kuonana naye
mkazungumza au hauko tayari”
akasema Oscar
“Oscar ninashindwa kutoa
jibu kwa sasa kwani simfahamu mtu huyo ni nani na
amenifahamuje mimi hadi
akafunga safari kutoka huko
alikotoka kunifuata mimi huku
Tanzania.Isitoshe mimi si
ndugu wa Edger kwa nini
anifuate mimi badala ya
kuwatafuta ndugu zake?Kwa
nini yeye mwenyewe asinifuate
hapa kazini akanieleza hilo
analotaka kunieleza?akauliza Dr
Olivia
“Dr Olivia,mgenihuyo si
mtu mdogo.Ni bilionea mkubwa
na anafahamu kwamba hapa si
sehemu ya maongezi ni sehemu ya kazi ndiyo maana akahitaji
kupata muda maalum wa
kuzungumza nawe.Nakuona
una wasiwasi sana.Usihofu
tafadhali hakuna chochote
kibaya.Usalama upo wa kutosha
katika hoteli yetu” akasema
Oscar na Dr Olivia akazama
katika tafakari kisha akasema
“Edger hakuwahi
kuniambia chochote kama ana
ndugu yake tajiri nje ya
nchi.Mtu huyo kama kweli
nindugu yake kwa nini
hakuwahi kuja kumuona
hospitali nchini Israel wakati Edger anaumwa? Kwa nini
hakujitokeza katika msiba wa
Edger? Akauliza Olivia
“Olivia maswali hayo ni
yeye mwenyewe anayepaswa
kuyajibu,mimi kazi yangu ni
kufikisha ujumbe kuwa anataka
kuonana nawe.Nakusihi
ukaonane naye tafadhali kwani
amekuja kuonana nawe lazima
ana jambo la muhimu sana
anataka kukueleza.Mimi ni
meneja wa hoteli ile kubwa
lakini nimelazimika kuacha
majukumu yangu yote na kuja
kuonana nawe.Nisingeweza kuja hapa kama nisingekuwa na
uhakika kwamba ana jambo la
muhimu la
kukueleza.Ninakushauri Olivia
nenda ukaonane naye”akasema
Oscar na kumfanya Dr Olivia
azame katika mawazo
“Dr Olivia please !!
akasisitiza Oscar
“Anataka nikaonane naye
wapi na muda gani? Dr Olivia
akauliza
“Utakutana naye leo jioni
pale pale hotelini” akasema
Oscar “Sawa Oscar nitafika hapo
hotelini kuonana naye
jioni.Nimeamua kuja kuonana
naye kwa sababu ya
kukuheshimu wewe”akasema
Dr OLivia
“Ahsante sana Dr OIivia
ninakuhakikishia kwamba
hautajutia muda wako.Usafiri
utakuja nyumbani kwako
kukuchukua”
“Tafadhali nitatumia gari
langu kuja hapo hotelini
kuonana na huyo mgeni
asiyekuwa na jina” “Tafadhali Olivia wewe ni
mgeni muhimu wa mgeni wetu
mkubwa hivyo mimi ndiye
nitakayehakikisha
nitashughulikia kila kitu kuhusu
wewe kuonana na huyo mtu
wako.Litakuja gari saa moja
jioni nyumbani kwako
kukuchukua kukupeleka
hotelini” akasema Oscar
wakaagana akaondoka
“Edger hakuwahi kunieleza
kama ana ndugu yake tajiri nje
ya nchi.Nilikaa naye hospitali
kwa muda mfupi lakini
sikuwahi kumsikia akizungumzia suala la familia
yake.Niliwahi kumuuliza suala
hilo la ilipo familia yake lakini
hakunijibu chochote na
hakutaka kabisa kuliongelea
suala hilo.Huyu aliyejitokeza na
kudai kwamba yeye ni ndugu
wa Edger ametoka
wapi?Ametokea nchi gani?Kwa
muda huu wote alikuwa wapi
hadi aibuke leo?Alipofariki
ilibainika kwamba hakuwa na
ndugu wengine kwani ndugu
zake walikwisha fariki wote
huyu katokea wapi? Dr Olivia
akajiuliza maswali mengi kuhusiana na mtu huyo
anayedai ni ndugu wa Edger
Kaka
“Nitakwenda kuonana naye
huyo mtu nifahamu kuhusu
undugu wake na Edger ni
undugu wa namna gani na kwa
nini amejitokeza sasa”akawaza
Dr Olivia.

*****************
Saa moja za jioni kama
alivyoahidiwa,likafika gari
kumchukua Dr Olivia
kumpeleka akaonane na mgeni wake ambaye hadi muda huo
hakuwa akimfahamu.Bado
kichwa chake kilijaa mawazo
kuhusiana na mtu huyo
anayekwenda kuonana naye.
Alitoka ndani na kuingia
katika gari lililokuja kumchukua
akaondoka kuelekea Loll’s
hotel.
“Huyu mtu ametokea na
kunikumbusha mambo mengi
kuhusu Edger
Kaka.Nilifahamiana naye kwa
muda mfupi na tukajikuta
tukiwa na ukaribu mkubwa
japo kuna wakati tuliwahi kuingia katika sintofahamu pale
aliponitamkia kwamba
ananipenda.Alinieleza ukweli
wake na kabla hatujaendelea
zaidi na ukaribu wetu akafariki
dunia kwa kifo cha kikatili
sana.Inaniumiza kila
nikimkumbuka ninaona kama
alinipa mkosi kwani toka
alipofariki ni miaka miwili sasa
hajawahi kujitokeza
mwanaume mwingine ambaye
amewahi kunitamkia kwamba
ananipenda.Yawezekana Edger
alikuwa ndiye chaguo langu
nililopewa na Mungu lakini hatukupata nafasi ya kuwa
pamoja.Laiti angekuwa hai
labda hivi sasa tungekwisha
ingia katika mahusiano na
yawezekana tungekwisha funga
ndoa kwani hata mimi tayari
nilianza kuvutiwa naye japo
sikuwa tayari kumueleza”
akawaza Dr Olivia akiwa garini
akielekea Loll’s Hotel.
“Miaka miwili sasa toka
afariki lakini bado uchunguzi
wa ajali ile haujakamilika.Suala
hili limebaki hewani mpaka leo
haijulikani kama ile ilikuwa ni
ajali au ni moja kati ya mipango ya maadui zake ya
kumuua.Yawezekana ajali ile
ikawa ni moja ya mpango wao
wa kummaliza baada ya
kushindwa kumuua kwa
sumu.Nilimkatalia Edger
kwamba asirejee nyumbani
mapema kwa ajili ya usalama
wake hakutaka kunisikia.Huyo
ndugu yake ambaye hakuwahi
kujitokeza hata katika msiba
amefahamuje kama nilikuwa na
ukaribu na Edger? Akajiuliza
Olivia.
Gari lilifika Loll’s
hotel,mlango ukafunguliwa Dr Olivia akashuka akapokewa na
Oscar
“Karibu Olivia.Umependeza
sana usiku wa leo” akasema
Oscar huku akimshika mkono
Olivia na kumuongoza kuelekea
ndani
“Oscar nimekuja hapa usiku
huu kwa sababu yako tafadhali
naomba suala lililonileta hapa
liwe ni suala la
msingi.Nitasikitika sana kama
kilichonileta hapa ni mambo
tofauti na Edger” akasema Dr
Olivia “Nashukuru kwa kuniamini
Olivia.Nisingeweza kukuomba
ufike hapa kama kusingekuwa
na suala la muhimu” akasema
Oscar
Walipanda lifti hadi ghorofa
ya ishirini na tatu wakashuka
na kuelekea katika chumba
chenye hadhi ya rais.Kulikuwa
na walinzi wawili mlangoni
waliovalia nadhifu
kabisa,mmoja akafungua
mlango Oscar na Dr Olivia
wakaingia ndani ya chumba kile
kikubwa na kizuri.Mtu mmoja
mwenye asili ya kiarabu aliyevalia suti nzuri nyeusi
akasimama huku akitabasamu
akawakaribisha ndani
“Karibuni wageni
wangu”akasema yule jamaa
“Ahsante sana” akajibu
Oscar halafu akamgeukia Dr
Olivia
“Olivia kutana na Abu dahir
mfanya biashara anatokea
nchini Saudi Arabia na ndiye
mgeni wako uliyekuja kuonana
naye usiku wa leo”akasema
Oscar na kumstua Dr Olivia
“Abu Dahir kutana na Dr
Olivia Themba huyu ndiye aliyeyaokoa maisha ya Edger
kaka kwa kumpeleka nchini
Israel” akasema Oscar
“Ahsante sana Oscar kwa
kumleta malaika huyu ambaye
ninahitaji sana kumuona”
akasema Abu dahir na kupeana
mkono na Oscar
“Dr Olivia I’ll be
outside.Tafadhali usihofu kitu”
akasema Oscar na kutoka
“Olivia karibu sana jisikie
amani.Najua una hofu kubwa
lakini nakuomba ondoa hofu
uko salama.Utatumia kinywaji
gani?akauliza Abu dahir “Ahsante nitatumia
maji”akajibu Dr Olivia na Abu
dahiri akammiminia maji katika
glasi
“Olivia naomba kwanza
nikushukuru sana kwa kukubali
kuonana nami japo
hunifahamu” akasema Abu
dahir
“Niliambiwa maongezi ni
kuhusu Edger Kaka ndiyo
maana nikakubali kuja kuonana
naye.Wewe ni nani?akauliza Dr
Olivia
“Mimi kama alivyokueleza
Oscar ninaitwa Abu dahir ni mfanya biashara ninaishi Saudi
Arabia kwa sasa,baba yangu
anatokea Palestina lakini mama
yangu anatokea Saudi
Arabia.Ninafanya biashara
mbali mbali lakini kubwa ni
biashara ya mafuta.Nina visima
vya mafuta katika nchi za Iraq
na Saudi Arabia” akasema Abu
“Abu naomba tujielekeze
moja kwa moja katika suala la
msingi lililotukutanisha hapa
ambalo ni Edger.Unahusiana
vipi na Edger? Hakuwahi
kuniambia kama ana ndugu
yake tena mwenye asili ya arabuni.Ulikuwa wapi muda
huu wote haukujitokeza hadi
sasa?akauliza Olivia
“Dr Olivia nitakueleza kila
kitu lakini kwanza
nakukaribisha tusipate chakula
nilichokiandaa maalum kwa
ajili yako halafu tutazungumza”
akasema Abu dahir na kuinuka
akamuongoza Dr Olivia katika
chumba cha chakula ambako
kulikuwa na meza
iliyotawanywa vyakula
vingi.Akamvutia kiti Dr Olivia
akaketi
 
SIRI
episode 23
Mtunzi. Patrick CK

“Karibu Dr Olivia” akasema
Abu ambaye alionekana ni mtu
mstaarabu sana.Dr Olivia
akaweka chakula kidogo katika
sahani na kumtazama Abu
“Nadhani tuendelee na
maongezi.Nilikuuliza kuhusiana
na mahusiano yako na Edger
Kaka.Hakuwahi kunieleza kama
ana ndugu yake tena ana asili ya
kiarabu” akasema Dr Olivia
“Dr Olivia kwanza kabla
sijakujibu swali lako nataka
nitumie nafasi hii kukushukuru
sana kwa kukayaokoa maisha
ya Edger.Kama si wewe Edger angefariki dunia”akasema Abu
dahir.Dr Olivia akala vijiko
kadhaa na kusema
“Siku zote daktari
anayeifahamu vyema kazi yake
atafanya kila linalowezekana
kuhakikisha kwamba mgonjwa
wake anapona na ndivyo
nilivyofanya kuhakikisha
kwamba Edger anapona”
akasema Dr Olivia
“Dr Olivia uliniuliza kuhusu
mahusiano yangu na Edger
kaka.Mimi na Edger ni
ndugu.Edger ni kaka yangu”
akasema Abu dahir na uso wa Olivia ukaonyesha mshangao
mkubwa
“Sijakuelewa Abu.Wewe na
Edger undugu wenu
ukoje?akauliza Dr Olivia kwa
mshangao
“Kama nilivyokueleza
kwamba Edger ni ndugu
yangu.Ni kaka yangu.Najua
unajiuliza inawezekanaje mimi
na yeye tukawa ndugu wakati
yeye ni mwafrika na mimi
ninaonekana kama mwarabu?
Akauliza Abu na kucheka
kidogo “Mimi si mwarabu kwa
asilimia mia moja
nimechanganya damu.Kwa
ufupi ni kwamba mimi na Edger
mama yetu ni mmoja”akasema
Abu na Dr Olivia akaweka kijiko
chini akamtazama
“Inavyojulikana wazazi
wote wa Edger
wamekwishafariki dunia na
wote walikuwa watanzania
iweje wewe na Edger mama
yenu awe mmoja?
“Dr Olivia nitakueleza
ukweli halisi lakini naomba kile
nitakachokueleza kisikustue.Nimeamua
kukueleza ukweli kwa sababu
ninakuamini” akasema Abu na
kunyamaza kidogo halafu
akasema
“Mama yake Edger au
mama yetu anaitwa Habiba
Jawad.Ni mzaliwa wa Kenya
lakini asili yake ni
Somalia.Aliolewa na Nasser
Jawad mfanya biashara
mkubwa nchini Kenya na
wakafanikiwa kumpata mtoto
mmoja tu ambaye ni
Edger.Alipofikisha umri wa
miaka mitano Edger akahamishiwa nchini Tanzania
akiwa chini ya uangalizi wa
mama mmoja anaitwa
Genevieve msika.Jina halisi la
Edger kaka ni Seif
Jawad.Alipohamishwa kutoka
Kenya kuja Tanzania
akabidilshwa jina na kuitwa
Edger Kaka akachukua jina la
baba yake mlezi aliyeitwa Eliud
kaka” akasema Abu na Olivia
akamkatisha
“Subiri kidogo Abu naona
unazidi
kunichanganya.Unasema
kwamba jina halisi la Edger kaka ni Seif jawad na jina Edger
alipewa alipohamishiwa
Tanzania.Nini sababu ya wazazi
wake kumuhamishia nchini
Tanzania?
“Seif kuhamishiwa
Tanzania kulikuwa na sababu
maalum na utaifahamu huko
mbeleni”akasema Abu na
kupiga vijiko kadhaa akafuta
mdomo kwa kitambaa
akaendelea
“Nataka umfahamu
kiundani Edger kaka ni nani na
kwa nini ninakueleza haya yote”
akasema Abu dahir “Nasser Jawad baba yake
mzazi Edger alifariki dunia kwa
ugonjwa wa saratani.Nasser
alipofariki dunia Habiba
aliolewa na mwanaume
mwingine ambaye ni baba
yangu anaitwa Abdul
dahir.Baba alikuwa tajiri sana
hivyo akamuhamisha mama
kutoka Kenya wakaenda nchini
Saudi Arabia na ndipo
nilipozaliwa mimi hivyo Edger
ni kaka yangu.Utofauti wetu ni
kwamba baba yangu mimi
alikuwa mwarabu na baba yake
Edger alikuwa mweusi” akanyamaza kidogo na
kumtazama Olivia,akaendelea.
“Baba yangu aliuawa na
vikosi vya Israel wakimtuhumu
kuhusika katika kufadhili
vikundi vya kigaidi ambavyo
vimekuwa vikiendesha
operesheni zake nchini Israel na
kuua raia” akasema Abu
dahir.Macho ya Dr Olivia
yalizidi kuonyesha woga
“Ni kweli alikuwa anafadhili
makundi hayo ya kigaidi?
akauliza Dr Olivia
“Hakuna ushahidi wa moja
kwa moja kwamba alikuwa anafadhili makundi hayo ya
kigaidi lakini baba ni mmoja wa
watu waliokuwa mstari wa
mbele sana katika kupigania
haki za wapalestina na ndiyo
sababu ya kuuawa
kwake.Tuachane na hayo
tujielekeze zaidi katika suala
lililotukutanisha hapa kuhusu
Edger kaka” akasema Abu na
kunyamaza kidogo
“Dr Olivia wewe ndiye
uliyempeleka Edger Israel na
ukayaokoa maisha yake na
baada ya hali yake kuwa nzuri
mkarudi wote Tanzania lakini hakuweza kufika nyumbani
kwake akafia njiani.Unaweza
ukanipa picha kidogo ya namna
tukio lile lilivyotokea? Akauliza
Abu dahir.Swali lile lilimfanya
Dr Olivia kuacha kabisa kula
chakula kwani lilimkumbusha
mbali sana usiku ule ambao
alishuhudia moto mkubwa
ukiwaka na ndani ya moto ule
Edger Kaka aliteketea.Machozi
yakamtoka
“Samahani Dr Olivia.Najua
nimekukumbusha mbali sana”
akasema Abu dahir “Ni kweli Abu
nimekumbuka mbali
sana.Kumbu kumbu ya tukio lile
imenitesa kwa muda mrefu
sana na kuna nyakati nikiwa
peke yangu kumbukumbu ile
hunijia kichwani na kuniumiza
sana.Ni moja ya kumbu kumbu
ambayo ninajaribu sana
kuitafuta kichwani kwangu”
akasema Dr Olivia na kufuta
machozi akaendelea
“Tulipokea taarifa kutoka
bungeni Dodoma kwamba
mbunge Edger kaka analetwa
kwa matibabu katika hospitali yetu.Tulimpokea akiwa katika
hali mbaya na baada ya jitihada
za kumuhudumia ilionekana
kwamba ugonjwa wake
unahitaji matibabu zaidi nje ya
nchi.Hospitali yetu ina
ushirikiano mkubwa na
hospitali ya Rambam iliyoko
Haifa Israel tuliwasiliana nao
wakakubali tumpeleke huko
lakini baada ya kulifikisha suala
hili kwa viongozi wake zilianza
sarakasi na badala ya
kukubaliana na pendekezo letu
la kumpeleka Edger nje ya nchi
wakafanya mpango ahamishwe kupelekwa katika hospitali ya
Muhimbili.Mimi kama daktari ni
jukumu langu kufanya kila lililo
ndani ya uwezo wangu
kuhakikisha kwamba ninaokoa
maisha ya mgonjwa hivyo
nilitumia nafasi yangu na uwezo
wangu kuhakikisha kwamba
Edger anasafirishwa kwenda
Israel.Baba yangu na rais ni
marafiki wakubwa tangu utoto
wao hivyo nilimtumia baba
kumuomba rais atumie uwezo
wake kumsaidia Edger na rais
akakubali akazungumza na
mamlaka za Israel na Edger akaruhusiwa kuingia Israel.Rais
Dr Evans alitoa ndege yake
ambayo ilitupeleka nchini
Israel” Akanyamza akavuta
pumzi kidogo halafu akaendelea
“Baada ya kufika nchini
Israel vipimo vilionyesha
kwamba aliwekewa sumu.Kama
unavyojua Edger alikuwa na
maadui wengi hivyo walijaribu
kumuua kwa sumu ile ambayo
inahisiwa kwamba ilipakwa
katika sabuni ya kuogea.Tukiwa
Israel na hali yake ikiendelea
vyema tulipata taarifa za
kuuawa kwa waziri mkuu katika mlipuko wa bomu na
jambo hili lilimuumiza sana
Edger kwani alikuwa ni mtu
mwenye msaada mkubwa
kwake katika mambo ya siasa
hivyo akapanga lazima
ahudhurie mazishi
yake.Nilijaribu kumzuia
asiondoke Israel asubiri hadi
atakapopona kabisa lakini
aliendelea na msimamo wake
kwamba lazima akahudhurie
mazishi ya waziri mkuu hivyo
tukajiandaa na kuondoka.Ndege
tuliyosafiri nayo ilipata hitilafu
ya kiufundi hivyo tukachelewa sana kufika Tanzania.Badala ya
kufika saa sita za mchana
tukafika saa sita usiku na Edger
hakuweza kuwahi mazishi ya
kitaifa ya waziri mkuu kama
alivyokuwa ametarajia.Baada ya
kushuka ndegeni tuliagana kwa
miadi ya kukutana tena siku
inayofuata na Edger akaondoka
uwanjani pale na watu wake
waliokuja kumpokea.Kilometa
chache baada ya kuondoka pale
uwanjani ndipo ilipotokea ajali
ile iliyochukua uhai wa Edger”
akasema Dr Olivia “Pole sana kwa
kumbukumbu hii yenye
kusikitisha.Bado kuna kitu
nataka kukifahamu kama
hutajali.Nataka kupata walau
picha ya namna ya ajali ile
ilivyotokea”akasema Abu dahir
“Sifahamu nini kilitokea
kwani Edger aliwahi kuondoka
pale uwanjani na mimi nilifuata
muda mfupi baadae na nilikuta
ajali tayari imetokea na moto
mkubwa
unawaka.Nilipoambiwa
kwamba magari ya msafara wa
Edger ndiyo yaliyopata ajali sikuamini na baada ya miili
kutolewa nikalazimika kwenda
hospitali kuhakikisha kama ni
kweli Edger amefariki dunia na
mimi ndiye niliyefanikisha
kuutambua mwili wake
uliokuwa umeungua vibaya
sana na kilichonisaidia
kuutambua mwili wake ni
mkufu aliokuwa amevaa
shingoni wenye kidani chenye
herufi E na pete alizokuwa
amevaa vidoleni.Hivyo ndivyo
ilivyotokea na Edger akapoteza
maisha” akasema Dr Olivia na
kuinama.Abu dahir akafuta mdomo kwa kitambaa kisha
akasema
“Ahsante sana Dr Olivia
kwa taarifa hii
uliyonipa.Nilihitaji sana
kufahamu kilichotokea na
kuondoa uhai wa kaka yangu”
akasema Abu na kimya kifupi
kikapita halafu akauliza
“Unadhani kwa nini mpaka
leo hii hakuna maelezo ya
kueleweka kuhusiana na ajali
ile namna ilivyotokea? Kwa nini
suala hili limebaki likielea?
akauliza Abu dahir “Hilo suala hata mimi
limekuwa linaniumiza sana
kichwa kwani hakuna taarifa
zozote mpaka sasa kuhusiana
na suala hili.Limekuwa ni suala
lililokosa ufumbuzi hadi leo”
“Unahisi Edger
aliuawa?akauliza Abu
“Ninahisi hivyo kutokana
na mazingira ya tukio
lenyewe.Edger alikuwa na
maadui wengi na ndiyo maana
walijaribu kumuua kwa sumu
wakamkosa.Naamini maadui
zake ndio waliopanga ajali ile siamini kama lile ilikuwa tukio
la bahati mbaya”
“Kwa nini unaamini hivyo
Olivia?Abu akauliza
“Ni kutokana na mazingira
yenyewe ya namna tukio
lilivyotokea.Kwa mfano mpaka
leo familia ya dereva wa lile lori
la mafuta lililosababisha
ajali,inandelea kutafutwa na
hawajulikani walipo.Kwa nini
wapotee ghafla?Wako
wapi?Nao wameuawa pia?Usiku
ule dereva yule alikuwa
anaelekea wapi? Haya ni baadhi
tu ya maswali ambayo yanaumiza kichwa sana na
yamekosa majibu mpaka leo na
ndiyo yanayonifanya niamini
kwamba ajali ile ilipangwa”
akasema Dr Olivia.Ukapita
ukimya wa dakika mbili Abu
dahir akasema
“Olivia ulikuwa ni mtu wa
karibu sana wa Edger na
kuanzia sasa utakuwa mtu
wangu wa karibu pia.Kuna
jambo nimekuja kukueleza
ambalo naamini litakustua
lakini nakuomba usistuke sana”
akasema Abu
“Jambo gani Abu? “Edger hajafa” akasema
Abu dahir.Dr Olivia
akamtazama kwa mshangao
mkubwa
“Sijakuelewa unamaanisha
nini” akasema Dr Olivia
“Edger hajafariki dunia
kama inavyoaminika”akasema
Abu dahir.Dr Olivia akasimama
“Si kweli Abu.Hizo ni hisia
tu lakini ukweli ni kwamba
Edger amefariki dunia na mimi
ndiye niliyeutambua mwili
wake” akasema Dr Olivia
“Tafadhali keti Dr Olivia”
akasema Abu na Olivia akaketi “Nikwambiacho ni kitu cha
kweli kabisa,Edger hajafa kama
inavyodaiwa.Tunazo kila
sababu za kuamini kwamba
Edger hakufa katika ile
ajali”akasema Abu
“Sikuelewi abu kwa nini
unaamini hivyo? Mimi ndiye
niliyekuwepo eneo la tukio na
ndiye niliyeutambua mwili
wake na tukauzika bila ndugu
yeyote kujitokeza.Iweje leo
ujitokeze na kudai kwamba
ndugu yako yuko hai?akauliza
Dr Olivia akionekana kukasirika “Dr Olivia nafahamu hili ni
suala ambalo litakustua sana
lakini huo ndio ukweli
wenyewe kwamba Edger ni
mzima hajafa.Kilichofanyika ni
mpango wa hali ya juu sana
ambao ulifanywa na majasusi
wa hali ya juu na kuiaminisha
dunia kwamba Edger amefariki
dunia lakini kumbe bado yuko
hai” akasema Abu
“Abu hapo ndipo
unaponichanganya.Kwa nini
unasisitiza kwamba Edger yuko
hai? Kama unadai kwamba ajali
ile ilikuwa ni mpango mzito nani waliofanya mpango huo na
kwa nini?Kama yuko hai yuko
wapi?akauliza Dr Olivia
“Olivia nisingeweza kuja
kwako kukupa taarifa hizi
kwamba Edger yuko hai kama
nisingekuwa na uhakika na
ushahidi wa kutosha wa
kulithibitisha suala hilo lakini
naomba uamini kwamba ni
kweli Edger yuko hai na
hakufariki dunia katika ile ajali
kama inavyodaiwa”
“Yuko wapi? akauliza Dr
Olivia “Dr Olivia hata sisi hatujui
mahala alipo Edger lakini
tunaamini yuko hai.Kuna
mambo kadhaa ambayo
itatulazimu kuyafanya katika
kuutafuta ukweli wa mahala
alipo Edger.Olivia ili kufahamu
ukweli kuhusiana na suala hili
la Edger na mahala alipo
tunakutegemea sana
wewe”akasema abu dahir na Dr
Olivia akaangua kicheko kidogo
“Abu unanishangaza
sana.Umeniletea taarifa
kwamba Edger hajafa yuko hai
halafu unasema tenba kwamba hujui mahala alipo na unahitaji
msaada wangu.Ninashindwa
kukuelewa nini hasa lengo lako
kwangu” akasema Dr Olivia
“Olivia sisi kama familia
tuna hakika Edger hajafa bali
alichukuliwa na anashikiliwa
sehemu Fulani na tunao
ushahidi wa kuamini
hivyokwamba Edger yuko hai
hata hivyo tunataka kuanza
mchakato wa kuutafuta ukweli
kuhusu Edger na wewe ndiye
mtu ambaye tunakutegemea
sana katika mchakato
huo.Uliyaokoa maisha yake mara ya kwanza bila kuombwa
na mtu yeyote lakini safari hii
ninakuomba ukubali tena
kumsaidia Edger.Huko aliko
hatujui ni mateso gani
anayapitia,hatujui maisha yake
yakoje.Tafadhali Dr Olivia
ninahitaji sana msaada wako”
akasema Abu dahir .Baada ya
kufikiria kidogo Dr Olivia
akauliza
“Unataka nikusaidie nini
Abu dahir?
“Kuna hatua tatu tutazipitia
hadi kuupata ukweli kuhusu
Edger.Tutaanza na hatua ya kwanza lakini kabla ya hatua
hiyo itakulazimu kufanya kitu
kimoja” akasema Abu
“Kitu gani unataka
nikifanye?akauliza Dr Olivia
“Itakulazimu uachane na
kazi unayoifanya sasa”
“Nini?akauliza Dr Olivia
kwa sauti ya ukali
“Usistuke Dr Olivia.Tulia
nisikilize hadi nimalize kile
ninachotaka kukueleza”
akasema Abu
“Umenistua sana kuniambia
eti niachane na kazi
ninayoifanya sasa.Wewe ni nani wa kuniamuru kuacha kazi
ninayoipenda?akasema Dr
Olivia
“Samahani kwa kukustua
Dr Olivia lakini unapaswa
unisikilize hadi mwisho.Nataka
uachane na kazi hii unayoifanya
sasa na badala yake utafungua
kituo kikubwa cha kufanya tafiti
za magonjwa mbali mbali ya
binadamu na wanyama
ambacho kitakuwa ni kikubwa
katika ukanda huu wa afrika
mashariki na kati.Gharama zote
za ujenzi wa kituo hicho
zitatoka kwangu na hautatumia hata shilingi yako moja ila
utakachokifanya ni kuanzisha
taasisi yako ambayo mimi na
wenzangu tutachangia fedha
ambazo utazitumia katika
ujenzi wa kituo hicho kikubwa
ambacho kikikamilika kitakuwa
mkombozi mkubwa sana kwa
watu wa ukanda huu kwani
utafiti wa magonjwa mbali
mbali utafanyika kupitia kituo
hicho.Baada ya hatua ya kwanza
kukamilika ambayo ni ujenzi wa
kituo hicho ndipo itafuata hatu
aya pili”akasema Abu dahir Haikuwa rahisi kwa Dr
Olivia kukubaliana na kile
alichokisema Abu dahir.Baada
ya mjadala mzito uliochukua
masaa zaidi ya mawili,hatimaye
Dr Olivia akakubali ombi la Abu
dahir la kuachana na kazi katika
hospitali kuu ya taifa ya moyo
na kuanzisha kituo kile cha
utafiti.Baada ya mazungumzo
yale marefu wakaagana na Dr
Olivia akaondoka
“Kuna ule msemo usemao
ukistaajabu ya Musa utayaona
ya Firauni.Haya aliyonieleza
Abu dahir kwamba Edger hajafariki dunia yamenistua
sana.Kama ni kweli ni maajabu
makubwa
kwangu.Inawezekanaje wakati
mimi ndiye niliyeutambua
mwili wa Edger hospitali na
niliweza kuutambua kutokana
na mkufu aliokuwa ameuvaa
iweje leo niambiwe eti Edger
hakufa na yuko hai?akajiuliza
Dr Olivia akiwa ndani ya gari
akirejeshwa nyumbani kwake
baada ya kutoka kuonana na
Abu dahir.
“Mwili wangu
unanitetemeka kila nikifikiria jambohili.Kama ni kweli Edger
hajafariki dunia yuko wapi?I’m
confused.Sitakiwi kuendelea
kulifirikiria suala hili kwani
litaniathiri sana
kisaikolojia.Kwa sasa ngoja
nielekeze nguvu katika ujenzi
wa kituo hicho cha utafiti
alichoelekeza Abu dahir.Nini
hasa malengo ya kujenga kituo
hiki hapa Tanzania? Kituo hicho
kina mchango gani katika
kumtafuta Edger? Nimekubali
maombi yake kwa ajili ya Edger
lakini kituo hicho pia kinaweza
kuwa na msaada mkubwa sana katika kufanya uchunguzi wa
magonjwa mbali mbali ya
binadamu na wanyama hasa
haya yanayoibuka mara kwa
mara na kuyatafutia tiba.Sioni
tatizo kujenga kituo hicho kwa
sababu sintantumia hata senti
yangu moja” akaendelea
kuwaza Dr Olivia
“Kwa nini wazazi wa Edger
walimleta Tanzania wakati
walikuwa na uwezo wa kumlea
na kumsomesha nchini
Kenya?Abu dahir aliniambia
kwamba Edger alihamishiwa
Tanzania kwa shughuli maalum.Ni shughuli gani hiyo?
Kwa nini hakutaka kuiweka
wazi? Kuna mambo mengi
yamejificha kuhusu Edger
ambayo natakiwa kuyajua”
akawaza Dr Olivia
MWAKA MMOJA - BAADAE
Ujenzi wa kituo kikubwa
kabisa cha utafiti wa magonjwa
ya binadamu na wanyama
kilichojengwa nje kidogo ya jiji
la Dar es salaam
ulikamilika.Kilikuwa ni kituo
kikubwa na cha aina yake katika ukanda wa afrika mashariki na
kati.Ujenzi wa kituo hicho
uligharimu fedha nyingi ambazo
zilichangwa na wafadhili wa
taasisi ya Olivia trust.
Kituo hicho cha aina yake
cha utafiti kilifunguliwa na rais
wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania na kazi za utafiti
zikaanza mara
moja.Wanasayansi wengi
kutoka ndani na nje ya nchi
waliajiriwa katika kituo hicho
na magonjwa mbali mbali ya
wanadamu na wanyama
yalifanyiwa utafiti na kupatiwa tiba yake.Ndani ya miezi sita ya
mwanzo tayari magonjwa zaidi
ya matano yalikwisha fanyiwa
utafiti na kutafutiwa
tiba,mafanikio ya kituo hiki
yalianza kuonekana
Miezi sita baada ya
kukamilika kwa kituo kile Dr
Olivia aliitwa na Abu dahir
nchini Saudi Arabia kwa ajili ya
mazungumzo.Siku mbili baada
ya kuwasili nchini Saudi Arabia
akachukuliwa na kupelekwa
kuonana na Abu
dahir.Wamekuwa
wakiwasiliana mara kwa mara lakini haya yalikuwa ni
mazungumzo maalum
kabisa.Alikaribishwa katika
himaya ya Abu dahir na
kutambulishwa kwa familia
yake kisha akamchukua hadi
katika nyumba iliyokuwa
pembeni ya jumba lake ambako
kulikuwa na ulinzi mkali
wakaingia ndani na kumkuta
mwanamke mmoja mtu mzima
aliyejitanda vito vya dhahabu.
“Dr Olivia karibu
sana,kutana na Habiba
Jawad.Huyu ndiye mama yangu
na ndiye mama yake Seif Jawad au Edger Kaka kama
anavyofahamika”Abu dahir
akafanya utambulisho.
“Mama kutana na Dr Olivia
Themba huyu ndiye
aliyeyaokoa maisha ya Seif kwa
kumpeleka Israel na ndiye
aliyekuwa naye hadi siku ya
mwisho alipopotea” akasema
Abu na Habiba akatabasamu.Dr
Olivia akamsogelea na kwa
adabu akapiga magoti
akamsalimu yule mama ambaye
alimshika mkono akamuinua
akamkumbatia “Nimefurahi sana kuonana
nawe Olivia ana kwa
ana.Nilikuwa ninakusikia na
niliomba sana siku hii ifike
haraka niweze kuonana nawe
na kuushika mkono wako na
hatimaye siku imefika na niko
nawe leo.Karibu sana Olivia
hapa ni nyumbani kwangu,huyu
ni mwanangu Abu ambaye
mnafahamiana tayari,
mwanangu mwingine ni Seif au
Edger kama unavyomfahamu”
akasema Habiba akitumia
Kiswahili safi. “Dr OIivia usiogope
tafadhali jisikie nyumbani”
akasema Habiba baada ya
kumuona Dr Olivia akiogopa.
“Olivia naomba tutembee
kidogo katika himaya yangu”
akasema Habiba Olivia
akainuka wakatoka na
kutembea taratibu kuelekea
katika bustani nzuri
“Habari za Tanzani Dr
Olivia.Shughuli za utafiti
zinakwendaje? Akauliza Habiba

“Tanzania kwema kabisa na
shughuli zinakwenda vizuri sana.Mpaka sasa tayari
tumekwisha kamilisha tafiti za
magonjwa matano ya binadamu
na tiba yake kupatikana.Bado
kuna tafiti nyingine nyingi
zinaendelea.Kwa ujumla
naweza kusema kwamba kituo
kile kimekuwa ni msaada na
mkombozi mkubwa sana kwa
watu.Ninamshukuru Abu dahir
kwa wazo la kujenga kituo kile
ingawa malengo makubwa ya
kujengwa kwa kituo kile
niliambiwa ni hatua ya kwanza
ya mchakato wa kumtafuta
Edger” akasema Dr Olivia “Dr Olivia kituo kile kina
dhumuni la kufanya tafiti za
magonjwa mbalimbali na
kuyatafutia tiba lakini kina kazi
nyingine mbili maalum
kabisa.Kabla ya kukueleza
kuhusiana na kazi hizo
ningependa kwanza kukujulisha
kwamba naitwa Habiba jawad
kama alivyonitambulisha Abu
dahir.Mimi ndiye mama mzazi
wa Edger kaka na Abu
dahir.Alipokuja Tanzania
kuonana nawe mwaka jana Abu
alikueleza machache kuhusiana
na Edger kaka ambaye jina lake halisi ni Seif Jawad.Mimi asili
yangu ni Somalia lakini
nilizaliwa na kukulia Kenya
nikaolewa na tajiri mmoja
anaitwa Nasser jawad
tukabahatika kumpata mtoto
mmoja tu ambaye ni
Seif.Alipokuwa na umri wa
miaka mitano seif alihamia
nchini Tanzania akiwa chini ya
uangalizi wa marafiki zetu na
toka hapo maisha yake yote
yamekuwa nchini Tanzania”
akasema Habiba
“Abu dahir alipokuja
kuonana nami alinieleza hayo yote na nilimuuliza sababu ya
Edger kuhamishiwa Tanzania
lakini hakunipa jibu.Ninaamini
leo nitapata jibu nini hasa
ilikuwa sababu ya
kumuhamishia Seif
Tanzania?akauliza Olivia
“Ipo sababu ya seif
kuhamishiwa Tanzania na
nitakueleza” akasema Habiba
na kunyamaza kidogo kisha
akaendelea
“Wazazi wangu waliuawa
nchini Tanzania nikiwa bado
msichana mdogo.Baba yangu
alikuwa anazunguka sehemu mbalimbali akitoa mihadhara
ya kidini na alipokuwa nchini
Tanzania yeye na mama yangu
walivamiwa na kuuawa na watu
wanaodaiwa ni majambazi.Vifo
vya wazazi wangu viliniumiza
sana kwani vilinifanya niishi
maisha ya taabu kubwa na
kutokana na magumu
niliyoyapitia niliweka ahadi ya
kuhakikisha kwamba wale wote
waliowaua wazazi wangu
wanapatikana na kulipa uovu
wao hata kama itapita miaka
mia moja.Nilipata tetesi
kwamba mauaji ya wazazi wangu ulikuwa ni mpango
maalum wa serikali za afrika
mashariki kumuua baba
wakidai kwamba baba yangu
alikuwa anazunguka
kuhamasisha watu kujiunga na
vikundi vya ugaidi.Nilimuingiza
Seif Tanzania ikiwa ni sehemu
ya mpango wangu wa kulipiza
kisasi kwa nchi za afrika
mashariki kwa kuwaua wazazi
wangu.Nilimuandaa seif kwa
ajili ya kushika madaraka
makubwa nchini Tanzania ili
mpango wangu uweze
kutimia.Nilitaka awe rais wa Tanzania” akasema Habiba na
sura ya Dr Olivia ilionyesha
mstuko mkubwa.
“Usistuke Olivia ni kweli
nilimuandaa Seif aje kushika
madaraka makubwa ya
nchi.Nilimkabidhi kwa familia
ya watanzania ambao
niliwawezesha kwa utajiri na
wakamsajili Seif kama mtoto
wao wa kumzaa wakambadili
jina na kumuita Edger
Kaka.Nasser baba yake Seif
alifariki dunia kwa ugonjwa wa
saratani, nikaolewa na
mwanaume mwingine anaitwa Abdul dahir ambaye ndiye baba
yake Abu dahir.Abdul alikuwa
ni mpalestina na alikuwa mstari
wa mbele katika kupigania haki
za taifa la Palestina.Alikuwa
tajiri sana hivyo alifadhili
vikundi mbali mbali
vilivyokuwa vinaendesha
mapambano dhidi ya
Israel.Naamini umekuwa
ukisikia juu ya mzozo
unaoendelea kati ya Palestina
na Israel.Umekuwa ni mzozo wa
muda mrefu na hakuna dalili
zozote za kumalizika licha ya
juhudi mbalimbali za kujaribu
 
SIRI

Episode 24
Mtunzi. Patrick CK

kuumaliza mzozo huo
kufanyika.Labda nikupe
maelezo mafupi kuhusiana na
mzozo huu wa palestina na
Israel.Mzozo huu ulianza karne
ya ishirini baina ya wakazi
wayahudi na waarabu wa
maeneo ambayo hivi sasa yako
chini ya Israel na mamlaka ya
palestina.Toka kuundwa kwa
taifa la Israel mwaka 1948
tayari taifa hili limekwisha
pigana vita sita na majirani zake
na hadi sasa mapambano
yanaendelea na hakuna dalili zozote za kupata suluhisho la
mzozo huu.
Mwaka 1947 Mkutano
Mkuu wa Umoja wa
Mataifa ulipigia kura mpango w
a ugawaji wa Palestina ambapo
mataifa 33 yalipiga kura
ya ndiyo,13 hapana na 10
hayakusimama upande wowote.
Kufuatia kura hiyo eneo la
Palestina lilitakiwa kugawiwa
kwa dola la Kiyahudi,dola la
Kiarabu na mji wa Yerusalemu.
Waarabu walipinga ugawaji
huo kwa kudokeza ya kwamba
mpango wa ugawaji wakazi wangekuwa
Waarabu.Sehemu kubwa ya
ardhi katika sehemu ya Dola la
Kiarabu ilikuwa mlimani na
haikufaa vema kwa ajili ya
kilimo.
Wawakilishi wa Kiyahudi
walisema idadi ya Wayahudi
itaongezeka haraka kutokana
na uhamiaji wa Wayahudi
wengine kwani wakati ule bado
kulikuwa na malaki ya
wayahudi katika makambi
kwenye nchi za Ulaya ambao
hawakuuawa na Wajerumani Mara baada ya azimio hilo
la umoja wa mataifa,mapigano
yalianza katika
Palestina.Vikundi
vya wanamgambo wa Kiarabu
vilishambulia makazi ya
Kiyahudi kote nchini.Wayahudi
pia walikuwa na vikundi vyao
vya wanamgambo.
Tarehe 14 Mei mkutano wa
wawakilishi Wayahudi
ulitangaza Dola la Israeli kama
nchi mpya. Tarehe 15 Mei 1948
majeshi ya
Misri, Yordani, Lebanoni, Syria
na Irak yaliingia Palestina yakatwaa maeneo ya Kiarabu
na kushambulia makazi ya
Kiyahudi.Katika vita ya miezi 10
jeshi la Israeli lilifaulu
kusimamisha wapinzani na
kuwarudisha nyuma.Wakati wa
kusimamisha mapigano Israeli
ilikuwa imeongezeka maeneo
yake ikatawala asilimia 78 ya
eneo iliyokabidhiwa awali na
Umoja wa Mataifa kwa ajili ya
Dola la Kiyahudi pamoja na
nusu ya maeneo
yaliyokusudiwa kwa ajili ya
Dola la Kiarabu. Zaidi ya wakazi Waarabu
700,000 walilazimika kukimbia
kutoka miji na vijiji
vyao,wakienda nje ya maeneo
yanayotawaliwa sasa na
Israeli.Waarabu takribani
150,000 walibaki ndani ya
maeneo hayo
kama raia Waarabu wa
Israeli.Baada ya vita kumalizika
Israeli ilikataa kurudi kwa watu
waliokuwa wamekimbia na hii
ndiyo asili ya wakimbizi
Wapalestina wanaoishi Syria,
Lebanoni, Jordani na Misri,
pamoja na wale wanaoendelea kukaa katika maeneo ya Gaza
na Ukingo wa Magharibi.
Nchi zote za kiarabu
isipokuwa Jordani zilikataa
kuwapa wakimbizi hao haki
za uraia,kwa hiyo hadi leo
wajukuu wamebaki kama
wakimbizi katika nchi za kigeni
bila uraia,wakisafiri wanatumia
vitambulisho vilivyotolewa
na umoja wa mataifa,wanakosa
haki ya kutafuta kazi au
kushiriki katika siasa kama raia
wa kawaida, hata
kama familia zimeshaishi katika
nchi hizo hadi kizazi cha tatu au nne.Nadhani unapata picha ni
mateso kiasi gani wanayapata
wapalestina ambao
wametolewa katika ardhi
yao.Baada ya vita ya 1948-1949
nchi jirani zilikataa kulitambua
taifa la Israeli.Hali ya vita
ikaendelea ingawa bila
mapigano kati ya majeshi
makubwa.Wanamgambo wa
wafedayin wapalestina
waliendelea kuvuka mpaka
kutoka makambi ya wakimbizi
na kushambulia vijiji vya
Kiyahudi. Wanamgambo hao
walipata mara nyingi silaha na mafunzo kutoka kwa majeshi ya
Misri na Syria.Mwaka 1964
chama cha ukombozi wa
Palestina PLO yaani Palestine
Liberation Organization
kilianzishwa kufuatia azimio la
nchi za kiarabu.Huu ulikuwa ni
muungano wa vikundi
mbalimbali vya wapalestina na
kiliendesha harakati za
kushambulia mipaka ya Israel
mara kwa mara.Olivia historia
ya mzozo huu ni ndefu lakini
kwa maelezo hayo mafupi
naamini umepata picha halisi ya
kwa nini raia wa Palestina wanamwaga damu zao kila
uchao kupigania ardhi yao
iliyoporwa.Abdul dahir alikuwa
mmoja wa wafadhili wa vikundi
hivi vidogo vilivyoendesha
mapambano dhidi ya Israel hadi
alipouawa” akanyamaza kidogo
“Ninayafahamu mateso
wanayoyapata ndugu zangu”
akaendelea
“Hivyo basi kifo cha Abdul
hakikuzuia harakati za kudai
haki kuendelea.Nilishika
hatamu na kuendelea kutoa
ufadhili kwa wapigania haki
lakini nikimtumia mtu anayeita Sayid Omar.Huyu
nilimuwezesha akawa tajiri
mkubwa na ndiye
ninayepitishia ufadhili wangu
kwake.Harakati hizi hazitakoma
hadi pale tutakapohakikisha
kwamba ardhi ya wapalestina
imerudishwa.Tukiachana na
hayo turejee nyumbani
Tanzania.Bado azma yangu ya
kutaka kulipiza kisasi kwa
wazazi wangu iliendelea na
nilimtengeneza Seif kwa ajili ya
hilo.Mipango ilikwenda vyema
na Seif akaingia katika
siasa,akashinda ubunge ,akawa na jina kubwa lengo kubwa
likiwa ni kumuandaa kuwa rais
wa Tanzania.Katika harakati
zangu niliungana na kikundi cha
IS na lengo letu ni kuanzisha
himaya kubwa ya IS katika
ukanda wa Afrika mashariki na
dhumuni kubwa ni kuwaandaa
vijana ambao watatusaidia
katika mapambano ya kudai
haki sehemu mbali mbali
duniani.Kuna vijana wengi
kutoika ukanda wa Afrika
mashariki ambao wanasafiri
umbali mrefu kujiunga na IS
hivyo tunataka kuanzisha kambi za siri za kuwakusanya
vijana na kuwapa mafunzo
kisha kuwatumia katika
mapambano yetu ” akasema
Habiba na Dr Olivia akatoa
kitambaa katika pochi yake
akajifuta jasho usoni
“Ee Mungu nisaidie niweze
kutoka salama huku
niliko.Nimejileta mwenyewe
katika mto wenye Mamba
niokoe ee Mungu wangu”
akaomba Dr Olivia kimya
kimya.Alikuwa anatetemeka
ndani.Aliogopa sana.Habiba
Jawad akalitambua hilo “Usiogope Olivia.Najua haya
niliyokueleza yamekustua sana
lakini ni lazima uyafahamu”
akasema Habiba
“Madam Habiba ni kweli
nimestuka sana hasa baada ya
kusikia kuhusu kikundi cha
IS.Hiki ni kikundi cha kigaidi na
kimekuwa kikiendesha mauaji
ya kikatili sehemu mbali mbali
duniani” akasema Dr Olivia kwa
woga
“Usiogope Dr Olivia.IS ni
kikundi chenye kupigania haki
za wanyonge waislamu na
wasio waislamu kote duniani na ndiyo maana nikakubali
kuungana nao na kwa sasa
tunaelekeza nguvu katika
kupambana na Israel”
“Madam Habiba hakuna
unachoweza kunieleza kuhusu
IS nikakuelewa.Hiki ni kikundi
cha kigaidi na kimekuwa
kikifanya mauaji ya kinyama
sehemu mbali mbali
duniani.Hakitetei mtu yeyote
zaidi ya kuendesha mauaji ya
kinyama.Laiti ningejua kuhusu
jambo hili mapema
nisingekubali katu kuungana nanyi.Edger alifahamu kuhusu
suala hili? Akauliza Dr Olivia
“Edger anafahamu kila
kitu”akajibu Habiba.Dr Olivia
akashika kichwa
“Oh my God !
“Sikiliza Olivia niliamua
kujiunga na IS ili kuongeza
nguvu kwa ajili ya kumsaidia
Edger aweze kushika nafasi ya
urais.Tunataka kulitumia eneo
la Afrika mashariki kama eneo
la mafunzo kupika watu wetu
ambao watakwenda kufanya
kazi sehemu mbali mbali
duniani.Tumechagua Tanzania iwe ni kambi yetu kuu ya
mafunzo na itakuwa rahisi
kwetu kuanzisha kambi ya
mafunzo endapo Edger atakuwa
rais.Tuliwekeza muda na fedha
nyingi kwake na tulifanikiwa
kwa asilimia tisini na nane
kumtengeneza mtu ambaye
alipendwa sana,mtu ambaye
alikuwa mtetezi wa
wanyonge,anayepambana na
mafisadi wanaohujumu uchumi
wa Tanzania na tulikuwa na
uhakika kwamba endapo
angegombea urais angeshinda
kwa asilimia kubwa sana lakini kwa bahati mbaya mpango
wetu ulivurugwa katika dakika
za mwisho kabisa” akasema
Habiba.
“Katika safari ya
kumuandaa Edger kushika
madaraka makubwa ya nchi
tulijikuta tukitengeneza pia
maadui ambao hawakumpenda
na walipanga kumuua na
mojawapo ya jaribio la kumuua
ni lile la kumuwekea sumu
jaribio ambalo lilishindwa na
ninakushukuru sana kwa
kuyaokoa maisha yake.Akiwa
hospitali bado maadui zake waliendelea kumfuatilia kwa
lengo la kumuua.Walitumwa
watu Israel kumfuata
kumuua.Katika chumba
alimokuwa amelazwa
kulifungwa kamera za ulinzi na
vyombo vya kunasa
mawasiliano ikiwa ni
muendelezo wa mipango ya
kumuua.Walikuwa wanafuatilia
mawasiliano yake yote na hata
alipoamua kurejea nyumbani
walifahamu kwamba anarejea
hivyo wakafanya jaribio lile la
kumuua” akasema Habiba “Abu dahir aliniambia
kwamba Edger hajafa.Kauli hii
imenitesa kwa mwaka mzima
nikitafakari hili
linawezekanaje? Mimi ndiye
niliyeutambua mwili wake
hospitali uliokuwa umeungua
sana na niliweza kuutambua
kutokana na mkufu aliokuwa
ameuvaa shingoni uliokuwa na
kidani chenye herufi E na pete
alizokuwa amevaa.Naamini leo
nitapata majibu ya suala hilii”
akasema Dr Olivia
“Alichokueleza Abu ni cha
kweli kabisa kwamba Seif hajafa.Kilichofanyika ulikuwa ni
mpango maalum kabisa wa
kumteka na kuiaminisha dunia
kwamba Edger amefariki lakini
ukweli ni kwamba Edger yuko
hai”akasma Habiba Jawad
“Madam Habiba bado
mnaendelea
kunichanganya.Kama yuko hai
mnafahamu mahala alipo?Nani
waliofanya mpango
huo?akauliza Dr Olivia
“Mpaka sasa bado
hatufahamu mahala alipo Edger
wala nani aliyefanya mpango
ule lakini tunaamini kabisa kwamba yuko hai sehemu
Fulani anashikiliwa” akasema
habiba
“Madam Habiba unakiri
kwamba hamjui mahala alipo
na wala wanaomshikilia mna
uhakika gani kwamba Edger
yuko hai?akauliza Olivia
“Olivia najua jambo hili
limekustua sana kusikia
kwamba Edger yuko hai lakini
nakuhakikishia kwamba Edger
yuko hai hakufa katika ile
ajali.Kuna sababu
zinazopelekea tuamini
hivyo.Nimekueleza kwa kirefu kuhusiana na mimi ni nani na
maisha yangu kwa ujumla na
kutokana na harakati zangu
hizo za kupigania haki
nimekuwa nikitafutwa sana na
nchi ya Israel.Miezi kadhaa
baada ya kuamini Edger
amefariki katika ile ajali
nilianza kufuatiliwa na majasusi
wa Mossad ambao walivamia
sehemu zangu mbali mbali za
siri lakini kwa bahati nzuri
hawakupata chochote kwani
mambo yangu ninayafanya kwa
umakini mkubwa
sana.Tulijiuliza na wenzangu namna Mossad walivyoweza
kupata taarifa zile kwani
zilikuwa ni taarifa nyeti sana na
waliokuwa wakifahamu
maficho yangu ni watu
wachache mno ambao hata
itokee nini hawataweza
kunisaliti ndipo hapo tulipoanza
kuwa na hisia kama kweli Edger
alifariki katika ajali ile.Tulianza
uchunguzi mara moja na
tukagundua kwamba kifo kile
ulikuwa ni mpango maalum
kabisa ulioandaliwa.Tulibaini
kwamba ndege ambayo Edger
aliondoka nayo ilichelewa kwa saa kumi zaidi ya muda ambao
ilitakiwa kuwasili jijini Dar es
salaam” akasema Habuba
“Nalifahamu hilo.Edger
alitaka kuwahi mazishi ya
waziri mkuu na ndiyo maana
tulichagua ndege ambayo
ingetuwezesha kufika Dar es
salaam saa sita mchana lakini
kulitokea hitilafu za kiufundi
zilizopelekea ndege ile ichelewe
kuondoka Tel aviv hivyo
tukachelewa sana kufika Dar es
salaam.Badala ya kufika saa sita
mchana tukafika saa sita za
usiku”akasema Dr Olivia “Uchunguzi wetu
unaonyesha kwamba hakukuwa
na hitilafu yoyote katika ile
ndege bali ulikuwa ni mpango
maalum wa kuichelewesha ifike
Dar es salaam usiku ili waweze
kukamilisha mpango wao wa
kumteka Edger na
kutuaminisha kwamba
amefariki lakini nina uhakika
mkubwa kwamba Edger hajafa
yupo sehemu Fulani
anashikiliwa” akasema Habiba
na kumfanya Dr Olivia azame
mawazoni “Madam Habiba ninaanza
kupata picha fulani kwa hayo
maelezo yako.Taarifa ya ndege
kuwa na hitilafu ilikuwa ya
ghafla sana na ilimshangaza kila
mtu.Hata mazingira ya ajali ile
yanatia shaka sana.Ni miaka
mitatu sasa lakini familia ya
dereva wa lori lililogonga gari la
Edger haijapatikana na
hawajulikani walipo na hii
inazidi kunifanya niamini
kwamba yawezekana kweli
Edger hajafa kama
tunavyodhani” akasema Dr
Olivia “Nashukuru kama umeanza
kuipata picha kubwa ya jambo
hili” akasema Habiba
“Lakini madam Habiba
kuna maswali ambayo nitahitaji
majibu.Kama Edger hajafa ule
mwili uliokutwa ndani ya gari
lake ukiwa umevaa mkufu ule
wa Edger ambao alikuwa
ameuvaa toka tukiwa Israel ni
wa nani?Na kama bado mzima
yuko wapi na nani
wanaomshikilia? akauliza Dr
Olivia
“Alikueleza Abu dahir
kwamba kutakuwa na hatua kadhaa katika kuutafuta ukweli
kuhusu Edger na hatua ya
kwanza ilikuwa ni kujenga kituo
kile cha utafiti ambacho
kimekamilika na sasa tunaingia
katika hatua ya pili ambayo ni
kuupata ukweli kuhusu Edger
kama kweli yuko hai.Mwili ule
ambao ulikutwa ndani ya gari
ukiwa na mkufu wa Edger na
wewe ukautambua kwamba ni
wa Edger tunataka kuufanyia
uchunguzi kubaini kama kweli
ni mwili wa Edger na hilo zoezi
litafanyika katika kile kituo
chako ambacho dhumuni kubwa la kujengwa kwake
lilikuwa hilo.Tutachukua
sampuli za mabaki ya ule mwili
tutaupima vinasaba kupata
ukweli kama kweli mwili ule
ulikuwa wa Edger na kama
vipimo vikituonyesha kwamba
mwili ule si wake basi tutakuwa
sahihikwamba Edger yuko hai
na hapo tutaingia katika hatua
ya tatu ya kumtafuta na kujua
mahala alipo” akasema Habiba
“Madam Habiba
nakubaliana na wazo hilo la
kuufanyia uchunguzi mwili ule
ambao tunaamini ni wa Edger ili kuupata ukweli.Kama mwili
ule utakuwa si wa Edger
unadhani nani waliomteka
nyara na kwa madhumuni gani?
Yuko wapi? akauliza Dr Olivia
“Ni mapema sana kusema
anashikiliwa wapi na nani lakini
baada ya kupata uhakika
kwamba mwili ule si wa Edger
hapo ndipo tutakapoanza
uchunguzi wetu kuhakikisha
tunafahamu mahala alipo na
nani anamshikilia.Dr Olivia nina
uhakika mkubwa sana kwamba
Edger yuko hai na nitakuomba
sana msaada wako ili tuweze kumpata.Huko aliko naamini
atakuwa anateswa mno na
tusipoharakisha kumuokoa
watamuua.Dr Olivia ninaamini
mambo niliyokueleza leo
yamekustua sana na
kukuogopesha lakini nakuomba
usiogope.Lengo la mimi
kushirikiana nawe ni kwa ajili
ya kunisaidia kumpata Edger
ambaye najua siwezi kumpata
bila msaada wako hivyo
nakuomba tushirikiane
kuhakikisha kwamba Edger
anapatikana akiwa mzima”
akasema Habiba “Madam Habiba ni kweli
mambo uliyonieleza leo
yamenistua na kuniogopesha
hasa baada ya kuifahamu
historia ya Edger.Sikujua kama
Edger ana mahusiano na
kikundi cha IS.Sikujua kwa nini
Edger alihamishiwa
Tanzania.Baada ya kufahamu
haya yote nimeingiwa na hofu
kubwa”
“Nini kinakupa hofu Dr
Olivia?akauliza Habiba
“Kila kitu nilichokifahamu
leo.Ninawaogopa magaidi.Watu
wengi wasio na hatia wanapoteza maisha sehemu
mbali mbali duniani kutokana
na vitendo vya ugaidi.IS ni
kikundi cha kigaidi na
kimekuwa kikifanya mauaji
sehemu mbali mbali
duniani.Nimeingiwa na woga
kufahamu kuwa Edger ana
mahusiano na kikundi hiki cha
kigaidi” akasema Dr Olivia
“Tafadhali usiogope Dr
Olivia” akasema Habiba
“Nchini Tanzania Edger ni
mbunge ambaye ana jina kubwa
sana,anapendwa na watu wengi
na amekuwa mstari wa mbele katika kuendesha mapambano
dhidi ya mafisadi na wahujumu
uchumi.Hana woga wala aibu
katika mapambano
hayo.Amekuwa ni mtetezi wa
wanyonge,amekuwa ni msemaji
wa wale wasiokuwa na sauti ya
kusema.Kutokana na nguvu
yake kubwa ya ushawishi
naamni kama angegombea urais
angeshinda kwa kishindo
kikubwa.Kinachonipa hofu
kwamba nyuma ya mafaniko
hayo yote makubwa aliyonayo
ana siri kubwa ambayo
watanzania hawaifahamu.Pindi watanzania wakijua kwamba
mtu ambaye walikuwa tayari
kumuamini awaongoze kwanza
si mtanzania na pili ana
mafungamano na kikundi cha IS
sina hakika nini kitatokea.Huu
unaweza ukawa ni mwisho wa
Edger.Hiyo ni hofu yangu
kubwa sana” akasema Dr
Olivia.Habiba akatabasamu
kidogo na kusema
“Huna sababu ya kuwa na
hofu Olivia.Hakuna atakayejua
siri hiyo.Ni watu wachache sana
wanaofahamu jambo hili na
wote wamekula kiapo cha utii cha kwenda kaburini na hii
siri.Hakuna atakayeweza kutoa
siri hii kuhusiana na
Edger.Katika watu wachache
wanaoifahamu hii siri
umeongezeka wewe hivyo
utalishwa kiapo cha uaminifu
kwamba hautatoa siri hii na
siku ukifungua ulimi wako
kutamka chochote kuhusiana na
siri hii uliyoifahamu leo
utakuwa ni mwisho wako wewe
na ukoo wako wote.Hakuna
serikali inayoweza kukusaidia
tunao mtandao mkubwa na
tunao uwezo wa kuingia sehemu yoyote.Sikuogopeshi Dr
Olivia lakini tayari nawe ni
mmoja wetu” akasema Habiba
na Dr Olivia akahisi haja ndogo
inataka kumtoka
“Dr Olivia umestuka sana
kusikia kwamba wewe tayari ni
mmoja wetu lakini hilo lilikuwa
ni angalizo tu kwamba
umezifahamu siri zetu hivyo
unapaswa ukae kimya.Hatuna
tatizo na wewe hakuna
atakayekugusa na badala yake
sisi ndio tutakaokuwa
tunakulinda na kuhakikisha
unakuwa salama.Hatuna lengo lolote baya na Tanzania na
ninakuhakikishia kwamba
hakuna damu ya mtanzania
itakayomwagika.Edger
unamfahamu ni mtu mzuri,ana
roho nzuri anaipenda Tanzania
na ni mtu mwenye malengo
makubwa sana na
Tanzania.Nilikueleza awali
kwamba mpango wa kumpeleka
Edger Tanzania ilikuwa ni kwa
ajili ya kulipiza kisasi kwa wale
waliowaua wazazi wangu lakini
baada ya Edger kuupata ubunge
na kuona mambo makubwa
aliyokuwa anayafanya hasa katika kufichua wizi mkubwa
wa rasilimali za nchi
unaofanywa na vigogo niliamua
kubadili malengo yangu na
kuanza kumuunga mkono
katika mapambano yake dhidi
ya wanyonge.Alinieleza namna
anavyoguswa na maisha
wanayoishi watu masikini
ukilinganishwa na utajiri
mkubwa ulioko nchini ambao ni
watu wachache wanaofaidika
nao.Licha ya mipango yetu
lakini umasikini wa
watanzaniani jambo
linalomgusa Edger kutoka moyoni.Aliniomba tuachane na
mpango ule wa kuwatafuta
watu watu waliowaua wazazi
wangu bali tujielekeze katika
kupambana na maadui wa kweli
wa maendeleo ya Tanzania
ambao ni mafisadi na baadhi ya
mataifa makubwa ambayo
yamekuwa yakizinyonya nchi
ndogo na Tanzania
ikiwemo.Wazo hili nililiona ni
zuri na nikaamua kumuunga
mkono,hivyo vita yetu ya sasa
ni kwa mataifa makubwa
ambayo yanazikandamiza nchi
ndogo na Tanzania ikiwemo na vita hii ni ngumu na ndiyo
maana ninataka Edger awe rais
wa Tanzania ili tuwe na nguvu
ya kupambana na mataifa haya
ya magharibi” akasema Habiba.
“Madam Habiba pamoja na
nia hiyo mnayosema ni njema
lakini hakuna atakayeelewa
akisikia kuhusu Edger kuwa na
mafungamano na IS.Bado
machoni pa wengi hiki ni
kikundi cha kigaidi na hakuna
mtanzania ambaye atakubali
kuongozwa na rais ambaye
kwanza si mtanzania na pili ana
mafungamano na kikundi cha kigaidi.Hata mimi siko tayari
madam Habiba kwa Edger
kuongoza nchi.Najua haya ni
maneno ambayo
hayakufurahishi lakini huo ni
ukweli kwamba siko tayari kwa
Edger kuwa rais wa
Tanzania.Nchi yangu Tanzania
ni nchi yenye kuheshimika
duniani kote.Ni nchi ya mfano
kwa mataifa mengine na
ambayo amani imetamalaki
kwa miaka na miaka na katu
siko tayari kuona amani yetu
ikianza kuchezewa.Endapo
Edger akishinda urais utakuwa ni mwanzo wa
kulisambaratisha taifa letu
kwani zitaanza kupandikizwa
chochochoko za dini na taifa lile
zuri ambalo limekuwa ni
kimbilio la wale wote wasio na
kwao litabomoka na hilo ni pigo
kubwa kwa Afrika
nzima.madam habiba
unapozungumzia Afrika
unaizungumzia Tanzania
ambayo kutokana nayo nchi
nyingi zimekombolewa kutoka
katika makucha ya
wakoloni.Tanzania imekuwa
msuluhishi wa mizozo katika nchi mbali mbali ndani ya bara
la Afrika,imekuwa ni nyumba ya
wakimbizi wanaokimbia
mapigano katika nchi zao,sifa
hii ya nchi hii nzuri
iliyobarikiwa haitakiwi
kuharibiwa.Tanzania inapaswa
ibaki kama ilivyo yaani kisiwa
cha amani” akasema Dr Olivia
na kushindwa kuyazuia
machozi kumtoka
“Dr Olivia usilie
tafadhali.Yote uliyoyasema
nimeyasikia lakini
nakuhakikishia kwamba hatuna
malengo mabaya na Tanzania.Tuna malengo mazuri
sana ya kuisaidia nchi yako
unayoipenda.Hata kama Edger
akiwa rais hakuna tatizo lolote
litakalotokea” akasema
Habiba.Ulipita ukimya halafu Dr
Olivia akasema
“Madam Habiba,mwanao
Edger au Seif ni mtu wangu wa
karibu katika kipindi kifupi
nilichofahamiana naye alidiriki
hata kunitamkia kwamba
ananipenda japo sikumpa jibu
lolote kwa sababu kwanza
tulikuwa hospitali na pili
kipindi tulichofahamiana kilikuwa kifupi sana lakini
nakiri kwako kwako kwamba
hata mimi nilikwisha anza kuwa
na hisia na Edger japo
sikumueleza.Nilitaka akitoka
hospitali tuoate muda wa
kutosha kuthibitsha kama hisia
zetu ni za kweli lakini
hatukupata huo muda
akatoweka.Baada ya kuufahamu
ukweli kuhusu Edger sina
hakika kama hata akipatikana
nitaendelea kuwa na urafiki
naye lakini nitashirikiana nanyi
katika kumtafuta.Pamoja na
hayo mimi na wewe lazima tuwe na makubaliano” akasema
Dr Olivia
“Edger hakuwahi
kunitamkia chochote kuhusu
kumpenda mwanamke yeyote
na sina hakika kama maneno
hayo aliyokutamkia amewahi
kumtamkia mwanamke
mwingine.Kitu gani mimi na
wewe unataka tukubaliane
Olivia?akauliza Habiba.Dr Olivia
akamtazama Habiba usoni kwa
muda halafu akasema
“Nitaendelea kushirikiana
nanyi katika kumtafuta Edger
lakini kwa sharti moja kwamba endapo akipatikana
hatajishughulisha tena na
mambo yoyote yanayohusiana
na siasa na mpango wa
kumtaka agombee urais
hautakuwepo tena” akasema Dr
Olivia.Habiba Jawad
akatabasamu na kuuliza
“Ni vipi kama nikisema
hapana?
“Sintashiriki katika mpango
wowote wa kumtafuta
Edger”akasema Dr Oliviana
sura ya Habiba ikabadilika
“Mungu nisaidie hiki
ninachokifanya ni hatari kubwa watu hawa wanaweza
wakaniua muda
wowote.Natakiwa kuwa makini
sana”akawaza Dr Olivia
akitazamana na Habiba
“Madam Habiba kwa sasa
mnanihitaji sana katika mpango
huu na ili nishiriki lazima
mkubaliane na hicho
ninachokitaka” akasema Dr
Olivia.Habiba alimtazama Dr
Olivia hadi akaingiwa na wasi
wasi
“Hakuna tatizo na hicho
unachokihitaji.Ninachokitaka
mimi ni mwanangu apatikane hata kama itakuwa ni kwa
kuvuruga mipango yetu yote
niko tayari,hata hivyo nawe
lazima ulishwe kiapo cha
kuilinda siri hii hadi
kaburini.Hatakiwi mtu
mwingine yeyote kujua”
akasema Habiba.
DAR ES SALAAM
Dr Olivia alirejea Dar es
salaam tayari kabisa kuanza
mchakato wa kuutafuta ukweli
kuhusu Edger Kaka ambaye kila ....
 
SIRI

Episode 24
Mtunzi. Patrick CK

kuumaliza mzozo huo
kufanyika.Labda nikupe
maelezo mafupi kuhusiana na
mzozo huu wa palestina na
Israel.Mzozo huu ulianza karne
ya ishirini baina ya wakazi
wayahudi na waarabu wa
maeneo ambayo hivi sasa yako
chini ya Israel na mamlaka ya
palestina.Toka kuundwa kwa
taifa la Israel mwaka 1948
tayari taifa hili limekwisha
pigana vita sita na majirani zake
na hadi sasa mapambano
yanaendelea na hakuna dalili zozote za kupata suluhisho la
mzozo huu.
Mwaka 1947 Mkutano
Mkuu wa Umoja wa
Mataifa ulipigia kura mpango w
a ugawaji wa Palestina ambapo
mataifa 33 yalipiga kura
ya ndiyo,13 hapana na 10
hayakusimama upande wowote.
Kufuatia kura hiyo eneo la
Palestina lilitakiwa kugawiwa
kwa dola la Kiyahudi,dola la
Kiarabu na mji wa Yerusalemu.
Waarabu walipinga ugawaji
huo kwa kudokeza ya kwamba
mpango wa ugawaji wakazi wangekuwa
Waarabu.Sehemu kubwa ya
ardhi katika sehemu ya Dola la
Kiarabu ilikuwa mlimani na
haikufaa vema kwa ajili ya
kilimo.
Wawakilishi wa Kiyahudi
walisema idadi ya Wayahudi
itaongezeka haraka kutokana
na uhamiaji wa Wayahudi
wengine kwani wakati ule bado
kulikuwa na malaki ya
wayahudi katika makambi
kwenye nchi za Ulaya ambao
hawakuuawa na Wajerumani Mara baada ya azimio hilo
la umoja wa mataifa,mapigano
yalianza katika
Palestina.Vikundi
vya wanamgambo wa Kiarabu
vilishambulia makazi ya
Kiyahudi kote nchini.Wayahudi
pia walikuwa na vikundi vyao
vya wanamgambo.
Tarehe 14 Mei mkutano wa
wawakilishi Wayahudi
ulitangaza Dola la Israeli kama
nchi mpya. Tarehe 15 Mei 1948
majeshi ya
Misri, Yordani, Lebanoni, Syria
na Irak yaliingia Palestina yakatwaa maeneo ya Kiarabu
na kushambulia makazi ya
Kiyahudi.Katika vita ya miezi 10
jeshi la Israeli lilifaulu
kusimamisha wapinzani na
kuwarudisha nyuma.Wakati wa
kusimamisha mapigano Israeli
ilikuwa imeongezeka maeneo
yake ikatawala asilimia 78 ya
eneo iliyokabidhiwa awali na
Umoja wa Mataifa kwa ajili ya
Dola la Kiyahudi pamoja na
nusu ya maeneo
yaliyokusudiwa kwa ajili ya
Dola la Kiarabu. Zaidi ya wakazi Waarabu
700,000 walilazimika kukimbia
kutoka miji na vijiji
vyao,wakienda nje ya maeneo
yanayotawaliwa sasa na
Israeli.Waarabu takribani
150,000 walibaki ndani ya
maeneo hayo
kama raia Waarabu wa
Israeli.Baada ya vita kumalizika
Israeli ilikataa kurudi kwa watu
waliokuwa wamekimbia na hii
ndiyo asili ya wakimbizi
Wapalestina wanaoishi Syria,
Lebanoni, Jordani na Misri,
pamoja na wale wanaoendelea kukaa katika maeneo ya Gaza
na Ukingo wa Magharibi.
Nchi zote za kiarabu
isipokuwa Jordani zilikataa
kuwapa wakimbizi hao haki
za uraia,kwa hiyo hadi leo
wajukuu wamebaki kama
wakimbizi katika nchi za kigeni
bila uraia,wakisafiri wanatumia
vitambulisho vilivyotolewa
na umoja wa mataifa,wanakosa
haki ya kutafuta kazi au
kushiriki katika siasa kama raia
wa kawaida, hata
kama familia zimeshaishi katika
nchi hizo hadi kizazi cha tatu au nne.Nadhani unapata picha ni
mateso kiasi gani wanayapata
wapalestina ambao
wametolewa katika ardhi
yao.Baada ya vita ya 1948-1949
nchi jirani zilikataa kulitambua
taifa la Israeli.Hali ya vita
ikaendelea ingawa bila
mapigano kati ya majeshi
makubwa.Wanamgambo wa
wafedayin wapalestina
waliendelea kuvuka mpaka
kutoka makambi ya wakimbizi
na kushambulia vijiji vya
Kiyahudi. Wanamgambo hao
walipata mara nyingi silaha na mafunzo kutoka kwa majeshi ya
Misri na Syria.Mwaka 1964
chama cha ukombozi wa
Palestina PLO yaani Palestine
Liberation Organization
kilianzishwa kufuatia azimio la
nchi za kiarabu.Huu ulikuwa ni
muungano wa vikundi
mbalimbali vya wapalestina na
kiliendesha harakati za
kushambulia mipaka ya Israel
mara kwa mara.Olivia historia
ya mzozo huu ni ndefu lakini
kwa maelezo hayo mafupi
naamini umepata picha halisi ya
kwa nini raia wa Palestina wanamwaga damu zao kila
uchao kupigania ardhi yao
iliyoporwa.Abdul dahir alikuwa
mmoja wa wafadhili wa vikundi
hivi vidogo vilivyoendesha
mapambano dhidi ya Israel hadi
alipouawa” akanyamaza kidogo
“Ninayafahamu mateso
wanayoyapata ndugu zangu”
akaendelea
“Hivyo basi kifo cha Abdul
hakikuzuia harakati za kudai
haki kuendelea.Nilishika
hatamu na kuendelea kutoa
ufadhili kwa wapigania haki
lakini nikimtumia mtu anayeita Sayid Omar.Huyu
nilimuwezesha akawa tajiri
mkubwa na ndiye
ninayepitishia ufadhili wangu
kwake.Harakati hizi hazitakoma
hadi pale tutakapohakikisha
kwamba ardhi ya wapalestina
imerudishwa.Tukiachana na
hayo turejee nyumbani
Tanzania.Bado azma yangu ya
kutaka kulipiza kisasi kwa
wazazi wangu iliendelea na
nilimtengeneza Seif kwa ajili ya
hilo.Mipango ilikwenda vyema
na Seif akaingia katika
siasa,akashinda ubunge ,akawa na jina kubwa lengo kubwa
likiwa ni kumuandaa kuwa rais
wa Tanzania.Katika harakati
zangu niliungana na kikundi cha
IS na lengo letu ni kuanzisha
himaya kubwa ya IS katika
ukanda wa Afrika mashariki na
dhumuni kubwa ni kuwaandaa
vijana ambao watatusaidia
katika mapambano ya kudai
haki sehemu mbali mbali
duniani.Kuna vijana wengi
kutoika ukanda wa Afrika
mashariki ambao wanasafiri
umbali mrefu kujiunga na IS
hivyo tunataka kuanzisha kambi za siri za kuwakusanya
vijana na kuwapa mafunzo
kisha kuwatumia katika
mapambano yetu ” akasema
Habiba na Dr Olivia akatoa
kitambaa katika pochi yake
akajifuta jasho usoni
“Ee Mungu nisaidie niweze
kutoka salama huku
niliko.Nimejileta mwenyewe
katika mto wenye Mamba
niokoe ee Mungu wangu”
akaomba Dr Olivia kimya
kimya.Alikuwa anatetemeka
ndani.Aliogopa sana.Habiba
Jawad akalitambua hilo “Usiogope Olivia.Najua haya
niliyokueleza yamekustua sana
lakini ni lazima uyafahamu”
akasema Habiba
“Madam Habiba ni kweli
nimestuka sana hasa baada ya
kusikia kuhusu kikundi cha
IS.Hiki ni kikundi cha kigaidi na
kimekuwa kikiendesha mauaji
ya kikatili sehemu mbali mbali
duniani” akasema Dr Olivia kwa
woga
“Usiogope Dr Olivia.IS ni
kikundi chenye kupigania haki
za wanyonge waislamu na
wasio waislamu kote duniani na ndiyo maana nikakubali
kuungana nao na kwa sasa
tunaelekeza nguvu katika
kupambana na Israel”
“Madam Habiba hakuna
unachoweza kunieleza kuhusu
IS nikakuelewa.Hiki ni kikundi
cha kigaidi na kimekuwa
kikifanya mauaji ya kinyama
sehemu mbali mbali
duniani.Hakitetei mtu yeyote
zaidi ya kuendesha mauaji ya
kinyama.Laiti ningejua kuhusu
jambo hili mapema
nisingekubali katu kuungana nanyi.Edger alifahamu kuhusu
suala hili? Akauliza Dr Olivia
“Edger anafahamu kila
kitu”akajibu Habiba.Dr Olivia
akashika kichwa
“Oh my God !
“Sikiliza Olivia niliamua
kujiunga na IS ili kuongeza
nguvu kwa ajili ya kumsaidia
Edger aweze kushika nafasi ya
urais.Tunataka kulitumia eneo
la Afrika mashariki kama eneo
la mafunzo kupika watu wetu
ambao watakwenda kufanya
kazi sehemu mbali mbali
duniani.Tumechagua Tanzania iwe ni kambi yetu kuu ya
mafunzo na itakuwa rahisi
kwetu kuanzisha kambi ya
mafunzo endapo Edger atakuwa
rais.Tuliwekeza muda na fedha
nyingi kwake na tulifanikiwa
kwa asilimia tisini na nane
kumtengeneza mtu ambaye
alipendwa sana,mtu ambaye
alikuwa mtetezi wa
wanyonge,anayepambana na
mafisadi wanaohujumu uchumi
wa Tanzania na tulikuwa na
uhakika kwamba endapo
angegombea urais angeshinda
kwa asilimia kubwa sana lakini kwa bahati mbaya mpango
wetu ulivurugwa katika dakika
za mwisho kabisa” akasema
Habiba.
“Katika safari ya
kumuandaa Edger kushika
madaraka makubwa ya nchi
tulijikuta tukitengeneza pia
maadui ambao hawakumpenda
na walipanga kumuua na
mojawapo ya jaribio la kumuua
ni lile la kumuwekea sumu
jaribio ambalo lilishindwa na
ninakushukuru sana kwa
kuyaokoa maisha yake.Akiwa
hospitali bado maadui zake waliendelea kumfuatilia kwa
lengo la kumuua.Walitumwa
watu Israel kumfuata
kumuua.Katika chumba
alimokuwa amelazwa
kulifungwa kamera za ulinzi na
vyombo vya kunasa
mawasiliano ikiwa ni
muendelezo wa mipango ya
kumuua.Walikuwa wanafuatilia
mawasiliano yake yote na hata
alipoamua kurejea nyumbani
walifahamu kwamba anarejea
hivyo wakafanya jaribio lile la
kumuua” akasema Habiba “Abu dahir aliniambia
kwamba Edger hajafa.Kauli hii
imenitesa kwa mwaka mzima
nikitafakari hili
linawezekanaje? Mimi ndiye
niliyeutambua mwili wake
hospitali uliokuwa umeungua
sana na niliweza kuutambua
kutokana na mkufu aliokuwa
ameuvaa shingoni uliokuwa na
kidani chenye herufi E na pete
alizokuwa amevaa.Naamini leo
nitapata majibu ya suala hilii”
akasema Dr Olivia
“Alichokueleza Abu ni cha
kweli kabisa kwamba Seif hajafa.Kilichofanyika ulikuwa ni
mpango maalum kabisa wa
kumteka na kuiaminisha dunia
kwamba Edger amefariki lakini
ukweli ni kwamba Edger yuko
hai”akasma Habiba Jawad
“Madam Habiba bado
mnaendelea
kunichanganya.Kama yuko hai
mnafahamu mahala alipo?Nani
waliofanya mpango
huo?akauliza Dr Olivia
“Mpaka sasa bado
hatufahamu mahala alipo Edger
wala nani aliyefanya mpango
ule lakini tunaamini kabisa kwamba yuko hai sehemu
Fulani anashikiliwa” akasema
habiba
“Madam Habiba unakiri
kwamba hamjui mahala alipo
na wala wanaomshikilia mna
uhakika gani kwamba Edger
yuko hai?akauliza Olivia
“Olivia najua jambo hili
limekustua sana kusikia
kwamba Edger yuko hai lakini
nakuhakikishia kwamba Edger
yuko hai hakufa katika ile
ajali.Kuna sababu
zinazopelekea tuamini
hivyo.Nimekueleza kwa kirefu kuhusiana na mimi ni nani na
maisha yangu kwa ujumla na
kutokana na harakati zangu
hizo za kupigania haki
nimekuwa nikitafutwa sana na
nchi ya Israel.Miezi kadhaa
baada ya kuamini Edger
amefariki katika ile ajali
nilianza kufuatiliwa na majasusi
wa Mossad ambao walivamia
sehemu zangu mbali mbali za
siri lakini kwa bahati nzuri
hawakupata chochote kwani
mambo yangu ninayafanya kwa
umakini mkubwa
sana.Tulijiuliza na wenzangu namna Mossad walivyoweza
kupata taarifa zile kwani
zilikuwa ni taarifa nyeti sana na
waliokuwa wakifahamu
maficho yangu ni watu
wachache mno ambao hata
itokee nini hawataweza
kunisaliti ndipo hapo tulipoanza
kuwa na hisia kama kweli Edger
alifariki katika ajali ile.Tulianza
uchunguzi mara moja na
tukagundua kwamba kifo kile
ulikuwa ni mpango maalum
kabisa ulioandaliwa.Tulibaini
kwamba ndege ambayo Edger
aliondoka nayo ilichelewa kwa saa kumi zaidi ya muda ambao
ilitakiwa kuwasili jijini Dar es
salaam” akasema Habuba
“Nalifahamu hilo.Edger
alitaka kuwahi mazishi ya
waziri mkuu na ndiyo maana
tulichagua ndege ambayo
ingetuwezesha kufika Dar es
salaam saa sita mchana lakini
kulitokea hitilafu za kiufundi
zilizopelekea ndege ile ichelewe
kuondoka Tel aviv hivyo
tukachelewa sana kufika Dar es
salaam.Badala ya kufika saa sita
mchana tukafika saa sita za
usiku”akasema Dr Olivia “Uchunguzi wetu
unaonyesha kwamba hakukuwa
na hitilafu yoyote katika ile
ndege bali ulikuwa ni mpango
maalum wa kuichelewesha ifike
Dar es salaam usiku ili waweze
kukamilisha mpango wao wa
kumteka Edger na
kutuaminisha kwamba
amefariki lakini nina uhakika
mkubwa kwamba Edger hajafa
yupo sehemu Fulani
anashikiliwa” akasema Habiba
na kumfanya Dr Olivia azame
mawazoni “Madam Habiba ninaanza
kupata picha fulani kwa hayo
maelezo yako.Taarifa ya ndege
kuwa na hitilafu ilikuwa ya
ghafla sana na ilimshangaza kila
mtu.Hata mazingira ya ajali ile
yanatia shaka sana.Ni miaka
mitatu sasa lakini familia ya
dereva wa lori lililogonga gari la
Edger haijapatikana na
hawajulikani walipo na hii
inazidi kunifanya niamini
kwamba yawezekana kweli
Edger hajafa kama
tunavyodhani” akasema Dr
Olivia “Nashukuru kama umeanza
kuipata picha kubwa ya jambo
hili” akasema Habiba
“Lakini madam Habiba
kuna maswali ambayo nitahitaji
majibu.Kama Edger hajafa ule
mwili uliokutwa ndani ya gari
lake ukiwa umevaa mkufu ule
wa Edger ambao alikuwa
ameuvaa toka tukiwa Israel ni
wa nani?Na kama bado mzima
yuko wapi na nani
wanaomshikilia? akauliza Dr
Olivia
“Alikueleza Abu dahir
kwamba kutakuwa na hatua kadhaa katika kuutafuta ukweli
kuhusu Edger na hatua ya
kwanza ilikuwa ni kujenga kituo
kile cha utafiti ambacho
kimekamilika na sasa tunaingia
katika hatua ya pili ambayo ni
kuupata ukweli kuhusu Edger
kama kweli yuko hai.Mwili ule
ambao ulikutwa ndani ya gari
ukiwa na mkufu wa Edger na
wewe ukautambua kwamba ni
wa Edger tunataka kuufanyia
uchunguzi kubaini kama kweli
ni mwili wa Edger na hilo zoezi
litafanyika katika kile kituo
chako ambacho dhumuni kubwa la kujengwa kwake
lilikuwa hilo.Tutachukua
sampuli za mabaki ya ule mwili
tutaupima vinasaba kupata
ukweli kama kweli mwili ule
ulikuwa wa Edger na kama
vipimo vikituonyesha kwamba
mwili ule si wake basi tutakuwa
sahihikwamba Edger yuko hai
na hapo tutaingia katika hatua
ya tatu ya kumtafuta na kujua
mahala alipo” akasema Habiba
“Madam Habiba
nakubaliana na wazo hilo la
kuufanyia uchunguzi mwili ule
ambao tunaamini ni wa Edger ili kuupata ukweli.Kama mwili
ule utakuwa si wa Edger
unadhani nani waliomteka
nyara na kwa madhumuni gani?
Yuko wapi? akauliza Dr Olivia
“Ni mapema sana kusema
anashikiliwa wapi na nani lakini
baada ya kupata uhakika
kwamba mwili ule si wa Edger
hapo ndipo tutakapoanza
uchunguzi wetu kuhakikisha
tunafahamu mahala alipo na
nani anamshikilia.Dr Olivia nina
uhakika mkubwa sana kwamba
Edger yuko hai na nitakuomba
sana msaada wako ili tuweze kumpata.Huko aliko naamini
atakuwa anateswa mno na
tusipoharakisha kumuokoa
watamuua.Dr Olivia ninaamini
mambo niliyokueleza leo
yamekustua sana na
kukuogopesha lakini nakuomba
usiogope.Lengo la mimi
kushirikiana nawe ni kwa ajili
ya kunisaidia kumpata Edger
ambaye najua siwezi kumpata
bila msaada wako hivyo
nakuomba tushirikiane
kuhakikisha kwamba Edger
anapatikana akiwa mzima”
akasema Habiba “Madam Habiba ni kweli
mambo uliyonieleza leo
yamenistua na kuniogopesha
hasa baada ya kuifahamu
historia ya Edger.Sikujua kama
Edger ana mahusiano na
kikundi cha IS.Sikujua kwa nini
Edger alihamishiwa
Tanzania.Baada ya kufahamu
haya yote nimeingiwa na hofu
kubwa”
“Nini kinakupa hofu Dr
Olivia?akauliza Habiba
“Kila kitu nilichokifahamu
leo.Ninawaogopa magaidi.Watu
wengi wasio na hatia wanapoteza maisha sehemu
mbali mbali duniani kutokana
na vitendo vya ugaidi.IS ni
kikundi cha kigaidi na
kimekuwa kikifanya mauaji
sehemu mbali mbali
duniani.Nimeingiwa na woga
kufahamu kuwa Edger ana
mahusiano na kikundi hiki cha
kigaidi” akasema Dr Olivia
“Tafadhali usiogope Dr
Olivia” akasema Habiba
“Nchini Tanzania Edger ni
mbunge ambaye ana jina kubwa
sana,anapendwa na watu wengi
na amekuwa mstari wa mbele katika kuendesha mapambano
dhidi ya mafisadi na wahujumu
uchumi.Hana woga wala aibu
katika mapambano
hayo.Amekuwa ni mtetezi wa
wanyonge,amekuwa ni msemaji
wa wale wasiokuwa na sauti ya
kusema.Kutokana na nguvu
yake kubwa ya ushawishi
naamni kama angegombea urais
angeshinda kwa kishindo
kikubwa.Kinachonipa hofu
kwamba nyuma ya mafaniko
hayo yote makubwa aliyonayo
ana siri kubwa ambayo
watanzania hawaifahamu.Pindi watanzania wakijua kwamba
mtu ambaye walikuwa tayari
kumuamini awaongoze kwanza
si mtanzania na pili ana
mafungamano na kikundi cha IS
sina hakika nini kitatokea.Huu
unaweza ukawa ni mwisho wa
Edger.Hiyo ni hofu yangu
kubwa sana” akasema Dr
Olivia.Habiba akatabasamu
kidogo na kusema
“Huna sababu ya kuwa na
hofu Olivia.Hakuna atakayejua
siri hiyo.Ni watu wachache sana
wanaofahamu jambo hili na
wote wamekula kiapo cha utii cha kwenda kaburini na hii
siri.Hakuna atakayeweza kutoa
siri hii kuhusiana na
Edger.Katika watu wachache
wanaoifahamu hii siri
umeongezeka wewe hivyo
utalishwa kiapo cha uaminifu
kwamba hautatoa siri hii na
siku ukifungua ulimi wako
kutamka chochote kuhusiana na
siri hii uliyoifahamu leo
utakuwa ni mwisho wako wewe
na ukoo wako wote.Hakuna
serikali inayoweza kukusaidia
tunao mtandao mkubwa na
tunao uwezo wa kuingia sehemu yoyote.Sikuogopeshi Dr
Olivia lakini tayari nawe ni
mmoja wetu” akasema Habiba
na Dr Olivia akahisi haja ndogo
inataka kumtoka
“Dr Olivia umestuka sana
kusikia kwamba wewe tayari ni
mmoja wetu lakini hilo lilikuwa
ni angalizo tu kwamba
umezifahamu siri zetu hivyo
unapaswa ukae kimya.Hatuna
tatizo na wewe hakuna
atakayekugusa na badala yake
sisi ndio tutakaokuwa
tunakulinda na kuhakikisha
unakuwa salama.Hatuna lengo lolote baya na Tanzania na
ninakuhakikishia kwamba
hakuna damu ya mtanzania
itakayomwagika.Edger
unamfahamu ni mtu mzuri,ana
roho nzuri anaipenda Tanzania
na ni mtu mwenye malengo
makubwa sana na
Tanzania.Nilikueleza awali
kwamba mpango wa kumpeleka
Edger Tanzania ilikuwa ni kwa
ajili ya kulipiza kisasi kwa wale
waliowaua wazazi wangu lakini
baada ya Edger kuupata ubunge
na kuona mambo makubwa
aliyokuwa anayafanya hasa katika kufichua wizi mkubwa
wa rasilimali za nchi
unaofanywa na vigogo niliamua
kubadili malengo yangu na
kuanza kumuunga mkono
katika mapambano yake dhidi
ya wanyonge.Alinieleza namna
anavyoguswa na maisha
wanayoishi watu masikini
ukilinganishwa na utajiri
mkubwa ulioko nchini ambao ni
watu wachache wanaofaidika
nao.Licha ya mipango yetu
lakini umasikini wa
watanzaniani jambo
linalomgusa Edger kutoka moyoni.Aliniomba tuachane na
mpango ule wa kuwatafuta
watu watu waliowaua wazazi
wangu bali tujielekeze katika
kupambana na maadui wa kweli
wa maendeleo ya Tanzania
ambao ni mafisadi na baadhi ya
mataifa makubwa ambayo
yamekuwa yakizinyonya nchi
ndogo na Tanzania
ikiwemo.Wazo hili nililiona ni
zuri na nikaamua kumuunga
mkono,hivyo vita yetu ya sasa
ni kwa mataifa makubwa
ambayo yanazikandamiza nchi
ndogo na Tanzania ikiwemo na vita hii ni ngumu na ndiyo
maana ninataka Edger awe rais
wa Tanzania ili tuwe na nguvu
ya kupambana na mataifa haya
ya magharibi” akasema Habiba.
“Madam Habiba pamoja na
nia hiyo mnayosema ni njema
lakini hakuna atakayeelewa
akisikia kuhusu Edger kuwa na
mafungamano na IS.Bado
machoni pa wengi hiki ni
kikundi cha kigaidi na hakuna
mtanzania ambaye atakubali
kuongozwa na rais ambaye
kwanza si mtanzania na pili ana
mafungamano na kikundi cha kigaidi.Hata mimi siko tayari
madam Habiba kwa Edger
kuongoza nchi.Najua haya ni
maneno ambayo
hayakufurahishi lakini huo ni
ukweli kwamba siko tayari kwa
Edger kuwa rais wa
Tanzania.Nchi yangu Tanzania
ni nchi yenye kuheshimika
duniani kote.Ni nchi ya mfano
kwa mataifa mengine na
ambayo amani imetamalaki
kwa miaka na miaka na katu
siko tayari kuona amani yetu
ikianza kuchezewa.Endapo
Edger akishinda urais utakuwa ni mwanzo wa
kulisambaratisha taifa letu
kwani zitaanza kupandikizwa
chochochoko za dini na taifa lile
zuri ambalo limekuwa ni
kimbilio la wale wote wasio na
kwao litabomoka na hilo ni pigo
kubwa kwa Afrika
nzima.madam habiba
unapozungumzia Afrika
unaizungumzia Tanzania
ambayo kutokana nayo nchi
nyingi zimekombolewa kutoka
katika makucha ya
wakoloni.Tanzania imekuwa
msuluhishi wa mizozo katika nchi mbali mbali ndani ya bara
la Afrika,imekuwa ni nyumba ya
wakimbizi wanaokimbia
mapigano katika nchi zao,sifa
hii ya nchi hii nzuri
iliyobarikiwa haitakiwi
kuharibiwa.Tanzania inapaswa
ibaki kama ilivyo yaani kisiwa
cha amani” akasema Dr Olivia
na kushindwa kuyazuia
machozi kumtoka
“Dr Olivia usilie
tafadhali.Yote uliyoyasema
nimeyasikia lakini
nakuhakikishia kwamba hatuna
malengo mabaya na Tanzania.Tuna malengo mazuri
sana ya kuisaidia nchi yako
unayoipenda.Hata kama Edger
akiwa rais hakuna tatizo lolote
litakalotokea” akasema
Habiba.Ulipita ukimya halafu Dr
Olivia akasema
“Madam Habiba,mwanao
Edger au Seif ni mtu wangu wa
karibu katika kipindi kifupi
nilichofahamiana naye alidiriki
hata kunitamkia kwamba
ananipenda japo sikumpa jibu
lolote kwa sababu kwanza
tulikuwa hospitali na pili
kipindi tulichofahamiana kilikuwa kifupi sana lakini
nakiri kwako kwako kwamba
hata mimi nilikwisha anza kuwa
na hisia na Edger japo
sikumueleza.Nilitaka akitoka
hospitali tuoate muda wa
kutosha kuthibitsha kama hisia
zetu ni za kweli lakini
hatukupata huo muda
akatoweka.Baada ya kuufahamu
ukweli kuhusu Edger sina
hakika kama hata akipatikana
nitaendelea kuwa na urafiki
naye lakini nitashirikiana nanyi
katika kumtafuta.Pamoja na
hayo mimi na wewe lazima tuwe na makubaliano” akasema
Dr Olivia
“Edger hakuwahi
kunitamkia chochote kuhusu
kumpenda mwanamke yeyote
na sina hakika kama maneno
hayo aliyokutamkia amewahi
kumtamkia mwanamke
mwingine.Kitu gani mimi na
wewe unataka tukubaliane
Olivia?akauliza Habiba.Dr Olivia
akamtazama Habiba usoni kwa
muda halafu akasema
“Nitaendelea kushirikiana
nanyi katika kumtafuta Edger
lakini kwa sharti moja kwamba endapo akipatikana
hatajishughulisha tena na
mambo yoyote yanayohusiana
na siasa na mpango wa
kumtaka agombee urais
hautakuwepo tena” akasema Dr
Olivia.Habiba Jawad
akatabasamu na kuuliza
“Ni vipi kama nikisema
hapana?
“Sintashiriki katika mpango
wowote wa kumtafuta
Edger”akasema Dr Oliviana
sura ya Habiba ikabadilika
“Mungu nisaidie hiki
ninachokifanya ni hatari kubwa watu hawa wanaweza
wakaniua muda
wowote.Natakiwa kuwa makini
sana”akawaza Dr Olivia
akitazamana na Habiba
“Madam Habiba kwa sasa
mnanihitaji sana katika mpango
huu na ili nishiriki lazima
mkubaliane na hicho
ninachokitaka” akasema Dr
Olivia.Habiba alimtazama Dr
Olivia hadi akaingiwa na wasi
wasi
“Hakuna tatizo na hicho
unachokihitaji.Ninachokitaka
mimi ni mwanangu apatikane hata kama itakuwa ni kwa
kuvuruga mipango yetu yote
niko tayari,hata hivyo nawe
lazima ulishwe kiapo cha
kuilinda siri hii hadi
kaburini.Hatakiwi mtu
mwingine yeyote kujua”
akasema Habiba.
DAR ES SALAAM
Dr Olivia alirejea Dar es
salaam tayari kabisa kuanza
mchakato wa kuutafuta ukweli
kuhusu Edger Kaka ambaye kila ....
OLIVIA MWANAMKE UNA ROHO NGUMU WEWE😊😊😊😊
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom