Riwaya: Siri

SIRI
Episode 19
Mtunzi. Patrick CK

Donald Nkebo akiwa
nyumbani kwake akijipumzisha
simu yake ya mkononi
ikaita.Akatazama mpigaji alikuwa
ni Paul.Akatabasamu kwa sababu
alijua kila Paul anapompigia basi
kuna taarifa nzuri.
“Hallo Paul” akasema
“Donald kazi
imekwisha.Mambo yamekwenda
vizuri sana na tayari fumanizi la
aina yake limefanyika na hivitunavyoongea Damian Mwamba
amekimbizwa hospitali baada ya
kupoteza fahamu mara tu
alipofumaniwa.Yule msichana
mwanafunzi aliyekuwa naye
amepelekwa kituo cha polisi kwa
ajili ya mahojiano” Paul akasema
“Ahahaha hahahaa
hahahaaaaa….haaaha..ahaahahaaaa
!! Donald akacheka kicheko
kikubwa sana baada ya taarifa ile.
“Paul katika maisha yangu
sijawahi kufurahi kama siku ya
leo.Nimepatwa na furaha
inayopitiliza.Mr Mwamba is down
now…ahahaahaa ahahaaha…”
Nkebo akaendelea kucheka
“Kazi nzuri sana umeifanya Paul.Wewe na vijana wako
mnastahili pongezi.Lakini
mheshimiwa rais alikwisha ahidi
kwamba baada ya kazi hii
mtafurahi wenyewe.”
“Mr Donald kwa upande wetu
naona suala la Mr Mwamba
tumelimaliza kilichobaki ni kwa
upande wenu kuhakiksha kwamba
anafungwa gerezani.Hata kama
ikitokea akishinda hii kesi basi
hataweza tena kugombea urais
kutokana na aibu kubwa
aliyoipata.Kwa maana hiyo baada
ya kumalizana na suala la Mwamba
kwa sasa nguvu zote tunazielekeza
kwa Edger.Lazima ndani ya muda
mfupi ujao Edger naye awe ametoweka katika ramani ya siasa.”
Paul akasema kwa kujiamini
“Nakubaliana nawe
Paul.Kuhusu Mwamba hapa
mlipofika panatosha na sisi
tutachukulia kuanzia hapa na
tutahakikisha kwamba ni lazima
afungwe gerezani.Kuhusu Edger
mmejipangaje?
“NInataka kuwasiliana na
mwenzetu aliyeko Israel ili kumpa
maelekezo nini cha kufanya kuhusu
Edger” akasema Paul
“Sawa Paul.Nitamfikishia
taarifa hizi mheshimiwa rais
naamini atafurahi mno.Tafadhali
nijulishe kila kinachoendelea katika
mikakati yenu kwa Edger” akasema Donald na kukata simu.Alikuwa
amefurahi kupita kiasi.
Mara tu baada ya kuzungumza
na Donald ,Paul akatazama
kompyuta yake kama Judy
ametuma ujumbe wowote lakini
hakukuwa na ujumbe wowote
kutoka kwa Judy
“Nimemtumia ujumbe
anitafute lakini mpaka sasa naona
kimya na mtandaoni
hapatikani.What’s the
problem?akajiuliza Paul na kutuma
tena ujumbe mwingine akimsisitiza
Judy amtafute haraka sana pindi
atakapoupata ujumbe ule.
“Kwa nini nisipige simu katika
hoteli ile aliyofikia na kuomba kuunganishwa na chumba chake?
Paul akapata wazo
“Nadhani hili ni wazo zuri”
akawaza Paul na kupiga simu
katika hoteli ile aliyokuwa amefikia
Judy akaomba kuunganishwa na
chumba chake.Jibu alilopewa
lilimstua na kumfanya aketi kitini.
“This in unbelievable !!
akasema .
“Nini kimemuua Judy?Mbona
hakuwa na tatizo lolote la
kiafya?akajiuliza na bila kupoteza
muda akampigia simu Donald
Nkebo
“Kuna habari mpya
paul?akauliza Donald baada ya
kupokea simu “Mr Donald we have a big
problem”akasema Paul na kumstua
sana Donald
“Kuna tatizo gani Paul?
“Judy yule mtu wetu aliyekuwa
Israel akimchunguza Edger
amekutwa amekufa chumbani
kwake”
“Paul hiyo ni taarifa ya
kweli?akauliza Donald kwa
wasiwasi
“Nimekuwa nikimtumia
ujumbe mtandaoni tuwasiliane
lakini hakujibu nikaamua kupiga
simu katika hoteli alikofikia na
wakanijulisha kuhusu kifo
chake.Nimechanganyikiwa hapa
nilipo kwani Judy alikuwa mzima na hakuwa na tatizo lolote la
kiafya”
“Paul hii taarifa imenistua
sana.Unahisi Judy atakuwa
ameuliwa?akauliza Donald
“Ninahisi hivyo kwani kifo
chake kimekuwa cha ghafla
sana.Kuna ulazima wa kufanya
uchunguzi haraka sana kujua
namna Judy alivyofariki.Donald
nataka vijana wawili watumwe
nchini Israel haraka sana kwenda
kufanya uchunguzi wa suala hili ili
tujue chanzo cha kifo chake.Nataka
utuwezeshe kwa hilo Donald”
akasema Paul
“Paul hilo ni suala zuri.Kuna
ulazima wa kufanya uchunguzi kufahamu chanzo cha kifo cha
Judy.Nipe majina ya watu ambao
watakwenda huko ili nianze
kushughulikia suala hilo haraka
iwez……”
“Donald I’ll call you back!!
Akasema Paul na kumkatisha
Donald aliyekuwa anazungumza
“Paul kuna tatizo?akauliza
“I’ll call y…aaagghh!! Paul
alitoa mlio.
“Paul ..Paul !! akaita Donald
lakini simu ikakatwa na kuzimwa
kabisa.
“What happened?.Mbona Paul
ametoa sauti ya kukugumia kwa
maumivu kama vile amepigwa na
kitu? akajiuliza Donald na kupiga simu ya mmoja wa wasaidizi wa
Paul lakini naye simu yake haikuwa
ikipatikana.
“Something is not right”
akawaza Donald
“Ninaanza kuwa na hisia
mbaya kwamba kuna jambo baya
limetokea kwa Paul.Nafahamu ilipo
ofisi yao lazima nikajue nini
kimetokea” akawaza Donald na
kuingia garini akaondoka kuelekea
katika ofisi za akina Paul.
Aliwasili katika nyumba iliko
ofisi ya akina Paul akashuka garini
kwa tahadhari kubwa akaenda
getini akajaribu kusukuma mlango
mdogo pembeni ya geti ulikuwa
wazi akaingia ndani.Magari matatu yalikuwamo mle ndani akalitambua
gari la Paul.Taa zilikuwa zinawaka
ndani kuashiria kulikuwa na watu.
“Gari la Paul hili hapa hii
inaonyesha kwamba yuko ndani”
akawaza Donald na kwenda katika
mlango mkubwa wa kuingilia
sebuleni akagonga lakini
hakujibiwa akakinyonga kitasa cha
mlango ukafunguka na mara tu
alipoingia sebuleni akakutana na
watu wanne wakiwa wamelala
sofani wote wakiwa wamepigwa
risasi vichwani.Moyo ulitaka
kumpasuka kwa mstuko mkubwa
alioupata.Akaenda katika chumba
ambacho Paul hukitumia kama ofisi
yake na kumkuta Paul akiwa amelala sakafuni katika dimbwi la
damu.Mwili wote ukaanza
kumtetemeka kwa woga akatoka
mbio hadi garini lakini kabla
hajawasha gari risasi ilipenya kioo
cha mbele cha gari lake na kutua
katika paji la uso na bila kelele uhai
ukamtoka.Mlango wa gari
ukafunguliwa na mtu mmoja
aliyevaa glovu mkononi akamsachi
na kuchukua simu ya Donald
“Orodha ya wote waliokuwa
wanawasiliana imekwisha amebaki
mmoja tu ambaye ni waziri
mkuu.Yeye tunamuondoa kesho
asubuhi” akasema yule jamaa
akizungumza na simu **************
Saa nane za usiku,katibu mkuu
wa chama alimpigia simu rais Dr
Evans akamfahamisha kuhusiana
na taarifa za kifo cha Damian
Mwamba.Dr Evans alionyesha
mstuko mkubwa kwa taarifa ile.
“Nini kimesababisha kifo
chake?akauliza DrEvans
kanakwamba hafahamu chochote
kuhusiana na kilichomtokea
Damian mwamba.Katibu mkuu
akamueleza kila kitu kilichotokea.
“Baada ya kupoteza fahamu
katika funamizi lile alipelekwa
hospitali kuu ya mjini Morogoro
lakini hali yake haikuwa nzuri ikalazimu akimbizwe hapa Dar es
salaam katika hospitali kuu ya
Muhimbili lakini alifariki muda
mfupi tu baada ya kufikishwa
katika hospitali ya Muhimbili.”
akasema katibu mkuu
“Nashindwa niseme nini
katibu mkuu kwa namna
nilivyostushwa na taarifa
hizi.Ninaelekea huko Muhimbili
kuthibitisha taarifa hizi” akasema
rais na kukata simu kisha
akatabasamu
“Mbuyu wa kwanza
umeanguka.Damian is down.Haya
ni mafanikio makubwa sana”
akawaza na kumpigia simu Donald
Nkebo lakini simu yake haikupatikana.
“Imekuaje Donald akazima
simu wakati tuna operesheni
kubwa inaendelea?akawaza na
kuagiza walinzi wake wajiandae
wanaelekea hospitali kuu ya
Muhimbili kuthibitisha kuhusu kifo
cha Damian Mwamba.
“Ni lazima nifike pale usiku
huu ili nihakikishe kama ni kweli
mwamba amefariki dunia.Lazima
nionyeshe kuguswa kwa hali ya juu
na kifo chake kwani nisipoonyesha
namna yoyote ya kuguswa na
msiba huu yanaweza yakaibuka
maswali mengi kwa sababu
inafahamika mimi na mwamba
tulikuwa marafiki wakubwa.” Akawaza Dr Evans akivaa koti lake
akatoka na kuingia garini kisha
msafara ukaondoka ikulu kuelekea
hospitali ya taifa ya Muhimbili.
Taarifa za kifo cha Damian
Mwamba zilisambaa kwa kasi ya
ajabu na japokuwa ni usiku lakini
watu walianza kufika pale hospitali
kuthibitisha taarifa zile kama ni za
kweli.Waandishi wa habari pia
walikuwepo wakijaribu kuripoti
kwa upana juu ya kifo kile cha
kustusha cha Damian mwamba.
Vingora vya gari la polisi
vilisikika na kuzidi kuikaribia
hospitali ya Muhimbili , viliashiria
kwamba kuna kiongozi wa kitaifa
aliyekuwa akielekea eneo lile.Msafara wa magari ukaingia
muhimbili na kuelekea moja kwa
moja hadi katika chumba cha maiti
na kisha akashuka rais.Baada tu ya
kushuka garini akasalimiana na
baadhi ya wabunge wa chama
chake waliokuwa wamefika pale na
kisha moja kwa moja akaingia
ndani ya chumba kile cha
kuhifadhia maiti na kuomba auone
mwili wa mheshimiwa mbunge
Damiani mwamba.Mwili wa
Damiani Mwamba ukaletwa mbele
ya mheshimiwa rais ambaye
akalifunua shuka lililokuwa
limemfunika na kwa mikono yake
akakishika kichwa cha
mwamba.Kwa dakika zipatazo mbili mheshimiwa rais bado
aliendelea kukishika kichwa cha
mheshimiwa mwamba huku macho
yake yakionyesha michirizi ya
machozi.Dr Evans alionyesha ni
jinsi gani alivyokuwa ameguswa na
kifo kile cha mmoja wa wanasiasa
wenye nguvu sana nchini.
Taratibu akalifunika shuka lile
na kisha mwili wa mr Mwamba
ukaondolewa na kurudishwa
ndani.Mheshimiwa rais akaanza
kutoka na mara akajikuta
amezungukwa na kundi la
waandishi wa habari waliotaka
kumuuliza maswali.
“Mheshimiwa rais umekuwa ni
mtu wa karibu sana na Damian Mwamba unaweza ukatueleza ni
kwa namna gani ulivyoguswa na
kifo hiki?
“Sipati maneno mazuri ya
kueleza namna nilivyoguswa na
kifo hiki cha rafiki yangu wa siku
nyingi sana Damian Mwamba ndiyo
maana mara tu nilipopata taarifa za
kifo chake imenilazimu kuja
hospitali kuthibitisha kama ni kweli
amefariki.Nimeumizwa sana na kifo
chake lakini hii ni njia ambayo sote
tunapita.Ninatoa pole kwa familia
yake,wanachama wa chama chetu
na watanzania kwa ujumla”
akasema Dr Evans
“Mheshimiwa rais unaweza
ukamuelezeaje Damian Mwamba?akauliza mmoja wa
waandishi wa habari
“Ukitaka nimuelezee Damian
ninaweza kutumia siku nzima na
nisimalize kwani ni mtu mwenye
mambo mengi sana ya
kumuelezea.Ana historia
ndefu.Ninaweza kusema Mwamba
alikuwa ni kiongozi wa
mfano.Alikuwa ni mwanasiasa
mzalendo ambaye alifahamu watu
wa Tanzania walihitaji nini.Mimi
nimebahatika kufanya naye kazi
kwa muda mrefu,hata nilipopata
urais nilimpatia nafasi katika
baraza la mawaziri na aliifanya kazi
yake kwa weledi mkubwa.Baada ya
kulivunja baraza la mawaziri,kwa hiari yake mwenyewe aliniomba
nisimuweke tena katika nafasi ya
uwaziri kwani alihitaji
kupumzika.Pamoja na kutokuwepo
katika baraza jipya la mawaziri
lakini bado ameendelea kuwa na
mchango mkubwa kwangu na kwa
serikali.Pamoja na dhoruba za hapa
na pale za maisha ya kibinadamu
lakini nathubutu kusema kwamba
tumempoteza kiongozi mahiri sana
katika kupigania haki za
wanyonge.Hakuna asiyefahamu
uhodari wa Damian Mwamba
katika kuwaletea wananchi
maendeleo,alikuwa ni mtu mwenye
misimamo isiyoyumba.Kuna mengi
sana ya kumuelezea Damian Mwamba itoshe tu kusema kwamba
ameacha pengo kubwa sana”
akasema Dr Evans
“Mheshimiwa rais
unaongeleaje tukio lililotokea mjini
Morogoro ambalo linadaiwa
kwamba ndilo limesababisha kifo
chake?akauliza mwandishi
mwingine wa habari
“Kwa suala hilo vipo vyombo
maalum vya kulisemea.Ahsanteni
san waandishi” akasema Dr Evans
na walinzi wake wakawazuia
waandishi wa habari wasimuulize
rais swali lingine,wakamuongoza
hadi katika gari lake na kuondoka
pale hospitali ****************
Damian Mwamba afariki
dunia..Utata kifo cha Damian
Mwamba…
Hivi ni baadhi tu ya vichwa vya
habari vilivyopamba kurasa za
mbele za magazeti mbali mbali
asubuhi kuhusiana na tukio la
kukamatwa kwa mbunge Damian
Mwamba aliyekamatwa akiwa
katika nyumba ya wageni na
mwanafunzi wa sekondari mjini
Morogoro pamoja na kifo chake
kilichotokea katika hospitali ya
Muhimbili.
Picha mbali mbali
zilizoonyesha namna hali
ilivyokuwa chumbani baada ya Damian Mwamba kufumaniwa
akiwa na mwanafunzi chumbani
zilisambaa katika mitandao mbali
mbali ya kijamii.Kwa ujumla hii
ndiyo taarifa kubwa iliyotikisa nchi
asubuhi.
Wakati suala la Damian
mwamba likizidi kuchukua nafasi
kubwa na kuzungumzwa kila kona
ya nchi,Jijini Dodoma waziri mkuu
wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania aliondoka katika makazi
yake na kuelekea ofisini kwake
kabla ya kuhudhuria kikao cha
bunge kinachoendelea jijini
Dodoma.Mara tu gari lake lilipokata
kona kuingia katika geti la kuingilia
katika ofisi yake ulitokea mlipuko mkubwa.Mabomu mawili
yaliyokuwa yametegwa katika
mapipa mawili ya kuhifadhia
takataka yaliyokuwa pembeni ya
geti kubwa yalilipuka.
Taarifa za mlipuko ule zilifika
haraka kwa jeshi la polisi na kwa
kasi kubwa magari yaliyojaza
askari yakafika kwa haraka.Vikosi
vya zimamoto na uokozi navyo
vilifika kwa haraka sana eneo la
tukio na kuuzima moto uliokuwa
unawaka katika magari yaliyokuwa
kwenye msafara wa waziri
mkuu.Waziri mkuu wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania pamoja na
watu wengine kumi na sita
walipoteza maisha katika mlipuko ule mkubwa.Hofu kuu ilianza
kutanda nchini
USIKOSE SEHEMU YA 3
 
Upande wa Zidaa ushafekwa mbali....hapa ni kama wanaanza upyaaaaaaaaaa....Edgar Kaka kashinda
 
SIRI
season 3
Episode 20
Mtunzi. Patrick CK

HAIFA – ISRAEL
Saa nane kasoro dakika
ishirini kwa saa za
Israel,mlango wa chumba
alimolazwa Edger kaka
ulifunguliwa na watu watano
wakaingia wakiongozwa na
mmoja aliyevaa koti la
daktari,wawili wakabaki
mlangoni.Edger alikuwa
amelala fofofo yule jamaa
mwenye koti la daktari
akamuamsha.
“Edger amka uzungumze na
wageni wako” akasema yule
jamaa aliyevaa koti la kidaktari.Edger akafumbua
macho na kukuta kuna watu
mle chumbani akainuka na
kukaa akafikicha macho ili
aweze kuona vizuri. Miongoni
mwa watu wale alikuwemo
mwanamama aliyejitanda
ushungi kichwani.
Baada ya Edger kuinuka na
kukaa watu watatu wakatoka
mle chumbani na kuwaacha
watu wawili tu.Yule
mwanamama akavua ule
ushungi aliokuwa amejitanda
na uso wa Edger ukachanua
kwa tabasamu pana “Mama ! akasema Edger na
kuinuka akaenda kumkumbatia
mama yake
“Edger ! Akasema
mwanamama yule ambaye ni
Habiba Jawad.Walikumbatiana
kwa dakika mbili halafu Edger
akapeana mkono na mtu
aliyekuwa pembenmi
“Sayid Omar,nafurahi
kukuona” akasema Edger
“Pole sana Edger” akasema
Sayid.Edger akawakaribisha
wageni wake katika sofa
lililokuwamo mle chumbani “Mama nimefurahi sana
kukuona.Ahsante kwa kuja
kunitembelea” akasema Edger
“Hata mimi nimefurahi sana
kukuona Edger.Imenilazimu
kufanya kila niwezalo kuja
kukuona
mwanangu.Nimeumizwa sana
na hawa washenzi waliotaka
kuyaondoa maisha
yako.Ninakuahidi kwamba wote
walioshiriki katika jaribio hili la
kukuua tutawasaka na hakuna
atakayebaki salama.Najua ni
mtandao mkubwa wa maadui
zako ambao hawalali wakipanga mipango ya
kukuangamiza” akasema
Habiba Jawad
“Jaribio lao
limeshindwa.Hali yangu ni
nzuri kwa sasa” akasema Edger
“Edger napenda pia
kukuhakikishia kwamba kwa
sasa kuwa na amani kwani uko
salama.Kama alivyosema
Habiba mtandao wa maadui
zako ni mkubwa na walituma
watu wao kukufuata hadi huku
kutafuta namna ya
kukumaliza.Watu waliotumwa
kukufuatilia walitega vifaa humu chumbani kwako bila
wewe kujua.Walitega kamera za
siri na walikuwa wanaangalia
kila unachokifanya,vilitegwa
vifaa vingine pia ambavyo
viliweza kunasa mawasiliano
yako yote uliyokuwa
unayafanya na kuwatumia
wakuu wao.Ni mtandao
mkubwa uliowahusisha pia
watu wakubwa serikalini lakini
taarifa nzuri ni kwamba tayari
tumekwisha ubaini mtandao
huo na tayari hatua za haraka za
kuuondoa zimeanza na hivi
tuongeavyo vijana wako kazini wakiendelea na kazi ya
kuusafisha na hatabaki mtu
yeyote tutahakikisha wote
tumewasafisha” akasema Sayid
Omar
“Nashukuru sana Sayid kwa
kuweza kulitambua hilo kwa
haraka kwani mimi sikuwa na
mawazo kama wangeweza
kunifuata hadi huku.Unaweza
ukanitajia baadhi ya watu
waliomo katika mtandao huo
niwafahamu? akauliza Edger
“Hapana Edger sintaweza
kukutajia kwa sasa lakini
ninachoweza kukushauri ni kuwa makini sana.Kuanzia sasa
usimuamini mtu yeyote
yule.Yule unayemuamini ndiye
huyo atakayekuingiza kwenye
shimo la moto hivyo jaribu
kuchagua watu wachache wa
kuwaamini na kuwaweka
karibu.Mipango yako
usimueleze mtu ambaye hauna
imani naye.Umenielewa Edger?
Akauliza Sayid
“Nimekuelewa Sayid”
akajibu Edger
“Edger” akaita Habiba
“Naam mama” “Hiki kilichotokea kimezidi
kutupa sababu ya wewe
kugombea urais.Hadi sasa
tayari umekwisha jenga maadui
wengi na mtandao wao unazidi
kutanuka na kila uchao
wanapanga
kukuangamiza.Wakati umefika
kwa wewe kugombea
urais.Hatuna tena muda wa
kusubiri kwani tunavyoendelea
kuvuta muda na kusubiri zaidi
maadui zako wanaendelea
kujipanga zaidi namna ya
kukuangamiza.Edger
tumekuandaa kwa muda mrefu kwa ajili ya nafasi hiyo na
mpaka hapa tulipofika
maandalizi yetu yanakwenda
vizuri.Tayari umekwisha
tengeneza wafuasi wengi
ambao ndio mtaji mkubwa kwa
mwanasiasa kushinda
chaguzi.Nguvu yako ni kubwa
na unazidi kuwapa hofu maadui
zako.Kwa upande Fulani
ninawashukuru hawa
waliofanya jaribio hili la kukuua
kwani wametufanya na sisi
macho yetu yafumbuke zaidi na
kung’amua kwamba wakati
umefika.Ninashukuru Edger kwa kukubali kugombea urais
kwani ile mipango yetu yote
inakwenda kutimia” akasema
Habiba
“Mama sikuwa nimepanga
kugombea urais kwa wakati
huu,mipango yangu ilikuwa
nigombee baada ya miaka
mitano ijayo lakini kwa hili
lililojitokeza na kwa ushauri
nilioupata kutoka kwa Sayid
nimeamua kugombea urais
katika uchaguzi mkuu ujao.Uko
sahihi kwamba tayari
nimekuwa na maadui wengi na
wanaongezeka kila uchao na njia pekee ya kuweza
kuwashinda maadui zangu ni
kwa kuwa rais.Nina uhakika
mkubwa wa kushinda uchaguzi
kutokana na mtaji mkubwa wa
wafuasi nilio nao.Tayari
nimejenga jina kubwa na
wananchi wengi wananiamini
na nina hakika nitashinda kwa
ushindi mkubwa. Lakini
…”akanyamaza kidogo
“Lakini nini Edger?akauliza
Habiba
“Nimeamua nitagombea
kupitia chama cha upinzani cha
Democratic ambacho tayari mazungumzo yamekwisha anza
ili niweze kujiunga nao”
“Hapana Edger” akasema
Habiba
“Hautagombea urais kupitia
chama cha upinzani.Utagombea
urais kupitia chama
chako.Kuhama chama
kunaweza kuzusha maswali
mengi,utaonekana u mroho wa
madaraka.Kampeni za rais ni
gharama kubwa hivyo basi kwa
vyama vidogo kama hicho
unachotaka kuhamia lazima
kitachunguzwa sana namna
kilivyoweza kugharamia kampeni na wanaweza
wakagundua mambo ambayo
hatutaki yajulikane.Ukiwa ndani
ya chama chako hakuna
atakayeweza kukuhisi chochote
kwani kampeni zako
zitagharamiwa na chama chako
ambacho ni kikubwa na kina
rasilimali za kutosha hivyo basi
utaendelea kugombea urais
lakini kupitia chama
chako”akasema Habiba Jawad
“Mama hayo uyasemayo
ninayafahamu na hata mimi
ningependa sana kugombea
urais kupitia chama changu lakini kuna tatizo ndiyo maana
nikafikiria kuhama chama”
“Kuna tatizo gani
Edger?akauliza Sayid Omar
“Tatizo ni kwamba nguvu
yangu kubwa iko nje ya
chama.Ndani ya chama sina
nguvu kubwa na sina uhakika
kama ninaweza kuteuliwa na
chama kugombea.Kuna
mchuano mkubwa ndani ya
chama vigogo wenye nguvu
wakichuana nani achaguliwe
kupeperusha bendera ya chama
katika uchaguzi mkuu
ujao.Kama nguvu yangu ingekuwa kubwa chamani
ningekubaliana nawe mama
lakini nguvu yangu kubwa iko
nje ya chama ndiyo maana
nikafikiria kuhama chama na
kujiunga na chama kingine ili
niweze kutumia nguvu yangu ya
nje kushinda urais.Nikiwa ndani
ya chama changu
ninawahakikishia kwamba
sintaweza kufika kokote”
akasema Edger
“Edger wasi wasi wangu ni
kwamba kuhama chama
kutakupunguzia mvuto.Ushauri
wangu ni kwamba endelea kubaki ndani ya chama chako
ila unachohitaji ni kuunda timu
yenye nguvu ambayo
itakuwezesha wewe uweze
kuteuliwa ndani ya chama
kupeperusha bendera katika
uchaguzi mkuu ujao wa
rais.Tutaunganisha baadhi ya
vigogo wenye ushawishi
chamani na watakubali kwani
kinachoongea ni fedha.Tuachie
sisi suala hilo tutalishughulikia
lakini achana kabisa na
mipango yoyote na vyama
pinzani.Utagombea urais kupitia chama chako na
utashinda” akasema Habiba
“Mama nimeamua
kugombea urais kupitia chama
cha upinzani kwa sababu mimi
ndiye niliye ndani ya chama na
ninafahamu kinachoendelea
ninafahamu fitina zilizopo
ndani ya chama hivyo naombeni
mkubaliane nami nijiunge na
chama cha upinzani.Msihofu
kitu kwani ninao mtaji mkubwa
wa wafuasi na kokote
nitakakoenda watanifuata.Wote
wanafahamu namna
ninavyoikososa serikali na kupambana na mafisadi ndani
ya chama changu na
wananiunga mkono.Kitendo cha
mimi kuwekewa sumu pia
kitakuwa ni kigezo kikubwa
sana cha mimi kuhama chama
na nitakapowaeleza wananchi
wataniamini” akasema
Edger.Habiba na Sayid
wakatazamana kwa muda kisha
Habiba akasema
“Tunakwenda kulijadili
suala hili tuone ipi itakuwa njia
bora zaidi ya wewe kugombea
urais aidha ukiwa ndani ya
chama chako au ukiwa nje ya chama.Jibu tutakalopata
tutakujulisha.Edger nimefurahi
nimekuona na yawezekana
hatutaweza kuonana tena
kwani usalama wetu ni mdogo
sana hapa Israel lakini
tutaendelea kuwasiliana kama
kawaida” akasema Habiba na
kumkumbatia Edger
wakaagana.
“Sayid ameniambia
kwamba walitumwa kuja
kunichunguza ni watu wangu
wa karibu,ni akina nani
hao?Watu nilio nao karibu hapa
hospitali ni Olivia na Judy je kuna mmojakati yao ametumwa
kunichunguza?Nahisi labda
anaweza kuwa Judy kwani
sidhani kama Olivia anaweza
akafanya hivyo.Yeye ndiye
aliyenileta hapana kuokoa
maisha yangu.Nilishuhudia
vifaa vile vilivyotolewa humu
chumbani vilivyotegwa
kunifuatilia nina hofu kama
wameweza kunasa mawasiliano
yangu na Sayid wanaweza
wakaniharibia kabisa mipango
yangu yote ya kuwania
urais.Wakigundua kwamba
Sayid ni mfadhili mkubwa wa kikundi cha IS jina langu
litachafuka mno na kitakuwa ni
kifo changu cha kisiasa.Sitaki
siri yangu ijulikane hadi hapo
lengo langu litakapotimia.Sayid
amenihakikishia kwamba
wanalifuatilia suala hili na
mtandao wote
wataufagia.wanatakjiwa
wafanye haraka sana kuufagia
mtandao huu kabla hawajaleta
madhara” Kichwa cha Edger
kilikuwa na mawazo mengi
sana baada ya Habiba na Sayid
kuondoka pale hospitali TEL AVIV – ISRAEL
Saa tatu za asubuhi katika
chumba kimoja ndani ya jengo
la makao makuu ya shirika la
ujasusi la Israel Mossad, watu
wanne walikuwa ndani ya
chumba cha mikutano
wanamsubiri mkurugenzi mkuu
wa shirika hilo kwa ajili ya
kikao muhimu.Mkurugenzi
mkuu ambaye alikuwa njiani
akitokea nyumbani kwake
aliwasili ndani ya muda mfupi
baada ya kupewa taarifa
kwamba anahitajika kwa jambo muhimu la usalama wa
taifa.Yitzhak Zamir mkurugenzi
mkuu wa Mossad alipowasili
katika chumba kile akaomba
wajielekeze moja kwa moja
katika kile kilichowakutanisha
pale kwani alikuwa na
mazungumzo na waziri mkuu
saa tano asubuhi.
“Mkurugenzi tumelazimika
kukuita hapa asubuhi hii
kuhusiana na suala muhimu”
akasema David Shiloah na
kumfanyia ishara Yair aendelee
kutoa maelezo “Siku chache zilizopita rais
wa Tanzania alimpigia simu
waziri mkuu na kuomba
mgonjwa wake ambaye ni
mbunge wa bunge la jamhuri ya
muungano wa Tanzania
aliyekuwa mahututi,aruhusiwe
kuingia hapa nchini kupata
matibabu.Kutokana na
mahusiano mazuri kati ya
Tanzania na Israel waziri mkuu
alitoa maelekezo kwa mgonjwa
huyo kuruhusiwa kuingia nchini
kutibiwa na alipoletwa hapa
nchini alipelekwa Haifa katika
hospitali ya Rambam.Wakati wakimpatia matibabu
madaktari waligundua kwamba
mbunge alipewa sumu.” Yair
akanyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Dr Olivia Themba kutoka
hospitali kuu ya moyo nchini
Tanzania ambaye ndiye
aliyeambatana na mgonjwa
huyo alimjulisha spika wa
bunge la jamhuri ya muungano
wa Tanzania suala hilo la Edger
kuwekewa sumu na spika
akamjulisha waziri
mkuu.Inahisiwa sababu ya
kutaka kuuawa kwa mbunge huyo ni chuki za kisiasa kwani
amekuwa ni mahiri sana katika
kufichua ufisadi unaofanywa
nchini mwake hasa na watu
wakubwa serikalini hivyo
amejijengea maadui
wengi.Baada ya kupata taarifa
kuwa Edger aliwekewa sumu
waziri mkuu wa Tanzania
aliamua kuchukua hatua za
kumlinda kwa kuhofia kwamba
watu waliotaka kumuua
wangeweza kumfuata hata kule
Israel kummalizia.Nina urafiki
na waziri mkuu wa
Tanzania,aliwahi kunisaidia kupata hifadhi Tanzania kwa
muda wa mwaka mmoja
nilipokuwa nawafuatilia wale
magaidi waliokwenda kujificha
Zanzibar.Kutokana na urafii
wetu alinipigia simu akaniomba
nimsaidie mmoja wa vijana
wake ambaye atamtuma hapa
Israel kumlinda
Edger.Niliwasilisha suala hili
kwa kiongozi wangu David
nikamueleza na yeye akanipa
ruhusa na kufanya
hivyo.Nilifanya maandalizi na
Dickson alipokuja hapa
nilimpeleka katika ile hospitali akiwa kama mgonjwa kutokea
nchini Zimbabwe.Dickson
aliweka kamera za siri katika
chumba cha Edger na aliweza
kuona kila kinachofanyika
ndani ya chumba kile.Usiku wa
kuamkia jana watu wawili
mwanamke na mwanaume
waliingia ndani ya chumba cha
Edger lakini hawakuweza
kuongea naye kwa kuwa
alikuwa amelala fofofo.Dick
alinitumia picha za mwanamke
yule akinitaka nimsaidie
kumtambua na nilipomuona tu
nilistuka baada ya kumuona mwanamke yule ni Habiba
Jawad”
“Habiba Jawad? Yitzhak
akastuka
“Ndiyo mkurugenzi”
akajibu Yair
“Mna uhakika ni
mwenyewe Habiba
Jawad?akauliza Yitzhak.
“Ndiyo mkurugenzi.Tuna
uhakika ni mwenyewe”
akasema Yair na kutoa picha
kutoka katika faili lililokuwa
mbele yake akampatia
mkurugenzi wake akazipitia
“Endelea” akasema Yitzhak “Aliposhindwa kuzungumza
na Edger,Habiba alimuachia
ujumbe uliokuwa katika
bahasha.Dick aliichukua
bahasha ile akakuta kuna
namba za simu ambazo Edger
alielekezwa apige.Alinipigia
simu na usiku ule ule bila
kupoteza muda nilifika pale
hospitali.Tuliamua kupiga
namba zile za simu Habiba
alizomuachia Edger ili
kufahamu mahala
alipo.Nilifanikiwa kupata simu
ambayo ingetusaidia kufahamu
mahala aliko Habiba na Dick akaitumia kupiga zile namba
alizoacha Habiba lakini baada
ya simu kupokelewa Habiba
aligundua kwamba yule hakuwa
Edger akakata simu haraka
hivyo hatukuweza kujua mahala
alipo.Hakukata tamaa Dick
aligundua kwamba Edger
alikuwa anatumia kompyuta
yake kuwasiliana na watu wake
muhimu kwa kutumia mtandao
wa Skype hivyo siku iliyofuata
Dick akafanikiwa kuipata
kompyuta ya Edger na
kugundua kwamba amekuwa
na mawasiliano na Sayid Omar” “Sayid Omar bin
Abdullah?akauliza Yitzhak
“Ndiyo mkurugenzi.Edger
amekuwa na mawasiliano
naye”akajibui Yair
“Sasa nimepata picha
nzuri.Kwa mujibu wa taarifa za
uchunguzi tulizonazo ni
kwamba Habiba na Sayid ni
washirika wakubwa na Sayid
anatumiwa na Habiba katika
kufadhili kikundi cha IS
ambacho kinaendeleza harakati
zake sehemu mbalimbali
duniani.Kama huyo Edger ana
mawasiliano na Sayid na akatembelewa hospitali na
Habiba hii inatuhakikishia
kwamba huyo mbunge ana
mahusiano ya karibu sana na
watu hao.Inashangaza sana kwa
mbunge huyo kuwa na
mahusiano na watu hawa
hatari.Serikali ya Tanzania
wanafahamau chochote
kuhusiana na suala hili? Idara
ya ujasusi Tanzania
wanafahamu kama mmoja wa
wabunge wa nchi yao ana
mahusiano na watu
wanaofadhili mtandao wa
IS?akauliza Yitzhak “Hapo ndipo penye tatizo
mkurugenzi.Dick alitumwa na
waziri mkuu wa Tanzania kuja
kumlinda Edger kwa siri na
suala hili limejitokeza wakati
akiendelea kutimiza jukumu
lake la kumlinda Edger na
hajamueleza mtu yeyote nchini
Tanzania.Nilimshauri
asimjulishe mtu yeyote bali
tuendelee kufanya uchunguzi
na kufahamu kinachoendelea
kati ya Edger na hawa watu wa
IS.Kwa bahati mbaya sana kabla
hatujafika mbali na uchunguzi
wetu Edger amefariki dunia” “Amefariki? Yitzhak
akashangaa
“Ndiyo amefariki dunia jana
usiku na inadaiwa kwamba
chanzo cha kifo chake ni
kupanda ghafla kwa shinikizo la
damu lakini hizo ni sababu tu
naamini kabisa Dick ameuawa
na IS.Nina uhakika waligundua
kwamba alikuwa anamfuatilia
Edger na
wakamuua.Kulithibitisha hilo
waziri mkuu wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania ambaye
ndiye aliyemtuma Dick kuja
hapa Israel kumlinda Edger naye pia ameuawa asubuhi ya
leo katika mlipuko wa bomu
lililotegwa nje ya ofisi
yake.Naamini kabisa kwamba IS
ndio waliofanya shambulio hilo
kwa ajili ya kuficha siri ya Edger
isigundulike.Waligundua
kwamba Edger amekuwa na
mawasiliano na waziri mkuu
hivyo wakaamini kwamba
lazima atakuwa amemueleza
kuhusiana na Edger kukutana
na Habiba hivyo wakalazimika
kuwaua wote” akasema Yair
“Habiba Jawad amekuwa
akimtumia Sayid Omar kufadhili kikundi cha IS
ambacho kimekuwa
kinaendesha mauaji ya watu
ndani ya ardhi ya
Israel.Nimeshangazwa na
kitendo cha watu hawa wawili
kuingia nchini mwetu bila ya
mamlaka kufahamu na kuwatia
nguvuni.Nalazimika kuamini
kwamba kuna watu ndani ya
serikali ambao wamewasaidia
watu hawa kuingia humu nchini
na hadi kufika hospitali
kuonana na Edger.Uchunguzi
mkali sana unatakiwa kufanywa
katika hili na kuwabaini hawa watu wanaoshirikiana na IS”
akasema Yitzhak kwa ukali
“Kitendo cha huyu mbunge
kukutana na watu hawa wawili
kinadhihirisha wazi kwamba
wana mahusiano ya karibu na
ninahisi kwamba yawezekana
naye akawa ni mwanachama wa
kikundi cha IS kwani kikundi
hiki kina wanachama wengi na
wamekuwa na wakipandikiza
watu wao ndani ya serikali
mbali mbali na ninaamini hata
ndani ya serikali yetu wana
watu wao ndiyo maana watu
hawa wawili Habiba na Sayid wameweza kuingia nchini Israel
bila mamlaka kuwa na
taarifa.Ninashawishika kuamini
kwamba huyo mbunge naye ni
mmoja wa watu
walipandikizwa na IS ndani ya
serikali ya Tanzania.Nini
mnafikiria kukifanya?akauliza
Yitzhak
“Tumelifikisha kwako suala
hili tunasubiri maelekezo yako
mkurugeni” akasema
David.Yitzhak akatoa sigara
akawasha na kuvuta mikupuo
kadhaa halafu akasema “Tunamuhitaji sana
Edger.Tumekuwa tunawatafuta
Sayid na Habiba kwa muda
mrefu na huyu anaonekana ni
mtu wao wa karibu sana hadi
wamehatarisha usalama wao
kwa kuingia hapa Israel kuja
kumtembelea hospitali.Hiki
walichokifanya
kinatuhakikishia kwamba huyu
ni mtu wao wa muhimu sana
hivyo basi tukimpata
atatusaidia kwanza kufahamu
walipo Habiba na sayid na pili
kufahamu mambo mengi ya IS
pamoja na mipango yao mbali mbali.Tuanze mikakati ya
kuhakikisha kwamba
tunampata huyu kijana.Yair
utasimamia hili zoezi.Weka
watu pale hospitali ambao
watafuatilia kwa karibu kila
kinachoendelea kwa huyu
jamaa.Chunguzeni watu
anaokutana nao na kama
akionekana Habiba au mtu
mwingine yeyote
watakayemtilia shaka basi
wakujulishe haraka sana”
akasema Yitzhak na kumgeukia
David “David nataka iandaliwe
operesheni maalum ya kumpata
Edger.Nataka ufanyike
uchunguzi kujua lini Edger
atarejea nyumbani
Tanzania.Operesheni kubwa
iandaliwe ya kwenda
kumchukua Edger nchini
Tanzania muda mfupi
atakapowasili akitokea huku
Israel.Nasema ni operesheni
nzito kwa sababu nataka
Tanzania na dunia nzima wajue
kwamba Edger amefariki
dunia.Huyu ni mtu muhimu
sana kwetu na serikali ya
Tanzania haipaswi kufahamu
chochote kuhusu operesheni hii
kubwa tunayokwenda
kuifanya.Uwezo wa kufanya
operesheni kubwa kama hiyo
tunao kwani shirika letu la
ujasusi ni shirika kubwa na
lenye uwezo mkubwa kabisa wa
kufanya chochote katika nchi
yoyote duniani. Tumekwisha
fanya operesheni kubwa katika
nchi mbali mbali duniani na
hatujawahi kushindwa hivyo
basi hatuwezi kushindwa pia
katika operesheni hii.Hii ni
operesheni muhimu sana na ipewe uzito
mkubwa.Ninakwenda kuonana
na waziri mkuu nitazungumza
naye kuhusu suala hili ili atupe
kibali chake na nitakaporejea
nataka nikute mpango maalum
umekwisha andaliwa namna
operesheni hii
itakavyoendeshwa” akasema
Yitzhak na kuwaachia jukumu
lile David na Yair kuandaa
operesheni ile ya kumpata
Edger
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom