Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 032

Kisu kilizamishwa katikati ya tumbo la mwanadada yule. Wana usalama wakatizamana na kutizamana. Mtu wa tatu mwenyekufahamu juu ya kilichotokea alikuwa ameuawa kinyama. Nani amelifanya na hili? Nani amemjua huyu mwanamke? Walikuwa kwenye bumbuwazi la takribani sekunde kumi. Kila mmoja alikuwa amesafiri kimawazo, kila mmoja alikuwa akiwaza kile walich0kutana nach0. Maiti ya msichana huyu ilikuwa imetulia kitandani. Binti aliyewasindikiza hapo naye alikuwa katika fadhaha. Hakuwa akiamini kile alichokuwa akikitizama mbele ya macho yake. Ni dakika tano zimepita tokea alipokuja yule mwanamke, mwanamke mwenye shangwe na bashasha, mwanamke aliyemchangamkia kana kwamba wanafahamiana. Ni mwanamke huyu aliyemuulizia marehemu, ni mwanamke huyu aliyeingia chunbani kwa marehemu na kutoka. Kutoka katika muda ule ule, hakukawia tokea kuingia na hata kutoka. "Ni yeye, ni yeye aliyemuua!! Hii ilikuwa sauti iliyotamkwa na kupenya katika ngoma za masikio ya makachero waliokuwa wamepigwa butwaa. Macho yakamuangalia dada huyu kisha swali likafuatia. Swali ambalo liliulizwa na makachero wote. "Nani?...
"Mwanamke!!. Akajibu huku akiendelea kufuta machozi. "Mwanamke gani? Wakauliza tena wanausalama. "Mliyenikuta naye hapo nje. Ni yeye aliyemuulizia marehemu na ni yeye aliyetoka humu chumbani. Harafu pia hata marehemu aliyoonyesha kutokumfahamu huyu mwanamke." Alijibu mwanamke yule.

Wanausalama wakamuangalia wakimkazia macho. Bado walikuwa katika kiza kizito. Sekunde mbili baadae simu zikasambaa kila kona. Mwanamke mwembamba mrefu afuatiliwe na kukamatwa. Kwa kuwa nyumba ile ilikuwa imezungukwa na wana usalama, haikuwa vigumu kumkunbuka mwanamama huyu. Kwani wakati akitoka kwenye ile nyumba walimuona. Licha ya kumuona lakini walikuwa wameshachelewa, kwani wakati taarifa inakuja tayari mwanamke yule alikuwa amekwisha tokomea. Licha ya wana usalama kuhangaika na kuwasiliana kwa muda ule, hapakupatikana taarifa yoyote ya kuwasaidia. Wote wakarudisha macho yao tena kwa binti yule. Walihitaji kupata mawili matatu kutoka kwa mwanadada yule juu ya mwanamke aliyemhisi kufanya mauaji hayo.

"Sisi ni maafisa wa polisi, tuko hapa kumfuatilia marehemu baada ya kuambiwa ana habari fulani." Vitambulisho vyao vilikuwa mbele kumuaminisha mwanamke yule. Baada ya kuviangalia kwa muda, mwanamke yule akawarudishia huku akionekana akitetemeka kwa mbali. "Tunahitaji kujua kuhusu marehemu. Alikuwa nani? Alifanya kazi wapi? Na kipi kingine unafahamu ambacho kinaweza kuwa ndio chanzo cha kifo chake. Yalikuwa maswali ambayo yalimfanya mwanadada yule kuangalia juu kama ni mwenye kufikiria kitu, kisha kwa sauti ya kukata tamaa akanena.

"Binti alikuwa ni changudoa, hiyo ndio kazi ambayo ilimuweka hapa mjini. Akajibu binti huku macho yake yakiusgangaa mshangao kutoka kwenye sura za makachero hawa.

"Enhe ukiacha uchangudoa kipi kingine ambacho alikifanya? Lilikuwa swali la pili.

"Hakuwa na kazi nyingine zaidi ya hiyo." Akajibu.

"Biashara hiyo alikuwa akiifanyia wapi?

"Travertine hapo usalama." Akajibu. Kwa mara nyingine wana usalama wakatizamana. Wakaki wakitizamana makachero wale, yule mwanamke akaongeza. "Kingine ambacho nahisi kimesababisha huyu binti kuuawa ni kushuhudia watu wa mwisho kuingia na waziri pale hotelini sambamba na rafiki yake kushudia mauaji ya Waziri mkuu. Wote walikubaliana leo hii wakaongee na vyombo vya usalama. "Wana usalama wakaangaliana tena. Watu wawili waliomuhimu na msaada mkubwa walikuwa wamesafirishwa kuzimu. Wamesafirishwa ili kuzibwa midomo. Hawakutakiwa kufumbua mdomo kuliongea hili popote na hilo lilikuwa limefanikiwa.

******

Alihitaji kujiondoa katika hili ambalo limetokea. Kucharuka kwa wana usalama kulizua hofu na mashaka miongoni mwao. Waliiona njia ya kujitoa katika hili ni kumchoma masimba kwenye vyombo vya usalama. Walitaka kushindilia msumari wakiamini Masimba bado alikuwa akitafutwa na vyombo vya usalama. Walilijua hilo kwa kuwa hata wao walikuwa washirika wa waziri mkuu. Hata wao walikuwa wakilijua shinikizo ambalo alikuwa akipewa mkurugenzi wa Idara ya ujasusi kuhusu kutafutwa kwa masimba. Wakata kulitumia hilo kump0teza masimba. Hawakujali kuwa wao ndi0 walikuwa chanzo, chanzo cha kile kinachoendelea. Leo hii walikuwa wamepanga kwenda kuonana na mkurugenzi wa idara ya ujasusi nyumbani kwake. Wali0na hii ni kama njia bora na sahihi kwao katika kujisafisha na hilo. Muda wao wa kukutana ilipangwa kufanyika usiku wa siku hiyo, ilikuwa ni lazima wamuone kwa njia yoyote.

Ilikuwa usiku wa saa tano, ukimya ulikuwa umetawala katika viunga vy0te vya oysterbey. Hapaku0nekana mtu y0y0te zaidi ya gari moja moja ambazo zilikuwa zikipita kuelekea sehemu mbalimbali huku nyingi zikiwa ni za wakazi wa eneo hilo. Pembeni kidogo mwa barabara ile alisimama mtu mmoja macho yake yakitizama nyumba fulani ambayo ilikuwa mbele yake. Mtu huyu alikuwa hapo baada ya kupenyezewa taarifa kuwa wapo watu ambao walipanga kwenda kulitangazia taifa kwamba yeye alikuwa ndiye muuaji aliyeitoa Roho ya waziri. Ilikuwa taarifa alioipuuza baada ya kuipata, lakini baada ya kuchunguza kwa makini majibu alioyapata yalikuwa ni yale yale. "Unataka upewe hii kesi. Unachotakiwa ni kuwawahi watu hao" ulisomeka ujumbe ambao alitumiwa na wake usiku wa siku ile. Hapo ndipo alipoamua kutos tiketi kwa watu hawa, watu ambao wao ndi0 chanzo cha haya yanayoendelea kufanyika.

Macho yake bad0 yalitizama nyumbani pale, hapakuonekana uwepo wa watu, hapaku0nyesha kama kuna mtu ndani yake. Wakati akiliwaza hilo akaziona taa za magari zikimulika mbele ya nyumba ile. Punde akaisikia honi ya gari. Moyoni akafurahi kwa kuamini mwenyeji wake alikuwa amerejea na ulikuwa muda wa kuipeleka tiketi yake. Akauvuta muda akisubiri geti lifunguliwe mtu wake aingie ndani. Muda wote mkono wake ulikuwa juu ya bast0la yake. Hazikupita dakika mbili gari ilikuwa imeshaegeshwa ndani. Mwanaume akaondoka pale pembezoni mwa barabara na kuanza kusogea taratibu kuelekea ndani ya nyumba ile. Giza la usiku lilimfanya ahisi ni mwanga katika macho yake. Alilipenda giza kama alivyokuwa akiipenda bastola yake, haikuwa bastola tu bali hata mwandani wake. Mwandani ambaye alimfanya ajihisi yu peponi kamasio paradise. Akaifikia nyumba ile kwa karibu san. Ilikuwa nyumba iliyozungushiwa ukuta mrefu sana mithili ya jumba la ikulu. Juu ya ukuta ule kulipitishwa nysta za umeme na kuufanya uzio ku0nekana ni hatari. Akaangalia kwa dakika kama mbili, baada ya hapo akaamua kuingilia kwenye lango la mbele kule ambapo alikuwepo mlinzi. Akatembea kama mpita njia mpaka alipotokea lango la mbele. Macho yake yapaka yalikuwa yakiangalia huku na huko.. muda kidogo akamuona mlinzi akizunguka zunguka.. Hapo akaamua naye kujitokeza na kuanza kutembea akielekea pale.
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 033

Muda mfupi baadae alikuwa akitizamana na mlinzi wa jumba lile. Masimba akas0gea kama mpita njia mwenye kutaka kuuliza kitu. Mlinzi naye hakushtuka katika hilo, akasogea kumsikiliza zaidi mtu huyu ambaye alimjia kama mhitaji. Hatua ya kwanza na yapili zilikwenda bila kutokea chochote, hatua mbili kabla hajamfikia mtu yule kikatokea kitu cha kustaajabisha kwake na hata kwa masimba, taa zote za jumba lile zilikuwa zimezimwa katika namna ya kushangaza. Hilo likamvuta masimba, likamvuta likimtoa pale alipokuwa na kumsogeza upande tofauti. Ni muda huo huo alipoisikia sauti ya mlinzi yule ikilalama katika aina ya maumivu. Lilikuwa lalamiko ambalo halikudumu hata kwa theruthi ya sekunde. Ukimya ukarudi tena katika utawala wake. Ukimya wa kutisha na kuogopesha. Masimba bado akaivuta dakika nyingine ya pili ili kuangalia kile kinachotokea. Kelele ya mlinzi ilimaanisha kuwa alipigwa shaba. Hilo halikubishwa katika kichwa na akili ya masimba. Hakujua huyu alikuwa nani katika wakati huu, wakati ambao alijipanga mwenyewe na hakuwa amemwambia mtu yoyote kuja kwake hapa. Haukuwa muda sahihi wa kujiuliza maswali, ulikuwa muda wa kukijua kile kilichotokea. Hilo likamfanya masimba airuhusu miguu yake kutembea, mkononi aliikamatia bastola yake, sasa akaamua kwenda ueleke0 tofauti, aliamua kurudi kule alipotoka. Akaufikia ukuta wa jumba lile, akautizama kwa makini safari hii akitaka kufanya kitu. Hakujua kile kilichotokea ndani na hata kile kilichompata mlinzi. Muda huu alikuwa juu ya mti mmoja kati ya mingi iliozungushiwa kwenye jumba lile. Aliupanda na alipofika usawa wa uzio ule akajitoa pale juu ya mti na kutua chini bila kutoa kishindo. Baada ya kutua, akachepuka na kubana pembeni. Bado ukimya wa kuogofya ulichukua sehemu kubwa. Akajitoa pale alipokuwa amebana na kusogea kuelekea mlango wa nyuma. Kila hatua yake moja ilikuwa ikienda sambamba na macho yake. Akaufikia mlango na kutulia hapo. Bado hakusikia chochote kutoka ndani. Hamu ya kujua kilichotokea ikaongezeka, hamu haikumithilika. Hilo likamfanya akinyonge kitasa ku0na kama mlango ungefunguka. Ni kweli mlango ulikuwa wazi, ni kweli mlango haukuleta kizuizi "ameingilia hapa" lilikuwa neno lililogonga kichwani kwake. Akausukuma mlango taratibu na kuruhusu macho yake kutangulia kutizama ndani. Lakini hakufanikiwa kukiona kitu kutokana na giza. Akaufungua zaidi kisha kuingia kabisa. Hatua tatu mbele alihisi kukanyaga kitu mfano wa maji. Hilo likamfanya kutaka kuinama kuangalia. Pua zake zikainasa harufu ya damu. Damu mbichi iliokuwa ikichuruzika kutoka mahala fulani katika mwili wa binadamu. Damu ikamsisimka. Akahisi kuwahiwa na mtu katika hili. Lakini alikuwa nani? Lilikuwa swali ambalo halikupata majibu. Na hakutaka kupata jibu kwa wakati ule. Akahama pale na kuendelea kusogea mbele, hakupiga hata hatua tatu akajikuta akijikwaa kwenye kitu mfano wa mwili wa binadamu. Akaongeza umakini na kuugusa mwili ule. Akajikuta akionyesha mshangao baada ya kugundua mwili uliolala chini ulikuwa mwili wa mtoto mdogo ukiwa hauna uhai. Alitegemea kuona mengi lakini hilo hakulitegemea. Mtoto kuuawa kwa risasi!!!ni nani huyu? Lilikuwa swali lisilo na majibu. Ina maana mzigo uliyopotea ndio chanzo cha hays yansyotokea? Bado alikuumiza kichwa chake kwa maswali.

Wakati anapewa kazi ya kufuatilia mzigo uliopotea hakujua kama kazi ingemfikisha huku. Hakujua kama yangetokea haya. Hamu yake ya kuwajua wauaji wa Asteria ndiyo sababu ya leo hii Masimba kutafutwa. Akaucha pale chini mwili wa yule mtoto asie na hatia. Akasogea zaidi na zaidi, kutokea tu sebuleni akashtuka baada ya taa zote kuwashwa. Hazikuwashwa patupu bali zikafuatiwa na mngurumo wa gari kutoka nje. "Wamekimbia" alinong'ona masimba huku sasa akishuhudia kile kilichotendeka. Watu watano walikuwa chini wamelaliana juu ya dimbwi la damu huku risasi zikionekana kuiharibu miili yao. Hilo likamshangaza Masimba, sio kushangazwa na nauaji yale bali watu waliouawa. Kwa mara ya kwanza akauhusudu uwezo wa mtu huyu, uwezo wa muuaji huyu. Watatu kati ya watu watano waliouwa pale walikuwa ni watu wake, watu ambao alitaka kuwapa tiketi zao. Lakini alishangaa kuwakuta wote wakiwa wamesafirishwa tayari tena na mtu ambaye hakuwa akimjua. Hili likampa shaka na hata wasiwasi kwamba inawezekana kuna watu au mtu anatembea naye katika hili.

********

Vifo vya wasichana watatu ambao ndio pekee waliokuwa wakiwajua wauaji kiliitikisa sana idara ya ujasusi. Sasa wapelelezi walikuwa wakikesha katika vyumba vya watu hudika wakizani kwamba wanaweza kupata chochote cha kuwasaidia. Licha ya kujaribu kupekuwa katika makazi yote ya marehemu hawakufanikiwa kupata chochote cha kuwasaidia. Mtu pekee aliyekuwa amebaki katika hilo alikuwa ni yule dereva tax. Huyu alikuwa amefichwa katika jengo moja linalomilikiwa na wana usalama. Leo waliamua kurudi tena baada ya mambo kuendelea kuwa magumu. Licha ya kuhojiana naye sana lakini waliamini kwamba wanaweza kupata chochote kwa mara nyingine. Hawakutaka kupuuza hilo. Muda mfupi baadae walikuwa ndani ya chumba wakihojiana na mtu huyu. Wana usalama wakaendelea hili na lile. Wakimtaka akumbuke zaidi kile ambacho alikiona kabla ya kukodiwa na watu hao ambao bado walikuwa wakisakwa na wana usalama mpaka muda ule
. Dereva wa tax akakaa kimya kwa muda akiwaza hili na kuwazua. Kwa mara ya kwanza alianza kukijutia kitendo cha kutoa siri ambayo akuwa nayo. Usumbufu wa maswali na hata vitisho ilikuwa kawaida kwa wanausalama wengi duniani hasa pale wanapohitaji kitu. Vitisho ilikuwa sehemu moja na mbinu ya mwisho kuitumia pale wanapokutana na ugumu katika mbinu zao nyingine. Dereva bado alikuwa kimya akijaribu kukumbuka kilichotokea kabla ya kuwapata watu wale watatu usiku ule. Haikupita dakika hata tatu tayari alikuwa ameshakumbuka kitu. Gari ya kifahari ikiingia, kisha walinzi watano wakashuka kabla ya mtu fulani kushuka. Mtu yule hakuwa ameshuka peke yake bali alikuwa sambamba na watu wengine watatu. Wawili walikuwa watu weusi na mmoja alikuwa raia mwenye asili ya Asia. Yeah walikuwa watu hao. Baada ya kukumbuka hilo akainua macho na kuwatizama tena wana usalama, kisha kwa sauti ya chini akasema. "Yeah nimekumbuka. Wakati mheshimiwa akishuka, alishuka sambsmba na watu wengine watatu. Wawili walikuwa weusi na mmoja alikuwa na Asili ya Kiasia. Hao walikuwa tofauti na walinzi ambao walishuka kabla." Wana usalama wakaangaliana kisha mmoja akanena..

"SURESH SIGH na JIMMY LAMBERT LAZIMA WATAFUTWE KUANZIA SASA. HAWA NI WATU AMBAO WATA...... kabla hajamaliza kauli yake, simu yake ya mkononi ikaiiita.. Kutupa macho juu ya kioo cha simu akakutana na Jina Chief. Hakupokea kwa muda ule.
 
Naomba niwakumbushe kuhusu kile nilichokiomba. Mpaka sasa nimepokea michango kutoka kwa watu wawili. Ndugu zangu hii kazi ni ngumu.. ni kazi ngumu kweli kweli ambayo hujuchukua muda sana. Tujitolee kwangu ili hata kesho nikiwa mtu fulani hata wewe utajivunia kwa mchango ulionipa. Tusiishie kusifia tu nguvu na sapoti yenu ni Muhimu kwangu.

Ukitaka kuchangia Ni cheki hapa

0675191162 Tigo Pesa

0745373585 m pesa

0628969272 halo pesa
 
Mkuu tunashukuru kwa muenɗelezo huu , kuhusu omɓi lako upanɗe wangu cjasahau mamɓo haijatulia tu kiuchumi ila nia ipo mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom