NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 032
Kisu kilizamishwa katikati ya tumbo la mwanadada yule. Wana usalama wakatizamana na kutizamana. Mtu wa tatu mwenyekufahamu juu ya kilichotokea alikuwa ameuawa kinyama. Nani amelifanya na hili? Nani amemjua huyu mwanamke? Walikuwa kwenye bumbuwazi la takribani sekunde kumi. Kila mmoja alikuwa amesafiri kimawazo, kila mmoja alikuwa akiwaza kile walich0kutana nach0. Maiti ya msichana huyu ilikuwa imetulia kitandani. Binti aliyewasindikiza hapo naye alikuwa katika fadhaha. Hakuwa akiamini kile alichokuwa akikitizama mbele ya macho yake. Ni dakika tano zimepita tokea alipokuja yule mwanamke, mwanamke mwenye shangwe na bashasha, mwanamke aliyemchangamkia kana kwamba wanafahamiana. Ni mwanamke huyu aliyemuulizia marehemu, ni mwanamke huyu aliyeingia chunbani kwa marehemu na kutoka. Kutoka katika muda ule ule, hakukawia tokea kuingia na hata kutoka. "Ni yeye, ni yeye aliyemuua!! Hii ilikuwa sauti iliyotamkwa na kupenya katika ngoma za masikio ya makachero waliokuwa wamepigwa butwaa. Macho yakamuangalia dada huyu kisha swali likafuatia. Swali ambalo liliulizwa na makachero wote. "Nani?...
"Mwanamke!!. Akajibu huku akiendelea kufuta machozi. "Mwanamke gani? Wakauliza tena wanausalama. "Mliyenikuta naye hapo nje. Ni yeye aliyemuulizia marehemu na ni yeye aliyetoka humu chumbani. Harafu pia hata marehemu aliyoonyesha kutokumfahamu huyu mwanamke." Alijibu mwanamke yule.
Wanausalama wakamuangalia wakimkazia macho. Bado walikuwa katika kiza kizito. Sekunde mbili baadae simu zikasambaa kila kona. Mwanamke mwembamba mrefu afuatiliwe na kukamatwa. Kwa kuwa nyumba ile ilikuwa imezungukwa na wana usalama, haikuwa vigumu kumkunbuka mwanamama huyu. Kwani wakati akitoka kwenye ile nyumba walimuona. Licha ya kumuona lakini walikuwa wameshachelewa, kwani wakati taarifa inakuja tayari mwanamke yule alikuwa amekwisha tokomea. Licha ya wana usalama kuhangaika na kuwasiliana kwa muda ule, hapakupatikana taarifa yoyote ya kuwasaidia. Wote wakarudisha macho yao tena kwa binti yule. Walihitaji kupata mawili matatu kutoka kwa mwanadada yule juu ya mwanamke aliyemhisi kufanya mauaji hayo.
"Sisi ni maafisa wa polisi, tuko hapa kumfuatilia marehemu baada ya kuambiwa ana habari fulani." Vitambulisho vyao vilikuwa mbele kumuaminisha mwanamke yule. Baada ya kuviangalia kwa muda, mwanamke yule akawarudishia huku akionekana akitetemeka kwa mbali. "Tunahitaji kujua kuhusu marehemu. Alikuwa nani? Alifanya kazi wapi? Na kipi kingine unafahamu ambacho kinaweza kuwa ndio chanzo cha kifo chake. Yalikuwa maswali ambayo yalimfanya mwanadada yule kuangalia juu kama ni mwenye kufikiria kitu, kisha kwa sauti ya kukata tamaa akanena.
"Binti alikuwa ni changudoa, hiyo ndio kazi ambayo ilimuweka hapa mjini. Akajibu binti huku macho yake yakiusgangaa mshangao kutoka kwenye sura za makachero hawa.
"Enhe ukiacha uchangudoa kipi kingine ambacho alikifanya? Lilikuwa swali la pili.
"Hakuwa na kazi nyingine zaidi ya hiyo." Akajibu.
"Biashara hiyo alikuwa akiifanyia wapi?
"Travertine hapo usalama." Akajibu. Kwa mara nyingine wana usalama wakatizamana. Wakaki wakitizamana makachero wale, yule mwanamke akaongeza. "Kingine ambacho nahisi kimesababisha huyu binti kuuawa ni kushuhudia watu wa mwisho kuingia na waziri pale hotelini sambamba na rafiki yake kushudia mauaji ya Waziri mkuu. Wote walikubaliana leo hii wakaongee na vyombo vya usalama. "Wana usalama wakaangaliana tena. Watu wawili waliomuhimu na msaada mkubwa walikuwa wamesafirishwa kuzimu. Wamesafirishwa ili kuzibwa midomo. Hawakutakiwa kufumbua mdomo kuliongea hili popote na hilo lilikuwa limefanikiwa.
******
Alihitaji kujiondoa katika hili ambalo limetokea. Kucharuka kwa wana usalama kulizua hofu na mashaka miongoni mwao. Waliiona njia ya kujitoa katika hili ni kumchoma masimba kwenye vyombo vya usalama. Walitaka kushindilia msumari wakiamini Masimba bado alikuwa akitafutwa na vyombo vya usalama. Walilijua hilo kwa kuwa hata wao walikuwa washirika wa waziri mkuu. Hata wao walikuwa wakilijua shinikizo ambalo alikuwa akipewa mkurugenzi wa Idara ya ujasusi kuhusu kutafutwa kwa masimba. Wakata kulitumia hilo kump0teza masimba. Hawakujali kuwa wao ndi0 walikuwa chanzo, chanzo cha kile kinachoendelea. Leo hii walikuwa wamepanga kwenda kuonana na mkurugenzi wa idara ya ujasusi nyumbani kwake. Wali0na hii ni kama njia bora na sahihi kwao katika kujisafisha na hilo. Muda wao wa kukutana ilipangwa kufanyika usiku wa siku hiyo, ilikuwa ni lazima wamuone kwa njia yoyote.
Ilikuwa usiku wa saa tano, ukimya ulikuwa umetawala katika viunga vy0te vya oysterbey. Hapaku0nekana mtu y0y0te zaidi ya gari moja moja ambazo zilikuwa zikipita kuelekea sehemu mbalimbali huku nyingi zikiwa ni za wakazi wa eneo hilo. Pembeni kidogo mwa barabara ile alisimama mtu mmoja macho yake yakitizama nyumba fulani ambayo ilikuwa mbele yake. Mtu huyu alikuwa hapo baada ya kupenyezewa taarifa kuwa wapo watu ambao walipanga kwenda kulitangazia taifa kwamba yeye alikuwa ndiye muuaji aliyeitoa Roho ya waziri. Ilikuwa taarifa alioipuuza baada ya kuipata, lakini baada ya kuchunguza kwa makini majibu alioyapata yalikuwa ni yale yale. "Unataka upewe hii kesi. Unachotakiwa ni kuwawahi watu hao" ulisomeka ujumbe ambao alitumiwa na wake usiku wa siku ile. Hapo ndipo alipoamua kutos tiketi kwa watu hawa, watu ambao wao ndi0 chanzo cha haya yanayoendelea kufanyika.
Macho yake bad0 yalitizama nyumbani pale, hapakuonekana uwepo wa watu, hapaku0nyesha kama kuna mtu ndani yake. Wakati akiliwaza hilo akaziona taa za magari zikimulika mbele ya nyumba ile. Punde akaisikia honi ya gari. Moyoni akafurahi kwa kuamini mwenyeji wake alikuwa amerejea na ulikuwa muda wa kuipeleka tiketi yake. Akauvuta muda akisubiri geti lifunguliwe mtu wake aingie ndani. Muda wote mkono wake ulikuwa juu ya bast0la yake. Hazikupita dakika mbili gari ilikuwa imeshaegeshwa ndani. Mwanaume akaondoka pale pembezoni mwa barabara na kuanza kusogea taratibu kuelekea ndani ya nyumba ile. Giza la usiku lilimfanya ahisi ni mwanga katika macho yake. Alilipenda giza kama alivyokuwa akiipenda bastola yake, haikuwa bastola tu bali hata mwandani wake. Mwandani ambaye alimfanya ajihisi yu peponi kamasio paradise. Akaifikia nyumba ile kwa karibu san. Ilikuwa nyumba iliyozungushiwa ukuta mrefu sana mithili ya jumba la ikulu. Juu ya ukuta ule kulipitishwa nysta za umeme na kuufanya uzio ku0nekana ni hatari. Akaangalia kwa dakika kama mbili, baada ya hapo akaamua kuingilia kwenye lango la mbele kule ambapo alikuwepo mlinzi. Akatembea kama mpita njia mpaka alipotokea lango la mbele. Macho yake yapaka yalikuwa yakiangalia huku na huko.. muda kidogo akamuona mlinzi akizunguka zunguka.. Hapo akaamua naye kujitokeza na kuanza kutembea akielekea pale.