Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 028

******
Kunachangudoa mmoja ambaye inasemekana alionekana akiwa na mwanaume ambaye begani alimbeba mtu, walichukua tax lakini walipofika magomeni mwembechai mwanamke yule alishuka na haukupita muda na huyo mwanaume naye akatelemka akimuaga mtoa taarifa kuwa kuna maagizo amesahau kumpa yule mwanamke. Alikwenda huko kwa muda wa dakika tano, kisha kurejea na kuomba apelekwe kimara. Yalikuwa maelezo kutoka kwa dereva wa tax aliyekodiwa usiku wa jana hotelini pale. Kikundi cha wanausalama kikatumwa huko na kingine kimara,wengine wakabaki pale hotelini wakihangaika na camera za usalama sambamba na mhudumu ambaye alikuwa zamu siku ya mauaji. Barabara zikafungwa kwa muda huku magari yakipekuliwa na madereva kutiwa kashkash. Mhudum Hakuwepo hotelini ama hakuonekana kabisa. Wanausalama walipekua hata chini ya mazuria. Kila kitu kilikuwa kikitiliwa shaka. Wengine ambao walielekea chumba cha kuongozea camera, nao wakapigwa na butwaa. Hapakuwa na chochote katika camera zile. Hapakuonekana mtu wala kikundi cha watu. Hapakuonekana mtu wa kutilia mashaka katika hilo. Bado wataalam wakahangaika huku na huko lakini hapakuonekana chochote. Hata wakati Waziri Mkuu akiingia haikuonekana kwenye camera. Hilo likawafanya wachoke. Kitu kwamba mpango huo ulipangwa mapema kama ya ujio wa mheshimiwa waziri likatawala akilini mwa wanausalama. "Nani amelifanya hili? Nani ameingia na kutekeleza mauaji haya ya waziri mkuu? Je kuna kisasi hapa? Kipi kilimtoa waziri nyumbani kwake mpaka kuja hapa? Ni mtu gani alimbeba mtu? Na ni nani aliyebebwa? Yalikuwa maswali yaliovisumbua vichwa vya wanausalama. Maswali ambayo hayakuwa rahisi kujibiwa kwa wakati ule. Wakatamani hata kumhoji marehemu mwenyewe awaambie. Walitamani waziri ainuke na kukitegua kitendawili kile. Lakini kilikuwa kitu kigumu kama kulazimisha jua kuwaka usiku na mbalamwezi kuangaza mchana. Vichwa vyao vilichoka na kuchokeana. Wakatafakari sana huku wakitamani zingekuwa zama zile, zama za kina Joram Kiango na Willy Gamba. Wasingesubiri waambiwe katika hili bali wangeamua wenyewe. Wasingesubiri muuaji apotee bali wangemtafuta na kumrudisha ama kumsafirisha. Zilikuwa Nuru na Tunu pekee katika nchi ya Tanzania. Nuru iliyong'ara kama Madini ya TANZANITE. Lakini hapakuwepo na Willy Gamba wala Joram Kiango, alikuwepo mtu mmoja aitwaye Masimba, alikuwepo mtu huyu ambaye uwezo wake ulijulikana katika mipaka na mataifa yote. Lakini wana usalama wengine hawakujua kilichopo nyuma. Ni hapo walipokuwa wakiliwaza hilo, wakapewa taarifa kuonekana kwa matone ya damu katika chumba fulani. Wote wakaelekea huko. Hata walipofika hapo ni kweli waliyaona matone ya damu. Damu ilikuwa imeganda kuonyesha haikuwa ya muda ule. Hatua kumi mbele ndani ya pipa ndani ya chunba kile wakauona mwili wa mwanamke ukiwa hauna uhai. Kila mmoja kengele ya hatari ikagonga kichwani. Hawakuamini kama hata huyo changudoa alikuwa salama. Kwa mara ya kwanza wakakili kuwa walikutqna na mtu anayeijua kazi yake. Mtu aliyewajua na kuwatambua.

*****
Baada ya Dee plus kupokea maelezo kutoka kwa masimba, alichokifanya ni kuondoka usiku ule akiamua kuanzia pale hotelini. Alitambua kazi ya kumpata changudoa yule ilikuwa rahisi kuliko kwenda kuharibu camera za usalama. Hakutaka kuchukua gari yake kwa kuhofia kujulikana. Bali alichofanya ni kuchukua usafiri wa pikipiki ambao ulimpeleka mpaka magomeni. Akashuka kama mtu wa kawaida, kisha akaongoza mpaka hotelini. Alipanda ngazi kama mteja, lakini wakati anatokea mapokezi akapokelewa na mhudumu anayeonekana ni mwenye wasiwasi. Uso wake ulikuwa ukiongea hofu tu. Alionyesha woga wawaziwazi. Dee plus akatabasamu ili kuitoa hofu kwa mwanamke yule. Lakini hilo halikufanikiwa, mwanadada yule alikuwa na hofu. Kuna wakati alijaribu kuongea vitu lakini hayakusika masikioni kwa dee plus.

"Habari yako mrembo? Dee plus aliamua kujizungumzisha ili kujaribu kumvuta mwanamke yule. Lakini bado salamu haikujibiwa.

"Kaka naomba nikwambie kitu lakini sio hapa." Akaropoka mwanamke yule akionyesha kupagawa. Dee plus akatingisha kichwa, kwa mara ya kwanza alikubaliana na masimba suala la kutaka kuwasafirisha watu hawa. Kwa muonekano wa huyu mhudumu asingeweza kuufumba mdomo wake kama angekutana na wanausalama. Hakuchelewa kumvuta mpaka sehemu aliyotakiwa. Binti naye bila kujua ameletewa tiketi ya kifo, akaufumbua mdomo na kutaka kuongea... hakupewa hiyo nafasi, tayari basi lilimfika tayari kwa kumchukua. Risasi mbili kutoka kwenye bastola yenye kuzuia mlio zilipenya upande wa kushoto wa kifua chake. Hakuweza kupiga ukelele wowote. Alitupwa umbali wa hatua tatu akaanguka chini. Alikuwa maiti tayari. Baada ya kuhakikisha mwanamke yule hatafumbua mdomo tena, akamuinua na kumtupia ndani ya pipa. Sasa alikuwa akihamia kwenye chumba cha camera za usalama katika hoteli ile. Aliwapita wana usalama akiwa amevaa kitamburisho kama mfanyakazi wa hoteli ile. Akaingia pasipokuonyesha wasiwasi. Muda wa dakika kumi akatoka ndani akiwa ameshaimaliza kazi na sasa ilikuwa safari ya kuelekea nyumbani kwa changudoa yule. Akawapita wanq usalama kwa mara ya pili bila kushtukiwa na yoyote yule.

*******

Ni nyumba yenye watu wengi, nyumba ambayo asubuhi hii iliwakuta watu wakiwa kwenye vikundi vidogo vidogo wakijadili na kuongea kuhusu kifo cha waziri mkuu wa nchi. Kila mmoja alikuwa akiongea kile ambacho ana uhakika nacho. Huku wengine wakiongelee kuuawa kwa waziri kunatokana na mwanamke, wengine walikuwa wakilihusisha hili suala na mtifuano wa kisiasa unaoendelea nchini. Watu kutekwa na watu wasiofahamika ni kitu ambacho kiliufanya mjadala juu ya kifo cha kiongozi mkuu wa nchi upambe moto. Wakati wakijadiliana hilo, wakashtushwa na gari jeusi likisimama mbele ya uwanja wa nyuma ile. Kabla hawajakaa vizuri, wakashtushwa na kuwaona watu wanne wakishuka. Ushukaji wa watu wale ulikuwa ukitia fora na kuogopesha miongoni mwa watu wachache waliokuwepo pale. Kila mmoja akaliacha alilokuwa anaongea, macho yao sasa yalikuwa kwa watu ambao tayari walishaufikia mlango wa nyumba ile. Hakuna aliyeinua mdomo kuongea chochote. Sura za watu hawa hazikuwa sura za kawaida. Punde mmiliki wa nyumba ile akafika naye akionekana ni mwenye wasiwasi. Macho ya watu waliokuwa wakimtizama yalimfanya atetemeke. Hakuna aliyeongea chochote zaidi kutoa kitu mfano wa picha na kumuonyesha. Mama yule akaipokea na kuitizama. Bila kuongea chochote akawaongoza watu wale kuingia ndani. Hatua mbili tatu akawaonyesha kwa kidole chumba anachoishi msichana yule. Sekunde moja wanausalama walikuwa mlangoni mwa chumba kile. Kila mmoja bastola ilikuwa ikitizama ndani. Ukagongwa kidogo, lakini cha kushangaza mlango ukafunguka kuonyesha haukuwa umefungwa.
Wanausalama wakaangaliana huku kengele za tahadhari zikigonga kichwani. Mmoja akaukamata mlango na kuufungua taratibu. Wote macho yao yakatizama ndani... wakaushuhudia mwili wa mwanamke ukiwa mtupu umelala kitandani pembeni kidogo kukiwa na dimbwi kubwa la damu. Wote wakaangaliana. Simu za upepo zikatembea kona zote za nchi. Sasa kila kitu kilikuwa kigumu. Wanausalama wakaingia na kuuanza kuuchunguza. Risasi mbili za kifua upande wa kushoto zilitosha kuuchukua uhai wa mwanamke huyu. Licha kupekuwa kila sehemu, lakini wanausalama wale hawakufanikiwa kugundua ama kupata chochote. Wakatoka nje na kumuita tena mama mwenye nyumba, safari hii wakamuomba awaitie wapangaji waliokuwepo hapo usiku uliopita.

Mama yule akawaita wote, kisha akawatambulisha kwa wana usalama. Kila mmoja akanyamaza kimyq huku wengine presha ikianza kupanda.

"Sisi ni wanausalama tumekuja hapa kufuatilia kuhusu mauaji yaliyotokea usiku wa jana." Alijitambulisha mmoja huku akionyesha kitambulisho chake. Wapangaji wote wakatizamana. Wakatizamana huku sura zao zikishindwa kuuficha mshangao. Mshangao ambao hata wana usalama wenyewe waliligundua hilo. Haiwezekani kifo cha mtu mkubwa nchini uchungizi uje ufanyike pale. Kama kawaida ya wanawake wa magomeni walivyo na midomo mirefu, hawakuchelewa kuuliza hilo.

"Sasa kipi mmetuitia hapa? Ina maana mauaji ya waziri yamefanywa na mtu wa nyumba? Alihoji mama chausiku huku akiwaangalia wana usalama kwa zamu.

Hawakumuangalia yeye bali walitoa ishara wapangaji wa sogee. Wakafanya hivyo, mmoja ya wana usalama akaufungua mlango na kuwataka wote waangalie ndani. Kila mmoja akafanya hivyo.
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 029

Wapangaji na mwenye nyumba wote wakatupa macho yao chumbani kwa msichana yule. Hakuna aliyeshindwa kunyamaza, kila mmoja akalitaja jina la mungu kwa imani yake. Wapo waliopiga mayowe na wapo walionung'unika moyoni. Mama mwenye nyumba akabaki ameduwaa kana kwamba alikuwa haamini kile alichokiona. Dimbwi la damu pembeni ya mpangaji wake lilimfanya ahisi presha kupanda. Wanausalama wakaufunga mlango na kuwageukia wapangaji tayari kwa kuwahoji.

"Nani ambaye alikuwepo jana wakati marehemu akirudi? Lilikuwa swali la kwanza kuulizwa. Wapangaji wote wakaacha kulia, wakanyamaza na kuanza kuwaangalia. Mara mmoja wa kike akajitokeza mbele.

"Wewe ndiye ulimuona akirudi? Akaulizwa tena.

"Hapana! Bali tulikuwa wote pale travertine hotel, mpaka pale alipotokea mkaka mmoja na kumchukua." Akajibu yule msichana huku akiendelea kulia. Jibu lake hilo likawafanya wapelelezi wale waangaliane.

"Yukoje huyo mtu? Na alikuja kama nani? Swali jingine akarushiwa.

"Ni kijana mmoja hivi mwenye mwili uliojengeka kimazoezi, ukimuangalia kwa woga unaweza kudhani ni mcheza sinema wa Hollywood. Na pale alikuja kama mteja na kumchukua mwenzetu." Akajibu yule dada. Jibu la kwanza likawafanya watizamane kwanza. "Ana mwili wa mazoezi, ukimtizama kwa woga unaweza kudhani ni mcheza sinema wa Hollywood. " yalikuwa maneno yaliyojirudia vichwani mwa wana usalama wale. Jina Masimba lilijengeka ndani ya akili zao.

"Baada ya hapo ikawaje baada ya kuondoka na huyo mtu? Lilikuwa swali jingine. "Baada ya hapo sikumuona tena mpaka sasa mlipokuja nyie ndio nagundua kumbe Rose ameuawa." Akajibu msichana yule na kuangua kilio. Wanausalama wakaangaliana tena. Wakiwa bado hawajaamua kuendelea na maswali, wakamuona msichana mwingine akisogea mbele na kusimama.

"Mimi nilimuona wakati anaingia, na muda mfupi baada ya kuingia alikuja mwanaume na kumuulizia. Kwa kuwa mara nyingi sana anafuatagwa sana, nikamuonyesha huyo kijana chumba chake. Baada kumuonyesha sikumuona huyo mwanaume alipotoka na muda huu ndio mmenishtua kuniambia Rose amekufa." Akaeleza mwanamke yule. "Je mtu aliyekuja mara hii anafanana na huyo aliyetajwa na mwenzako? Wakauluza wana usalama. "Hapana hawafanani kabisa, huyu hakuwa yule aliyeshuka kule hotelini. Licha ya huyu naye kuwa na mwili wa mazoezi, pia alikuwa mweupe na mwenye kovu kwenye jicho la kushoto." Akajibu mdada yule.
"Dee plus" lilikuwa jina lililopita vichwani mwao. Sasa walikuwa wamepata picha, aliyeshuka kule hotelini yalikofanyika mauaji alikuwa masimba. Aliyekuja kufanya mauaji ya changudoa aliyenunuliwa na Masimba alikuwa Dee plus. Hapa imekuaje? Kwa nini mtu aingie ndani na masimba kisha aje auawe na Dee plus? Ina maana huyu Changudoa alikuwa na Masimba wakati akitekeleza mauaji ya waziri mkuu? Kwa hiyo baada yachangudoa huyu kushuhudia kifo cha waziri mkuu kilichofanywa na Masimba, wakaona nao wampoteze ili kupoteza ushahidi? Kipi kipo nyuma ya mauaji haya? Kwa nini waziri alikuwa akimshawishi DG wa TISS wampoteze masimba? Yalikuwa maswali mazito ambayo yangepaswa kujibiwa na wahusika wenyewe. Wakati wakijiuliza hayo ikaingia simu kutoka kwa wenzao ambao walikuwa hoteli. Ni simu hiyo ambayo ilizidi kuwachanganya. Camera za usalama hazikuonyesha chochote katika hoteli hiyo. Hata waziri mkuu akiingia hazikuonyesha chochote. Kubwa zaidi ni kwamba mhudumu aliyekuwa zamu usiku hapo hotelini ameuawa kwa kupigwa Risasi mbili kifuani tena kwa staili kama aliyouawa huyu changudoa. Wakaangaliana tena na tena. Kazi ilikuwa ngumu kupindukia.

******
Kwanza alihisi kama alikuwa ndotoni akiota kitu ambacho kamwe kisingeweza kutokea. Akajaribu kujitingisha kuona kama alikuwa kweli anaota. Hapana haikuwa hivyo, haikuwa hivyo kwa kuwa bado alikuwa akikisikia kilekile alichokisikia hapo mwanzo. Ilikuwa sauti ya mtangazaji wa Televsheni akitangaza kifo cha mtu anayemfahamu kwa ukaribu zaidi. Sekunde hii alikuwa akifumbua macho yake na kushangaa akipokewa na nuru safi yenye kuangaza mfano wa Jua la asubuhi. Alikuwa hana nguo hata moja mwilini huku akiwa amefunikwa kwa shuka safi na zito. Hilo hakulitilia mashaka, bado alitaka kuliona kwa macho kile alichokuwa akikisikia. Maumivu ya kisogoni bado hakutaka kuyaulizia maswali. Alitaka kuona na kusikia, alitaka kujua kama ni kweli kile alichokisia. Kwa taratibu akageuza macho yake na kutizama kule ilipo tv. Macho yake yakapokewa na wana Usalama wakionyesja kuhaha. Polisi walikuwa wametanda kila sehemu wakipekua na kuwahoji watu wote. Maandishi yaliyopita chini ndio yaliyompa kiwewe. Ni kweli ama naota? Waziri ameuawa vipi? Ni nani amemuua huyu? Yalikuwa maswali ambayo yalimfanya akae kitako na kushika tama. Akauona muda ule ni wakujua alikuaje mpaka akafika pale. Kumbukumbu yake ikaanza kurudi taratibu, kwanza alikuwa mkuranga kummaliza mama wa asteria. Wakarudi mpaka katikati ya mji katika moja ya majengo ya siri ya usalama wa taifa. Hapo wakajaribu kumpigia masimba ili kumjua alipo kwa kutumia mitambo yao. Simu ya Masimba haikupokelewa.. lakini ndani ya nusu saa masimba akapiga tena akiwa jirani na hapo. Akakumbuka walipoondoka mpaka kinondoni akiwa sambamba na mwamvita. Punde tukio zima likajirudia. Hasa kuwekewa bunduki kisha kupigwa kwa kitako cha bastola kisogoni. Machozi taritibu ya kaanza kushuka. Alijitolea kwa kila kitu kwa sababu ya kikundi chao. Akamsaliti masimba kwa sababu yao. Alifanya kila kitu kwa sababu ya faida yao, lakini leo walikuwa wakimsaliti na kutaka kumuua. Hilo likamuuma sana. Bado macho yake hayakubanduka kwenye Tv. "Nani amemuua waziri na kuniokoa mimi? Ina maana masimba ndio amefanya hay..... Kabla hajamaliza kujiuliza maswali mlango wa chumba alichopo ukafunguliwa. Akageuka na kutizama huko. Macho yake yakakutana na macho ya masimba aliyekuwa akiingia. Teddy hakuuficha mshangao machoni mwake sambamba na hofu usoni mwake. Macho yake yakashindwa kumiangalia kwa muda mrefu. Maswali na aibu ya usaliti vikauvaa uso wake. Ni masimba huyu huyu aliyemuokoa mara ya kwanza katika mazingira ya kifo. Ni masimba huyu tena amemuokoa kwa mara ya pili tena kwa kumuua mtu ambaye yeye alimuogopa sana. Hakuwa na shaka kwamba masimba ndiye aliyemuua waziri mkuu. Lakini swali alimuuaje mtu ambaye alikuwa na VIP PROTECTION kwa kila anapotembea na kuwa mahala popote? Je baada ya kuzimia kutokana na kupigwa alipelekwa wapi? Na kwa nini walimgeuka wakati alishaamua kurudi kwao? Hapo ndipo alipoukaza uso wake na kumuangalia masimba usoni, akitegemea kukutana na mikunjo ya hasira. Haikuwa hivyo, tabasamu lilitanda usoni kwa masimba. Macho yake yalikuwa yakimuangalia Teddy katika utulivu. Teddy akashindwa kuvumilia, sekunde hii alikuwa amesimama akipiga hatua kumfuata Masimba. Alikuwa akitembea kwa kuyumba. Bado tabasamu lilitanda usoni kwa masimba. Tabasamu ambalo lilitoweka ghafla baada ya teddy kusimama mbele yake. Tukio la kulipuka nyumba ya mama wa asteria na kusababisha kifo chake na mjukuu lilijirudia. Bastola ilikuwa mkononi mdomo wake ukimtizama teddy. Hapakuwepo utani kabisa machoni kwa masimba. Teddy akashtuka kisha baridi ikauvaa mwili wake. Kidole cha masimba kikashuka mpaka kwenye trigger. Sasa alikuwa akikivuta kitufe tayari kwa kumlipua teddy. NIWAKATI HUO HUO MLIPUKO MDOGO UKASIKIKA HUMO NDANI.

ITAENDELEA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom