NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 025
Teddy pekee ndiye aliyekuwa akiifahamu safari yake. Safari ya kwenda kuongea na Mama wa Asteria. Lakini ni Teddy huyu huyu ambaye alimuona akiwa sambamba na mwamvita. Teddy ambaye alimueleza kuwa hakuwa tena kule. Teddy ambaye alimuamini na kuamini maneno yake. Lakini leo hii teddy alikuwa ameamua kuimaliza familia ya Asteria. Mama yake alikuwa akiendelea kuteketea na moto, huku mtoto mdogo wa kike akiwa amelala mbele yake akiwa hana uhai tena. Hilo likamuuma sana? Licha ya kuumia lakini hakutakiwa kuwa pale. Ulikuwa muda wa kuondoka na kupotea kabisa. Hakujali macho yaliokuwa yakimtizama, hakujali vilio na ving'ora vya polisi.. aliondoka akiwa amechanganyikiwa, aliondoka akiwa na Hasira na teddy, alitamani kupiga Risasi katika kichwa chake. Alianza na Asteria akafuatia Mwamvua, kisha dada yake na familia yake akiwemo Mumewe, Mr Godfrey Maboba. Sasa ameamua kuwamaliza wote. Kuna siri gani hapa nyuma? Ina maana ni mzigo tu wa madawa ndio sababu ya vifo vyote vile? Hapo akahisi kitu kingine, alihisu kuna kitu kingine nyuma ya mauaji haya. Alihisi hivyo na aliamini hivyo. Akaamua sasa kumfungia kazi Teddy, alitaka kwenda kumuonyesha kuwa yeye ni mtu mwingine katika medani ile. Kama mzigo wa madawa ameshauchukua kipi kinampa hofu teddy? Kwa nini aendelee kuua? Hakuweza kujibu hilo swali bali akasonya na kutukana tusi zito. Baada ya kutembea sana akajikuta akitokea sehemu yenye kituo cha daladala, bila kujali macho ya watu, akajipakia ndani ya costa moja na safari ya kurudu dar ikaanza. Muda wote wa safari alikuwa amekiinamisha kichwa chake kwenye siti akiliwaza tukio lililotokea punde. Sauti ya mama wa Asteria ilikuwa ikijirudia kila wakati. Tukio zima liliendelea kumtesa. Akatamani afike Dar akamuone Teddy. Alikuwa tayari ameapa kwenda kuitumbukiza Risasi Kichwani kwa Teddy. Ni wakati akiliwaza hilo akausikia Ujumbe ukiingia kwenye simu yake. Akataka kupuuza, alitaka kutoitazama simu, lakini akaisikia sauti ikimwambia "wewe ni mpelelezi unayetafutwa usipuuze kitu."!!! Akaitii sauti ile. Muda mfupi vidole vyake vilikuwa na kazi ya kuifungua Meseji.
"Uko salama, nasikia kuna nyumba imelipuliwa huko!!!? Ulisomeka Ujumbe ulionekana kutumwa na Teddy. Hilo pia hakuliacha lipite hivi hivi. Teddy alikuwa akimchezea akili yake, teddy alikuwa akimuona mjinga. Lakini kingine kilichomfurahisha ni kule kugundua kuwa teddy hakuwa amemuona wakati akitoka ndani. Hilo likampa uhuweni wa kumfikia pasipo rabsha yoyote. Teddy alikuwa ameingiwa na tamaa, ni yeye na mwamvita waliotoka ndani ya nyumba ya mama wa Asteria. Lakini muda huu anamtumia Ujumbe kuhusu kilichotokea, alikuwa akiipima akili ya masimba. Hakuona sababu ya kumjibu, akaitizama simu kwa muda kisha kuirudisha mfukoni. Alimchukia teddy na bado alitamani kufika Dar es salaam akutane nae.
*******
Alishuka maeneo ya mbagala saa moja na nusu usiku. Baada ya kushuka hapo akaona ilikuwa muhimu kumpigia teddy kutaka kujua wapi alipo. Akatafuta sehemu yenye utulivu akaipiga simu ya teddy, lakini cha ajabu haikuwa hewani. Akajaribu tena na Tena lakini bado hali ikawa ni hivyo. Simu ya teddy haikuwa ikipatikana. Akakiona kitu ambacho alikihisi hapo mwanzo. Teddy alikuwa amemchezea akili yake, inawezekana alimuona kule ndio maana akamtumia ule ujumbe. Sasa kutokupatikana kwa teddy kilikuwa ni kitu kingine cha kushangaza. Akaona haukuwa muda wa kuendelea kubaki mbagala. Ilikuwa ni lazima arudi kinondoni kwa usiku ule. Lakini kabla hajaamua kurudi lazima awasiliane na rafiki zake ambao wapo katika nafasi nyeti nchini. Wa kwanza kumpigia alikuwa Dee Plus, huyu alikuwa mmoja kati ya vijana wake. Aliongea naye mawili matatu. Baada ya hapo akarudi tena kituo cha daladala. Hapo akachukua usafiri wa kuelekea huko.
********
"Masimba anaelekea mkuranga kwa mama wa Asteria. Hakikisheni anazuia au mama anafutwa katika uso huu wa Dunia." Ilikuwa sauti ya teddy akiongea na mwamvita. Simu hiyo alipiga baada ya kikao kizito kati yake na washirika wenzake kufanyika na kufanikiwa kumrudisha teddy kundini. Ni simu hiyo ambayo iliwalazimu teddy na mwamvita kuelekea mkuranga. Ni simu hiyo iliyotumika kumtumia ujumbe masimba kwamba alikuwa akisakwa na wanausalama. Ujumbe ule kwenda kwa masimba ulitumwa na teddy wakati huo wakiwa mkuranga. Aliutuma mahususi ili kumfanya masimba achelewe kurudi Jijini, ili watu wao waendelee na utafutaji wa mzigo wao ambao uliibiwa. Licha ya watu waliotumwa kuipekua nyumba ya masimba nje ndani na ndani nje. Hawakuweza kupata chochote. Hawakuweza kuupata mzigo wao, mzigo ambao ndio chanzo cha mauaji na uasi uliofanywa na Teddy. Lakini kingine ambacho kiliwashangaza Jimmy na washirika wake, nikule kuambiwa hata masimba hawakumuona kule mkuranga. Ni taarifa hiyo ambayo bado ili wachanganya na kuwafanya kila mmoja awaze lake.. ndipo hapo amri ilipotoka kwamba wategeshe bomu ndani ya nyumba ya mama wa Asteria na kabla ya hapo walipewa amri ya kumsubiri masimba hapo. Muda ulivyokuwa ukisonga na kutokuonekana kwa masimba ndipo maamuzi ya kilichotokea mkuranga yakafanyika. Hawamuona masimba wakati akisogea pale, hawakumuona kwa kuwa walikuwa katika uharaka wa kuondoka. Na hicho ndicho walichokosea.
**********
Simu ya teddy bado haikupatikana licha ya kuipiga mara kwa mara. Bado hakikuwa kitu cha kawaida kwake, teddy amtumie meseji lakini ndani ya muda huu alikuwa hapatikani. Haikuwa kawaida kwake, haikuwa kawaida kwa kuwa alimfahamu teddy. Wakati akiwaza hilo akausikia mlio wa simu yake kuonyesha kwamba alikuwa akipigiwa. Ikaichomoa simu, akatupa macho Juu ya kioo, akakutana na namba mpya. Akaitizama ile simu kwa muda bila kuipokea mpaka ilipokatika. Hakuwa na utaratibu wa kupokea namba ngeni katika kazi yake hii ya hatari. Baada ya ile simu kuita na kukata bila kuipokea, akapata hisia za kuingalia namba ile vizuri, alitaka kumjua mmiliki na alitaka kujua inapigwa kutoka wapi. Muda mfupi alikuwa akiongea na simu Nyingine hewani. Baada ya kukata akatulia akisubiri kupata maelekezo kutoka kwa mtu wake. Haikupita muda muda mrefu simu yake ikaita tena. Alikuwa ni yule mtu wake. Akaipokea na kuongea kwa dakika kama moja hivi kabla ya kuikata simu. Mwili wake ulisisimkwa na kushikwa na ubaridi. Namba mpya iliompigia ilipigwa kutokea katikati ya jiji la dar es salaam maeneo ya posta. Ilikuwa taarifa aliyoitegemea kqbisa. Alijua simu hiyo ilitoka kwenye moja ya majengo yanayomilikiwa na Idara ya Usalama Wa Nchi. Hilo likamfanya aamue kuelekea huko, alitaka kwenda kumjua mwenye namba ile. Hakuwa na sababu ya kuogopa wakati alikuwa akisakwa. Baada ya daladala aliopanda kufika maeneo ya uhasibu alishuka, kisha akachukua usafiri wa pikipiki mpaka maeneo ya posta. Alishuka na kulipa ujira kisha kuongoza kuelekea pale ambapo alipakusudia. Alitembea kwa uangalifu mpaka maeneo ya bandarini nje ya kituo cha mabasi yaendayo kasi. Kulikuwa na umbali mfupi sana kutoka kwenye jengo binafsi linalotumiwa na usalama wa taifa. Jengo ambao lilikuwa likitizamana na Makao makuu ya Mamlaka ya mapato Tanzania. Vilevile ulikuwa umbali mfupi na kilipo kituo kikuu cha polisi Dar es salaam (Central police) baada ya kusimama hapo kwa muda akiangalia hili na lile, akaichomoa simu yake, kisha akaitafuta ile namba harafu akaipiga akiwa mkononi pasipo kuipeleka sikioni. Baada ya kuita tu, akaikata kisha akaondoka pale kwa haraka mpaka pale kituo cha posta ya Zamani. Akatulia pale huku macho yake yakitizama kule alipotoka. Haikupita hata sekunde thelathini, akawaona watu wanne ambao hawakuonyesha kama wako pamoja wakipishana huku na huko. Hakuwa mgeni na majasusi, aliwajua na kuwatambua hata kama wamejibadilisha kwa kiasi gani.