MNYONGA TAI—07
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
MAWASILIANO: 0673056571
Walipofanikiwa kuondoka nyumbani kwa Cheyaya, Askofu Ponera na Chiku waliongozana na wale mateka wao hadi alipokuwa anaishi Chiku. Wakawahifadhi wale askari kwenye moja ya chumba, kisha wao wakajipa utulivu. Walipumzika sebuleni.
Mazingira ya nyumba kwa ujumla hayakuwa vyema. Uchafu ulikithiri kwa kukosa matunzo, lakini hiyo haikuwa sababu ya kuwazuia wasitumie. Walipoona utulivu unaanza kuwakinai, ndipo walijiondoa hadi chumbani kwa wale askari. Waliwafunga kudu mikononi.
“Naamini mumeshatafakari vya kutosha,” Askofu Ponera alisema, akiwa anachukua pozi la uketiji kitini. Chiku alisimama mlangoni.
Wale askari hawakumjibu. Badala yake walimkodolea mboni zilizompa picha wanapitia katika hali ngumu ya ukinzani akilini kumtafakari mwanaume huyo anajivunia nini.
“Chiku.” Askofu Ponera akamgeukia. “Njoo wakague hawa.”
Chiku alitii.
“Usiache kitu chochote utakachowakutanacho,” Askofu Ponera akamsisitizia.
Zoezi hilo lilichukua dakika chache sana, Chiku akawasilisha alivyowakutanavyo kwa Askofu Ponera. Vitambulisho na pingu. Baadaye Askofu Ponera alimwita mmoja baada ya mwingine kwa kufuatisha majina yaliyopo kwenye vitambulisho. Mmoja kati yao alikuwa na cheo cha koplo. Wengine ni ma-konstebo.
“Koplo Mvuanyingi,” Askofu Ponera aliita, mboni amezitoa kumwangalia mwitwaji. “Nataka tushirikiane kubadilishana taarifa. Vipi, upo tayari?”
Koplo Mvuanyingi hakujibu. Ndiyo kwanza, alibadili uelekeo wa utazamaji. Wengine vivyo hivyo walivyoulizwa.
“Okay, sio kesi. Nawapa muda zaidi mtafakari. Nitawarudia baadaye.” Askofu Ponera akainuka, na kuondoka mle chumbani kwa mwambatano na Chiku.
“Una uhakika watasema?” Chiku alidadisi.
“Usiwe na shaka.”
“Nahofia tukikutwa na ma-askari wenzao, watatufanyia kitu mbaya hatujawahi ona. Au nawe ni askari?” Chiku akamgeukia Askofu Ponera, huku wakizidi kupiga hatua kupotelea ushorobani.
“Hapana. Mimi ni mtu wa kawaida niliye na machungu na nchi yangu. Napenda kuona haki ikitawala.”
“Huogopi polisi? Maana unajichukulia sheria mkononi.”
Askofu Ponera akasimama na kumgeukia Chiku. Alimsaili kwa muda, kabla hajatokwa na kauli, “Upo na mtu makini sana.”
Wakaendeleza mwendo.
Dakika kumi baadaye Askofu Ponera akawa anamtoa askari mmoja baada ya mwingine anahojiana naye sebuleni. Akishamaliza, humpeleka chumba kingine tofauti na cha awali. Mahojiano ya muda huu hayakuwa na wema. Alitembeza vitu fulanifulani mwilini kwa walengwa vilivyowashinikiza wafunguke baadhi ya mambo.
“Tumeahidiwa donge nono tukifanikisha kumkamata Cheyaya,” Koplo Mvuanyingi alifunguka. Ndiyo alikuwa wa mwisho kuhojiwa. Viadhabu vya kuchomwa chomwa sindano vilipeperusha msimamo wake.
“Nani mtoaji wa hiyo hela?”
“Mbunge. Mheshimiwa Mbunge ndiyo kila kitu katika hili.”
“Nanyi mnajiona mko sahihi?”
“Njaa kaka. Njaa. Kwani hata ungekuwa ewe, usingelikataa ofa yake.”
Askofu Ponera akatabasamu.
“Kwa nini huyo Mbunge anamtaka Cheyaya?”
“Aaah! Hilo nitakudanganya, sijui sababu.”
“Umesahau kazi yake hii?” Askofu Ponera akamwonyesha sindano.
Koplo Mvuanyingi akatokwa na kauli huku akitetemeka, “Kweli ndu... Ndugu sijui...te. Sijui chochote ndugu. Nisamehe bure.”
Kwa kiasi fulani Askofu Ponera aliyaamini maneno ya Koplo Mvuanyingi. Hivyo hakuona haja ya kuendelea kumsulubu. Alimwacha, kisha alitoa taarifa kwa Fadhy kwa njia ya simu.
“Nimefanikiwa kupata madini yenye manufaa kwa ustawi wa nchi yetu,” Askofu Ponera alimtaarifu.
“Yawahishe mahali salama kwa ulinzi zaidi.”
“Timamu kwa utekelezaji.”
“Hakikisha unakuwa usafirishaji salama.”
“Hamna shaka chifu.”
Simu ikakatwa.
***
Luteni Ringo aliongoza timu kama ilivyoamriwa. Mwendo ulikuwa wa mnyato, hadhari wameikumbata vya kutosha wasishtukiwe kiasi cha kuwapa taarifa walengwa wao. Kila mmoja alikuwa na bastola, kwa kujihami na shambulizi lolote lihusishalo zana.
Walivyoufikia mlango wa mbele wakajibanza ukutani kwa mgawanyiko; wawili upande huu-Luteni Ringo na Pte Pemba. Halafu mmoja upande mwingine-Pte Bayo. Mlango waliuweka kati. Baada ya mtuo wa mihemo ya utulivu Luteni Ringo akatoa ishara kwa Pte Bayo. Naye kwa utiifu, aliitekeleza kwa haraka sana. Alibisha hodi kwa kugonga mlango na viganja vya vidole.
Kama ilivyo jadi ya wema kwa watanzania wengi, mlango ulivyogongwa kwa mara ya pili mwenye nyumba akampa subira mgongaji.
“Naja,” ilisikika sauti kutoka ndani. Pasi na umuhimu wa kuhoji mgongaji ni nani.
Ilipita dakika moja toka itikio litolewe, mlango ukashughulishwa na hatimaye kufunguliwa. Yule waliyemhisi awali kuwa mhusika wa nyumba ndiyo alifungua. Akajijaza mlangoni. Mboni zote akazielekeza kwa Pte Bayo.
“Karibu.”
“Nashukuru mzee. Naitwa...” Pte Bayo akakatishwa.
“Nikusaidie ni...?” naye hakumalizia kauli yake, pigo la wastani lilitua shingoni. Alivyonuia kugeuka amwangalie afanyaye, alipigwa kabali akavutwa nje zaidi. Yote hayo yalifanywa na Luteni Ringo.
Pale alipopepesukia mwenye nyumba akafikia kudakwa na Pte Pemba. Kabla hajafungua mdomo kuzungumza jambo akazibwa kwa mkono, kiasi cha kupelekea aheme kwa tabu. Kwani viganja viliziba sehemu ya pua pia.
“Kamwihifadhi garini, wacha sisi tuingie,” Luteni Ringo alipendekeza.
Pte Pemba alifanya alivyoombwa. Luteni Ringo na Pte Bayo wakafanya kusudio lao pia. Waliingia ndani kwa hatua fupifupi, hadhari wameikumbata kidete.
Baada ya hatua kadhaa waliikaribia sebule. Wakaweka pozi kwa muda, kisha kusikilizia maongezi ya wahusika waliopo. Waliyanasa barabara viwamboni. Waliyasikilizia mazungumzo kwa takribani dakika mbili, walipoanza kuingiwa mashaka dhidi ya mwenye nyumba kutorejea wala kumsikia, ndipo Luteni Ringo na Pte Bayo walipojitokeza mbele yao.
Walijitokeza bastola wakiwa wamezielekeza usawa wa ushambuliaji.
“Mikono juu,” Luteni Ringo aliwaamuru kwa sauti kali.
Hakuna ajawaye ujasiri kwenye uvamizi.
Hivyo, Nalimuka na wenzie walipata hofu kwa muda, iliyowashurutisha wajiinue walipoketi kutafuta sehemu ya uficho-kila mmoja alipoona panamfaa. Lakini kabla hawajayafikia, Luteni Ringo aliruhusu mitupo kadhaa ya risasi ukutani. Hakukuwa na amani tena, wakabaki kugongana gongana mithili ya kuruta wapatapo ruhusa ya kupumzika wakiwa kwenye kusanyiko.
Kwa kuwa ile bastola haikufungwa kiwambo, mshindo wa sauti ukawa mkubwa. Huo ndiyo uliwatetemesha zaidi.
“Kwa amani, wote rudini hapa kabla sijawafumua bongo zenu,” Luteni Ringo aliwaamuru kwa mara nyingine. Ile bastola akimwelekezea mmoja baada ya mwingine.
Fikra ya haraka iliyotapakaa bongoni kina Nalimuka kwamba wamevamiwa na majambazi. Wafanye nini zaidi ya kukubaliana na waamriwacho? Walitii bila shuruti.
Kwa hofu, Nalimuka na u-waziri wake, jasho chapachapa limemkithiri, aliwaongoza wenzie hadi walipoamriwa wakae. Mkao wa pigo la goti.
“Hivi mnafahamu sisi ni kina nani?” Ocd alijitutumua kuuliza. Si kamanda wa jeshi bhana!
“Haitotusaidia,” Pte Bayo alijibu. “Kwanza, nyoosheni mikono juu mwite mvua.” Akawazawadia vibao. Wazee walinyanyasika hadi huruma.
Wakatii.
Pindi wanakazana kuita mvua, Luteni Ringo alinuia kutumia wasaa huo kuwafunga pingu. Alianza na Jovin. Alimfunga mkono mmoja, alipotaka kuunganisha mkono wa pili, Jovin aliteremsha mikono na kumsukuma. Luteni Ringo akateleza na kuanguka. Anguko lililomtanguliza makalio sakafuni, huku mkono aliokamatia bastola ukishindwa zoezi la udhibiti na kuruhusu imponyoke.
Pte Bayo akaiwahi ile bastola.
Wapewe nafasi mara ngapi tena? Waliinuka na kufungua riadha kuelekea nje. Pte Pemba akabaki kuwashangaa asijue nini cha kufanya.
“Tutapata taarifa zao kupitia huyu mwenzao,” Luteni Ringo alisema, wakiwa wamesharejea garini.
“Mambo hayajaenda vyema?” Pte Pemba aliuliza.
Pte Bayo ikabidi amweleze kilichojiri.
Mwisho wa maelezo hayo wakatoa mboni kali kwa yule mfanyabiashara, aitwaye Mjimile. Walimtathmini, ataonyesha ushirikiano kiasi gani utakaowasaidia.
***
Walihema juujuu pale walipopumzika, wakiwa wamekimbia umbali wa takribani kilomita mbili kutoka nyumbani kwa Mjimile. Kwani hawakutumia magari. Walihisi yatawachelewesha kiasi cha kukutwa na wabaya wao pindi wanafanya taratibu za ufunguaji na uwashaji. Sambamba na hilo, magari yalikuwa target rahisi kwa wao kushambuliwa na risasi.
“Tunaliamuaje hili kiongozi?” Ocd aliuliza.
“Hata sijui tunafanyaje. Na vipi kuhusu Mjimile? Au ametugeuka na kuamua kutuuza?”
“Sidhani.”
“Ametugeuka bhana. Iweje baada ya yeye kutoka ndiyo yametutokea haya?”
Jovin akadakia. Ile pingu iliendelea kuwepo mkononi, “Sahihi bosi. Ameamua kuuza mechi kwa wapinzani wako.”
Nalimuka akasonya. Ishara ya kujipuuzia namna mambo yaendavyo kombo. Baadaye akatokwa na kauli, “Kuna jambo limenitamanisha kufanya katika hisia zangu.”
Akavuta umakini wa wenzie. Wakamtolea mboni zilizomwashiria aendelee kuzungumza.
“Nataka nikaonane na Kasembe,” alisema na kutulia. Akawasaili kwa muda, bado walikuwa wenye umakini. “Nataka ifanyike namna Kasembe aonane na familia yake na ile ya Cheyaya, wakae wayajenge watamalizaje kesi.”
“Umewaza mbali sana.” Jovin aliafiki.
“Na litatupunguzua mihangaiko.” Ocd akapigilia msumari.
Siku iliyofuata Nalimuka alitekeleza alichokiwazua. Alizuru mahabusu, akiambatana na Meneja wa mamlaka ya mapato mkoa wa Mtwara. Nia ya Nalimuka kwa wakati huo ni uhitaji wa pesa na kifo cha Cheyaya. Cheyaya alimchukia mazima-kwa sababu zake binafsi.
Mazingira ya maongezi yaliandaliwa vyema na uongozi wa gereza. Si waziri bhana! Lolote atakaloliamuru, hutekelezwa kwa utii.
“Kasembe, tajiri,” Nalimuka aliita kwa dharau.
Badala ya kuitika, Kasembe akamwonyeshea dharau.
“Nimekuja kukusabahi, ikiwezekana tukubaliane jambo.”
Kasembe aliendelea kutotoa ushirikiano.
“Inaonekana unayafurahia sana maisha ya gerezani. Sasa vuta picha, ndiyo yanakuwa maisha yako milele, unahisi itakuaje?”
Kasembe hakujibu.
“Haa! Hutaki kuongea?”
“Sema kilichokuleta kisha uondoke,” Kasembe akakata mzizi wa fitna.
“Namtaka Cheyaya humu ndani tumalize hili jambo. Ongea na familia yako, kama haiji, mimi nitafanya mpango waje, uongee nao, mwone jinsi gani watampata Cheyaya. Akipatikana, tufanye mambo ya kiutu uzima ili muurejee uhuru wenu.”
Kasembe ikawa kama ametoneshwa jeraha. Hasira zilimpanda. Kifua kikapwitapwita kama mbogo aliyejeruhiwa. Mpwito ulivyopoa, alivuta kohozi na kuliachia wajihini kwa Nalimuka. Akafuatia kuinuka na kuondoka eneo lile kwa hatua fupifupi za kibabe.
Nalimuka na yule meneja mamlaka ya mapato nao waliinuka. Akachukua leso kutoka mfuko wa nyuma wa suruali, kisha akalifuta lile kohozi kwa hadhari. Asije kulieneza.
“Nimekuja kwa amani ili usiteseke huku, kwani pesa lazima ichukuliwe. Hivyo ridhia nilichokuambia usije kupoteza vyote viwili; pesa na uhuru wako.” Nalimuka alijigamba. Kasembe alisimama na kuwageukia. Ile kauli ilimwingia kwa kiasi fulani.
“Habari ndiyo hiyo. Hivyo chagua moja,” Nalimuka alisisitiza.
***
“Tunazidi kupiga hatua,” Fadhy alisema. Dorice, Stella na Pendo wakiwa makini kumsikiliza. Awamu hii ilikuwa nyumbani kwake wakipata chakula-mlo wa mchana.
“Kwa maana hiyo?” Dorice aliuliza.
“Vijana wangu walifanya uvamizi kwenye ile nyumba pindi wakusudiwa wetu wakiwemo. Isivyobahati, wamefanikiwa kumshikilia mmoja-yule mwenye nyumba, wengine walifanikiwa kutoroka.”
“Walipataje mwanya wa kufanya hivyo?” Dorice aliuliza. Ndiyo aliyekuwa wa kwanza wa kuhoji. Pendo moja ya sifa yake ya ukimya, ilimwondolea kuwa kimbelembele.
“Makosa ni jambo la kawaida katika haya mambo yetu. Ni kama mchezo wa mpira, one mistake, one goal.”
Ufafanuzi huu kwa Stella uliendeleza hasira dhidi ya Jovin.
“Kama ameweza kutoroka, basi ni mkomavu katika maovu,” Stella alijisemeza. Wakati huo akimpambanua Jovin, mwanaume aliyetokea kumwamini. “Lakini siwezi kuruhusu huyu mjinga azidi kufurahia maisha. Lazima nimkamatishe. Akamatwe kwa malipo ya ulaghai alionitendea.” Uchungu ukamkaba, uliomshinikiza atamani kulia, lakini akajikaza.
Kitendo cha kubaini amegawa siri nyingi za nyumbani kwao kwa mwanaume huyo kilimuumuza sana.
“Unaonekana kutokuwa sawa. Vipi, kuna tatizo?” Dorice ndiyo alikuwa wa kwanza kumgundua.
“Niliahidiana na rafiki yangu nimtembelee.”
“Wewe nenda tu, lakini kuwa makini.”
“Sio safari ya siku moja.”
“Siku ngapi? Na wapi huko unakoenda?”
“Morogoro. Na nahitaji nikakae japo kwa siku nne.”
Wote wakamgeukia na kujenga umakini wajihini pake.
Alionesha kiasi fulani cha hofu, lakini baadaye alipiga moyo konde, “Namtembelea yule mtoto wa mzee Koba, niliyekuwa naye pamoja chuo.”
“Unaweza kumruhusu. Kikubwa ni umakini tu-awe mwangalifu.” Fadhy alipendekeza.
“Sawa, unaweza kwenda. Lakini fanya kama ulivyoshauriwa na baba'ko.”
“Nashukuru mama.” Stella akaondoka.
Dhamirio la Stella halikuwa kama alivyoomba ruhusa. Alitaka kusafiri. Lakini sio kuelekea alipowatajia wazazi wake. Lengo afike Mangaka akakutane na Jovin-akamwonyeshe machungu aliyonayo.
***
Cheyaya alisaidizana na mwenyeji wake kuandika mabango yenye jumbe mbalimbali aliyoyakusudia kumwonyesha Waziri Mkuu atakapowasili. Waliyaandika kwenye vipande vya boksi kwa kalamu kubwa. Yalikuwa mabango kumi. Mengine alinuia kuwapa wananchi watakaohudhuria mkutanoni wamsaidie kupaza sauti.
“Hili ndilo nitakalolichukua mwenyewe,” Cheyaya alisema, akilishika shika moja ya bango, lililobeba ujumbe usomekao, ‘Sina amani tena na Taifa langu. Jitihada nilizopigania usiku kucha kwa kuvuja jasho, nataka kudhulumiwa na mliowaamini mkawapatia mamlaka.’
“Inabidi ukae mbelembele ili lionekane kwa urahisi.”
“Upo mawazoni mwangu. Tena ikibidi Waziri Mkuu atakavyoingia tu jukwaani, ninyanyuke na kumkimbilia.”
Mwenyeji akacheka kwa muda. Ile hoja ilimvunja mbavu, “Walinzi hawatokuacha salama.”
“Bora iwe hivyo. Maana si ndiyo nitaonekana kwa uwazi?”
Mwenyeji akatoa msonyo mdogo, kisha akaafikiana na wazo la Cheyaya. “Upo sahihi. Fanya vivyo hivyo. Walinzi wakileta za kuleta unaangua kilio. Yule mzee hawawezi akakuchunia. Lazima akuite tu, afahamu shida yako.”
Wakatabasamu. Matumaini ya ushindi yakajitwalia nafasi kwenye kuta za moyo wa Cheyaya.
“Hapa kilichobakia ni misumari, ili tupigilie kwenye hivi vibao.”
“Nitaenda kununua,” mwenyeji wake alijitolea.
“Kwa sababu ki-giza kimeshaingia, na nimekaa humu ndani kwa muda mrefu, acha nikaoshe oshe macho kwanza.”
“Lakini...” mwenyeji akakatishwa.
“Tulia. Usiku huu, hamna kushangaana.”
“Sawa. Lakini umakini ni muhimu.”
“Hamna noma.”
Dakika kadhaa baadaye Cheyaya alikuwa kwenye badiliko la mavazi. Yule mwenyeji alimnunulia nguo mpya. Chini alipigilia raba. Akavaa suruali ya kadeti rangi ya kahawia. Fulana mchinjo-juu yake prova. Akafunga kazi kwa kapelo rangi nyeusi aliyoiteremsha hadi usawa wa nyusi.
Ilikuwa ngumu kubainika kwa urahisi.
Mara baada ya hapo akauanza mwendo kwa hatua fupifupi zenye ukakamavu kuutafuta mji. Yalipo maduka yatakayomwezesha kupata misumari.
***
Jovin alikuwa amejitawala akiisafisha moja ya silaha anazozimiliki sebuleni-nyumbani kwake. Bunduki, aina ya Dragunov. Lilikuwa zoezi alilolitekeleza kwa utulivu wa hali ya juu. Alipomaliza usafishaji, akawa anafunga taratibu, huku mdomo ukifanya kazi ya ziada ya kuunda mabiti mbalimbali kwa mluzi.
Karibu na hitimisho, kikisalia kifaa kimoja akamilishe ufungaji, mlango ukagongwa. Akasitisha zoezi, akajipa utulivu kusikiliza kwa makini. Ulipogongwa kwa mara nyingine, ndipo alipojihakikishia mbisha hodi yupo mbele ya mlango wa kuingilia nyumbani kwake. Akaacha bunduki tenge, akaenda kumfunglia.
“Stella!” Alistaajabu.
“Ndiyo mimi laazizi. Niambie,” Stella akajibebisha-kwa sauti laini iliyoficha machungu aliyonayo.
“Imekuwa ghafla mno.”
“Kwani ulikwishanipangia muda wa kukutembelea?”
Jovin hakujibu. Alishikwa na kigugumizi kwa muda. Na kilichosababisha ni ile bunduki aliyoiacha kihasarahasara. Atamruhusu vipi aingie ndani?
“Ni mgeni wako kwa hii wiki. Nimekuja kukuondolea manung'uniko ya kunipata mara chache kutibu hisia zako,” Stella aliendelea kusema huku akimrembulia. Alishajidhatiti kuweka makazi hapo, kwani alibeba begi ndogo lililo na utuno kiasi uoneshao kuna kilichobebwa ndanimwe.
***
Cheyaya alishapata huduma, katika moja ya duka lililopo maeneo ya Jangwani. Pindi anaondoka, kukatokea purkushani za hapa na pale za wateja kwenye upishani. Isivyobahati, Cheyaya alikuwa mmoja wa waathirika na kitendo hicho, aligongwa, akasukumizwa mita kadhaa huku akiwaparamia wenzie. Mparamo, ukamdondoshea kofia.
Aliyemgonga akaiokota na kumkabidhi.
“Naomba uniwie radhi, kuna mtu alinisukuma kutoka nyuma nikashindwa kujihimili,” msukumaji alisema.
“Hamna shida ndugu,” Cheyaya alimwondoa hofu pindi akiichukua ile kapelo.
Wakatazamana.
Hamad! Kila mmoja mapigo ya moyo yakambadilika kwa kutoamini. Hata hamu ya kuipokea ile kapelo, Cheyaya ikamtoka. Alikuwa Nalimuka.
Kabla yale matazamano hayajashika hatamu, Cheyaya alimsukumiza Nalimuka kisha akafungua mbio. Nalimuka naye akaunga nyuma yake. Mashuhuda hawakukosekena, wengine wasio na kazi wakathubutu kufuata mkumbo wamsaidie mheshimiwa wao.
“Mwizii huyoo... Mwizii huyooo, mwizii... mwizii,” baadaye ikawabidi wapaze sauti iwarahisishie katika ukamataji kwa kuwashirikisha watu wengine waliopo uelekeo akimbiliao Cheyaya.
TUKUTANE TOLEO LIJALO.MNYONGA TAI—07
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
MAWASILIANO: 0673056571
Walipofanikiwa kuondoka nyumbani kwa Cheyaya, Askofu Ponera na Chiku waliongozana na wale mateka wao hadi alipokuwa anaishi Chiku. Wakawahifadhi wale askari kwenye moja ya chumba, kisha wao wakajipa utulivu. Walipumzika sebuleni.
Mazingira ya nyumba kwa ujumla hayakuwa vyema. Uchafu ulikithiri kwa kukosa matunzo, lakini hiyo haikuwa sababu ya kuwazuia wasitumie. Walipoona utulivu unaanza kuwakinai, ndipo walijiondoa hadi chumbani kwa wale askari. Waliwafunga kudu mikononi.
“Naamini mumeshatafakari vya kutosha,” Askofu Ponera alisema, akiwa anachukua pozi la uketiji kitini. Chiku alisimama mlangoni.
Wale askari hawakumjibu. Badala yake walimkodolea mboni zilizompa picha wanapitia katika hali ngumu ya ukinzani akilini kumtafakari mwanaume huyo anajivunia nini.
“Chiku.” Askofu Ponera akamgeukia. “Njoo wakague hawa.”
Chiku alitii.
“Usiache kitu chochote utakachowakutanacho,” Askofu Ponera akamsisitizia.
Zoezi hilo lilichukua dakika chache sana, Chiku akawasilisha alivyowakutanavyo kwa Askofu Ponera. Vitambulisho na pingu. Baadaye Askofu Ponera alimwita mmoja baada ya mwingine kwa kufuatisha majina yaliyopo kwenye vitambulisho. Mmoja kati yao alikuwa na cheo cha koplo. Wengine ni ma-konstebo.
“Koplo Mvuanyingi,” Askofu Ponera aliita, mboni amezitoa kumwangalia mwitwaji. “Nataka tushirikiane kubadilishana taarifa. Vipi, upo tayari?”
Koplo Mvuanyingi hakujibu. Ndiyo kwanza, alibadili uelekeo wa utazamaji. Wengine vivyo hivyo walivyoulizwa.
“Okay, sio kesi. Nawapa muda zaidi mtafakari. Nitawarudia baadaye.” Askofu Ponera akainuka, na kuondoka mle chumbani kwa mwambatano na Chiku.
“Una uhakika watasema?” Chiku alidadisi.
“Usiwe na shaka.”
“Nahofia tukikutwa na ma-askari wenzao, watatufanyia kitu mbaya hatujawahi ona. Au nawe ni askari?” Chiku akamgeukia Askofu Ponera, huku wakizidi kupiga hatua kupotelea ushorobani.
“Hapana. Mimi ni mtu wa kawaida niliye na machungu na nchi yangu. Napenda kuona haki ikitawala.”
“Huogopi polisi? Maana unajichukulia sheria mkononi.”
Askofu Ponera akasimama na kumgeukia Chiku. Alimsaili kwa muda, kabla hajatokwa na kauli, “Upo na mtu makini sana.”
Wakaendeleza mwendo.
Dakika kumi baadaye Askofu Ponera akawa anamtoa askari mmoja baada ya mwingine anahojiana naye sebuleni. Akishamaliza, humpeleka chumba kingine tofauti na cha awali. Mahojiano ya muda huu hayakuwa na wema. Alitembeza vitu fulanifulani mwilini kwa walengwa vilivyowashinikiza wafunguke baadhi ya mambo.
“Tumeahidiwa donge nono tukifanikisha kumkamata Cheyaya,” Koplo Mvuanyingi alifunguka. Ndiyo alikuwa wa mwisho kuhojiwa. Viadhabu vya kuchomwa chomwa sindano vilipeperusha msimamo wake.
“Nani mtoaji wa hiyo hela?”
“Mbunge. Mheshimiwa Mbunge ndiyo kila kitu katika hili.”
“Nanyi mnajiona mko sahihi?”
“Njaa kaka. Njaa. Kwani hata ungekuwa ewe, usingelikataa ofa yake.”
Askofu Ponera akatabasamu.
“Kwa nini huyo Mbunge anamtaka Cheyaya?”
“Aaah! Hilo nitakudanganya, sijui sababu.”
“Umesahau kazi yake hii?” Askofu Ponera akamwonyesha sindano.
Koplo Mvuanyingi akatokwa na kauli huku akitetemeka, “Kweli ndu... Ndugu sijui...te. Sijui chochote ndugu. Nisamehe bure.”
Kwa kiasi fulani Askofu Ponera aliyaamini maneno ya Koplo Mvuanyingi. Hivyo hakuona haja ya kuendelea kumsulubu. Alimwacha, kisha alitoa taarifa kwa Fadhy kwa njia ya simu.
“Nimefanikiwa kupata madini yenye manufaa kwa ustawi wa nchi yetu,” Askofu Ponera alimtaarifu.
“Yawahishe mahali salama kwa ulinzi zaidi.”
“Timamu kwa utekelezaji.”
“Hakikisha unakuwa usafirishaji salama.”
“Hamna shaka chifu.”
Simu ikakatwa.
***
Luteni Ringo aliongoza timu kama ilivyoamriwa. Mwendo ulikuwa wa mnyato, hadhari wameikumbata vya kutosha wasishtukiwe kiasi cha kuwapa taarifa walengwa wao. Kila mmoja alikuwa na bastola, kwa kujihami na shambulizi lolote lihusishalo zana.
Walivyoufikia mlango wa mbele wakajibanza ukutani kwa mgawanyiko; wawili upande huu-Luteni Ringo na Pte Pemba. Halafu mmoja upande mwingine-Pte Bayo. Mlango waliuweka kati. Baada ya mtuo wa mihemo ya utulivu Luteni Ringo akatoa ishara kwa Pte Bayo. Naye kwa utiifu, aliitekeleza kwa haraka sana. Alibisha hodi kwa kugonga mlango na viganja vya vidole.
Kama ilivyo jadi ya wema kwa watanzania wengi, mlango ulivyogongwa kwa mara ya pili mwenye nyumba akampa subira mgongaji.
“Naja,” ilisikika sauti kutoka ndani. Pasi na umuhimu wa kuhoji mgongaji ni nani.
Ilipita dakika moja toka itikio litolewe, mlango ukashughulishwa na hatimaye kufunguliwa. Yule waliyemhisi awali kuwa mhusika wa nyumba ndiyo alifungua. Akajijaza mlangoni. Mboni zote akazielekeza kwa Pte Bayo.
“Karibu.”
“Nashukuru mzee. Naitwa...” Pte Bayo akakatishwa.
“Nikusaidie ni...?” naye hakumalizia kauli yake, pigo la wastani lilitua shingoni. Alivyonuia kugeuka amwangalie afanyaye, alipigwa kabali akavutwa nje zaidi. Yote hayo yalifanywa na Luteni Ringo.
Pale alipopepesukia mwenye nyumba akafikia kudakwa na Pte Pemba. Kabla hajafungua mdomo kuzungumza jambo akazibwa kwa mkono, kiasi cha kupelekea aheme kwa tabu. Kwani viganja viliziba sehemu ya pua pia.
“Kamwihifadhi garini, wacha sisi tuingie,” Luteni Ringo alipendekeza.
Pte Pemba alifanya alivyoombwa. Luteni Ringo na Pte Bayo wakafanya kusudio lao pia. Waliingia ndani kwa hatua fupifupi, hadhari wameikumbata kidete.
Baada ya hatua kadhaa waliikaribia sebule. Wakaweka pozi kwa muda, kisha kusikilizia maongezi ya wahusika waliopo. Waliyanasa barabara viwamboni. Waliyasikilizia mazungumzo kwa takribani dakika mbili, walipoanza kuingiwa mashaka dhidi ya mwenye nyumba kutorejea wala kumsikia, ndipo Luteni Ringo na Pte Bayo walipojitokeza mbele yao.
Walijitokeza bastola wakiwa wamezielekeza usawa wa ushambuliaji.
“Mikono juu,” Luteni Ringo aliwaamuru kwa sauti kali.
Hakuna ajawaye ujasiri kwenye uvamizi.
Hivyo, Nalimuka na wenzie walipata hofu kwa muda, iliyowashurutisha wajiinue walipoketi kutafuta sehemu ya uficho-kila mmoja alipoona panamfaa. Lakini kabla hawajayafikia, Luteni Ringo aliruhusu mitupo kadhaa ya risasi ukutani. Hakukuwa na amani tena, wakabaki kugongana gongana mithili ya kuruta wapatapo ruhusa ya kupumzika wakiwa kwenye kusanyiko.
Kwa kuwa ile bastola haikufungwa kiwambo, mshindo wa sauti ukawa mkubwa. Huo ndiyo uliwatetemesha zaidi.
“Kwa amani, wote rudini hapa kabla sijawafumua bongo zenu,” Luteni Ringo aliwaamuru kwa mara nyingine. Ile bastola akimwelekezea mmoja baada ya mwingine.
Fikra ya haraka iliyotapakaa bongoni kina Nalimuka kwamba wamevamiwa na majambazi. Wafanye nini zaidi ya kukubaliana na waamriwacho? Walitii bila shuruti.
Kwa hofu, Nalimuka na u-waziri wake, jasho chapachapa limemkithiri, aliwaongoza wenzie hadi walipoamriwa wakae. Mkao wa pigo la goti.
“Hivi mnafahamu sisi ni kina nani?” Ocd alijitutumua kuuliza. Si kamanda wa jeshi bhana!
“Haitotusaidia,” Pte Bayo alijibu. “Kwanza, nyoosheni mikono juu mwite mvua.” Akawazawadia vibao. Wazee walinyanyasika hadi huruma.
Wakatii.
Pindi wanakazana kuita mvua, Luteni Ringo alinuia kutumia wasaa huo kuwafunga pingu. Alianza na Jovin. Alimfunga mkono mmoja, alipotaka kuunganisha mkono wa pili, Jovin aliteremsha mikono na kumsukuma. Luteni Ringo akateleza na kuanguka. Anguko lililomtanguliza makalio sakafuni, huku mkono aliokamatia bastola ukishindwa zoezi la udhibiti na kuruhusu imponyoke.
Pte Bayo akaiwahi ile bastola.
Wapewe nafasi mara ngapi tena? Waliinuka na kufungua riadha kuelekea nje. Pte Pemba akabaki kuwashangaa asijue nini cha kufanya.
“Tutapata taarifa zao kupitia huyu mwenzao,” Luteni Ringo alisema, wakiwa wamesharejea garini.
“Mambo hayajaenda vyema?” Pte Pemba aliuliza.
Pte Bayo ikabidi amweleze kilichojiri.
Mwisho wa maelezo hayo wakatoa mboni kali kwa yule mfanyabiashara, aitwaye Mjimile. Walimtathmini, ataonyesha ushirikiano kiasi gani utakaowasaidia.
***
Walihema juujuu pale walipopumzika, wakiwa wamekimbia umbali wa takribani kilomita mbili kutoka nyumbani kwa Mjimile. Kwani hawakutumia magari. Walihisi yatawachelewesha kiasi cha kukutwa na wabaya wao pindi wanafanya taratibu za ufunguaji na uwashaji. Sambamba na hilo, magari yalikuwa target rahisi kwa wao kushambuliwa na risasi.
“Tunaliamuaje hili kiongozi?” Ocd aliuliza.
“Hata sijui tunafanyaje. Na vipi kuhusu Mjimile? Au ametugeuka na kuamua kutuuza?”
“Sidhani.”
“Ametugeuka bhana. Iweje baada ya yeye kutoka ndiyo yametutokea haya?”
Jovin akadakia. Ile pingu iliendelea kuwepo mkononi, “Sahihi bosi. Ameamua kuuza mechi kwa wapinzani wako.”
Nalimuka akasonya. Ishara ya kujipuuzia namna mambo yaendavyo kombo. Baadaye akatokwa na kauli, “Kuna jambo limenitamanisha kufanya katika hisia zangu.”
Akavuta umakini wa wenzie. Wakamtolea mboni zilizomwashiria aendelee kuzungumza.
“Nataka nikaonane na Kasembe,” alisema na kutulia. Akawasaili kwa muda, bado walikuwa wenye umakini. “Nataka ifanyike namna Kasembe aonane na familia yake na ile ya Cheyaya, wakae wayajenge watamalizaje kesi.”
“Umewaza mbali sana.” Jovin aliafiki.
“Na litatupunguzua mihangaiko.” Ocd akapigilia msumari.
Siku iliyofuata Nalimuka alitekeleza alichokiwazua. Alizuru mahabusu, akiambatana na Meneja wa mamlaka ya mapato mkoa wa Mtwara. Nia ya Nalimuka kwa wakati huo ni uhitaji wa pesa na kifo cha Cheyaya. Cheyaya alimchukia mazima-kwa sababu zake binafsi.
Mazingira ya maongezi yaliandaliwa vyema na uongozi wa gereza. Si waziri bhana! Lolote atakaloliamuru, hutekelezwa kwa utii.
“Kasembe, tajiri,” Nalimuka aliita kwa dharau.
Badala ya kuitika, Kasembe akamwonyeshea dharau.
“Nimekuja kukusabahi, ikiwezekana tukubaliane jambo.”
Kasembe aliendelea kutotoa ushirikiano.
“Inaonekana unayafurahia sana maisha ya gerezani. Sasa vuta picha, ndiyo yanakuwa maisha yako milele, unahisi itakuaje?”
Kasembe hakujibu.
“Haa! Hutaki kuongea?”
“Sema kilichokuleta kisha uondoke,” Kasembe akakata mzizi wa fitna.
“Namtaka Cheyaya humu ndani tumalize hili jambo. Ongea na familia yako, kama haiji, mimi nitafanya mpango waje, uongee nao, mwone jinsi gani watampata Cheyaya. Akipatikana, tufanye mambo ya kiutu uzima ili muurejee uhuru wenu.”
Kasembe ikawa kama ametoneshwa jeraha. Hasira zilimpanda. Kifua kikapwitapwita kama mbogo aliyejeruhiwa. Mpwito ulivyopoa, alivuta kohozi na kuliachia wajihini kwa Nalimuka. Akafuatia kuinuka na kuondoka eneo lile kwa hatua fupifupi za kibabe.
Nalimuka na yule meneja mamlaka ya mapato nao waliinuka. Akachukua leso kutoka mfuko wa nyuma wa suruali, kisha akalifuta lile kohozi kwa hadhari. Asije kulieneza.
“Nimekuja kwa amani ili usiteseke huku, kwani pesa lazima ichukuliwe. Hivyo ridhia nilichokuambia usije kupoteza vyote viwili; pesa na uhuru wako.” Nalimuka alijigamba. Kasembe alisimama na kuwageukia. Ile kauli ilimwingia kwa kiasi fulani.
“Habari ndiyo hiyo. Hivyo chagua moja,” Nalimuka alisisitiza.
***
“Tunazidi kupiga hatua,” Fadhy alisema. Dorice, Stella na Pendo wakiwa makini kumsikiliza. Awamu hii ilikuwa nyumbani kwake wakipata chakula-mlo wa mchana.
“Kwa maana hiyo?” Dorice aliuliza.
“Vijana wangu walifanya uvamizi kwenye ile nyumba pindi wakusudiwa wetu wakiwemo. Isivyobahati, wamefanikiwa kumshikilia mmoja-yule mwenye nyumba, wengine walifanikiwa kutoroka.”
“Walipataje mwanya wa kufanya hivyo?” Dorice aliuliza. Ndiyo aliyekuwa wa kwanza wa kuhoji. Pendo moja ya sifa yake ya ukimya, ilimwondolea kuwa kimbelembele.
“Makosa ni jambo la kawaida katika haya mambo yetu. Ni kama mchezo wa mpira, one mistake, one goal.”
Ufafanuzi huu kwa Stella uliendeleza hasira dhidi ya Jovin.
“Kama ameweza kutoroka, basi ni mkomavu katika maovu,” Stella alijisemeza. Wakati huo akimpambanua Jovin, mwanaume aliyetokea kumwamini. “Lakini siwezi kuruhusu huyu mjinga azidi kufurahia maisha. Lazima nimkamatishe. Akamatwe kwa malipo ya ulaghai alionitendea.” Uchungu ukamkaba, uliomshinikiza atamani kulia, lakini akajikaza.
Kitendo cha kubaini amegawa siri nyingi za nyumbani kwao kwa mwanaume huyo kilimuumuza sana.
“Unaonekana kutokuwa sawa. Vipi, kuna tatizo?” Dorice ndiyo alikuwa wa kwanza kumgundua.
“Niliahidiana na rafiki yangu nimtembelee.”
“Wewe nenda tu, lakini kuwa makini.”
“Sio safari ya siku moja.”
“Siku ngapi? Na wapi huko unakoenda?”
“Morogoro. Na nahitaji nikakae japo kwa siku nne.”
Wote wakamgeukia na kujenga umakini wajihini pake.
Alionesha kiasi fulani cha hofu, lakini baadaye alipiga moyo konde, “Namtembelea yule mtoto wa mzee Koba, niliyekuwa naye pamoja chuo.”
“Unaweza kumruhusu. Kikubwa ni umakini tu-awe mwangalifu.” Fadhy alipendekeza.
“Sawa, unaweza kwenda. Lakini fanya kama ulivyoshauriwa na baba'ko.”
“Nashukuru mama.” Stella akaondoka.
Dhamirio la Stella halikuwa kama alivyoomba ruhusa. Alitaka kusafiri. Lakini sio kuelekea alipowatajia wazazi wake. Lengo afike Mangaka akakutane na Jovin-akamwonyeshe machungu aliyonayo.
***
Cheyaya alisaidizana na mwenyeji wake kuandika mabango yenye jumbe mbalimbali aliyoyakusudia kumwonyesha Waziri Mkuu atakapowasili. Waliyaandika kwenye vipande vya boksi kwa kalamu kubwa. Yalikuwa mabango kumi. Mengine alinuia kuwapa wananchi watakaohudhuria mkutanoni wamsaidie kupaza sauti.
“Hili ndilo nitakalolichukua mwenyewe,” Cheyaya alisema, akilishika shika moja ya bango, lililobeba ujumbe usomekao, ‘Sina amani tena na Taifa langu. Jitihada nilizopigania usiku kucha kwa kuvuja jasho, nataka kudhulumiwa na mliowaamini mkawapatia mamlaka.’
“Inabidi ukae mbelembele ili lionekane kwa urahisi.”
“Upo mawazoni mwangu. Tena ikibidi Waziri Mkuu atakavyoingia tu jukwaani, ninyanyuke na kumkimbilia.”
Mwenyeji akacheka kwa muda. Ile hoja ilimvunja mbavu, “Walinzi hawatokuacha salama.”
“Bora iwe hivyo. Maana si ndiyo nitaonekana kwa uwazi?”
Mwenyeji akatoa msonyo mdogo, kisha akaafikiana na wazo la Cheyaya. “Upo sahihi. Fanya vivyo hivyo. Walinzi wakileta za kuleta unaangua kilio. Yule mzee hawawezi akakuchunia. Lazima akuite tu, afahamu shida yako.”
Wakatabasamu. Matumaini ya ushindi yakajitwalia nafasi kwenye kuta za moyo wa Cheyaya.
“Hapa kilichobakia ni misumari, ili tupigilie kwenye hivi vibao.”
“Nitaenda kununua,” mwenyeji wake alijitolea.
“Kwa sababu ki-giza kimeshaingia, na nimekaa humu ndani kwa muda mrefu, acha nikaoshe oshe macho kwanza.”
“Lakini...” mwenyeji akakatishwa.
“Tulia. Usiku huu, hamna kushangaana.”
“Sawa. Lakini umakini ni muhimu.”
“Hamna noma.”
Dakika kadhaa baadaye Cheyaya alikuwa kwenye badiliko la mavazi. Yule mwenyeji alimnunulia nguo mpya. Chini alipigilia raba. Akavaa suruali ya kadeti rangi ya kahawia. Fulana mchinjo-juu yake prova. Akafunga kazi kwa kapelo rangi nyeusi aliyoiteremsha hadi usawa wa nyusi.
Ilikuwa ngumu kubainika kwa urahisi.
Mara baada ya hapo akauanza mwendo kwa hatua fupifupi zenye ukakamavu kuutafuta mji. Yalipo maduka yatakayomwezesha kupata misumari.
***
Jovin alikuwa amejitawala akiisafisha moja ya silaha anazozimiliki sebuleni-nyumbani kwake. Bunduki, aina ya Dragunov. Lilikuwa zoezi alilolitekeleza kwa utulivu wa hali ya juu. Alipomaliza usafishaji, akawa anafunga taratibu, huku mdomo ukifanya kazi ya ziada ya kuunda mabiti mbalimbali kwa mluzi.
Karibu na hitimisho, kikisalia kifaa kimoja akamilishe ufungaji, mlango ukagongwa. Akasitisha zoezi, akajipa utulivu kusikiliza kwa makini. Ulipogongwa kwa mara nyingine, ndipo alipojihakikishia mbisha hodi yupo mbele ya mlango wa kuingilia nyumbani kwake. Akaacha bunduki tenge, akaenda kumfunglia.
“Stella!” Alistaajabu.
“Ndiyo mimi laazizi. Niambie,” Stella akajibebisha-kwa sauti laini iliyoficha machungu aliyonayo.
“Imekuwa ghafla mno.”
“Kwani ulikwishanipangia muda wa kukutembelea?”
Jovin hakujibu. Alishikwa na kigugumizi kwa muda. Na kilichosababisha ni ile bunduki aliyoiacha kihasarahasara. Atamruhusu vipi aingie ndani?
“Ni mgeni wako kwa hii wiki. Nimekuja kukuondolea manung'uniko ya kunipata mara chache kutibu hisia zako,” Stella aliendelea kusema huku akimrembulia. Alishajidhatiti kuweka makazi hapo, kwani alibeba begi ndogo lililo na utuno kiasi uoneshao kuna kilichobebwa ndanimwe.
***
Cheyaya alishapata huduma, katika moja ya duka lililopo maeneo ya Jangwani. Pindi anaondoka, kukatokea purkushani za hapa na pale za wateja kwenye upishani. Isivyobahati, Cheyaya alikuwa mmoja wa waathirika na kitendo hicho, aligongwa, akasukumizwa mita kadhaa huku akiwaparamia wenzie. Mparamo, ukamdondoshea kofia.
Aliyemgonga akaiokota na kumkabidhi.
“Naomba uniwie radhi, kuna mtu alinisukuma kutoka nyuma nikashindwa kujihimili,” msukumaji alisema.
“Hamna shida ndugu,” Cheyaya alimwondoa hofu pindi akiichukua ile kapelo.
Wakatazamana.
Hamad! Kila mmoja mapigo ya moyo yakambadilika kwa kutoamini. Hata hamu ya kuipokea ile kapelo, Cheyaya ikamtoka. Alikuwa Nalimuka.
Kabla yale matazamano hayajashika hatamu, Cheyaya alimsukumiza Nalimuka kisha akafungua mbio. Nalimuka naye akaunga nyuma yake. Mashuhuda hawakukosekena, wengine wasio na kazi wakathubutu kufuata mkumbo wamsaidie mheshimiwa wao.
“Mwizii huyoo... Mwizii huyooo, mwizii... mwizii,” baadaye ikawabidi wapaze sauti iwarahisishie katika ukamataji kwa kuwashirikisha watu wengine waliopo uelekeo akimbiliao Cheyaya.
TUKUTANE TOLEO LIJALO.