Riwaya: Mkoloni Mzawa

Riwaya: Mkoloni Mzawa

RIWAYA: MKOLONI MZAWA—2
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
SEHEMU YA 23.

Hali ya Babigamba ilikuwa mbaya. Katika yale matupiano ya risasi kuna kadhaa zilimpata mwilini. Zilizoshambuliwa kupitia pembezoni mwa ukuta uliotengenezwa na Luteni Jenerali Kipozi na Luteni Mwaipeta. Zilimpata begani, nyingine mguuni. Ilhali muda wote hakuwa mwenye fahamu.

Na walivyoondoka eneo la tukio, kituo chao kilikuwa kwenye makazi yao kule Ngowe. Wakamuhifadhi Babigamba ndani ya chumba kimoja wapo, kisha pasi na kukawia, akaanza kupatiwa matibabu. Makamu wa Rais, Lilian alimtafuta daktari pamoja na vifaa tiba vitakiwavyo.

Pindi Babigamba akiendelea kupatiwa matibabu wao waliketi pembeni wakishuhudia. Makamu wa rais, Lilian. Ambaye alikuwa amevaa suruali ya jinzi-rangi ya kahawia, fulana nyekunde na raba rangi ya njano chini. Juu alipigilia boshori aliyoiteremsha na kuzuia masikio. Jenerali Namkumba, alivaa pensi rangi ya khaki, shati lenye mchanganyiko wa rangi; nyeusi, nyeupe na kijani. Chini alivaa sendoz. IGP Lukanga, alivaa kanzu rangi ya hudhurungi, chini sendoz. Ndalama naye alipigilia kanzu rangi nyeusi. Luteni Mwaipeta, Koplo Namaya na Konstebo Babaa nao walikuwepo pia.

Kila kitu walikielekezea kwenye matibabu. Kuanzia akili, masikio, macho; na mwili wote kwa ujumla. Ijapokuwa, hawakuacha kuwa na mashaka juu ya Luteni Jenerali Kipozi kwa muda fulani.
“Muna uhakika...” Makamu wa Rais, Lilian aliongea. Kabla hajamalizia kauli yake kikasikika kishindo kilichomshtua kila mmoja. Kilikuwa kishindo cha nguvu.

Luteni Mwaipeta akainuka na kwenda kuchungulia apate kufahamu nini tatizo. Alikumbana na sura za kina Kinyonga, Mauten na Shida. Akawarejea wenzie.
“Tumevamiwa,” aliwataarifu. Akiwa na muonekano wa wajihi wenye wahka.

Mshtuko ukawazidi! Hasa Makamu wa Rais, Lilian, Jenerali Namkumba, Ndalama na IGP Lukanga.
“Vijana, njooni tupambane,” Luteni Mwaipeta alisema. Baada ya kauli hiyo Koplo Namaya na Konstebo Babaa waliinuka na kumfuata Luteni Mwaipeta.

Cha kwanza walipiga hatua hadi kwenye chumba fulani wakabeba bunduki. Luteni Mwaipeta na Konstebo Babaa walibeba bunduki watumiazo siku zote kwenye majukumu yao. Isipokuwa Koplo Namaya. Alibadili. Alibeba LRR (Long Range Rifle) M 93. Baada ya hapo waliondoka.

Makamu wa Rais, Lilian, Jenerali Namkumba, Ndalama na IGP Lukanga walisalia mule mule chumbani apatiwapo Babigamba matibabu wakiwa wenye hofu. Mioyo yao ilikuwa juu juu, huku muda wote wakiomba, Luteni Mwaipeta na wenzie wafanikiwe kuwadhibiti kina Kinyonga haraka iwezekanavyo. Walihofia bainikolao la wazi kama nao ni sehemu ya mkumbo unaohitaji Rais Sharabu ang’oke madarakani.

Haikuchukua muda mrefu, milio ya risasi ikaanza kusikika kwa ukaribu. Iliyoashiria maadui zao wameshafanikiwa kuingia ndani ya jengo. Nao walivyokuwa wajinga, walishambulia ili mradi tu. Pasi na kuangalia kama kuna umuhimu kwa upande wao. Tena walishambulia huku wakisonga mbele.

Luteni Mwaipeta na wenzie wakatega kwenye moja ya kuta koridoni kuwapimia.
“Koplo Namaya, take your position,” Luteni Mwaipeta aliongea. Kauli iliyotekelezwa kwa vitendo na Koplo Namaya. Aliondoka pale walipojificha, akaingia kwenye moja ya chumba.

Pindi anaondoka alionwa na Shida. Aliyekuwa anaangaza huku na kule kwa uchunguzi zaidi wa mazingira.
“Wamejificha kule mbele,” Shida aliwanong’oneza wenzie.

Wakapiga hatua kwa hadhari kuelekea walikoambiwa.

Luteni Mwaipeta akamuamuru Konstebo Babaa avukie upande wa pili. Konstebo Babaa alivyotekeleza alionwa. Kitendo kilichowashinikiza Kinyonga, Mauten na Shida wamshambulie kwa pamoja. Lakini shabaha yao haikuzaa matunda.

Muundo wa nyumba mule ndani; ulikuwa na vyumba vinne, sebule, sehemu ya chakula, jiko, stoo na choo cha umma. Achilia mbali vyoo vya kila chumba. Vyumba viletenganishwa na korido, wakati sebule iliambatana na sehemu ya chakula. Huku stoo, jiko na choo vikiwa mbele mara baada ya vyumba. Ikiwa na maana upande wa nyuma wa nyumba hiyo. Lakini palikuwa na korido pia iliyotenganisha vyumba, choo, stoo na hilo jiko. Hapo ndipo walijificha Luteni Mwaipeta na Konstebo Babaa.

Kinyonga na wenzie nao walijigawa; wawili waliambaa ambaa kiambaza hiki-Kinyonga na Shida, mmoja-Mauten, kile kiambaza kingine. Mwendo wao ukawa wa mnyato, mitutu ya bunduki imeelekezwa usawa wa mapambano. Katikati ya vile viambaza pale koridoni kulikuwa na mapipa mawili. Yakawa kama kinga kwa kina Kinyonga.

Luteni Mwaipeta akatoa ishara kwa Konstebo Babaa ya kuwataka washambulie kwa pamoja.

Wakafanya hivyo. Kwa kujitokeza kidogo mbele ya korido na kushambulia risasi kadhaa kisha walijirudisha mafichoni. Risasi zao zikaenda kugonga kwenye yale mapipa. Kinyonga na wenzie waka-dash down kwa kuchuchumaa.

Pale chini Kinyonga na wenzie walitulia kwa sekunde kadhaa, baadaye Mauten alinyanyuka na kushambulia mitupo mitatu ya risasi moja ya kona, aliyojificha Konstebo Babaa kisha alijirudisha chini.

Kabla harufu ya baruti haijapoa kufukiza, Shida naye alinyanyuka. Mnyanyuko ulioambatana na bunduki kuketishwa kwenye nyama ya bega. Akakumbana na Luteni Mwaipeta titi fo tati. Naye akiwa ameiketisha vyema bunduki yake.
Kwa pamoja wakaruhusu shambulizi. Lakini Luteni Mwaipeta alikuwa kasi sana. Alivyominya kifyatulio tu, alilala chini na kujirudisha mafichoni kinyume nyume. Mtupo wa risasi wa Shida ulipita kapa, na kwenda kukita mlango wa choo. Ilipasua na kupotelea upande wa pili.

Mtupo wa risasi wa Luteni Mwaipeta ulimpata Shida kwenye bega ya mkono wa kushoto. Ulimyumbisha. Na kumpotezea uhimili wa kusimama na umiliki wa bunduki mikononi. Baadaye alitoa mguno uliobeba hisia za kiasi cha maumivu ayasikiayo.

Kinyonga akamvuta chini kwa nguvu.

“Amenishambulia huyo mbwa,” Shida alilalama.

Kinyonga akamtuliza, “Punguza jazba.” Akatoa kitambaa katika mfuko wa suruali aliyovaa, akamfunga Shida kwenye lile jeraha.

Yakaibuka mashambulizi ya kuviziana.

Baadaye, takribani muda wa nusu saa toka waanze kushambuliana, timu ya makomando iliyoandaliwa ile siku kumpatia ulinzi Rais Sharabu ikaongeza nguvu. Ilikuwa timu ya watu watano. Hawakuvaa mavazi ya kijeshi, walivaa kiraia, kila mmoja akiwa na bunduki ya kivita.

Ujio wao ulitokana na mkazo kutoka kwa Rais Sharabu. Kusipambazuke vyema pasipo kusikia mabadiliko ya majina ya wabaya wake. Wauwawe.

Ule mgawanyiko walioufanya awali uliweza kuwasaidia kina Luteni Mwaipeta. Kwani kule alipoelekea Koplo Namaya alifikia kupanda darini na kwenda kuweka pozi kwenye moja ya kona, karibu na siling board iliyokaribia kudondoka. Hivyo mazingira ya chini, hasa pale sebuleni na koridoni aliyaona vyema.

Makomando walivyoiingia kwa papara yenye hadhari, Koplo Namaya alikoki bunduki na kuanza ushambuliaji. Alimshambulia mmoja baada ya mwingine. Tena sio kwa kuwarembesha, shabaha zote alizielekezea kichwani.

Kitendo hicho kiliwashtua kina Kinyonga pale walipo. Na komando wawili waliobakia. Waliona ngoma ni nzito, ijapokuwa walishahisi mshambuliaji wapi amejificha. Wakaamua kutoka nduki hadi walipoegesha gari zao. Walipanda kwa haraka, kisha komando mmoja wao alichukua RPG (Rocket Propelled Grenade) akapachika kombora na kuliachia kuelekea lilipo lile jengo. Walilopo kina Luteni Mwaipeta.

Halikuwa kombora moja pekee, alirusha makombora manne, yaliyopelekea kuisambaratisha ile nyuma kama imetokwa kujengwa juzi.

***

“Kwa mantiki ya maelezo yao ina maana wameshindwa kutambua sura za wahusika waliopo ndani ya ile nyumba,” Rais Sharabu aliongea. Akionekana kuwa mwenye ghadhibiko kubwa nafsini mwake.
“Sahihi mheshimiwa,” Killa alijibu kwa sauti iliyojaa unyenyekevu.

Rais Sharabu alimaka, “Ni ujinga huo. Sasa tutawatambuaje hao watu kama ndiye wale tuwadhaniao?”
“Shambulizi walilolifanya hawawezi kutoka salama. Kwa namna yoyote lazima wafe. Hivyo kama watakuwa wameshafariki, kutoonekana kwao ndiyo utakuwa uthibitisho.”
“Hawakupaswa kuuwawa ki-rahisi hivyo. Ilibidi wapite mbele yangu kabla ya vifo vyao. Lakini bado siamini kama hao watu watakuwa wamefariki.”
“Kama huamini mwamuru Sacp Chiwila apeleke vijana wake eneo la tukio wakalidhibiti,” Killa alishauri.
“Umeshauri kitu sahihi,” Rais Sharabu aliafiki huku akitingisha kichwa. Baadaye alitoa simu kwenye mfuko wa suruali, alibonyeza vitufe kadhaa na kuisogeza usawa wa sikio.

Ilivyopokelewa, akawa kwenye mazungumzo na mtu wa upande wa pili.

***

Zilipita dakika tano, toka Rais Sharabu atoe amri kwa Kamanda wa polisi kanda maalum ya Nufaiko. Gofu la jengo walilokuwemo kina Luteni Mwaipeta likazingirwa na askari polisi; kutoka vitengo vya kutuliza ghasia, Upelelezi (Makachero), Intellijensia na wa General Duty (GD). Sacp Chiwila ndiyo aliongoza vikosi vyote hivyo, kwa kusaidizana na wakuu wa Kamandi husika.

Askari wa kutuliza ghasia walikuwa mahususi kwa ulinzi, Makachero, kwa ajili ya uchunguzi, General Duty kudhibiti halaika ya watu waliokusanyika kushuhudia tukio, wakati wa Intellijensia kukusanya taarifa.

Kwa uhitaji wa kufanya kazi vuzuri, askari walizungusha utepe wa njano kulizunguka gofu umbali wa mita kumi kila upande. Wananchi wakasimama nje ya utepe huo.

Uchunguzi ukachukua nafasi.

Pindi askari wa vyeo vya chini wakiwa bize kufanya uchunguzi na ulinzi sehemu za nje ya jengo, Sacp Chiwila aliteka vyombo vya habari. Kuuhabarisha umma juu ya tukio lililotendeka.
“Kwa muda mrefu tulipata taarifa za uwepo wenye nia ovu ndani ya hii nyumba. Watu waliobeba maono ya uasi dhidi ya serikali yetu. Nimshukuru mtoa taarifa wetu, na niwaombe wananchi wengine, pale mtakapowabaini watu wa namna hii.
“Na kwa kuwahakikishia, wote ambao walikuwa wahusika katika hii nyumba tutawakamata, kisha hatua za kisheria zitachukua mkondo wake.”
“Aah! Kamanda, mumebahatika kuwafahamu japo kwa sura au majina?” mmoja wa waandishi wa habari alimtupia swali.
“Hilo suala la ki-upelelezi. Hatuwezi kuweka wazi kwa sasa. Mambo yakishakamilisha tutawabainisha wananchi wawatambue.”

***

Shambulizi la makombora liliharibu kila kitu kwa kina Luteni Mwaipeta na timu nzima. Kule juu alikokuwa Koplo Namaya alifurumushwa na kuanguka chini kama mtu asiye na utimamu wa akili. Alipofikia mgongo ukampa tahadhari ya maumivu yaliyopo kutokana na mwanguko ulivyokuwa. Juu yake yakafuatia mabati, mbao na matofali.

Ilikuwa vivyo hivyo kwa Luteni Mwaipeta na Konstebo Babaa, waliangukiwa na vitu kadha wa kadha. Pasi na kusahau Makamu wa Rais, Lilian, Jenerali Namkumba, Ndalama na IGP Lukanga. Daktari na Babigamba nao pia. Kwa ujumla waliangukiwa na kifusi, huku moto ukiteketeza vitu mbalimbali vyenye uwezo wa kuungua.

Lakini chumba cha matibabu kulikuwa na nafuu kiasi. Hawakupata madhara makubwa sana, hivyo waliweza kujiinua kutoka kwenye kifusi na kuanza kupanga mbinu za kujinusuru.
“Hapa si salama tena kwetu,” Ndalama alisema. Akiwa anafuta vumbi kwenye kope.
“Hakika. Na yatupasa tuwe faster, tukizembea tunaweza kukutwa,” Jenerali Namkumba alikazia kauli ya Ndalama.
“Tuwaangalie na vijana tuone wapo katika hali gani,” Makamu wa Rais, Lilian naye hakuwa nyuma kuchangia. Muonekano wake ukibadilishwa na vumbi lililomzingira.

Wawili baina yao; Jenerali Namkumba na Ndalama wakatoka kwenda kuwaangalia. Walipiga hatua moja tu kutoka chumbani. Walivyohitaji kupiga kupiga ya pili waifikie korido, vikasikika ving’ora umbali mfupi toka hapo vilivyowabainisha kuwa ni magari ya polisi. Wakarudi ndani chap.
“Kuna magari ya polisi. Nahisi yanakuja hapa,” Ndalama aliongea. Mapigo ya moyo yakimwenda kasi.

Wengine wakatega masikio vyema kusikilizia. Sauti ya ving’ora ilizidi kusogea.

“Tunafanyaje?” Makamu wa Rais, Lilian aliuliza.
“Tunaweza kutumia huu upande wa nyuma kutoroka,” IGP Lukanga alishauri.
“Vipi kuhusu vijana?”
“Mmmh! Ni mtihani. Yumkini wamepatwa na tatizo, laiti kama wangelikuwa sawa wangerejea humu ndani.”
“Kwa hiyo tuwaache? Na ukizingatia hatuna uhakika; kama ni wazima ama wameshafariki.”

Ukapita ukimya mfupi. Ulifukuzwa na Jenerali Namkumba baadaye, “Babigamba ndiyo mwenye umuhimu wa kwanza kwetu. Tupiganie uhai wake, ili tukamalizie hatua zilizosalia.”
“Kwa hiyo tuondoke?” Makamu wa Rais, Lilian alipachika swali lingine. Kisha alimsaili mmoja baada ya mwingine.
IGP Lukanga alijibu kwa niaba ya wengine, “Hatuna namna. Tufanye hivyo.”

Wakajiandaa kutoka. Kwa kugawana majukumu, kwamba wawili baina yao wabebe machela atakayolazwa Babigamba. Ndalama na Makamu wa Rais, Lilian walijitolea kutekeleza jukumu hilo. Wakati Jenerali Namkumba na IGP Lukanga walijipa jukumu la ki-ulinzi. Daktari, aliendelea kubaki sehemu yake. Ya uangalizi wa afya ya Babigamba.

Kabla hawajatoka, Jenerali Namkumba aliangazia njia wanayohitaji kutumia kwa ajili ya kutoroka. Uwepo wa askari waliozunguka kwa ulinzi ukamnyong’onyesha. Akawapa taarifa wenzie, “Askari wamezingira karibia kila pande. Tutatokaje?”

Wote walipigwa na butwaa.

***

Kutokana na ukubwa wa kifusi ililetwa Katapila kwa ajili ya kusawazisha kwa haraka ndani ya jengo. Sanjari na gari la zimamoto, kuzima ule moto uliozidi kuongezeka kadri sekunde zilivyozidi kusonga mbele. Wahusika wakafanyiana zamu; walianza wa zimamoto, walivyomaliza ndipo watu wa katapila nao walianza shughuli yao.

Muda wote askari paswa wa uchunguzi hawakuingia ndani. Walisubiri mazoezi hayo yakamilike ndipo waianze shughuli kwa upande wa ndani.

Ile mwaga mwaga ya maji ilimpatia nguvu Koplo Namaya pale alipoangukia. Alianguka na bunduki yake. Akajitutumua, lakini sehemu ya paa iliyomwangukia ilimpa kizuizi. Hakukata tamaa. Aliendelea kujitutumua, baada ya muda alipata nafasi ya kuliinua lile paa kiurahisi na kupata mwanya wa kujiondoa. Lakini kabla hajaondoka, alisaili mazingira kwa jicho kengeza. Alimuona dereva wa katapila akipiga mwendo kusonga mbele.
“Huyu anaweza kuwa kikwazo cha kujinusuru,” Koplo Namaya alijisemeza. Taratibu akivuta bunduki yake na kuipakata vyema kifuani.

Baadaye aliikita ile bunduki kwenye nyama ya bega. Akaisaili changing liver, akabaini ipo wazi. Ipo sehemu ya kuruhusu mashambulizi. Hakuremba, alioanisha shabaha kwenda sehemu kusudiwa. Kwa dereva.

Mtupo mmoja tu wa risasi ulimwezesha kuwa malengoni. Alimpiga dereva kwenye paji la uso. Dereva akatulia tuli na uelekeo wa katapila kupotea. Askari wakashikwa na bumbuwazi, wananchi pia. Mbona katapila halisongi mbele?
“Afande, mbona katapila halitembei tena?” mmoja wa askari alimtaarifu Sacp Chiwila kwa mfumo wa swali.

Sacp Chiwila aliacha kuzungumza na wanahabari akaangazia kule lilipo katapila. Naye hakuelewa picha lililopo.
“Hebu twendeni kwanza,” Sacp Chiwila aliwaamuru wakuu wa Kamandi.

Kwa pamoja walitekeleza.

Koplo Namaya alitumia hiyo nafasi kutoka pale alipoangukia kwa mbio yenye upindo hadi chumba alichokuwa anapatiwa matibabu Babigamba.

Wote walishtuka walipomuona.

“Upo vizuri?”
“Hali vipi?”
“Ulikuwa wapi muda wote huo? Vipi wenzako, nao wapo wapi?”

Walimtupia maulizo lukuki. Huku wakijitahidi kumsaili muonekano wa mwili wake ulivyo.
“Nipo vizuri, japo si sana. Nina maumivu kidogo upande wa mbavu za kushoto na kifuani,” Koplo Namaya alijibu, huku akijinyoosha nyoosha kuweka mwili sawa.
“Vipi kuhusu wenzio?” Makamu wa Rais, Lilian aliuliza.
“Tuligawana majukumu. Wao walikuwa chini, mimi nikapanda darini. Hamjawaona?”

Makamu wa Rais, Lilian alijibu kwa kuanza kutingisha kichwa, “Hatujawaona.”
“Kuwatafuta?”
“Tumeshindwa kuwatafuta kutokana na hiyo hali ya huko nje. Kingine, sura zetu hazipaswi kuonekana.”

Koplo Namaya alivuta pumzi na kuzitua kwa nguvu, “Kuna lolote mlilokubaliana?” baadaye alitokwa na ulizo.
“Yeah! Tumedhamiria kuo...” Jenerali Namkumba alijibu. Kabla hajahitimisha, alikatishwa kauli na ujio wa Luteni Mwaipeta na Konstebo Babaa. Waliingia mule chumbani kwa mwendo wa mitambao. Hasa crowing.

Nao hawakuwa na hali nzuri ki-afya. Walikuwa na majeraha machache yaliyoruhusu damu kuwatoka pasi na kusahau maumivu. Hasa mgongoni.
“Tumedhamiria kutoroka, kupitia huu upande wa nyuma,” Makamu wa Rais, Lilian alifukuza hoja ya usaili wa afya. Na kuingiza namna watakavyojikomboa.
“Hamna shida. Kila kitu kimeshapangwa?” Luteni Mwaipeta aliuliza.
“Yeah! Na laiti kama musingelitokea, tungeliwaacha.”
“Okay! Tusipoteze muda, tuondokeni.”

Wahusika wa kumbeba Babigamba walimtwaa na kuanza kuondoka. Wengine walifuata nyuma yao. Huku sehemu ya ulinzi wakiongezeka Luteni Mwaipeta, Koplo Namaya na Konstebo Babaa.

Mwendo ulikuwa wa unyapio wenye haraka pale ndani. Walivyofikia uwazi, yaani baada ya kuliacha jengo, walipiga hatua za haraka zaidi ili waupite kwa muda mfupi na kupotelea msituni.

Ile nyumba ilizungukwa na msitu wa miti ya kupanda. Ukiacha zile mita kumi kila upande zilizozungushwa utepe. Ambazo zimepambwa kwa nyasi fupi.

Wananchi walivyowaona, walianza kupiga yowe. Lililowashtua askari, na kuwafanya wazidi kupiga hatua kuelekea walipo. Nao walivyowaona, walijipanga na kuruhusu mashambulizi kuwaelekezea.

ITAENDELEA...

HABARI NJEMA

KITABU CHA RIWAYA YA NENDA SASA KINAPATIKANA RENICS BOOKSHOP TAWI LA MOSHI KWA GHARAMA YA TSH. 10,000/= MAWASILIANO: 0767826134
 
RIWAYA: MKOLONI MZAWA—2
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
SEHEMU YA 24.

Askari wa ulinzi hawakusubiri wapewe amri. Walijiamrisha wenyewe kuwashambulia kina Luteni Mwaipeta nao kujibu pia. Jenerali Namkumba, IGP Lukanga, Luteni Mwaipeta, Koplo Namaya na Konstebo Babaa walijibu mashambulizi huku wakizidi kusonga kurudi nyuma.

Ushambuliaji wao ulikuwa wa zamu; walishambulia kwa makundi. Walijigawa makundi mawili; moja, lilikuwa la Jenerali Namkumba na Konstebo Babaa, la pili, IGP Lukanga, Luteni Mwaipeta na Koplo Namaya.

Hivyo pindi Jenerali Namkumba na Konstebo Babaa wanashambulia, lile la pili lilirudi nyuma kwa kasi. Kina Jenerali Namkumba walivyoacha kushambulia, kundi liongozwalo na IGP Lukanga lilichukua usukani wa kuendeleza mashambulizi wakati Jenerali Namkumba na Konstebo Babaa wakirudi nyuma.

Isivyo bahati, katika mashambulizi hayo daktari alipigwa risasi shingoni na kupoteza maisha. Kwa pamoja walihuzunika. Lakini hawakuwa na namna, walimuacha na wao kuzidi kusonga mbele. Walipotelea msituni. Askari wakiwa kidete nyuma yao.
“Mtaarifu Oc (officer commanding) wa dog alete mbwa haraka sana,” Sacp Chiwila aliamuru. Wajihi ukiwa umejaa ghadhibiko. Jasho likimtiririka mithili ya mchungi anayeswaga ng’ombe uwanda wa wazi, jua kali likimpiga.

Kila kilichozungumzwa na Sacp Chiwila kwa wakati huo kilitekelezwa kwa uharaka sana. Hakuna alilotamka likapingwa. Hivyo dakika chache baadaye, askari wa kikosi cha mbwa waliwasili. Wakiwa na mbwa wanne.

Kabla ya yote wale mbwa walinusishwa vitu kadhaa kwenye kile chumba walichokuwemo kina Ndalama kisha waliachiwa kuongoza msako. Askari wakapita mbwa walimopita.

Makamu wa Rais, Lilian na wenzie waliambaa ambaa na msitu, walivyoumaliza, walikutana na barabara ya lami ambayo hawakufahamu uelekeo wake ni upi.
“Tunashauriana vipi hapa?” Makamu wa Rais, Lilian aliuliza. Wakiwa wamesimama pembezoni mwa barabara kwa mapumziko ya muda. Maana walishaanza kuchoka, nguvu taratibu zikianza kuwaponyoka.

Kuonesha kiasi gani wamechoka, machela aliyolazwa Babigamba waliitua chini.

Hakuna aliyejibu kwa haraka.

***

Miongoni mwa wananchi watazamaji, kuna mmoja alifuatilia tukio hilo kwa umakini zaidi. Askari walivyoanza kupambana na kina Luteni Mwaipeta, yeye aliondoka taratibu eneo hilo. Mithili ya mtu aliyetosheka na ushuhuda alioufanya.

Mwisho wa mwendo wake haukuwa mbali sana kutoka nyuma ya watazamaji. Eneo ambalo miongoni mwa watazamaji waliegesha vyombo vya usafiri. Naye ni mmoja wapo. Aliifuata gari yake-Town hiace, iliyopambwa kwa rangi nyeusi na vioo full tinted. Alivyoingia aliungurumisha injini na kuondoka kwa kasi eneo hilo.

Baada ya mwendo wa mita kadhaa alifunga breki usawa waliopo kina Luteni Mwaipeta pale barabarani. Aliteremka garini na kuwafuata. Wakati huo Makamu wa Rais, Lilian na wenzie walishaanza kujiinua kwa ajili ya kuondoka.
“Nipo kwa ajili ya msaada wenu,” yule mtu alizungumza. Mwanaume; mwenye rika la uzee, akipambwa kwa umbo jembamba, mrefu wastani, rangi iliyosawili ngozi ikiwa ni nyeusi. Alivaa kaunda suti rangi nyeusi.

Makamu wa Rais na wenzake wakatulia na kumsaili.
“Ondoeni hofu juu yangu. Mimi ni mwema kwenu, naomba niwasaidie mupate kukamilisha mlichodhamiria,” aliendelea kuzungumza yule mtu.

Kidogo walimuelewa. Japo hawakukosa hofu.
Cha kufia nini?

Baadaye walikubaliana na yule msamaria mwema. Waliingia ndani ya gari lake safari ikaendelea.

Wakiwa ndani ya gari yule aliyejinasibu kama msamaria mwema alifanya mawasiliano ya simu kwa njia ya ujumbe mfupi na watu fulani. Kina Luteni Mwaipeta hawakufahamu, akili zao zilikuwa bize kufikiria maisha yao yatakuaje mara baada ya msamaria huyo kuhitimisha msaada wake.

Dakika tatu baadaye pale walipoondoka askari wakatia miguu na mbwa wao. Mbwa walibweka kuelekea uelekeo ule ule gari ilipoelekea.

***

Msako mkali uliibuka ghafla kwa watu wenye vyombo vya usafiri kutoka kwa askari wa jeshi la polisi. Askari walitanda barabarani-wa vitengo vyote, na kufanya hali ya hewa kuchafuka kwa watu wenye mioyo miepesi. Hawakuisha kuogopa.

Hakuna gari iliyopita pasi na kupekuliwa katika barabara zote ndani ya mji wa Ngowe. Kwa ufupi, barabara zilifungwa. Check point zilikuwa lukuki kana kwamba wanaotafutwa ndiyo wameshikilia uhai wa watu wengine.

Haukuwa msako mdogo. Ulikuwa mkubwa, ulichosha na kukerehesha wengi waliopekuliwa. Kwa sababu kila mita kadhaa kulikuwa na check point. Heri, ukaguliwapo check point moja unapatiwa uthibitisho wa kupekuliwa. Lakini haikuwa hivyo.

Katika pita pita ile town hiace inayoendeshwa na yule msamaria mwema ilitokeza kwenye moja ya check point umbali mdogo ili aufikie mji. Dereva akiwa hana hili wala lile, alishtuka kumuona askari mbele yake akimpiga mkono na kuonyeshwa uhitaji wa gari yake kuwekwa pembeni.

Awali alishtuka. Mapigo ya moyo yakamwenda kasi ghafla na kuhisi kijasho kikichanua kwenye vinyweleo.

Hakuleta ubishi. Alipunguza mwendo na kuegesha gari upande alioelekezwa. Akiwa kwenye masubirio ya kumngoja askari aliyemsimamisha, alijikuta akivuta pumzi na kuzitua kwa nguvu. Kisha aligeuka nyuma kuangalia mazingira ya garini.

Askari alivyomfikia, aliteremsha kioo usawa wa yeye alipokaa, na kufungua uwanja mdogo wa mazungumzo yaliyopo nje ya hitajio la yule askari.

***

Alikuwa Askofu. Yule aliyewasiliana na Luteni Jenerali Kipozi. Askofu Mwanjabeki, ndiye aliyewapatia msaada kina Luteni Mwaipeta.
“Aaah! Askofu,” yule askari aliita.
“Ndiyo, ni mimi. Mzima?”
“Mzima mzee wangu. Mji umechafuka leo.”
“Kuna nini tena?”
“Hujapata habari? Kuna watu wamejinasibu kuwa ni waasi wamegundulika hapo msitu wa...”

Kabla hajamalizia Askofu Mwanjabeki alimkatisha, “Kwa hiyo wametoroka?”
“Yeah! Sasa hivi tunapambana kufanya msako kuwatafuta.”
“Haya karibu kwa ukaguzi.”

Yule askari alizungukia upande wa pili, Askofu Mwanjabeki alimfungulia mlango akaingia ndani kwa ukaguzi zaidi.

Pindi gari la Askofu Mwanjabeki linakaguliwa lilipita gari la wagonjwa limilikiwayo na Dayosisi ya Nufaiko. Lilipita pasi na kukaguliwa, ijapokuwa walikuwepo askari wengine ukiachilia mbali yule anayekagua.

Upitaji wake ulikuwa wa kasi mno, king’ora kikilia muda wote, kiasi kwamba waliopo pembeni kushuhudia hawakuacha kuwa wenye mshangazo. Walishangazwa na mwendo, huku wakijenga maulizo, mgonjwa aliyopo garini yu’katika hali gani.

Mwisho wa ukaguzi, Askofu Mwanjabeki aliruhusiwa kuendelea na safari.

***

Askofu Mwanjabeki kabla hajasimamishwa kukaguliwa na yule askari, alisimama mara moja mahali kwa ajili ya mabadilishano. Hakutaka aende nao kina Luteni Mwaipeta moja kwa moja kule alikokusudia.

Sehemu waliyosimama, kina Luteni Mwaipeta waliteremka na kuingia gari nyingine safari ikaendelea. Hiyo pia hawakufika nayo, walibadilishwa na kupakizwa kwenye gari lingine. Ndiyo lile gari la wagonjwa.

Hii ndiyo iliwafikisha sehemu husika. Nyumbani kwa Askofu Mwanjabeki. Walipokelewa kwa mikono miwili na wafanyakazi waliowakuta, askofu mwenyewe aliwasili robo saa baadaye.

Awali, walipewa chakula. Walikula, walioga, baadaye walipumzika. Wakati huo Babigamba akifanyiwa harakati za matibabu.

***

Rais Sharabu, Killa na Maua walichanganyikiwa walivyopatiwa taarifa juu ya kile kilichojiri Ngowe. Walipatiwa taarifa hiyo wakiwa Ikulu. Rais Sharabu ndiye aliyeonekana kuchanganyikiwa zaidi ya wote. Ile taarifa hakuhistahimili. Ilimuumiza, na kunyanyasa vilivyo nafsi yake.
“Wamefanikiwa vipi kutoroka?” Rais Sharabu aliuliza.
“Sijafahamishwa mheshimiwa.”
“Nyumba si ilishambuliwa wao wakiwa ndani?”
“Ndiyo.”
“Sasa inawezekanaje kutoka wakiwa hai?”
“Ni jambo linaloshangaza.”
“Wakusudiwa wetu walikuwepo?”
“Kwa kitendo hiki tunashindwa kupata uhakika.”
“Duh!” Rais Sharabu aliguna na kutingisha kichwa.

Baadaye Maua alishauri, “Kama vipi itisha kikao cha Baraza la usalama wa taifa. Kufanya hivyo kunaweza kukupa kile unachohitaji.”
“Kwa namna ipi?”
“Kupitia muonekano wao wa kimwili. Kama walikuwepo, nina hakika watakuwa na alama ambazo zitakupa shauku ya kuwatilia shaka.”
“Killa, unaonaje kuhusu hilo?”
“Ni mbinu mzuri mheshimiwa.”
“Okay! Fanya mpango wa kuwafikishia taarifa wahusika wa hicho kikao. Msisitizo...”
“Ndiyo.”
“Hicho kikao kinafanyika leo hii saa tatu asubuhi.”
“Hamna shida mtukufu Rais,” Killa alisema na kuonyesha utii.

Baada ya kutoa amri hiyo, Rais Sharabu aliwasiliana na mtu mwingine kwa njia ya ujumbe kwenye simu. Kisha alirejea kwenye maongezi na kina Killa.

Saa mbili baadaye wahusika wa Baraza la usalama wa taifa walikutana; Rais Sharabu, Makamu wa Rais, Lilian, Waziri Mkuu na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Muda wote walioketi mboni za Rais Sharabu zilitua kwa Makamu wa Rais, Lilian, Jenerali Namkumba na IGP Lukanga. Muonekano wao ulimpatia shaka, kuwa ile hisia aliyoambiwa na Killa ni sahihi.
“Ninyi watu! Ombeni musiwe,” Rais Sharabu alijisemeza. Taratibu akichezea chezea vidole vyake, mboni kazitumbua pima kumsaili mmoja baada ya mwingine.

Karibu na kikao kuanza, Rais Sharabu alikabidhiwa simu na mlinzi wake wa karibu.
“Kuna ujumbe,” yule mlinzi alimnong’oneza.

Pasi na kukawia Rais Sharabu aliperuzi sehemu kusudiwa, akakutana na ujumbe kutoka kwa yule mtu aliyempatia agizo awali.
“Tumebaini, kuwa nao ni miongoni mwa wahusika ambao walikuwemo kwenye lile jengo. Vipimo vya DNA vimetubainishia hilo,” ulisomeka ujumbe aliotumiwa.

Akiwa amenyong’onyea, Rais Sharabu aliinua uso na kuwatazama kwa jicho kali. Hasira ikimkaba koo mfano wa vibwengo waamuapo kumzubaisha mtu aliye usingizini.

Siku zote alihitaji ushahidi uliotimilika. Ushahidi wa uhakika ili awashughulikie vizuri. Sasa ameshaupata. Mwisho, alitingisha kichwa na kusonya. Msonyo uliomtoka kwa sauti ya juu wastani, ishara kama anawahurumia.

ITAENDELEA...

HABARI NJEMA

KITABU CHA RIWAYA YA NENDA SASA KINAPATIKANA RENICS BOOKSHOP TAWI LA MOSHI KWA GHARAMA YA TSH. 10,000/= MAWASILIANO: 0767826134
 
RIWAYA: MKOLONI MZAWA—2
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
SEHEMU YA 24.

Askari wa ulinzi hawakusubiri wapewe amri. Walijiamrisha wenyewe kuwashambulia kina Luteni Mwaipeta nao kujibu pia. Jenerali Namkumba, IGP Lukanga, Luteni Mwaipeta, Koplo Namaya na Konstebo Babaa walijibu mashambulizi huku wakizidi kusonga kurudi nyuma.

Ushambuliaji wao ulikuwa wa zamu; walishambulia kwa makundi. Walijigawa makundi mawili; moja, lilikuwa la Jenerali Namkumba na Konstebo Babaa, la pili, IGP Lukanga, Luteni Mwaipeta na Koplo Namaya.

Hivyo pindi Jenerali Namkumba na Konstebo Babaa wanashambulia, lile la pili lilirudi nyuma kwa kasi. Kina Jenerali Namkumba walivyoacha kushambulia, kundi liongozwalo na IGP Lukanga lilichukua usukani wa kuendeleza mashambulizi wakati Jenerali Namkumba na Konstebo Babaa wakirudi nyuma.

Isivyo bahati, katika mashambulizi hayo daktari alipigwa risasi shingoni na kupoteza maisha. Kwa pamoja walihuzunika. Lakini hawakuwa na namna, walimuacha na wao kuzidi kusonga mbele. Walipotelea msituni. Askari wakiwa kidete nyuma yao.
“Mtaarifu Oc (officer commanding) wa dog alete mbwa haraka sana,” Sacp Chiwila aliamuru. Wajihi ukiwa umejaa ghadhibiko. Jasho likimtiririka mithili ya mchungi anayeswaga ng’ombe uwanda wa wazi, jua kali likimpiga.

Kila kilichozungumzwa na Sacp Chiwila kwa wakati huo kilitekelezwa kwa uharaka sana. Hakuna alilotamka likapingwa. Hivyo dakika chache baadaye, askari wa kikosi cha mbwa waliwasili. Wakiwa na mbwa wanne.

Kabla ya yote wale mbwa walinusishwa vitu kadhaa kwenye kile chumba walichokuwemo kina Ndalama kisha waliachiwa kuongoza msako. Askari wakapita mbwa walimopita.

Makamu wa Rais, Lilian na wenzie waliambaa ambaa na msitu, walivyoumaliza, walikutana na barabara ya lami ambayo hawakufahamu uelekeo wake ni upi.
“Tunashauriana vipi hapa?” Makamu wa Rais, Lilian aliuliza. Wakiwa wamesimama pembezoni mwa barabara kwa mapumziko ya muda. Maana walishaanza kuchoka, nguvu taratibu zikianza kuwaponyoka.

Kuonesha kiasi gani wamechoka, machela aliyolazwa Babigamba waliitua chini.

Hakuna aliyejibu kwa haraka.

***

Miongoni mwa wananchi watazamaji, kuna mmoja alifuatilia tukio hilo kwa umakini zaidi. Askari walivyoanza kupambana na kina Luteni Mwaipeta, yeye aliondoka taratibu eneo hilo. Mithili ya mtu aliyetosheka na ushuhuda alioufanya.

Mwisho wa mwendo wake haukuwa mbali sana kutoka nyuma ya watazamaji. Eneo ambalo miongoni mwa watazamaji waliegesha vyombo vya usafiri. Naye ni mmoja wapo. Aliifuata gari yake-Town hiace, iliyopambwa kwa rangi nyeusi na vioo full tinted. Alivyoingia aliungurumisha injini na kuondoka kwa kasi eneo hilo.

Baada ya mwendo wa mita kadhaa alifunga breki usawa waliopo kina Luteni Mwaipeta pale barabarani. Aliteremka garini na kuwafuata. Wakati huo Makamu wa Rais, Lilian na wenzie walishaanza kujiinua kwa ajili ya kuondoka.
“Nipo kwa ajili ya msaada wenu,” yule mtu alizungumza. Mwanaume; mwenye rika la uzee, akipambwa kwa umbo jembamba, mrefu wastani, rangi iliyosawili ngozi ikiwa ni nyeusi. Alivaa kaunda suti rangi nyeusi.

Makamu wa Rais na wenzake wakatulia na kumsaili.
“Ondoeni hofu juu yangu. Mimi ni mwema kwenu, naomba niwasaidie mupate kukamilisha mlichodhamiria,” aliendelea kuzungumza yule mtu.

Kidogo walimuelewa. Japo hawakukosa hofu.
Cha kufia nini?

Baadaye walikubaliana na yule msamaria mwema. Waliingia ndani ya gari lake safari ikaendelea.

Wakiwa ndani ya gari yule aliyejinasibu kama msamaria mwema alifanya mawasiliano ya simu kwa njia ya ujumbe mfupi na watu fulani. Kina Luteni Mwaipeta hawakufahamu, akili zao zilikuwa bize kufikiria maisha yao yatakuaje mara baada ya msamaria huyo kuhitimisha msaada wake.

Dakika tatu baadaye pale walipoondoka askari wakatia miguu na mbwa wao. Mbwa walibweka kuelekea uelekeo ule ule gari ilipoelekea.

***

Msako mkali uliibuka ghafla kwa watu wenye vyombo vya usafiri kutoka kwa askari wa jeshi la polisi. Askari walitanda barabarani-wa vitengo vyote, na kufanya hali ya hewa kuchafuka kwa watu wenye mioyo miepesi. Hawakuisha kuogopa.

Hakuna gari iliyopita pasi na kupekuliwa katika barabara zote ndani ya mji wa Ngowe. Kwa ufupi, barabara zilifungwa. Check point zilikuwa lukuki kana kwamba wanaotafutwa ndiyo wameshikilia uhai wa watu wengine.

Haukuwa msako mdogo. Ulikuwa mkubwa, ulichosha na kukerehesha wengi waliopekuliwa. Kwa sababu kila mita kadhaa kulikuwa na check point. Heri, ukaguliwapo check point moja unapatiwa uthibitisho wa kupekuliwa. Lakini haikuwa hivyo.

Katika pita pita ile town hiace inayoendeshwa na yule msamaria mwema ilitokeza kwenye moja ya check point umbali mdogo ili aufikie mji. Dereva akiwa hana hili wala lile, alishtuka kumuona askari mbele yake akimpiga mkono na kuonyeshwa uhitaji wa gari yake kuwekwa pembeni.

Awali alishtuka. Mapigo ya moyo yakamwenda kasi ghafla na kuhisi kijasho kikichanua kwenye vinyweleo.

Hakuleta ubishi. Alipunguza mwendo na kuegesha gari upande alioelekezwa. Akiwa kwenye masubirio ya kumngoja askari aliyemsimamisha, alijikuta akivuta pumzi na kuzitua kwa nguvu. Kisha aligeuka nyuma kuangalia mazingira ya garini.

Askari alivyomfikia, aliteremsha kioo usawa wa yeye alipokaa, na kufungua uwanja mdogo wa mazungumzo yaliyopo nje ya hitajio la yule askari.

***

Alikuwa Askofu. Yule aliyewasiliana na Luteni Jenerali Kipozi. Askofu Mwanjabeki, ndiye aliyewapatia msaada kina Luteni Mwaipeta.
“Aaah! Askofu,” yule askari aliita.
“Ndiyo, ni mimi. Mzima?”
“Mzima mzee wangu. Mji umechafuka leo.”
“Kuna nini tena?”
“Hujapata habari? Kuna watu wamejinasibu kuwa ni waasi wamegundulika hapo msitu wa...”

Kabla hajamalizia Askofu Mwanjabeki alimkatisha, “Kwa hiyo wametoroka?”
“Yeah! Sasa hivi tunapambana kufanya msako kuwatafuta.”
“Haya karibu kwa ukaguzi.”

Yule askari alizungukia upande wa pili, Askofu Mwanjabeki alimfungulia mlango akaingia ndani kwa ukaguzi zaidi.

Pindi gari la Askofu Mwanjabeki linakaguliwa lilipita gari la wagonjwa limilikiwayo na Dayosisi ya Nufaiko. Lilipita pasi na kukaguliwa, ijapokuwa walikuwepo askari wengine ukiachilia mbali yule anayekagua.

Upitaji wake ulikuwa wa kasi mno, king’ora kikilia muda wote, kiasi kwamba waliopo pembeni kushuhudia hawakuacha kuwa wenye mshangazo. Walishangazwa na mwendo, huku wakijenga maulizo, mgonjwa aliyopo garini yu’katika hali gani.

Mwisho wa ukaguzi, Askofu Mwanjabeki aliruhusiwa kuendelea na safari.

***

Askofu Mwanjabeki kabla hajasimamishwa kukaguliwa na yule askari, alisimama mara moja mahali kwa ajili ya mabadilishano. Hakutaka aende nao kina Luteni Mwaipeta moja kwa moja kule alikokusudia.

Sehemu waliyosimama, kina Luteni Mwaipeta waliteremka na kuingia gari nyingine safari ikaendelea. Hiyo pia hawakufika nayo, walibadilishwa na kupakizwa kwenye gari lingine. Ndiyo lile gari la wagonjwa.

Hii ndiyo iliwafikisha sehemu husika. Nyumbani kwa Askofu Mwanjabeki. Walipokelewa kwa mikono miwili na wafanyakazi waliowakuta, askofu mwenyewe aliwasili robo saa baadaye.

Awali, walipewa chakula. Walikula, walioga, baadaye walipumzika. Wakati huo Babigamba akifanyiwa harakati za matibabu.

***

Rais Sharabu, Killa na Maua walichanganyikiwa walivyopatiwa taarifa juu ya kile kilichojiri Ngowe. Walipatiwa taarifa hiyo wakiwa Ikulu. Rais Sharabu ndiye aliyeonekana kuchanganyikiwa zaidi ya wote. Ile taarifa hakuhistahimili. Ilimuumiza, na kunyanyasa vilivyo nafsi yake.
“Wamefanikiwa vipi kutoroka?” Rais Sharabu aliuliza.
“Sijafahamishwa mheshimiwa.”
“Nyumba si ilishambuliwa wao wakiwa ndani?”
“Ndiyo.”
“Sasa inawezekanaje kutoka wakiwa hai?”
“Ni jambo linaloshangaza.”
“Wakusudiwa wetu walikuwepo?”
“Kwa kitendo hiki tunashindwa kupata uhakika.”
“Duh!” Rais Sharabu aliguna na kutingisha kichwa.

Baadaye Maua alishauri, “Kama vipi itisha kikao cha Baraza la usalama wa taifa. Kufanya hivyo kunaweza kukupa kile unachohitaji.”
“Kwa namna ipi?”
“Kupitia muonekano wao wa kimwili. Kama walikuwepo, nina hakika watakuwa na alama ambazo zitakupa shauku ya kuwatilia shaka.”
“Killa, unaonaje kuhusu hilo?”
“Ni mbinu mzuri mheshimiwa.”
“Okay! Fanya mpango wa kuwafikishia taarifa wahusika wa hicho kikao. Msisitizo...”
“Ndiyo.”
“Hicho kikao kinafanyika leo hii saa tatu asubuhi.”
“Hamna shida mtukufu Rais,” Killa alisema na kuonyesha utii.

Baada ya kutoa amri hiyo, Rais Sharabu aliwasiliana na mtu mwingine kwa njia ya ujumbe kwenye simu. Kisha alirejea kwenye maongezi na kina Killa.

Saa mbili baadaye wahusika wa Baraza la usalama wa taifa walikutana; Rais Sharabu, Makamu wa Rais, Lilian, Waziri Mkuu na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Muda wote walioketi mboni za Rais Sharabu zilitua kwa Makamu wa Rais, Lilian, Jenerali Namkumba na IGP Lukanga. Muonekano wao ulimpatia shaka, kuwa ile hisia aliyoambiwa na Killa ni sahihi.
“Ninyi watu! Ombeni musiwe,” Rais Sharabu alijisemeza. Taratibu akichezea chezea vidole vyake, mboni kazitumbua pima kumsaili mmoja baada ya mwingine.

Karibu na kikao kuanza, Rais Sharabu alikabidhiwa simu na mlinzi wake wa karibu.
“Kuna ujumbe,” yule mlinzi alimnong’oneza.

Pasi na kukawia Rais Sharabu aliperuzi sehemu kusudiwa, akakutana na ujumbe kutoka kwa yule mtu aliyempatia agizo awali.
“Tumebaini, kuwa nao ni miongoni mwa wahusika ambao walikuwemo kwenye lile jengo. Vipimo vya DNA vimetubainishia hilo,” ulisomeka ujumbe aliotumiwa.

Akiwa amenyong’onyea, Rais Sharabu aliinua uso na kuwatazama kwa jicho kali. Hasira ikimkaba koo mfano wa vibwengo waamuapo kumzubaisha mtu aliye usingizini.

Siku zote alihitaji ushahidi uliotimilika. Ushahidi wa uhakika ili awashughulikie vizuri. Sasa ameshaupata. Mwisho, alitingisha kichwa na kusonya. Msonyo uliomtoka kwa sauti ya juu wastani, ishara kama anawahurumia.

ITAENDELEA...

HABARI NJEMA

KITABU CHA RIWAYA YA NENDA SASA KINAPATIKANA RENICS BOOKSHOP TAWI LA MOSHI KWA GHARAMA YA TSH. 10,000/= MAWASILIANO: 0767826134
Aisee
 
RIWAYA: MKOLONI MZAWA—2
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
SEHEMU YA 25.

Mtaalamu wa alama za vidole (forensic finger print specialist) ndiye alimtumia Rais Sharabu ule ujumbe. Kutokana na hasira, Rais Sharabu aliamua kughairisha kikao. Na kutoka ukumbini kwa jazba kiasi kwamba wajumbe wengine walibaki na maulizo lukuki waliyokosa kujijibu.

Mwisho wa ondoko lake ulikuwa chumba jirani na kile cha ukumbi wa mikutano. Chumba kilichomwezesha kuona mazingira ya nje ya jengo kwa uzuri. Na ndicho alichokihitaji. Awaone vyema wabaya wake. Pindi wanaondoka, akajipa wasaa wa tafakuri. Namna gani awashughulikie pasi na kufahamika?

Baadaye alimpigia simu Killa, iliyobeba ujumbe wa hitajio la uwepo wake alipo. Killa alitekeleza agizo hilo kwa haraka sana.
“Nimefanikiwa kupata uthibitisho unaowaonyesha wadhaniwa wako ni sehemu ya hujuma,” Rais Sharabu alifungua maongezi.
“Kwa namna ipi?” Killa aliuliza.
“Niliwatuma wataalamu wa finger print. Unashauri niwafanyaje hawa watu?” Raia Sharabu aliuliza, na kumgeukia Killa.
“Dah!”
“Sikia, usiumize sana akili. Tufanye kama tulivyofanya kwa Babigamba. Wafuatiliwe, kisha wasababishiwe ajali.”

***

Rais Sharabu alijisikia mwenye maumivu makali kila awaonapo Makamu wa Rais, Lilian, Jenerali Namkumba na IGP Lukanga. Kilichomuumiza ni kitendo cha kutambua watu hao ndiyo kikwazo cha mipango yake. Hakuisha kuwachukia, kila apatapo kumbukizi kuwahusu.

Moja ya siku ikambidi awaite Killa na Maua wampatie mrejesho wa mipango. Alichoka kuendelea kuwaona mtaani wakiwa wenye buheri wa furaha muda wote.
“Bado munaamini kuna harufu ya kuniwezesha kutimiza matakwa yangu?” Rais Sharabu aliuliza. Walikuwa wameketi kwenye moja ya bustani ndani ya viunga vya Ikulu.
“Yaeh! Mimi naamini,” Maua alijibu.
“Kwa namna ipi?”
“Kwa tukio lililojiri, hakika yangu hali ya Babigamba si shwari. Na yawezekana ameshafariki, lakini taarifa zake zimeshindwa kuvuma. Hivyo utumie mwanya wa kutoonekana kwa Babigamba kujiandalia njia. Wazee wa chama hawawezi kukuangusha.”
“Kama wameweza kuniangusha mwanzo, sasa watashindwaje?”

Ukapita ukimya mfupi.

Maua aliufukuza baadaye, “Amini kuwa Babigamba hayupo. Fanya hiyo fitna. Wagombea mulikuwa wawili pekee, hivyo kama Babigamba hayupo chama kitakupendekeza wewe.”

Killa alidakia, “Sahihi mheshimiwa. Ushauri wa Maua ni mzuri. Jaribu kuufanyia kazi pindi tunaendelea kuwaweka kwenye kilengeo wale watu.”
“Kwa hiyo mnatakaje?”
Maua alijibu, “Itisha kikao cha Kamati kuu.”

Baada ya majadiliano ya kina Rais Sharabu alitekeleza ushauri wao.

Kikao cha dharura cha kamati kuu kiliitishwa. Kila mmoja aliyesikia hakuisha kushangazwa. Ku’nani? Na waliojitokeza kuhoji uhalali wa kikao hicho, walijibiwa, tunaenda kumtathmini mgombea wetu.

Kwa Makamu wa Rais, Lilian na watu wake waliishia kupigwa na butwaa lililowatafakarisha muda mwingi. Lakini walishadhamiria kutoruhusu ushindwa kwa mara nyingine tena.

Siku ya kikao iliyojaa matarajio kwa Rais Sharabu kuwa mwanzo wa kufuta hatua za hujuma, ilienda kinyume. Babigamba alihudhuria kikaoni. Akiwa mwenye afya iliyoimarika na kutoa picha kama hakuna matatizo yaliyompata.

Rais Sharabu akabaki kutatizika.

***

Askofu Mwanjabeki alisaidia kwa kiasi kikubwa matibabu ya Babigamba. Kwani ukiachilia mbali taaluma ya dini, alikuwa daktari pia. Hivyo alishiriki kwa ukaribu kila hatua ambayo Babigamba alipaswa apitie.

Mungu akawa upande wao, ndani ya muda mfupi tu, Babigamba alitengemaa na kurejea kwenye ukawaida wake. Kitendo kilicholeta faraja kwa wana timu. Walifurahia, na kumshukuru vilivyo Askofu Mwanjabeki.
“Wacha tuseme ahsante. Ndiyo malipo pekee kwetu kwako,” Makamu wa Rais, Lilian alisema.
“Nimefanya haya kwa niaba ya wale mnaowapigania,” Askofu Mwanjabeki aliongea. Sauti yake ikiwa imebeba kiasi cha furaha ajisikiacho.

Kutengemaa kwake haukuwa mwisho wa wao kuendelea kujihifadhi nyumbani kwa Askofu Mwanjabeki. Waliendeleza uwepo wao. Na walipatiwa kila aina ya msaada waliouhitaji.

Kutaka kufanya mambo kwa uhuru zaidi, Babigamba aliwasiliana na mkewe akamtoa hofu. Juu ya hilo, alimuomba wahamishe makazi yao kwa muda mpaka pale hitimisho litakapopatikana. Kwani aliamini, wapinzani wanaweza kuitumia familia yake kwa mara nyingine kumshurutisha.

***

Mara baada ya kutoka kikaoni, kile cha Kamati kuu, Babigamba alifuatiliwa na kina Kinyonga nyuma yake. Lakini Luteni Mwaipeta, Koplo Namaya na Konstebo Babaa nao hawakuwa mbali kufuatilia nyendo kwa ajili ya ulinzi zaidi.

Isivyo bahati, wawindaji hawa hawakuonana. Hadi Babigamba anaingia ndani ya ngome ya Askofu Mwanjabeki, si mwenyewe, wala walinzi walioweza kunusa harufu ya nyendo za kina Kinyonga, Mauten na Shida.
“Deal done,” Kinyonga aliongea kwa bashasha, baada ya kumshuhudia Babigamba akiingia nyumbani kwa Askofu Mwanjabeki.

Fika wakafahamu, hayo ndiyo makazi ya Babigamba ndiyo maana haonekani onekani sana mtaani.

Hawakulipooza tukio hilo. Haraka sana liliwasilishwa kwa Killa.

“Tumebahatika kufahamu hifadhi ya Babigamba,” Kinyonga aliongea. Pindi akiwasiliana na Killa kwa njia ya simu. Muda huo walikuwa ndani ya gari. Noah.
“Wapi?” Killa aliuliza.

Kwa umakini wa hali ya juu, Kinyonga alimsimulia Killa hatua kwa hatua hadi mwisho wa ubainisho wao.
“Hongereni sana. Nina hakika mjuba atafurahia. Kwa sasa mnaweza kuendelea na kawaida yenu, nitawarudia baada ya muda kidogo.”
“Sawa mkuu.”

Simu ikakatwa.

Muda mfupi baadaye Killa aliripoti ofisini kwa Rais Sharabu.

“Nipe ripoti,” Rais Sharabu aliongea hata kabla hajaketi kitini.
“Vijana wamefanikiwa,” Killa alijibu mara baada ya kuketi.
“Nini hicho walichofanikiwa?” Rais Sharabu aliuliza na kumtumbulia Killa pima mboni zake. Wajihi ulijaa shauku tele.
“Wamefanikiwa kufahamu makazi ya Babigamba kwa sasa.”
“Wapi? Vipi kuhusu hawa wajinga wengine?”

Killa hakujibu. Alichomoa picha ya mnato kutoka kwenye mfuko wa koti alilovaa na kuiweka juu ya meza. Meza, iliyomtenganisha baina yake na Rais Sharabu.

Rais Sharabu aliisogeza ile picha karibu yake na kuanza kuisaili.

Ilikuwa picha imuonyeshayo Askofu Mwanjabeki.

“Anahusika vipi?” Rais Sharabu aliuliza. Huku kaishikilia ile picha mikononi mwake na kuigeuza geuza.
“Huyo ndiyo mdhamini wa walengwa wetu.”

Rais Sharabu akaikazia kuiangalia ile picha kwa makini kwa mara nyingine tena.

“Kuna uhakika?”
“Sahihi mheshimiwa.”
“Shenzz! Siku zote tunam-beba m-beba kumbe ni panya tu. Anang’ata huku akipuliza ili tusisikie maumivu atuachiayo?”
“Hakika.”
“Sasa sikia.”
“Ndiyo mheshimiwa.”
“Nahitaji aondoke hapa nchini haraka sana. Sitaki kumsikia wala kumuona.”

Killa aliinua na kupiga hatua moja nyuma. Alisimama katikati ya usawa wa ile meza iliyowatenganisha, akapindisha kidogo mgongo na kukumbata viganja vya mikono kifuani.
“Nitatekeleza hilo.”
“Kesi rahisi ya kumuondoa...” Rais Sharabu alisema na kutulia kwa muda.
“Ndiyo mheshimiwa.”

Rais Sharabu alimsaili Killa kwa sekunde kadhaa ndipo aliongea, “Uraia. Mpeni tuhuma ya kutokuwa raia wa Tuleane na aondoke ndani ya saa ishirini na nne kuanzia sasa.”
“Hamna shida mheshimiwa.”

Siku zote kauli za Rais Sharabu zilikuwa kama sheria. Hivyo Killa alitekeleza agizo alilopatiwa kwa kumshirikisha Kamanda wa polisi kanda maalum ya Nufaiko, Sacp Chiwila pamoja na Kamanda wa idara ya uhamiaji mkoa wa Nufaiko. Rasmi tamko likatoka, kuwa Askofu Mwanjabeki si raia wa Tuleane. Na anapaswa kuondoka ndani ya saa zilizoamriwa na Rais Sharabu.

Hilo likatekelezwa na mitutu juu juu. Askofu Mwanjabeki alihamishwa chini ya ulinzi mkali wa askari polisi na vijana wa usalama wa taifa. Alihamishwa pasi na kuhojiwa. Wapi aelekeako? Ni yeye binafsi ndiyo alifahamu.

Baada ya kukamilisha hatua hiyo walihamishia majeshi kwa Babigamba. Magazeti mengi, blogu na tovuti zilikesha kumshambulia kwa kuandika habari mbaya pekee zimuhusuzo. Zingine hazikuwa hata na ukweli.

Rais Sharabu alifanya yote haya ili Babigamba achafuke ndani ya chama kisha nafasi yake apatiwe yeye. Kama hilo halitoshi, vurugu la kampeni lilivyokaribia kuanza likaamshwa fukuto la uasi. Viongozi wanaoshirikiana na watu waliowapachika jina waasi katika lile tukio la Ngowe. Majina ya Makamu wa Rais, Lilian, Jenerali Namkumba na IGP Lukanga yalikuwa kwenye orodha.
“Haina haja ya msamaha, hatua kali zichukuliwe dhidi yao,” Rais Sharabu aliamuru.

ITAENDELEA...

HABARI NJEMA

KITABU CHA RIWAYA YA NENDA SASA KINAPATIKANA RENICS BOOKSHOP TAWI LA MOSHI KWA GHARAMA YA TSH. 10,000/= MAWASILIANO: 0767826134
 
Figisu Figisu hizo ni za kupita tu lzm kieleweke poti
 
RIWAYA: MKOLONI MZAWA—2
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
SEHEMU YA 26.

Rais Sharabu alifanya yote haya ili Babigamba achafuke ndani ya chama kisha nafasi yake apatiwe yeye. Kama hilo halitoshi, vurugu la kampeni lilivyokaribia kuanza likaamshwa fukuto la uasi. Viongozi wanaoshirikiana na watu waliowapachika jina waasi katika lile tukio la Ngowe. Majina ya Makamu wa Rais, Lilian, Jenerali Namkumba na IGP Lukanga yalikuwa kwenye orodha.
“Haina haja ya msamaha, hatua kali zichukuliwe dhidi yao,” Rais Sharabu aliamuru.

***

Ilikuwa ni jioni, Makamu wa Rais, Lilian alivyokutana na washirika wa timu yao. Walikutana kwenye moja ya hoteli katikati ya mji.
“Nadhani sote tumeshafahamu na kujionea liendelealo,” Makamu wa Rais, Lilian alifungua maongezi.
“Tumechafuka vya kutosha,” Ndalama alikazia.
“Juu ya hilo tunahitaji kumuokoa mwenzetu, Luteni Jenerali Kipozi.”
“Hakika,” Jenerali Namkumba alisema na kutingisha kichwa kilichobeba ishara ya msisitizo.
“Kwa hiyo lipi pendekezo?” IGP Lukanga aliuliza.
“Binafsi, nimeonelea tujiuzulu nafasi zetu,” Makamu wa Rais, Lilian alisema. Kauli iliyowashangaza wote.

Baadaye ulipita ukimya wenye fikirio. Kwa pamoja wakisailiana kila baada ya muda fulani.

Siku iliyofuata maamuzi yao yaliwekwa wazi. Jackson ndiye aliyefanya kazi hiyo. Jambo lililoibua mpasuko na taharuki ambayo hawakuhitaji ijibainishe. Wanachama wa Chama cha Chautu nao wakaanza kutengeneza makundi, lakini awamu hii Babigamba alijizolea mamia ya wanachama. Wengi walimuunga mkono wakiamini kuwa ananyanyaswa.

Hatimaye baada ya kujiuzulu kwa Makamu wa Rais, Lilian na watu wake walikamatwa na kufunguliwa mashtaka. Mashtaka ambayo yalipelekwa puta, wakati huo huo, ndani ya siku kumi na nne Rais Sharabu aliteua watu wengine wa kushikilia nafasi zao.

Mtu ambaye aliteuliwa kuwa Makamu wa Rais, jina lake liliwasilishwa Bungeni na kupigiwa kura. Wingi wa wabunge wa kura ya ndiyo ilithibisha uteuzi wake.
***

Luteni Mwaipeta aliongoza timu kwa mara nyingine kufuatilia gari la kina Kinyonga lililokuwa linachanja mbuga kumuhamisha Luteni Jenerali Kipozi. Kutoka kwenye yale makazi yao ya uficho kuelekea ofisi za idara ya usalama wa taifa.

Luteni Mwaipeta na wenzake walikuwa ndani ya gari ndogo aina ya Toyota Premio.

Baada ya kuifuatilia kwa umbali wa takribani kilomita moja, walilipita gari walilopo kina Kinyonga na kuwawekea kizuizi kwa mbele. Mauten aliyekuwa anaendesha, akafunga breki ghafla.
“Kuna nini?” Kinyonga aliuliza. Huku akimwangazia Mauten, aliyeonekana kuwa mwenye hofu kiasi cha jasho kuanza kumtoka.
“Kuna jamaa wametu-block hapo mbele.”
Kinyonga akatupa mboni zake alipoelekezwa. Akajaa hasira, iliyomshinikiza kufungua mlango kwa nguvu na kuteremka garini moja ya mkono kakamatia bunduki kaelekezea mtutu juu.

Likawa kosa.

Kwani Koplo Namaya aliyekuwa tayari ameshateremka ndani ya gari na kupiga goti nyuma ya mlango, aliiketisha bunduki kwenye nyama ya bega na kuruhusu mtupo mmoja wa risasi katika paji la uso wa Kinyonga. Kinyonga akaanguka kama tikiti lililooza. Bunduki aliitupia kando na kupoteza maisha.

Kuona hivyo, Mauten alirudisha gari nyuma ili abadili uelekeo. Luteni Mwaipeta akawahi wakati gari ikiwa hatua za mwisho za kumalizia mageuko warudi watokako. Aliteremka ndani ya gari haraka na kufanya mitupo kadhaa ya risasi. Ilienda kukita kwenye tairi, nyingine, ilimpata Mauten kwenye bega.
“Wanaweza wakatutoka kimasihara hawa,” Konstebo Babaa alisema. Naye akiwa ameteremka garini na kuoanisha vilengeo.
“Tusiruhusu hilo. Hawapaswi kutoka salama. Kingine, ni lazima tumuokoe mtu wetu. Luteni Jenerali Kipozi lazima arejee kwenye mikono salama,” Luteni Mwaipeta aliongea. Akibadili uelekeo wa mkao. Alitoka maeneo ya garini na kukimbilia kichakani. Huko aliinyemelea gari waliyopo kina Mauten.

Hali ilizidi kuwa mbaya kwa kina Mauten na Shida. Mauten ilimtoka damu nyingi sana iliyopelekea kadri sekunde zilivyozidi kusonga mbele nguvu kumpungua.
“Shida. Sh...ida,” Mauten aliita kwa utetemeshi na sauti nyongefu. Akiwa amejilaza kitini pasi na kujiwekea tahadhari ya usalama wake. Alishakata tamaa, na kukubali lolote litakalojitokeza ni sawa tu.
“Una hali gani?” Shida aliuliza. Katumbua mboni zake pima kusaili yaendeleayo nje.
“Hali yangu ni mbaya sana. Mchukue huyo mshenzi muondoke hapa haraka iwezekanavyo.”
“Nitakuachaje?”
“Nasema ondoka na huyo kima. Umuhimu wangu kundini hauna thamani tena, kwani hata nikitoka sitofika mbali kabla ya kuaga dunia.”

Shida akamsaili Mauten kwa muda baadaye alimwangazia Luteni Jenerali Kipozi ambaye alikuwa anasikiliza mazungumzo yao.
“Ni lazima tuondoke wote,” Shida alisema. Akinyanyuka alipoketi na kumfuata Luteni Jenerali Kipozi. Alimuinua na kumkaba kabari ya shingo, mkono mwingine alimuelekezea kichwani.
“Mauten, nifuate,” Shida aliendelea kuongea, huku akitoka naye Luteni Jenerali Kipozi nje.

Wakati huo Luteni Jenerali Kipozi alifungwa pingu mikononi na miguuni, kiasi cha kushindwa kutembea vyema. Akawa anakokotwa.

Kitendo kilichofanywa na Shida kilitoa ishara hapaswi kushambuliwa. Na endapo watakaidi agizo lake atafanya maamuzi magumu ya kumshambulia Luteni Jenerali Kipozi. Hivyo alimtumia kama kinga ya kujiondoa eneo hilo.

Mauten naye alitekeleza kauli ya Shida. Alijiondoa pale sitini kwa tabu sana, na kutoka nje. Huko aliketi nyuma ya Shida, aliyeendelea kumkamatia Luteni Jenerali Kipozi kwa mtindo wa kumtanguliza mbele.
“Teremsheni bunduki chini, la sivyo nam-maliza mbweha wenu,” Shida alimaka. Taratibu wakipiga hatua za kurudi nyuma.

Koplo Namaya na Konstebo Babaa wakaishiwa pozi.

“Nini tena hii!” Koplo Namaya alisema. Kwa sauti nyongefu yenye kukata tamaa.
“Tumeshapoteza,” Konstebo Babaa alikazia.
“Lakini inawezekanaje? Hatuwezi kufanya namna yoyote kweli?”
“Nikuulize wewe.”
“Oooh! Shiit,” Koplo Namaya alimaka na kumwangazia Shida jinsi anavyoendelea kuwatoka.
“Tumepoteza,” Konstebo Babaa alirudia kuongea kauli ya awali, naye akimtupia mboni zake Shida.
“Hakika. Anaweza kututoroka, na tusivyokuwa makini, atamshambulia Luteni Jenerali Kipozi ndipo atoroke.”

Kule alipokuwa anaelekea Shida kulikuwa na gari ikitoka nyuma yao. Gari ndogo, aina ya Toyota Brevis. Mauten aliipunga mkono, dereva akatii. Kwa kupunguza mwendo na kusimama alipowafikia.

“Wamesimamisha gari, wanataka kuingia,” Konstebo Babaa aliongea. Huku akiwashuhudia maadui zao kwa tabu sana, kutokana na kizuizi cha gari. Kilimsababishia asione mazingira ya nyuma kwa usahihi. Koplo Namaya hakuweza kuona kabisa.

Hawakuremba. Gari liliposimama walifungua mlango na kuanza taratibu za kuingia ndani. Lakini Luteni Mwaipeta kule alipokimbilia, tayari alisham-bamba Shida kwenye vilengeo.

Kitendo cha Shida kugeuka nyuma, ili amtangulize Luteni Jenerali Kipozi kuingia ndani ya gari, Luteni Mwaipeta alitumia vyema nafasi hiyo kuruhusu mtupo wa risasi. Ikampata Shida kisogoni na kukata safari yake duniani.

Mauten akajaa hasira, iliyomshinikiza kupeleka moja ya mkono wake kuchomoa bastola alipoihifadhi, hata kabla hajaimiliki vyema, Luteni Mwaipeta aliruhusu mtupo mwingine kufuata. Risasi ikampata kwenye paji la uso na kuzima uwepo wake duniani.

Cha kufia nini, dereva wa lile gari, aliteremka garini na kutimua mbio kichakani.

Ushwari ulivyotapakaa kiasi, Luteni Mwaipeta alijichomoa kichani na kupiga hatua hadi kwenye lile gari. Alimchomoa Luteni Jenerali Kipozi, alimfungua zile pingu, kisha aliondoka naye hadi walipo wenzake.

Koplo Namaya na Konstebo Babaa wakashusha pumzi lililosheheni tabasamu.

Baadaye waliondoka. Moja kwa moja hospitalini na Luteni Jenerali Kipozi akaanza kupatiwa matibabu. Alivyotengemaa, alipatiwa mkasa mzima wa nini kilichojiri kwa kipindi chote ambacho hakuwepo.
“Kuna mwanaharakati anaitwa Jenerali Ulimwengu nchini Tanzania, alishawahi kusema, nanukuu, moja wapo ya matatizo makubwa tuliyonayo ni waliopo madarakani kudhani madaraka yanawapa akili na busara kubwa kuliko wenzao wasio madarakani. Ni kama vile kuna imani kwamba unapokuwa madarakani huna lolote la kujifunza kwa watu wasio madarakani. Mwisho wa kunukuu.”
Luteni Mwaipeta alidakia, “Nadhani ndicho kinachotokea nchini kwetu kwa sasa.”
“Naam! Kwa asilimia zote.”

***

Wajihi ulijaa simanzi kwa Rais Sharabu, Killa na Maua. Taarifa za vifo vya watu wao ziliwaumiza. Lakini kutoroshwa Luteni Jenerali Kipozi, kuliwaumiza zaidi.
“Ina maana tumeshindwa?” Rais Sharabu aliuliza. Sauti ikiwa nyongefu.

Hakuna aliyejibu. Waulizwa walitazama chini kwa aibu, walivyoinua nyuso zao, walimtazama Rais Sharabu kwa ishara ya kutaka kupewa maagizo nini wafanye.
“Akili yangu imefikia ukomo wa kufikiri. Nipo radhi kumwachia Babigamba aendeleze harakati zake. Lakini...”

Killa na Maua waliitikia kwa pamoja, “Ndiyo mheshimiwa.”
“Sitaki aendeleze kwa amani.”
“Una maanisha nini?”

Badala ya kujibu, Rais Sharabu alichomoa bahasha ndogo yenye rangi ya khaki kutoka kwenye mfuko wa ndani wa koti la suti alilovaa na kuitua mezani. Mkao walioketi, katikati yao kulikuwa na meza. Killa aliitwaa ile bahasha akaifungua. Alikuta picha moja ya mnato ndani. Aliichomoa, akashtuka kwanza, alivyoitambua sura ya muhusika.

Maua naye vivyo hivyo. Alishangazwa na ile picha. Kwa pamoja, wakainua nyuso kumtazama Rais Sharabu.

Rais Sharabu alitingisha kichwa ishara ya msisitizo. Baadaye alitokwa na kauli, “Ni mtu muhimu kwa upande wangu kwa sasa. Namuhitaji, ili nizibe matundu ya machungu niliyonayo. Lakini, haipaswi kufahamika kama mimi nipo nyuma ya mpango huo.”

Killa na Maua wakarudia kuiangalia ile picha kwa mara nyingine.

ITAENDELEA...
 
RIWAYA: MKOLONI MZAWA—2
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
SEHEMU YA 26.

Rais Sharabu alifanya yote haya ili Babigamba achafuke ndani ya chama kisha nafasi yake apatiwe yeye. Kama hilo halitoshi, vurugu la kampeni lilivyokaribia kuanza likaamshwa fukuto la uasi. Viongozi wanaoshirikiana na watu waliowapachika jina waasi katika lile tukio la Ngowe. Majina ya Makamu wa Rais, Lilian, Jenerali Namkumba na IGP Lukanga yalikuwa kwenye orodha.
“Haina haja ya msamaha, hatua kali zichukuliwe dhidi yao,” Rais Sharabu aliamuru.

***

Ilikuwa ni jioni, Makamu wa Rais, Lilian alivyokutana na washirika wa timu yao. Walikutana kwenye moja ya hoteli katikati ya mji.
“Nadhani sote tumeshafahamu na kujionea liendelealo,” Makamu wa Rais, Lilian alifungua maongezi.
“Tumechafuka vya kutosha,” Ndalama alikazia.
“Juu ya hilo tunahitaji kumuokoa mwenzetu, Luteni Jenerali Kipozi.”
“Hakika,” Jenerali Namkumba alisema na kutingisha kichwa kilichobeba ishara ya msisitizo.
“Kwa hiyo lipi pendekezo?” IGP Lukanga aliuliza.
“Binafsi, nimeonelea tujiuzulu nafasi zetu,” Makamu wa Rais, Lilian alisema. Kauli iliyowashangaza wote.

Baadaye ulipita ukimya wenye fikirio. Kwa pamoja wakisailiana kila baada ya muda fulani.

Siku iliyofuata maamuzi yao yaliwekwa wazi. Jackson ndiye aliyefanya kazi hiyo. Jambo lililoibua mpasuko na taharuki ambayo hawakuhitaji ijibainishe. Wanachama wa Chama cha Chautu nao wakaanza kutengeneza makundi, lakini awamu hii Babigamba alijizolea mamia ya wanachama. Wengi walimuunga mkono wakiamini kuwa ananyanyaswa.

Hatimaye baada ya kujiuzulu kwa Makamu wa Rais, Lilian na watu wake walikamatwa na kufunguliwa mashtaka. Mashtaka ambayo yalipelekwa puta, wakati huo huo, ndani ya siku kumi na nne Rais Sharabu aliteua watu wengine wa kushikilia nafasi zao.

Mtu ambaye aliteuliwa kuwa Makamu wa Rais, jina lake liliwasilishwa Bungeni na kupigiwa kura. Wingi wa wabunge wa kura ya ndiyo ilithibisha uteuzi wake.
***

Luteni Mwaipeta aliongoza timu kwa mara nyingine kufuatilia gari la kina Kinyonga lililokuwa linachanja mbuga kumuhamisha Luteni Jenerali Kipozi. Kutoka kwenye yale makazi yao ya uficho kuelekea ofisi za idara ya usalama wa taifa.

Luteni Mwaipeta na wenzake walikuwa ndani ya gari ndogo aina ya Toyota Premio.

Baada ya kuifuatilia kwa umbali wa takribani kilomita moja, walilipita gari walilopo kina Kinyonga na kuwawekea kizuizi kwa mbele. Mauten aliyekuwa anaendesha, akafunga breki ghafla.
“Kuna nini?” Kinyonga aliuliza. Huku akimwangazia Mauten, aliyeonekana kuwa mwenye hofu kiasi cha jasho kuanza kumtoka.
“Kuna jamaa wametu-block hapo mbele.”
Kinyonga akatupa mboni zake alipoelekezwa. Akajaa hasira, iliyomshinikiza kufungua mlango kwa nguvu na kuteremka garini moja ya mkono kakamatia bunduki kaelekezea mtutu juu.

Likawa kosa.

Kwani Koplo Namaya aliyekuwa tayari ameshateremka ndani ya gari na kupiga goti nyuma ya mlango, aliiketisha bunduki kwenye nyama ya bega na kuruhusu mtupo mmoja wa risasi katika paji la uso wa Kinyonga. Kinyonga akaanguka kama tikiti lililooza. Bunduki aliitupia kando na kupoteza maisha.

Kuona hivyo, Mauten alirudisha gari nyuma ili abadili uelekeo. Luteni Mwaipeta akawahi wakati gari ikiwa hatua za mwisho za kumalizia mageuko warudi watokako. Aliteremka ndani ya gari haraka na kufanya mitupo kadhaa ya risasi. Ilienda kukita kwenye tairi, nyingine, ilimpata Mauten kwenye bega.
“Wanaweza wakatutoka kimasihara hawa,” Konstebo Babaa alisema. Naye akiwa ameteremka garini na kuoanisha vilengeo.
“Tusiruhusu hilo. Hawapaswi kutoka salama. Kingine, ni lazima tumuokoe mtu wetu. Luteni Jenerali Kipozi lazima arejee kwenye mikono salama,” Luteni Mwaipeta aliongea. Akibadili uelekeo wa mkao. Alitoka maeneo ya garini na kukimbilia kichakani. Huko aliinyemelea gari waliyopo kina Mauten.

Hali ilizidi kuwa mbaya kwa kina Mauten na Shida. Mauten ilimtoka damu nyingi sana iliyopelekea kadri sekunde zilivyozidi kusonga mbele nguvu kumpungua.
“Shida. Sh...ida,” Mauten aliita kwa utetemeshi na sauti nyongefu. Akiwa amejilaza kitini pasi na kujiwekea tahadhari ya usalama wake. Alishakata tamaa, na kukubali lolote litakalojitokeza ni sawa tu.
“Una hali gani?” Shida aliuliza. Katumbua mboni zake pima kusaili yaendeleayo nje.
“Hali yangu ni mbaya sana. Mchukue huyo mshenzi muondoke hapa haraka iwezekanavyo.”
“Nitakuachaje?”
“Nasema ondoka na huyo kima. Umuhimu wangu kundini hauna thamani tena, kwani hata nikitoka sitofika mbali kabla ya kuaga dunia.”

Shida akamsaili Mauten kwa muda baadaye alimwangazia Luteni Jenerali Kipozi ambaye alikuwa anasikiliza mazungumzo yao.
“Ni lazima tuondoke wote,” Shida alisema. Akinyanyuka alipoketi na kumfuata Luteni Jenerali Kipozi. Alimuinua na kumkaba kabari ya shingo, mkono mwingine alimuelekezea kichwani.
“Mauten, nifuate,” Shida aliendelea kuongea, huku akitoka naye Luteni Jenerali Kipozi nje.

Wakati huo Luteni Jenerali Kipozi alifungwa pingu mikononi na miguuni, kiasi cha kushindwa kutembea vyema. Akawa anakokotwa.

Kitendo kilichofanywa na Shida kilitoa ishara hapaswi kushambuliwa. Na endapo watakaidi agizo lake atafanya maamuzi magumu ya kumshambulia Luteni Jenerali Kipozi. Hivyo alimtumia kama kinga ya kujiondoa eneo hilo.

Mauten naye alitekeleza kauli ya Shida. Alijiondoa pale sitini kwa tabu sana, na kutoka nje. Huko aliketi nyuma ya Shida, aliyeendelea kumkamatia Luteni Jenerali Kipozi kwa mtindo wa kumtanguliza mbele.
“Teremsheni bunduki chini, la sivyo nam-maliza mbweha wenu,” Shida alimaka. Taratibu wakipiga hatua za kurudi nyuma.

Koplo Namaya na Konstebo Babaa wakaishiwa pozi.

“Nini tena hii!” Koplo Namaya alisema. Kwa sauti nyongefu yenye kukata tamaa.
“Tumeshapoteza,” Konstebo Babaa alikazia.
“Lakini inawezekanaje? Hatuwezi kufanya namna yoyote kweli?”
“Nikuulize wewe.”
“Oooh! Shiit,” Koplo Namaya alimaka na kumwangazia Shida jinsi anavyoendelea kuwatoka.
“Tumepoteza,” Konstebo Babaa alirudia kuongea kauli ya awali, naye akimtupia mboni zake Shida.
“Hakika. Anaweza kututoroka, na tusivyokuwa makini, atamshambulia Luteni Jenerali Kipozi ndipo atoroke.”

Kule alipokuwa anaelekea Shida kulikuwa na gari ikitoka nyuma yao. Gari ndogo, aina ya Toyota Brevis. Mauten aliipunga mkono, dereva akatii. Kwa kupunguza mwendo na kusimama alipowafikia.

“Wamesimamisha gari, wanataka kuingia,” Konstebo Babaa aliongea. Huku akiwashuhudia maadui zao kwa tabu sana, kutokana na kizuizi cha gari. Kilimsababishia asione mazingira ya nyuma kwa usahihi. Koplo Namaya hakuweza kuona kabisa.

Hawakuremba. Gari liliposimama walifungua mlango na kuanza taratibu za kuingia ndani. Lakini Luteni Mwaipeta kule alipokimbilia, tayari alisham-bamba Shida kwenye vilengeo.

Kitendo cha Shida kugeuka nyuma, ili amtangulize Luteni Jenerali Kipozi kuingia ndani ya gari, Luteni Mwaipeta alitumia vyema nafasi hiyo kuruhusu mtupo wa risasi. Ikampata Shida kisogoni na kukata safari yake duniani.

Mauten akajaa hasira, iliyomshinikiza kupeleka moja ya mkono wake kuchomoa bastola alipoihifadhi, hata kabla hajaimiliki vyema, Luteni Mwaipeta aliruhusu mtupo mwingine kufuata. Risasi ikampata kwenye paji la uso na kuzima uwepo wake duniani.

Cha kufia nini, dereva wa lile gari, aliteremka garini na kutimua mbio kichakani.

Ushwari ulivyotapakaa kiasi, Luteni Mwaipeta alijichomoa kichani na kupiga hatua hadi kwenye lile gari. Alimchomoa Luteni Jenerali Kipozi, alimfungua zile pingu, kisha aliondoka naye hadi walipo wenzake.

Koplo Namaya na Konstebo Babaa wakashusha pumzi lililosheheni tabasamu.

Baadaye waliondoka. Moja kwa moja hospitalini na Luteni Jenerali Kipozi akaanza kupatiwa matibabu. Alivyotengemaa, alipatiwa mkasa mzima wa nini kilichojiri kwa kipindi chote ambacho hakuwepo.
“Kuna mwanaharakati anaitwa Jenerali Ulimwengu nchini Tanzania, alishawahi kusema, nanukuu, moja wapo ya matatizo makubwa tuliyonayo ni waliopo madarakani kudhani madaraka yanawapa akili na busara kubwa kuliko wenzao wasio madarakani. Ni kama vile kuna imani kwamba unapokuwa madarakani huna lolote la kujifunza kwa watu wasio madarakani. Mwisho wa kunukuu.”
Luteni Mwaipeta alidakia, “Nadhani ndicho kinachotokea nchini kwetu kwa sasa.”
“Naam! Kwa asilimia zote.”

***

Wajihi ulijaa simanzi kwa Rais Sharabu, Killa na Maua. Taarifa za vifo vya watu wao ziliwaumiza. Lakini kutoroshwa Luteni Jenerali Kipozi, kuliwaumiza zaidi.
“Ina maana tumeshindwa?” Rais Sharabu aliuliza. Sauti ikiwa nyongefu.

Hakuna aliyejibu. Waulizwa walitazama chini kwa aibu, walivyoinua nyuso zao, walimtazama Rais Sharabu kwa ishara ya kutaka kupewa maagizo nini wafanye.
“Akili yangu imefikia ukomo wa kufikiri. Nipo radhi kumwachia Babigamba aendeleze harakati zake. Lakini...”

Killa na Maua waliitikia kwa pamoja, “Ndiyo mheshimiwa.”
“Sitaki aendeleze kwa amani.”
“Una maanisha nini?”

Badala ya kujibu, Rais Sharabu alichomoa bahasha ndogo yenye rangi ya khaki kutoka kwenye mfuko wa ndani wa koti la suti alilovaa na kuitua mezani. Mkao walioketi, katikati yao kulikuwa na meza. Killa aliitwaa ile bahasha akaifungua. Alikuta picha moja ya mnato ndani. Aliichomoa, akashtuka kwanza, alivyoitambua sura ya muhusika.

Maua naye vivyo hivyo. Alishangazwa na ile picha. Kwa pamoja, wakainua nyuso kumtazama Rais Sharabu.

Rais Sharabu alitingisha kichwa ishara ya msisitizo. Baadaye alitokwa na kauli, “Ni mtu muhimu kwa upande wangu kwa sasa. Namuhitaji, ili nizibe matundu ya machungu niliyonayo. Lakini, haipaswi kufahamika kama mimi nipo nyuma ya mpango huo.”

Killa na Maua wakarudia kuiangalia ile picha kwa mara nyingine.

ITAENDELEA...
Ni dhahma
 
RIWAYA: MKOLONI MZAWA—2
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
SEHEMU YA 27.

IMEPITA miaka mitatu na miezi tisa, tangu ahukumiwe kifungo cha maisha jela kwa kosa la kufanya mauaji ya kukusudia ya halaiki waliyopo kwenye maandamano jijini Nufaiko. Mazingira ya magereza yakambadilisha, kwa kupoteza muonekano wa sura na umbo kwa ujumla. Hakuwa yule aliyezoeleka kuonekana machoni mwa watu wengi. Brigedia Jenerali Mstaafu Bakari Kiboko.

Mkasa ulioibua kisa cha kwenda gerezani ni mahusiano. Mahusiano aliyoyaanzisha na kigogo mmoja wa wilaya. Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Butu. Binti, mwali, m-dada akadiriwaye miaka thelathini na nne. Afahamikaye kwa jina la Siwema Ndomondo.

Hisia zake kwa binti huyu zilimponza. Kwani aliingilia kati penzi la pembeni la mtawala wa taifa lao, Rais Sharabu. Alionywa, lakini hakuwa radhi kuonyeka. Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko aliweka kibri, kilichopelekea manyanyaso mwisho wa siku. Alipata manyanyaso kwenye familia, akapata manyanyaso kazini. Ya kazini yakaleta chuki, iliyomshikiniza kustaafu jeshi kwa hiyari.

Alistaafu, huku akiwa na kisasi dhidi ya Rais Sharabu na serikali yake kwa ujumla. Kwa kifupi, penzi lilimjutisha. Penzi lilimfanya afilisike na kumpotezea heshima mtaani.

Ilikuwa ijumaa, siku moja nyuma kabla ya kufikia siku ya uchaguzi mkuu wa Tuleane. Mazingira ya gereza kuu la Nufaiko yalibadilika. Siku hiyo kulikuwa na ulinzi mkali wa askari wa jeshi la Magereza kuzunguka viunga mbalimbali. Palikuwa na kikao cha maafisa waandamizi kutoka Makao Makuu ya jeshi hilo na wengine kutoka pale Magereza.
“Nadhani mulipokea wito kutoka makao makuu...” kiongozi wa kile kikao alisema.

Waandamizi kutoka pale magereza walijibu kwa kutingisha kichwa; juu-chini.

“Hivyo atasafirishwa mchana wa leo hii. Mkuu wa gereza, andaa utaratibu mapema, ili huyu mtu awasilishwe kwa wakati katika lile gereza lingine.”

Mkuu wa gereza aliinuka alipoketi, alipiga saluti na kutokwa na kauli, “Hamna shida afande. Tumeshafikia hatua ya mwisho ya maandalizi yetu. Nakuhakikishia, kufikia mchana wa leo, saa saba, tutakuwa tumeianza safari.” Akaketi.
“Musipoteze miadi.”

Kikao kikahitimishwa.

Baadaye wale maafisa waandamizi kutoka makao makuu waliondoka. Maafisa waandamizi wa pale pale magereza wakaanza kuwajibika juu ya kile kilichokuwa kinajadiliwa kikaoni.

Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko alipaswa kuhamishwa gereza.

***

Saa saba mchana ilivyowadia tayari Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko alitolewa gerezani na kupakizwa ndani ya gari, basi. Ambalo hutumika mara kwa mara kusafirisha wafungwa. Zaidi yake, kulikuwa na askari wanne kutoka kitengo maalumu cha kutuliza ghasia magerezani, pamoja na dereva.

Achilia mbali askari hao, kulikuwa na magari manne ya usindikizaji; mbele mawili, nyuma mawili, yote yakiwa yamesheheni askari wa ulinzi, waliokamatia bunduki mbalimbali za kivita. Na kufanya jumla ya msafara wa magari matano.

Saa 7:15 mchana safari ilianza, kwa mwendo kasi uliosafishiwa njia na ving’ora. Kila mmoja akimuomba Mwenyezi Mungu, wawe na mwisho mwema wa safari yao.

Ilikuwa ni safari yenye kutumia kilomita mia nne, kutoka gereza kuu Nufaiko hadi kufikia ukomo, gereza kuu Liamba. Gereza lililoaminika na kusifika kuwa ndilo gereza pekee gumu nchini Tuleane. Baada ya mwendo wa takribani nusu saa, waliuacha mkoa wa Nufaiko na kuingia mkoa wa Ndwika, hata kabla hawajaifikia Maswera, msafara ukavamiwa.

Ulivamiwa na maharamia, waliojidhatiti ki-mashambulizi ya kutumia bunduki.

“Tumevamiwa. Take cover, take cover,” mmoja kati ya askari magereza aliwaamrisha wenzie. Waliteremka kwenye magari na kutafuta maficho yatakayowasaidia dhidi ya wapinzani wao. Ambao walikuwa wanne tu.

Namna walivyojipanga wavamizi iliwarahisishia kupeleka moto mkali kwa maadui zao. Waliwashambulia wale askari magereza utadhani hawana mafunzo yoyote ya kimedani. Ndani ya dakika mbili tu, waliwamaliza wote ambao walikuwemo kwenye gari za usindikizaji. Wakasalia wale wa kwenye basi.

Kabla hawajateremka, walimsaili kwanza Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko pale alipofungwa. Naye aliwarudishia jicho la namna hiyo hiyo ambalo wao walipata kumtolea. Ki-ujumla walishangaana. Nini sababu ya tukio hilo kutokea?

Pasi na papara, ijapokuwa walikuwa wenye hofu tele, wale askari walipiga hatua hadi mlangoni ikiwa njia ya kujiokoa kwa upande wao.

Likawa kosa.

Kwani muda huo huo, wavamizi wawili walitoka kwenye pointi zao na kusogea hadi usawa wa mlango. Wakatega kilipuzi na kusogea pembeni.

Kule pembeni hawakukaa kizembe. Walikaa mkao wa uvamizi mara tu kilipulizi kitakavyolipuka. Ikawa hivyo. Haikuchukua muda mrefu, ulitokea mlipuko mdogo ulioambatana na kishindo kuelekea ndani ya gari. Pasi na kusahau moshi.

Wavamizi walitumia nafasi hiyo kuingia ndani, na walivyokuwa makini, hawakuwaacha wale askari magereza wajitafutie pumzi kutokana na ule moshi. Waliwawasha chuma, baadaye walimfungua Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko pale alipofungwa, wakatoka naye nje.

Moja kwa moja walienda kumpakiza garini mwao. Ambayo waliiegesha mita chache kutoka eneo la mapambano.
“Mpe ulinzi. Asikukimbie, sisi tunaenda kusafisha eneo la tukio,” mvamizi mmoja wapo alisema. Akimwambia mwenzie aliyeketi nyuma ya usukani.
“Hamna shida mkuu, nipo makini, hivyo hawezi kunitoka kizembe.”

Wavamizi watatu wakarejea eneo la tukio.

Usafi walioufanya eneo la tukio ni kuondoa miili ya wafu. Waliibeba na kutupia maporomokoni, walifuatia kuyasukumizia magari na kurusha makombora kadhaa kuyaelekezea.

Walivyojiridhisha pako shwari walielekea lilipo gari lao, dereva aliungurumisha injini na kuondoka.

Muda mchache baadaye, ulioruhusu kusambaa kwa habari za tukio hilo, kisa cha tukio kikageuzwa. Kila chombo cha habari kilitangaza kuwa msafara huo umepinduka na kusererekea maporomokoni. Huko kilifuatia kitendo cha kulipuka. Wahusika wa uvamizi waliratibu hili kwa umakini wa hali ya juu, hawakutoa nafasi ya aina yoyote ya shaka.

Uhalisia wa tukio haukuelezwa, ukizingatia muda wa tukio hakukuwa na pita pita za vyombo vingine vya usafiri. Viluzuiliwa na askari wa usalama barabarani maeneo ya mjini, kwa kisingizio cha kuepusha usumbufu kwa msafara husika.

***

Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko alifikishwa kwenye jengo la kifahari ndani ya jiji la Nufaiko maeneo ya Bondeni. Hakuisha kuwa mwenye mshangao, na maulizo mengi aliyoshindwa kuyapatia ufumbuzi, lakini kamwe hakukenua kingo za mdomo kuwatupia swali wale wavamizi.

Klichomfanya ashindwe kuwauliza alifahamu, watu hao sio wabaya kwa upande wake. Kwani laiti kama wangelikuwa wabaya, wasingelimuokoa na kuendelea kumfanya aishi. Kama hiyo haitoshi, wavamizi hawakumsemesha jambo lolote toka mwanzo wa safari hadi hapo walipofikia.

Muendelezo wa imani ya kuwa watu hao sio wabaya, walimpatia huduma nzuri ya malazi. Huduma iliyomfanya ang’ae na kuonekana kama nuru gizani.
“Jiandae ki-akili, kesho kuna mtu utaenda kuonana naye,” kiongozi wa kundi la wavamizi aliongea. Wakati huo Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko akiwa amestopisha hatua alizokuwa anazipiga kuelekea chumbani kulala. Aliitafakari kauli hiyo, akaitafakari pia siku aliyoelezwa; siku mahususi kwa zoezi la upigaji kura. Siku ya uchaguzi.
“Ndiyo muhusika wa huu mpango?” Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko aliuliza.
“Hujapewa nafasi ya kuzungumza, hivyo acha kimuhe muhe.”

Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko alimsaili yule mvamizi aongeaye kisha aliondoka. Hakumpatia picha, huku akiwa mwingi wa shauku ya kumfahamu huyo atakayeenda kuonana naye, na nini sababu ya kuokolewa.

Asubuhi kulivyopambazuka, hata kabla hawajapata stafutahi, wale wavamizi walimtwaa Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko wakaondoka naye. Safari yao haikuwa mbali sana na pale walipokuwa awali. Ulikuwa kama umbali wa mita mia mbili themanini, wakaegesha gari lao ndani ya nyumba ya kifahari yenye mfanano na ile waliyotoka.

Walimteremsha Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko, kisha waliongozana naye hadi ndani ya jengo. Ukomo wao ulikuwa sebuleni.

“Karibuni sana,” mwenyeji wao aliwalaki.
“Tumeshakaribia bosi,” kiongozi wa wavamizi alijibu kwa niaba.

Mwenyeji aliwaonyesha sehemu ya kuketi, lakini wale wavamizi hawakutaka kuketi. Walimuongoza Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko wapi aketi, baadaye waliondoka.

“Karibu sana kamanda,” yule mwenyeji aliongea, akiwa anamkabidhi Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko kikombe cha chai ya kahawa. Naye kuipokea, mboni kazitumbua pima kumsaili mwenyeji wake.

Hakuamini!

Kama zoezi lote lililofanyika ni kwa ajili ya kukutanishwa na huyo mtu. Rais Sharabu.

Akapandwa na hasira. Ambazo zilifahamika kwa haraka akilini mwa Rais Sharabu. Hasira zilizomfanya afikirie, kutolewa kwake gerezani ni kwa sababu maalumu yenye manufaa kwa Rais Sharabu. Mtu ambaye amemfanya aishi kwa tabu na kufikia hatua aliyopo, anaanzaje kumsaidia?
“Punguza jazba ili tuelewane,” Rais Sharabu alifungua uwanja wa mazungumzo.
“Umesahau nini maishani mwangu?”
“Tulia. Tulia, sasa sio muda wa wewe na mimi kuwa maadui.”
“Una maanisha nini? Au kuna yeyote ambaye kwake jua limezama mapema hivyo haitaji kuona likichomoza siku ya kesho?”
“Ndiyo maana nimekuhitaji.”
“Sio muumini wa ushiriki wa hizo kazi kwa sasa. Na kingine, ewe ndiyo adui yangu pekee hapa duniani.” Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko alisema na kugida funda kadhaa za chai.
“Okay! Tuachane na hayo. Nina zawadi nahitaji nikupatie,” Rais Sharabu alichomoa mkanda wa CD, kutoka kwenye begi ndogo aliloliweka jirani na pale alipoketi, akamkabidhi Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko. Kisha aliendelea na kauli, “Nenda kaitazame, ukishamaliza, utanipatia majibu ya kile utakachokutana nacho. Pasi na kusahau hitajio langu.”

Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko alinyanyuka na kuondoka. Alipofikia mlango Rais alitokwa na kauli iliyosheheni msisitizo, “Endapo utaafikiana nami, kupitia hicho utakachokiona, mjulishe mlinzi atakayekuwa anasimamia usalama wako huko utakakopelekwa.”

Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko hakujibu. Aliishia kumwangalia, baadaye aliendelea na safari. Alivyofika nje, aliingia ndani ya gari waliyotumia awali kisha aliwaamuru wale wavamizi wamrudishe. Nao hawakuwa na hiyana, walimrudisha kwenye lile lile jengo la awali.

Alirudi akiwa mwenye kughafirika. Hakupendezwa na dhihaka alizofanyiwa na Rais Sharabu. Yaani juu ya utu uzima wote alionao, anataka amuendeshe kama mtoto mdogo!

Jambo la kwanza mara baada ya kuwasili aliweka ule mkanda wa CD kwenye deki na kuangalia picha jongefu iliyopo. Alistaajabu alichokiona, familia yake ilishikiliwa. Fika akafahamu, Rais Sharabu ndiye mwamuzi wa mipango yote hiyo.

Alichanganyikiwa.

Kiasi cha kutomaliza kuitazama, akaamua kumfuata mlinzi na kuomba miadi ya kukutanishwa na Rais Sharabu.
“Mwambieni huyo mbwa wenu, nahitaji kuonana naye haraka iwezekanavyo na asifanye jambo lolote kwa familia yangu,” Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko alisema akionekana mwenye jazba isiyotatuzuka.
“Ujumbe wako umefika. Hivyo urudi ukapumzike pindi unafanyiwa kazi.”

***

Uchaguzi ulifanyika kwa amani. Babigamba akaibuka kidedea. Nafasi ya wabunge na madiwani, chama tawala na kile cha upinzani vikatofautiana idadi ndogo ya uwakilishi. Ijapokuwa chama tawala ndicho kiliongoza.

Baada ya siku kadhaa iliandaliwa hafla ya uapisho. Hafla iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya nchi. Rais Sharabu alikuwa mmoja wao. Alihudhuria akiwa na kijiba cha roho. Lakini kabla hajaelekea eneo la tukio alikutana na Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko kwenye ile ile nyumba waliyokutana siku zilizopita.
“Nina uhakika tayari umeshatazama?” Rais Sharabu alifungua mjadala wa mazungumzo.

Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko hakujibu kwa uharaka. Alijitafakarisha kwa sekunde chache, huku akiuma uma kingo ya chini ya mdomo na kutikisa kichwa. Baada ya sekunde chache, tafakuri yake ilipoisha ndipo alijibu, “Yeah!” Sauti ikiwa kavu. Sura kaikunyata mithili ya katuni wa kuchorwa.
“Jibu halijajitosheleza.”
“Nipo tayari. Lakini acha kucheza na familia. Acha kucheza na familia yangu wewe mbwa.”

Rais Sharabu aliangua cheko la dhihaka. Kwa muda mfupi kisha alimgeukia Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko. Alipiga hatua moja mbele, alipomfikia, alitumia moja ya mkono wake kukamata bega.
“Usijali. Chukua hii,” Rais Sharabu alisema na kumkabidhi Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko kikaratasi kidogo kilichokunjwa.

Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko alikikunjua kile kikaratasi, akakumbana na maandishi machache yaliyompigisha moyo kite kwa mshangao. Aliinua uso, akamwangalia Rais Sharabu kwa sekunde chache kisha alirejea kuangalia yale maandishi.
“Kama kweli unahitaji heshima kwa familia yako. Hauhitaji kuchezewa, huna budi kutekeleza hilo.” Rais Sharabu akaondoka kuelekea kwenye sherehe za uapisho.

Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko akabaki kutumbulia yale maandishi.

***

Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko aliandaa vijana na kuwapatia mafunzo ya medani za kivita. Mafunzo hayo yalifanyika kwenye moja ya msitu mkubwa uliopo mkoani Ndonya. Juu ya hilo, yalifanyika usiku kucha. Huku washiriki wengi wakianzia umri wa miaka kumi na mbili na mwisho mwenye umri wa miaka thelathini na tano.
“Tufanye haya maazoezi kwa morali ya juu, ili siku tutakayoenda mjini, tuuonyeshe uhodari wetu,” mara kwa mara Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko aliwaasa vijana wake.

Hakika, hayakuwa mazoezi ya kizembe. Yalikuwa mazoezi haswa, yaliyohusisha mbinu zote za kijeshi na matumizi ya silaha za kivita. Kwani sio bunduki, risasi, mabomu wala makombora, kwao yalisheheni. Mtu ambaye alikuwa nyuma ya Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko, hakuwa wa mchezo. Ni zaidi ya mwenye mamlaka na ukwasi wa kutosha.

Baada ya miezi kadhaa, Brigedia Jenerali Mstaafu Kiboko alifanya tathmini ya mafunzo kwa vijana wake. Aliangalia maonyesho mbalimbali yaliyoandaliwa, alivyomaliza, alienda ofisini kwake, alifungua moja ya droo akachukua kile kikaratasi alichopatiwaga na Rais Sharabu. Ambaye kwa wakati huo alikuwa mstaafu. Akarudia kusoma yaliyoandikwa.
“Sitaki kuona Babigamba akitawala kwa amani. Hivyo hakikisha, Tuleane inanuka kwa matendo ovu yaliyobeba ugaidi.”

Baadaye alikigeuza na kuangalia upande wa nyuma. Alikutana na maandishi mengine, yaliyobeba mikakati anayopaswa kutekeleza. Alichukua kalamu na kuweka tiki kwenye mkakati wa kwanza, kuonyesha tayari ameshaufanyia kazi.

ITAENDELEA...

HABARI NJEMA

KITABU CHA RIWAYA YA NENDA SASA KINAPATIKANA RENICS BOOKSHOP TAWI LA MOSHI KWA GHARAMA YA TSH. 10,000/= MAWASILIANO: 0767826134
 
Dah poti yaani ni hatari sana ngoja tuone upande wa uasi itakuaje poti
 
Back
Top Bottom