Hassan Mboneche
Member
- Jun 15, 2020
- 61
- 197
- Thread starter
- #101
MNYONGA TAI—08
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
MAWASILIANO: 0673056571
Mjimile na wale askari waliwasilishwa jijini Dar es salaam kwa haraka sana. Fadhy aliwapokea. Akaenda kuwahifadhi kwenye moja ya majengo ya siri yaliyopo chini ya kitengo chake maeneo ya Mbweni. Safe house, ndivyo zilivyotambulishwa kwa urahisi.
Kila mmoja alihifadhiwa chumba chake. Na kwa mazingira yalivyo ulikosekana upenyo wa kuwashinikiza washirikiane kwa jambo lolote lile. Walikuwa zaidi ya wafungwa. Ijapokuwa waliwekewa maji ya kunywa ya chupa nyenye ujazo wa nusu lita, na kasha moja la biskuti.
“Huo ndiyo mlo wenu kwa siku zote mtakazokuwa humu. Ukimaliza kabla ya wakati, utajua mwenyewe utakakopata chakula,” Fadhy aliwaasa kwa wema. Ili wawe na matumizi mazuri ya vile vitu.
Zilipita siku tatu, pasi na kutokea mtu yeyote kwenye lile jengo walilohifadhiwa. Siku ya nne, ndipo Fadhy alipotembelea, tena kwa lengo la kumhoji mtu mmoja tu. Wakati huo, wengi wao walishamaliza vile vitu walivyopatiwa kwa ajili ya kuchangamsha tumbo. Hivyo njaa ikawa inawasumbua mbaya.
Wa kwanza kuhojiwa alikuwa Mjimile. Alitolewa chumbani kwake, akapelekwa kwenye ukumbi husika.
“Tajiri,” Fadhy aliita. Mjimile akamtumbilia mboni kali.
“Pole kwa matatizo. Lakini ukiuhitaji uhuru wako ni wewe tu, namna tutakavyoshirikiana katika hili. Upo tayari?”
Mjimile hakujibu.
“Kama haupo tayari sema, niamuru urudishwe chumbani kwako.”
Badala ya kujibu kwa kauli, Mjimile alionyesha ishara. Ya uhitaji wa chakula. Fadhy akamsaili. Mjimile akaonyesha ile ishara kwa mara nyingine kwa msisitizo zaidi.
“Upo tayari kwa ushirikiano?”
Mjimile akatingisha kichwa; juu-chini. Ishara ya kuridhia.
Kwa msisito huo, Fadhy aliondoka mle ofisini na kurejea baada ya dakika kadhaa. Alibeba kibakuli kilicho na chakula, akamkabidhi Mjimile. Kutokana na njaa, Mjimile alikifakamia kile chakula na kumaliza ndani ya muda mfupi sana. Akapewa na maji kishuke vyema.
“Upo sawa?”
“Ndiyo,” Mjimile alijibu.
“Sihitaji uongofu katika hili.” Akamtumbulia mboni kali za usaili. Mjimile hakujibu.
“Okay, unawafahamu hawa?” Fadhy akamsogezea picha mnato ziwaonyeshazo Cheyaya na Kasembe.
Mjimile alishtuka kidogo alivyozibaini. Mshituko uliobainika na Fadhy.
“Unawafahamuje hao?”
“Ni wafanyabiashara wenzangu.”
“Zaidi ya hivyo?”
Mjimile hakujibu kwa uharaka. Jambo lililotengeneza ukimya kwa muda, karibu na kushika hatamu, Fadhy akaufukuza, “Unafahamu sababu ya matatizo wapitiayo hivi sasa?”
“Aaah, sina ukaribu nao kiasi hicho. Hivyo ni ngumu...”
Fadhy akadakia, “Lakini unashirikiana na wasababishi wa tatizo.”
Mjimile izara ikamjaa.
“Nilikutahadharisha mwanzo, sihitaji uongofu. Au nitumie nguvu ya ziada?” akavuta saraka, akatoa mjeledi, bisibisi na nyundo.
Mjimile akabaki kumstaajabu.
“Nakuuliza kwa mara ya mwisho kabla hivi vitu havijagusa mwilini mwako. Nini sababu ya hao wafanyabiashara kupitia matatizo waliyonayo?”
Kwa hofu ya mwili wake kupata maumivu, Mjimile ikambidi afunguke anachokifahamu. “Nalimuka ndiyo sababu,” alisema na kutulia. Sauti ikiwa nyongefu. Hofu ikimtukuta nafsini. Anasaliti wenzie. “Nalimuka anahitaji hela za wale watu.”
“Kwa nini anahitaji hela zao? Na kwa nini anatumia mgongo wa serikali kufanya kitu kama hicho?”
“Ndiyo njia rahisi ya kujihalalishia. Hata ungelikuwa wewe ungelifanya hivyo. Wanyonga tai wote wana kawaida hiyo.”
“Okay, nitakurudia siku nyingine kwa mahojiano zaidi.” Fadhy akainuka.
“Kwa hiyo narudishwa kwenye kilekile chumba?” akamtumbulia mboni za huruma.
“Utapelekwa sehemu nyingine.” Akaondoka.
Siku zilizofuatia aliwahoji wale askari. Mbinu ya kuwashindisha njaa ilimsaidia sana, akapata ushirikiano mzuri uliompa mwangaza baada ya kuunganisha doti. Alijihakikishia kile alichotaarifiwa hapo awali.
Awamu zote za mahojiano, alikuwa na tepurekoda iliyomsaidia kuhifadhi yale mazungumzo.
“Na vipi kama Nalimuka anatekeleza haya kwa amri ya Rais? Na hata kama ni amri yake, kwa nini iwe kwa uonevu?” Fadhy alijiuliza, baada ya kuyatafakari kwa kina mahojiano ya watu wote. Alikuwa amesimama hatua chache kutoka dirishani ndani ya ofisi yake akiyasaili mandhari ya jiji.
Akili ilivyoduwazwa na mwonekano wa jiji kwa usawa aliouchukulia umakini, wazo jipya likamwingia. Nini anapaswa kufanya kwa wakati huo.
“Meneja mamlaka ya mapato Mtwara,” alijisemeza. “Yeah, huyu mtu anahitajika upenuni mwangu,” alijihakikishia kwa utingishaji wa kichwa.
***
Baada ya mafikirio ya muda wa dakika kadhaa Jovin alikata shauri na hatimaye kumruhusu Stella kuingia ndani. Yeye ndiyo alitangulia, alipofika usawa alipoiacha bunduki, aliisukumizia uvunguni mwa sofa kwa mguu pasi na Stella kuona.
“Tumekuwa adimu kwa hizi siku kadhaa, tunashindwa kutafutana,” Jovin alisema, pindi wakichukua mkao sofani.
“Nilisafiri kidogo. Si unajua hili tatizo lililomkumba mzee linahitaji mihangaiko?”
“Ulienda na mama?”
“Ndiyo.”
“Wapi?”
“Mmmh! Kwenye miji ya watu. Huko mbelembele.”
Jovin akavuta pumzi na kuzitua kwa nguvu. Alionekana kuguswa, kana kwamba ndiyo mtendewa. Stella akampimia tu.
“Kwa hiyo mama bado yupo huko?”
“Ndiyo, anaendelea kushughulikia mambo yakae sawa.”
Mtiririko huu wa maswali ulimhakikishia Stella, Jovin sio mtu mzuri katika ustawi wa familia yao.
Mwito wa simu ya Jovin ndiyo ilisitisha kwa muda mazungumzo yao. Alimsaili mpigaji kwa sekunde chache kisha aliipokea. Ilikuwa simu kutoka kwa Nalimuka.
“Jiandae kwa ugeni wangu.” Ikakatwa pasi na Jovin kujibu ameridhia kwa mapokeo ama lah.
Akaiondoa kwa unyonge sikioni.
“Kuna tatizo?” Stella aliuliza, muda wote hakubandukua mboni zake kumsaili Jovin.
“Hapana.”
“Sasa mbona umebadilika ghafla?”
“Amenichanganya tu huyu niliyewasiliana naye pasi na kunipatia wasaa wa kuchangia mazungumzo.” Ikambidi aongope. Maana kilichomtatiza ni namna gani watazungumza na Nalimuka Stella akiwepo mazingira yale. Ilimtatizisha.
“Sasa si umpigie ili mwelewane?” Stella akamwondoa mawazoni.
“Haina salio.”
“Chukua hii.” Stella akatoa simu yake, akamkabidhi.
Pindi Jovin yu'mbioni kuiopokea, sauti ya kugongwa mlango ishara ya hodi ikasikika. Akasitisha uchukuaji simu, akaenda kufungua mlango. Akakumbana na Nalimuka.
“Nimetoka...” Nalimuka alisema, mwili ukiwa umefura, lakini kabla hajahitimisha kauli yake akaoneshwa ishara fulani ya kuzibwa mdomo-ina maana asiendelee kuzungumza na Jovin.
Jovin akamnong'oneza, “Mazingira ya ndani sio mazuri, twende tukaongelee huku hivi.” Akamsukumiza kidogo Nalimuka, kisha alimwaga Stella, “Dakika tano kipenzi.” Akatoka nje, akafuatia kufunga mlango.
“Kuna nini ndani?” Nalimuka uvumilivu ulimshinda.
“Nipo na mtoto wa Cheyaya mle ndani. Yule bintiye.”
Nalimuka akasitisha mwendo na kumgeukia Jovin. “Amefuata nini?” aliuliza.
“Mambo ya wanaume. Na ni sehemu ya chanzo cha taarifa katika ufanikishaji wa mambo yangu.”
“Asije kuwa naye anakufanyia ushushushu?”
“Hajabaini hilo.”
Wakarejelea mwendo.
Walipoweka tuo hapakuwa mbali sana na nyumba. Wakafungua uwanja wa mazungumzo kwa mara nyingine. Awamu hii, ilikuwa kwa unong'ozi.
“Nimekutana na Cheyaya leo tukafukuzana kama mbwa. Sijui wapi amenichenga yule mjinga, tulikuwa tunamaliza kazi kabisa.”
“Acha bhana!” Jovin alistaajabu.
“Ndiyo hivyo. Ilinibidi nifanye. Tambua siku zimesalia chache za Waziri Mkuu kuwasili halafu yule mjinga bado anadunda. Hiyo inanipa mashaka sana. Inanifanya nikose amani.”
“Ukiwa hivyo unaweza kuharibu mpango mzima. Ulinikabidhi kazi, ya nini uingiwe mashaka wakati siku tuliyoahidiana bado haijawadia?”
“Ndugu. Akijificha, kama alivyofanya siku zilizopita unadhani tutampatia wapi?”
“Haijalishi. Ni lazima tu, alambe mchanga.”
“Utafanyaje fanyaje?”
Jovin alikaa kimya kwa muda akifikiri jambo, alivyoridhishwa na alilolipata, aliliweka wazi, “Nitachoma moto nyumba yao. Kama atakuwa papa hapa mjini, atatokeza tu katika mazingira hayo. Hapo ndipo nitakapomfumua.”
“Basi na iwe hivyo,” Nalimuka aliafikiana naye.
Kitu pekee ambacho hawakukifahamu, Stella alikuwa jirani nao na alifanikiwa kunyaka kwa ufasaha mipango hiyo. Ilimbidi tu ajikaze, lakini hali iliyomkumba haikuwa ya kawaida. Mapigo ya moyo yalimbadilika mara kwa mara na kumfanya azidi kuwa mwenye hasira dhidi ya Jovin.
Hasira hizo zilipelekea ashindwe hata kupata ufafanuzi sahihi kumhusu Jovin. Amkamatishe muda huohuo? Au ajipe subira?
Akabaki kugugumia.
***
Cheyaya aliwasili kwa mwenyeji wake akiwa mwenye mihemo juujuu. Hakusita kumhadithia mwenzie mkasa mzima, mara baada ya hapo walimalizia ngwe ya kasi iliyosalia na kufuatia usakaji wa usingizi.
Sauti ya mwito ya mwenyeji wake aliyetoka mazoezini asubuhi hiyo ndiyo ilimwamsha Cheyaya. Alilala usingizi mzito hasa, kutokana na uchovu wa mabio aliyoyafanya.
“Nimechoka sana. Maana jinsi ninayoisikia hiyo miguu, sitamani hata kutoka hapa kitandani,” Cheyaya alisema, huku akiamka.
“Kuna taarifa mbaya.” Cheyaya akapotezea hali ajisikiayo na kushawishika asikie hicho chenye ubaya. “Nyumba yako inaungua moto muda huu,” mwenyeji alizidi kumpasha.
Moyo ulipiga kite kwa mshituko. Kile alichokisikia kilishindwa kujituliza, hivyo kilifukunyua kila sehemu iliyohusika na chimbuko la furaha.
“Ina ukweli hiyo taarifa?” Cheyaya aliuliza, akiwa ameshainuka. Akili haikutuliana kabisa.
“Hakika.”
Cheyaya alianza kwa kuguna, kisha akatingisha kichwa kuonyesha masikitiko yake, “Yaani.” Akaguna tena. “Mbona matatizo hayaniishi?”
“Mungu ndiyo anajua.”
“Nataka nikaisaidie familia yangu iweze kuokokana na hili. Sipati picha namna wanavyoteseka huko,” Cheyaya alisema, akiwa ameshaanza kuvaa tayari kwa kuondoka.
“Huisi...” kabla mwenye nyumba hajamaliza kauli yake, Cheyaya alikwishaanza mwendo. Naye akaona isiwe tabu, akaungana naye.
***
Stella naye asubuhi hiyo alikuwa kwenye mizunguko iliyomshinikiza aifikie nyumba yao. Kile alichokisikia kutoka kwa Jovin hakikubanduka akilini. Alikesha kukijengea picha jinsi kitakavyotokea. Alivyohitimisha, machozi yalishatengeneza njia mashavuni.
Alivyokaribia nyumbani kwao, akaanza kuushuhudia moshi angani. Akaingiwa mashaka; Jovin ameshatekeleza kile alichokiahidi, ama lah. Moyo ukabaki njia panda, huku akijitahidi kuomba kile akionacho kisitokee nyumbani kwao.
Akajitengenezea hali ya ukosefu wa amani nafsini.
Nusuru adondoke, pale aliposhuhudia nyumba yao ndiyo iteketeayo. Kabla hajajua afanye nini, aliduwaa kwa muda na kuruhusu kumbukizi ya maongezi ya kina Jovin.
“Ina maana amefanya kweli!” Stella alijisemeza chozi likimtiririka. Wakati huo mpwito wa mapigo ya moyo si ya kawaida. “Kweli anataka kwenda kumuua baba'ngu?” Kumbukizi ya baba'ke kuhitajika kuuwawa katika tukio hilo likamwondolea mduwao na kutimua mbio. Alikimbia mboni zikihangaika huku na kule kusaili halaiki iliyopo.
Wakati huo Jovin alikuwa kwenye paa ya moja ya nyumba, umbali wa mita kadhaa akikazana kuwasaili watu waliopo katika lile tukio kupitia darubini iliyofungwa juu ya bunduki. Azma ampate Cheyaya.
Hangaiko hilo lilichukua dakika chache tu, akafanikiwa kumwona Cheyaya akiwa mbio kuifikia nyumba yake. Ndiyo alikuwa anawasili kutoka mafichoni na yule mwenyeji wake. Zilisalia takribani mita kumi na saba, Cheyaya ajiunge na halaiki iliyokuja kushuhudia na kutoa msaada pia, Jovin akafanikiwa kumweka kilengeoni kwa usahihi. Tena shabaha ilisoma pajini.
Mungu ampe nini.
Jovin akabana pumzi. Akajihakikishia mkito wa bunduki kwenye nyama ya bega, kisha akakisereresha kidole cha shahada taratibu kuelekea kilipo kifyatulio. Hakukawiza, akaruhusu mtupo wa risasi.
Kitendo cha kushangaza, kilengeoni akasomeka Stella.
***
Askofu Ponera ndiyo alikuwa wa kwanza kufikwa na taarifa ya lile tukio kupitia vijiweni. Hakuwa mroho, aliwataarifu wenzie, kisha na Fadhy pia. Fadhy alipatiwa kwa njia ya video call wakiwa kwenye makazi yao waliyofikia-Meswaki.
“Hilo tukio linahusiana na tatizo tunalokumbana nalo?” Fadhy aliuliza.
“Haina uhakika chifu.”
“Awali, hili tukio nilihisi halitofikia ukubwa huu.”
“Tupe mwongozo sasa.”
“Uhitaji wa taarifa bado ni mkubwa sana. Askofu lishughulikie hilo. Wakati Luteni Ringo na wenzio, kuna kazi ya kufanya Mtwara mjini.”
“Ipi?”
“Namhitaji Meneja mamlaka ya mapato mkoa.”
“Sawa chifu.”
Maongezi yakahitimika.
Fadhy naye hakuwa mchoyo, aliwafikishia ile taarifa kina Dorice. Kwa sababu ya wepesi wa uhimilivu, wakaangua vilio na kumpa Fadhy zoezi la kuwatuliza. Walitulia walipojisikia wenyewe, baada ya kuamini wameondoa kiasi fulani cha uchungu.
“Tumtaarifu Stella?” Dorice aliuliza.
“Aaah, sio vibaya naye akafahamu. Ukizingatia hatujapata uthibitisho wa moja kwa moja kuwa hili la moto linahusiana na kadhia ya waume zenu katika biashara zao.”
Dorice akapiga simu. Isivyo bahati, hakupatikana hewani.
“Sio kesi, unaweza kumweleza hata baadaye,” Fadhy akamtuliza. Maana kichwa kilishaanza kupata moto na alikwishaanza kulengwa na machozi.
“Shem, toka nifahamu Stella anamiliki simu, sijawahi kimsikia akilalamikia bahari za kuisha chaji.”
“Sasa...,” Fadhy alidakia. Kabla hajahitimisha akapata simu kutoka kwa Askofu Ponera. Hakuchelea kuipokea.
“Ndiyo,” Fadhy alisema.
“Imeshabainika nani amepigwa risasi.”
“Nani?” Fadhy aliuliza kwa shauku.
“Mtoto wa Cheyaya.”
Moyo ukapiga kite kwa mshituko. Wajihi ukambadilika, kiasi cha kuwashtua kina Dorice na kuwajaza hamu wafahamishwe apatiwacho.
“Ina ukweli wowote?” Fadhy aliuliza na kutulia kwa sekunde kadhaa. Bado alikuwa anaichakata ile taarifa. “Nikiwa na maana umeifanyia utafiti ukajihakikishia.”
“Pasi na shaka. Sambamba na hilo, mkusudiwa wetu mbaroni. Cheyaya amekamatwa na askari polisi. Alikuwa hapa hospitalini.”
Fadhy akazidi kunyong'onyea.
“Kuna jambo lolote ninaloweza kufanya kwa idhini yako?” Askofu Ponera akamzindua.
“Askofu, hii vita sio ya kuichukulia poa. Kama wapinzani wetu wanafanya vitendo vya kikatili zaidi ili wafanikishe walifikirialo, basi tuna kazi nzito sana.” Fadhy akainuka, na kupiga hatua ndogondogo akipotelea ushorobani.
Akawaacha kina Dorice mzuka umewapanda.
Fadhy akaendelea, “Nafikiria nini tufanye ili tuwashinde kwa haraka. Maana hiki walichozidi kukifanya hakivumiliki.”
“Kwa hiyo tuwaache tu wakiondoka na huyu?”
“Stella. Tafuta taarifa za kina kumhusu Stella. Nini matokeo ya risasi aliyopigwa.”
“Sawa chifu.”
“Fanya hima ujitahidi.” Fadhy akakata simu. Akarejea sebuleni.
“Kuna tatizo?” Dorice kimuhemuhe akafanya kazi yake. Hakumpooza.
“Halihusiani na hili tunalolishughulikia,” Fadhy akawaongopea.
“Mmh! Shem...”
“Kuna jambo lingine tu linalohusiana na majukumu ya kazi yangu. Kukiwa na utofauti wa hili letu siwezi kuwanyima taarifa zake. Kuweni na amani.”
“Unanifanya nianze kukuogopa. Kwani sura yako inaficha kilichopo moyoni ambacho umetoka kutaarifiwa.”
Wakati wote wa maongezi Fadhy alikuwa amesimama. Baadaye ikambidi ajibweteke sofani, kisha kuwasaili ma-shemeji zake tuo kwa tuo, huku akijipa fikra, aanzaje kuwataarifu ile taarifa ya Stella kupigwa risasi na Cheyaya kukamatwa?
Alichokuwa anakikwepa, ni kuona wanawake hao wanaondoka jijini na kurudi Mangaka. Aliamini, kwa namna yoyote ile, akiwaambia watakuwa na uhitaji huo. Jambo litakalochangia ugumu wa ufanikishaji wa kuwaweka hatiani washukiwa wao.
“Sasa umeamini kuwa lipo unalotuficha?” Dorice akamgutusha.
“Kwa nini umekuwa hivyo shem?”
“Nina uchungu namna uhuru wetu unavyozidi kupotea kila uchao pasi na kosa lolote tulilolifanya. Jitihada zote za upambanaji tulizozifanya hadi kuutwaa ubilionea leo hii tumegeuka wahujumu uchumi kwa sababu tumekataa matakwa yao.
“Nina uchungu na huu uonevu unaozidi kuendelea shem. Kwa nini tunaonewa? Wanatuoneaje? Wanatuoneaje hawa?” alilalama hadi machozi yakaanza kumlenga. Uvumilivu ulipomshinda kilio kikawa nafuu yake.
“Ni lini hao tunaowaamini wataacha uonevu? Wataendelea kuongoza kwa kudhulumu? Au ndiyo miiko ya uongozi inavyotaka eeh?” Dorice aliendelea kulalama.
“Ndiyo maana nimechukua maamuzi ya kushughulikia ili kufutilia mbali dhana hii iliyokita mizizi kila nyanja. Nitaitokomeza, na kujenga nidhamu kwa watumishi wengine. Kupitia hili, litakuwa fundisho kwao,” Fadhy alimtuliza.
Dorice akafuta machozi, kisha akamsaili Fadhy.
“Nakuhakikishia tena, niaminini. Tunaenda kushinda huu mchezo,” alimsisitizia.
TUKUTANE TOLEO LIJALO.
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
MAWASILIANO: 0673056571
Mjimile na wale askari waliwasilishwa jijini Dar es salaam kwa haraka sana. Fadhy aliwapokea. Akaenda kuwahifadhi kwenye moja ya majengo ya siri yaliyopo chini ya kitengo chake maeneo ya Mbweni. Safe house, ndivyo zilivyotambulishwa kwa urahisi.
Kila mmoja alihifadhiwa chumba chake. Na kwa mazingira yalivyo ulikosekana upenyo wa kuwashinikiza washirikiane kwa jambo lolote lile. Walikuwa zaidi ya wafungwa. Ijapokuwa waliwekewa maji ya kunywa ya chupa nyenye ujazo wa nusu lita, na kasha moja la biskuti.
“Huo ndiyo mlo wenu kwa siku zote mtakazokuwa humu. Ukimaliza kabla ya wakati, utajua mwenyewe utakakopata chakula,” Fadhy aliwaasa kwa wema. Ili wawe na matumizi mazuri ya vile vitu.
Zilipita siku tatu, pasi na kutokea mtu yeyote kwenye lile jengo walilohifadhiwa. Siku ya nne, ndipo Fadhy alipotembelea, tena kwa lengo la kumhoji mtu mmoja tu. Wakati huo, wengi wao walishamaliza vile vitu walivyopatiwa kwa ajili ya kuchangamsha tumbo. Hivyo njaa ikawa inawasumbua mbaya.
Wa kwanza kuhojiwa alikuwa Mjimile. Alitolewa chumbani kwake, akapelekwa kwenye ukumbi husika.
“Tajiri,” Fadhy aliita. Mjimile akamtumbilia mboni kali.
“Pole kwa matatizo. Lakini ukiuhitaji uhuru wako ni wewe tu, namna tutakavyoshirikiana katika hili. Upo tayari?”
Mjimile hakujibu.
“Kama haupo tayari sema, niamuru urudishwe chumbani kwako.”
Badala ya kujibu kwa kauli, Mjimile alionyesha ishara. Ya uhitaji wa chakula. Fadhy akamsaili. Mjimile akaonyesha ile ishara kwa mara nyingine kwa msisitizo zaidi.
“Upo tayari kwa ushirikiano?”
Mjimile akatingisha kichwa; juu-chini. Ishara ya kuridhia.
Kwa msisito huo, Fadhy aliondoka mle ofisini na kurejea baada ya dakika kadhaa. Alibeba kibakuli kilicho na chakula, akamkabidhi Mjimile. Kutokana na njaa, Mjimile alikifakamia kile chakula na kumaliza ndani ya muda mfupi sana. Akapewa na maji kishuke vyema.
“Upo sawa?”
“Ndiyo,” Mjimile alijibu.
“Sihitaji uongofu katika hili.” Akamtumbulia mboni kali za usaili. Mjimile hakujibu.
“Okay, unawafahamu hawa?” Fadhy akamsogezea picha mnato ziwaonyeshazo Cheyaya na Kasembe.
Mjimile alishtuka kidogo alivyozibaini. Mshituko uliobainika na Fadhy.
“Unawafahamuje hao?”
“Ni wafanyabiashara wenzangu.”
“Zaidi ya hivyo?”
Mjimile hakujibu kwa uharaka. Jambo lililotengeneza ukimya kwa muda, karibu na kushika hatamu, Fadhy akaufukuza, “Unafahamu sababu ya matatizo wapitiayo hivi sasa?”
“Aaah, sina ukaribu nao kiasi hicho. Hivyo ni ngumu...”
Fadhy akadakia, “Lakini unashirikiana na wasababishi wa tatizo.”
Mjimile izara ikamjaa.
“Nilikutahadharisha mwanzo, sihitaji uongofu. Au nitumie nguvu ya ziada?” akavuta saraka, akatoa mjeledi, bisibisi na nyundo.
Mjimile akabaki kumstaajabu.
“Nakuuliza kwa mara ya mwisho kabla hivi vitu havijagusa mwilini mwako. Nini sababu ya hao wafanyabiashara kupitia matatizo waliyonayo?”
Kwa hofu ya mwili wake kupata maumivu, Mjimile ikambidi afunguke anachokifahamu. “Nalimuka ndiyo sababu,” alisema na kutulia. Sauti ikiwa nyongefu. Hofu ikimtukuta nafsini. Anasaliti wenzie. “Nalimuka anahitaji hela za wale watu.”
“Kwa nini anahitaji hela zao? Na kwa nini anatumia mgongo wa serikali kufanya kitu kama hicho?”
“Ndiyo njia rahisi ya kujihalalishia. Hata ungelikuwa wewe ungelifanya hivyo. Wanyonga tai wote wana kawaida hiyo.”
“Okay, nitakurudia siku nyingine kwa mahojiano zaidi.” Fadhy akainuka.
“Kwa hiyo narudishwa kwenye kilekile chumba?” akamtumbulia mboni za huruma.
“Utapelekwa sehemu nyingine.” Akaondoka.
Siku zilizofuatia aliwahoji wale askari. Mbinu ya kuwashindisha njaa ilimsaidia sana, akapata ushirikiano mzuri uliompa mwangaza baada ya kuunganisha doti. Alijihakikishia kile alichotaarifiwa hapo awali.
Awamu zote za mahojiano, alikuwa na tepurekoda iliyomsaidia kuhifadhi yale mazungumzo.
“Na vipi kama Nalimuka anatekeleza haya kwa amri ya Rais? Na hata kama ni amri yake, kwa nini iwe kwa uonevu?” Fadhy alijiuliza, baada ya kuyatafakari kwa kina mahojiano ya watu wote. Alikuwa amesimama hatua chache kutoka dirishani ndani ya ofisi yake akiyasaili mandhari ya jiji.
Akili ilivyoduwazwa na mwonekano wa jiji kwa usawa aliouchukulia umakini, wazo jipya likamwingia. Nini anapaswa kufanya kwa wakati huo.
“Meneja mamlaka ya mapato Mtwara,” alijisemeza. “Yeah, huyu mtu anahitajika upenuni mwangu,” alijihakikishia kwa utingishaji wa kichwa.
***
Baada ya mafikirio ya muda wa dakika kadhaa Jovin alikata shauri na hatimaye kumruhusu Stella kuingia ndani. Yeye ndiyo alitangulia, alipofika usawa alipoiacha bunduki, aliisukumizia uvunguni mwa sofa kwa mguu pasi na Stella kuona.
“Tumekuwa adimu kwa hizi siku kadhaa, tunashindwa kutafutana,” Jovin alisema, pindi wakichukua mkao sofani.
“Nilisafiri kidogo. Si unajua hili tatizo lililomkumba mzee linahitaji mihangaiko?”
“Ulienda na mama?”
“Ndiyo.”
“Wapi?”
“Mmmh! Kwenye miji ya watu. Huko mbelembele.”
Jovin akavuta pumzi na kuzitua kwa nguvu. Alionekana kuguswa, kana kwamba ndiyo mtendewa. Stella akampimia tu.
“Kwa hiyo mama bado yupo huko?”
“Ndiyo, anaendelea kushughulikia mambo yakae sawa.”
Mtiririko huu wa maswali ulimhakikishia Stella, Jovin sio mtu mzuri katika ustawi wa familia yao.
Mwito wa simu ya Jovin ndiyo ilisitisha kwa muda mazungumzo yao. Alimsaili mpigaji kwa sekunde chache kisha aliipokea. Ilikuwa simu kutoka kwa Nalimuka.
“Jiandae kwa ugeni wangu.” Ikakatwa pasi na Jovin kujibu ameridhia kwa mapokeo ama lah.
Akaiondoa kwa unyonge sikioni.
“Kuna tatizo?” Stella aliuliza, muda wote hakubandukua mboni zake kumsaili Jovin.
“Hapana.”
“Sasa mbona umebadilika ghafla?”
“Amenichanganya tu huyu niliyewasiliana naye pasi na kunipatia wasaa wa kuchangia mazungumzo.” Ikambidi aongope. Maana kilichomtatiza ni namna gani watazungumza na Nalimuka Stella akiwepo mazingira yale. Ilimtatizisha.
“Sasa si umpigie ili mwelewane?” Stella akamwondoa mawazoni.
“Haina salio.”
“Chukua hii.” Stella akatoa simu yake, akamkabidhi.
Pindi Jovin yu'mbioni kuiopokea, sauti ya kugongwa mlango ishara ya hodi ikasikika. Akasitisha uchukuaji simu, akaenda kufungua mlango. Akakumbana na Nalimuka.
“Nimetoka...” Nalimuka alisema, mwili ukiwa umefura, lakini kabla hajahitimisha kauli yake akaoneshwa ishara fulani ya kuzibwa mdomo-ina maana asiendelee kuzungumza na Jovin.
Jovin akamnong'oneza, “Mazingira ya ndani sio mazuri, twende tukaongelee huku hivi.” Akamsukumiza kidogo Nalimuka, kisha alimwaga Stella, “Dakika tano kipenzi.” Akatoka nje, akafuatia kufunga mlango.
“Kuna nini ndani?” Nalimuka uvumilivu ulimshinda.
“Nipo na mtoto wa Cheyaya mle ndani. Yule bintiye.”
Nalimuka akasitisha mwendo na kumgeukia Jovin. “Amefuata nini?” aliuliza.
“Mambo ya wanaume. Na ni sehemu ya chanzo cha taarifa katika ufanikishaji wa mambo yangu.”
“Asije kuwa naye anakufanyia ushushushu?”
“Hajabaini hilo.”
Wakarejelea mwendo.
Walipoweka tuo hapakuwa mbali sana na nyumba. Wakafungua uwanja wa mazungumzo kwa mara nyingine. Awamu hii, ilikuwa kwa unong'ozi.
“Nimekutana na Cheyaya leo tukafukuzana kama mbwa. Sijui wapi amenichenga yule mjinga, tulikuwa tunamaliza kazi kabisa.”
“Acha bhana!” Jovin alistaajabu.
“Ndiyo hivyo. Ilinibidi nifanye. Tambua siku zimesalia chache za Waziri Mkuu kuwasili halafu yule mjinga bado anadunda. Hiyo inanipa mashaka sana. Inanifanya nikose amani.”
“Ukiwa hivyo unaweza kuharibu mpango mzima. Ulinikabidhi kazi, ya nini uingiwe mashaka wakati siku tuliyoahidiana bado haijawadia?”
“Ndugu. Akijificha, kama alivyofanya siku zilizopita unadhani tutampatia wapi?”
“Haijalishi. Ni lazima tu, alambe mchanga.”
“Utafanyaje fanyaje?”
Jovin alikaa kimya kwa muda akifikiri jambo, alivyoridhishwa na alilolipata, aliliweka wazi, “Nitachoma moto nyumba yao. Kama atakuwa papa hapa mjini, atatokeza tu katika mazingira hayo. Hapo ndipo nitakapomfumua.”
“Basi na iwe hivyo,” Nalimuka aliafikiana naye.
Kitu pekee ambacho hawakukifahamu, Stella alikuwa jirani nao na alifanikiwa kunyaka kwa ufasaha mipango hiyo. Ilimbidi tu ajikaze, lakini hali iliyomkumba haikuwa ya kawaida. Mapigo ya moyo yalimbadilika mara kwa mara na kumfanya azidi kuwa mwenye hasira dhidi ya Jovin.
Hasira hizo zilipelekea ashindwe hata kupata ufafanuzi sahihi kumhusu Jovin. Amkamatishe muda huohuo? Au ajipe subira?
Akabaki kugugumia.
***
Cheyaya aliwasili kwa mwenyeji wake akiwa mwenye mihemo juujuu. Hakusita kumhadithia mwenzie mkasa mzima, mara baada ya hapo walimalizia ngwe ya kasi iliyosalia na kufuatia usakaji wa usingizi.
Sauti ya mwito ya mwenyeji wake aliyetoka mazoezini asubuhi hiyo ndiyo ilimwamsha Cheyaya. Alilala usingizi mzito hasa, kutokana na uchovu wa mabio aliyoyafanya.
“Nimechoka sana. Maana jinsi ninayoisikia hiyo miguu, sitamani hata kutoka hapa kitandani,” Cheyaya alisema, huku akiamka.
“Kuna taarifa mbaya.” Cheyaya akapotezea hali ajisikiayo na kushawishika asikie hicho chenye ubaya. “Nyumba yako inaungua moto muda huu,” mwenyeji alizidi kumpasha.
Moyo ulipiga kite kwa mshituko. Kile alichokisikia kilishindwa kujituliza, hivyo kilifukunyua kila sehemu iliyohusika na chimbuko la furaha.
“Ina ukweli hiyo taarifa?” Cheyaya aliuliza, akiwa ameshainuka. Akili haikutuliana kabisa.
“Hakika.”
Cheyaya alianza kwa kuguna, kisha akatingisha kichwa kuonyesha masikitiko yake, “Yaani.” Akaguna tena. “Mbona matatizo hayaniishi?”
“Mungu ndiyo anajua.”
“Nataka nikaisaidie familia yangu iweze kuokokana na hili. Sipati picha namna wanavyoteseka huko,” Cheyaya alisema, akiwa ameshaanza kuvaa tayari kwa kuondoka.
“Huisi...” kabla mwenye nyumba hajamaliza kauli yake, Cheyaya alikwishaanza mwendo. Naye akaona isiwe tabu, akaungana naye.
***
Stella naye asubuhi hiyo alikuwa kwenye mizunguko iliyomshinikiza aifikie nyumba yao. Kile alichokisikia kutoka kwa Jovin hakikubanduka akilini. Alikesha kukijengea picha jinsi kitakavyotokea. Alivyohitimisha, machozi yalishatengeneza njia mashavuni.
Alivyokaribia nyumbani kwao, akaanza kuushuhudia moshi angani. Akaingiwa mashaka; Jovin ameshatekeleza kile alichokiahidi, ama lah. Moyo ukabaki njia panda, huku akijitahidi kuomba kile akionacho kisitokee nyumbani kwao.
Akajitengenezea hali ya ukosefu wa amani nafsini.
Nusuru adondoke, pale aliposhuhudia nyumba yao ndiyo iteketeayo. Kabla hajajua afanye nini, aliduwaa kwa muda na kuruhusu kumbukizi ya maongezi ya kina Jovin.
“Ina maana amefanya kweli!” Stella alijisemeza chozi likimtiririka. Wakati huo mpwito wa mapigo ya moyo si ya kawaida. “Kweli anataka kwenda kumuua baba'ngu?” Kumbukizi ya baba'ke kuhitajika kuuwawa katika tukio hilo likamwondolea mduwao na kutimua mbio. Alikimbia mboni zikihangaika huku na kule kusaili halaiki iliyopo.
Wakati huo Jovin alikuwa kwenye paa ya moja ya nyumba, umbali wa mita kadhaa akikazana kuwasaili watu waliopo katika lile tukio kupitia darubini iliyofungwa juu ya bunduki. Azma ampate Cheyaya.
Hangaiko hilo lilichukua dakika chache tu, akafanikiwa kumwona Cheyaya akiwa mbio kuifikia nyumba yake. Ndiyo alikuwa anawasili kutoka mafichoni na yule mwenyeji wake. Zilisalia takribani mita kumi na saba, Cheyaya ajiunge na halaiki iliyokuja kushuhudia na kutoa msaada pia, Jovin akafanikiwa kumweka kilengeoni kwa usahihi. Tena shabaha ilisoma pajini.
Mungu ampe nini.
Jovin akabana pumzi. Akajihakikishia mkito wa bunduki kwenye nyama ya bega, kisha akakisereresha kidole cha shahada taratibu kuelekea kilipo kifyatulio. Hakukawiza, akaruhusu mtupo wa risasi.
Kitendo cha kushangaza, kilengeoni akasomeka Stella.
***
Askofu Ponera ndiyo alikuwa wa kwanza kufikwa na taarifa ya lile tukio kupitia vijiweni. Hakuwa mroho, aliwataarifu wenzie, kisha na Fadhy pia. Fadhy alipatiwa kwa njia ya video call wakiwa kwenye makazi yao waliyofikia-Meswaki.
“Hilo tukio linahusiana na tatizo tunalokumbana nalo?” Fadhy aliuliza.
“Haina uhakika chifu.”
“Awali, hili tukio nilihisi halitofikia ukubwa huu.”
“Tupe mwongozo sasa.”
“Uhitaji wa taarifa bado ni mkubwa sana. Askofu lishughulikie hilo. Wakati Luteni Ringo na wenzio, kuna kazi ya kufanya Mtwara mjini.”
“Ipi?”
“Namhitaji Meneja mamlaka ya mapato mkoa.”
“Sawa chifu.”
Maongezi yakahitimika.
Fadhy naye hakuwa mchoyo, aliwafikishia ile taarifa kina Dorice. Kwa sababu ya wepesi wa uhimilivu, wakaangua vilio na kumpa Fadhy zoezi la kuwatuliza. Walitulia walipojisikia wenyewe, baada ya kuamini wameondoa kiasi fulani cha uchungu.
“Tumtaarifu Stella?” Dorice aliuliza.
“Aaah, sio vibaya naye akafahamu. Ukizingatia hatujapata uthibitisho wa moja kwa moja kuwa hili la moto linahusiana na kadhia ya waume zenu katika biashara zao.”
Dorice akapiga simu. Isivyo bahati, hakupatikana hewani.
“Sio kesi, unaweza kumweleza hata baadaye,” Fadhy akamtuliza. Maana kichwa kilishaanza kupata moto na alikwishaanza kulengwa na machozi.
“Shem, toka nifahamu Stella anamiliki simu, sijawahi kimsikia akilalamikia bahari za kuisha chaji.”
“Sasa...,” Fadhy alidakia. Kabla hajahitimisha akapata simu kutoka kwa Askofu Ponera. Hakuchelea kuipokea.
“Ndiyo,” Fadhy alisema.
“Imeshabainika nani amepigwa risasi.”
“Nani?” Fadhy aliuliza kwa shauku.
“Mtoto wa Cheyaya.”
Moyo ukapiga kite kwa mshituko. Wajihi ukambadilika, kiasi cha kuwashtua kina Dorice na kuwajaza hamu wafahamishwe apatiwacho.
“Ina ukweli wowote?” Fadhy aliuliza na kutulia kwa sekunde kadhaa. Bado alikuwa anaichakata ile taarifa. “Nikiwa na maana umeifanyia utafiti ukajihakikishia.”
“Pasi na shaka. Sambamba na hilo, mkusudiwa wetu mbaroni. Cheyaya amekamatwa na askari polisi. Alikuwa hapa hospitalini.”
Fadhy akazidi kunyong'onyea.
“Kuna jambo lolote ninaloweza kufanya kwa idhini yako?” Askofu Ponera akamzindua.
“Askofu, hii vita sio ya kuichukulia poa. Kama wapinzani wetu wanafanya vitendo vya kikatili zaidi ili wafanikishe walifikirialo, basi tuna kazi nzito sana.” Fadhy akainuka, na kupiga hatua ndogondogo akipotelea ushorobani.
Akawaacha kina Dorice mzuka umewapanda.
Fadhy akaendelea, “Nafikiria nini tufanye ili tuwashinde kwa haraka. Maana hiki walichozidi kukifanya hakivumiliki.”
“Kwa hiyo tuwaache tu wakiondoka na huyu?”
“Stella. Tafuta taarifa za kina kumhusu Stella. Nini matokeo ya risasi aliyopigwa.”
“Sawa chifu.”
“Fanya hima ujitahidi.” Fadhy akakata simu. Akarejea sebuleni.
“Kuna tatizo?” Dorice kimuhemuhe akafanya kazi yake. Hakumpooza.
“Halihusiani na hili tunalolishughulikia,” Fadhy akawaongopea.
“Mmh! Shem...”
“Kuna jambo lingine tu linalohusiana na majukumu ya kazi yangu. Kukiwa na utofauti wa hili letu siwezi kuwanyima taarifa zake. Kuweni na amani.”
“Unanifanya nianze kukuogopa. Kwani sura yako inaficha kilichopo moyoni ambacho umetoka kutaarifiwa.”
Wakati wote wa maongezi Fadhy alikuwa amesimama. Baadaye ikambidi ajibweteke sofani, kisha kuwasaili ma-shemeji zake tuo kwa tuo, huku akijipa fikra, aanzaje kuwataarifu ile taarifa ya Stella kupigwa risasi na Cheyaya kukamatwa?
Alichokuwa anakikwepa, ni kuona wanawake hao wanaondoka jijini na kurudi Mangaka. Aliamini, kwa namna yoyote ile, akiwaambia watakuwa na uhitaji huo. Jambo litakalochangia ugumu wa ufanikishaji wa kuwaweka hatiani washukiwa wao.
“Sasa umeamini kuwa lipo unalotuficha?” Dorice akamgutusha.
“Kwa nini umekuwa hivyo shem?”
“Nina uchungu namna uhuru wetu unavyozidi kupotea kila uchao pasi na kosa lolote tulilolifanya. Jitihada zote za upambanaji tulizozifanya hadi kuutwaa ubilionea leo hii tumegeuka wahujumu uchumi kwa sababu tumekataa matakwa yao.
“Nina uchungu na huu uonevu unaozidi kuendelea shem. Kwa nini tunaonewa? Wanatuoneaje? Wanatuoneaje hawa?” alilalama hadi machozi yakaanza kumlenga. Uvumilivu ulipomshinda kilio kikawa nafuu yake.
“Ni lini hao tunaowaamini wataacha uonevu? Wataendelea kuongoza kwa kudhulumu? Au ndiyo miiko ya uongozi inavyotaka eeh?” Dorice aliendelea kulalama.
“Ndiyo maana nimechukua maamuzi ya kushughulikia ili kufutilia mbali dhana hii iliyokita mizizi kila nyanja. Nitaitokomeza, na kujenga nidhamu kwa watumishi wengine. Kupitia hili, litakuwa fundisho kwao,” Fadhy alimtuliza.
Dorice akafuta machozi, kisha akamsaili Fadhy.
“Nakuhakikishia tena, niaminini. Tunaenda kushinda huu mchezo,” alimsisitizia.
TUKUTANE TOLEO LIJALO.