Hassan Mboneche
Member
- Jun 15, 2020
- 61
- 197
RIWAYA: MKOLONI MZAWA—2
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
SEHEMU YA 03.
ROMA, ITALY.
Ulikuwa ni usiku. Kamishna wa intellijensia Barabara Ndirimwe alivyokutana na vijana wa PSU, ambao kwa wakati huo walikuwa kama wahaini. Walikutana kwenye moja ya hoteli ya kifahari nje kidogo ya jiji la Roma.
“Hali si nzuri kule nchini. Nadhani mumewahi kupata taarifa juu ya hilo?” Kamishna Ndirimwe aliongea akiwa anamuangazia mmoja baada ya mwingine.
Walikuwa vijana watatu pekee; Luteni Mwaipeta, Konstebo Babaa na Jackson.
“Yeah! Taarifa tunazo,” walijibu kwa pamoja.
Kamishna Ndirimwe alijikohoza kidogo kisha akaendelea na maongezi, “Kwa sasa amani imekosekana nchini. Nafsi nyingi zimetawaliwa hofu juu ya viongozi wa serikali. Maana wakijaribu tu kukosoa, matokeo wanayokumbana nayo ni adha kubwa.”
“Hivyo lengo la ujio wako ni upi? Maana binafsi kuna tukio limenitokea kiasi kwamba linanipa wakati mgumu,” Luteni Mwaipeta alisema.
“Lipi?” Kamishna Ndirimwe aliuliza kwa shauku.
“Nimeshambuliwa usiku wa jana na mtu nisiyemfahamu. Lakini niliweza kutambua jinsia yake. Alikuwa mwanamke.”
Wengine nao wakachangia matukio yao. Lililowaacha katika sintofahamu ni lile la Konstebo Babaa.
“Ina maana kwamba mumeshashtukiwa? Oooh!...”
“Tueleweshe vyema kiongozi. Kwanza, bado tupo kwenye system?”
Kamishna Ndirimwe hakujibu kwa haraka. Alitulia kwa sekunde chache akionekana kufikiri jambo, alivyolipatia muafaka ndipo alijibu, “Yeah! Bado mupo. Lakini munahesabika kama watoro.”
“Mnh! Tupashe sasa lengo la ujio.”
“Kama ambavyo mumesikia yaendeleayo huko nchini, hali ni mbaya sana. Si wananchi, si viongozi ambao wanaaminiwa na wananchi wanaweza kuwa sehemu ya msaada; wote wapo sehemu moja kwa bwana mkubwa. Hawana amani na uhuru wao. Sasa binafsi nimeonelea kuiondoa hii hali.”
Ukapita ukimya mfupi.
Jackson akaufukuza, “Peke yako?”
“Hapana. Ndiyo maana nimekuja kwenu ili muwe sehemu ya msaada.”
“Unahitaji msaada gani?”
“Nahitaji kurejesha amani ya kila mmoja nchini. Ule uhuru wa kutoa maoni, kukosoa na kutoa ushauri urejee. Ki-ujumla, nahitaji kubadilisha mfumo wa serikali yetu.”
“Mzee, mpango kama huo unawezaje...”
“Mpango wowote huanza na mtu mmoja.”
“Sisi msaada wetu utakuwa wa namna gani?”
“Sasa hivi mzee wa nchi kakamata kila sehemu, lakini hatuwezi kuwakosa washiriki. Wapo wengi tu wenye nia kama yangu, wanashindwa kujitokeza kwa sababu ya woga wanaojazwa.”
“Fafanua basi, nini unataka kifanyike?”
“Nia yangu kama nilivyowaambia awali, kurejesha uhuru wa kila mmoja nchini. Nahitaji kuurejesha uhuru huu kwa msaada wenu na Ndalama Machicho.”
“Tupe full usituhadithie nusu nusu.”
“Rais Sharabu anataka kuwaondoa uraiani wanasiasa wote wenye nguvu mtaani. Ili wakati wa uchaguzi asipate ukinzani mkubwa. Kitendo cha kumweka Ndalama gerezani linadhihirisha hili. Sasa mimi nahitaji nimuondoe Ndalama kule gerezani tuje kushirikiana katika hili. Sifurahishwi na yale yafanywayo na Rais Sharabu. Anawakosea sana watangulizi wake. Hasa kwa kutofuata misingi ya katiba.
“Hivyo nimeandaa kampeni ya kumtoa kwa kumchangia kiasi cha faini alichoambiwa alipe...”
“Wewe ndiyo umeandaa ile harakati?” Luteni Mwaipeta aliuliza kwa mshangao.
“Yeah! Sasa ninyi wajibu wenu ni kurudi nchini ili mukawalinde wakusanyaji wa michango. Nina wasiwasi wanaweza wakawekwa kati na kunyang’anywa, kitendo ambacho kitaniweka katika wakati mgumu. Na ukizingatia sihitaji huu mpango ufeli.”
“Binafsi sitoweza. Nahitaji nimuuguze mke wangu,” Konstebo Babaa alisema.
“Najua. Lakini huu mpango upo kwa ajili ya ukombozi wa wanatuleane. Huna budi kushiriki kwa namna yoyote. Jipe muda ufikirie. Vipi wengine?”
“Binafsi sina pingamizi,” Luteni Mwaipeta alijibu.
“Mimi wajibu wangu utakuwa nini?” Jackson aliuliza.
“Utarudi na kubaki kwenye ujuzi wako. Kuna mahali nimekuandalia. Utaingia hapo ili uwape hamasa wananchi. Maana wengi wao wameshindwa kutambua umuhimu walionao juu ya uamuzi kwa kiongozi wa ki-serikali.”
“Okay!”
“Lazima turejeshe hili hitajio kwa gharama yoyote.”
“Hakika.”
***
Asubuhi ya siku iliyofuata walikutana hospitalini alikolazwa Dc/cpl Amina (Annastazia). Daktari amsimamiaye Dc/cpl Amina (Annastazia) akawaongoza kuingia wodini. Ilivyo bahati, walimkuta amerejewa na fahamu.
“Hongera sana dokta,” Kamishna Ndirimwe alishukuru.
“Ni Mwenyezi Mungu pekee ndiye afaaye kushukuriwa katika hili.” Wakatabasamu.
“Yupo huru kufanya mazungumzo?”
“Yeah! Lakini jitahidini msimchoshe.”
“Hamna shida. Naomba utuachie nafasi.”
Daktari akaondoka.
Wakajipanga vyema kwa kuzunguka kitanda.
Awali, kwa pamoja walimpatia pole. Nyuso zao zikiwa zimetamalaki huzuni iliyoshindwa kuelezeka.
“Mwenyezi Mungu azidi kukujalia heri, upone haraka ili urudi majukumuni.”
“Hakika atajalia,” Dc/cpl Amina (Annastazia) alijibu.
“Tupo hapa kwa mambo mawili; moja, kukutakia hali. Pili, kukupasha yaendeleayo nchini. Naamini kuna machache unayoyafahamu.”
“Yeah!”
“Basi nimekuja kwa lengo la kuwafuata vijana wangu. Lakini nasikitika ewe hautokuwepo awamu hii kutokana na hali uliyonayo.”
Dc/cpl Amina (Annastazia) akatokwa na machozi.
Konstebo Babaa akafuta lile chozi kwa kitambaa chake. Nafsi ikitokota kwa uchungu.
“Natamani nami ningekuwa pamoja.”
“Labda kwa siku zijazo. Maana hali ya sasa haikuruhusu katika ushiriki wowote. Juu ya hilo, bwana mkubwa hataki.”
“Kwa nini?”
“Muulize?”
“Eti kwa nini hutaki mume wangu?”
“Nani atakuuguza nikiondoka?”
“Naamini Kamishna hajakosea hadi awafuate huku. Anajua nini anafanya. Kubaliana naye, sitokosa mtu wa kuniuguza.”
Ukapita ukimya mfupi.
Mwisho, Kamishna Ndirimwe alitoa bahasha mbili katika mfuko wa suruali aliyovaa. Moja alimkabidhi Luteni Mwaipeta, nyingine Konstebo Babaa.
“Babaa, naamini utafanyia kazi. Detective, ugua pole,” Kamishna Ndirimwe aliongea na kuwashtua Luteni Mwaipeta na Jackson waondoke.
Wakaondoka.
Konstebo Babaa akasalia na mkewe mule wodini, wakati wote akiisaili bahasha aliyokabidhiwa.
Muda mfupi baadaye Kamishna Ndirimwe alirejea tena mule wodini.
“Babaa, Mwaipeta anakuhitaji mara moja,” Kamishna Ndirimwe alizungumza.
Konstebo Babaa akatii.
Konstebo Babaa alivyoondoka, Kamishna Ndirimwe alipiga hatua hadi pale alipokuwa amesimama awali. Akaziangazia mboni zake kwa nguvu kumwelekezea Dc/cpl Amina (Annastazia).
“Don’t lose your target,” Kamishna Ndirimwe aliongea kwa msisitizo.
“Ondoa shaka, kila kitu kitakaa kwenye mstari namna kilivyopangwa.”
Kamishna Ndirimwe akaondoka. Konstebo Babaa akarejea wodini. Walipishana mlangoni. Kila mmoja akiwa makini na uelekeo wa mwendo wake.
“Inabidi ufanye ulivyoambiwa. Acha kuniangalia mimi. Kwa sababu nitapona tu kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu. Waangalie wale waliopo nyumbani kwa jicho la tatu, nenda mukawarejeshee kile walichokipoteza kwa ukosefu wa usikivu wa viongozi wetu,” Dc/cpl Amina aliongea. Sauti ikiwa nyenyekevu, iliyojaa ushawishi.
Konstebo Babaa hakujibu. Aliishia kumwangalia mkewe kwa jicho lililoshesheni huruma, huku kwa mbali akilengwa lengwa na machozi.
***
Siku iliyofuata Luteni Mwaipeta na Konstebo Babaa walifunga safari kwa muda tofauti tofauti, kutokana na maelezo waliyoyakuta kwenye bahasha. Hayakuwa maelezo mengi. Yalikuwa machache tu, lakini yaliwapatia ukinzani mkubwa wa kutambua yanamaanisha nini.
Juu ya maelezo hayo, walikutana na tiketi walizotumia kusafiria. Jackson aliondoka na Kamishna Ndirimwe.
“5+4” Huu ndiyo ujumbe aliokutana nao Konstebo Babaa.
Luteni Mwaipeta alikutana na ujumbe uliosomeka, “5+5”
Ilikuwa changanyikeni. Kwani ilisumbua sana akili zao.
Luteni Mwaipeta ndiye alikuwa wa kwanza kuwasili jijini Nufaiko. Mara baada ya kuteremka ndani ya ndege na kukamilisha taratibu zote za ki-usalama alichanja mbuga kutafuta uelekeo. Alivyofika eneo la mapokezi ya wasafiri wanaowasili, aliangaza huku na kule, akamuona kijana mmoja amebeba bango lililoandikwa ile namba aliyokuta kwenye ujumbe aliopatiwa. 5+5.
Akasita kuendelea na safari. Akamwangalia yule kijana aliyebeba lile bango huku akiwazua nini afanye. Baadaye alikata shauri, akaamua kumfuata.
“Karibu sana,” yule kijana alimlaki. Wakati huo huo akipokea begi la Luteni Mwaipeta. Lilikuwa begi dogo la kuvaa mgongoni.
Hatimaye wakaongozana.
Walivyofikia eneo la maegesho waliingia kwenye gari fulani na kuondoka. Ilikuwa Range rover vogue, yenye rangi nyeusi, iliyopambwa kwa tinted zenye rangi nyeusi pia.
Hiyo ilikuwa alfajiri.
Baada ya mwendo wa dakika kadhaa waliripoti kwenye jengo moja katikati ya jiji. Maeneo ya Bondeni. Waliteremka, kisha wakaongozana kuingia ndani ya jengo hilo. Lililotoa picha ya wazi kuwa ni ofisi.
“Ingia mlango namba kumi,” yule mpokezi alimwambia Luteni Mwaipeta pindi akimkabidhi lile begi lake.
Luteni Mwaipeta akafanya kama alivyoamriwa. Cha kushangaza, kile chumba kilitawaliwa na kiza cha kuogofya. Akatamani awashe taa, lakini pindi akiwa kwenye harakati za kutafuta swichi sauti iliyojaa ngurumo ikamshtua.
“Hupaswi kufanya hivyo.” Akatulia.
“Naomba unikabidhi ujumbe uliopatiwa,” ile sauti ilijirudia kwa mara nyingine. Ilikuwa kama inatoka mtungini. Na muongeaji hakuwa ndani ya kile chumba.
Luteni Mwaipeta alifungua begi na kuitoa ile bahasha.
“Weka juu ya meza.”
Pale aliposimama, mbele yake kulikuwa na meza.
Kila alichoambiwa hakupinga. Alitii kwa haraka kwa sababu ya ukerehekaji uliojaa nafsini mwake kutokana na kile kiza. Hivyo alitamani mambo yaende haraka ili apate kuondoka.
“Kifuatacho?” Luteni Mwaipeta aliuliza.
“Upo tayari kwa kazi?”
“Yeah!”
“Okay! Chukua bahasha uionayo hapo mezani. Jitahidi, uhakikishe unampatia ulinzi huyo mtu. Ulinzi wa nguvu, lakini usibainike. Kwani ndiyo sehemu nyingine ya kuelekea ukombozi wa wanatuleane kuwarejeshea uhuru wao.”
Luteni Mwaipeta akaichukua ile bahasha na kuiweka ndani ya begi.
“Sasa unaweza kuondoka.”
Akaondoka.
Alipofika nje alipokelewa na yule kijana aliyempokea uwanja wa ndege. Akamuongoza aingie kwenye gari na kuondoka. Walihitimisha safari yao nje kidogo ya maeneo yale yale ya Bondeni, katika hoteli ya Nyangenyange.
Jambo la kwanza kufanya baada ya kuingia kwenye chumba chake katika ile hoteli, aliitoa begini ile bahasha aliyoambiwa aifanyie kazi. Aliisaili, na kukutana na maandishi machache pale juu. Yaliyoandikwa, ROAD TO LIBERATION. Akaifungua.
Ndani ya bahasha alikutana na picha ya mnato. Picha ya mtu anayemfahamu. Kidogo ilimshangaza.
“Inawezekanaje?” alijiuliza. Akiwa katumbua pima mboni zake kumsaili yule mtu amuonaye.
Ni picha imuonyeshayo Makamu Mwenyekiti wa chama cha Chautu, Ndg. Patrick Babigamba.
Alijiuliza maswali mengi kumuhusu, lakini hakuna hata moja alilolipatia ufumbuzi. Mwisho, alichukua simu na kumpigia Kamishna Ndirimwe.
“Naamini umeshafika,” sauti ya upande wa pili ilisikika. Mara baada ya simu kupokelewa. Sauti ya Kamishna Ndirimwe.
“Yap! Lakini...”
Akakatishwa kabla hajamalizia, “Huo ndiyo mpango mkakati. Kikubwa kuutekeleza. Ewe fuata kila utaratibu utaokapatiwa, ndiyo mafanikio yenyewe hayo.”
“Naweza kukuanimi?”
“Exactly!” Kamishna Ndirimwe aliongea na kukata simu.
Luteni Mwaipeta hakuitoa ile simu sikioni juu ya kuwa ilishakatwa. Usaili wa picha ulimpa butwaa asilolitarajia.
Baadaye alivyozinduka, aliirudisha picha begini akawasha runinga. Aliweka kwenye moja ya idhaa nchini, akakutana na taarifa ya dharura. Iliyobeba ujumbe, Makamu Mwenyekiti wa chama cha Chautu akimbizwa hospitali ya Litunu baada ya kuanguka ghafla ofisini kwake. Akatega sikio vyema kuisikiliza.
“...kwa maelezo ya awali, baadaya kufanyiwa uchunguzi, inasadikika kiongozi huyo amekutwa na sumu mwilini mwake, hivyo...” ilikuwa sehemu ya maelezo ya mtangazaji aliyekuwa anaripoti habari hiyo.
Luteni Mwaipeta alivuta pumzi na kuzitua kwa nguvu akiwa anaachia kiungambali na kuketi kitandani. Habari ilizidi kumtatanisha. Akavuta begi na kuitoa ile picha kwa mara nyingine. Taratibu, akaanza kuisaili upya.
“There is something which is not right,” alijisemeza. Akizidi kuichunguza ile picha.
Huyo ndiyo mtu aliyeambiwa ampatie ulinzi. Ana nini cha muhimu hadi apatiwe ulinzi? Hakujua.
ITAENDELEA...
MTUNZI: HASSAN MBONECHE
SEHEMU YA 03.
ROMA, ITALY.
Ulikuwa ni usiku. Kamishna wa intellijensia Barabara Ndirimwe alivyokutana na vijana wa PSU, ambao kwa wakati huo walikuwa kama wahaini. Walikutana kwenye moja ya hoteli ya kifahari nje kidogo ya jiji la Roma.
“Hali si nzuri kule nchini. Nadhani mumewahi kupata taarifa juu ya hilo?” Kamishna Ndirimwe aliongea akiwa anamuangazia mmoja baada ya mwingine.
Walikuwa vijana watatu pekee; Luteni Mwaipeta, Konstebo Babaa na Jackson.
“Yeah! Taarifa tunazo,” walijibu kwa pamoja.
Kamishna Ndirimwe alijikohoza kidogo kisha akaendelea na maongezi, “Kwa sasa amani imekosekana nchini. Nafsi nyingi zimetawaliwa hofu juu ya viongozi wa serikali. Maana wakijaribu tu kukosoa, matokeo wanayokumbana nayo ni adha kubwa.”
“Hivyo lengo la ujio wako ni upi? Maana binafsi kuna tukio limenitokea kiasi kwamba linanipa wakati mgumu,” Luteni Mwaipeta alisema.
“Lipi?” Kamishna Ndirimwe aliuliza kwa shauku.
“Nimeshambuliwa usiku wa jana na mtu nisiyemfahamu. Lakini niliweza kutambua jinsia yake. Alikuwa mwanamke.”
Wengine nao wakachangia matukio yao. Lililowaacha katika sintofahamu ni lile la Konstebo Babaa.
“Ina maana kwamba mumeshashtukiwa? Oooh!...”
“Tueleweshe vyema kiongozi. Kwanza, bado tupo kwenye system?”
Kamishna Ndirimwe hakujibu kwa haraka. Alitulia kwa sekunde chache akionekana kufikiri jambo, alivyolipatia muafaka ndipo alijibu, “Yeah! Bado mupo. Lakini munahesabika kama watoro.”
“Mnh! Tupashe sasa lengo la ujio.”
“Kama ambavyo mumesikia yaendeleayo huko nchini, hali ni mbaya sana. Si wananchi, si viongozi ambao wanaaminiwa na wananchi wanaweza kuwa sehemu ya msaada; wote wapo sehemu moja kwa bwana mkubwa. Hawana amani na uhuru wao. Sasa binafsi nimeonelea kuiondoa hii hali.”
Ukapita ukimya mfupi.
Jackson akaufukuza, “Peke yako?”
“Hapana. Ndiyo maana nimekuja kwenu ili muwe sehemu ya msaada.”
“Unahitaji msaada gani?”
“Nahitaji kurejesha amani ya kila mmoja nchini. Ule uhuru wa kutoa maoni, kukosoa na kutoa ushauri urejee. Ki-ujumla, nahitaji kubadilisha mfumo wa serikali yetu.”
“Mzee, mpango kama huo unawezaje...”
“Mpango wowote huanza na mtu mmoja.”
“Sisi msaada wetu utakuwa wa namna gani?”
“Sasa hivi mzee wa nchi kakamata kila sehemu, lakini hatuwezi kuwakosa washiriki. Wapo wengi tu wenye nia kama yangu, wanashindwa kujitokeza kwa sababu ya woga wanaojazwa.”
“Fafanua basi, nini unataka kifanyike?”
“Nia yangu kama nilivyowaambia awali, kurejesha uhuru wa kila mmoja nchini. Nahitaji kuurejesha uhuru huu kwa msaada wenu na Ndalama Machicho.”
“Tupe full usituhadithie nusu nusu.”
“Rais Sharabu anataka kuwaondoa uraiani wanasiasa wote wenye nguvu mtaani. Ili wakati wa uchaguzi asipate ukinzani mkubwa. Kitendo cha kumweka Ndalama gerezani linadhihirisha hili. Sasa mimi nahitaji nimuondoe Ndalama kule gerezani tuje kushirikiana katika hili. Sifurahishwi na yale yafanywayo na Rais Sharabu. Anawakosea sana watangulizi wake. Hasa kwa kutofuata misingi ya katiba.
“Hivyo nimeandaa kampeni ya kumtoa kwa kumchangia kiasi cha faini alichoambiwa alipe...”
“Wewe ndiyo umeandaa ile harakati?” Luteni Mwaipeta aliuliza kwa mshangao.
“Yeah! Sasa ninyi wajibu wenu ni kurudi nchini ili mukawalinde wakusanyaji wa michango. Nina wasiwasi wanaweza wakawekwa kati na kunyang’anywa, kitendo ambacho kitaniweka katika wakati mgumu. Na ukizingatia sihitaji huu mpango ufeli.”
“Binafsi sitoweza. Nahitaji nimuuguze mke wangu,” Konstebo Babaa alisema.
“Najua. Lakini huu mpango upo kwa ajili ya ukombozi wa wanatuleane. Huna budi kushiriki kwa namna yoyote. Jipe muda ufikirie. Vipi wengine?”
“Binafsi sina pingamizi,” Luteni Mwaipeta alijibu.
“Mimi wajibu wangu utakuwa nini?” Jackson aliuliza.
“Utarudi na kubaki kwenye ujuzi wako. Kuna mahali nimekuandalia. Utaingia hapo ili uwape hamasa wananchi. Maana wengi wao wameshindwa kutambua umuhimu walionao juu ya uamuzi kwa kiongozi wa ki-serikali.”
“Okay!”
“Lazima turejeshe hili hitajio kwa gharama yoyote.”
“Hakika.”
***
Asubuhi ya siku iliyofuata walikutana hospitalini alikolazwa Dc/cpl Amina (Annastazia). Daktari amsimamiaye Dc/cpl Amina (Annastazia) akawaongoza kuingia wodini. Ilivyo bahati, walimkuta amerejewa na fahamu.
“Hongera sana dokta,” Kamishna Ndirimwe alishukuru.
“Ni Mwenyezi Mungu pekee ndiye afaaye kushukuriwa katika hili.” Wakatabasamu.
“Yupo huru kufanya mazungumzo?”
“Yeah! Lakini jitahidini msimchoshe.”
“Hamna shida. Naomba utuachie nafasi.”
Daktari akaondoka.
Wakajipanga vyema kwa kuzunguka kitanda.
Awali, kwa pamoja walimpatia pole. Nyuso zao zikiwa zimetamalaki huzuni iliyoshindwa kuelezeka.
“Mwenyezi Mungu azidi kukujalia heri, upone haraka ili urudi majukumuni.”
“Hakika atajalia,” Dc/cpl Amina (Annastazia) alijibu.
“Tupo hapa kwa mambo mawili; moja, kukutakia hali. Pili, kukupasha yaendeleayo nchini. Naamini kuna machache unayoyafahamu.”
“Yeah!”
“Basi nimekuja kwa lengo la kuwafuata vijana wangu. Lakini nasikitika ewe hautokuwepo awamu hii kutokana na hali uliyonayo.”
Dc/cpl Amina (Annastazia) akatokwa na machozi.
Konstebo Babaa akafuta lile chozi kwa kitambaa chake. Nafsi ikitokota kwa uchungu.
“Natamani nami ningekuwa pamoja.”
“Labda kwa siku zijazo. Maana hali ya sasa haikuruhusu katika ushiriki wowote. Juu ya hilo, bwana mkubwa hataki.”
“Kwa nini?”
“Muulize?”
“Eti kwa nini hutaki mume wangu?”
“Nani atakuuguza nikiondoka?”
“Naamini Kamishna hajakosea hadi awafuate huku. Anajua nini anafanya. Kubaliana naye, sitokosa mtu wa kuniuguza.”
Ukapita ukimya mfupi.
Mwisho, Kamishna Ndirimwe alitoa bahasha mbili katika mfuko wa suruali aliyovaa. Moja alimkabidhi Luteni Mwaipeta, nyingine Konstebo Babaa.
“Babaa, naamini utafanyia kazi. Detective, ugua pole,” Kamishna Ndirimwe aliongea na kuwashtua Luteni Mwaipeta na Jackson waondoke.
Wakaondoka.
Konstebo Babaa akasalia na mkewe mule wodini, wakati wote akiisaili bahasha aliyokabidhiwa.
Muda mfupi baadaye Kamishna Ndirimwe alirejea tena mule wodini.
“Babaa, Mwaipeta anakuhitaji mara moja,” Kamishna Ndirimwe alizungumza.
Konstebo Babaa akatii.
Konstebo Babaa alivyoondoka, Kamishna Ndirimwe alipiga hatua hadi pale alipokuwa amesimama awali. Akaziangazia mboni zake kwa nguvu kumwelekezea Dc/cpl Amina (Annastazia).
“Don’t lose your target,” Kamishna Ndirimwe aliongea kwa msisitizo.
“Ondoa shaka, kila kitu kitakaa kwenye mstari namna kilivyopangwa.”
Kamishna Ndirimwe akaondoka. Konstebo Babaa akarejea wodini. Walipishana mlangoni. Kila mmoja akiwa makini na uelekeo wa mwendo wake.
“Inabidi ufanye ulivyoambiwa. Acha kuniangalia mimi. Kwa sababu nitapona tu kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu. Waangalie wale waliopo nyumbani kwa jicho la tatu, nenda mukawarejeshee kile walichokipoteza kwa ukosefu wa usikivu wa viongozi wetu,” Dc/cpl Amina aliongea. Sauti ikiwa nyenyekevu, iliyojaa ushawishi.
Konstebo Babaa hakujibu. Aliishia kumwangalia mkewe kwa jicho lililoshesheni huruma, huku kwa mbali akilengwa lengwa na machozi.
***
Siku iliyofuata Luteni Mwaipeta na Konstebo Babaa walifunga safari kwa muda tofauti tofauti, kutokana na maelezo waliyoyakuta kwenye bahasha. Hayakuwa maelezo mengi. Yalikuwa machache tu, lakini yaliwapatia ukinzani mkubwa wa kutambua yanamaanisha nini.
Juu ya maelezo hayo, walikutana na tiketi walizotumia kusafiria. Jackson aliondoka na Kamishna Ndirimwe.
“5+4” Huu ndiyo ujumbe aliokutana nao Konstebo Babaa.
Luteni Mwaipeta alikutana na ujumbe uliosomeka, “5+5”
Ilikuwa changanyikeni. Kwani ilisumbua sana akili zao.
Luteni Mwaipeta ndiye alikuwa wa kwanza kuwasili jijini Nufaiko. Mara baada ya kuteremka ndani ya ndege na kukamilisha taratibu zote za ki-usalama alichanja mbuga kutafuta uelekeo. Alivyofika eneo la mapokezi ya wasafiri wanaowasili, aliangaza huku na kule, akamuona kijana mmoja amebeba bango lililoandikwa ile namba aliyokuta kwenye ujumbe aliopatiwa. 5+5.
Akasita kuendelea na safari. Akamwangalia yule kijana aliyebeba lile bango huku akiwazua nini afanye. Baadaye alikata shauri, akaamua kumfuata.
“Karibu sana,” yule kijana alimlaki. Wakati huo huo akipokea begi la Luteni Mwaipeta. Lilikuwa begi dogo la kuvaa mgongoni.
Hatimaye wakaongozana.
Walivyofikia eneo la maegesho waliingia kwenye gari fulani na kuondoka. Ilikuwa Range rover vogue, yenye rangi nyeusi, iliyopambwa kwa tinted zenye rangi nyeusi pia.
Hiyo ilikuwa alfajiri.
Baada ya mwendo wa dakika kadhaa waliripoti kwenye jengo moja katikati ya jiji. Maeneo ya Bondeni. Waliteremka, kisha wakaongozana kuingia ndani ya jengo hilo. Lililotoa picha ya wazi kuwa ni ofisi.
“Ingia mlango namba kumi,” yule mpokezi alimwambia Luteni Mwaipeta pindi akimkabidhi lile begi lake.
Luteni Mwaipeta akafanya kama alivyoamriwa. Cha kushangaza, kile chumba kilitawaliwa na kiza cha kuogofya. Akatamani awashe taa, lakini pindi akiwa kwenye harakati za kutafuta swichi sauti iliyojaa ngurumo ikamshtua.
“Hupaswi kufanya hivyo.” Akatulia.
“Naomba unikabidhi ujumbe uliopatiwa,” ile sauti ilijirudia kwa mara nyingine. Ilikuwa kama inatoka mtungini. Na muongeaji hakuwa ndani ya kile chumba.
Luteni Mwaipeta alifungua begi na kuitoa ile bahasha.
“Weka juu ya meza.”
Pale aliposimama, mbele yake kulikuwa na meza.
Kila alichoambiwa hakupinga. Alitii kwa haraka kwa sababu ya ukerehekaji uliojaa nafsini mwake kutokana na kile kiza. Hivyo alitamani mambo yaende haraka ili apate kuondoka.
“Kifuatacho?” Luteni Mwaipeta aliuliza.
“Upo tayari kwa kazi?”
“Yeah!”
“Okay! Chukua bahasha uionayo hapo mezani. Jitahidi, uhakikishe unampatia ulinzi huyo mtu. Ulinzi wa nguvu, lakini usibainike. Kwani ndiyo sehemu nyingine ya kuelekea ukombozi wa wanatuleane kuwarejeshea uhuru wao.”
Luteni Mwaipeta akaichukua ile bahasha na kuiweka ndani ya begi.
“Sasa unaweza kuondoka.”
Akaondoka.
Alipofika nje alipokelewa na yule kijana aliyempokea uwanja wa ndege. Akamuongoza aingie kwenye gari na kuondoka. Walihitimisha safari yao nje kidogo ya maeneo yale yale ya Bondeni, katika hoteli ya Nyangenyange.
Jambo la kwanza kufanya baada ya kuingia kwenye chumba chake katika ile hoteli, aliitoa begini ile bahasha aliyoambiwa aifanyie kazi. Aliisaili, na kukutana na maandishi machache pale juu. Yaliyoandikwa, ROAD TO LIBERATION. Akaifungua.
Ndani ya bahasha alikutana na picha ya mnato. Picha ya mtu anayemfahamu. Kidogo ilimshangaza.
“Inawezekanaje?” alijiuliza. Akiwa katumbua pima mboni zake kumsaili yule mtu amuonaye.
Ni picha imuonyeshayo Makamu Mwenyekiti wa chama cha Chautu, Ndg. Patrick Babigamba.
Alijiuliza maswali mengi kumuhusu, lakini hakuna hata moja alilolipatia ufumbuzi. Mwisho, alichukua simu na kumpigia Kamishna Ndirimwe.
“Naamini umeshafika,” sauti ya upande wa pili ilisikika. Mara baada ya simu kupokelewa. Sauti ya Kamishna Ndirimwe.
“Yap! Lakini...”
Akakatishwa kabla hajamalizia, “Huo ndiyo mpango mkakati. Kikubwa kuutekeleza. Ewe fuata kila utaratibu utaokapatiwa, ndiyo mafanikio yenyewe hayo.”
“Naweza kukuanimi?”
“Exactly!” Kamishna Ndirimwe aliongea na kukata simu.
Luteni Mwaipeta hakuitoa ile simu sikioni juu ya kuwa ilishakatwa. Usaili wa picha ulimpa butwaa asilolitarajia.
Baadaye alivyozinduka, aliirudisha picha begini akawasha runinga. Aliweka kwenye moja ya idhaa nchini, akakutana na taarifa ya dharura. Iliyobeba ujumbe, Makamu Mwenyekiti wa chama cha Chautu akimbizwa hospitali ya Litunu baada ya kuanguka ghafla ofisini kwake. Akatega sikio vyema kuisikiliza.
“...kwa maelezo ya awali, baadaya kufanyiwa uchunguzi, inasadikika kiongozi huyo amekutwa na sumu mwilini mwake, hivyo...” ilikuwa sehemu ya maelezo ya mtangazaji aliyekuwa anaripoti habari hiyo.
Luteni Mwaipeta alivuta pumzi na kuzitua kwa nguvu akiwa anaachia kiungambali na kuketi kitandani. Habari ilizidi kumtatanisha. Akavuta begi na kuitoa ile picha kwa mara nyingine. Taratibu, akaanza kuisaili upya.
“There is something which is not right,” alijisemeza. Akizidi kuichunguza ile picha.
Huyo ndiyo mtu aliyeambiwa ampatie ulinzi. Ana nini cha muhimu hadi apatiwe ulinzi? Hakujua.
ITAENDELEA...