Riwaya magnum22

Riwaya magnum22

MAGNUM 22

Sehemu 23

Kutoka Barabara ya Alem Gena, Chiba aliendelea kupekua kompyuta yake ndogo huku akiwa kamwachia Gina usukani. Kimya kati yao kilikuwa kama wimbo usio na mwisho kwa muda huo. Giza nalo lilikuwa limechachamaa na kuzifanya taa za barabarani kupendeza kwa rangi yake ya dhahabu.
“Moyo wangu unanambia Amata hayupo salama!” Gina akasema huku akiwa amekilaza kiti chake.
“Hapa namwona alikuwa Barabara ya Daleti na sasa anamove sijajua anaelekea wapi,” Chiba akamwambia Gina.
“Kwa nini asitupe taarifa kuwa anatoka? Hapana Chiba!” Gina akawasha gari na kulirudisha barabarani, “Nipe uelekeo,” akamwambia Chiba.
“Subiri wanakuja upande huu huu!” akamjibu na Gina akatulia lakini gari lilikuwa likiunguruma. Dakika kama saba hivi baadae, magari manne ya polisi yakawapita kwa kasi, Chiba akatazama kompyuta yake na ndipo akagundua kuwa katika magari hayo yumo Amata.
“Fuata hayo magari ya polisi!” akamwambia na Gina hakupoteza muda akaingia barabarani na kufuata nyuma. Wakiwa njiani, saa ya Chiba ikamfinya katika mkono wake wa kushoto, akainua mkono na kuitazama, ikamwonesha mwanga hafifu wa kuashiria kuna ujumbe. Saa hiyo haikutoa ujumbe wowote wa maandishi ila iliendelea kuwaka mwanga ule hafifu. Chiba akaelewa ni nini maana yake.
“Amata yupo kwenye matatizo,” akamwambia Gina.
“Ametumia kodi gani?” Gina akauliza.
“Red Code!”
“Unafikiri atakuwa kachukuliwa na polisi?”
“Bila shaka!”
Dakika kama ishirini na sita hivi, yale magari ya polisi yakaingia katika kituo kikubwa cha Akaki Kality, katikati tu ya jiji hilo. Gina ikambidi akunje kona na kuingia mtaa mwingine kadiri ya sheria ya barabara hiyo ilivyomtaka na alipozunguka akajikuta katokea upande mwingine.
“Tutajiridhisha vipi kuwa yumo?” Gina akauliza.
“Namwona hapa yupo kituoni,” Chiba akajibu.
“Ah useng* huu sasa, kazi yote itaharibika sasa na tuna saa chache sana kutoka sasa,” Gina akaongea kwa hasira yenye gadhabu.
“Tulia Gina, maadam yupo kwenye mikono ya polisi, basi yuko salama, cha muhimu sasa tufanye utaratibu wa kumpata…”
“Ni sawa Chiba, ila sasa lipi tutafanya, kumshughulikia Amata au kuendelea kuwanasa akina Gupter?”
“Huo ndiyo mtihani maana hapa sasa ni sawa na mwalimu akuulize A na B ipi kubwa, any way, tutumie busara, hatuwezi kwenda kituoni, ila hatuna budi kuripoti kwa Balozi ili hatua za kidiplomasia zifanyike…”
XIII
SIKU ILIYOFUATA
SIKU HII BARABARA ZA ADDIS Ababa hazikuwa zikipitika kwani viongozi wan chi za Afrika walikuwa wakipita kuelekea mkutanoni wakisindikizwa na pikipiki nyingi za polisi. Wanausalama wa kila aina walikuwapo, askari wa farasi, mbwa na wale watembeao kwa miguu nao walikuwapo ili mradi ‘usalama umeimarishwa’. Siku hii, shughuli nyingi za usafiri ziliathiriwa na kimuhemuhe hiki.
Asubuhi hii ya saa nne ilimkuta Amanda Keller katika Barabara ndogo ya Roosevelt, akiegesha gari lake kadiri ya maelekezo ya askari kisha akateremka na kamera yake akifuatiwa na kijana mwingine mwenye kifaa kama cha kunasa sauti. Mavazi waliyovaa usingekuwa na swali kutaka kujua kuwa hawa ni waandishi wa habari, tena wa shirika fulani kubwa huko Ughaibuni. Mwendo wao ulikuwa waharakaharaka huku wakisindikizwa na askari wawili waliokuwa wakiwasaidia kupita kirahisi katika makundi makubwa ya wanaharakati waliokuja na mabango yao kufikisha jumbe anuai kwa viongozi wao.
‘Free Somaliland’ (Somaliland iwe huru) mabango mengi yalisomeka namna hii kwa sababu katika kikao hiki licha ya kuwa na agenda nyingine ndogo ndogo, hii ilikuwa kubwa zaidi na ndiyo iliyosubiriwa na wengi katika kona za dunia.
‘How long shall kill our leaders while we stand aside and look?’ (mpaka lini wataua viongozi wetu na sisi tumesimama pembeni tukiangalia?) bango jingine kubwa liliandikwa.
Mara baada ya kuwasili katika lango kuu la jengo hilo la kisasa, Amanda na mwenzake wakakaguliwa na walipoonekana wapo ‘Clean’ wakaruhusiwa kuungana na wanahabari wengine. Hawakuchelewa, waliwahi dakika kama ishirini kabla ya kikao kuanza.
Ndani ya ukumbi huu kulikuwa na watu wachache kwenye viti, hawa walikuwa ni kama wasikilizaji au wawakilishi wa mashirika fulani fulani. Upande mwingine ambako ndiko haswa kamera nyingi zilielekezwa bado viti vilikuwa wazi, wahusika hawakuwa wameingia tayari nah ii ndiyo ilikuwa itifaki ya siku zote. Kila mtu alikuwa na kabrasha mkononi mwake akipekua kurasa hii na ile, akisoma hiki na kile.
Amanda na Martin, ndani ya jingo hili hawakugundulika kabisa kama wao ni kenge kati ya msafara wa mamba. Kwa jinsi walivyojibadili sura na mionekano yao, ingekuwa ngumu sana kwa askari wa kawaida kama hawa kuwagundua, hata wao walilijua hilo na ndiyo maana hawakuogopa hata kidogo. Hawakuwa na nia ya kupiga picha wala kuandika habari japo waliijua vyema kazi hiyo. Hapa walikuja kutazama ni jinsi gani uzito wa ulinzi uliopo kwa viongozi hawa na pia kupata uhakika nini hasa umoja huu utaamua kuhusu kuigawa Somalia vipande viwili, na hili ndilo hasa lilikuwa ni mkataba kwao wenye pesa nyingi sana toka kwa tajiri Jaffer Bakhari.
Muda ulipofika viongozi wakaingia na kuketi kwenye viti vyao na kisha muongoza shughuli akaanza kuongea maneno machache ikiwamo kutambulisha waliokuwamo ukumbini humo na kutoa mwongozo wa shughuli nzima kwa ujumla.
Wakati huo huo Gina na Chiba walifikia uamuzi wa kuacha kila kitu na kulivalia njuga swala la Amata wakishirikiana na maofisa wa ubalozi wa Tanzania. Wao hawakutaka kuwaambia polisi wa jiji hilo kuwa huyo waliyemfunga ni nani bali walitaka kumtoa kama mwanadiplomasia, lakini ilikuwa ngumu kwani mkuu wa kituo hicho alidai kuwa amri aliyopewa ni kumshikiria mpaka atakapohojiwa na watu wa usalama wa AU. Shughuli ikawa si ndogo kituoni hapo, mwisho wa yote ikaonekana, Amata ashikiliwe kwa sababu amewekwa hapo na kamati ya usalama ya AU na hakuna nchi yenye sauti juu ya umoja huo isipokuwa umoja wenyewe juu ya nchi zake.
Kwa hasira ambayo Gina na Chiba iliwakaba kooni laity wangekuwa na grenade wangelipua kituo hicho.
“Ok, nafikiri, muendelee na shughuli nyinge na baada ya mkutano tutafanya mazungumzo na watu wa usalama, ataachiwa huru tu maadam Ubalozi tuna taarifa!” afisa mmoka akawaambia akina Gina na wao wakakubaliana naye kwa kuwa hawakuwa na la kufanya, wakaingia garini na kundoka huku wakiwa kimya.
“Sasa tunaanzia wapi? Maana mi kichwa change kimeshavurugwa!” Gina akasema.
“Kwenye mkutano!” Chiba akajibu na wote wakaelekea huko. Mnamo saa saba mchana ndipo walipowasili nnje ya jingo hilo na kukuta umati wa watu umezagaa huku polisi wakiwa katika kazi nzito ya kuwaweka sawa. Kundi kubwa lilionekana likipiga kelele na kunyanyua mabango juu yaliyosomeka ‘Free Somaliland’.
“Kumekucha kaka! Sasa kwa vurugu hii huyu Gupter akiamua si anadungua kiurahisi tu!” Gina akasema huku akichukua darubini yake na kuangalia majengo yaliyozunguka eneo hilo akiwa ndani ya gari.
“Tuteremke, twende tukapande katika jingo hili kisha tuangalie huku…”
“Tugawane, na tutakayemhisi tu tule naye sahani moja,” Gina akapendekeza. Wakateremka garini na kuvaa vifaa vyao vya mawasiliano, wakatawanyika kila mtu eneo analoona lingemfaa.
“Vipi huko, kuna chochote?” Chiba akauliza baada ya dakika kama kumi hivi.
“Huku ni clean kabisa!” Gina akajibu. Chiba licha ya kuwa alikuwa akiwasiliana na Gina bado alikuwa na mashine ndogo iliyoweza kukamata mawimbi yoyote ya mawasiliano yanayopita hewani. Akaendelea kuahangaika kuzungusha nobu kidogo kidogo huku akiwasiliana na Gina. Wakati bado askari wakituliza ghasia nje ya ukumbi huo, akanasa sauti ambazo zilikuja na kupotea.
“…we have to accomplish the task ova!” (tunatakiwa kumaliza kazi)
“…target! Target!...ova” (lengo! Lengo)
“…target the table in black color…ova” (lengo meza kwenye rangi nyeusi)
“To the nest to the nest, retreat” (kiotani, kiotani) sauti ya kike ikaingilia kati, kisha Chiba akasikia mawimbi yakikatika.
Wamestuka! Akina nani hawa? Akajiuliza. Wakati akiwaza hayo ving’ora vya magari ya polisi vikasikika, tayari misafara ikaanza kuondoka eneo hilo. Chiba akatoka alipoketi na kumpa ishara Gina kisha wote wakakutana garini.
“NImenasa mawasiliano ambayo sijayaelewa,” Chiba akasema huku akimsikilizisha Gina kauli zile chache. Wakajaribu kuweka mawazo pamoja kuona kama wanaweza kugundua maana yoyote katika mzungumzo hayo, wakashindwa, walichoambulia tu ni kugundua kuwa wazungumzaji wamegundua kuwa wamenaswa hivyo wakazima mtambo.
* * *
Mara baada ya kikao kile kumalizika bila ya muafaka wowote juu ya ajenda ya kuigawa nchi ya Somalia, jopo la wajumbe waliokuwa wakidai uhuru wa nchi yao waliamua kuondoka bila kuaga na kufanya kikao hicho kisiwe na maana kwa waliobaki. Kiongozi wa mkutano huo, rais wa Gambia aliamua kukivunja kwa kuwa upande mmoja wa mazungumzo uliondoka ukumbini.
Baada ya kutoka, moja kwa moja walikwenda uwanja wa ndege tayari kwa safari ya kurudi walikotoka. Kiongozi wa msafara huo Bwana Fadicky hakusema chochote hata alipobembelezwa na wanaitifaki wa AU, hakutaka kuwasikiliza aliwajibu kwa kauli mja tu, “Damu haitakauka Somalia mpaka mtupatie ardhi yetu,” hata alipokutana na mwenyekiti wa umoja huo mara baada ya mambo kuvurugika alimjibu maneno tata, “Hamtaki kukubali, nasi hatuachi,” kisha akaondoka zake.
Nje ya jingo hilo la makao makuu ambako kikao hicho kilikuwa kikifanyika, watu walikuwa wakisubiri kujua hasa ni nini kitafikiwa muafaka, vurugu zikazuka pale waliposikia kuwa hoja hiyo imetupiliwa mbali na Somalia itabaki kuwa moja.
Maili zaidi ya 10000 kutoka katika jengo hilo, katika jiji la Abu Dhabi, Jaffer Bakhari alijikuta mapigo ya moyo yakishuka, kijasho chembamba kikimtiririka, ugumu wa kutoa sauti ukamfika. Vijana wake kwa haraka wakaita madaktari wake na kuanza kumshughulikia mara moja. Hali hii ilitokana na taarifa ambayo hakuitegemea kutoka kwa mtu aliyemtuma huko Addis Ababa. Jaffer katika harakati zake, tayari alikuwa amekwishapanga kila kitu kuhusu serikali ya Somalia mpya yeye mwenyewe akiwa rais, na kutokana na utajiri wake tayari alikuwa ametenga kiasi kikubwa cha dolari kwa kuiendesha nchi hiyo huku akiahidiwa zaidi na wadau wake kuboresha elimu, afya, miundombinu na kadhalika. Lakini jibu la kikao hicho kuwa Somalia itabaki kuwa moja lilimuongezea shida na kuamsha magonjwa yaliyojificha.
“Unalopaswa kutenda, litende haraka!” ilikuwa kauli ya Jaffer akiwa kitandani akiongea na simu na mtu aliye upande wa pili. Ndani ya chumba hicho alikuwa peke yake kwa kuwa hakutaka kuwe na mtu yeyote yule wakati akiongea na simu hiyo.
Sasa wataujutia uamuzi wao, jeshi langu litaingia na kuisumbua Afrika mpaka ukamilifu wa dahari! Jaffer akawaza akiwa kitandani huku mashine zikiendelea kusoma mienendo ya viungo anuai vya mwili wake.
* * *
Martin Gupter akaitua simu yake na kuiweka juu ya dashboard, akamtazama Fredy aliyekuwa akiendesha kwa umakini wa hali ya juu na Amanda ambaye alionekana amechoka sana.
“Jamani tunatakiwa kufunga kazi hii mapema iwezekanavyo, Fredy umeshajiweka tayari?” Martin akauliza
“Tayari!” Fredy akajibu.
“Amanda! Vipi upo sawa?”
“Yes! Naye akajibu.
“Ok! Sasa mimi najua nini nitafanya cha muhimu jinsi tutakavyotoka humu nchini naomba kila mmoja ajipange, safari hii tukitumia gari moja itatugharimu, ni bora kutawanyika…” martin akapendekeza.
“Usiingilie kazi za watu, we fanya kazi ukimaliza nikute pale pale nilipokwambia, mi ndo najua nini natakiwa kufanya kukuokoeni ninyi, na kama wakitugundua mi najiuzulu kazi hii…” Fredy akasema wakati akiegesha gari kando ya bustani kubwa iliyo pembezoni mwa mji huo.
“Nahitaji kutengeza sumu mbaya kabisa kwa ajili ya kuwamaliza wabaya wetu!” Martin akaeleza.
“Safari hii sumu?” Amanda akaeelza.
“Ndiyo! Nataka nimmalize kwa sumu….”
“Hapana Martin mi naona huyu ni wa kumdungua tu, kwa sumu inaweza kutuletea shida na kukamatwa…” Fredy akasema.
“Anyway, nipeni muda nifikiri, dakika kumi tu!”
“Mimi nilishakuandalia kila kitu!” Amanda akasema. Martin akageuka na kumtazama, “Kila kitu?” akauliza.
“Yes! Njoo…” Amanda akamwita Martin, wakazunguka nyuma ya gari na Fredy akafungua buti. Ndani ya buti hilo kulikuwa na kasha kubwa tu lililotengenezwa kwa mbao. Amanda akakamata mfuniko na kuufungua, akauweka kando. Gupter hakuamini anachokiona bunduki mpya, kubwa, ilikuwa imelala kimya huku kikasha kidogo cha risasi kikiwa kando, ndani ya kasha kubwa. Martin akamatazama Amanda.
“Unanipa risasi ngapi?” akamuuliza Amanda.
“Moja tu, najua shabaha yako haikosei,” Amanda akamjibu na kijana huyo akafunga buti.
“Turudi mjini!” akawaambia wenzake.
* * *
Ofisi Nyeti ya Usalama Addis
“Nashangaa ni vipi muuaji ameshindwa kufika, na nilimpania nimtie nguvuni, yaani angejuta kuzaliwa dume,” mmoja wa wajumbe wa kamati ya usalama akawaambia wenzake.
“Ameogopa, anajua kwa vyovyote angefika hapa hasingechomoka,” mwingine akadakia.
“Kwa kweli, hata kama hajaja atasakwa tu, huyu waliyemkamata jana sijaelewa habari yake imekaaje!” mwingine akaongeza kusema.
“Mmmh huyu wamemuhisi tu, lakini inaonekana Mr. M ana uhakika kuwa huyu jamaa ana data za muuaji, kwa sababu katuambia kuwa hata tafutishi za wale vijana zimemtaja sana huyu kuanzia Angola, Ivory Coast cha kushangaza inasemekana ni Mtanzania…” mjumbe wa kwanza akasema na wakati huo huo Mr. M akaingia kikaoni.
“Wajumbe hatuna haja ya kuchelewa, bado tnahitaji kuimarisha ulizi kila mmoja katika upande wake maana kuanzi saa tisa alasiri, viongozi watawasili katika Hoteli ya Golden Tulip kwa ajili ya chakula cha pamoja. Mwanzoni ilipangwa kuwa mlo huu maalum ufanyike usiku lakini watu wa itifaki na mipango wamebadili kwa kuwa wanasema viongozi wengi wataanza kuondoka saa mbili usiku. La pili ni kuwa, jana tumemkamata mtu mwenye data nyingi kuhusu muuaji na inaonekana ndiye master plan wa mipango hii, yeye yupo kituoni na tutashughulika naye pindi tu viongozi wote watakapoondoka, hata hivyo kutokana na usalama wa kituo kile nimeamua ahamishwe na kupelekwa kwenye kituo kingine chenye ulinzi mkali zaidi,” Mr. M akawaambia huku kijasho kikimvuja na kuvunja kikao ili kila mmoja aingie majukumuni.
* * *
KITUO CHA POLISI – AKAKI KALITY
Kamanda Amata alikuwa kimya katika selo aliyofungiwa, akiwa kajilaza sakafuni na macho kayafumba akijaribu kukusanya wazo hili na lile, labda atapata lingine. Mara akastuliwa na sauti ya viatru vitambeavyo kuelekea uande huo. Kwa haraka haraka alisikiliza sauti zile akajua ni watu watano wanaokuja. Mara ikatulia na ukimya ukarejea, akainua uso kutazama, naam, mlangoni kulikuwa na watu watano, askari wa kawaida wenye virungu wawili, na wawili walikuwa na pingu na mnyororo na mmoja alionekana kuwa ni afisa kwa jinsi alivyovaa.
“We gaidi, amka!” yule askari akamwamuru Amata, naye akatii maana alikumbuka kauli mbiu ya jeshi la polisi la kwao Tanzania ‘Tii sheri bila shuruti’, “Mtieni disprin!” akawaambia vijana wake.
Wale vijana wawili wenye virungu wakafungua lile lango la chuma na kuingia ndani kisha wakaanza kumsulubu Amata sehemu mbalimbali za mwili kwa virungu vile na kumwacha hoi bin taaban. Baada ya kipigo hicho kilichodumu dakika kama tatu hivi wakaingia wengine na kumfunga pingu mikononi na ule mnyororo miguuni wakamwinua na kuanza kumkokota akiwa peku na suruali tu juu kifua wazi. Japokuwa aipigwa sana tangu usiku uliotangulia, Amata hakutetereka sana kwa sababu tayari mwili wake ulishajengwa katika mazingira ya uvumilivu na hiyo ni moja ya mafunzo yao, kuufanya mwili kuwa mkakamavu na wenye kuvumilia shida na maumivu. Nje ya kituo kulikuwa tayari na gari lililoandaliwa maalum kumbeba, akaingizwa ndani na mikono yake yote ikafungwa kwenye chuma maalumu ndani ya gari hilo huku wale askari waliokuwa wakimsulubu wakiketi nyuma kabisa ya gari hilo umbali kama wa mita moja hivi kutoka alipo yeye. Milango ikafungwa na lile gari likaondoka huku likisindikizwa na ving’ora vya polisi nyuma na mbele.
* * *
Gina aliendesha gari taratibu kwenye barabara za jiji la Addis huku kichwani akiwa na mawazo lukuki. Chiba yeye alikuwa ametingwa na kwenye kompyuta yake ndogo huku akiwa na kifaa cha kusikiliza masikioni mwake.
“Uelekeo!” Gina akasema.
“Tunarudi ubalozini, lazima tuhakikishe tunampata Amata leo, kwanza mpaka sasa wamevuruga utaratibu wetu,” akamwambia Gina.
“Kwa hiyo tuachane na ‘kina Gupter?”
“Sasa tufanyeje, mi nafikiri tuache kila kitu tumpate Amata, kwa maana yeye tukimpata huyo mwendazimu Gupter tutamsaka tu,” akamjibu.
“Sawa!”
Wakiwa katika mazungumzo hayo, simu ya Chiba ikaita, akainyakuwa na kuitazama, “Madam S!” akatamka.
“Mh!” Gina akaguna.
“TSA 2!” Chiba akaitika.
“HOT! Sikio?”
“Sikio zima,” Chiba akaitikia kwa fumbo.
“Nini kimempata Amata?”
“Amechukuliwa na wanausalama wa AU,”
“Imani…”
“Hatuna!”
“Uelekeo…”
“Cameroon Street, Addis,”
“TSA 1 kwetu ni muhimu kuliko upumbavu mwingine, sitisha kila misheni mhakikishe mmempata kwa gharama yoyote, kisha nipe jibu… ova and out!” Madam S akamaliza.
“Copy!”
Mazungumzo ya Chiba na bosi wake yakakamilika, akamtazama Gina akiingiza gari katika Mtaa wa Cameroon ambako ubalozi wa Tanzania ulipo. Hawakupata shida kuingia ubalozini hapo kwa kuwa walitumia vitambulisho vyao vya uraia na vingine vya kazi ambavyo bado vilificha uhalisia wa kazi yao. Katika ofisi hizo walikutana na afisa mmoja anayefanya kazi ya kuhakikisha usalama wa Watanzania waishio nchini hapo.
“Swala la huyu bwana tunalifuatilia, na nimepata ujumbe kuwa ataachiwa lakini si leo, labda kesho…”
“Shiiiiiitttt!”
“…hata hivyo hivi sasa tunavyoongea anatakiwa kuhamishwa kutoka pale na kupelekwa mahala pengine kuhifadhiwa kwa ajili ya mahojiano zaidi…”
“Noooo! Haiwezekani!” Chiba akaongea huku amesimama, sura yake ilinesha wazi makwinyanzi ya hasira.
“Kwani, ninyi ni nani hasa hata mumtake huyu mtu leo? Kwa sababu sisi tuna utaratibu wetu wa kidiplomasia na kuna taratibu za kufuata ili kumtoa, lakini kwa kesi yake ambayo imefanya akamatwe, tutakuwa na kazi ngumu kumpata kwa sababu yupo chini ya kamati ya usalama ya AU wenyewe…” yule bwana akaeleza vizuri kabisa.
“Sawa, tutakuja kesho ili tujue kinachoendelea…”Chiba akamwambia yule afisa na kupeana mikono huku wakikaribishwa tena.
Nje ya ofisi zile, Chiba akamtazama Gina kabla hawajaingia garini.
“Sasa?” Gina akauliza.
“Sasa ni kumsaka Amata kufa na kupona, na ni lazima tumpate,” Chiba akasema huku akiingia garini, akawasha kifaa chake ambacho humsaidia kujua wapi mtu yeyote wa TSA yupo kwa wakati huo endapo tu bado atakuwasha kifaa chake cha kumuunganisha na wenzake ambavyo huwekwa ama kwenye saa, au simu, ikibidi sana mwilini.
“Gina, fuata barabara ya Airport haraka, naona signal inanionesha huko…” Chiba akasema na mwanamke huyo akakanyaga mafuta kufuata uelekeo aliyoambiwa.
 
MAGNUM 22

Sehemu 23

Kutoka Barabara ya Alem Gena, Chiba aliendelea kupekua kompyuta yake ndogo huku akiwa kamwachia Gina usukani. Kimya kati yao kilikuwa kama wimbo usio na mwisho kwa muda huo. Giza nalo lilikuwa limechachamaa na kuzifanya taa za barabarani kupendeza kwa rangi yake ya dhahabu.
“Moyo wangu unanambia Amata hayupo salama!” Gina akasema huku akiwa amekilaza kiti chake.
“Hapa namwona alikuwa Barabara ya Daleti na sasa anamove sijajua anaelekea wapi,” Chiba akamwambia Gina.
“Kwa nini asitupe taarifa kuwa anatoka? Hapana Chiba!” Gina akawasha gari na kulirudisha barabarani, “Nipe uelekeo,” akamwambia Chiba.
“Subiri wanakuja upande huu huu!” akamjibu na Gina akatulia lakini gari lilikuwa likiunguruma. Dakika kama saba hivi baadae, magari manne ya polisi yakawapita kwa kasi, Chiba akatazama kompyuta yake na ndipo akagundua kuwa katika magari hayo yumo Amata.
“Fuata hayo magari ya polisi!” akamwambia na Gina hakupoteza muda akaingia barabarani na kufuata nyuma. Wakiwa njiani, saa ya Chiba ikamfinya katika mkono wake wa kushoto, akainua mkono na kuitazama, ikamwonesha mwanga hafifu wa kuashiria kuna ujumbe. Saa hiyo haikutoa ujumbe wowote wa maandishi ila iliendelea kuwaka mwanga ule hafifu. Chiba akaelewa ni nini maana yake.
“Amata yupo kwenye matatizo,” akamwambia Gina.
“Ametumia kodi gani?” Gina akauliza.
“Red Code!”
“Unafikiri atakuwa kachukuliwa na polisi?”
“Bila shaka!”
Dakika kama ishirini na sita hivi, yale magari ya polisi yakaingia katika kituo kikubwa cha Akaki Kality, katikati tu ya jiji hilo. Gina ikambidi akunje kona na kuingia mtaa mwingine kadiri ya sheria ya barabara hiyo ilivyomtaka na alipozunguka akajikuta katokea upande mwingine.
“Tutajiridhisha vipi kuwa yumo?” Gina akauliza.
“Namwona hapa yupo kituoni,” Chiba akajibu.
“Ah useng* huu sasa, kazi yote itaharibika sasa na tuna saa chache sana kutoka sasa,” Gina akaongea kwa hasira yenye gadhabu.
“Tulia Gina, maadam yupo kwenye mikono ya polisi, basi yuko salama, cha muhimu sasa tufanye utaratibu wa kumpata…”
“Ni sawa Chiba, ila sasa lipi tutafanya, kumshughulikia Amata au kuendelea kuwanasa akina Gupter?”
“Huo ndiyo mtihani maana hapa sasa ni sawa na mwalimu akuulize A na B ipi kubwa, any way, tutumie busara, hatuwezi kwenda kituoni, ila hatuna budi kuripoti kwa Balozi ili hatua za kidiplomasia zifanyike…”
XIII
SIKU ILIYOFUATA
SIKU HII BARABARA ZA ADDIS Ababa hazikuwa zikipitika kwani viongozi wan chi za Afrika walikuwa wakipita kuelekea mkutanoni wakisindikizwa na pikipiki nyingi za polisi. Wanausalama wa kila aina walikuwapo, askari wa farasi, mbwa na wale watembeao kwa miguu nao walikuwapo ili mradi ‘usalama umeimarishwa’. Siku hii, shughuli nyingi za usafiri ziliathiriwa na kimuhemuhe hiki.
Asubuhi hii ya saa nne ilimkuta Amanda Keller katika Barabara ndogo ya Roosevelt, akiegesha gari lake kadiri ya maelekezo ya askari kisha akateremka na kamera yake akifuatiwa na kijana mwingine mwenye kifaa kama cha kunasa sauti. Mavazi waliyovaa usingekuwa na swali kutaka kujua kuwa hawa ni waandishi wa habari, tena wa shirika fulani kubwa huko Ughaibuni. Mwendo wao ulikuwa waharakaharaka huku wakisindikizwa na askari wawili waliokuwa wakiwasaidia kupita kirahisi katika makundi makubwa ya wanaharakati waliokuja na mabango yao kufikisha jumbe anuai kwa viongozi wao.
‘Free Somaliland’ (Somaliland iwe huru) mabango mengi yalisomeka namna hii kwa sababu katika kikao hiki licha ya kuwa na agenda nyingine ndogo ndogo, hii ilikuwa kubwa zaidi na ndiyo iliyosubiriwa na wengi katika kona za dunia.
‘How long shall kill our leaders while we stand aside and look?’ (mpaka lini wataua viongozi wetu na sisi tumesimama pembeni tukiangalia?) bango jingine kubwa liliandikwa.
Mara baada ya kuwasili katika lango kuu la jengo hilo la kisasa, Amanda na mwenzake wakakaguliwa na walipoonekana wapo ‘Clean’ wakaruhusiwa kuungana na wanahabari wengine. Hawakuchelewa, waliwahi dakika kama ishirini kabla ya kikao kuanza.
Ndani ya ukumbi huu kulikuwa na watu wachache kwenye viti, hawa walikuwa ni kama wasikilizaji au wawakilishi wa mashirika fulani fulani. Upande mwingine ambako ndiko haswa kamera nyingi zilielekezwa bado viti vilikuwa wazi, wahusika hawakuwa wameingia tayari nah ii ndiyo ilikuwa itifaki ya siku zote. Kila mtu alikuwa na kabrasha mkononi mwake akipekua kurasa hii na ile, akisoma hiki na kile.
Amanda na Martin, ndani ya jingo hili hawakugundulika kabisa kama wao ni kenge kati ya msafara wa mamba. Kwa jinsi walivyojibadili sura na mionekano yao, ingekuwa ngumu sana kwa askari wa kawaida kama hawa kuwagundua, hata wao walilijua hilo na ndiyo maana hawakuogopa hata kidogo. Hawakuwa na nia ya kupiga picha wala kuandika habari japo waliijua vyema kazi hiyo. Hapa walikuja kutazama ni jinsi gani uzito wa ulinzi uliopo kwa viongozi hawa na pia kupata uhakika nini hasa umoja huu utaamua kuhusu kuigawa Somalia vipande viwili, na hili ndilo hasa lilikuwa ni mkataba kwao wenye pesa nyingi sana toka kwa tajiri Jaffer Bakhari.
Muda ulipofika viongozi wakaingia na kuketi kwenye viti vyao na kisha muongoza shughuli akaanza kuongea maneno machache ikiwamo kutambulisha waliokuwamo ukumbini humo na kutoa mwongozo wa shughuli nzima kwa ujumla.
Wakati huo huo Gina na Chiba walifikia uamuzi wa kuacha kila kitu na kulivalia njuga swala la Amata wakishirikiana na maofisa wa ubalozi wa Tanzania. Wao hawakutaka kuwaambia polisi wa jiji hilo kuwa huyo waliyemfunga ni nani bali walitaka kumtoa kama mwanadiplomasia, lakini ilikuwa ngumu kwani mkuu wa kituo hicho alidai kuwa amri aliyopewa ni kumshikiria mpaka atakapohojiwa na watu wa usalama wa AU. Shughuli ikawa si ndogo kituoni hapo, mwisho wa yote ikaonekana, Amata ashikiliwe kwa sababu amewekwa hapo na kamati ya usalama ya AU na hakuna nchi yenye sauti juu ya umoja huo isipokuwa umoja wenyewe juu ya nchi zake.
Kwa hasira ambayo Gina na Chiba iliwakaba kooni laity wangekuwa na grenade wangelipua kituo hicho.
“Ok, nafikiri, muendelee na shughuli nyinge na baada ya mkutano tutafanya mazungumzo na watu wa usalama, ataachiwa huru tu maadam Ubalozi tuna taarifa!” afisa mmoka akawaambia akina Gina na wao wakakubaliana naye kwa kuwa hawakuwa na la kufanya, wakaingia garini na kundoka huku wakiwa kimya.
“Sasa tunaanzia wapi? Maana mi kichwa change kimeshavurugwa!” Gina akasema.
“Kwenye mkutano!” Chiba akajibu na wote wakaelekea huko. Mnamo saa saba mchana ndipo walipowasili nnje ya jingo hilo na kukuta umati wa watu umezagaa huku polisi wakiwa katika kazi nzito ya kuwaweka sawa. Kundi kubwa lilionekana likipiga kelele na kunyanyua mabango juu yaliyosomeka ‘Free Somaliland’.
“Kumekucha kaka! Sasa kwa vurugu hii huyu Gupter akiamua si anadungua kiurahisi tu!” Gina akasema huku akichukua darubini yake na kuangalia majengo yaliyozunguka eneo hilo akiwa ndani ya gari.
“Tuteremke, twende tukapande katika jingo hili kisha tuangalie huku…”
“Tugawane, na tutakayemhisi tu tule naye sahani moja,” Gina akapendekeza. Wakateremka garini na kuvaa vifaa vyao vya mawasiliano, wakatawanyika kila mtu eneo analoona lingemfaa.
“Vipi huko, kuna chochote?” Chiba akauliza baada ya dakika kama kumi hivi.
“Huku ni clean kabisa!” Gina akajibu. Chiba licha ya kuwa alikuwa akiwasiliana na Gina bado alikuwa na mashine ndogo iliyoweza kukamata mawimbi yoyote ya mawasiliano yanayopita hewani. Akaendelea kuahangaika kuzungusha nobu kidogo kidogo huku akiwasiliana na Gina. Wakati bado askari wakituliza ghasia nje ya ukumbi huo, akanasa sauti ambazo zilikuja na kupotea.
“…we have to accomplish the task ova!” (tunatakiwa kumaliza kazi)
“…target! Target!...ova” (lengo! Lengo)
“…target the table in black color…ova” (lengo meza kwenye rangi nyeusi)
“To the nest to the nest, retreat” (kiotani, kiotani) sauti ya kike ikaingilia kati, kisha Chiba akasikia mawimbi yakikatika.
Wamestuka! Akina nani hawa? Akajiuliza. Wakati akiwaza hayo ving’ora vya magari ya polisi vikasikika, tayari misafara ikaanza kuondoka eneo hilo. Chiba akatoka alipoketi na kumpa ishara Gina kisha wote wakakutana garini.
“NImenasa mawasiliano ambayo sijayaelewa,” Chiba akasema huku akimsikilizisha Gina kauli zile chache. Wakajaribu kuweka mawazo pamoja kuona kama wanaweza kugundua maana yoyote katika mzungumzo hayo, wakashindwa, walichoambulia tu ni kugundua kuwa wazungumzaji wamegundua kuwa wamenaswa hivyo wakazima mtambo.
* * *
Mara baada ya kikao kile kumalizika bila ya muafaka wowote juu ya ajenda ya kuigawa nchi ya Somalia, jopo la wajumbe waliokuwa wakidai uhuru wa nchi yao waliamua kuondoka bila kuaga na kufanya kikao hicho kisiwe na maana kwa waliobaki. Kiongozi wa mkutano huo, rais wa Gambia aliamua kukivunja kwa kuwa upande mmoja wa mazungumzo uliondoka ukumbini.
Baada ya kutoka, moja kwa moja walikwenda uwanja wa ndege tayari kwa safari ya kurudi walikotoka. Kiongozi wa msafara huo Bwana Fadicky hakusema chochote hata alipobembelezwa na wanaitifaki wa AU, hakutaka kuwasikiliza aliwajibu kwa kauli mja tu, “Damu haitakauka Somalia mpaka mtupatie ardhi yetu,” hata alipokutana na mwenyekiti wa umoja huo mara baada ya mambo kuvurugika alimjibu maneno tata, “Hamtaki kukubali, nasi hatuachi,” kisha akaondoka zake.
Nje ya jingo hilo la makao makuu ambako kikao hicho kilikuwa kikifanyika, watu walikuwa wakisubiri kujua hasa ni nini kitafikiwa muafaka, vurugu zikazuka pale waliposikia kuwa hoja hiyo imetupiliwa mbali na Somalia itabaki kuwa moja.
Maili zaidi ya 10000 kutoka katika jengo hilo, katika jiji la Abu Dhabi, Jaffer Bakhari alijikuta mapigo ya moyo yakishuka, kijasho chembamba kikimtiririka, ugumu wa kutoa sauti ukamfika. Vijana wake kwa haraka wakaita madaktari wake na kuanza kumshughulikia mara moja. Hali hii ilitokana na taarifa ambayo hakuitegemea kutoka kwa mtu aliyemtuma huko Addis Ababa. Jaffer katika harakati zake, tayari alikuwa amekwishapanga kila kitu kuhusu serikali ya Somalia mpya yeye mwenyewe akiwa rais, na kutokana na utajiri wake tayari alikuwa ametenga kiasi kikubwa cha dolari kwa kuiendesha nchi hiyo huku akiahidiwa zaidi na wadau wake kuboresha elimu, afya, miundombinu na kadhalika. Lakini jibu la kikao hicho kuwa Somalia itabaki kuwa moja lilimuongezea shida na kuamsha magonjwa yaliyojificha.
“Unalopaswa kutenda, litende haraka!” ilikuwa kauli ya Jaffer akiwa kitandani akiongea na simu na mtu aliye upande wa pili. Ndani ya chumba hicho alikuwa peke yake kwa kuwa hakutaka kuwe na mtu yeyote yule wakati akiongea na simu hiyo.
Sasa wataujutia uamuzi wao, jeshi langu litaingia na kuisumbua Afrika mpaka ukamilifu wa dahari! Jaffer akawaza akiwa kitandani huku mashine zikiendelea kusoma mienendo ya viungo anuai vya mwili wake.
* * *
Martin Gupter akaitua simu yake na kuiweka juu ya dashboard, akamtazama Fredy aliyekuwa akiendesha kwa umakini wa hali ya juu na Amanda ambaye alionekana amechoka sana.
“Jamani tunatakiwa kufunga kazi hii mapema iwezekanavyo, Fredy umeshajiweka tayari?” Martin akauliza
“Tayari!” Fredy akajibu.
“Amanda! Vipi upo sawa?”
“Yes! Naye akajibu.
“Ok! Sasa mimi najua nini nitafanya cha muhimu jinsi tutakavyotoka humu nchini naomba kila mmoja ajipange, safari hii tukitumia gari moja itatugharimu, ni bora kutawanyika…” martin akapendekeza.
“Usiingilie kazi za watu, we fanya kazi ukimaliza nikute pale pale nilipokwambia, mi ndo najua nini natakiwa kufanya kukuokoeni ninyi, na kama wakitugundua mi najiuzulu kazi hii…” Fredy akasema wakati akiegesha gari kando ya bustani kubwa iliyo pembezoni mwa mji huo.
“Nahitaji kutengeza sumu mbaya kabisa kwa ajili ya kuwamaliza wabaya wetu!” Martin akaeleza.
“Safari hii sumu?” Amanda akaeelza.
“Ndiyo! Nataka nimmalize kwa sumu….”
“Hapana Martin mi naona huyu ni wa kumdungua tu, kwa sumu inaweza kutuletea shida na kukamatwa…” Fredy akasema.
“Anyway, nipeni muda nifikiri, dakika kumi tu!”
“Mimi nilishakuandalia kila kitu!” Amanda akasema. Martin akageuka na kumtazama, “Kila kitu?” akauliza.
“Yes! Njoo…” Amanda akamwita Martin, wakazunguka nyuma ya gari na Fredy akafungua buti. Ndani ya buti hilo kulikuwa na kasha kubwa tu lililotengenezwa kwa mbao. Amanda akakamata mfuniko na kuufungua, akauweka kando. Gupter hakuamini anachokiona bunduki mpya, kubwa, ilikuwa imelala kimya huku kikasha kidogo cha risasi kikiwa kando, ndani ya kasha kubwa. Martin akamatazama Amanda.
“Unanipa risasi ngapi?” akamuuliza Amanda.
“Moja tu, najua shabaha yako haikosei,” Amanda akamjibu na kijana huyo akafunga buti.
“Turudi mjini!” akawaambia wenzake.
* * *
Ofisi Nyeti ya Usalama Addis
“Nashangaa ni vipi muuaji ameshindwa kufika, na nilimpania nimtie nguvuni, yaani angejuta kuzaliwa dume,” mmoja wa wajumbe wa kamati ya usalama akawaambia wenzake.
“Ameogopa, anajua kwa vyovyote angefika hapa hasingechomoka,” mwingine akadakia.
“Kwa kweli, hata kama hajaja atasakwa tu, huyu waliyemkamata jana sijaelewa habari yake imekaaje!” mwingine akaongeza kusema.
“Mmmh huyu wamemuhisi tu, lakini inaonekana Mr. M ana uhakika kuwa huyu jamaa ana data za muuaji, kwa sababu katuambia kuwa hata tafutishi za wale vijana zimemtaja sana huyu kuanzia Angola, Ivory Coast cha kushangaza inasemekana ni Mtanzania…” mjumbe wa kwanza akasema na wakati huo huo Mr. M akaingia kikaoni.
“Wajumbe hatuna haja ya kuchelewa, bado tnahitaji kuimarisha ulizi kila mmoja katika upande wake maana kuanzi saa tisa alasiri, viongozi watawasili katika Hoteli ya Golden Tulip kwa ajili ya chakula cha pamoja. Mwanzoni ilipangwa kuwa mlo huu maalum ufanyike usiku lakini watu wa itifaki na mipango wamebadili kwa kuwa wanasema viongozi wengi wataanza kuondoka saa mbili usiku. La pili ni kuwa, jana tumemkamata mtu mwenye data nyingi kuhusu muuaji na inaonekana ndiye master plan wa mipango hii, yeye yupo kituoni na tutashughulika naye pindi tu viongozi wote watakapoondoka, hata hivyo kutokana na usalama wa kituo kile nimeamua ahamishwe na kupelekwa kwenye kituo kingine chenye ulinzi mkali zaidi,” Mr. M akawaambia huku kijasho kikimvuja na kuvunja kikao ili kila mmoja aingie majukumuni.
* * *
KITUO CHA POLISI – AKAKI KALITY
Kamanda Amata alikuwa kimya katika selo aliyofungiwa, akiwa kajilaza sakafuni na macho kayafumba akijaribu kukusanya wazo hili na lile, labda atapata lingine. Mara akastuliwa na sauti ya viatru vitambeavyo kuelekea uande huo. Kwa haraka haraka alisikiliza sauti zile akajua ni watu watano wanaokuja. Mara ikatulia na ukimya ukarejea, akainua uso kutazama, naam, mlangoni kulikuwa na watu watano, askari wa kawaida wenye virungu wawili, na wawili walikuwa na pingu na mnyororo na mmoja alionekana kuwa ni afisa kwa jinsi alivyovaa.
“We gaidi, amka!” yule askari akamwamuru Amata, naye akatii maana alikumbuka kauli mbiu ya jeshi la polisi la kwao Tanzania ‘Tii sheri bila shuruti’, “Mtieni disprin!” akawaambia vijana wake.
Wale vijana wawili wenye virungu wakafungua lile lango la chuma na kuingia ndani kisha wakaanza kumsulubu Amata sehemu mbalimbali za mwili kwa virungu vile na kumwacha hoi bin taaban. Baada ya kipigo hicho kilichodumu dakika kama tatu hivi wakaingia wengine na kumfunga pingu mikononi na ule mnyororo miguuni wakamwinua na kuanza kumkokota akiwa peku na suruali tu juu kifua wazi. Japokuwa aipigwa sana tangu usiku uliotangulia, Amata hakutetereka sana kwa sababu tayari mwili wake ulishajengwa katika mazingira ya uvumilivu na hiyo ni moja ya mafunzo yao, kuufanya mwili kuwa mkakamavu na wenye kuvumilia shida na maumivu. Nje ya kituo kulikuwa tayari na gari lililoandaliwa maalum kumbeba, akaingizwa ndani na mikono yake yote ikafungwa kwenye chuma maalumu ndani ya gari hilo huku wale askari waliokuwa wakimsulubu wakiketi nyuma kabisa ya gari hilo umbali kama wa mita moja hivi kutoka alipo yeye. Milango ikafungwa na lile gari likaondoka huku likisindikizwa na ving’ora vya polisi nyuma na mbele.
* * *
Gina aliendesha gari taratibu kwenye barabara za jiji la Addis huku kichwani akiwa na mawazo lukuki. Chiba yeye alikuwa ametingwa na kwenye kompyuta yake ndogo huku akiwa na kifaa cha kusikiliza masikioni mwake.
“Uelekeo!” Gina akasema.
“Tunarudi ubalozini, lazima tuhakikishe tunampata Amata leo, kwanza mpaka sasa wamevuruga utaratibu wetu,” akamwambia Gina.
“Kwa hiyo tuachane na ‘kina Gupter?”
“Sasa tufanyeje, mi nafikiri tuache kila kitu tumpate Amata, kwa maana yeye tukimpata huyo mwendazimu Gupter tutamsaka tu,” akamjibu.
“Sawa!”
Wakiwa katika mazungumzo hayo, simu ya Chiba ikaita, akainyakuwa na kuitazama, “Madam S!” akatamka.
“Mh!” Gina akaguna.
“TSA 2!” Chiba akaitika.
“HOT! Sikio?”
“Sikio zima,” Chiba akaitikia kwa fumbo.
“Nini kimempata Amata?”
“Amechukuliwa na wanausalama wa AU,”
“Imani…”
“Hatuna!”
“Uelekeo…”
“Cameroon Street, Addis,”
“TSA 1 kwetu ni muhimu kuliko upumbavu mwingine, sitisha kila misheni mhakikishe mmempata kwa gharama yoyote, kisha nipe jibu… ova and out!” Madam S akamaliza.
“Copy!”
Mazungumzo ya Chiba na bosi wake yakakamilika, akamtazama Gina akiingiza gari katika Mtaa wa Cameroon ambako ubalozi wa Tanzania ulipo. Hawakupata shida kuingia ubalozini hapo kwa kuwa walitumia vitambulisho vyao vya uraia na vingine vya kazi ambavyo bado vilificha uhalisia wa kazi yao. Katika ofisi hizo walikutana na afisa mmoja anayefanya kazi ya kuhakikisha usalama wa Watanzania waishio nchini hapo.
“Swala la huyu bwana tunalifuatilia, na nimepata ujumbe kuwa ataachiwa lakini si leo, labda kesho…”
“Shiiiiiitttt!”
“…hata hivyo hivi sasa tunavyoongea anatakiwa kuhamishwa kutoka pale na kupelekwa mahala pengine kuhifadhiwa kwa ajili ya mahojiano zaidi…”
“Noooo! Haiwezekani!” Chiba akaongea huku amesimama, sura yake ilinesha wazi makwinyanzi ya hasira.
“Kwani, ninyi ni nani hasa hata mumtake huyu mtu leo? Kwa sababu sisi tuna utaratibu wetu wa kidiplomasia na kuna taratibu za kufuata ili kumtoa, lakini kwa kesi yake ambayo imefanya akamatwe, tutakuwa na kazi ngumu kumpata kwa sababu yupo chini ya kamati ya usalama ya AU wenyewe…” yule bwana akaeleza vizuri kabisa.
“Sawa, tutakuja kesho ili tujue kinachoendelea…”Chiba akamwambia yule afisa na kupeana mikono huku wakikaribishwa tena.
Nje ya ofisi zile, Chiba akamtazama Gina kabla hawajaingia garini.
“Sasa?” Gina akauliza.
“Sasa ni kumsaka Amata kufa na kupona, na ni lazima tumpate,” Chiba akasema huku akiingia garini, akawasha kifaa chake ambacho humsaidia kujua wapi mtu yeyote wa TSA yupo kwa wakati huo endapo tu bado atakuwasha kifaa chake cha kumuunganisha na wenzake ambavyo huwekwa ama kwenye saa, au simu, ikibidi sana mwilini.
“Gina, fuata barabara ya Airport haraka, naona signal inanionesha huko…” Chiba akasema na mwanamke huyo akakanyaga mafuta kufuata uelekeo aliyoambiwa.
Ubarikiwe kulubule
 
Ubarikiwe mpaka ushangae kulubule kiukweli speed yako nimeipenda kila upatapo nafasi unatupia
 
MAGNUM 22

Sehemu 23

Kutoka Barabara ya Alem Gena, Chiba aliendelea kupekua kompyuta yake ndogo huku akiwa kamwachia Gina usukani. Kimya kati yao kilikuwa kama wimbo usio na mwisho kwa muda huo. Giza nalo lilikuwa limechachamaa na kuzifanya taa za barabarani kupendeza kwa rangi yake ya dhahabu.
“Moyo wangu unanambia Amata hayupo salama!” Gina akasema huku akiwa amekilaza kiti chake.
“Hapa namwona alikuwa Barabara ya Daleti na sasa anamove sijajua anaelekea wapi,” Chiba akamwambia Gina.
“Kwa nini asitupe taarifa kuwa anatoka? Hapana Chiba!” Gina akawasha gari na kulirudisha barabarani, “Nipe uelekeo,” akamwambia Chiba.
“Subiri wanakuja upande huu huu!” akamjibu na Gina akatulia lakini gari lilikuwa likiunguruma. Dakika kama saba hivi baadae, magari manne ya polisi yakawapita kwa kasi, Chiba akatazama kompyuta yake na ndipo akagundua kuwa katika magari hayo yumo Amata.
“Fuata hayo magari ya polisi!” akamwambia na Gina hakupoteza muda akaingia barabarani na kufuata nyuma. Wakiwa njiani, saa ya Chiba ikamfinya katika mkono wake wa kushoto, akainua mkono na kuitazama, ikamwonesha mwanga hafifu wa kuashiria kuna ujumbe. Saa hiyo haikutoa ujumbe wowote wa maandishi ila iliendelea kuwaka mwanga ule hafifu. Chiba akaelewa ni nini maana yake.
“Amata yupo kwenye matatizo,” akamwambia Gina.
“Ametumia kodi gani?” Gina akauliza.
“Red Code!”
“Unafikiri atakuwa kachukuliwa na polisi?”
“Bila shaka!”
Dakika kama ishirini na sita hivi, yale magari ya polisi yakaingia katika kituo kikubwa cha Akaki Kality, katikati tu ya jiji hilo. Gina ikambidi akunje kona na kuingia mtaa mwingine kadiri ya sheria ya barabara hiyo ilivyomtaka na alipozunguka akajikuta katokea upande mwingine.
“Tutajiridhisha vipi kuwa yumo?” Gina akauliza.
“Namwona hapa yupo kituoni,” Chiba akajibu.
“Ah useng* huu sasa, kazi yote itaharibika sasa na tuna saa chache sana kutoka sasa,” Gina akaongea kwa hasira yenye gadhabu.
“Tulia Gina, maadam yupo kwenye mikono ya polisi, basi yuko salama, cha muhimu sasa tufanye utaratibu wa kumpata…”
“Ni sawa Chiba, ila sasa lipi tutafanya, kumshughulikia Amata au kuendelea kuwanasa akina Gupter?”
“Huo ndiyo mtihani maana hapa sasa ni sawa na mwalimu akuulize A na B ipi kubwa, any way, tutumie busara, hatuwezi kwenda kituoni, ila hatuna budi kuripoti kwa Balozi ili hatua za kidiplomasia zifanyike…”
XIII
SIKU ILIYOFUATA
SIKU HII BARABARA ZA ADDIS Ababa hazikuwa zikipitika kwani viongozi wan chi za Afrika walikuwa wakipita kuelekea mkutanoni wakisindikizwa na pikipiki nyingi za polisi. Wanausalama wa kila aina walikuwapo, askari wa farasi, mbwa na wale watembeao kwa miguu nao walikuwapo ili mradi ‘usalama umeimarishwa’. Siku hii, shughuli nyingi za usafiri ziliathiriwa na kimuhemuhe hiki.
Asubuhi hii ya saa nne ilimkuta Amanda Keller katika Barabara ndogo ya Roosevelt, akiegesha gari lake kadiri ya maelekezo ya askari kisha akateremka na kamera yake akifuatiwa na kijana mwingine mwenye kifaa kama cha kunasa sauti. Mavazi waliyovaa usingekuwa na swali kutaka kujua kuwa hawa ni waandishi wa habari, tena wa shirika fulani kubwa huko Ughaibuni. Mwendo wao ulikuwa waharakaharaka huku wakisindikizwa na askari wawili waliokuwa wakiwasaidia kupita kirahisi katika makundi makubwa ya wanaharakati waliokuja na mabango yao kufikisha jumbe anuai kwa viongozi wao.
‘Free Somaliland’ (Somaliland iwe huru) mabango mengi yalisomeka namna hii kwa sababu katika kikao hiki licha ya kuwa na agenda nyingine ndogo ndogo, hii ilikuwa kubwa zaidi na ndiyo iliyosubiriwa na wengi katika kona za dunia.
‘How long shall kill our leaders while we stand aside and look?’ (mpaka lini wataua viongozi wetu na sisi tumesimama pembeni tukiangalia?) bango jingine kubwa liliandikwa.
Mara baada ya kuwasili katika lango kuu la jengo hilo la kisasa, Amanda na mwenzake wakakaguliwa na walipoonekana wapo ‘Clean’ wakaruhusiwa kuungana na wanahabari wengine. Hawakuchelewa, waliwahi dakika kama ishirini kabla ya kikao kuanza.
Ndani ya ukumbi huu kulikuwa na watu wachache kwenye viti, hawa walikuwa ni kama wasikilizaji au wawakilishi wa mashirika fulani fulani. Upande mwingine ambako ndiko haswa kamera nyingi zilielekezwa bado viti vilikuwa wazi, wahusika hawakuwa wameingia tayari nah ii ndiyo ilikuwa itifaki ya siku zote. Kila mtu alikuwa na kabrasha mkononi mwake akipekua kurasa hii na ile, akisoma hiki na kile.
Amanda na Martin, ndani ya jingo hili hawakugundulika kabisa kama wao ni kenge kati ya msafara wa mamba. Kwa jinsi walivyojibadili sura na mionekano yao, ingekuwa ngumu sana kwa askari wa kawaida kama hawa kuwagundua, hata wao walilijua hilo na ndiyo maana hawakuogopa hata kidogo. Hawakuwa na nia ya kupiga picha wala kuandika habari japo waliijua vyema kazi hiyo. Hapa walikuja kutazama ni jinsi gani uzito wa ulinzi uliopo kwa viongozi hawa na pia kupata uhakika nini hasa umoja huu utaamua kuhusu kuigawa Somalia vipande viwili, na hili ndilo hasa lilikuwa ni mkataba kwao wenye pesa nyingi sana toka kwa tajiri Jaffer Bakhari.
Muda ulipofika viongozi wakaingia na kuketi kwenye viti vyao na kisha muongoza shughuli akaanza kuongea maneno machache ikiwamo kutambulisha waliokuwamo ukumbini humo na kutoa mwongozo wa shughuli nzima kwa ujumla.
Wakati huo huo Gina na Chiba walifikia uamuzi wa kuacha kila kitu na kulivalia njuga swala la Amata wakishirikiana na maofisa wa ubalozi wa Tanzania. Wao hawakutaka kuwaambia polisi wa jiji hilo kuwa huyo waliyemfunga ni nani bali walitaka kumtoa kama mwanadiplomasia, lakini ilikuwa ngumu kwani mkuu wa kituo hicho alidai kuwa amri aliyopewa ni kumshikiria mpaka atakapohojiwa na watu wa usalama wa AU. Shughuli ikawa si ndogo kituoni hapo, mwisho wa yote ikaonekana, Amata ashikiliwe kwa sababu amewekwa hapo na kamati ya usalama ya AU na hakuna nchi yenye sauti juu ya umoja huo isipokuwa umoja wenyewe juu ya nchi zake.
Kwa hasira ambayo Gina na Chiba iliwakaba kooni laity wangekuwa na grenade wangelipua kituo hicho.
“Ok, nafikiri, muendelee na shughuli nyinge na baada ya mkutano tutafanya mazungumzo na watu wa usalama, ataachiwa huru tu maadam Ubalozi tuna taarifa!” afisa mmoka akawaambia akina Gina na wao wakakubaliana naye kwa kuwa hawakuwa na la kufanya, wakaingia garini na kundoka huku wakiwa kimya.
“Sasa tunaanzia wapi? Maana mi kichwa change kimeshavurugwa!” Gina akasema.
“Kwenye mkutano!” Chiba akajibu na wote wakaelekea huko. Mnamo saa saba mchana ndipo walipowasili nnje ya jingo hilo na kukuta umati wa watu umezagaa huku polisi wakiwa katika kazi nzito ya kuwaweka sawa. Kundi kubwa lilionekana likipiga kelele na kunyanyua mabango juu yaliyosomeka ‘Free Somaliland’.
“Kumekucha kaka! Sasa kwa vurugu hii huyu Gupter akiamua si anadungua kiurahisi tu!” Gina akasema huku akichukua darubini yake na kuangalia majengo yaliyozunguka eneo hilo akiwa ndani ya gari.
“Tuteremke, twende tukapande katika jingo hili kisha tuangalie huku…”
“Tugawane, na tutakayemhisi tu tule naye sahani moja,” Gina akapendekeza. Wakateremka garini na kuvaa vifaa vyao vya mawasiliano, wakatawanyika kila mtu eneo analoona lingemfaa.
“Vipi huko, kuna chochote?” Chiba akauliza baada ya dakika kama kumi hivi.
“Huku ni clean kabisa!” Gina akajibu. Chiba licha ya kuwa alikuwa akiwasiliana na Gina bado alikuwa na mashine ndogo iliyoweza kukamata mawimbi yoyote ya mawasiliano yanayopita hewani. Akaendelea kuahangaika kuzungusha nobu kidogo kidogo huku akiwasiliana na Gina. Wakati bado askari wakituliza ghasia nje ya ukumbi huo, akanasa sauti ambazo zilikuja na kupotea.
“…we have to accomplish the task ova!” (tunatakiwa kumaliza kazi)
“…target! Target!...ova” (lengo! Lengo)
“…target the table in black color…ova” (lengo meza kwenye rangi nyeusi)
“To the nest to the nest, retreat” (kiotani, kiotani) sauti ya kike ikaingilia kati, kisha Chiba akasikia mawimbi yakikatika.
Wamestuka! Akina nani hawa? Akajiuliza. Wakati akiwaza hayo ving’ora vya magari ya polisi vikasikika, tayari misafara ikaanza kuondoka eneo hilo. Chiba akatoka alipoketi na kumpa ishara Gina kisha wote wakakutana garini.
“NImenasa mawasiliano ambayo sijayaelewa,” Chiba akasema huku akimsikilizisha Gina kauli zile chache. Wakajaribu kuweka mawazo pamoja kuona kama wanaweza kugundua maana yoyote katika mzungumzo hayo, wakashindwa, walichoambulia tu ni kugundua kuwa wazungumzaji wamegundua kuwa wamenaswa hivyo wakazima mtambo.
* * *
Mara baada ya kikao kile kumalizika bila ya muafaka wowote juu ya ajenda ya kuigawa nchi ya Somalia, jopo la wajumbe waliokuwa wakidai uhuru wa nchi yao waliamua kuondoka bila kuaga na kufanya kikao hicho kisiwe na maana kwa waliobaki. Kiongozi wa mkutano huo, rais wa Gambia aliamua kukivunja kwa kuwa upande mmoja wa mazungumzo uliondoka ukumbini.
Baada ya kutoka, moja kwa moja walikwenda uwanja wa ndege tayari kwa safari ya kurudi walikotoka. Kiongozi wa msafara huo Bwana Fadicky hakusema chochote hata alipobembelezwa na wanaitifaki wa AU, hakutaka kuwasikiliza aliwajibu kwa kauli mja tu, “Damu haitakauka Somalia mpaka mtupatie ardhi yetu,” hata alipokutana na mwenyekiti wa umoja huo mara baada ya mambo kuvurugika alimjibu maneno tata, “Hamtaki kukubali, nasi hatuachi,” kisha akaondoka zake.
Nje ya jingo hilo la makao makuu ambako kikao hicho kilikuwa kikifanyika, watu walikuwa wakisubiri kujua hasa ni nini kitafikiwa muafaka, vurugu zikazuka pale waliposikia kuwa hoja hiyo imetupiliwa mbali na Somalia itabaki kuwa moja.
Maili zaidi ya 10000 kutoka katika jengo hilo, katika jiji la Abu Dhabi, Jaffer Bakhari alijikuta mapigo ya moyo yakishuka, kijasho chembamba kikimtiririka, ugumu wa kutoa sauti ukamfika. Vijana wake kwa haraka wakaita madaktari wake na kuanza kumshughulikia mara moja. Hali hii ilitokana na taarifa ambayo hakuitegemea kutoka kwa mtu aliyemtuma huko Addis Ababa. Jaffer katika harakati zake, tayari alikuwa amekwishapanga kila kitu kuhusu serikali ya Somalia mpya yeye mwenyewe akiwa rais, na kutokana na utajiri wake tayari alikuwa ametenga kiasi kikubwa cha dolari kwa kuiendesha nchi hiyo huku akiahidiwa zaidi na wadau wake kuboresha elimu, afya, miundombinu na kadhalika. Lakini jibu la kikao hicho kuwa Somalia itabaki kuwa moja lilimuongezea shida na kuamsha magonjwa yaliyojificha.
“Unalopaswa kutenda, litende haraka!” ilikuwa kauli ya Jaffer akiwa kitandani akiongea na simu na mtu aliye upande wa pili. Ndani ya chumba hicho alikuwa peke yake kwa kuwa hakutaka kuwe na mtu yeyote yule wakati akiongea na simu hiyo.
Sasa wataujutia uamuzi wao, jeshi langu litaingia na kuisumbua Afrika mpaka ukamilifu wa dahari! Jaffer akawaza akiwa kitandani huku mashine zikiendelea kusoma mienendo ya viungo anuai vya mwili wake.
* * *
Martin Gupter akaitua simu yake na kuiweka juu ya dashboard, akamtazama Fredy aliyekuwa akiendesha kwa umakini wa hali ya juu na Amanda ambaye alionekana amechoka sana.
“Jamani tunatakiwa kufunga kazi hii mapema iwezekanavyo, Fredy umeshajiweka tayari?” Martin akauliza
“Tayari!” Fredy akajibu.
“Amanda! Vipi upo sawa?”
“Yes! Naye akajibu.
“Ok! Sasa mimi najua nini nitafanya cha muhimu jinsi tutakavyotoka humu nchini naomba kila mmoja ajipange, safari hii tukitumia gari moja itatugharimu, ni bora kutawanyika…” martin akapendekeza.
“Usiingilie kazi za watu, we fanya kazi ukimaliza nikute pale pale nilipokwambia, mi ndo najua nini natakiwa kufanya kukuokoeni ninyi, na kama wakitugundua mi najiuzulu kazi hii…” Fredy akasema wakati akiegesha gari kando ya bustani kubwa iliyo pembezoni mwa mji huo.
“Nahitaji kutengeza sumu mbaya kabisa kwa ajili ya kuwamaliza wabaya wetu!” Martin akaeleza.
“Safari hii sumu?” Amanda akaeelza.
“Ndiyo! Nataka nimmalize kwa sumu….”
“Hapana Martin mi naona huyu ni wa kumdungua tu, kwa sumu inaweza kutuletea shida na kukamatwa…” Fredy akasema.
“Anyway, nipeni muda nifikiri, dakika kumi tu!”
“Mimi nilishakuandalia kila kitu!” Amanda akasema. Martin akageuka na kumtazama, “Kila kitu?” akauliza.
“Yes! Njoo…” Amanda akamwita Martin, wakazunguka nyuma ya gari na Fredy akafungua buti. Ndani ya buti hilo kulikuwa na kasha kubwa tu lililotengenezwa kwa mbao. Amanda akakamata mfuniko na kuufungua, akauweka kando. Gupter hakuamini anachokiona bunduki mpya, kubwa, ilikuwa imelala kimya huku kikasha kidogo cha risasi kikiwa kando, ndani ya kasha kubwa. Martin akamatazama Amanda.
“Unanipa risasi ngapi?” akamuuliza Amanda.
“Moja tu, najua shabaha yako haikosei,” Amanda akamjibu na kijana huyo akafunga buti.
“Turudi mjini!” akawaambia wenzake.
* * *
Ofisi Nyeti ya Usalama Addis
“Nashangaa ni vipi muuaji ameshindwa kufika, na nilimpania nimtie nguvuni, yaani angejuta kuzaliwa dume,” mmoja wa wajumbe wa kamati ya usalama akawaambia wenzake.
“Ameogopa, anajua kwa vyovyote angefika hapa hasingechomoka,” mwingine akadakia.
“Kwa kweli, hata kama hajaja atasakwa tu, huyu waliyemkamata jana sijaelewa habari yake imekaaje!” mwingine akaongeza kusema.
“Mmmh huyu wamemuhisi tu, lakini inaonekana Mr. M ana uhakika kuwa huyu jamaa ana data za muuaji, kwa sababu katuambia kuwa hata tafutishi za wale vijana zimemtaja sana huyu kuanzia Angola, Ivory Coast cha kushangaza inasemekana ni Mtanzania…” mjumbe wa kwanza akasema na wakati huo huo Mr. M akaingia kikaoni.
“Wajumbe hatuna haja ya kuchelewa, bado tnahitaji kuimarisha ulizi kila mmoja katika upande wake maana kuanzi saa tisa alasiri, viongozi watawasili katika Hoteli ya Golden Tulip kwa ajili ya chakula cha pamoja. Mwanzoni ilipangwa kuwa mlo huu maalum ufanyike usiku lakini watu wa itifaki na mipango wamebadili kwa kuwa wanasema viongozi wengi wataanza kuondoka saa mbili usiku. La pili ni kuwa, jana tumemkamata mtu mwenye data nyingi kuhusu muuaji na inaonekana ndiye master plan wa mipango hii, yeye yupo kituoni na tutashughulika naye pindi tu viongozi wote watakapoondoka, hata hivyo kutokana na usalama wa kituo kile nimeamua ahamishwe na kupelekwa kwenye kituo kingine chenye ulinzi mkali zaidi,” Mr. M akawaambia huku kijasho kikimvuja na kuvunja kikao ili kila mmoja aingie majukumuni.
* * *
KITUO CHA POLISI – AKAKI KALITY
Kamanda Amata alikuwa kimya katika selo aliyofungiwa, akiwa kajilaza sakafuni na macho kayafumba akijaribu kukusanya wazo hili na lile, labda atapata lingine. Mara akastuliwa na sauti ya viatru vitambeavyo kuelekea uande huo. Kwa haraka haraka alisikiliza sauti zile akajua ni watu watano wanaokuja. Mara ikatulia na ukimya ukarejea, akainua uso kutazama, naam, mlangoni kulikuwa na watu watano, askari wa kawaida wenye virungu wawili, na wawili walikuwa na pingu na mnyororo na mmoja alionekana kuwa ni afisa kwa jinsi alivyovaa.
“We gaidi, amka!” yule askari akamwamuru Amata, naye akatii maana alikumbuka kauli mbiu ya jeshi la polisi la kwao Tanzania ‘Tii sheri bila shuruti’, “Mtieni disprin!” akawaambia vijana wake.
Wale vijana wawili wenye virungu wakafungua lile lango la chuma na kuingia ndani kisha wakaanza kumsulubu Amata sehemu mbalimbali za mwili kwa virungu vile na kumwacha hoi bin taaban. Baada ya kipigo hicho kilichodumu dakika kama tatu hivi wakaingia wengine na kumfunga pingu mikononi na ule mnyororo miguuni wakamwinua na kuanza kumkokota akiwa peku na suruali tu juu kifua wazi. Japokuwa aipigwa sana tangu usiku uliotangulia, Amata hakutetereka sana kwa sababu tayari mwili wake ulishajengwa katika mazingira ya uvumilivu na hiyo ni moja ya mafunzo yao, kuufanya mwili kuwa mkakamavu na wenye kuvumilia shida na maumivu. Nje ya kituo kulikuwa tayari na gari lililoandaliwa maalum kumbeba, akaingizwa ndani na mikono yake yote ikafungwa kwenye chuma maalumu ndani ya gari hilo huku wale askari waliokuwa wakimsulubu wakiketi nyuma kabisa ya gari hilo umbali kama wa mita moja hivi kutoka alipo yeye. Milango ikafungwa na lile gari likaondoka huku likisindikizwa na ving’ora vya polisi nyuma na mbele.
* * *
Gina aliendesha gari taratibu kwenye barabara za jiji la Addis huku kichwani akiwa na mawazo lukuki. Chiba yeye alikuwa ametingwa na kwenye kompyuta yake ndogo huku akiwa na kifaa cha kusikiliza masikioni mwake.
“Uelekeo!” Gina akasema.
“Tunarudi ubalozini, lazima tuhakikishe tunampata Amata leo, kwanza mpaka sasa wamevuruga utaratibu wetu,” akamwambia Gina.
“Kwa hiyo tuachane na ‘kina Gupter?”
“Sasa tufanyeje, mi nafikiri tuache kila kitu tumpate Amata, kwa maana yeye tukimpata huyo mwendazimu Gupter tutamsaka tu,” akamjibu.
“Sawa!”
Wakiwa katika mazungumzo hayo, simu ya Chiba ikaita, akainyakuwa na kuitazama, “Madam S!” akatamka.
“Mh!” Gina akaguna.
“TSA 2!” Chiba akaitika.
“HOT! Sikio?”
“Sikio zima,” Chiba akaitikia kwa fumbo.
“Nini kimempata Amata?”
“Amechukuliwa na wanausalama wa AU,”
“Imani…”
“Hatuna!”
“Uelekeo…”
“Cameroon Street, Addis,”
“TSA 1 kwetu ni muhimu kuliko upumbavu mwingine, sitisha kila misheni mhakikishe mmempata kwa gharama yoyote, kisha nipe jibu… ova and out!” Madam S akamaliza.
“Copy!”
Mazungumzo ya Chiba na bosi wake yakakamilika, akamtazama Gina akiingiza gari katika Mtaa wa Cameroon ambako ubalozi wa Tanzania ulipo. Hawakupata shida kuingia ubalozini hapo kwa kuwa walitumia vitambulisho vyao vya uraia na vingine vya kazi ambavyo bado vilificha uhalisia wa kazi yao. Katika ofisi hizo walikutana na afisa mmoja anayefanya kazi ya kuhakikisha usalama wa Watanzania waishio nchini hapo.
“Swala la huyu bwana tunalifuatilia, na nimepata ujumbe kuwa ataachiwa lakini si leo, labda kesho…”
“Shiiiiiitttt!”
“…hata hivyo hivi sasa tunavyoongea anatakiwa kuhamishwa kutoka pale na kupelekwa mahala pengine kuhifadhiwa kwa ajili ya mahojiano zaidi…”
“Noooo! Haiwezekani!” Chiba akaongea huku amesimama, sura yake ilinesha wazi makwinyanzi ya hasira.
“Kwani, ninyi ni nani hasa hata mumtake huyu mtu leo? Kwa sababu sisi tuna utaratibu wetu wa kidiplomasia na kuna taratibu za kufuata ili kumtoa, lakini kwa kesi yake ambayo imefanya akamatwe, tutakuwa na kazi ngumu kumpata kwa sababu yupo chini ya kamati ya usalama ya AU wenyewe…” yule bwana akaeleza vizuri kabisa.
“Sawa, tutakuja kesho ili tujue kinachoendelea…”Chiba akamwambia yule afisa na kupeana mikono huku wakikaribishwa tena.
Nje ya ofisi zile, Chiba akamtazama Gina kabla hawajaingia garini.
“Sasa?” Gina akauliza.
“Sasa ni kumsaka Amata kufa na kupona, na ni lazima tumpate,” Chiba akasema huku akiingia garini, akawasha kifaa chake ambacho humsaidia kujua wapi mtu yeyote wa TSA yupo kwa wakati huo endapo tu bado atakuwasha kifaa chake cha kumuunganisha na wenzake ambavyo huwekwa ama kwenye saa, au simu, ikibidi sana mwilini.
“Gina, fuata barabara ya Airport haraka, naona signal inanionesha huko…” Chiba akasema na mwanamke huyo akakanyaga mafuta kufuata uelekeo aliyoambiwa.
Mambo ni motoo!
 
Nimegundua kuwa Amata ni mwepesi kama sufi tu,anakamatwa kibwegebwege sana
 
MAGNUM 22

Sehemu 24

Barabara ya Airport
Mwendo ambao magari haya ya polisi yalikuwa yakitembea haukuwa wa kawaida, njia nzima walitawanyika wao huku gari lile ambalo Amata alikuwemo likiwa katikati. Ndani ya gari hilo Kamanda alikuwa katulia kimya huku akiwasikiliza askari wale wakiwa wanaongea yao kwa ugha ya Ki-Amharic.
Sasa nitawaonesha kama mi ni kauzu na hawatanisahau! Akawaza Amata kisha akautafuta mkojo popote ulipo akajikojolea. Mmoja wa wae polisi akamwona na kumshtua mwenzake.
“Pumbavu sana! Hivi unajua kuwa unachafua gari la waheshimiwa? We Mtanzania wa wapi wewe? Nakutia adabu!” yule polisi akamwambia kwa gadhabu huki akimwendea. Kutokana na urefu wa bodi la gari lile, huyu bwana alisimama bila ya taabu.
“Hakikisha unamwadabisha!” yule mwingine akasema.
Jambo moja pekee ni kuwa hawakujua ni nani wanayemwambia maneno yote hayo. Yule polisi akamfikia lakini kabla hajafanya lolote akajikuta akipigwa ngwala, na ule mnyororo ukamchota sawia akajibamiza kwenye bodi la gari na kuanguka jirani tu na Amata. Katika kuanguka kule, mguu mmoja ukampiga mwingine naye akasukumwa kutoka alipoketi, akasimama kuja kumsaidia mwenzake, akainua kirungu kutaka kumtandika Kamanda. Kwa ustadi wa hali ya juu, alifanya kama anataka kubinukia upande wa pili na miguu ikaelekea juu na kuunasa mkono wa yule polisi naye akavutwa na kujibwaga juu ya mwengine. Kwa kutumia miguu, akambamizia kwa nguvu kwenye chuma la pembeni, jamaa akapoteza fahamu.
Askari yule wa kwanza akajaribu kujiinua lakini akajikuta anapewa pigo la miguu akarudi chini, kimya! Kwa kutumia miguu akachukua funguo zilizokuwa zinaning’inia kwenye huku ya suruari ya mmoja wao akafanikiwa japo kwa tabu sana. Akaikunja miguu yake na kuikamata funguo hiyo kwa kinywa chake akaibana na meno na kujaribu kuzifyatua pingu za miguu, Mungu si Athumani ikafunguka. Kwa kutumia mkono ulio huru akafungua na mwingine, kisha akajifungua na ule mnyororo. Kwa haraka akachukua bastola ya askari mmoja na kufyatua risasi mbili tu moja kwenye sakafu ya gari upande wa kulia na nyingine upande wa kushoto. Ghafla lile gari likayumba na kujibamiza kwenye ukingo wa barabara na kupinduka kama mara tano hivi. Kutokana na kishindo kile mlango wa nyuma gari hilo ukafunguka nah ii ikampa Amata wepesi wa kutoka, ijapokuwa alikuwa na maumivu ya hapa na pale. Alipokanyaga nje akakuta magari ya polisi yamesimama mbele na nyuma yakitazama pande tofauti kutokana na kusimama ghafla. Hakusubiri amri, alichokifanya ni kufyatua risasi na kupiga tanki la gari lile alilokuwamo, mlipuko mkubwa ukatokea na lile gari likanyanyuliwa juu kama unyoya.
Si kwamba alikuwa anajua, bali baada ya kutoka ndipo akagundua kuwa walikuwa darajani wanauvuka Mto Bulbula. Wakati askari wale wakilitazama lile gari, Amata hakujali, alikamata ukingo wa daraja na kuruka hewani kuelekea mtoni umbali wa kama mita ishirini hivi.
“Anatoroooookkaaa!!!!!” askari mmoja akapiga kelele na wengine wote ndipo wakashtuka na kukumbuka walikuwa na mfungwa garini na ndiye aliyesababisha hayo. Haraka, wakaziweka sawa silaha zao na wengine tayari walikwishafyatua upande ule ambako Amata amekimbilia. Wakafika katika ukingo ule na kusimama huku wakielekeza mitutu ya bunduki zao majini, hakuna mtu. Maji ya mto huo yalikuwa yakienda kasi sana, Amata mara tu baada ya kutumbukia aliogelea ka kupiga mbizi na kufanya maadui wake wasimwone.
* * *
Dakika kumi zilikuwa nyingi sana, habari zikasambaa kila kona kuwa gaidi lililokamatwa usiku wa jana limetoroka. Habari hii iliwachanganya wanausalama lakini ilimfanya Gina na Chiba kufurahi sana. Wakati huo huo wakawasili eneo hilo na kukuta magari mengi ya polisi yamesimama na kufanya foleni kwa magari mengine. Gina akapunguza mwendo baada ya kuamriwa na askari kisha akaongozwa kuwa apite upande mwingine, naye akafanya hivyo. Baada ya kuliacha eneo hilo na kuvuka daraja kubwa la mto huo, Gina akaegesha gari pembeni.
“Mcheki, tujue wapi yupo tukamchukue,” akamwambia Chiba.
“Ndicho ninachofanya hapa, bado sipati signal vizuri mpaka atakapokuwa eneo zuri,” Chiba akajibu.
“Lazima katorokea mtoni…”
“Na ndiyo njia salama kwa sababu hata waje na mbwa kamwe hawawezi kukupata,” Chiba akamwambia Gina huku akiendelea na kazi yake.
Kule mtoni, Amata aliibuka kama mita 500 mbele hivi, eneo aliloibukia halikuwa na majumba mengi isipokuwa machache ya kifahari yaliyojengwa mbali kidogo na mto. Akajivuta kando ya mto na kuegamia mti ulikuwa jirani huku akitweta kwa kuchoka. Dakika si nyingi akasikia muungurumo wa helikopta, akajua kumekucha.
Wanatumia chopa kunitafuta, wamedhamiria! Akawaza na kuanza kuondoka eneo hilo huku akielekea kwenye yale majumba, hakuonesha kujali kama kuna chopa inayozunguka eneo la mto kumtafuta, aliendelea kutembea taratibu mpaka katika barabara ndogo ambayo ukiiona tu utajua kuwa upita gari moja. Aliposimama hapo akiwa tumbo wazi na suruari iliyotota maji, akaona gari moja jeusi likija upande wake kabla hajaamua afanye nini, gari lile likawasha taa mara tatu na kupiga honi kwa mtindo ambao ulimshtua, akasimama na kulitazama, nalo likasimama miguuni pake kabisa. Hakuuliza, akafungua mlango na kujitupia katika kiti cha nyuma, lile gari likaondoka kasi na kuendelea kuifuata hiyo barabara.
“Pole sana Kamanda!” Chiba akamwambia huku akimpa mkono.
“Usijali Chiba, ndiyo kazi yetu….” Akajibu huku akimtazama Gina anavyopenya kwenye vichochoro ambavyo hata mwenyewe havijui.
“Tuna kazi ngumu Chiba, ngumu sana!” Amata akasema.
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Adui wetu ana macho na masikio mengi, tunaye, tunazunguka naye nay u miongoni mwetu…”
“Sure?”
“Sure, twende chimbo nitakuelezeni mengi, mengi ambayo hata hamkuyategemea, kwa ujumla kazi imeisha…” akasema Amata. Ukimya ukatawala wakati Gina akaiendelea kuongoza kile chombo. Dakika kama arobaini baadae aliegesha lile gari kwenye maegesho ya eneo lile alilooneshwa tangu mwanzoni, wakateremka na kuingia kwa milango ya siri na kuibukia ndani ya jingo lile la misheni ambalo Archimedius aliwahifadhi.
* * *
Kama kuna mtu ambaye habari ile ilimchukiza basi ni huyu Bwana Malirekc FikrMaryam, simu yake iliita akiwa ofisini na wajumbe wengine wane wa kamati ya usaalma ya muda na hapa walipoketi walikuwa wakijadiliana kuhusu mtu huyo huyo. Alipoishusha simu, akajikuta kijasho kikimtiririka, akatikisa kichwa kama mtu ambaye kaingiliwa na mdudu sikioni. Baada ya kutulia ndipo akawapa habari ile wengine wote. Kikao haikikuendelea tena, akakivunja na kuwataka wajumbe kuweka ulinzi imara katika hoteli ya Golden Tulip kwani viongozi hao wa juu wa AU wangekuwapo kwa chakula na mazungumzo maalum. Yeye akatoka na kuingia katika gari lake, mja kwa moja akaelekea katika ofisi yake ya siri ambako huko alikutana na vijana wake waliomkamata Amata usiku wa jana yake.
“Hata sisi tumepata taarifa, lakini tunashindwa kujua huyu jamaa katoroka vipi katika gari lile!” mmoja akasema.
“Hilo lisituumize kichwa, cha kufanya sasa ni kuhakikisha anasakwa, popote atakapopatikana akamatwe,” Marilekc alitoa maagizo, “yaani naweza kusema kuwa tuna saa mbili tu tuwe tumemtia mkononi, ninyi mnajua ni wapi mtaanzia upelelezi wenu kumsaka,” akamaliza na kuagana nao, wale vijana wakajipanga kikazi na kuelekea maeneo nyeti katika jiji hilo ambayo kwayo walihisi wanaweza kupata fununu yoyote. Hiki kilikuwa ni kikosikazi maalumu kabisa cha AU katika medani ya kikachero na kilikuwa kinaongozwa na mtu mzima, Marilekc FikrMaryam raia wa Ethiopia ambaye amefanya kazi za kijasusi kwa miaka mingi sana na kubobea kwenye medani hiyo. Katika sakata la mauaji ya viongozi wa Afrika, umoja wa nchi za bara hili ukaona umpe kazi yeye na kumwekea watu wengine kama watano hivi wenye IQ za halia ya juu sana katika chunguzi za mtindo huu ili kumbaini adui, ndipo wakapiga kambi Dar es salaama hasa baada ya kukoswakoswa rais wa Gambiua ambaye ndiye mwenyekiti wa umoja huo.
* * *
Ndani ya nyumba ile ya siri ambayo hata ujenzi wake ni wa kumchanganya mtu Amata alifikishwa salama kabisa na Chiba na Gina. Jambo la kwanza alilolifanya ni kuingia maliwato kujisafisha na kisha kujiganga kidogo mwili wake huku Gina naye akiwa jirani kumkanda kwa maji ya moto hapa na pale.
“Fanya haraka Gina, muda umekwisha!” Amata akamwambia.
“Muda umekwisha? Kwani unataka kwenda wapi?” Gina akauliza.
“Kwenda wapi, unafikiri kazi hii imekwisha? Mpaka sasa ninahisi last target ilipo,” akaeleza.
Wanausalama wanajinasibu kuwa Gupter hayupo nchini lakini ukweli ninaokwambia ni kuwa hatan mabosi wake wapo, na mshenzi huyu anaweza kufanya madhara muda wowote tunaoongea hapa…” alipoeleza hayo Gina akaacha kumkanda na kuzunguka akasimama mbele yake.
“Bado unamtaka Gupter?” akamuuliza Amata.
“Yes! Laziamapatikane,” akajibu.
Nusu saa baadae, Amata akwa katika hali ya kawaida, si kwamba alikuwa amepona kabisa ila sehemu kubwa ya mwili ilikuwa imepata afuu, Gina akampatia vidonge vya kutuliza maumivu vyenye nguvu , akameza. Kutoka kabatini akachukua suti mpya kabisa na kujitupia mwilini mwake. Dakika kumi baadae tayari alikuwa Kamanda Amata mwenyewe.
“Sina bastola,” akamwambia Gina naye akamletea mbili na kumkabidhi, akazitazama na kuziweka vizuri, akahakikisha kuna risasi za kutosha kwenye magazine yake, akazipachika katika mikanda maalumu mwilini mwake, akavhukua koti na kuvaa juu yake. Katika sebule ya nyumba hiyo, Chiba tayari alikuwa ndani ya suti, keshavaa, kiwalo cha gharama, akahakikisha ana kila kitu mwilini mwake, nikimaanisha silaha na vitu vingine muhimu.
“Tunapiga ngumi kichakani?” akamwuliza Amata.
“No, katika tafautishi niliyoipata kule kwenye makazi yao, Gupter amejipangia kuua kwa njia mbilia ama risasi au sumu, sasa hapa hisia zangu zinaniambia kabisa kuwa huyu mshenzi atatumia sumu,” akamweleza Chiba.
“Na unajua kuwa hawa jamaa watakuwa wanakusaka kwa udi na uvumba…”
“Achana nao, kwanza wameshaniharibisa hesabu zangu, naanza na Martin Gupter na wenzake kisha nitamaliaza na wao, nitawafata na kuwaumbua bila aibu, nilimsoma Marilekc kwenye kabrasha nililolipata Angola lakni sikumjua kuwa ni huyu mshenzi… yaani AU haijui kuwa imempa kazi kibaraka, kaahidiwa uwaziri siujui unini sijui kama Somalia ikigawanyika, baada ya kuona msimamo wa Madam S ndiye aliyemtengenezea ajali siku ile pale Dar es salaam,” Amata akamwambia Chiba.
“Usinambie! Ina maana yupo kwenye kamati…?”
“Ukisema yupo kwenye kamati unakosea, ndiye mwenyekiti wa kamati hiyo, yaani yeye anajua hata uwepo wa Gupter na wenzake hapa Addis, na kunikamata mimi jana ilikuwa ni kunifungia ndani ili nisitegue kitendawili chao, mbele ya vijana wake naaminisha umma kuwa mimi ni gaidi, wamenitesa sana ili niwapatie kabrasha la mpango wa mauaji nililolipata Luanda…” akamweleza Chiba ambaye alibaki kimya kabisa pasi na kusema lolote.
“Nipo tayari!” Gina akawaambia na kisha kila mtu akachukua kifaa chake.
Ndani ya gari, Chiba alikuwa akiendesha, Gina alikweti pembeni na Amata siti ya nyuma, safari ya mjini ikaanza. Chiba akatoa kitu kama simu kubwa ambayo juu yake imewekwa kioo kikubwa tu.
“Chukua ditector hii, humu ndani nimeijaza sura ya Gupter, Freddy na yule mwanamke katika mionekano tofauti, ukimhisi mtu we fanya kama unampiga picha tu, ukioanisha, hata kama kajibadili vipi, kifaa hiki kitamtambua tu,” akamwambia Amata na kumkabidhi.
“Hapa umenirahisishia kazi, nakumbuka nimetumia kidubwasha hiki katika lile sakata la Persona Non Grata,” akamwambia huku akikipokea.
“Nimeamua kukupa hicho kwa sababu, Gupter na wenzake wana sifa ya kujibadili sura na ndiyo maana hawatambuliki kirahisi,” Chiba akamwambia Amata huku akizidi kutokomea mjini.
“Sawasawa, na inaonekana wazi kuna ujanja mwingi unafanyika, laiti wangejua… ila leo siri itafichuka, na nitayaanika wazi, huwezi kutumia uzalendo kwa kuficha madhambia yako, tukipeana mikono unacheka, nikigeuka unaning’ong’a…ama zao ama zangu!” Amata akamaliza kusema na kukipachika kile kifaa mfukoni.

XIV
HOTELI YA GOLDEN TULIP
Saa 11:05 Jioni
Magari ya polisi, askari wa kwenye farasi na mbwa wote walijazana kuzunguka hoteli hiyo, ukiachana na wale waliovaa sare za kazi bado kuna ambao walifika hapo kiraia na walikuwa na kazi maalum. Makachero wa ndani na nje walikuwa kwenye shughuli mbalimbal wakihakikisha usalama wa viongozi ambao muda mfupi ulopita walikuwa wameingia ndani ya jingo hilo lenye kila aina ya starehe. Miongoni mwa wageni hao kulikuwa na marais wan chi mbalimbali za Afrika, mawaziri wawakilishi na wajumbe kadhaa achilia mbali waandishi wa habari na wafanyakazi.
Karibu kabisa na jengo hilo kulikuwa na ghorofa jingine refu, juu yake kulikuwa na askari wenye darubini na bunduki kubwa ambazo walizitumia pia kuongeza usalama wa eneo hilo na walaimriwa kuwa yeyote watakayemhisi kuwa ni mbaya basi wasisite kundungua.
Freddy aliegesha gari mbele ya supermarket kubwa ambayo jioni hiyo kulikuwa na watu wengi wakiingia na kutok ukizingatia ilikuwa mwisho wa juma.
“Umeona ee! Yaani hapa kutumia bunduki ni kujimaliza…” Martin Gupter akamwambia Freddy.
“Nimeona jamaa wamejizatiti safari hii…”
“Hata kama, lazima nitekeleze, sikiliza mpango upo hivi, wewe nisubiri nilipokwambia kwa dakika thelathini tu, ikifika ya thelethini na moja sijafika, ondoka tena kimbia usionekane na yale mapesa we tumia uwezavyo…” Martin Gupter akamwambia Freddy.
“Na vipi kuhusu Amanda?” Freddy akauliza.
“Kwa mpango niliyoupanga, Amanda naye atafika hapa dakika tatu kabla na mi pia…”
“Unatumia mbinu gani sasa kukamilisha kazi?” Freddy akahoji.
“Freddy! Muda ni tishu, siri ya kuua anaijua muuaji tu, we fanya nililokwambia,” akamwambia huku akichukua kjikoba chake kidogo na kukivaa kiunoni, lile gari likafunguka katika sakafu yake na kubaki sehemu kubwa wazi, Martin akachukua amtungi mdogo wa hewa safi akauvaa mgongoni kisha akashuka na kuuondoa mfuniko wa chemba ya maji machafu, akaingia ndani yake na kuurudishia vizuri ule mfuniko. Freddy akaondoa gari eneo lile na kuelekea mahala alikoambiwa akasubiri. Tayari mpango mzima wa ramani ya jiji hilo ulifanyika chini ya mwanadada Amanda, ambaye hakuona shida kukupa mwili wake ilimradi tu apate anachotaka. Na safari hii katika jji hili alikuwa na mapenzi mazito na matu mkubwa tu na mwisho akafanikiwa kuiba ramani nyeti ya jiji la Addis’ ambayo iliwaonesha mipangilio yote ya maji taka na maji safi na makazi ya watu na kila aina ya mpango wa mji huo. Isitoshe ilionesha mpaka njia za siri kabisa mabazo mtu mwingine hapaswi kujua. Martin Gupter aliitumia ramani hii kuweza kuifikia hoteli hiyo bila kugundulika na alihakikisha kufanikisha hilo.
Baada ya kutemba katika bomba hilo kubwa la maji machafu alifika eneo ambalo alilihisi kuwa yuko uvunguni mwa hoteli hiyo. Akawasha simu yake ya kisasa na kutazama tena ile ramani ambayo tayari alikuwa ameiweka katika mfum wa simu hiyo, akagundua kuwa hajakosea, ni hapo, akatembea kama hatua nyingine mia moja hivi na kufika mwisho wa bomba moja wapo ambalo juu yake kulikuwa na mfuniko kama ule ule wa kule alikoingilia. Akauvua ule mtungi na kuweka vizuri kisha akakamata ngazi ya chuma inayopanda juu mpaka akaufikia mfuniko, akausukuma taratibu na kuchungulia kama kuna tatizo lolote. Kama alivyoona kwenye ramani ile, hapa alipltlkea ni katikati ya hoteli ile ambapo pana bustani kubwa na nzuri, viti vya kupumzikia na bwawa la kuogelea. Siku hii eneo hili halikuwa na mtu kabisa kwani palifungwa kwa ajili ya usalama, akaingiza mko mfukoni na kuto kamera ndogo iliyopachikwa kwenye kitu kama spoku ya basikeli, akaipenyesha kwenye uwazi huo mdogo na kuizungusha pande zote, akajihakikishia kweli hakuna mtu eneo hilo, akarudisha mahala pake ile kamera na kuufungua ule mfuniko haraka, akatoka na kuufunga, akasimama nje tuli akiwa na mavazi yaliyochafuka uchafu, akavuta hatua na kuingia katika korido mojawapo kisha akapotele katika vyoo vilivyokuwa jirani hapo ambavyo watu hutumia kujisafisha mwili kabla hawajajitupa katika bwawa la kuogelea.
Dakika tano zilimtosha, akatoka akiwa kava suti safi, ya kisasa na ya gharama, sura aliyoingia nayo si aliyotoka nayo, huyu alikuwa Gupter mwingine kabisa. Jambo la kwanza alilolifanya ni kutafuta chumba cha usalama ambacho aliajua kwa vyovyote kama ni kumshuku, basi hawa watakuwa namba moja kwani wanaongoza kamera zote za usalama ndani na nje ya hoteli hii. Lakini bahati mbaya siku hii walikodolea macho zaidi kamera za ndani kwenye sherehe kuliko zile za nje.
* * *
Nyuma ya hoteli ile kulikuwa na maegesho ya magari ya wageni na siku hii kulikuwa kumejaa magari mengi sana na zaidi ya walinzi wa kawaida, kulikuwa na askari wengi waliozngira pande zote.
“Mtaingiaje?” Chiba akauliza.
“Usijali hilo niachie mimi!” akateremka na Gina akafuatia, akachukua kifaa chake na kukipachika sikioni, Gina akafanya vivyo hvyo hku na Chiba naye akakipachka cha kwake.
“Signal test!” Chiba akafanya jaribio la kuhakikisha kama vinanasa sauti. Wote wakaonesha alama ya dole gumba wakiashiri kuwa iko sawa. Mlango wa nyuma uliwaruhusu Amata na Gina kuingia ndani ya hoteli hii baada ya kuonesha vitambulisho kuwa ni wafanyakazi wa kitengo cha usalama cha hoteli hiyo. Kwa kutumia ufunguo wake usioshindwa akafungua na mlango ukatoa ushirikiano mzuri tu, wakaingia dani kwa kupitia chumba cha kufulia ‘laudry’.
“Gina, ungana na hawa wadada kwenye huduma ya mezani mimi nitaendelea kurandaranda humu ndani na kuchunguza mtu mmoja mmoja,” Amata akamwambia Gina naye hakujibu bali aliingia ndani ya chumba fulani na kutoka baada ya dakika kumi akiwa na sare za wahudumu na kuanza kusaidia kuhudumia vinywaji na mambo mengine katika meza za wageni huko ukumbi mkubwa. Kamanda Amata aliendelea kutembea kwenye korido hii na ile, akazikwea ngazi na na kutokea ghorofa ya juu ambako huko alikutana na watu wengine wakiwa wametingwa na kazi mbalimbali, hawa walikuwa waandishi wa habari. Kutoka pale aliweza kuona ukumbi wote kwa uzuri kwabisa. Hakuna aliyemjali kwani kil aliyemtazama alikutana na kitambulisho kilichoandikwa, ‘Internal Security-Golden Tulip Hotel Addis Ababa’.
Ni hapo tu aliposimama akiwatazama watu ndani ya ukumbi huo, pembeni yake alikuwapo mwanamke wa kizungu aliyekuwa bize kuandika andika huku kifuani akiwa na kamera kubwa aina ya Ricoh yenye lensi kubwa ya kuona mbali. Amata akamtazama kwa chati na kilichomshtua na kumfanya avutike naye ni alama iliyoonekana kwa mbali kwenye shavu la mwanamke huyu, alama ya jeraha, lakini iliyofanyiwa make up za gharama kuipoteza, lakini kovu ni kovu tu. Mwanamke huyu naye alimwona Amata tangu anaingia lakini hakumgundua na wala hakumjali, kilichomshtua baadae ni jinsi mwanaume huyu alivyokuwa akimtazama kwa chati na kuchezea simu yake mara kwa mara. Huyu hakuwa mwingine, Amanda Keller ambaye ni master plan wa kundi hili na daima hutumia njia ya uandishi habari ili apenye vizuri katika maeneo kama haya.
Kamanda Amata hakutaka kupoteza muda, akaliacha eneo lile na kuteremka ghorofa ya chini kwa minajiri ya kuwa afike katika eneo ambalo angeweza kuwaona watu kwa usahhi zaidi. Akatoa miwani yake na kuivaa kisha akawa anatembea taratibu kufuata korido iliyokuwa ikielekea huko. Miwani ile ilikuwa na kamera ndogo inayonasa picha jongefu na kuzisafirisha mpaka kwenye kompyuta ya Chiba ambako naye anaweza kufanya anayoweza na kuwatambua wale wawatakao.
* * *
Martin Gupter, katikati ya wahudumu wa kiume alikuwa akihudumu kama wafanyavyo wengine, tena yeye alionekana kuwa hodari sana katika kutembeza chano cha vinywaji. Kwa jinsi alivyojibadili sura yake ingekuwa vigumu kumgundua kuwa yeye ni Mzungu, hakuwa mbali na sura za kihabeshi, hakika alikuwa Muethiopia haswa.
Baada ya kama nusu saa hivi, Martin alikuwa tayari keshayasoma mazingira yote, tabua na yendo za watu. Alipomaliza kugaw avinywaji na kumjua ni nani aliyeandaliwa kwa ajili ya kuhudumia meza kuu tu.
Namtumia huyu huyu! Akawaza huku akiuacha ukumbi wa tafrija na kueleakea katika chumba maalumu ambacho ndiko hupatiwa huduma hizi. Martin Gupter aliitazama saa yake na kuona wazi muda ukiyoyoma kupita kawaida, akawaza na kuwazua kwa nini alifikiri kuwa kazi hiyo angeweza kuifanya kwa muda mfupi, hakupata jibu.
Maadam nimeahidi, sina budi kutekeleza! Akajisemea moyoni mwake, hakuna aliyemsikia zaidi ya kujisikia yeye mwenyewe.
“Martin, Time is up!” sauti ya Amanda ikamfikia masikioni kupitia kifaa kidogo mno ambachjo alikitumbukiza sikioni.
“Yes I know, and now im goind to accomplish the tasks!’ Ndiyo najua, na sasa ninakwenda kukamilisha zoezi,” akamjibu.
“Kuna sura sina imani nayo humu ndani, chukua tahadhari,” Amanda akasema tena.
“Tahadhari zote zi mkononi mwangu, jiandae uliache eneo lile,” Martin akamwambia Amanda, naye akasikia vyema. Kutoka kule juu, Amanda akaanza kujiweka sawa tayari kwa kuondoka.
 
MAGNUM 22

Sehemu 24

Barabara ya Airport
Mwendo ambao magari haya ya polisi yalikuwa yakitembea haukuwa wa kawaida, njia nzima walitawanyika wao huku gari lile ambalo Amata alikuwemo likiwa katikati. Ndani ya gari hilo Kamanda alikuwa katulia kimya huku akiwasikiliza askari wale wakiwa wanaongea yao kwa ugha ya Ki-Amharic.
Sasa nitawaonesha kama mi ni kauzu na hawatanisahau! Akawaza Amata kisha akautafuta mkojo popote ulipo akajikojolea. Mmoja wa wae polisi akamwona na kumshtua mwenzake.
“Pumbavu sana! Hivi unajua kuwa unachafua gari la waheshimiwa? We Mtanzania wa wapi wewe? Nakutia adabu!” yule polisi akamwambia kwa gadhabu huki akimwendea. Kutokana na urefu wa bodi la gari lile, huyu bwana alisimama bila ya taabu.
“Hakikisha unamwadabisha!” yule mwingine akasema.
Jambo moja pekee ni kuwa hawakujua ni nani wanayemwambia maneno yote hayo. Yule polisi akamfikia lakini kabla hajafanya lolote akajikuta akipigwa ngwala, na ule mnyororo ukamchota sawia akajibamiza kwenye bodi la gari na kuanguka jirani tu na Amata. Katika kuanguka kule, mguu mmoja ukampiga mwingine naye akasukumwa kutoka alipoketi, akasimama kuja kumsaidia mwenzake, akainua kirungu kutaka kumtandika Kamanda. Kwa ustadi wa hali ya juu, alifanya kama anataka kubinukia upande wa pili na miguu ikaelekea juu na kuunasa mkono wa yule polisi naye akavutwa na kujibwaga juu ya mwengine. Kwa kutumia miguu, akambamizia kwa nguvu kwenye chuma la pembeni, jamaa akapoteza fahamu.
Askari yule wa kwanza akajaribu kujiinua lakini akajikuta anapewa pigo la miguu akarudi chini, kimya! Kwa kutumia miguu akachukua funguo zilizokuwa zinaning’inia kwenye huku ya suruari ya mmoja wao akafanikiwa japo kwa tabu sana. Akaikunja miguu yake na kuikamata funguo hiyo kwa kinywa chake akaibana na meno na kujaribu kuzifyatua pingu za miguu, Mungu si Athumani ikafunguka. Kwa kutumia mkono ulio huru akafungua na mwingine, kisha akajifungua na ule mnyororo. Kwa haraka akachukua bastola ya askari mmoja na kufyatua risasi mbili tu moja kwenye sakafu ya gari upande wa kulia na nyingine upande wa kushoto. Ghafla lile gari likayumba na kujibamiza kwenye ukingo wa barabara na kupinduka kama mara tano hivi. Kutokana na kishindo kile mlango wa nyuma gari hilo ukafunguka nah ii ikampa Amata wepesi wa kutoka, ijapokuwa alikuwa na maumivu ya hapa na pale. Alipokanyaga nje akakuta magari ya polisi yamesimama mbele na nyuma yakitazama pande tofauti kutokana na kusimama ghafla. Hakusubiri amri, alichokifanya ni kufyatua risasi na kupiga tanki la gari lile alilokuwamo, mlipuko mkubwa ukatokea na lile gari likanyanyuliwa juu kama unyoya.
Si kwamba alikuwa anajua, bali baada ya kutoka ndipo akagundua kuwa walikuwa darajani wanauvuka Mto Bulbula. Wakati askari wale wakilitazama lile gari, Amata hakujali, alikamata ukingo wa daraja na kuruka hewani kuelekea mtoni umbali wa kama mita ishirini hivi.
“Anatoroooookkaaa!!!!!” askari mmoja akapiga kelele na wengine wote ndipo wakashtuka na kukumbuka walikuwa na mfungwa garini na ndiye aliyesababisha hayo. Haraka, wakaziweka sawa silaha zao na wengine tayari walikwishafyatua upande ule ambako Amata amekimbilia. Wakafika katika ukingo ule na kusimama huku wakielekeza mitutu ya bunduki zao majini, hakuna mtu. Maji ya mto huo yalikuwa yakienda kasi sana, Amata mara tu baada ya kutumbukia aliogelea ka kupiga mbizi na kufanya maadui wake wasimwone.
* * *
Dakika kumi zilikuwa nyingi sana, habari zikasambaa kila kona kuwa gaidi lililokamatwa usiku wa jana limetoroka. Habari hii iliwachanganya wanausalama lakini ilimfanya Gina na Chiba kufurahi sana. Wakati huo huo wakawasili eneo hilo na kukuta magari mengi ya polisi yamesimama na kufanya foleni kwa magari mengine. Gina akapunguza mwendo baada ya kuamriwa na askari kisha akaongozwa kuwa apite upande mwingine, naye akafanya hivyo. Baada ya kuliacha eneo hilo na kuvuka daraja kubwa la mto huo, Gina akaegesha gari pembeni.
“Mcheki, tujue wapi yupo tukamchukue,” akamwambia Chiba.
“Ndicho ninachofanya hapa, bado sipati signal vizuri mpaka atakapokuwa eneo zuri,” Chiba akajibu.
“Lazima katorokea mtoni…”
“Na ndiyo njia salama kwa sababu hata waje na mbwa kamwe hawawezi kukupata,” Chiba akamwambia Gina huku akiendelea na kazi yake.
Kule mtoni, Amata aliibuka kama mita 500 mbele hivi, eneo aliloibukia halikuwa na majumba mengi isipokuwa machache ya kifahari yaliyojengwa mbali kidogo na mto. Akajivuta kando ya mto na kuegamia mti ulikuwa jirani huku akitweta kwa kuchoka. Dakika si nyingi akasikia muungurumo wa helikopta, akajua kumekucha.
Wanatumia chopa kunitafuta, wamedhamiria! Akawaza na kuanza kuondoka eneo hilo huku akielekea kwenye yale majumba, hakuonesha kujali kama kuna chopa inayozunguka eneo la mto kumtafuta, aliendelea kutembea taratibu mpaka katika barabara ndogo ambayo ukiiona tu utajua kuwa upita gari moja. Aliposimama hapo akiwa tumbo wazi na suruari iliyotota maji, akaona gari moja jeusi likija upande wake kabla hajaamua afanye nini, gari lile likawasha taa mara tatu na kupiga honi kwa mtindo ambao ulimshtua, akasimama na kulitazama, nalo likasimama miguuni pake kabisa. Hakuuliza, akafungua mlango na kujitupia katika kiti cha nyuma, lile gari likaondoka kasi na kuendelea kuifuata hiyo barabara.
“Pole sana Kamanda!” Chiba akamwambia huku akimpa mkono.
“Usijali Chiba, ndiyo kazi yetu….” Akajibu huku akimtazama Gina anavyopenya kwenye vichochoro ambavyo hata mwenyewe havijui.
“Tuna kazi ngumu Chiba, ngumu sana!” Amata akasema.
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Adui wetu ana macho na masikio mengi, tunaye, tunazunguka naye nay u miongoni mwetu…”
“Sure?”
“Sure, twende chimbo nitakuelezeni mengi, mengi ambayo hata hamkuyategemea, kwa ujumla kazi imeisha…” akasema Amata. Ukimya ukatawala wakati Gina akaiendelea kuongoza kile chombo. Dakika kama arobaini baadae aliegesha lile gari kwenye maegesho ya eneo lile alilooneshwa tangu mwanzoni, wakateremka na kuingia kwa milango ya siri na kuibukia ndani ya jingo lile la misheni ambalo Archimedius aliwahifadhi.
* * *
Kama kuna mtu ambaye habari ile ilimchukiza basi ni huyu Bwana Malirekc FikrMaryam, simu yake iliita akiwa ofisini na wajumbe wengine wane wa kamati ya usaalma ya muda na hapa walipoketi walikuwa wakijadiliana kuhusu mtu huyo huyo. Alipoishusha simu, akajikuta kijasho kikimtiririka, akatikisa kichwa kama mtu ambaye kaingiliwa na mdudu sikioni. Baada ya kutulia ndipo akawapa habari ile wengine wote. Kikao haikikuendelea tena, akakivunja na kuwataka wajumbe kuweka ulinzi imara katika hoteli ya Golden Tulip kwani viongozi hao wa juu wa AU wangekuwapo kwa chakula na mazungumzo maalum. Yeye akatoka na kuingia katika gari lake, mja kwa moja akaelekea katika ofisi yake ya siri ambako huko alikutana na vijana wake waliomkamata Amata usiku wa jana yake.
“Hata sisi tumepata taarifa, lakini tunashindwa kujua huyu jamaa katoroka vipi katika gari lile!” mmoja akasema.
“Hilo lisituumize kichwa, cha kufanya sasa ni kuhakikisha anasakwa, popote atakapopatikana akamatwe,” Marilekc alitoa maagizo, “yaani naweza kusema kuwa tuna saa mbili tu tuwe tumemtia mkononi, ninyi mnajua ni wapi mtaanzia upelelezi wenu kumsaka,” akamaliza na kuagana nao, wale vijana wakajipanga kikazi na kuelekea maeneo nyeti katika jiji hilo ambayo kwayo walihisi wanaweza kupata fununu yoyote. Hiki kilikuwa ni kikosikazi maalumu kabisa cha AU katika medani ya kikachero na kilikuwa kinaongozwa na mtu mzima, Marilekc FikrMaryam raia wa Ethiopia ambaye amefanya kazi za kijasusi kwa miaka mingi sana na kubobea kwenye medani hiyo. Katika sakata la mauaji ya viongozi wa Afrika, umoja wa nchi za bara hili ukaona umpe kazi yeye na kumwekea watu wengine kama watano hivi wenye IQ za halia ya juu sana katika chunguzi za mtindo huu ili kumbaini adui, ndipo wakapiga kambi Dar es salaama hasa baada ya kukoswakoswa rais wa Gambiua ambaye ndiye mwenyekiti wa umoja huo.
* * *
Ndani ya nyumba ile ya siri ambayo hata ujenzi wake ni wa kumchanganya mtu Amata alifikishwa salama kabisa na Chiba na Gina. Jambo la kwanza alilolifanya ni kuingia maliwato kujisafisha na kisha kujiganga kidogo mwili wake huku Gina naye akiwa jirani kumkanda kwa maji ya moto hapa na pale.
“Fanya haraka Gina, muda umekwisha!” Amata akamwambia.
“Muda umekwisha? Kwani unataka kwenda wapi?” Gina akauliza.
“Kwenda wapi, unafikiri kazi hii imekwisha? Mpaka sasa ninahisi last target ilipo,” akaeleza.
Wanausalama wanajinasibu kuwa Gupter hayupo nchini lakini ukweli ninaokwambia ni kuwa hatan mabosi wake wapo, na mshenzi huyu anaweza kufanya madhara muda wowote tunaoongea hapa…” alipoeleza hayo Gina akaacha kumkanda na kuzunguka akasimama mbele yake.
“Bado unamtaka Gupter?” akamuuliza Amata.
“Yes! Laziamapatikane,” akajibu.
Nusu saa baadae, Amata akwa katika hali ya kawaida, si kwamba alikuwa amepona kabisa ila sehemu kubwa ya mwili ilikuwa imepata afuu, Gina akampatia vidonge vya kutuliza maumivu vyenye nguvu , akameza. Kutoka kabatini akachukua suti mpya kabisa na kujitupia mwilini mwake. Dakika kumi baadae tayari alikuwa Kamanda Amata mwenyewe.
“Sina bastola,” akamwambia Gina naye akamletea mbili na kumkabidhi, akazitazama na kuziweka vizuri, akahakikisha kuna risasi za kutosha kwenye magazine yake, akazipachika katika mikanda maalumu mwilini mwake, akavhukua koti na kuvaa juu yake. Katika sebule ya nyumba hiyo, Chiba tayari alikuwa ndani ya suti, keshavaa, kiwalo cha gharama, akahakikisha ana kila kitu mwilini mwake, nikimaanisha silaha na vitu vingine muhimu.
“Tunapiga ngumi kichakani?” akamwuliza Amata.
“No, katika tafautishi niliyoipata kule kwenye makazi yao, Gupter amejipangia kuua kwa njia mbilia ama risasi au sumu, sasa hapa hisia zangu zinaniambia kabisa kuwa huyu mshenzi atatumia sumu,” akamweleza Chiba.
“Na unajua kuwa hawa jamaa watakuwa wanakusaka kwa udi na uvumba…”
“Achana nao, kwanza wameshaniharibisa hesabu zangu, naanza na Martin Gupter na wenzake kisha nitamaliaza na wao, nitawafata na kuwaumbua bila aibu, nilimsoma Marilekc kwenye kabrasha nililolipata Angola lakni sikumjua kuwa ni huyu mshenzi… yaani AU haijui kuwa imempa kazi kibaraka, kaahidiwa uwaziri siujui unini sijui kama Somalia ikigawanyika, baada ya kuona msimamo wa Madam S ndiye aliyemtengenezea ajali siku ile pale Dar es salaam,” Amata akamwambia Chiba.
“Usinambie! Ina maana yupo kwenye kamati…?”
“Ukisema yupo kwenye kamati unakosea, ndiye mwenyekiti wa kamati hiyo, yaani yeye anajua hata uwepo wa Gupter na wenzake hapa Addis, na kunikamata mimi jana ilikuwa ni kunifungia ndani ili nisitegue kitendawili chao, mbele ya vijana wake naaminisha umma kuwa mimi ni gaidi, wamenitesa sana ili niwapatie kabrasha la mpango wa mauaji nililolipata Luanda…” akamweleza Chiba ambaye alibaki kimya kabisa pasi na kusema lolote.
“Nipo tayari!” Gina akawaambia na kisha kila mtu akachukua kifaa chake.
Ndani ya gari, Chiba alikuwa akiendesha, Gina alikweti pembeni na Amata siti ya nyuma, safari ya mjini ikaanza. Chiba akatoa kitu kama simu kubwa ambayo juu yake imewekwa kioo kikubwa tu.
“Chukua ditector hii, humu ndani nimeijaza sura ya Gupter, Freddy na yule mwanamke katika mionekano tofauti, ukimhisi mtu we fanya kama unampiga picha tu, ukioanisha, hata kama kajibadili vipi, kifaa hiki kitamtambua tu,” akamwambia Amata na kumkabidhi.
“Hapa umenirahisishia kazi, nakumbuka nimetumia kidubwasha hiki katika lile sakata la Persona Non Grata,” akamwambia huku akikipokea.
“Nimeamua kukupa hicho kwa sababu, Gupter na wenzake wana sifa ya kujibadili sura na ndiyo maana hawatambuliki kirahisi,” Chiba akamwambia Amata huku akizidi kutokomea mjini.
“Sawasawa, na inaonekana wazi kuna ujanja mwingi unafanyika, laiti wangejua… ila leo siri itafichuka, na nitayaanika wazi, huwezi kutumia uzalendo kwa kuficha madhambia yako, tukipeana mikono unacheka, nikigeuka unaning’ong’a…ama zao ama zangu!” Amata akamaliza kusema na kukipachika kile kifaa mfukoni.

XIV
HOTELI YA GOLDEN TULIP
Saa 11:05 Jioni
Magari ya polisi, askari wa kwenye farasi na mbwa wote walijazana kuzunguka hoteli hiyo, ukiachana na wale waliovaa sare za kazi bado kuna ambao walifika hapo kiraia na walikuwa na kazi maalum. Makachero wa ndani na nje walikuwa kwenye shughuli mbalimbal wakihakikisha usalama wa viongozi ambao muda mfupi ulopita walikuwa wameingia ndani ya jingo hilo lenye kila aina ya starehe. Miongoni mwa wageni hao kulikuwa na marais wan chi mbalimbali za Afrika, mawaziri wawakilishi na wajumbe kadhaa achilia mbali waandishi wa habari na wafanyakazi.
Karibu kabisa na jengo hilo kulikuwa na ghorofa jingine refu, juu yake kulikuwa na askari wenye darubini na bunduki kubwa ambazo walizitumia pia kuongeza usalama wa eneo hilo na walaimriwa kuwa yeyote watakayemhisi kuwa ni mbaya basi wasisite kundungua.
Freddy aliegesha gari mbele ya supermarket kubwa ambayo jioni hiyo kulikuwa na watu wengi wakiingia na kutok ukizingatia ilikuwa mwisho wa juma.
“Umeona ee! Yaani hapa kutumia bunduki ni kujimaliza…” Martin Gupter akamwambia Freddy.
“Nimeona jamaa wamejizatiti safari hii…”
“Hata kama, lazima nitekeleze, sikiliza mpango upo hivi, wewe nisubiri nilipokwambia kwa dakika thelathini tu, ikifika ya thelethini na moja sijafika, ondoka tena kimbia usionekane na yale mapesa we tumia uwezavyo…” Martin Gupter akamwambia Freddy.
“Na vipi kuhusu Amanda?” Freddy akauliza.
“Kwa mpango niliyoupanga, Amanda naye atafika hapa dakika tatu kabla na mi pia…”
“Unatumia mbinu gani sasa kukamilisha kazi?” Freddy akahoji.
“Freddy! Muda ni tishu, siri ya kuua anaijua muuaji tu, we fanya nililokwambia,” akamwambia huku akichukua kjikoba chake kidogo na kukivaa kiunoni, lile gari likafunguka katika sakafu yake na kubaki sehemu kubwa wazi, Martin akachukua amtungi mdogo wa hewa safi akauvaa mgongoni kisha akashuka na kuuondoa mfuniko wa chemba ya maji machafu, akaingia ndani yake na kuurudishia vizuri ule mfuniko. Freddy akaondoa gari eneo lile na kuelekea mahala alikoambiwa akasubiri. Tayari mpango mzima wa ramani ya jiji hilo ulifanyika chini ya mwanadada Amanda, ambaye hakuona shida kukupa mwili wake ilimradi tu apate anachotaka. Na safari hii katika jji hili alikuwa na mapenzi mazito na matu mkubwa tu na mwisho akafanikiwa kuiba ramani nyeti ya jiji la Addis’ ambayo iliwaonesha mipangilio yote ya maji taka na maji safi na makazi ya watu na kila aina ya mpango wa mji huo. Isitoshe ilionesha mpaka njia za siri kabisa mabazo mtu mwingine hapaswi kujua. Martin Gupter aliitumia ramani hii kuweza kuifikia hoteli hiyo bila kugundulika na alihakikisha kufanikisha hilo.
Baada ya kutemba katika bomba hilo kubwa la maji machafu alifika eneo ambalo alilihisi kuwa yuko uvunguni mwa hoteli hiyo. Akawasha simu yake ya kisasa na kutazama tena ile ramani ambayo tayari alikuwa ameiweka katika mfum wa simu hiyo, akagundua kuwa hajakosea, ni hapo, akatembea kama hatua nyingine mia moja hivi na kufika mwisho wa bomba moja wapo ambalo juu yake kulikuwa na mfuniko kama ule ule wa kule alikoingilia. Akauvua ule mtungi na kuweka vizuri kisha akakamata ngazi ya chuma inayopanda juu mpaka akaufikia mfuniko, akausukuma taratibu na kuchungulia kama kuna tatizo lolote. Kama alivyoona kwenye ramani ile, hapa alipltlkea ni katikati ya hoteli ile ambapo pana bustani kubwa na nzuri, viti vya kupumzikia na bwawa la kuogelea. Siku hii eneo hili halikuwa na mtu kabisa kwani palifungwa kwa ajili ya usalama, akaingiza mko mfukoni na kuto kamera ndogo iliyopachikwa kwenye kitu kama spoku ya basikeli, akaipenyesha kwenye uwazi huo mdogo na kuizungusha pande zote, akajihakikishia kweli hakuna mtu eneo hilo, akarudisha mahala pake ile kamera na kuufungua ule mfuniko haraka, akatoka na kuufunga, akasimama nje tuli akiwa na mavazi yaliyochafuka uchafu, akavuta hatua na kuingia katika korido mojawapo kisha akapotele katika vyoo vilivyokuwa jirani hapo ambavyo watu hutumia kujisafisha mwili kabla hawajajitupa katika bwawa la kuogelea.
Dakika tano zilimtosha, akatoka akiwa kava suti safi, ya kisasa na ya gharama, sura aliyoingia nayo si aliyotoka nayo, huyu alikuwa Gupter mwingine kabisa. Jambo la kwanza alilolifanya ni kutafuta chumba cha usalama ambacho aliajua kwa vyovyote kama ni kumshuku, basi hawa watakuwa namba moja kwani wanaongoza kamera zote za usalama ndani na nje ya hoteli hii. Lakini bahati mbaya siku hii walikodolea macho zaidi kamera za ndani kwenye sherehe kuliko zile za nje.
* * *
Nyuma ya hoteli ile kulikuwa na maegesho ya magari ya wageni na siku hii kulikuwa kumejaa magari mengi sana na zaidi ya walinzi wa kawaida, kulikuwa na askari wengi waliozngira pande zote.
“Mtaingiaje?” Chiba akauliza.
“Usijali hilo niachie mimi!” akateremka na Gina akafuatia, akachukua kifaa chake na kukipachika sikioni, Gina akafanya vivyo hvyo hku na Chiba naye akakipachka cha kwake.
“Signal test!” Chiba akafanya jaribio la kuhakikisha kama vinanasa sauti. Wote wakaonesha alama ya dole gumba wakiashiri kuwa iko sawa. Mlango wa nyuma uliwaruhusu Amata na Gina kuingia ndani ya hoteli hii baada ya kuonesha vitambulisho kuwa ni wafanyakazi wa kitengo cha usalama cha hoteli hiyo. Kwa kutumia ufunguo wake usioshindwa akafungua na mlango ukatoa ushirikiano mzuri tu, wakaingia dani kwa kupitia chumba cha kufulia ‘laudry’.
“Gina, ungana na hawa wadada kwenye huduma ya mezani mimi nitaendelea kurandaranda humu ndani na kuchunguza mtu mmoja mmoja,” Amata akamwambia Gina naye hakujibu bali aliingia ndani ya chumba fulani na kutoka baada ya dakika kumi akiwa na sare za wahudumu na kuanza kusaidia kuhudumia vinywaji na mambo mengine katika meza za wageni huko ukumbi mkubwa. Kamanda Amata aliendelea kutembea kwenye korido hii na ile, akazikwea ngazi na na kutokea ghorofa ya juu ambako huko alikutana na watu wengine wakiwa wametingwa na kazi mbalimbali, hawa walikuwa waandishi wa habari. Kutoka pale aliweza kuona ukumbi wote kwa uzuri kwabisa. Hakuna aliyemjali kwani kil aliyemtazama alikutana na kitambulisho kilichoandikwa, ‘Internal Security-Golden Tulip Hotel Addis Ababa’.
Ni hapo tu aliposimama akiwatazama watu ndani ya ukumbi huo, pembeni yake alikuwapo mwanamke wa kizungu aliyekuwa bize kuandika andika huku kifuani akiwa na kamera kubwa aina ya Ricoh yenye lensi kubwa ya kuona mbali. Amata akamtazama kwa chati na kilichomshtua na kumfanya avutike naye ni alama iliyoonekana kwa mbali kwenye shavu la mwanamke huyu, alama ya jeraha, lakini iliyofanyiwa make up za gharama kuipoteza, lakini kovu ni kovu tu. Mwanamke huyu naye alimwona Amata tangu anaingia lakini hakumgundua na wala hakumjali, kilichomshtua baadae ni jinsi mwanaume huyu alivyokuwa akimtazama kwa chati na kuchezea simu yake mara kwa mara. Huyu hakuwa mwingine, Amanda Keller ambaye ni master plan wa kundi hili na daima hutumia njia ya uandishi habari ili apenye vizuri katika maeneo kama haya.
Kamanda Amata hakutaka kupoteza muda, akaliacha eneo lile na kuteremka ghorofa ya chini kwa minajiri ya kuwa afike katika eneo ambalo angeweza kuwaona watu kwa usahhi zaidi. Akatoa miwani yake na kuivaa kisha akawa anatembea taratibu kufuata korido iliyokuwa ikielekea huko. Miwani ile ilikuwa na kamera ndogo inayonasa picha jongefu na kuzisafirisha mpaka kwenye kompyuta ya Chiba ambako naye anaweza kufanya anayoweza na kuwatambua wale wawatakao.
* * *
Martin Gupter, katikati ya wahudumu wa kiume alikuwa akihudumu kama wafanyavyo wengine, tena yeye alionekana kuwa hodari sana katika kutembeza chano cha vinywaji. Kwa jinsi alivyojibadili sura yake ingekuwa vigumu kumgundua kuwa yeye ni Mzungu, hakuwa mbali na sura za kihabeshi, hakika alikuwa Muethiopia haswa.
Baada ya kama nusu saa hivi, Martin alikuwa tayari keshayasoma mazingira yote, tabua na yendo za watu. Alipomaliza kugaw avinywaji na kumjua ni nani aliyeandaliwa kwa ajili ya kuhudumia meza kuu tu.
Namtumia huyu huyu! Akawaza huku akiuacha ukumbi wa tafrija na kueleakea katika chumba maalumu ambacho ndiko hupatiwa huduma hizi. Martin Gupter aliitazama saa yake na kuona wazi muda ukiyoyoma kupita kawaida, akawaza na kuwazua kwa nini alifikiri kuwa kazi hiyo angeweza kuifanya kwa muda mfupi, hakupata jibu.
Maadam nimeahidi, sina budi kutekeleza! Akajisemea moyoni mwake, hakuna aliyemsikia zaidi ya kujisikia yeye mwenyewe.
“Martin, Time is up!” sauti ya Amanda ikamfikia masikioni kupitia kifaa kidogo mno ambachjo alikitumbukiza sikioni.
“Yes I know, and now im goind to accomplish the tasks!’ Ndiyo najua, na sasa ninakwenda kukamilisha zoezi,” akamjibu.
“Kuna sura sina imani nayo humu ndani, chukua tahadhari,” Amanda akasema tena.
“Tahadhari zote zi mkononi mwangu, jiandae uliache eneo lile,” Martin akamwambia Amanda, naye akasikia vyema. Kutoka kule juu, Amanda akaanza kujiweka sawa tayari kwa kuondoka.
Kamanda Amanta ni moto wa kuotea mbali, si wa kisport sport kabisa na moto wake usijaribu kuuotea karibu utakuunguza vibaya. Gupter huenda akaisoma namba time hii!!!
 
dah hii ni kari sana unaweza kusahau kula asante sana kulubule
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom