HaMachiach
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 3,445
- 6,207
- Thread starter
- #241
MAGNUM 22
Sehemu 25
kifaa cha Amata kikampigia alarm akakitoa na kukikamata kiganjani mwake, akatupia jicho kwenye kioo na hapo ndipo mapigo ya moyo yakabadili uelekeo. Akiwa pale juu ambapo alifika mara ya kwanza, alimpiga picha mwanamke huyu, picha ya wizi na sasa kile kifa kilikuwa kikifanaya crosssmatch ya picha za mwanamke huyo.
Amanda Keller! Akasoma jina la mwanamke huyo na mambo mengine mengine, hakusubiri sekunde wala nukta, akabadili uelekeo na kurudi kupanda tena zile ngazi kwa minajiri ya kumtia mkononi mwanamke yule. Kamanda Amata akiwa katika harakati hiyo akatoa taarifa kwa swahiba zake; yaani Gina na Chiba kuwa wachukue tahadahari kuhusu mwanamke huyo na waweke macho yao kodo ili kujmwona kama atajaribu kutoka tika jingo lile kwa njia nyingine. Ghafla akaibukia katika eneo lile la mwanzo, ambapo kulijawa na waandishi wa habari kutoka mashirika mbalimbali. Akasimama na kuangaza macho, mwanamke yule hakuonekana.
Wameniweza, kaeda wapi? Akajiuliza na kuanza kuteremka ngazi zile kwa haraka sana, mara hii hakuwa na sehemu nyingine za kwenda zaidi ya chumba cha usalama ambacho kina luninga nyingi zinasoonesha picha kutoka pande tafauti za hoteli hiyo. Alipoufikia mlango, umefungwa, akautikisa, umefungwa. Akatazama huku na huku asione mtu wa kumhofia, akachukua funguo zake na kuzitumbukiza kwenye tundu la kitasa hicho akazungusha kama mara nne hivi na mlango ukafunguka. Amata akajitoma ndani, lakini ghafla akasimama na macho yake yakatua juu ya miili miwili ya vijana wafu. Akachomo bastola yake na kurandaranda ndani ya chumba hicho, hakuna mtu, akatazama vyema miili ya watu wale na kujiridhisha kwa macho kuwa hawana uhai.
Martin Gupter! Akawaza na kuiridisha bastola ile haraka kiunoni akafunga mlango kwa ndani na kuiendea luninga moja wapo na kutazama matukio kadhaa hasa alitaka kuona nani alikuwa wa mwisho kuingi ndani ya chumba hicho. Baada ya kurudisha matukio nyuma kama dakika kumi au kumi na tano hivi ndipo akamwona anayemtaka. Kijana wamakamo, aliyevalia sare ya wahudumu wa hoteli hiyo, picha ikamwonesha akiingia na kuanza kuwashambulia mpaka kuwaua, kisha ikamwonesha akichakurachakura kwenye baadhi ya picha za siku hiyo, Amata akajua tu kuwa bila shaka alikuwa akifuta matukio kadhaa yanayomhusu yeye. Kamanda Amata akachukua flashi yake na kuipachika kwenye kompyuta nyingine na kuanza kunakila mienendo yote ya siku hiyo, aliporidhika akainyakua na kuitia mfukoni kisha akatoka ndani ya chumba kile, akafunga mlango kwa nje na kukivunja kitasa akitaka mtu asiingie kirahisi ili yeye apate muda wa kumsaka huyo hayawani.
* * *
Martin Guter hakutaka kupoteza muda, akaingia katika chumba ambacho vinywaj na vyakula mbalimbali vimehifadhiwa haswa kwa wageni maalumu. Hakuzuiwa kwa kuwa alishahabiana kabisa na wahudumu wa hoteli, na pia kwa kuwa alikwishaingia ndani ya chumba hicho kama mara tatu kama si nne. Ndani humo alijuwa wazi ni chano ipi na chakula gani ambacho kitachukuliwa na kupelekwa mezakuu. Akajifanya akiongea na wahudumua wengine huku akimimina vinywaji vikali katika bilauri. Hapa ndipo akafanya kile anachotaka, akatoa kijichupa kidogo cha pombe kali, lakini ndani yake kulikuwa na sumu mbaya inayoua kwa dakika thelathini tu kama aliyetumia kachelewa hospitali.
Baada ya kuhakikisha bilauri zote sita keshazifanyia hujuma hiyo, akabadili na chano chake kisha akachukua kingine na kuendelea na kazi ya kupelekea vinywaji. Askari waliokuwa mlangoni waliendelea kuweka ulinzi bila kujua kuwa muuaji anawapita kuingia na kutoka. Ni dakika hiyo hiyo ambayo Kamanda Amata alikuwa akipita kwenye korido hiyo na kukutana macho kwa macho na Gupter, akahisi vinyweleo vikimsimama tangu mbali, haraka aakachukua kile kifaa chake kama simu na kuanza kujifanya akiandika jambo fulani kumbe alikuwa akimpiga picha kijana huyo.
Martin Gupter naye alipomwona Amata akahisi kama anataka kuzimia, hakuamini kama anayemwona mbele yake ni yeye au kivuli wakati kichwani ana kumbukumbu kuwa mpelelezi huyo keshakufa zamani sana kule Waterloo. Almanusura amwage vinywaji lakini akajikaza, hali hii Amata aliigundua, akana wazi kuwa kuna kitu hakiko sawa. Akamtazama kwa nyuma akitembea na kuufananisha mwendo wake na sehemu tatu tu ambazo alimwona kwa karibu.
Ni yeye! Akawaza, na wakati huo akaufikia ule mlango ambao nje yake kulikuwa na ulinzi mkali. Alipofika alikuta kuna hekaheka ndani yake, kijana mmoja akiwa chini akitokwa na povu huku wenzake wakihaha kumsaidia. Kamanda hakuuliza, akaingia haraka na kujichanganya kusaidia.
“Nini kimetokea?” akamuuliza mmoja wa wahudumu.
“Hatujui, amekuywa tu kinywaji hicho kwenye glass mara akaanguka na hali ndiyo hiyo!” Amata akajibiwa, akainuka na kutazama huku na huku asione mtu wa msaada. Akaingiza mkono mfukoni na kuto kijichupa kingine cha plastiki ndani yake kulikuwa na vidonge kama kumi hivi akatoa kimoja na kwa nguvu za ziada wakambana mpaka akaachama kinywa na kukitumbukiza kile kidonge. Amata akamwacha na kuwaambia wahakikishe hakitemi. Akafika mlangoni na kuwapa amri wale askari kumtafuta yule kijana. Nao wakajikuta wakichanganyikiwa wasijue cha kufanya, akachomoa bastola yake na kutoka kasi kueleke ukumbi mkubwa.
“Martini Gupter yupo hapa, kila mmoja akae tahadhari sasa!” akasema, na taarifa ile ikamfikia Gina na Chiba.
“Copy!” akajibiwa.
Wakati Amata anafika katika ukumbi mkubwa, kwa kuwa alikuwa katika mwendo wa kukimbia walinzi wenye nguvu wakamdaka kabla hajaingia. Akatumia nguvu kujikwamua lakini akajikuta amebanwa na mikono mine yenye nguvu za vice.
“Poisssoooonnn!!!” akatamka kwa nguvu, lakini wale jamaa ndiyo kwanza wakambana barabara huku askari wengine wakielekea eneo hilo. Wakati wote huu Gina alikuwa upande wa ndani wa ukumbi huo na aliliona tukio hilo, akashindwa nini cha kufanya, baada ya kusikia neno ‘poison’, akili yake ikafanya kazi haraka sana na kutazama meza ya wakuu yule mwanadada tayari alikuwa akigawa vinywaji kwa waheshimiwa. Kutoka aliposimama alikimbia kwa hatua ndefundefu na kumfikia mwanadada yule, hakuna muda wa kuzungumza bali kumnyang’anya ile chano na bilauri zote zikamwagika na kuvunjika, tafrani.
Amata kutoka katika mikono ya watu wale wenye nguvu, alimwona Marilekc FikrMaryam akiwa jirani na kutoa amri kuwa wamkamate barabara. Hii ni kauli ambayo ilimtia hasira, kwa nguvu zake zote akajitutumua na kuwasukuma kando wale jamaa, wakapamiana na kuanguka kisha akawaruka huku bastola yake bado ikiwa mkononi. Akiwa hewani mmoja wa walinzi akajaribu kumshika mguu na kumkosa, Amata akaangukia ukumbini na kubiringita, alipokuja kuinuka na kupiga goti, akaweka bastola sawa na kufanya shabaha ya maana, akafyatua risasi mbili, ni yeye tu aliyemwona Martin Gupter wapi kasimama. Wakati Amata akifanya hayo yote, Martin Guter alijua wazi mbinu yake haiwezi kufaulu, kwa kutumi bastola yake akafyatua kabla ya Amata, na lengo la risasi ile lilikuwa ni kummaliza rais wa Gambia ambaye pia ni mwenyekiti wa AU. Lakini kwa hekaheka zile, risasi ikampata yule mwanadada aliyekuwa akigawa vinywaji naye akaanguka chini kama mzigo huku akitoa yowe la mauti. Walinzi wa marais wote wakawa macho tayari wakawawekea ulinzi wakuu wao na kuanza kuwaondosha ukumbini.
Amata akaanza kumfuata Gupter kwa mbio, kijana huyo alipoona kuwa njia zote zimebana, akajitupa kwenye kioo na kukitawanya vipande vipande na kuangukia nje. Amata naye akapita hapo hapo na kujikuta chini, akatzama huku na huku na kumwona Gupter akiingia kwenye gari moja wapo hapo maegeshoni. Naye akatazama huku na huko, akachukua pikipiki moja kubwa la polisi lililokuwa limeegeshwa hapo. Akwapa taarifa Gina na Chiba kuwa anamfukuza kiumbe huyo, nao akawapa kazi kuhakikisha Freddy na Amanda wanapatikana. Katika barabara hiyo Amata alipiga king’ora na magari yakaacha njia akaendelea kumtimua Gupter huku nyuma yake magari mengine ya polisi nayo yakija kwa kasi. Martin Gupter akakanyaga mafuta na gari lile lilikuwa likienda mwendo kichaa, likikata kona za hatari mpaka bodi inasugua barabara, huku bado akitafuta njia ya kumlenga Amata. Alipoona shabaha zote ni ngumu akawa amekaribia kabisa na wapi ambapo Fredy ameegesha gari, akajua sasa hapa ni kufa na kupona hakuna njia nyingine. Akafunga breki za ghafla na pikipiki la Amata llikagonga nyuma ya gari hilo. Kamanda akapaishwa juu na kutupwa mbele, akaanguka vibaya lakini kwa uzofu wake akajitahidi kutua kwa usalama, haraka akachomo bastola yake na wakati huo Martin Gupter alikuwa keshaliacha gari lile na kuingia katika lile la Fredy.
Freddy akaonesha umahiri wa kucheza na gari, akalizungusha na kusugua barabara kiasi kwamba moshi unaotokana na msuguano huo ukawachanganya polisi na magari yao yakagongana ovyo. Lakini haikuwa hivyo kwa Amata. Yote yakitukia, bastola yake ilikuwa mkononi na alipoona zile kelele zimetuli na gari likijitokeza katikati ya moshi kuja kwake hakuchelewa, akafyatua risasi ya kwanza, ya pili kisha yeye akaruka sarakasi na kutu upande wapili lile gari likapita kasi na kuacha njia likaenda kugonga mgahawa na kuingia mpka ndani. Risasi ya pili ya Amata ilizama katikati ya paji la uso la Freddy, hakuwa na ujanja, roho ikaacha mwili, gari likagonga mgahawa.
Martin Gupter akajitokeza nje ya mgahawa huo akipiga risasi ovyo na kujeruhi askari kadhaa, wakati askari wale wakitaka kumshambulia, amri ikasikika wamwache, Amata akatazama na kumwona Marilekc, hakujali, alivuta hatua na kuruka hewani kisha akagtua miguu miwili kifuani mwa Gupter na kuwenda na ye chini. Martin akainuka haraka na kumuwahi Amata kabla hajainuka, akarusha teke, Amata akaliona na kuudaka mguu kisha akauzungusha lakini kijana huyo akawa amjanja, akaruka heani na kujigeuza kisha akatua chini kwa miguu miwili na kujikunja kujiweka sawa kwa mapigano. Amata akasimama na kujifuta damu iliyokuwa ikimtoka juu ya jicho baada ya kupasuka alipoanguka barabarani.
Mapigo ya Gupter yakamfikia bila kizuizi, kila alipojaribu kujikinga akashindwa na kuanguka upande wa pili, uso wake ukakutana na wa Marilekc, akaliona tabasamu baya na dhalimu la mtu mzima huyu. Kamanda akainuka kama mbogo, Gupter alipojaribu kupelekea tena mapigo akakuntana na kigingi. Kamanda Amata aliyapangua mapigo yote na kisha akaanza kumtandika kwa mapigo ya kifo. Pigo moja zito likamvunja mbavu, Gupter kabla hajakaa sawa, akatandika pigo jingine kwenye uti wa mgongo likatengua pingili, akapewa la tatu lenye ujazo wa kilo za kutosha liakavunja mifupa miwili ya bega.
Marilekc alipoona Gupter anazidiwa, akatoa amri Amata akamatwe, akachelewa kwani kamanda aliijua hila yake, akamweka sawa Gupter na kumtandika pigo moja maridadi lililomzungusha mpaka na kumbwaga chini akiwa kinyume na sura yake, ulimi nje.
“Mwisho wa udhalimu wako umefika Marilekc, jina lako lipo kwenye mpango wa mauaji ya viongozi wetu ambao mimi mwenyewe nimeupata kule Angola. Hivi ninavyoongea vibaraka wenzako wote wamekamatwa kuanzia mjinga mwenzio Fernandes Pereira wa Angol ambaye mpango huu wewe nay eye pamoja na Ambasador Bilhani wa Tanzania mliuficha kwenye kisiwa cha Ilha Da Canzaga, mlifikiri siri haitafichuka?” Amata akazungumza kwa jaza huku mwili wa Gupter ukiwa chini na mwanamke Amanda Keller akiwa tayari kapigwa pingu na kuwekwa katika gari maalumu la wahalifu sugu, Freddy yeye aikuwa wa kwanza kukata roho kwa risasi ya Amata. Kamera za waandishi na vipaza sauti vilikuwa vimemzunguka Amata na mbele yake mtu mzima Marilekc alikuwa akimiminika jasho.
“Mwisho wa ubaya aibu, Somalia kugawanywa mara mbili ingekusaidia nini wewe? Ukamfanyia ajali Madama Selina ili upoteze ushahidi? Basi utakaa jela na kushuhudia wenzako wakifaidi maisha duniani,” akamliza na kupita katikati ya waandishi huku wengine wakitaka kumhoji na picha kadhaa zikipigwa.
Kamanda Amata baada ya hatua kadhaa mbele, akageuka nyuma na kumwona Marilekc bado amesimama palepale, akawageukia polisi na kuwaambia.
“Arrest that man!”
Wale askari wakamfuata kwa minajiri ya kumweka chini ya ulinzi mzee huyo aliyekuwa akiaminiwa na kila mmoja katika medani za usalama. Lakini hawakuhai hata kumfikia, mzee yule akachomoa bastola na kujididimiza kinywani, sekunde hiyo hiyo akafyatua na kujifumua kichwa chote kwa risasi moja tu, akaanguka chini.
Kamanda Amata akashtuka na kugeuka nyuma akamkuta ndiyo anafika chini kama kiroba cha pumba.
“Magnum 22,” akasema huku akitikisa kichwa. Kamanda Amata alikuwa na kipaji cha pekee cha kutambua aina ya bunduki kwa kusikia mlio tu pindi ikifyatuliwa. Gina na Chiba waliwasili katika eneo la tukio na moja kwa moja wakamchukua Amata na kumwingiza garini lakini. Mkuu wa polisi wale aliwafuata na kuwataka kumwacha kwani hata huyo ni mhalifu tu.
“Una uhakika na unachokisema?” Gina akamuuliza na kumwonesha kitambulisho na Chiba akafanya vivyo hivyo. Yule mkuu wa polisi akagwaya na kuwaomba tu kufika kituoni ili kuweka maelezo sawa. Amata, Chiba, Gina wakaingia garini na kuondoka eneo hilo pikipiki moja likiwasindikiza.
Na huu ndiyo ukawa mwisho wa Martin Gupter, muuaji wa kukodi aliyeinyanyasa dunia, kila kona alitafutwa asipatikane mpaka wengine akadhani kuwa ni shetani na si binadamu. Ama kweli za mwizi ni arobaini, yeye na genge lake wote walijikuta wakitumia mbinu mbovu iliyowagaharimu maisha yao nah ii ni kwa sababu waswahili husema akili nyingi mbele kiza.
TAMATI
Sehemu 25
kifaa cha Amata kikampigia alarm akakitoa na kukikamata kiganjani mwake, akatupia jicho kwenye kioo na hapo ndipo mapigo ya moyo yakabadili uelekeo. Akiwa pale juu ambapo alifika mara ya kwanza, alimpiga picha mwanamke huyu, picha ya wizi na sasa kile kifa kilikuwa kikifanaya crosssmatch ya picha za mwanamke huyo.
Amanda Keller! Akasoma jina la mwanamke huyo na mambo mengine mengine, hakusubiri sekunde wala nukta, akabadili uelekeo na kurudi kupanda tena zile ngazi kwa minajiri ya kumtia mkononi mwanamke yule. Kamanda Amata akiwa katika harakati hiyo akatoa taarifa kwa swahiba zake; yaani Gina na Chiba kuwa wachukue tahadahari kuhusu mwanamke huyo na waweke macho yao kodo ili kujmwona kama atajaribu kutoka tika jingo lile kwa njia nyingine. Ghafla akaibukia katika eneo lile la mwanzo, ambapo kulijawa na waandishi wa habari kutoka mashirika mbalimbali. Akasimama na kuangaza macho, mwanamke yule hakuonekana.
Wameniweza, kaeda wapi? Akajiuliza na kuanza kuteremka ngazi zile kwa haraka sana, mara hii hakuwa na sehemu nyingine za kwenda zaidi ya chumba cha usalama ambacho kina luninga nyingi zinasoonesha picha kutoka pande tafauti za hoteli hiyo. Alipoufikia mlango, umefungwa, akautikisa, umefungwa. Akatazama huku na huku asione mtu wa kumhofia, akachukua funguo zake na kuzitumbukiza kwenye tundu la kitasa hicho akazungusha kama mara nne hivi na mlango ukafunguka. Amata akajitoma ndani, lakini ghafla akasimama na macho yake yakatua juu ya miili miwili ya vijana wafu. Akachomo bastola yake na kurandaranda ndani ya chumba hicho, hakuna mtu, akatazama vyema miili ya watu wale na kujiridhisha kwa macho kuwa hawana uhai.
Martin Gupter! Akawaza na kuiridisha bastola ile haraka kiunoni akafunga mlango kwa ndani na kuiendea luninga moja wapo na kutazama matukio kadhaa hasa alitaka kuona nani alikuwa wa mwisho kuingi ndani ya chumba hicho. Baada ya kurudisha matukio nyuma kama dakika kumi au kumi na tano hivi ndipo akamwona anayemtaka. Kijana wamakamo, aliyevalia sare ya wahudumu wa hoteli hiyo, picha ikamwonesha akiingia na kuanza kuwashambulia mpaka kuwaua, kisha ikamwonesha akichakurachakura kwenye baadhi ya picha za siku hiyo, Amata akajua tu kuwa bila shaka alikuwa akifuta matukio kadhaa yanayomhusu yeye. Kamanda Amata akachukua flashi yake na kuipachika kwenye kompyuta nyingine na kuanza kunakila mienendo yote ya siku hiyo, aliporidhika akainyakua na kuitia mfukoni kisha akatoka ndani ya chumba kile, akafunga mlango kwa nje na kukivunja kitasa akitaka mtu asiingie kirahisi ili yeye apate muda wa kumsaka huyo hayawani.
* * *
Martin Guter hakutaka kupoteza muda, akaingia katika chumba ambacho vinywaj na vyakula mbalimbali vimehifadhiwa haswa kwa wageni maalumu. Hakuzuiwa kwa kuwa alishahabiana kabisa na wahudumu wa hoteli, na pia kwa kuwa alikwishaingia ndani ya chumba hicho kama mara tatu kama si nne. Ndani humo alijuwa wazi ni chano ipi na chakula gani ambacho kitachukuliwa na kupelekwa mezakuu. Akajifanya akiongea na wahudumua wengine huku akimimina vinywaji vikali katika bilauri. Hapa ndipo akafanya kile anachotaka, akatoa kijichupa kidogo cha pombe kali, lakini ndani yake kulikuwa na sumu mbaya inayoua kwa dakika thelathini tu kama aliyetumia kachelewa hospitali.
Baada ya kuhakikisha bilauri zote sita keshazifanyia hujuma hiyo, akabadili na chano chake kisha akachukua kingine na kuendelea na kazi ya kupelekea vinywaji. Askari waliokuwa mlangoni waliendelea kuweka ulinzi bila kujua kuwa muuaji anawapita kuingia na kutoka. Ni dakika hiyo hiyo ambayo Kamanda Amata alikuwa akipita kwenye korido hiyo na kukutana macho kwa macho na Gupter, akahisi vinyweleo vikimsimama tangu mbali, haraka aakachukua kile kifaa chake kama simu na kuanza kujifanya akiandika jambo fulani kumbe alikuwa akimpiga picha kijana huyo.
Martin Gupter naye alipomwona Amata akahisi kama anataka kuzimia, hakuamini kama anayemwona mbele yake ni yeye au kivuli wakati kichwani ana kumbukumbu kuwa mpelelezi huyo keshakufa zamani sana kule Waterloo. Almanusura amwage vinywaji lakini akajikaza, hali hii Amata aliigundua, akana wazi kuwa kuna kitu hakiko sawa. Akamtazama kwa nyuma akitembea na kuufananisha mwendo wake na sehemu tatu tu ambazo alimwona kwa karibu.
Ni yeye! Akawaza, na wakati huo akaufikia ule mlango ambao nje yake kulikuwa na ulinzi mkali. Alipofika alikuta kuna hekaheka ndani yake, kijana mmoja akiwa chini akitokwa na povu huku wenzake wakihaha kumsaidia. Kamanda hakuuliza, akaingia haraka na kujichanganya kusaidia.
“Nini kimetokea?” akamuuliza mmoja wa wahudumu.
“Hatujui, amekuywa tu kinywaji hicho kwenye glass mara akaanguka na hali ndiyo hiyo!” Amata akajibiwa, akainuka na kutazama huku na huku asione mtu wa msaada. Akaingiza mkono mfukoni na kuto kijichupa kingine cha plastiki ndani yake kulikuwa na vidonge kama kumi hivi akatoa kimoja na kwa nguvu za ziada wakambana mpaka akaachama kinywa na kukitumbukiza kile kidonge. Amata akamwacha na kuwaambia wahakikishe hakitemi. Akafika mlangoni na kuwapa amri wale askari kumtafuta yule kijana. Nao wakajikuta wakichanganyikiwa wasijue cha kufanya, akachomoa bastola yake na kutoka kasi kueleke ukumbi mkubwa.
“Martini Gupter yupo hapa, kila mmoja akae tahadhari sasa!” akasema, na taarifa ile ikamfikia Gina na Chiba.
“Copy!” akajibiwa.
Wakati Amata anafika katika ukumbi mkubwa, kwa kuwa alikuwa katika mwendo wa kukimbia walinzi wenye nguvu wakamdaka kabla hajaingia. Akatumia nguvu kujikwamua lakini akajikuta amebanwa na mikono mine yenye nguvu za vice.
“Poisssoooonnn!!!” akatamka kwa nguvu, lakini wale jamaa ndiyo kwanza wakambana barabara huku askari wengine wakielekea eneo hilo. Wakati wote huu Gina alikuwa upande wa ndani wa ukumbi huo na aliliona tukio hilo, akashindwa nini cha kufanya, baada ya kusikia neno ‘poison’, akili yake ikafanya kazi haraka sana na kutazama meza ya wakuu yule mwanadada tayari alikuwa akigawa vinywaji kwa waheshimiwa. Kutoka aliposimama alikimbia kwa hatua ndefundefu na kumfikia mwanadada yule, hakuna muda wa kuzungumza bali kumnyang’anya ile chano na bilauri zote zikamwagika na kuvunjika, tafrani.
Amata kutoka katika mikono ya watu wale wenye nguvu, alimwona Marilekc FikrMaryam akiwa jirani na kutoa amri kuwa wamkamate barabara. Hii ni kauli ambayo ilimtia hasira, kwa nguvu zake zote akajitutumua na kuwasukuma kando wale jamaa, wakapamiana na kuanguka kisha akawaruka huku bastola yake bado ikiwa mkononi. Akiwa hewani mmoja wa walinzi akajaribu kumshika mguu na kumkosa, Amata akaangukia ukumbini na kubiringita, alipokuja kuinuka na kupiga goti, akaweka bastola sawa na kufanya shabaha ya maana, akafyatua risasi mbili, ni yeye tu aliyemwona Martin Gupter wapi kasimama. Wakati Amata akifanya hayo yote, Martin Guter alijua wazi mbinu yake haiwezi kufaulu, kwa kutumi bastola yake akafyatua kabla ya Amata, na lengo la risasi ile lilikuwa ni kummaliza rais wa Gambia ambaye pia ni mwenyekiti wa AU. Lakini kwa hekaheka zile, risasi ikampata yule mwanadada aliyekuwa akigawa vinywaji naye akaanguka chini kama mzigo huku akitoa yowe la mauti. Walinzi wa marais wote wakawa macho tayari wakawawekea ulinzi wakuu wao na kuanza kuwaondosha ukumbini.
Amata akaanza kumfuata Gupter kwa mbio, kijana huyo alipoona kuwa njia zote zimebana, akajitupa kwenye kioo na kukitawanya vipande vipande na kuangukia nje. Amata naye akapita hapo hapo na kujikuta chini, akatzama huku na huku na kumwona Gupter akiingia kwenye gari moja wapo hapo maegeshoni. Naye akatazama huku na huko, akachukua pikipiki moja kubwa la polisi lililokuwa limeegeshwa hapo. Akwapa taarifa Gina na Chiba kuwa anamfukuza kiumbe huyo, nao akawapa kazi kuhakikisha Freddy na Amanda wanapatikana. Katika barabara hiyo Amata alipiga king’ora na magari yakaacha njia akaendelea kumtimua Gupter huku nyuma yake magari mengine ya polisi nayo yakija kwa kasi. Martin Gupter akakanyaga mafuta na gari lile lilikuwa likienda mwendo kichaa, likikata kona za hatari mpaka bodi inasugua barabara, huku bado akitafuta njia ya kumlenga Amata. Alipoona shabaha zote ni ngumu akawa amekaribia kabisa na wapi ambapo Fredy ameegesha gari, akajua sasa hapa ni kufa na kupona hakuna njia nyingine. Akafunga breki za ghafla na pikipiki la Amata llikagonga nyuma ya gari hilo. Kamanda akapaishwa juu na kutupwa mbele, akaanguka vibaya lakini kwa uzofu wake akajitahidi kutua kwa usalama, haraka akachomo bastola yake na wakati huo Martin Gupter alikuwa keshaliacha gari lile na kuingia katika lile la Fredy.
Freddy akaonesha umahiri wa kucheza na gari, akalizungusha na kusugua barabara kiasi kwamba moshi unaotokana na msuguano huo ukawachanganya polisi na magari yao yakagongana ovyo. Lakini haikuwa hivyo kwa Amata. Yote yakitukia, bastola yake ilikuwa mkononi na alipoona zile kelele zimetuli na gari likijitokeza katikati ya moshi kuja kwake hakuchelewa, akafyatua risasi ya kwanza, ya pili kisha yeye akaruka sarakasi na kutu upande wapili lile gari likapita kasi na kuacha njia likaenda kugonga mgahawa na kuingia mpka ndani. Risasi ya pili ya Amata ilizama katikati ya paji la uso la Freddy, hakuwa na ujanja, roho ikaacha mwili, gari likagonga mgahawa.
Martin Gupter akajitokeza nje ya mgahawa huo akipiga risasi ovyo na kujeruhi askari kadhaa, wakati askari wale wakitaka kumshambulia, amri ikasikika wamwache, Amata akatazama na kumwona Marilekc, hakujali, alivuta hatua na kuruka hewani kisha akagtua miguu miwili kifuani mwa Gupter na kuwenda na ye chini. Martin akainuka haraka na kumuwahi Amata kabla hajainuka, akarusha teke, Amata akaliona na kuudaka mguu kisha akauzungusha lakini kijana huyo akawa amjanja, akaruka heani na kujigeuza kisha akatua chini kwa miguu miwili na kujikunja kujiweka sawa kwa mapigano. Amata akasimama na kujifuta damu iliyokuwa ikimtoka juu ya jicho baada ya kupasuka alipoanguka barabarani.
Mapigo ya Gupter yakamfikia bila kizuizi, kila alipojaribu kujikinga akashindwa na kuanguka upande wa pili, uso wake ukakutana na wa Marilekc, akaliona tabasamu baya na dhalimu la mtu mzima huyu. Kamanda akainuka kama mbogo, Gupter alipojaribu kupelekea tena mapigo akakuntana na kigingi. Kamanda Amata aliyapangua mapigo yote na kisha akaanza kumtandika kwa mapigo ya kifo. Pigo moja zito likamvunja mbavu, Gupter kabla hajakaa sawa, akatandika pigo jingine kwenye uti wa mgongo likatengua pingili, akapewa la tatu lenye ujazo wa kilo za kutosha liakavunja mifupa miwili ya bega.
Marilekc alipoona Gupter anazidiwa, akatoa amri Amata akamatwe, akachelewa kwani kamanda aliijua hila yake, akamweka sawa Gupter na kumtandika pigo moja maridadi lililomzungusha mpaka na kumbwaga chini akiwa kinyume na sura yake, ulimi nje.
“Mwisho wa udhalimu wako umefika Marilekc, jina lako lipo kwenye mpango wa mauaji ya viongozi wetu ambao mimi mwenyewe nimeupata kule Angola. Hivi ninavyoongea vibaraka wenzako wote wamekamatwa kuanzia mjinga mwenzio Fernandes Pereira wa Angol ambaye mpango huu wewe nay eye pamoja na Ambasador Bilhani wa Tanzania mliuficha kwenye kisiwa cha Ilha Da Canzaga, mlifikiri siri haitafichuka?” Amata akazungumza kwa jaza huku mwili wa Gupter ukiwa chini na mwanamke Amanda Keller akiwa tayari kapigwa pingu na kuwekwa katika gari maalumu la wahalifu sugu, Freddy yeye aikuwa wa kwanza kukata roho kwa risasi ya Amata. Kamera za waandishi na vipaza sauti vilikuwa vimemzunguka Amata na mbele yake mtu mzima Marilekc alikuwa akimiminika jasho.
“Mwisho wa ubaya aibu, Somalia kugawanywa mara mbili ingekusaidia nini wewe? Ukamfanyia ajali Madama Selina ili upoteze ushahidi? Basi utakaa jela na kushuhudia wenzako wakifaidi maisha duniani,” akamliza na kupita katikati ya waandishi huku wengine wakitaka kumhoji na picha kadhaa zikipigwa.
Kamanda Amata baada ya hatua kadhaa mbele, akageuka nyuma na kumwona Marilekc bado amesimama palepale, akawageukia polisi na kuwaambia.
“Arrest that man!”
Wale askari wakamfuata kwa minajiri ya kumweka chini ya ulinzi mzee huyo aliyekuwa akiaminiwa na kila mmoja katika medani za usalama. Lakini hawakuhai hata kumfikia, mzee yule akachomoa bastola na kujididimiza kinywani, sekunde hiyo hiyo akafyatua na kujifumua kichwa chote kwa risasi moja tu, akaanguka chini.
Kamanda Amata akashtuka na kugeuka nyuma akamkuta ndiyo anafika chini kama kiroba cha pumba.
“Magnum 22,” akasema huku akitikisa kichwa. Kamanda Amata alikuwa na kipaji cha pekee cha kutambua aina ya bunduki kwa kusikia mlio tu pindi ikifyatuliwa. Gina na Chiba waliwasili katika eneo la tukio na moja kwa moja wakamchukua Amata na kumwingiza garini lakini. Mkuu wa polisi wale aliwafuata na kuwataka kumwacha kwani hata huyo ni mhalifu tu.
“Una uhakika na unachokisema?” Gina akamuuliza na kumwonesha kitambulisho na Chiba akafanya vivyo hivyo. Yule mkuu wa polisi akagwaya na kuwaomba tu kufika kituoni ili kuweka maelezo sawa. Amata, Chiba, Gina wakaingia garini na kuondoka eneo hilo pikipiki moja likiwasindikiza.
Na huu ndiyo ukawa mwisho wa Martin Gupter, muuaji wa kukodi aliyeinyanyasa dunia, kila kona alitafutwa asipatikane mpaka wengine akadhani kuwa ni shetani na si binadamu. Ama kweli za mwizi ni arobaini, yeye na genge lake wote walijikuta wakitumia mbinu mbovu iliyowagaharimu maisha yao nah ii ni kwa sababu waswahili husema akili nyingi mbele kiza.
TAMATI