- Thread starter
- #81
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya
"Anakuja kesho jioni utamuona. Usimuogope kuwa muwazi. Atakusaidia amini Frida amini kuwa bado unao umuhimu mkubwa sana katika hii jamii. Jiamini kuwa Tanzania inakuhitaji sana." Kasuku alisisitiza.
Frida alijenga tumaini jipya baada ya kusikia kuwa atakutanishwa na muwezeshaji wa yatima na watoto wasiokuwa na makazi.
Muda mwingi Frida alikuwa akizungumza na Kasuku mambo mbalimbali ambayo yalimjenga tena kisaikolojia.
"Frida..hutakiwi kuwa mtu wa kukata tamaa, ni kweli maisha ya mtaani yana kero kubwa lakini jiulize, mfano sasa u mjamzito. Ulitaka kukiua hicho kiumbe bila kosa. Ni upendo gani unao wewe hadi kufikia kuiua damu yako?? Lazima ujifikirie na iwapo ni sahihi basi wasilaumiwe wale waliowatupa watoto wao, asilaumiwe mama aliyekuzaa akiwa gerezani na hata mkuu wa gereza, mkuu wa kituo cha watoto yatima wote wasilaumiwe. Wapo sawa." Maneno haya makali na yenye kuuweka ukweli wazi yalimgusa sana Frida. Sasa akajutia kitendo chake cha kujaribu kujitosa majini ili aweze kufa.
"Hivi ulijifikiria nini na wewe ukajirusha baharini. Ungekufa je?" hatimaye alimuuliza huku akitabasamu, kana kwamba haamini kabisa kuwa inawezekana mwanadamu wa kawaida kujitosa majini kwa ajili ya kumwokoa mtu.
"Ni kiherehere changu tu, naitwa Kasuku napenda kujua mengi hata yasiyonihusu." Alijibu kwa sauti iliyojaa utani. Wakacheka kisha kugonganisha mikono.
Wakati wakifanya hayo, jicho kali sana liliwatazama bila wao kujua kama wametazamwa. Jicho hili likafanya tafsiri ya kuchezewa shere ama kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa. Wivu ukatambaa na kuusulubisha moyo wake wa nyama.
Furaha ya Kasuku na Frida haikumpendeza.
Akakimbilia chumbani, kukiwahi kilio chake kisiweze kusikiwa na wengi.
Akiwa chumbani binti huyu alijikuta akiilaani kazi aliyokuwa anaifanya Kasuku, kazi ya uandishi wa habari. Kwani kazi hii ilimfanya kukutana na wanawake wengi tena wenye mvuto kumshinda yeye.
"Emiliana amka amka umelala.." aliongea maneno hayo huku akijipigapiga kichwa chake. Hakika alikuwa amelala. Analetewa mwanamke nyumbani kwake!!
Hisia potofu zikamtuma kuwa Frida na Kasuku wana mahusiano na wanatumia kigezo cha uandishi wa makala kuficha maovu yao.
Emiliana alikuwa na haki ya kulalamika, alikuwa na haki ya kuwa na wivu. Mara ya kwanza alimkuta Kasuku akiwa anambembeleza yule binti tena akiwa amemlaza mapajani.
Mara ya pili akaenda naye kumfanyia manunuzi ya nguo. Tena nzurinzuri zilizoufanya urembo wake uanze kuonekana. Na zile nywele zenye asili ya kiarabu kwa mbali zikang'ara.
Sasa amewafumania wakicheka kisha wakagonga mikono.
Hata!! Wanafahamiana hawa, tena siku nyingi. Alipitisha jibu hilo binti huyu ambaye ndio kwanza alikuwa anakaribia kufunga ndoa na Kasuku. Mwandishi wa habari na makala katika magazeti.
Leo namweleza kila kitu!!
Ulipofika wakati wa chakula cha mchana, Emmy akiwa analazimisha tabasamu usoni alimwandalia mumewe mtarajiwa chakula chumbani badala ya meza ya kulia kama ilivyo kawaida.
Meza kuu akasalia Frida peke yake. Hilo halikumuumiza kichwa.
Huko chumbani Emmy akautua uchungu wake!!
"Kwa hiyo kuna mawili Kasuku, aidha niondoke ama huyo hawara yako aiache nyumba hii. Msaada uliompatia imetosha. Iam not mtoto mdogo ujue." Alipandisha jazba, Kasuku akaamua kuyatatua haya kwa busara. Alijua yale ni mapenzi tu na si kwamba Emmy ana roho mbaya.
"Ataondoka mpenzi usijali!!" alikubali yaishe.
"Lini?"
"Nimekwambia usijali." Alizungumza kwa hasira kiasi, hakupendezwa na yale maswali ya mahakamani.
Chakula hakikulika tena.
Kasuku aliporejea mezani ili kuzungumza na Frida. Tayari muda wa kumpokea mgeni ulikuwa umefika.
Ni kama alikuwa mzungu mwenye ngozi nyeusi bwana Mathias.
Alifika kwa wakati. Akapokelewa.
Furaha ya Kasuku ikarejea kiasi fulani.
Walifika nyumbani na kuingia moja kwa moja katika mazungumzo.
Walizungumza mengi sana. Mathias Dembele akionekana kuguswa sana na yaliyomtokea Frida.
Kwa kumtazama mbele yake hakuamini kama kweli yule ni chokoraa. Alikuwa amependeza tena kwa hizo siku kadhaa alizoishi kwa Kasuku.
Baadaye Kasuku ili kupata ushauri aliamua kumuelezea Mathiasi juu ya tatizo la mchumba wake.
"Hiyo ni kawaida ya wanawake. Ila anyway usijali, naweza kukusaidia bwana Kasuku. Nitampeleka mahali kama utaniruhusu. Nimeguswa sana." Mathias alitoa kauli ambayo ilimpa ahueni Kasuku.
Wakati wa kuondoka waliandamana na Frida.
Akahakikishiwa kuwa yu katika mikono salama.
Mikono ya Mathias Dembele.
*****
Nyumba kubwa ya kifahari iliyozungushiwa uzio unaodhibitiwa na umeme ilimshangaza mwanadada Frida. Nyumba hizi alizoea kuziona mandhari yake ya nje tu maeneo ya posta na kwingineko Kariakoo.
Baada ya kengele kubonyezwa geti lilifunguliwa.
Gari ikazama ndani!! Injini ikazimwa. Wakashuka.
Kimya kikubwa kilikuwa kimetanda, ndege aina ya kasuku akawapokea kwa shangwe. Mathias akachekelea kuitwa bosi na yule kasuku.
Akamshika kichwa kasuku akajichekesha. Frida naye akacheka.
Maajabu haya ndege anaongea!!
Mlango ulikuwa wazi, akakaribishwa, ndani aliwakuta watu wawili wanaume. Wakatoa tabasamu na kumkaribisha kwa Kiswahili kibovu. Baada ya hapo hakujua linaloendelea maana walikuwa wakiongea lugha ya kigeni.
Frida akawa mgeni katika hili.
Kisha mathias akamvuta kando wakanong'ona kidogo. Mathias akatoweka, Frida akabaki na wenyeji wasioelewa Kiswahili.
Frida akatamani kuwa mtaani alale nje usiku kuliko kuishi mahali pazuri bila kuwa na amani.
*****
Mwanaidi baada ya kuwa amempoteza Frida katika mazingira ya kustaajabisha. Sasa aliikumbuka furaha yake nyingine iliyosahaulika.
Alimkumbuka mama yake George. Ile sura aliyokutana nayo usiku ule ikamkimbiza haikutaka kutoweka katika ubongo wake. Akajiuliza kwa nini iwe hivyo.
Kwa mara nyingine akaamua kurejea katika maeneo yale. Sasa alikuwa anaulizia kwa kila namna aliyoweza.
Kuhusu mama mlemavu hapo hakuambulia kitu.
Lakini mama kichaa, hapa majibu kadhaa yalikuwepo.
"Yule si ndo aliyechukuliwa na Dembele au?" alijibu bwana mmoja kwa njia ya kuwauliza wenzake.
Wote wakakubaliana kuwa ni kweli. Frida akawalipa pesa kwa malipo ya kuuliza na kujibiwa.
Hapo ndiyo Dar es salaam!! Kila kitu ni biashara.
Malipo yaliyofuata ni kupelekwa nyumbani kwa Dembele.
Mwanaidi akapatazama siku hiyo lakini hakuingia nia yake ilikuwa kumfahamu kwanza Dembele.
Alikuwa maarufu haikumchukua muda kumfahamu baada tu ya kupita na gari lake.
Kama ilivyo kawaida yake, hakurupuki anafanya mambo kwa hatua.
Alianza rasmi kuzifuatilia nyendo za Dembele. Hatimaye akapata nafasi ya kuingia kwake kama msichana anayetafuta kazi. Aliingia akiwa anatambua fika kuwa Dembele hayupo nyumbani.
Japo hakupata kazi. Hata huyo mama anayesadikiwa kuchukuliwa na Dembele hakuweza kumuona pia.
Duniani hakuna siri, katika harakati zake za kumfuatilia bwana huyu alizipata habari za juu juu kuwa bwana Mathias ni ‘zungu la unga'. Tetesi hizi zikamkuna. Akahisi kuna jambo.
Hatua iliyofuata ni kuonana moja kwa moja na Mathiasi Dembele, lakini katika njia ya siri sana.
Subira yavuta heri. Siku ikawadia aliyoingoja Mwanaidi.
Mathias Dembele alikuwa analewa na rafiki zake.
Mwanaidi akaivaa fani ya uigizaji, akayaigiza maisha yake halisi ya uchokoraa. Akamvamia Dembele huku akiwa na huzuni, akamlilia sana akalia akiuhitaji msaada wake. Kwa kilio chake hata walevi walishikwa na huruma.
Mathias Dembele akauvaa mkenge.
Akakatisha shughuli ya kujiongezea ulevi kichwani.
Akamchukua Mwanaidi hadi garini.
Akaaga na kuondoka naye. Mwanaidi akaombea mahesabu yake yaende sawa. Alikuwa na ile silaha yake ya kila siku ya kujilinda.
Kisu!!
*****
Suala la Frida kuwa mjamzito na mzigo mkubwa uliokuwepo kwa ajili ya kusafirishwa kuelekea ughaibuni lilimuumiza kichwa Mathiasi. Ni kweli aliguswa sana na maisha aliyopitia Frida lakini baada ya kumweka katika himaya yake ile huruma ikatoweka akawa Mathias yuleyule.
Alijiuliza ni wapi anaweza kupata mtu wa upesiupesi kuubeba mzigo ule. Sasa bahati ikajileta mbele yake.
Akakutana na binti aliyepevuka katika kilabu cha walevi.
Mwanaidi!!
Kwa umbo lake komavu aliamini kuwa anaweza kubeba kete kadhaa za madawa ya kulevya bila wasiwasi.
Kisha hiyo inakuwa safari yake ya mwisho maana akirejea Tanzania atazua tafrani.
Mbebaji aliyeruhusiwa kwenda Tanzania na kurudi alikuwa ni mmoja tu. Mwanamke mnene asiyekuwa na akili timamu. Huyu hata akiachiwa kuingia mitaani bado hataweza kusema lolote.
Nani wa kumuamini?
Mathiasi aliamua kumfikisha Mwanaidi moja kwa moja katika machinjio yake. Nyumba inayomwaga damu za yatima na chokoraa.
Kwa mtazamo wan je alimchukulia Mwanaidi kama chokoraa wengine dhaifu wa kike waliobakwa sana na hatimaye kuwa legelege wanaokubali kusukumwa hovyo.
Akamfikisha katika jumba lile akamkabidhi kwa wale wanaume wasiojua kishwahili vizuri.
Akaagana naye kwa ahadi kama alizompa Frida siku tano zilizopita.
Kisha akatoweka na gari lake akiamini kila kitu kitaenda barabara.
Alipofika nyumbani alipokelewa na magazeti. Akafunua ukurasa wa kasuku.
"MATHIAS DEMBELE: Mwanadamu mmoja kati ya mamilioni ya watu!!" ilikuwa makala ya kumpongeza kwa moyo wake wa kujitolea na kufanikisha ndoto za Yatima wengi.
Mathias akatabasamu.
Wajinga ndio waliwao!!
Alidhihaki!!
Kisha akalala akitegemea kila kitu kitaenda kama alivyopanga.
Mzigo ulitarajiwa kuondoka alfajiri sana!!
***DEMBELE anawatoa kafara watoto kwa faida zake binafsi..sasa amemuweka kikaangoni Mwanaidi. Je ndo mwisho wake?? Je ataonana na Frida? Vipi kuhusu mama mwendawazimu?
***GEORGE NA ISHA NA mimba yao kitajiri nini???
ITAENDELEA!! !!
VAN HEIST muuza ubuyu amina mabata shabani hassani culbby sam II ram BPM mbalu saljar MAVUNO Khantwe
MTUNZI: George Iron Mosenya
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI
"Nilikwambia..haooo wameanza kupiga simu…ile simulizi yako lazima kwa mwanadamu mwenye nyama aguswe ipasavyo. Huyu aliyepiga simu ni mmoja kati ya wadau wakubwa hapa nchini kwa kuwezesha yatima." Alisema bwana Kasuku huku akinyanyua mabega yake juu.
"Anakuja kesho jioni utamuona. Usimuogope kuwa muwazi. Atakusaidia amini Frida amini kuwa bado unao umuhimu mkubwa sana katika hii jamii. Jiamini kuwa Tanzania inakuhitaji sana." Kasuku alisisitiza.
Frida alijenga tumaini jipya baada ya kusikia kuwa atakutanishwa na muwezeshaji wa yatima na watoto wasiokuwa na makazi.
Muda mwingi Frida alikuwa akizungumza na Kasuku mambo mbalimbali ambayo yalimjenga tena kisaikolojia.
"Frida..hutakiwi kuwa mtu wa kukata tamaa, ni kweli maisha ya mtaani yana kero kubwa lakini jiulize, mfano sasa u mjamzito. Ulitaka kukiua hicho kiumbe bila kosa. Ni upendo gani unao wewe hadi kufikia kuiua damu yako?? Lazima ujifikirie na iwapo ni sahihi basi wasilaumiwe wale waliowatupa watoto wao, asilaumiwe mama aliyekuzaa akiwa gerezani na hata mkuu wa gereza, mkuu wa kituo cha watoto yatima wote wasilaumiwe. Wapo sawa." Maneno haya makali na yenye kuuweka ukweli wazi yalimgusa sana Frida. Sasa akajutia kitendo chake cha kujaribu kujitosa majini ili aweze kufa.
"Hivi ulijifikiria nini na wewe ukajirusha baharini. Ungekufa je?" hatimaye alimuuliza huku akitabasamu, kana kwamba haamini kabisa kuwa inawezekana mwanadamu wa kawaida kujitosa majini kwa ajili ya kumwokoa mtu.
"Ni kiherehere changu tu, naitwa Kasuku napenda kujua mengi hata yasiyonihusu." Alijibu kwa sauti iliyojaa utani. Wakacheka kisha kugonganisha mikono.
Wakati wakifanya hayo, jicho kali sana liliwatazama bila wao kujua kama wametazamwa. Jicho hili likafanya tafsiri ya kuchezewa shere ama kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa. Wivu ukatambaa na kuusulubisha moyo wake wa nyama.
Furaha ya Kasuku na Frida haikumpendeza.
Akakimbilia chumbani, kukiwahi kilio chake kisiweze kusikiwa na wengi.
Akiwa chumbani binti huyu alijikuta akiilaani kazi aliyokuwa anaifanya Kasuku, kazi ya uandishi wa habari. Kwani kazi hii ilimfanya kukutana na wanawake wengi tena wenye mvuto kumshinda yeye.
"Emiliana amka amka umelala.." aliongea maneno hayo huku akijipigapiga kichwa chake. Hakika alikuwa amelala. Analetewa mwanamke nyumbani kwake!!
Hisia potofu zikamtuma kuwa Frida na Kasuku wana mahusiano na wanatumia kigezo cha uandishi wa makala kuficha maovu yao.
Emiliana alikuwa na haki ya kulalamika, alikuwa na haki ya kuwa na wivu. Mara ya kwanza alimkuta Kasuku akiwa anambembeleza yule binti tena akiwa amemlaza mapajani.
Mara ya pili akaenda naye kumfanyia manunuzi ya nguo. Tena nzurinzuri zilizoufanya urembo wake uanze kuonekana. Na zile nywele zenye asili ya kiarabu kwa mbali zikang'ara.
Sasa amewafumania wakicheka kisha wakagonga mikono.
Hata!! Wanafahamiana hawa, tena siku nyingi. Alipitisha jibu hilo binti huyu ambaye ndio kwanza alikuwa anakaribia kufunga ndoa na Kasuku. Mwandishi wa habari na makala katika magazeti.
Leo namweleza kila kitu!!
Ulipofika wakati wa chakula cha mchana, Emmy akiwa analazimisha tabasamu usoni alimwandalia mumewe mtarajiwa chakula chumbani badala ya meza ya kulia kama ilivyo kawaida.
Meza kuu akasalia Frida peke yake. Hilo halikumuumiza kichwa.
Huko chumbani Emmy akautua uchungu wake!!
"Kwa hiyo kuna mawili Kasuku, aidha niondoke ama huyo hawara yako aiache nyumba hii. Msaada uliompatia imetosha. Iam not mtoto mdogo ujue." Alipandisha jazba, Kasuku akaamua kuyatatua haya kwa busara. Alijua yale ni mapenzi tu na si kwamba Emmy ana roho mbaya.
"Ataondoka mpenzi usijali!!" alikubali yaishe.
"Lini?"
"Nimekwambia usijali." Alizungumza kwa hasira kiasi, hakupendezwa na yale maswali ya mahakamani.
Chakula hakikulika tena.
Kasuku aliporejea mezani ili kuzungumza na Frida. Tayari muda wa kumpokea mgeni ulikuwa umefika.
Ni kama alikuwa mzungu mwenye ngozi nyeusi bwana Mathias.
Alifika kwa wakati. Akapokelewa.
Furaha ya Kasuku ikarejea kiasi fulani.
Walifika nyumbani na kuingia moja kwa moja katika mazungumzo.
Walizungumza mengi sana. Mathias Dembele akionekana kuguswa sana na yaliyomtokea Frida.
Kwa kumtazama mbele yake hakuamini kama kweli yule ni chokoraa. Alikuwa amependeza tena kwa hizo siku kadhaa alizoishi kwa Kasuku.
Baadaye Kasuku ili kupata ushauri aliamua kumuelezea Mathiasi juu ya tatizo la mchumba wake.
"Hiyo ni kawaida ya wanawake. Ila anyway usijali, naweza kukusaidia bwana Kasuku. Nitampeleka mahali kama utaniruhusu. Nimeguswa sana." Mathias alitoa kauli ambayo ilimpa ahueni Kasuku.
Wakati wa kuondoka waliandamana na Frida.
Akahakikishiwa kuwa yu katika mikono salama.
Mikono ya Mathias Dembele.
*****
Nyumba kubwa ya kifahari iliyozungushiwa uzio unaodhibitiwa na umeme ilimshangaza mwanadada Frida. Nyumba hizi alizoea kuziona mandhari yake ya nje tu maeneo ya posta na kwingineko Kariakoo.
Baada ya kengele kubonyezwa geti lilifunguliwa.
Gari ikazama ndani!! Injini ikazimwa. Wakashuka.
Kimya kikubwa kilikuwa kimetanda, ndege aina ya kasuku akawapokea kwa shangwe. Mathias akachekelea kuitwa bosi na yule kasuku.
Akamshika kichwa kasuku akajichekesha. Frida naye akacheka.
Maajabu haya ndege anaongea!!
Mlango ulikuwa wazi, akakaribishwa, ndani aliwakuta watu wawili wanaume. Wakatoa tabasamu na kumkaribisha kwa Kiswahili kibovu. Baada ya hapo hakujua linaloendelea maana walikuwa wakiongea lugha ya kigeni.
Frida akawa mgeni katika hili.
Kisha mathias akamvuta kando wakanong'ona kidogo. Mathias akatoweka, Frida akabaki na wenyeji wasioelewa Kiswahili.
Frida akatamani kuwa mtaani alale nje usiku kuliko kuishi mahali pazuri bila kuwa na amani.
*****
Mwanaidi baada ya kuwa amempoteza Frida katika mazingira ya kustaajabisha. Sasa aliikumbuka furaha yake nyingine iliyosahaulika.
Alimkumbuka mama yake George. Ile sura aliyokutana nayo usiku ule ikamkimbiza haikutaka kutoweka katika ubongo wake. Akajiuliza kwa nini iwe hivyo.
Kwa mara nyingine akaamua kurejea katika maeneo yale. Sasa alikuwa anaulizia kwa kila namna aliyoweza.
Kuhusu mama mlemavu hapo hakuambulia kitu.
Lakini mama kichaa, hapa majibu kadhaa yalikuwepo.
"Yule si ndo aliyechukuliwa na Dembele au?" alijibu bwana mmoja kwa njia ya kuwauliza wenzake.
Wote wakakubaliana kuwa ni kweli. Frida akawalipa pesa kwa malipo ya kuuliza na kujibiwa.
Hapo ndiyo Dar es salaam!! Kila kitu ni biashara.
Malipo yaliyofuata ni kupelekwa nyumbani kwa Dembele.
Mwanaidi akapatazama siku hiyo lakini hakuingia nia yake ilikuwa kumfahamu kwanza Dembele.
Alikuwa maarufu haikumchukua muda kumfahamu baada tu ya kupita na gari lake.
Kama ilivyo kawaida yake, hakurupuki anafanya mambo kwa hatua.
Alianza rasmi kuzifuatilia nyendo za Dembele. Hatimaye akapata nafasi ya kuingia kwake kama msichana anayetafuta kazi. Aliingia akiwa anatambua fika kuwa Dembele hayupo nyumbani.
Japo hakupata kazi. Hata huyo mama anayesadikiwa kuchukuliwa na Dembele hakuweza kumuona pia.
Duniani hakuna siri, katika harakati zake za kumfuatilia bwana huyu alizipata habari za juu juu kuwa bwana Mathias ni ‘zungu la unga'. Tetesi hizi zikamkuna. Akahisi kuna jambo.
Hatua iliyofuata ni kuonana moja kwa moja na Mathiasi Dembele, lakini katika njia ya siri sana.
Subira yavuta heri. Siku ikawadia aliyoingoja Mwanaidi.
Mathias Dembele alikuwa analewa na rafiki zake.
Mwanaidi akaivaa fani ya uigizaji, akayaigiza maisha yake halisi ya uchokoraa. Akamvamia Dembele huku akiwa na huzuni, akamlilia sana akalia akiuhitaji msaada wake. Kwa kilio chake hata walevi walishikwa na huruma.
Mathias Dembele akauvaa mkenge.
Akakatisha shughuli ya kujiongezea ulevi kichwani.
Akamchukua Mwanaidi hadi garini.
Akaaga na kuondoka naye. Mwanaidi akaombea mahesabu yake yaende sawa. Alikuwa na ile silaha yake ya kila siku ya kujilinda.
Kisu!!
*****
Suala la Frida kuwa mjamzito na mzigo mkubwa uliokuwepo kwa ajili ya kusafirishwa kuelekea ughaibuni lilimuumiza kichwa Mathiasi. Ni kweli aliguswa sana na maisha aliyopitia Frida lakini baada ya kumweka katika himaya yake ile huruma ikatoweka akawa Mathias yuleyule.
Alijiuliza ni wapi anaweza kupata mtu wa upesiupesi kuubeba mzigo ule. Sasa bahati ikajileta mbele yake.
Akakutana na binti aliyepevuka katika kilabu cha walevi.
Mwanaidi!!
Kwa umbo lake komavu aliamini kuwa anaweza kubeba kete kadhaa za madawa ya kulevya bila wasiwasi.
Kisha hiyo inakuwa safari yake ya mwisho maana akirejea Tanzania atazua tafrani.
Mbebaji aliyeruhusiwa kwenda Tanzania na kurudi alikuwa ni mmoja tu. Mwanamke mnene asiyekuwa na akili timamu. Huyu hata akiachiwa kuingia mitaani bado hataweza kusema lolote.
Nani wa kumuamini?
Mathiasi aliamua kumfikisha Mwanaidi moja kwa moja katika machinjio yake. Nyumba inayomwaga damu za yatima na chokoraa.
Kwa mtazamo wan je alimchukulia Mwanaidi kama chokoraa wengine dhaifu wa kike waliobakwa sana na hatimaye kuwa legelege wanaokubali kusukumwa hovyo.
Akamfikisha katika jumba lile akamkabidhi kwa wale wanaume wasiojua kishwahili vizuri.
Akaagana naye kwa ahadi kama alizompa Frida siku tano zilizopita.
Kisha akatoweka na gari lake akiamini kila kitu kitaenda barabara.
Alipofika nyumbani alipokelewa na magazeti. Akafunua ukurasa wa kasuku.
"MATHIAS DEMBELE: Mwanadamu mmoja kati ya mamilioni ya watu!!" ilikuwa makala ya kumpongeza kwa moyo wake wa kujitolea na kufanikisha ndoto za Yatima wengi.
Mathias akatabasamu.
Wajinga ndio waliwao!!
Alidhihaki!!
Kisha akalala akitegemea kila kitu kitaenda kama alivyopanga.
Mzigo ulitarajiwa kuondoka alfajiri sana!!
***DEMBELE anawatoa kafara watoto kwa faida zake binafsi..sasa amemuweka kikaangoni Mwanaidi. Je ndo mwisho wake?? Je ataonana na Frida? Vipi kuhusu mama mwendawazimu?
***GEORGE NA ISHA NA mimba yao kitajiri nini???
ITAENDELEA!! !!
VAN HEIST muuza ubuyu amina mabata shabani hassani culbby sam II ram BPM mbalu saljar MAVUNO Khantwe