Riwaya: Chokoraa

Riwaya: Chokoraa

RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya




SEHEMU YA KUMI NA SABA

Mwanaume anasita kwa muda anafanya tafakari. Tamaa inazidi nguvu maamuzi. Anamkumbatia yule msichana aliyekondeana.
“Bonge kuna UKIMWI…kuna kisonono, kuna fangasi…Bonge…Bonge!! Shauri zako.” Sauti ilimwambia katika nafsi yake. Akatamani kuacha lakini alikuwa amtamanika tayari!! Angefanya nini.
Akaitawanya kanga ya yule binti. Akaanguka naye chini. Badala ya kutua chini wakatua katika kitu kingine. Kikaunguruma.
Wakatulia. Bonge suruali magotini, binti kanga pembeni.
Kikaunguruma tena.
Hapa sasa Bonge akawa mwanariadha mzuri, huku Isha akimfuatia kwa kasi.
Walienda pande mbili tofauti.
Dada mkubwa Regina naye alishtushwa na hali hii. Chokoraa hana ngojangoja. Naye akatimua mbio.
Walifurahisha kuwatazama.


Bonge hakugeuka nyuma, japo zilikuwa njia za kubumba lakini aliweza kufika katika handaki bila kukosea. Alikuwa anathema juu juu, wakati wa kuondoka hakuaga mtu lakini mwanasoka huyu wa zamani baada ya matatizo haya sasa anamkurupua Kelvin.
Anamtoa nje ya handaki na kumsimulia mkasa wote. Hapa akiwa ameikamata vyema suruali yake kiunoni isiweze kudondoka. Miguuni palikuwa patupu, viatu vyake alivisahau maksudi kutokana na kashkash aliyokumbana nayo huko alipotoka. NDIYO, asingeweza kujiuliza mara mbilimbili iwapo achukue kwanza viatu ama atimue mbio kuokoa uhai wake.


Kelvin alikuwa akicheka tangu simulizi ile inaanza kuhadithiwa. Hadi Bonge alipoweka kituo cha mwisho. Hapakuwa na la kushauriana zaidi ya kungoja asubuhi waende kutazama kulikoni.
Wakarejea ndani ya handaki waweze kulala tena.
Baada ya dakika chache walikuwa wanakoroma.
Wakati chokoraa hawa wanakoroma na kuota ndoto mbalimbali za utajiri siku za usoni, kuna watu walikuwa wanaamka na kuingia katika shughuli zao. Na wengine hawakuwa wamelala kabisa.


*****


Huyu alitamani kulala lakini usingizi ulizidiwa nguvu na maumivu ya ajabu aliyokuwa anayapata katika sehemu zake za siri. Alikuwa anajikuna kwa jitihada zote lakini bado hali ilikuwa tete.
Akaanza kutetemeka, alitokwa machozi hakuwepo wa kuyafuta. Alikuwa peke yake nje ya chumba cha hospitali ya Mwananyamala jijini Dar. Hapakuwa na dalili yoyote ya kuhudumiwa. Kwani yeye nani?
Wamelia wanawake wengi miaka nenda rudi. Yeye kilio chake kina tofauti gani?
Mbaya zaidi hana pesa. Ilimuumiza.
Muwasho ulizidi kukua na kusambaa. Mwili nao ukashikwa ganzi.
Ni kama alikuwa anaumwa uchungu.
Hali hii ya kuwashwa kwa siku hii ilikuwa imezidi siku mbili zilizopita alipoanza kuwashwa akiwa katika chumba cha mahabusu akingoja kesi yake kuanza kusikilizwa.
Hakuwahi kuyajua magonjwa ya zinaa zaidi ya kusikia mara moja moja katika vyombo vya habari na kwa kutumia elimu yake ndogo ya shule ya msingi.
Sasa alikuwa anadhani ni muwasho wa kawaida, lakini muwasho huu sasa unamtesa.
“Umefanya ngono lini? Na nani?” daktari alimuuliza.
“Sikumbuki..” alijibu huku akitetemeka kwa uchungu unaomkabiri.
Daktari akakerwa na jibu hilo akamtupia tusi la nguoni, akimtukania ukoo wake mzima.
Binti hakusema lolote.
Daktari aliendelea na yake baada ya kuwa amemchukua vipimo na kupata majibu kuwa binti huyu alikuwa na kisonono kilichokomaa ndani kwa ndani kutokana na kukosa tiba ya upesi.
Dawa kwa ajili ya kisonono kilichokomaa ilikuwa inagharimu pesa ambayo kwa namna yoyote yule binti asingeweza kuipata kwa wakati ule.
“Mwanaidi nakupatia dawa ya kutuliza muwasho kwa masaa. Nenda ukatafute pesa kwa ajili ya dawa. Msaada wangu wa mwisho umekuwa huo mdogo wangu. Hakikisha unaipata hiyo pesa vinginevyo hautaweza kutibika tena ugonjwa huo” Daktari alijieleza kwa utulivu. Mwanaidi akatikisa kichwa kukubali. Alikuwa ana hofu!!
Daktari akaandika madawa kasha akamsogelea na kunong’ona, “Ukipona mwambie awe anatumia kinga….”
Mwanaidi akakubali yaishe!! Hakujua hata huyo mtu anayezungumziwa ni nani. Je ni yule askari aliyembaka siku mbili zilizopita wakiwa rumande ama ni yule mwanaume aliyelala naye kabla ya kutiwa mikononi mwa polisi.
Akapatiwa dawa na kuimeza pale pale.
“Unaishi wapi.” Daktari huyu aliyekuwa na matusi alimuuliza.
“Magomeni Mikumi.” Alijibu huku akijua kuwa anaishi mitaani katika jamii yake ya chokoraa.
Daktari akampatia shilingi elfu mbili. Akaondoka na kujituliza nje katika viti.
Dawa ikafanya kazi, muwasho ukapungua hatimaye ukapoa.
Mwanaidi akatoweka. Akaenda katika mtaa aliouzoea akajichanganya hapa na pale akapata mahali akajilaza.
Saa kumi na moja alfajiri alikuwa macho tayari. Wima anajiuliza aanzie wapi, kuitafuta pesa ya madawa.
Kama ilivyokuwa ngumu kupata jibu la aanzie wapi kuipata pesa. Ndivyo ilivyokuwa ngumu kwa upande wa pili.
Isha naye alikuwa wima akijiuliza arejee kuifuata kanga yake aliyoisahau kule chemba alipotakiwa kubakwa, ama atimue mbio kuelekea atakapojua yeye.
Kutimua mbio halikuwa jibu la swali lake. Akaamua kumuamsha Frida.
Wakajikongoja pembeni ambapo hawakuweza kusikiwa na mtu. Isha akahadithia kilichotokea.
Frida alikuwa na asili ya uoga. Hakukubaliana na suala la kurejea tena kule katika chemba kutazama nini kilichokoroma na kuwashtua wawili hawa.
“Hapa tuondoke mwenzangu…bora hata posta.” Frida alishauri.
Saa kumi na mbili hawakuwa eneo lile.


*****
Upande wa Mwanaidi naye alikuwa amepata jawabu baada ya kujizungusha hapa na pale, jua likachomoza, akatafuta kibanda cha hadhi ya chini kabisa cha mama n’tilie, akaingia kuitibu njaa yake. Kasha akapanda gari.
Safari ya kwenda nyumbani kwa Emma ambaye alikuwa mikononi mwa polisi. Nia ya Mwanaidi ilikuwa kuonana na yule mama.
Aliamini anaweza kupata msaada. Walau wa pesa ndogo.
Alifika akiwa na tumaini kubwa sana la kuitatua shida yake tena huenda ni zaidi ya hapo anapofikiri.
Aliamini huruma ya yule mama hasahasa baada ya kuujua ukweli itakuwa juu yake na atamsaidia maradufu.
Imetamkwa kuwa ‘baada ya dhiki ni faraja’ lakini kwa Mwanaidi dhiki moja inapanda juu ya dhiki mwingine na kuzua dhiki maradufu.
Mama Emma na familia yake hawakuwepo, nyumba ilikuwa kama haijawahi kukaliwa na watu.
Geti lilikuwa limefungwa.


Mwanaidi akajikongoja kichwa chini mikono nyuma. Akarejea katika kituo cha mabasi alichotoka.
Akapanda basi bila kujua atashuka kituo gani.
Maskini, hakuwa na kwao msichana huyu!!
“Kipati!! Wakushuka Kipati!!” kondakta akapiga kelele. Mwanaidi akakurupuka kutoka katika mawazo yake. Akasema ashushwe!!
Kondakta akatii akamshusha!!


Kwanza hakuwahi kutegemea kuwa ipo siku atarejea katika kituo alichowahi kufukuzwa kwa kufanyiwa njama. Lakini sasa anarejea kutokana na shida inayomkabili.
Anarejea katika kituo cha watoto yatima. Alipolitazama geti la kuingilia akaanza kumkumbuka rafiki yake mpenzi Farida!!
Akayakumbuka mabaya aliyotendewa na mkuu wa kituo. Alivyobakwa kwa ahadi kwamba ataishi kituoni milele.
Mawazo yake yakakatishwa na honi kubwa ya gari.
Alipotazama pembeni kina sura ilikuwa inatabasamu. Sura hii ilizibwa na miwani nyeusi ya jua.
Miwani ilipotolewa.
Mkuu wa kituo akaonekana.
Mwanaidi akamsalimia kwa heshima ya uoga. Moyoni alimchukia.
Akajieleza kwa ufupi kuwa alikuwa anamtafuta yeye.
Akaamuriwa kupanda ndani ya gari. Akapanda gari likatoweka.


Mbagala Kuu, Kijichi. Nje ya jiji la Dar es salaam huku ndipo gari lilisimama.
Wakashuka na kuingia katika nyumba ambayo ilikuwa mpya kabisa.
“Nyumba yangu hii…nimemaliza kuijenga mwezi uliopita naishi mwenyewe….vipi nzuri eeh!” alizungumza kwa ,majivuno Mwanaidi akamuunga mkono. Moyoni akilaani sana jinsi watu hawa wanavyotumia misaada inayotumwa kwa yatima kujinufaisha.


Hata kabla Mwanaidi ajajieleza shida yake tayari yule bwana mwenye tama akaanza kumgusa. Mara amtoe uchafu katika nywele mara amfute shavuni.
Ni kweli Mwanaidi alikuwa anavutia. Hakuwa amekaa rumande siku nyingi. Bado alikuwa Mwanaidi yuleyule. Lakini huyu bwana aliwahi sana kuonyesha tamaa kwa yatima huyu.
Mwanaidi mwenye shida alikuwa annakubali kila jambo lakini moja tu alilojiwekea moyoni ni kwamba. Udhalilishwaji wa Frida ulikuwa unatosha sana. Kwake itakuwa uzembe kudhalilishwa.
Bwana mpenda sifa akajitapa zaidi ili kumvuta Mwanaidi. Akaonyesha pesa zake nyingi. Mwana akajichekesha.
Akajifanya naye ni mwepesi kama wasichana wa mjini mbele ya pesa.
Chumba kikawapokea kwa furaha. Mashuka meupe yakachukia kuvurugwa na viumbe hawa.
Bwana matamaa, akawasha kiyoyozi. Kasha akasaula nguo zake moja baada ya nyingine.
Mwanaidi akamtazama huku mengi yakipita kichwani mwake.
Nani atajua huenda alikuwa anamchagulia aina ya kifo ambacho kitamfaa….au…au….hakika ilikuwa hivyo.
Papara za dakika mbili tu zilitosha kuyafanya mashuka yashangae kulikoni huyu bwana amaebaki peke yake kitandani halafu hata hachezichezi. Mashuka yakakosa jawabu.
Alipoanza kuharibika tena mashuka yakajiuliza kulikoni?
Hapakuwa na jibu, lakini safari hii swali lao lilipata jibu.
Mkuu wa kituo cha watoto yatima anagundulika kuaga dunia baada ya kugandamizwa na mto wa kulalia na kukosa pumzi hadi umauti ulipomkuta.
Marehemu alikuwa mtu wa watu!, alikuwa mkarimu, mwenye upendo, aliyejitolea kwa ajili ya yatima na wasiojiweza. Mungu amlaze pema pepeoni.
Wasiojua maovu yake wakajibu Amin!.


*****


Viwiliwili viwili vya vilikuwa vinafuatilia tukio moja katika nyakati na umbali tofauti.
Kiwiliwili cha kiume kilikuwa kinanyata huku kikishangaa ili kupata uhakika kama kinachoshuhudia ni sahihi ama la.
Kile cha kike kilikuwa kimepata uhakika kabisa na jambo lile.
Kikatimua mbio na kumsimamisha mwanamke wa makamo aliyekuwa katika mizunguko yake isiyokuwa na uelekeo rasmi.
“Kanga yangu hii umeitoa wapi.” Aliuliza kwa shari huku akiwa na furushi lake la chupa tupu za plastiki.
Mwanamke badala ya kujibu alitoa tabasamu. Kasha kicheko.
“Huyu vipi? Hivi viatu vyangu ujue.” sauti ya kiume iliuliza katika kuhamaki na kushangaa.
“Kanga yangu hii…namwam…..” alishindwa kuendelea kuzungumza akamtazama mwanaume aliyekondeana. Mabega juu kama mgonjwa wa Ukimwi.
Mwanaume akadondosha zigo lake la machuma.
“Isha!!” aliita.
Msichana akazidi kuduwaa, alikuwa hajapata uhakika kama yule ndiye ama siye.
Alipomuita jina akaamini alikuwa ni George.
George mkombozi wa yatima na chokoraa.
George ambaye sasa anaitwa Bonge!!


Mwanamke waliyemshutumu kuwa ana vitu vyao alikuwa anawatazama kama anayeyafuatilia maongezi yao na kuyapenda.
Mara akawasogelea. Isha akajisogeza kwa George, mwanamke akazidi kuwasogelea huku akicheka.
Mara akawakamata nguo zao.
Wakachomoka. Akaokota mawe!!
Riadha mpya ikaanza tena.
Ni katika namna yao ya kukimbia kila mmoja akauvuta ule usiku. Usiku wa ubakaji.
Ubakaji ulioingiliwa na kukoroma.
Wakakimbia. Sasa ni mchana wanakimbia tena.
Wanamkimbia mwanamke wanayeweza kumuona sasa.


Kila mmoja anajiuliza iwapo ni kweli juu ya kuwa kwao pamoja usiku ule.
Hakuna mwenye jibu. Mbio zikaendelea kumkimbia mwanamke mwenye mawe aliyedhaniwa kuwa ni mwendawazimu.


****ISHA na BONGE….ana kwa ana…kumbuka BONGE alitaka kumbaka ISHA…..je watatazamana kweli???


***MWANAIDI amemuondoa duniani mkuu wa kituo……bila shaka alichukua pesa…….je nini kitaendelea katika riwaya hii…..


ITAENDELEA


VAN HEIST muuza ubuyu amina mabata shabani hassani culbby sam II ram BPM mbalu saljar MAVUNO
 
nakuaminia kamanda wa hadithi. tupe mautamu. huyo kichaa atakuwa ni mamayake BONGE
 
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya


SEHEMU YA KUMI NA NANE




Mwanamke waliyemshutumu kuwa ana vitu vyao alikuwa anawatazama kama anayeyafuatilia maongezi yao na kuyapenda.
Mara akawasogelea. Isha akajisogeza kwa George, mwanamke akazidi kuwasogelea huku akicheka.
Mara akawakamata nguo zao.
Wakachomoka. Akaokota mawe!!
Riadha mpya ikaanza tena.
Ni katika namna yao ya kukimbia kila mmoja akauvuta ule usiku. Usiku wa ubakaji.
Ubakaji ulioingiliwa na kukoroma.
Wakakimbia. Sasa ni mchana wanakimbia tena.
Wanamkimbia mwanamke wanayeweza kumuona sasa.


Kila mmoja anajiuliza iwapo ni kweli juu ya kuwa kwao pamoja usiku ule.
Hakuna mwenye jibu. Mbio zikaendelea kumkimbia mwanamke mwenye mawe aliyedhaniwa kuwa ni mwendawazimu.




Yule mwanamke aliyeonekana kama hana akili timamu baada ya kuachwa mbali na akina Isha, alianza kuwacheka pasi na kikomo. Alicheka sana mwisho akaanza kujigalagaza chini.
George akaelekea kule alipokuwa Isha. Wakakumbatiana viumbe hawa wasiokuwa na afya. Kila mmoja akalihisi joto la mwenzake, wakajikuta wanatokwa na machozi. George akawa wa kwanza kumbembeleza Isha.
Baada ya mazungumzo marefu huku kila mmoja akiogopa kuyaanzisha maongezi yanayohusu jaribio la kubakwa Isha, walitembea hadi ambapo mwanadada Frida alikuwa katika harakati zake za utafutaji. Ni katika mgahawa mmoja wa kimasikini sana. Alikuwa anaosha masufuria kwa ujira wa chakula cha mchana na usiku.
Kwanza Frida hakumtambua George upesi. Lakini baada ya kukaribia sana alimtambua. Vyombo alivyokuwa anaosha vikakosa umuhimu. Akatimua mbio akamfikia akamrukia, George asiyekuwa na afya akakosa muhimili. Akayumba lakini hakuanguka. Matusi aliyokuwa anayatoa mama muuza genge aliyempa ajira Frida hayakuathiri masikio ya watoto hawa watatu.
Kwa pamoja wakakumbatiana, kama machozi yao yalivyolowanisha kile chumba ambacho George alikuwa amewapangia wasichana hawa ndivyo sasa yalidondoka katika ardhi kavu inayowazomea wenye shida.
Tofauti ya kilio cha kwanza ambapo walikuwa wamenawiri na kunukia marashi, hivi sasa walikuwa wamekonda na walikuwa wakinuka jasho.
Tofauti hii haikupunguza furaha yao.
Siku ikamalizika kwa furaha ya maajabu. Isha na George walipita tena jioni wakati Frida amemaliza kazi. Walitaka kuondoka naye lakini kauli hiyo ikamfanya apoteze furaha, kuna jambo lilikuwa linamchanganya kichwani.
Alikuwa amekula vya watu. Kuna mwanaume alikuwa amemnunulia pedi na kumpatia kiasi Fulani cha pesa. Sasa alikuwa anahitaji malipo.
Frida alishindwa aanze vipi kumwelezea George. Akamvuta Isha pembeni akamueleza, Isha aliumia lakini hakuwa na ujanja wowote. Akamkubalia.
George akapigwa change la macho akaridhika kuwa, Frida anatakiwa kulala pale katika lile genge hadi maharage ambayo bado hayajawekwa jikoni yaive.
Isha akaondoka na George kuelekea mahali watakapoweka migongo yao.
Safari yao ya usiku ikaishia katika uchochoro. Wakakaa kidogo, hawakuliogopa giza. Giza lilikuwa halina mamlaka ya kuogopesha nafsi zao. Kwani walikuwa wanaishi katika giza.
George akayaanzisha maongezi. Japo alikuwa mzito kusema, lakini alilazimika. Akauzungumzia usiku ule wa jaribio la kubaka.
Alikuwa anongea kwa sauti ya chini sana lakini iliyosikika vyema katika masikio ya Isha.
Kiupepo kutoka baharini kiliwapuliza wakati maongezi yanaendelea. Isha akalalamika baridi.
George akavua shati lake akampatia, japo hata yeye baridi ilikuwa inamsumbua.
Maongezi yakaendelea. Mwisho jibu likapatikana kuwa hakika ni Isha na George walikuwa pamoja usiku ule. Isha hakumlaumu George, alimuelewa na kumsisitiza kuwa lile ni jambo la kawaida tu mtaani.
Katika kushukuru, George akamkumbatia Isha.
Miili yao ikabadilishana joto. Zile hisia zilizomkabili George usiku ule na kujikuta anahitaji msichana sasa ziliamka tena, huku hizi za sasa zikiwa kali zaidi.
Akamkumbatia kwa muda mrefu. Isha naye akahama kimawazo akalihisi joto la kiume likitambaa mwilini. Nguo zilizochanika zikaruhusu miili yao kugusana.
Hili likawa kosa kubwa sana. Akili za kujitambua zikapaa. Wakajikuta wanafikiria kuhalalisha lililopo mbele yao.
Giza likawafichia siri. Wakajuana palepale.


******
Wakati Isha na George wakizidiwa na kujikuta wakifanya wasilotarajia. Frida alikuwa amepamabana sasa alikuwa amezidiwa. Bwana aliyemchukua alikuwa anamlazimisha kufanya mapenzi pasipo kutumia kinga.
Ni kweli alikuwa amemtunza kipindi akiwa katika magonjwa ya kike ya kila mwezi. Lakini malipo yake yalikuwa makubwa sana.
Frida hakupata hisia zozote kwa yule bwana. Lakini alilazimishwa.
Mwanaume ni mwanaume tu.
Asubuhi wakati anatoka pale mwanaume alikuwa ameridhika.


Walipokutana na Isha, hakumueleza kilichotokea, naye Isha hakusema alichofanya na George usiku kichakani.
George kwa mara ya kwanza katika maisha yake akagundua amefanya tendo kutokana na msukumo wa kimwili. Akajilaumu sana kimyakimya.


Hapana siri chini ya jua. Kila mmoja akaendelea na maisha haya.
George akachakarika akapanga chumba kisichokuwa na umeme. Kilichowagharimu shilingi elfu kumi kila mwezi. Akawachukua Frida na Isha.


Ni huku ambapo mzozo mkubwa ulitokea. Mzozo ambao ulimuhitaji mwanaume kufanya kazi mara mia ya awali ili kuubeba mzigo huu.
Isha alikuwa mjamzito.
Hapa George akarukwa na akili kuwa Frida atamfikiriaje.
Wakati George akimuwazia Frida atamfikiriaje. Frida naye alikuwa hoi kimawazo akifikiria ni kwa jinsi gani atamueleza George kuwa yu mjamzito. Alimuonea huruma sana kwa majukumu aliyonayo kama kaka mkubwa wa familia hiyo duni.
Frida aliamini kabisa kuwa yule bwana aliyemnunulia pedi ndiye muhusika wa hiyo mimba lakini alitambua kuwa yupo katika ndoa na kamwe asingeweza kuikubali mimba ile.
Sasa kikawa kizaazaa. Mimba mbili katika nyumba moja. Tena ziliingia katika usiku mmoja.
Mimba za chokoraa.
Kizungumkuti!!.


*****


Aliwakumbuka sana chokoraa wenzake, hasahasa alioishi nao kwa muda mrefu na kushirikiana katika harakati za hapa na pale. Ugonjwa pekee ndio ulimuweka kitandani na kumfanya ashindwe kuwatafuta.
Kisonono kilichokomaa!!
Alikuwa anajitibu huku akiwa amelala katika godoro lake alilonunua ndani ya chumba alichokuwa amepanga.
Sindano zilikuwa zinampelekesha sana na alishauriwa kuwa mvumilivu hadi hapo atakapopona vizuri.
Pesa ilikuwepo ya kutosha. Hakuwa na papara. Alitulia kama alivyoagizwa. Tiba ikaendelea. Vidonge, sindano pamoja na kula vizuri.
Hatimaye akarejea vyema katika hali yake ya kawaida. Mwezi mmoja na siku kadhaa za kulala kitandani na kula. Akawa amenenepa.
Hakujali kuwa zile pesa amezipata kwa kuondoa uhai wa mtu. Na kwanini ajali iwapo yeye hayupo hata mmoja wa kumjali?


Alipokumbuka kuhusu kutokuwepo mtu wa kumjali akakumbuka kuwa ana mama katika dunia hii aliyewahi kuishi naye kwa siku kadhaa. Akamkumbuka mama George. Yule alikuwa ana hadhi zote za kuwa mama wa chokoraa.
Kumbukumbu za kumuona mara ya mwisho ilikuwa ni katika chumba kimojawapo katika nyumba ya kulala wageni akiwa amezimia…
Ama alikuwa amekufa? Alijiuliza huku akikaa kitako. Macho kayakodoa bila kujua anachokiangalia kwa wakati ule.
Hofu ikatanda. Akajishangaa na kwa mara ya kwanza akauhisi uchungu unaopatikana kwa kio cha mtu unayempenda. Hakuwahi kuumia kwa kukisikia kifo cha yule bwana mnene katika nyumba ya kulala wageni, wala mama mweupe mmiliki wa danguro hakuishtua nafsi yake huku bwana matamaa kiongozi wa kituo cha watoto yatima naye hakumuhuzunisha.
Kwanini mama George? Alijiuliza.
Upendo wa dhati!!
Alipata jawabu la kinachomsumbua hadi kuumizwa na msiba huu. Aliamini kuwa alikuwa amempenda yule mama kwa dhati. Na alikuwa amemfanya kuwa mama yake wa kumzaa kwa kipindi kifupi.
Uchungu ukapitiliza. Macho yakapoteza uwezo wa kuona. Yakazibwa na machozi. Mwanaidi akaomboleza.
Aliomboleza kwa muda lakini hakaona kuwa bado si suluhisho.
George hawezi kumuelewa kuwa kweli mama yake alikuwa anaishi kwa kipindi chote cha kukua kwake.
Au George tayari anajua? Kama hajui itakuwaje? Maswali yakawa mengi sana. Akafikiria kuhusu kupata ushahidi wowote utakaothibitisha kuwa yule mama anayedhaniwa kuwa mfu aliwahi kuishi.
Hapa Mwanaidi akaamini kuwa kama alikufa bila shaka alizikwa na jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Akawaza kukutana na yule askari aliyemgeuza mke kwa siku mbili tatu rumande.
Aliamini kuwa ni huyu anaweza kumsaidia kujua walau alizikwa wapi, halafu baada ya hapo atajua ni adhabu gani ya kumpa kwa kiushiriki katika kumuambukiza kisonono.
Kulingana na maelezo ya daktari. Askari huyu hakuwa akihusika katika kumuambukiza kisonono kilichokomaa. Lakini ‘mkamatwa na ngozi ndiye aliyekula nyama', Mwanaidi akamuuzia kesi askari yule mwenye cheo cha chini.




Siku iliyofuiata Mwanaidi akiwa katika mavazi mapya yaliyovutia. Macho yake yakiwa yamezibwa na miwani nyekundu ya kisasa. Viatu vya kiuanamitindo vikistahi visigino vyake alikuwa anakatiza mitaa miwili mitatu, alijisikia mpya kabisa kimwili lakini kiroho akiwa na madeni mengi.
Alijitazama vyema. Akagundua alikuwa amependeza sana. Akawatazama wavuja jasho wanavyozigombania daladala. Akatabasamu na kugundua kuwa kwa siku hiyo alikuwa katika hadhi tofauti.
Akaabiri Bajaji. Dereva akatii amri.
Safari aliyoipanga ikaanzia hapo.
Kama kawaida katika kiuno chake kuna silaha ilihifadhiwa kwa kujihami iwapo yeyote atajaribu kumsumbua.




***MWANAIDI amepona na amerejea katika harakati…..je atakuwa na moto uleule.


***GEORGE a.k.a Bonge akiwa hajui kesho yake mwenyewe anakumbwa na jinamizi la kumpachika mimba ISHA……pagumu hapo!! Na FRIDA akijua itakuwaje???
***FRIDA naye ameibeba mimba ya pili katika maisha yake…ule mzimu wa mama yake aliyefia jela bado unamuandama….je atafanya nini na hataki GEORGE ajue???

VAN HEIST muuza ubuyu amina mabata shabani hassani culbby sam II ram BPM mbalu saljar MAVUNO
 
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya


SEHEMU YA KUMI NA TISA




Siku iliyofuiata Mwanaidi akiwa katika mavazi mapya yaliyovutia. Macho yake yakiwa yamezibwa na miwani nyekundu ya kisasa. Viatu vya kiuanamitindo vikistahi visigino vyake alikuwa anakatiza mitaa miwili mitatu, alijisikia mpya kabisa kimwili lakini kiroho akiwa na madeni mengi.
Alijitazama vyema. Akagundua alikuwa amependeza sana. Akawatazama wavuja jasho wanavyozigombania daladala. Akatabasamu na kugundua kuwa kwa siku hiyo alikuwa katika hadhi tofauti.
Akaabiri Bajaji. Dereva akatii amri.
Safari aliyoipanga ikaanzia hapo.
Kama kawaida katika kiuno chake kuna silaha ilihifadhiwa kwa kujihami iwapo yeyote atajaribu kumsumbua.




***MWANAIDI amepona na amerejea katika harakati…..je atakuwa na moto uleule.


***GEORGE a.k.a Bonge akiwa hajui kesho yake mwenyewe anakumbwa na jinamizi la kumpachika mimba ISHA……pagumu hapo!! Na FRIDA akijua itakuwaje???
***FRIDA naye ameibeba mimba ya pili katika maisha yake…ule mzimu wa mama yake aliyefia jela bado unamuandama….je atafanya nini na hataki GEORGE ajue???




**SHARE TENA NA TENA IWEZE KUSAFIRI MBALI ZAIDI….
**LIKE IWAPO TUPO PAMOJA




Ilikuwa kama bahati iliyokuja katika wakati muafaka, Mwanaidi hata kabla hajakifikia kituo cha polisi alimuona yule askari barabarani. Alikuwa amenyong'onyea na sura yake ilitangaza matatizo tupu.
"Dogo upo….." askari alimsalimia Mwanaidi.
"Shkamoo…" alijibu.
Akamkaribia wakapeana mawili matatu bila kuzungumzia uhusiano wao wa kulazimishana kule rumande. Mwanaidi akajielezea shida yake. Bahati nzuri yule askari alikuwa mpenda kujua mengi ‘kiherehere' hizo taarifa alikuwanazo.
"Mbona alitolewa mapema tu yule." Alianza kujielezea, akaelezea kila kitu alichokuwa anakifahamu kuhusu mama mlemavu.
"Sasa alitoka vipi mwenyewe wakati hawezi kutembea au mlimtupa jamani." Alilalamika mwanaidi.
"Hapana hakutupwa lakini aliwekwa mahali akaachwa kama alivyo. Ndiyo serikali yetu ilivyo." Alimaliza.
Kisha akamuaga Mwanaidi na kutaka kuondoka.
"Mbona umenywea hivyo lakini."
"Matatizo mdogo wangu…"
"Nini tena."
"Wifi yako anaumwa na mtoto wake mchanga dah we acha tu." Alijibu yule askari.
Mwanaidi akamtazama huku akimuwazia mawili matatu. Lakini kubwa lililotawala kichwa chake ni kuhusu mama George ambaye alielekezwa ni wapi alipotelekezwa.
Akatoweka eneo lile.


Majira ya saa moja usiku alikuwa maeneo ya Kariakoo gerezani ambapo alielekezwa kuwa upo uwezekano wa kumkuta anayemtafuta.
Alikuwa makini akitazama huku na huko, kabla ya kuvamiwa na kundi la machokoraa waliomuhoji ni kipi anatafuta eneo lile.
Chokoraa walidhani ile ni bahati yao usiku ule aidha wanaweza kumuibia alichonacho. Hawakujua kama ni mwenzao.
Mwanaidi alijitetea kuwa kuna mtu anamtafuta. Hakika alikuwa hafananii na kuwa chokoraa alikuwa amependeza sana siku hiyo.
Sauti nyingi zikauizidi sauti yake. Wakadhani ni polisi.
"Njagu, Njagu!!" kelele zilianza wakimaanisha polisi.
Kama wasivyowapenda mgambo wa jiji ni hivyohivyo kwa askari polisi wasivyopendwa na chokoraa. Kwao ni kama sumu.
Wakati mgambo huwasumbua chokoraa mchana, askari polisi katika doria zao huwasumbua viumbe hawa usiku.
Sasa Mwanaidi anaonekana kufanana nao. Nywele zake fupi na mavazi yake yanamuingiza matatani. Sauti hizi zikawavuta wengine.
Wakajisogeza eneo la tukio ili kujua nini kinatokea.
George aliwazuia Isha na Frida kusogea eneo hilo la kelele. Yeye akajongea kushuhudia kuna nini.
Heleni ikavutwa na kulichana sikio la Mwanaidi. Akapiga yowe la uchungu. Yowe kubwa sana. Yowe lililotetemesha ngoma za sikio la George. Akakaza mwendo na kufika eneo lile.
Akapenyeza katikati akafika mbele. Kila aliyemuona George alijua kuna suluhu. Japo kwa muda alikuwa amehamia nyumba ya kupanga lakini bado mara kwa mara alikuwa akirejea kambini. Na siku hii pia alikuwa bado kambini hapo.
Kila mtu akasubiri uamuzi wa George.
"We ni nani?" akauliza kwa jazba, mkononi akiwa amekamata fimbo.
"Naitwa Mwanaidi." Alijibu yule binti huku akiwa amekaa chini akiugulia maumivu ya sikio lililokuwa linavuja damu.
Jina hilo likamshtua George akainama na kumtazama.
Hilo likawa kosa kubwa sana kwa chokoraa huyu mwenye uzoefu wa kutosha mtaani. Ule upenyo uliotumika kumwachia njia George apite akautumia kama nafasi ya wazi ya kufunga goli.
George alikuwa amemshika mkono kumdhibiti asiweze kutoroka. Mwanaidi akajichezesha kidogo na kujidai anajikuna akachomoka na alichokihitaji. Kisu kidogo kikali cha kutahiria kilichohifadhiwa katika pindo la nguo yake.
Ama kwa hakika ilikuwa ni lazima kwa namna yoyote binti huyu ajaribu kujihami. Chokoraa wanaweza kukuua bila kujuta. Wana hasira na maisha yao magumu, hawakuyapata malezi bora ya wazazi wala walezi na hata watu wazima wanaoitwa walimwengu hawakuweza kuwafunza lolote la kimaadili. Huenda angeendelea kulaza damu, angebakwa na kuibiwa kila kitu. Alipokumbuka kuwa ana jukunu la kumtafuta mama George, akili ikamchemka.
Akamuweka katika rada huyu mwanaume mwembamba aliyemshika mkono.
George ambaye hakujua nini kinaweza kutokea na kamwe asingeweza kutegemea. Alishtushwa na ubaridi fulani wenye ladha tamu isiyosimulika, lakini ladha ambayo haikudumu kwa muda mrefu ikageuka kuwa maumivu makali. Yowe kubwa likamtoka Bonge. Waliomzunguka wakasogea mbali naye bila kujua nini kimetokea.
Hili likawa kosa la mwisho ambalo Mwanaidi alilisubiria. Chokoraa wakiwa katika taharuki ya ajabu kabisa. Chokoraa mwingine alitabasamu, na kisha kikafuata kitendo.
Waliishia kubaki na viatu vyake pekee.
Mwanaidi alitoka mbio za ajabu. Hakuna aliyeweza kumfikia.


Laiti kama angejua kuwa yule muulizaji ni George ambaye asingeweza kumdhuru hata kama angekuwa upande wa makosa, basi angeweza kubaki. Lakini hakuyajua haya yote. Sasa alikuwa amemfyeka vyema mkono na kisu chake kikali. Amakweli usilolijua…..


*****


IKAWA kazi pevu ya Isha na Frida kumuuguza George ambaye alikuwa ana jeraha mkononi. Walitumia tiba za kuungaunga hapa na pale.
Licha ya kuwa na jeraha George aliendelea kuhangaika huku na huko. Na asubuhi iliyofuata majira ya saa mbili asubuhi alikuwa katika geti kubwa jeusi akiwa na rafiki yake wa mtaani. Alikuwa amempeleka mahali alipokuwa anafanya kazi.
Ndoo ikatolewa, ilikuwa na vinywaji mbalimbali baridi vilivyotolewa katika jokofu.
"Utamuelekeza mwenzako inavyokuwa." Mwanaume wa kiarabu alimuambia kijana aliyeambatana na George aliyejifunga kitambaa katika mkono wake.
Baada ya kuvipanga vinywaji katika mkebe mdogo. Waliaga na kuingia mjini. Huku sasa ikawa shughuli ya kukimbilia magari ya abiria na kuwasihi wanunue vinywaji aidha maji ama juisi. Ilikuwa shughuli pevu hasahasa kwa George ambaye alikuwa anaianza.
Alikuwa ana aibu kukariri sauti na maneno ‘Maji, sayona, Azam Cola, azam Mango'.
"George wewe ni chokoraa, hauna thamani yoyote na hauna ndugu anayekutazama hapa duniani…usimuonee mtu yeyote aibu, pigana pigana kaka….aibu yako itakufanya ulale njaa kaka." Yule rafiki yake alimwambia huku jasho likiwa linamtiririka usoni kutokana na jua kali sana kuwapiga. George alikuwa mnyonge sana huku kapu lake likiwa bado lina vinywaji vingi huku mwenzake akiwa anakaribia kumaliza.
Jasho lililokuwa linamtiririka Roja lilikuwa funzo tosha kwa George. Akaukumbuka ule usemi katika maandiko ukisema mwanaume atakula kwa jasho.
Ni kweli alikuwa amewahi kuokota vyuma, kuokota makopo tupu ya plastiki lakini sasa alikuwa katika kulitoa jasho jingine.
George hakusema neno. Alitikisa kichwa na kuyakariri kichwani maneno ya Roja. "George wewe ni chokoraa, hauna thamani yoyote na hauna ndugu anayekutazama hapa duniani…usimuonee mtu yeyote aibu, pigana pigana kaka….aibu yako itakufanya ulale njaa kaka."
Yakamkaa vyema kichwani. Akayafanyia kazi.
Baada ya siku mbili alikuwa mzoefu zaidi yaw engine. Ni kama alikuwa katika kazi hiyo kwa miaka miwili nyuma.
George alijitoa ufahamu. Akasahau kabisa juu ya elimu aliyoipata ya chuo kikuu. Hata kama angeiwazia angevipata wapi vyeti vyake tena?? Aliamini kuwa aliyekuwa na mamlaka yote ni George na hakutaka kuonana naye tena.
Mimi ni chokoraa natakiwa kuishi na chokoraa. Lilikuwa neno lake mara kwa mara.
Kilichosikitisha ni malipo. Unalipwa kadri ya mapato utakayoyawasilisha jioni kwa bosi. Mapato yakiwa kidogo na malipo yanakuwa kiduchu.
Sala na maombi yote kwao waliendelea kulitaka jua zaidi kuliko mvua. Maana siku za mvua……wanajua wao.


******


SIRI haiwezi kudumu milele.
Mimba nayo haina dogo. Isipokuvimbisha tumbo upesi basi lazima tu itakuletea balaa jingine.
Kwa Frida ilikuwa afadhali yake tumbo lilikuwa kama hana siri sirini lakini kwa Isha mambo yalikuwa vingine.
Tumbo lake liliwahi sana.
Isha alipogundua hilo alizungumza na George kuhusu Frida. Itakuwaje akigundua kuwa ana mimba yake.
Wakakubaliana asimtaje yeye bali asingizie lolote lile. Uongo huu ukabarikiwa.
Siku iliyofuata, Isha akamuweka chokoraa mwenzake kitako.
Akamueleza juu ya mimba aliyonayo. Frida akataharuki tofauti na mategemeo ya Isha.
"Lakini ni ya nanii huyu….yaani sijui hata nji nani kwakweli.." alijikanyaga Isha. Frida akabaki kuwa kimya. Mshangao ukiendelea kumtafuna.
Ilimchukua dakika mbili Frida kusema neno.
"Mwenzangu..sasa itakuwaje hapo. Maana nashindwa hata nisemeje. Kwani ina miezi mingapi hadi sasa."
"Itakuwa miwili au..ni miwili."
Frida akashtuka tena, safari hii sasa akaamini kuwa huenda Isha alikuwa akiongea kwa niaba yake, maana kila kitu kilifanana.
"We Isha jamani….yaani sijui hata nikuambiaje labda."
"Yaani we acha tu…mi mwenyewe sielewi hapa patakalikaje."
"Isha nina mimba pia." Hatimaye Frida alisema kwa sauti ya chini sana.
Ikawa zamu ya Isha kushtuka sasa.
Lakini si kama ilivyokuwa kwa Frida. Waliendelea kuzungumza mengi huku kila mmoja akidai anahofia George akijua itakuwaje.
Isha aliunga mkono hoja kinafiki. Maana George alikuwa anajua tayari kuhusu mimba yake na alikuwa ndiye muhusika mkuu.


*****
Mwanaidi alikuwa ndani ya chumba chake, akijisafisha sikio lake ambalo lilikuwa limejeruhiwa siku kadhaa nyuma. Wakati anakitazama kioo kilichokuwa kikimsaidia kuliona sikio lake, alirejewa na kumbukumbu juu ya mwanamke ambaye alimsaidia kuongeza kasi yake ya kukimbia baada ya kuwa amechoka.
Anakumbuka kuwa aliwahi kumuona mahali.
Feri? Posta? Kigogo? Koko Beach? Hayo yalikuwa mashwali makuu aliyokuwa anajiuliza. Hakupata jawabu. Japo ulikuwa ni usiku bado aliweza kumuona kiasi kidogo.
Akakuna kichwa chake na kuachana na jinamizi hilo linalomkabiri.
Maajabu, bado aliendelea kuhangaishwa na sura hiyo.
Akajilaza katika godoro lake sakafuni akaanza tena kufikiria upya.
Sasa akaijenga picha kisha akatabasamu.
"Kumbe namuwaza mama yake George?" alisema kisha akacheka. Ile sura aliyodhani ameiona gizani ilikuwa ni ya mama George.
Akaendelea na shughuli zake huku akipuuzia mawazo yale.
Laiti kama angekuwa mlemavu hapo sawa. Yule mwanamke anakimbia balaa, sijui alikuwa anataka nini kwangu au kichaa yule? Alijiuliza Mwanaidi.
Lakini amenisaidia kukimbia kwakweli. Alikiri.


Usiku huu ambao Mwanaidi alikuwa akiwaza haya.
Mjeruhiwa wa kisu kile alikuwa akilitazama jeraha lake lililokosa huduma bora. Wakati analitazama akawa anawaza juu ya maongezi yake na Isha juu ya kutoa mimba.
Alijiuliza yule msichana atayachukulia vipi maamuzi haya magumu. Je atakubaliana na hali hiyo ama ataweka ngumu? Hayo yalikuwa maswali.
George alikiri moyoni kuwa alikuwa akimuhitaji sana mtoto lakini atamtunza vipi? Hilo lilikuwa tatizo.
Japo ilimuuma sana, akaamua kuheshimu ule usemi wa ‘Heri nusu shari kuliko shari kamili'. Akaamua kuchukua maamuzi na usiku huu aliamua kwa namna yoyote ile kumshawishi Isha akubali wafanye mpango wa kuitoa mimba.
Sasa alikuwa mlangoni, moyo ukawa mzito sana kwa maamuzi yale lakini hakuwa na namna ya kujizuia.




**Bonge/George amefikia maamuzi ya kumshawishi ISHA atoe mimba….ugumu wa maisha ndio chanzo….Je Isha atakubali?? Na vipi akijua kuhusu mimba ya FRIDA pia???


**HARAKATI za Mwanaidi nazo zipo pagumu…….


***NINI HATMA YA UMOJA HUU KUUNGANA TENA…NINI HATMA YA MAISHA YA CHOKORAA


VAN HEIST muuza ubuyu amina mabata shabani hassani culbby sam II ram BPM mbalu saljar MAVUNO Khantwe
 
Last edited by a moderator:
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya
Mawasiliano: 0655 727325


SEHEMU YA ISHIRINI




Akakuna kichwa chake na kuachana na jinamizi hilo linalomkabiri.
Maajabu, bado aliendelea kuhangaishwa na sura hiyo.
Akajilaza katika godoro lake sakafuni akaanza tena kufikiria upya.
Sasa akaijenga picha kisha akatabasamu.
"Kumbe namuwaza mama yake George?" alisema kisha akacheka. Ile sura aliyodhani ameiona gizani ilikuwa ni ya mama George.
Akaendelea na shughuli zake huku akipuuzia mawazo yale.
Laiti kama angekuwa mlemavu hapo sawa. Yule mwanamke anakimbia balaa, sijui alikuwa anataka nini kwangu au kichaa yule? Alijiuliza Mwanaidi.
Lakini amenisaidia kukimbia kwakweli. Alikiri.


Usiku huu ambao Mwanaidi alikuwa akiwaza haya.
Mjeruhiwa wa kisu kile alikuwa akilitazama jeraha lake lililokosa huduma bora. Wakati analitazama akawa anawaza juu ya maongezi yake na Isha juu ya kutoa mimba.
Alijiuliza yule msichana atayachukulia vipi maamuzi haya magumu. Je atakubaliana na hali hiyo ama ataweka ngumu? Hayo yalikuwa maswali.
George alikiri moyoni kuwa alikuwa akimuhitaji sana mtoto lakini atamtunza vipi? Hilo lilikuwa tatizo.
Japo ilimuuma sana, akaamua kuheshimu ule usemi wa ‘Heri nusu shari kuliko shari kamili'. Akaamua kuchukua maamuzi na usiku huu aliamua kwa namna yoyote ile kumshawishi Isha akubali wafanye mpango wa kuitoa mimba.
Sasa alikuwa mlangoni, moyo ukawa mzito sana kwa maamuzi yale lakini hakuwa na namna ya kujizuia.


George aliingia hatimaye, akapokelewa na ukimya mkubwa. Frida na Isha walikuwa hoi kwa usingizi.
Alitamani amuamshe Isha ili waweze kuongea kuhusu jambo alilokuwa amefikiria. Lakini akahofia kumsumbua na pia akahisi kuwa hatakuwa na umakini mkubwa wa kuelewa kutokana na kuelemewa na usingizi.
George akalala, kutokana na mawazo mengi yaliyohitaji maamuzi yake, alijikuta akilala fofofo.
Alipokuja kushtuka alikutana na miale ya jua ikimaanisha ni muda umepita tangu mapambazuko yaingie.
Akayapikicha macho yake aweze kuona mbele vyema. Akakutana na kiwiliwili kimoja kikiwa bado kimelala. Alikuwa ni Isha.
Akamuamsha ili aweze kuzungumza naye kabla Frida hajarejea kutoka popote alipoelekea.
Isha akaamka huku akisumbuliwa na mang'amung'amu ya usingizi.
George akalazimisha tabasamu. Isha akalipokea.
"Nahitaji tuzungumze Isha." George alimwambia kwa sauti ya upole. Isha akajiweka sawa katika mkeka aweze kumsikiliza vizuri.
"Frida yupo wapi?" aliuliza Isha, baada ya kujiweka vyema.
"Nikuulize wewe hapo uliyelala naye."
Isha hakuwa na cha kujibu na mazungumzo hayo yakasahaulika.
George akaingiza mada zake. Akajizungusha mbali sana akiweka busara anazojua yeye ilimradi kuhalalisha visivyokuwa halali.
Akafikia lengo lake hatimaye. Akamueleza Isha juu ya kuitoa ile mimba. Hapo Isha akasimama wima mtoto huyu wa kizaramo, akashika kiuno. Akaanza kuwaka, George akajaribu kumpooza hakufanikiwa kitu.
Isha akazungumza mengi sana huku akimlaumu George kuwa ni mgandamizaji tena muonevu mkubwa.
Katika kulalamika huko hasira ikapanda sana, ule ubaya wa kauli ya ‘hasira hasara' ukachukua nafasi. Hasara ikaingia kati. Isha akajikuta akimtaja Frida katika mazungumzo yake, akafichua siri ya Frida kuwa na mimba bila yeye mwenyewe kujua kama amefichua siri.
George akashtushwa na kauli hiyo.
"Frida ana mimba??" aliuliza, hakujibiwa badala yake wote wakajikuta wapo kimya.
George aliwahi kujifunza kidogo juu ya saikolojia ya mwanadamu alipokuwa katika masomo yake chuoni. Upesi alimsoma Isha akagundua kuwa alikuwa katika kujutia alichosema na sasa alikuwa anajaribu kukificha.
George akakazania swali lake. Isha hakuwa na jinsi akamueleza George ukweli kuwa Frida ni mjamzito.
Hapo sasa, kwa pamoja wakajiuliza.
"Yupo wapi?" hakuna aliyemjibu mwenzake.


******


Wakati wawili hawa wakilumbana na hatimaye kufikia kumwongelea Frida. Muongelewa alikuwa katika kuwania kupanda pantoni ambalo lilikuwa linapiga honi za mwisho za kuondoka kivukoni.
Bahati nzuri aliliwahi pantoni lile.
Hakuwa na uhakika sana ni wapi alikuwa anataka kwenda lakini alijikuta tu anaelekea katika pantoni.
Ndani ya pantoni lile Frida alikuwa akijiuliza mengi sana.
Alijihakikishia kuwa yupo sawa kabisa kuamua kuondoka katika makazi yale bila kuaga.
Aliamini kwa namna yoyote ile Isha atamshirikisha George juu ya mimba yake.
Frida aliamini fika George atajisikia vibaya sana akigundua jambo hilo na kama hiyo haitoshi atakuwa amebebeshwa mzigo mkubwa sana.
Mzigo wa kulea mimba mbili.
Uamuzi wa kuondoka bila kuaga akaubariki.
Lakini hakujua anaelekea wapi hilo lilikuwa tatizo.
Baadaye akakumbuka zile tenda za kuwafulia wanafunzi nguo. Hapo akili ikasogeleana na kukumbuka nia yake.
Alikuwa ameamua kujipatia kipato kama alivyokuwa anafanya awali.
Pantoni ndio kwanza lilikuwa limeanza kuondoka, mahali alipokuwa amekaa Frida palikuwa na familia ambayo kwa mtazamo wa haraka ilikuwa inaelekea aidha ufukweni ama katika sherehe fulani.
Frida alivutiwa na mtoto mdogo aliyekuwa amesimama huku akicheza kwa furaha nawenzake. Frida akajifananisha na mtoto huyo mwenye malezi ya wazazi wawili. Akamshika mkono akawa anauchezea huku akivuta picha nyuma, ikajijenga picha ya kuzaliwa gerezani, mama yake anakufa akiwa katika kifungo, anasoma akiwa anaishi kwa mkuu wa gereza.
Anafukuzwa pasipo na makosa, anageuzwa mtumwa wa ngono na mkuu wa kituo cha yatima, anabebeshwa mimba, anaitoa kwa uchungu mkub wa, mara mbili anawekwa rumande na kisha kuachiwa, anabakwa hovyo. Anadharaulika na sasa ana mimba tena.
Kilio cha yule mtoto mdogo kinamshtua, anajarib u kuyafunua macho yake yanashindwa kuona mbele. Sasa akagundua kumbe yule mtoto alikuwa analia baada ya yeye kuanza kulia.
Mara yule mtoto akanyakuliwa kutoka katika mikono yake na wazazi wake. Frida akauhisi upweke wa hali ya juu. Akajipa jibu moja kuwa vikwazo alivyokuwa anapitia ni njia ya kumuonyesha kuwa hakustahili kuishi katika ulimwengu huu. Basi tu alikuja kwa bahati mbaya. Walioletwa kwa maksudi mazuri walikuwa wanaishi maisha ya kupendeza.
Hasira, chuki na mfadhaiko. Vyote vikamuelemea Frida.
Pepo la kukata tamaa likamnyanyua juu juu. Yule pepo wa umauti akafanya msaada wa ajabu wa kumpatia Frida nguvu. Akajitoa pale alipo akajirusha majini kabla pantoni halijakimaliza kivuko.
Kila mtu mdomo wazi wakati anatapatapa kwenye maji ili kukamilisha ule usemi wa mfa maji haishi kutapatapa.
Nani ajirushe ndani ya maji haya kumuokoa yatima huyu?
Hakuna hata mmoja. Akina mama waliishia kupiga kelele, kelele zisizokuwa na manufaa.
Hata wanaume nao walitulia tuli bila kufanya jitihada zozote.


Frida akapanda juu kwa mara ya kwanza, akazama akaibuka tena kwa mara ya pili.
Hapo sasa likatokea tukio la maajabu mengine. Kiwiliwili kilichokuwa ndani ya nguo mpya zilizong'ara. Kilijichomoa katika kundi la watu kisha kikapaa hewani na kutua katika maji.
Filamu ya kushangaza.
Waliofika upande wa pili wa kivuko. Walingoja sana kumshuhudia huyo aliyekuwa amejirusha katika maji ni nani na huyo aliyejirusha kwa mara ya pili ni nani.
Hawakutokea.


******


Mwanaidi alikuwa anaufurahia mchezo aliokuwa anaufanya kwa rafiki yake wa mtaani. Alifurahi sana kumfuatilia bila kumpoteza, kila mara alitaka kumshtua lakini akaendelea kuvuta subira.
Moyoni alikuwa na furaha sana kwa ushuhuda huu, hakutegemea kuonana naye kwa wepesi hivyo.
Sasa alikuwa anapiga hatua nyuma yake bila mlengwa kuelewa nini kinaendelea.
Walianzia Kariakoo, kwa miguu hadi Posta, bado kamchezo kakendelea wakafika feri. Wakakata tiketi wakaingia katika ukumbi wa kungoja pantoni. Wakajituliza hapa, Mwanaidi bado alikuwa makini sana kumfuatilia rafiki yake huyu. Hakutaka kumpoteza.
Sasa aliamini kumfuatilia huku kulikuwa kumetosha na alijiahidi kuwa wakati wa kushuka katika pantoni atawahi kushuka chini ili aweze kumshangaza mwenzake.
Wakiwa ndani ya pantoni alimwangalia kwa kuibia ibia rafiki yake hadi pale alipoanza kulia kwa uchungu.
Mwanaidi alitambua kuwa huu ulikuwa uchungu wa maisha magumu ya kutengwa. Maisha ya uchokoraa.
"Leo ni mwisho wa kilio hiki ee Mungu tutazame wanao." Mwanaidi alifanya dua hiyo fupi.
Kishja akairefusha zaidi, na yeye machozi yalikuwa yanamtoka sasa, alikuwa akijisitiri na kitambaa cha mkononi.
Alipomaliza sala yake ya kuwaombea yatima. Akayafumbua macho yake kwa tabu. Kelele za akina mama zilishtua, akadhani pantoni linazama, mara akadhani kuna mtu amekufa.
Mara akaona macho yote yakitazama majini, na yeye akatazama lakini hakuona kitu.
Akiwa bado anashangashangaa mara alisukumwa kwa kishindo kikubwa akaanguka chini. Yule mtu aliyemsukuma kama mwendawazimu vile akajirusha majini.
Mwanaidi kuja kusimama tena hakupata nafasi ya kuangalia majini.
Akaangaza huku na huko. Hakumuona Frida.
Akajaribu kutelemsha ngazi za pantoni. Bado hakumuona Frida wala mtu anayefanana naye, wasiwasi ukatanda akajiuliza amekwenda wapi? Ule utani wake ukaanza kumtafuna. Akajuta kuchelewa kumkabili Frida.
Mwanaidi akawahi kuwa wa kwanxza kushuka katika pantoni kisha akakaa katika mlango wa kutokea akawa makini kutazama wanaotoka. Umakini wake mkubwa haukusaidia kitu hakumuona Frida.


"Kwani nini kimetokea?" hatimaye aliwauliza watu waliokuwa wanashangaa majini.
"Kuna dada amejirusha ndani maji. Sijui kama amepona."
"He, mdada yukoje?"
"Nenda majini ukamtafute labda." Alijibiwa jibu lililojaa sanifu.
Mwanaidi anachanganyikiwa. Hajui nini cha kufanya. Hisia kuwa kile kilio alichotoa Frida kilikuwa cha mwisho katika ulimwengu huu zilimshambulia na hakutaka kudumu katika hilo wazo.
Akili ikashindwa kufanya kazi ipasavyo.
Hakuwa na mwingine wa kumlilia aweze kumsaidia kimawazo.
Kama alivyobarikiwa kipaji cha kufikiri upesi, akafanya maamuzi. Akawafikia chokoraa wa feri ambao hutumia muda wao mwingi kuogelea katika bahari ya hindi.
Pesa ikaongea akawasihi warejee na yule binti.
Vijana wanne wakazama majini, kama samaki, wakaibukia mbali.
Pesa iliwasukuma.


***JE? MWANAIDI ATAFANIKIWA KUMUOKOA FRIDA.
NI NANI ALIYEJITOSA KATIKA MAJI KUMWOKOA FRIDA.
***ISHA na GEORGE. Je hiyo mimba itatolewa???

VAN HEIST muuza ubuyu amina mabata shabani hassani culbby sam II ram BPM mbalu saljar MAVUNO Khantwe
 
Aiseee..... Frida jamani!
Hope utapona
 
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya


SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA


Jitihada zilizofanywa na wale vijana waliokuwa wamekubaliana bei na Mwanaidi, hazikuzaa matunda, hapa sasa Mwanaidi akazidi kuhamanika, alijiona yu katika hatia ya waziwazi kwa kosa la kumchezea shere Frida hadi kumwingiza katika mauti hayo.
Mchelea mwana kulia hakika hulia mwenyewe. Sasa Mwanaidi alikuwa katika majuto makuu. Alikuwa ameichezea nafasi ya kuonana na Frida.
Alisubiri sana walau aweze kuuona mwili wa Frida, lakini hata harakati za kumuibua kutoka majini hazikufanyika. Alikuwa na jina gani hadi ashtue vichwa vya watu, waache kazi zao na kuja kumtafuta??
Hakuwa na lolote, hata roho yake pia haikuwa na lolote lile.
Majira ya saa moja usiku, Mwanaidi aliyashika maji ya bahari. Kwa imani yake ndogo akamuombea alazwe pema peponi.
Machozi yake yakachukuliwa na bahari ile ambayo aliamini ilikuwa imemmeza rafiki yake. Bahari isiyokuwa na huruma, inameza hadi machokoraa.


*******


Wakati Mwanaidi analia na bahari, Isha na George walikuwa wamegeuziana migongo, kila mmoja akiwaza lake. Walikuwa wamezunguka sana bila kupata walau tetesi za Frida kuonekana.
Isha alikuwa ameuvuta mdomo wake baada ya George kuwa amemlaumu sana kwa kuchelewa kumweleza juu ya Frida kuwa mjamzito. Licha ya Isha kujitetea kuwa hakuwa akijua lolote hadi Frida alipomweleza mwenyewe bado George aliendelea kulalamika, sasa Isha ambaye alikuwa amebeba mtoto wa George tumboni alifikia hatua ya kununa.
George ambaye alikuwa anamuwaza Frida hakuwa tayari kumwomba msamaha Isha. Mtafaruku!!
Usiku ukapita huku kila mmoja akijiona yupo sahihi.
Palipokucha, zile Baraka walizopewa wanawake wachache zikajionyesha kwa Isha. Akajishusha na kumchangamkia George.
Amani ikarejea!!
Sasa waliweza kuzungumza tena!.
Juma zima likakatika bila Frida kuonekana. Walijadiliana kwenda kutoa taarifa polisi lakini hata kabla ya kukubaliana wakatambua kuwa hawatapata msaada wowote huko. Waliamini kuwa hawakuwa wakithaminiwa na jamii. Hizo ndizo hisia halisi za Chokoraa, hata siku moja haamini kama ana usawa na wanadamu wengine. Wao huamini kuwa wapo katika dunia yao ya kipekee. Dunia iliyojaa mateso, dhiki na manyanyaso.
Hawakwenda kutoa taarifa!
Walisubiri muujiza.


****


UPARA wake kichwani haukutangaza umasikini, bali utajiri wa hali ya juu. Tumbo lake liliunda mfano wa kijimlima kidogo, kilichonakishiwa kwa jina la kitambi. Alikuwa akilikuna tumbo hilo kwa ujivuni wa hali ya juu.
Mlango ulipogongwa alikuwa anatazama taarifa ya habari ya asubuhi.
"Nani?" aliuliza. Badala ya kujibiwa, magazeti mbalimbali ya siku hiyo yalipitishwa chini ya mlango.
"Karume za asubuhi bwana!" alisalimia mzee huyu, alitambua tayari ni nani aliyeugonga mlango huo.
Mkewe alipopita pale sebuleni alimuagiza amchukulie yale magazeti.


Siasa ilikuwa imemkaa kichwani na kwa siku za usoni alikuwa amefikilia kugombea udiwani ama ubunge kama ikiwezekana.
Kama ilivyo kawaida magazeti ya udaku ambayo ni magazeti pendwa kwa mkewe na mwanaye wa kike akayaweka kando. Akapekua yale ya siasa. Akaanza kuyapitia moja baada ya jingine.
Huyu Kasuku ana nini leo! Alijiuliza mzee Mathias huku akifanya tabasamu hafifu, akajiweka sawa katika sofa akaiweka sawa miwani yake.
Kila mara alipoliona hilo jina alikuwa akimfikiria Kasuku wake ambaye kila asubuhi alikuwa akimuamsha kwa kumuita ‘bosi'.
Kasuku huyu wa gazetini yeye alikuwa akimuamsha akili yake kwa kumfungua mengi yanayotokea katika jamii na yeye hayatambui.
"MTANZAGIZA GIZANI, MWONYESHE NJIA EWE MWENYE MACHO" Kilisomeka hivyo kichwa cha habari. Mathiasi akacheka kwa sauti ya juu kidogo, kisha akajisemea "Kuna watu wabunifu…sasa hapa lazima mtu usome utake usitake…ama kweli kasuku huyu."
Makala iliyoanza kwa kichwa cha habari chenye mashiko, ilianza kutiririka. Makala hii ilimzungumzia binti aliyekata tamaa na kuilaumu serikali kwa kutowajali yatima, binti huyu aliyejiita mtanzagiza bila kutaja jina lake halisi alizidi kulaumu wale wote wenye uwezo wa kuwasaidia watoto yatima lakini wanawafumbia macho na kuwatukana kisha kuwanyayasa kila siku.
"Sijawahi kucheka kwa furaha, sijui mama yangu aliikosea nini Tanzania. Kwa nini wananifumbia macho, kila mahali sikubaliki, ama kwa kuwa katika jina langu kuna nyongeza ya majina mengine mawili, yatima na chokoraa? Ama kwa kuwa si msomi na siwezi kusimama mbele ya watu kuzungumza?
Tanzania inaninyanyasa.
Mimba yangu ilipatikana mama yangu akiwa huru, ikakua akiwa gerezani. Nimezaliwa na kuwa mtoto wa gereza. Mtoto huru bila kosa anayelelewa na gereza. Mama yangu alidhalilishwa nikishuhudia kwa jicho langu. Nilipokuwa na kuufikisha umri wa shule nilisomea shule iliyopo jirani na mwalimu alikuwa akiniita mtoto wa gereza pale nilipomkosea.
Mama yule anayetumikia kifungo cha miaka mingi aliugua!! Nilishuhudia huduma mbovu alizokuwa anapewa!! Hakuna aliyemjali hatimaye akaaga dunia huku akiita CHOKORAA!!
Mkuu wa gereza akanitwaa na kunilea nikiwa mmoja wa familia yake!! Watoto wake walinitenga, walinitukana walivyotaka!! Nilinyimwa chakula na hakuna aliyejali!! Nilipojaribu kulalamika nilipigwa sana kichwani. Hata chanzo cha kufeli masomo yangu ni mateso haya!!
Walitafuta mbinu ya kunifukuza licha ya kuwanyenyekea!!
Hatimaye wakaipata sababu!! Ni mimba mimba!!! Mimba aliyopata mtoto wa mkuu wa gereza!! Nikaambiwa nahusika nayo!!
Kwa amri yake nikawekwa gerezani. Chumba kile ambacho marehemu mama aliishi!! Baada ya miezi sita nikaachiwa huru!!
Sasa baada ya miaka kadhaa nikaingia mtaani. Mtaa nisioufahamu. Mtaa ambao haunifahamu pia!! Bila ndugu bila rafiki nikaingia mtaani!!!
Niliyakumbuka maneno ya mama yangu!! Aliniita CHOKORAA. Sasa nikawa chokoraa rasmi lakini CHOKORAA MWENYE CHUKI, KISASI NA ALIYEKATA TAMAA!!


Maneno haya makali yakamgusa Mathiasi, lile tabasamu lake likafutika kabisa, mawazo juu ya kumfananisha mwandishi na kasuku wake yakafutika mara moja. Akashtushwa na matone yaliyodondoka katika ile kurasa.
Mathiasi alikuwa analia!!
Akashangaa, haijawahi kutokea katika ukubwa wake kutokwa na machozi. Hata misibani alikuwa anavaa uso wa huzuni lakini kamwe sio kutokwa machozi.
Iweje leo analizwa na makala hii. Akajikuta akihisi amewahi kumuona huyu binti aliyemsoma. Ni wapi lakini amewahi kumuona sasa?
Akakumbuka ni katika vituo vya watoto yatima ambavyo huwa anaenda kwa ajili ya kutoa misaada huku moyoni akijua huo msaada malipo yake ni yapi.
Mathiasi alikuwa akichukua watoto yatima wenye vipaji kwa ajili ya kuwasomesha nje ya nchi lakini kamwe hawakurejea. Na ni nani wa kuuliza wapi walipo watoto hao?
Walikufa na kutupwa kama mizoga huko wanapopelekwa kwa danganya toto ya kusomeshwa.
Mathias alikuwa ni ‘zungu la unga' na alikuwa akiwatumia watoto yatima na machokoraa katika kusafirisha madawa ya kulevya. Hakuwa na huruma kwao, alichoangalia yeye ni masilahi yake.
Sasa alikuwa na pesa nyingi sana na alikuwa anaendelea na biashara ile haramu. Biashara iliyokuwa inaondoka na roho za watoto wasio na hatia. Watoto wanaotumikia dhambi ya wazazi wao. Watoto wasioelezeka kwa neno moja. Walitia huruma!!


Iweje sasa leo anatoa machozi kwa maneno ya mtu ambaye hajawahi kumuona hapo kabla. Mtu amabye hayajui matendo yake maovu? Aliduwaa.
Akatamani kujificha. Ni kama yule mwandishi na muhusika wa hiyo makala walikuwa wanamtazama. Mathiasi akajihisi kupatwa na hofu. Hofu akiwa katika himaya yake, himaya iliyojengwa kwa damu ya yatima na chokoraa. Mzee huyu akapatwa na ubaridi wa hali ya juu.
Mara akajikuta akinakiri namba ya Kasuku, akabonyeza kitufe cha kupiga simu ikaita. Ikapokelewa upesi wakati Mathias hajajiandaa nini cha kusema.
"Bwana Mathiasi naongea…..hongera kwa makala yako nzuri bwana Kasuku."
"Asante sana, Mathiasi…."
"Mtanzagiza ndo nani natamani kuonana naye sana."
"Upo maeneo gani?" iliuliza sauti ya Kasuku.
"Mbweni Masaiti lakini mara kwa mara nakuwa Kariakoo….hata hapo ofisini kwenu huwa nafika. Kuna sijui umewahi kuniona?" alizungumza bila kituo bwana Mathias.
"Hapana sijawahi kwani unafanya kazi hapa."
"Hapana nilikuja kwa ajili ya mahojiano…kuhusu watoto yatima."
"Ohoooo!! Bwana Mathiasi Dembele!! Bila shaka."
"Ewalaaa!! Ndio mimi, ni wapi naweza kumpata mtanzagiza?"
"Nipo naye maeneo ya huku Tandika ndio nyumbani kwangu. Karibu bwana Dembele karibu sana."
Waliagana baada ya kupeana ahadi ya kuonana.
Simu ilipokatika. Upande wa Mathias alishusha pumzi kwa nguvu huku akiwa bado hajajielewa nia yake.


Upande wa bwana Kasuku, alichanua tabasamu pana.
Frida aliyekuwa pembeni yake alimtazama kwa macho ya kitafiti.
"Nilikwambia..haooo wameanza kupiga simu…ile simulizi yako lazima kwa mwanadamu mwenye nyama aguswe ipasavyo. Huyu aliyepiga simu ni mmoja kati ya wadau wakubwa hapa nchini kwa kuwezesha yatima." Alisema bwana Kasuku huku akinyanyua mabega yake juu.
"Anakuja kesho jioni utamuona. Usimuogope kuwa muwazi. Atakusaidia amini Frida amini kuwa bado unao umuhimu mkubwa sana katika hii jamii. Jiamini kuwa Tanzania inakuhitaji sana." Kasuku alisisitiza.


***MATHIAS anashiriki biashara haramu ya kusafirisha madawa ya kulevya kwa kutumia kivuli cha kusomesha watoto yatima. Sasa anataka kukutana na chokoraa mwingine. Nini hatma yaFRIDA.
***Na je ni nani alimuokoa FRIDA kutoka katika maji ya bahari.
***MWANAIDI, ISHA NA GEORGE wote wanamuwaza FRIDA……Nani atawakutanisha tena??

VAN HEIST muuza ubuyu amina mabata shabani hassani culbby sam II ram BPM mbalu saljar MAVUNO Khantwe
 
Inazidi kuwa tamu kila siku.....
Leta episode nyingine basi Casuist
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom