RIWAYA: BANGUZI
NA: HASSAN O MAMBOSASA
_______SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI_____
"Roja nisipajue tena bloki unayoishi, mchanganuo uwepo tu", Derva alisema.
"Poa we twende
_________TIRIRIKA NAYO
Dakika takribani kumi baadaye, waliwasili chini ya ghorofa ambalo Roja anaishi. Wote kwa pamoja walishuka na kumlipa dereva, gari ilipondoka walianza kutembEa huku wakipiga domo na kuzifikia ngazi ya eneo hilo na kuzipandisha kwa maringo hadi walipofika ghorofa ya kwanza ambapo ndipo kituo chao.
Roja akiwa mbele aliwaongoza wenzake hadi mlangoni mwa chumba kimojawapo, alinyonga kitasa lakini akakuta umefungwa na kupelekea agonge.
"Aaargh! Huyu kevi si bure atakuwa amelala leo kapiga msuli sana", Aliwaambia wenzake.
"He! Mnajua kuna watu wabaya dunia hii, na wale wambea walivyomwambia ana mwanamke humo ndani. Ona sasa Radhia ungekuja kujitia presha bure, nilikwambia usisikilize ya watu shosti", Mmoja wa wasichan alimwambia yule abinti aliyekaa mbele walipopanda teksi.
Banati yule naye alijikuta akikosa la kusema, ingawa bado alionekana ni mwenye shaka. Mlango ulipofunguliwa na kumwona Kevi akiwa amekunja uso kuashiria akionekana ametoka kulala, kidogo alionekana ni mwenye ahueni na aliachia tabasmau kisha akamsogelea na kumkumbatia kwa nguvu.
"Jamaa yaani huko ilikuwa ni tifu mno alikuwa haniamini huyu, haya huyo hapo. Shem tatizo wewe una wivu kupitiliza", Roja alisema.
"Akaa! Babu wee! Abiria huchunga chake, wivu sunna", Radhia alisema na kupelekea wengine wacheke.
"Haya jamani karibuni ndani", Kevi aliwakaribisha ndani huku akimtazama Roja halafu akampa ishara.
"Yaani mtu wangu tuache tu, kuna magashi hapa wanajua kumsemea mtu kam vile wanamwona", Mvulana mwingine aliyeongozana nao alisema.
"Jofu unajua kabisa, nina maadui wengi hapa chuoni fikiria wamemjua hadi Radhia anayesoma IFM huko. Jiulize hatujawahi kumwambia mtu, walimjua vipi?"
"Ndiyo hapo mtu wangu, Radhia leo alimpa kampani shosti wake tukiwa klabu, sasa kuja kutuona tu ndiyo wakaleta sumu zao hawajui watakuja kumuua mtu wale maboya", Jofu alisema.
"Sasa hivi roho yangu nyeupee!", Radhia alisema.
"Shosti nawe una wivu kupitiliza, unaweza kumtoa masikio dada yake huyu ukimwona naye", Binti mmoja alisema.
"Khaaa! Tabu jamani yashaisha basi" Radhia alisema kisha akamgukia Kevi na kumshika kidevu halafu akaendelea, "Eti baby kuna mapenzi bila wivu? Wivu si ndiyo mapenzi ati, au wewe hunioni wivu?"
"Haki ya Mungu natamani hata kushika bunduki nikikuona umesimama tu na ndugu yako kwa jinsi nilivyokuwa na wivu. Sasa fikiri nikikukuta na mwingine", Kevi alisema na kupelekea wengine wacheke.
"Kumbe bilabila hapa", Tabu alisema.
"Unafikiria ni mchezo nini kupenda sikieni, oyaa Kevi kile kitasa mbona hujakiweka freshi mwanangu?", Roja alisema kisha akaongezea kwa kumuuliza swali Kevi.
"Halafu unajua sikukusoma jamaa ulitaka kiwe namna gani maana ninakiona kipo sawa", Kevi alinena
"Hebu ngoja nikakuoneshe jamaa", Roja alisema huku akiinuka halafu akawaambia wengine, "Jamani tunarudi sasa hivi tunaenda kucheki kitasa, kuna ishu nilimpa akiweke sawa nikasahau kumpa maelekezo"
"Poa", Jofu ndiyo akawa wa kwanza kuitikia na kuwafanya hata wengine waone inatosha si lazima wainue wao midomo.
Wavulana hawa waliongozana hadi mlangoni na waliufungua, kisha wakatoka nje na kuufunga. Baada ya kufanya hivyo Roja alikichezesha kitasa karibia mara nne, halafu akamgeukia Kevi. Walipotazama kila mmoja aliweka mkono mdomoni na kuanza kucheka kimyakimya, kuhofia wangeweza kusikiwa ndani.
"Ma**na wewe ungefumwa leo yaani ushukuru nilivyompanga mimi na Jofu", Roja alisema kwa sauti ya chini.
"Mam*e yaani leo nilikuwa naadhirika mtu wangu, hivi ulipata wapi huo muda wa kunipigia simu jamaa maana ulikuwa na Tabu"
"Mtu wangu ilibidi nichomoke fasta na kwenda chooni kule klabu, huko ndiyo nikakupa data zote anataka kuja huku ajihakikishe.Yaani hatujakaa hata hilo tifu lake, imebidi turudi tu. Hivi Sara umemtoa vipi hapa ulikuwa ushapiga show"
"Mtu wangu tayari mchezo na kalala pono, nilitaka niliamshe dude asubuhi ila uliponipigia simu nikamwambia Mgaya katonywa nimeingiza demu ndani anakuja huku yaani kafura kwa hasira", Kevi aliposema hayo Roja alicheka nusura atoe sauti, tena huku akiendelea kukichezesha kitasa ili wa ndani wajue wanaelekezana.
"Dadeki wewe mtu mbaya sana, yaani mademu wanavyomwogopa yule, umemuweza. Tuzame ndani jamaa yangu, stori zingine kesho si unajua huyo mtu wako leo hatoki leo", Jofu alisema huku akifungua mlango, aliingia ndani huku akitembea kwa taratibu na kwenda kuketi jirani na Tabu.
Kevi naye aliingia huku akisikitika halafu akasema, "Jamaa siku nyingine uache ubishi, kitasa chenyewe kumbe cha kufunguliwa kabisa maana hakifai kufix bila kufungua kile kimeshalegea chuma cha ndani"
"Beibi utamuweza basi huyu Roja, yaani ubishi wake kama Tatu hapa. Naona Mungu hakukosea kuwaweka pamoja", Radhia alidakia pasipo kujua hiyo ni sehemu ya kuzuga tu.
"Si unajua tena ndege wafafanao hukaa pamoja, huwezi kukuta Kipanga akakaa na Kuku", Jofu alisema na kupelekea waliyomo humo ndani wacheke mno.
"Sawa leo mmetuweza", Roja alisema huku akiinamisha uso chini.
_______________
Sarah akijua kule anakuja mjomba wa Kevi mule ndani, alifika jengo analoishi na mwenzake akiwa na hofu kubwa. Aliwasili chumba chake na kukuta tayari taa imezimwa na mlango umefungwa, aliugonga mlango kwa nguvu. Hakujibiwa jambo llilomfanya aendelee kufanya hivyo, ukimya ulipozidi alijikuta akichukua simu huku bado mapigo ya moyo yakimwenda mbio. Mawazoni aliona kama vile ndiyo anafuatwa na kaimu mkuu wa chuo hicho, hofu ilimtawala haswa.
Aliipiga simu ya mwenzake anayeishi naye humo ndani, lakini iliita haikpokelewa. Hali hiyo alijikuta akipigapiga nyayo zake zilizo ndani ya viatu alivyovivaa njiani hapo sakafuni. Alijaribu kwa mara ya nyingine, ila haikujiiwa mambo yakawa ni yaleyale. Alijikuta akikata tamaa ila nafsi ikamsihi apige tena, safari hii simu ilijibiwa. Alianza kuongea kwa pupa, "Atu! Ni.......nipo mlangoni nifungulie haraka..... usiniulize nifungulie niingie ndiyo nitakujibu....haya".
Simu ilikatwa na alijikuta akitazama kushoto na kulia kwa eneo hilo, hakuona mtu yeyote na alishusha pumzi za ahueni. Mlango ulifunguliwa na aliingia ndani kwa papara kuu, kisha akaufunga mwenyewe akabaki akihema kwa nguvu.
"Sara vipi mbona tunatishana? Kwani huko kwa shem kumetokea nini?", Atu aliuliza huku akifikicha macho.
"Atu acha tu, yule mzee mnoko si kaambiwa yupo na mwanamke hosteli. Yaani alikuwa yupo njiani anawahi kuja huko, asingepigiwa simu na rafiki yake aliyesikia hiyo habari sijui ingekuwaje?", Sara alisema.
"He! Nani?"
"Mjomba wake Kevi, Professa Mgaya"
"(Huku akiweka mikono kichwani) Mungu wangu yaani ingekula kwako leo, cha moto ungekiona, sijasahau alichomfanyia mwanae wa kumzaa na demu wake"
"Shosti mwenzangu yaani nimetoka mbio hata sijui nimepata wapi spidi ile. Chupi yenyewe sijavaa nimewekewa mfukoni kama leso", Atu aliposikia maneno hayo ya Sara, alijikuta akicheka kwa nguvu mno.
"Unacheka unaona mazuri siyo?" Sara aliuliza kwa sauti ya kulalamika.
"Yaani ulivyotoka huko wacha nicheke tu shosti, mbio unazijua kumbe siku zote unajifanya umechoka tu ukitembea umbali mrefu tu"
" Nyoo ingekuwa ni wewe ungefanyaje sasa?"
"Hebu tuache hayo, jitazame huko usije ukawa umejichafua kama kaenda bila ganda"
"Ngoja nivue tu nguo nikaoge usiku huuhuu", Sara aliongea huku akainza kutoa nguo ya juu.
Hakujua kama aliyoambiwa ni uongo uliyopangwa kikamilifu, kutokana na jinsi Kevi alivyoonekana kuwa na hofu kubwa alijua wazi siku hiyo ni sawa na kiama. Kumbe alichoelezwa hakijatokea, aliingia himaya ya waongo waliyotaka kumwepusha mwenzio asigonganishe magari.
_________
Asubuhi ya siku iliyofuata Jamal aliamka kwa kuchelewa kutokana na kulala muda mbaya, alikuta anayeishi naye chumba kimoja akiwa hayupo ndani. Alijiinua kwa uchovu mkubwa kisha akaketi kitako, hapo alijikuta akitokwa na tabasamu usoni mwake na alibaki ni mwenye kutafakari jambo fulani kichwani mwake.
Alipoteza muda kitandani na hatimaye alishuka kisha akachukua taulo na mswaki wake, alitoka nje ambapo alitumia robo saa akawa amerejea akiwa ameoga. Jamal alibadili nguo akatoka chumbani anapoishi na kufika hadi nje akaanza kutembea kwa taratibu akikata mitaa ya mahali hapo. Jamal hakuwa na hili wala lile majira hayo akitembea, alishtuka tu akipigiwa honi ya gari. Alishtuka na kusoge kando ya njia kabla hajaangalia nyuma, ila alipogeuka alijikuta akiachia tabasamua baada ya kuona msafara wa baba yake ukisimama.
Walinzi walishuka na kufungua mlango wa gari alilopanda bosi wao, JD alishuka akiwa na uso wenye furaha. Alifika na kumkumbatia mwanae, huku walinzi wakiwa wamesimama imara kuhakikisha usalama unakuwepo.
"Baba mbona ghafla hivyo?", Jamal aliuliza.
"Yote ni kuhakikisha tu kama upo ok, nilikuja muda mrefu mno nikatuma mtu aje kuangalia nikaambiwa umelala. Nimengoja umeamka hadi umetoka nje, ndiyo nikaja mahala hapa", JD alisema.
"Sasa baba kwanini usingekuja tu ndani, ulipaswa uniamshe mimi mtoto hukupaswa kunisubiri namna hiyo. Mimi ndiyo ninatakiwa kukusubiri hivyo nikikukuta umepumzika"
"Hapana nipo sahihi kufanya hivi nifanyavyo, nikuache upumzike kijana wangu sijajua umelala saa ngapi hadi nije nifikie kukumsha tu"
"Sawa, ila kuna kitu kimoja kama mwanao huwa sikipendi sana"
"Uko huru kusema"
"Sipendi mno kuongozana na walinzi wengi hivi baba, napenda uwe mwenyewe kama nilivyo mie", Jamal aliposema hivyo, JD aliuzungusha mkono shingoni mwake na kuanza kutembea kuelekea lilipo gari aliloshuka.
"Nimetokea familia yenye uhasama mno, Baba yangu alikuwa akiendesha mipango yake kibabe na kunipelekea mimi niingie kundi hilo. Hivyo nina maadui wengi mno, ukiachana na hilo ukumbuke nimetoroka Argentina. Sipaswi kujiamini muda wowote"
"Ok nimekuelewa, nahitaji uwe salama siku zote"
"Nimekufuata hapa tuwahi nyumbani kwa Bi Agatha si unajua kuna nini leo, ingia garini twende. Kwanza nafikiri tupitie ukaptae chai, nina uhakika hapo ulipo bado hujatia kitu tumboni"
"Hujakosea hata", Waliingia kwa pamoja garini, msafara huo uliondoka mahali hapo huku baadhi ya wanafunzi wakiwa wameona kile kinachoendelea na walibaki wakitazama tu kwa mbali.
____________
"Mwanangu Kevi we mbaya sijapata kuona yaani, una mbinu hatari", Jofu alisema huku akicheka, muda huo ni tayari mabinti wale waliyokuja nao usiku walishaondoka. Walibaki wenyewe tu, ndipo wakaanza kuijadili mada ya jana jinsi mwenzao alivyoweza kuepuka kikwazo kikubwa kwenye mahusiano yake.
"Yaani hizi harakati kama mjeda, vita nyingi ndiyo ujuzi unazidi. Ulitegemea ningefanyaje nimtoe gashi mule. Radhia naye si alikomalia aje huku", Kevi alisema.
"Ila we boya umezidi yaani sisi tunaenda klabu ukaona ni njia nzuri tu kujipiga mwenyewe humu. Ulitaka ukeshe kabisaa", Roja alisema.
"Sasa ulisema hurudi unachukua chumba kwa juu ujisevie, ulitegemea nifanye nini na mtoto kaingia kumi na nane yule. Sikuwa na mpango wa kupiga jana ila kaja humu mwenyewe eti kupiga stori, nikaona usinitanie wewe. Uingie pango la mamba utoke mzima wewe"
'Ukajipigia tu kumbe huko tulipo moto umewaka hata kuchukua vyumba tuliacha tuje tumwoneshe kadanganywa", Roja alisema.
"Wana tuacheni utani mimi ni mwongo wa kupanga mbinu za kila namna, ila gredi ya huyu boya sijafikia aisee. Una mbinu za ajabu", Jofu alisema.
"Mtu wangu ukizoea kudanganya akili inakuwa fasta tu kutunga uongo mwingine, nimepiga dabo sasa. Sara nikimwona namlia boksi kama simjui, yaani nakuwa nimepoteza kumbukumbu zake kabisaa"
"Namna hiyohiyo si kajileta, ufanyaje?", Jofu alisema.
"Dah! Akiniona atajua nina tintedi simwoni, yaani mikausho tu ninaangalia mwingine nani atajileta"
"Sema nini yule happy mnene fulani hivi kaingia saiti tayari, inabidi uniachie chinjio hili usiku wa leo namaliza mchezo humu", Roja alisema.
"Kupigia asteaste kwa Tabu umeona uje kutulizia kwa yule yote", Jofu alisema.
"Sasa kumbe je nifanyeje mimi, Mungu atupe nini sisi yaani watoto wenyewe wanakuja. Wacha nijipigie mwenyewe", Roja alisema.
"Sawasawa balozi wa shirika la wakataa mimba, Katibu mkuu wa wizara ya wasiyotumia ndomu"
"Sawa Spika wa Bunge la wavua chupi, mbunge wa jimbo la uzinzi", Roja alisema na kupelekea wote wacheke huku wakigonganisha mikono yao.
*LOH! HAWA WAHUNI HAWA WAMEZIDI
*DUH! KUNA WATU UONGO KAMA WALIINGIA CHUONI KUUSOMEA
*SARA KAINGIA ORODHA YA KEVI
*JE NINI HATMA YAO HAWA WAHUNI?
ITAENDELEA!!!