Kumbuka huyu jaji ni mmojawapo wa wale ................ Tazama taarifa ya Lisu. Naona Nchimbi alikuwa anataka kupigia mstari utetezi wa Lisu.
This leaves me to wonder kama ripoti ya Baraza la Habari Tanzania na Jukwaa la Wahariri Tanzania ndiyo hii, tutegemee nini kwenye hizo ripoti za Polisi na Nchimbi?
Tazama Ukurasa wa 29, ripoti inasema hivi "Hata hivyo uchunguzi hauwezi kuthibitisha kama mauaji hayo ya
Mwangosi yalipangwa". Hii sio kazi yao. Hii ingeachwa mikononi mwa makachero waliobobea, wangeweza
kubaini hili.
Hawa akina Mukama wasituzingue, tangu lini siasa zikaamia kwenye miongozo ya spika kibao. Halafu spika mwenyewe kada pamoja na naibu wake wenyeviti na wabunge wa CCM ambao ni mavuvuzela tu. Siasa ziko mtaani kwa mikutano, maandamano, hamasa, nyimbo, ngoma nk.
CCM wanatafuta kila njia Watanzania wasielewe unafiki na udhaifu wao. Sekondari za kata zimeshawamaliza.
"Kwa misingi hiyo Kamati imeona kwamba nguvu iliyotumika mwanzo hadi kumaliza Operesheni haikuwa kubwa. Kuhusu tukio la kuuawa Bw. Daud Mwangosi na kuumizwa baadhi ya Askari Polisi halikustahili kabisa."
Hii sentence sijaielewa. Imeandikwa na Jaji, Wahariri (Editors) wawili na Kanali Dr mmoja!!!
Mods, naomba kwa mara ya kwanza toka nijiunge na JF nitukane mtu. Walioandika hii ripoti ingefaa wakamatwe mara moja na kufikishwa wanakostahili kwa uwongo na wizi wa kujipatia hela kwa njia ya udanganyifu bila kuifanyia kazi. Hawana tofauti na mlevi aliyeshiba pombe ya pingu na kama ilivyo kawaida kalowa na bila akili anajipitisha pitisha mbele za watu bila kujitambua kuwa anatoa harufu kali ya kunuka hadi hata nzi wanamkwepa. Naapa na nasema wazi kuwa kama moja wa hawa watu angekuwa ndugu yangu, nisingeongea naye tena katika maisha yangu...ni aibu, ni aibu na ni aibu. Halafu moja wao anajiita Jaji na mwingine anajiita Mwandishi, what? Hivi tumemkosea nini Mungu? Naomba niishie hapa!