Nguruvi3, I don't know what is more painful, kuangalia picha ya mabaki ya Daudi Mwangosi au kusoma hii report ya Nchimbi? Report inaonesha ni jinsi gani Jaji Ihema na wapambe wake wanavyoona watanzania ni mazuzu! Na inaelekea walichokifuata Iringa ni eneo la kukaa na kuandika mambo ambayo walishakubaliana.
Nimesoma kwa kurukaruka sehemu maana report imejaa upuuzi wa viwango vya juu sana. Inaharibu kabisa taswira ya majaji wetu pamoja na mwandishi wa habari Theophil. Yaani pamoja na vielelezo vyote (stilll and moving pictures) bado wanaleta habari za kutunga? Kama sio madharau kwa watanzania ni nini?
Kama huyu Jaji na wenzake walikuwa na nia njema wangeanza kwa kuuliza amri ya vyama vya siasa kutofanya mikutano wakati wa sensa ilihusu chama kimoja au vyote? Na amri hiyo ilihusu mikutano ya hadhara au mikutano ya ndani? Na CHADEMA walikuwa na mkutano wa hadhara au wa ndani?
Pili, maaskari waliokuwa kwenye eneo la tukio wote ni wa mahali hapo? kama jibu ni hapana, walikuja lini, na kwa sababu zipi?
Lakini kuna mambo kwenye hii report yanatia kichefuchefu. Jaji Ihema anaonekana ku-suggest kuwa Daudi Mwangosi aliuwawa na mtu/watu wengine mbali na polisi! Na anaenda mbele zaidi na kutoa maoni kuwa vikundi vya ulinzi kama Green guards, blue, guards and red guards viangaliwe upya. Moja kwa moja utaona kuwa anachosema jaji ni kwamba Daudi Mwangosi aliuliwa na moja ya hivyo vikundi?
Yote tisa, kumi Jaji anatoa mapendekezo ya kufuta shughuli za siasa nje ya bunge!
Kwa maoni yangu, hii tume ilikuwa na kazi maalum, kazi ya kuungaunga habari ili wapate nafasi ya kuchomekeza mapendekezo 'maalum' kama kuweka sheria ya kukandamiza vyama 'vya msimu' na kumpa msajili wa vyama vya siasa nguvu ya kuburuza vyama vinavyosumbuwa wakubwa.
Kwa zama tunazoishi sasa, ni kituko tena kituko kweli kweli kuandaa report chafu kama hiyo. Watanzania wengi wanajua mkanda mzima wa mauaji ya Daudi Mwangosi. Kamati ingejiwekea heshma kwa kuleta report inayoeleka na sio hizo ngonjera za mwaka 47. Yaani wameingiza mpaka points za Shibuda?!