Ripoti ya Kifo cha Mwangosi

nimepitia kwa haraka nimegundua in upendeleo kwa vyama vingine sijui kama wameliona hilo mfana kirefu cha chadema kimeelezewa vizuri ila cha ccm hamna ingawa neno ccm limetumiwa mara nyingi sana ndani ya ripoti yenyewe ina maana hili hawakuliona au ni makusudi mazima.

CCM ni taifa kubwa hakuna CCM nyingine duniani ndio maana hakuna haja ya kuweka kirefu chake! hata mtoto alozaliwa leo anajua CCM inastand for what !
 
hii ndio ile kamati ya nchimbi au nimeuliza dumb question?nimeisoma yote,kamuhanda should be hanged

What about John HEche? mimi mtazamo wangu huyu ndio sababu ya yot, hebu fikiri angewaambia wafuasi wake wasifanye mkutano, na watii amri ya police, hivi unadhani Mwangosi angeuawa? be fair soma vizuri report
 
Hii report inakosa kitu fulani hivi, kama vile ina-hang haijaonyesha uhalisia wa ishu yenyewe, nilitamani nipate vinjo vingi vya watu waliohojiwa, kweli bado naiona ni nyepesi sana hebu tutbiri na hio nyingine labda
 
Dr. Nchimbi wants to send this report to UN? why it is written in english? Majority of Tanzanias will not benefit from this bias report. We want Swahili edition Please
 
Mbona waliyoandika yote tunayajua? hii tume nayo ilitumia hela za walipa kodi?
 
Mwangosi aliuwawa na Polisi hiki ndicho ripoti inaonesha japo imezunguka
 
Report imesaidia sana kuweka kumbukumbu sawa kwa kuonesha kila kitu kilichotokea.

Ingawa haikati kiu ya baadhi ya watu nikiwemo mimi...Naona inakidhi matakwa ya malengo (objectives) ya uchunguzi wenyewe...

Pia hitimisho lake halijitoshelezi kabisa kwa sababu halikujibu malengo ya uchunguzi. Pia sikuelewa kwa nini waliamua kutumia maneno mengi kiasi hicho (>3pages) kuhitimisha report ya page 30!!
 
ripoti haijaeleza kwa nini Godfrey Mushi alikuwa akipigwa na
polisi mpaka Mwangosi kuingilia kati,na kugeuziwa kibao
 
Nimeisoma kwa makini, neno kwa neno, hakika CHADEMA ni wa kulaumiwa, kwa sababu katika report hii sehemu kubwa ni ubishi wa CHADEMA ndio ulomuuwa Mwangosi, sijui CHADEMA mtamlipa nini mjane na watoto hawa YATIMA wa mwangosi, Namlaumu Joh Heche kwa yote haya yalotokea, tubu kwa Mola wako na waombee sana watoto wa MWangosi wapate malezi bora au sivyo sijui kizazi chako wewe kitakuwa vipi! NAWAPA POLE SANA FAIMIA YA MWANGOSI ... na MOLA AWAFARIJI WAKATI WOTE NA AWAKUZE WATOTO WENU KATIKA MAADILI MEMA YENYE UCHA MUNGU.
Kamuhanda umeanza lini kumjua Mungu? Mzimu wa Mwangosi hautakuacha mpaka siku unakwenda kaburini na utakufa kifo kibaya sana ww.
 
Lengo la uchunguzi huo ni kuweka rekodi sawa ya mazingira yaliyopelekea kuuawa kwa Mwangoso. Hata hivyo uchunguzi hauwezi kuthibitisha kama mauaji hayo ya Mwangosi yalipangwa. Hadidu za rejea tuu zinaonyesha hawakuwa na jipya la kuchunguza. Hili linadhibishwa na uchunguzi wenyewe kuchukua siku nane tuu.

Hii ripoti siyo sawa kuita ni ya kichunguzi kwa sababu haijakidhi matakwa hao. Hakuna analysis or any sort of investigations iliyofanywa hapa. Kila mtu aliyefuatilia hili suala anajua zaidi ya kilichomo kwenye hii ripoti. Tatizo waandishi wetu wamezoea kuripoti mambo bila kuyafanyia analysis na uchunguzi wa kina.

With all the information available on the internet, hata mie nisiye mwandishi wa habari, I could have sat in front of my PC na kundaa ripoti kama hiyo ndani ya siku nane!


This leaves me to wonder kama ripoti ya Baraza la Habari Tanzania na Jukwaa la Wahariri Tanzania ndiyo hii, tutegemee nini kwenye hizo ripoti za Polisi na Nchimbi?
 
Nimeisoma ripoti yote. Kwa kweli inasikitisha sana. Waandishi wa Habari hamko salama tena chini ya Huyu Rais mliyemweka madarakani wenyewe. Hamna haja yoyote ya kuwa neutral katika mambo kama haya. Kisusieni chama chake, ongozeni vuguvugu la mapinduzi!
 
Ohh. CCM itaendelea kutawala, CCM ni chama nikadumisha amani. >>>>>>So what??<<<<<<:shock:
 
Back
Top Bottom