Ripoti ya Kifo cha Mwangosi

Ripoti ya Kifo cha Mwangosi

FJM, yapo mengi sana yanyotia uchungu kama kifo cha Mwangosi aliyekuwa anatafuta mkate wa familia.
Yapo yanayoudhi sana na kutia hasira:
1. Kutumia kifo cha Mwangosi kuficha 'wahalifu' wakubwa akina Chagonja, Kamuhanda n.k.
2. Kutumia kifo cha Mwangosi kuficha wahuni wa siasa kama akina Nchimbi
3. Kutumia kifo cha Mwangosi kuudanganya umma
4. Kutumia kifo cha mwangosi kukaa mahali na kutunga uongo

Kinachosikitisha sana ni kuelewa kuwa wapo watu wengi waliohukumiwa na Jaji Ihema. Watu hawa wahawakutendewa haki kwasababu Jaji Ihema ameonyesha uelewa kidogo (in fact kutoelewa) anachokifanya.
Ameandika ripoti ambayo mtoto wa kidato cha sita angeweza kuiandika vizuri zaidi kama insha.

Kinachotia kichefu chefu ni Theophili Makunga, mtu anayedhaniwa kuwa mwandishi na mwenye weledi kukaa pamoja na Jaji Ihema na kutunga upuuzi usiolingana na taaluma yoyote isipokuwa kama ipo ya wapuuzi.

Tunaichambua habari hiyo na tutarejea na kipengele kimoja baada ya kingine ili kuonyesha kuwa hatumtukani wala kumdhalilisha Ihema na Makunga, bali wamejidhalilisha wenye.
 
Nguruvi3, I don't know what is more painful, kuangalia picha ya mabaki ya Daudi Mwangosi au kusoma hii report ya Nchimbi? Report inaonesha ni jinsi gani Jaji Ihema na wapambe wake wanavyoona watanzania ni mazuzu! Na inaelekea walichokifuata Iringa ni eneo la kukaa na kuandika mambo ambayo walishakubaliana.

Nimesoma kwa kurukaruka sehemu maana report imejaa upuuzi wa viwango vya juu sana. Inaharibu kabisa taswira ya majaji wetu pamoja na mwandishi wa habari Theophil. Yaani pamoja na vielelezo vyote (stilll and moving pictures) bado wanaleta habari za kutunga? Kama sio madharau kwa watanzania ni nini?

Kama huyu Jaji na wenzake walikuwa na nia njema wangeanza kwa kuuliza amri ya vyama vya siasa kutofanya mikutano wakati wa sensa ilihusu chama kimoja au vyote? Na amri hiyo ilihusu mikutano ya hadhara au mikutano ya ndani? Na CHADEMA walikuwa na mkutano wa hadhara au wa ndani?

Pili, maaskari waliokuwa kwenye eneo la tukio wote ni wa mahali hapo? kama jibu ni hapana, walikuja lini, na kwa sababu zipi?

Lakini kuna mambo kwenye hii report yanatia kichefuchefu. Jaji Ihema anaonekana ku-suggest kuwa Daudi Mwangosi aliuwawa na mtu/watu wengine mbali na polisi! Na anaenda mbele zaidi na kutoa maoni kuwa vikundi vya ulinzi kama Green guards, blue, guards and red guards viangaliwe upya. Moja kwa moja utaona kuwa anachosema jaji ni kwamba Daudi Mwangosi aliuliwa na moja ya hivyo vikundi?

Yote tisa, kumi Jaji anatoa mapendekezo ya kufuta shughuli za siasa nje ya bunge!

Kwa maoni yangu, hii tume ilikuwa na kazi maalum, kazi ya kuungaunga habari ili wapate nafasi ya kuchomekeza mapendekezo 'maalum' kama kuweka sheria ya kukandamiza vyama 'vya msimu' na kumpa msajili wa vyama vya siasa nguvu ya kuburuza vyama vinavyosumbuwa wakubwa.

Kwa zama tunazoishi sasa, ni kituko tena kituko kweli kweli kuandaa report chafu kama hiyo. Watanzania wengi wanajua mkanda mzima wa mauaji ya Daudi Mwangosi. Kamati ingejiwekea heshma kwa kuleta report inayoeleka na sio hizo ngonjera za mwaka 47. Yaani wameingiza mpaka points za Shibuda?!

Mkuu huu ni upuuzz wa hali ya juu!!!
Wnadhani sie majuha kama wao hebu angalia hiki kipande....

" -Nafasi za Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa kiutendaji ziangaliwe upya ili zisitumike na mhusika kwa ajili ya manufaa ya kisiasa.

-Kwa kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kuwa ndiye mlinzi wa usalama wa raia na mali zao, siasa za ubabe kwa vyama vya siasa ziepukwe kwa kuwa zinaleta msuguano usio wa lazima na Jeshi la Polisi

-Kuhusu operesheni ya uzuiaji wa mkutano wa CHADEMA usio halali Kijijini Nyololo tarehe 02 Septemba 2012, Jeshi la Polisi lilitekeleza wajibu wake ipasavyo na kutumia nguvu sahihi. Operesheni iliyoandaliwa na kufanyika ilikamilika kwa kuwatawanya watu waliofika kwenye mkutano, kukamata baadhi ya Viongozi na wafuasi wa CHADEMA na hali ya utulivu ilirejea kwenye eneo husika. "




...



..


...
Nafasi ya mkuu wa wilaya na wa mkoa kiutendaji ziangaliwe vipi, ilhali umesema polisi walitenda vema.....

Huku si kuweweseka kwa hali yajuu kwa wanafiki hawa?

 
  • Thanks
Reactions: FJM

-Kuhusu operesheni ya uzuiaji wa mkutano wa CHADEMA usio halali Kijijini Nyololo tarehe 02 Septemba 2012, Jeshi la Polisi lilitekeleza wajibu wake ipasavyo na kutumia nguvu sahihi. Operesheni iliyoandaliwa na kufanyika ilikamilika kwa kuwatawanya watu waliofika kwenye mkutano, kukamata baadhi ya Viongozi na wafuasi wa CHADEMA na hali ya utulivu ilirejea kwenye eneo husika. "


Report ya cheusi-chekundu.
Hapo kwenye red: Kama police ilitekeleza wajibu wake kama ipasavyo, kwanini mmoja wa hao police ana kesi mahakamani?
 
vichekesho,aisee eti hayati baba wa taifa sijui nini nini,ripoti haina taarifa za kiuchunguzi
 
mods tunaomba ruhusa ya lugha chafu japo dk 5 tu kwa hili liripoti la kik..

Upuuzi kama huu ndio unapelekea mahitaji ya kuwepo jukwaa ambalo ni "Ban Free Zone" yazidi kua makubwa.
Mods tufungulieni jukwaa hili japo kwa leo tu tumalizie hasira zetu kisha mtalifunga!!
 
Ukimpa mtu kazi akaboronga, na wewe ukaipokea, nadhani mwenye tatizo kubwa zaidi ni wewe uliyetoa kazi.

Nchimbi, kama umeipokea ripoti hii, hata udaktari wako tunautilia mashaka, na hatuna imani nawe katika kazi yako.
 
Sina uhakika kama hawa wachovu ( kamati ) huwa wanaingia katika jf, wangeona mawazo na maoni ya watz juu ya thread hii. Sehemu kubwa wameegemea kulaani chadema kutotii amri halali ya polisi badala ya kupima iwapo hiyo amri ilikuwa na 'logic ' hasa kwa kuwa watu waliokuwa wamebaki kuhesabiwa kwa nchi nzima walikuwa ni 5% tu tena utaratibu kwa hao ulishawekwa ili wahesabiwe. Utaona kuwa ile amri ya kutofanya mikutano ya siasa haikuwa halali na haikuwa na maana bali ililenga kuvuruga amani kwa kupitia mgongo wa chadema . ieleweke wazi kuwa siku na tarehe hiyohiyo ccm ilifanya mkutano mkubwa wa kuzindua kampeni za ubunge kule bububu zanzibar na polisi haohao waliulinda mkutano ule. kwa nini nyie kamati mnaongeza hasira kwa wa tz kwa uongo na unafiki wenu ? Kwani hamna dini nyie ?. mjue kuwa hayo mnayowafanyia wa tz sasa yanawekwa katika kumbukumbu msije mkajilaumu baadaye kwani mungu ni wa wote na hwezi kuwapendelea nyie milele. mmeniudhi sana hata elimu yenu ni ya bure.
 
Kwanza naomba posho walizopewa wajumbe wa kamati wajiandae kuzirejesha ikiwa ni pamoja na lap top waliyoibiwa pale iringa wakati wakipanga uongo waliouleta. Cag huwa unazikagua kamati kama hii ? Tafadhali fanya hivo sasa.
 
Nyerere aliwahi kusema "mtu mwenye akili akijua kuwa na wewe una akili akakushauri jambo la kipumbavu na wewe ukakubali atakudharau". Hili ni kweli pia kwenye suala hili. Mtu mwenye akili akijua na wewe una akili ahalafu akakuandikia jambo la kijinga na wewe ukalikubali atakudharau!

Hii ripoti ni ushahidi wa kile ambacho wengine tunaamini ni kweli; CCM na serikali yake ni lazima waondolewe madarakani sooner kwa sababu wanatudharau! Ni dharau ya ajabu sana hii. Fikiria mtu anaandika hivi kwenye ripoti:

Kwa minajili hii basi Kamati imeshindwa kubaini baada ya kumalizika operesheni na askari Polisi kuanza kuondoka, kwa nini Mwangosi alishambuliwa kwa kipigo kabla ya kulipuliwa na bomu la kishindo?

Hili swali ni la msingi sana katika tukio zima.

Lakini Kamati imeshindwa kujibu swali ambalo kwa walioona iile video ya mauaji wanalikumbuka sana yaani linalohusiana na kukatazwa kufanyika kwa mikutano ya ndani ya chama. Msingi wa maelezo kuwa sijui kulikuwa na amri inayokataza mikusanyiko hayana msingi hasa kwa vile ripoti haijaweka hadharani hilo katazo linasemaje. Kamati imeweka barua tu lakini haijatuambia katazo lilisemaje.

Lakini kuthibitisha upuuzi wa kamati hii imeshindwa kuelezea kuwa kwanini katazo hilo liwe halali Iringa lakini Zanzibar lisiwe halali wakati CCM walipofanya uzinduzi wa kampeni yao ya Bububu?

Ni ripoti ya kijinga.
 
duh ukisoma ripoti ya MCT na ya Nchimbi --- BIG DIFERENCE
Ya MCT mpaka nimepata shule ya jinsi ya kuandika vitu. Good one.

Watu 3 vs watu 7 akiwamo Jaji....
 
FJM, yapo mengi sana yanyotia uchungu kama kifo cha Mwangosi aliyekuwa anatafuta mkate wa familia.
Yapo yanayoudhi sana na kutia hasira:
1. Kutumia kifo cha Mwangosi kuficha 'wahalifu' wakubwa akina Chagonja, Kamuhanda n.k.
2. Kutumia kifo cha Mwangosi kuficha wahuni wa siasa kama akina Nchimbi
3. Kutumia kifo cha Mwangosi kuudanganya umma
4. Kutumia kifo cha mwangosi kukaa mahali na kutunga uongo

Kinachosikitisha sana ni kuelewa kuwa wapo watu wengi waliohukumiwa na Jaji Ihema. Watu hawa wahawakutendewa haki kwasababu Jaji Ihema ameonyesha uelewa kidogo (in fact kutoelewa) anachokifanya.
Ameandika ripoti ambayo mtoto wa kidato cha sita angeweza kuiandika vizuri zaidi kama insha.

Kinachotia kichefu chefu ni Theophili Makunga, mtu anayedhaniwa kuwa mwandishi na mwenye weledi kukaa pamoja na Jaji Ihema na kutunga upuuzi usiolingana na taaluma yoyote isipokuwa kama ipo ya wapuuzi.

Tunaichambua habari hiyo na tutarejea na kipengele kimoja baada ya kingine ili kuonyesha kuwa hatumtukani wala kumdhalilisha Ihema na Makunga, bali wamejidhalilisha wenye.
The dirty dozen hawa hapa;


The-dirty-dozen.jpg

Mods, naomba kwa mara ya kwanza toka nijiunge na JF nitukane mtu. Walioandika hii ripoti ingefaa wakamatwe mara moja na kufikishwa wanakostahili kwa uwongo na wizi wa kujipatia hela kwa njia ya udanganyifu bila kuifanyia kazi. Hawana tofauti na mlevi aliyeshiba pombe ya pingu na kama ilivyo kawaida kalowa na bila akili anajipitisha pitisha mbele za watu bila kujitambua kuwa anatoa harufu kali ya kunuka hadi hata nzi wanamkwepa. Naapa na nasema wazi kuwa kama moja wa hawa watu angekuwa ndugu yangu, nisingeongea naye tena katika maisha yangu...ni aibu, ni aibu na ni aibu. Halafu moja wao anajiita Jaji na mwingine anajiita Mwandishi, what? Hivi tumemkosea nini Mungu? Naomba niishie hapa!
 
Watanzania kama hatutaiondoa hii CCM madarakani tutakuwa kweli mazuzu. Kilichoandikwa katika hii report ni ukandamizaji wa hali ya juu kwa vyama vya upinzani especially CDM. Damu ya Mwangosi ilimwaga kwa chuki ya Kamuhanda dhidi yake na upinzani kwa ujumla hata mtoto wa miaka miwili akiangalia zile picha ataweza kuelewa. Sasa hawa wazee wanalipwa na kodi zetu kututungia hizi ngonjera wanatoka wapi?
Kwa UDHAIFU huu na uonevu hii serikali yetu imeshindwa kabisa. Hata wazuie vyama vyote vya upinzani tunalazimika kuiondoa madarakani. Ni vyema tukatoka ndani na mapanga, visu, mashami, na silaha zote za jadi tukapigania haki ya kweli ya taifa letu. Yaani hadi inatia aibu. Waziri, jaji, sijui wajumbe gani wanatuandalia ujinga kama huu eti report? Kwani sisi wote ni vipofu? CCM kweli inanuka kabla haijaoza na kumaliza kabisa! Shame on them all! Thay are just dogs for the CCM and its interest!
 
Presidents.jpg

[h=2]Kamati ya Nchimbi imeteleza kutoweka mizani maoni ya CCM/Chadema[/h]Mambo kadhaa ambayo kamati imefanya ni mazuri ingawa riport yao inapokelewa kwa mitazamo tofauti ya kiitikadi. Kwamba wakuu wa mikoa na wilaya wanatumiwa kisiasa kamati hainabudi kuungwa mkono kwani ndio kilio cha mara kwa mara toka vyama vya upinzani nchini, jambo ambalo hata uchaguzi mkuu uliopita taarifa ya waangalizi (observers) toka umoja wa nchi za ulaya walibaini kuwa vyombo vya dola vinaibeba CCM.

Kuna mapungufu kadhaa ya kibinadamu, kiitikadi na kimizani. Jambo ambalo nimeliona limeegemea upande mmoja wa uwazi ni
kuchukua maoni ya Katibu Mkuu mmoja wa Chama cha siasa na kufanya ndio pakuegemea kugeuza sheria ya haki za vyama vya siasa kujijenga na kujitanua kisiasa nchini ili kukuza demokrasia ya vyama vingi.

Jambo moja ambalo naona kamati hii imeteleza ni kwamba, kati ya vyama vikuu viwili vya kisiasa nchini, maoni yamechukuliwa kutoka Katibu Mkuu wa CCM Wilson Mukama na kuyachukulia kama ajenda ya maoni ya kuyafanyia kazi wakati Katibu Mkuu/Mwenyekiti wa Chadema maoni yao kutopewa nafasi katika taarifa yao. Kwa hili hakuna uwiano mzuri katika watu waliowatumia katika uchunguzi huu ajenda hiyo ili ifanyiwe kazi kuitungia sheria ya kusitisha vyama vya siasa kujijenga kisiasa, badala yake kusitisha vyama vya siasa kujitanua na kujijenga, kwa maneno mengine ni sheria inayoandaliwa kuvinyima vyama vya siasa kujijenga na hivyo kuzidi kuweka wigo wa demokrasia kukua nchini.


Chadema kama wahusika wakuu katika tukio lililopeleka kuundwa kamati hiyo na Waziri walitakiwa kupewa nafasi ya kutosha kutoa maoni yao na mapendekezo yao kufikiriwa vya kutosha kwa vile ndio waadhirika kisiasa. Kamati haijawapa nafasi ya kutosha na wala kutoa mwanya wa kuoanisha maoni ya pande zote mbili, yaani ya Mukama wa CCM na Chadema kwa vile Chadema haikupewa nafasi ya kujenga utetezi wake stahiki.

Tungetazamia kamati ingetoa mapendekezo ya Katibu Mkuu au Mwenyekiti wa CCM ni haya na Katibu Mkuu au Mwenyekiti wa Chadema mapendekezo yao ni haya. Kutokana na mapendekezo yao hayo kamati inaridhia mapendekezo kadhaa kutoka kwao yafanyiwe kazi baada ya kuwianisha na kupima uzito stahiki kutoka pande zote. Lakini ni pendekezo kutoka upande mmoja na hivyo kutoweka mizani stahiki katika uwanja wa siasa kuleta usawa katika demokrasia kukua nchini.

Kinachoonekana katika taarifa ya kamati hii ni kama Chadema imeshtakiwa na kuhukumiwa badala ya kuwapa nafasi na haki ya kushirikishwa katika uchunguzi huo na maoni yao kupata uzito stahiki, ingawa kwa kiasi fulani imeonyesha dhahiri katika taarifa wazi kuwa ni Mikutano ya Chadema tu ndiyo inayoonekana kwa mawe na Polisi kwa kuwa na nguvu kubwa isiyo ya kawaida ambapo hakuna kesi hata moja ambayo inaonekana Polisi kutumia nguvu katika mikutano ya CCM.


Chadema haijaonyeshwa moja kwa moja katika taarifa ya uchunguzi kutoa mchango wao au mmoja wa viongozi wa Juu kitaifa kushirikishwa kama Katibu Mkuu wa CCM Mukama alivyoshirikishwa, hapa kuna kuteleza kidogo kwa kamati hii. Athari yake ni kama ifuatavyo:

  • Maoni ya Mukama ambaye ni Katibu Mkuu CCM kwamba mikutano ya siasa isitishwe baada ya uchaguzi mkuu na siasa zihamie bungeni jambo ambalo kisiasa linaipa nguvu CCM kwa vile imeshajijenga na vyama vingine vya siasa kukosa nguvu na nafasi ya kujijenga na kujitanua.
  • Kamati kwa kuegemea hoja ya Mukama pekee inaonyesha dosari ambayo hata mazuri mengie ambayo yamefanyika yataonekana kutopokeleka vizuri na vyama vya upinzani kwa sababu hoja ya CCM ambayo imeshajijenga imepenyezwa na kukubaliwa na kamati hii ambayo imeundwa na waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi.
  • Vyama vya upinzani kunyimwa uhuru wa kujijenga, kujiendeza na kuuza sera zao kwa wananchi.

Hali hii imetokana na kamati iliyoundwa kutokuwa na mizani ya uwiano kwa vile imeundwa na kioogozi mwandamizi serikalini ambaye katika hoja iliyotokea Nyororo-Iringa ni mmoja wapo ambaye anabeba lawama za uwajibikaji. Mazingira kama hayo yanaonyesha kamati kutokuwa huru katika uchunguzi wake kwa vile imeundwa na chombo kile kile ambacho kimehusika katika kashfa ya mauaji hayo.
 
Bomu la kishindo lililomua Mwangosi RIP,
Sio la machozi, hili tuasaidianeWana jf ndio gani hili.
Kwa lugha za watengenezaji linaitwaje na properties zake zipoje. Nakiri sijawahi kulisikia
 
Back
Top Bottom