Ripoti ya Kifo cha Mwangosi

Ripoti ya Kifo cha Mwangosi

Wadau tuipitie ripoti yote kuhusu kifo cha Daudi mwangosi iliyowasilishwa hapo jana na timu maalumu ya uchunguzi kwa Baraza la Habari Tanzana na kisha tuilinganishe na ripoti ya kamati ya Nchimbi. wana JF mwenye ripoti kamili ya Kamati ya Nchimbi anaombwa aiwakilishe tuijadili.
 
Nimepitia ripoti ya kamati iliyoundwa na Mheshimiwa Nchimbi, sijaona mahali ilipoandikwa kwamba Polisi hawakuhusika na kifo cha Daudi Mwangosi. Lakini kauli kwamba Polisi hawakuhusika ilitolewa na aliyekuwa mwenyekiti wa Kamati hiyo Jaji Steven Ihema kwenye mkutano na wanahabari jana. Kauli hiyo imepamba kurasa za mbele za magazeti ya leo, pia ilinukuliwa na runinga na radio mbalimbali.

Baadhi ya vipengele vilivyo kwenye ripoti hiyo ni kama hivi hapa chini

Upelelezi wa awali pamoja na picha za mnato unaonyesha kwamba marehemu alikuwa amemkumbatia Mkuu wa Polisi Kituo cha Mafinga ASP Assel Mwampamba na huku akiwa amezungukwa na Askari Polisi wasiopungua sita ambao licha ya kumzunguka marehemu Daud Mwangosi kuna madai yaliyotolewa na mwandishi wa Habari Joseph Senga kwamba, Askari Polisi hao walikuwa wanamshambulia marehemu kwa kumpiga, ndipo askari mmoja aliyetambuliwa kuwa ni G 2573 PC Pasificus Cleophace Simon alifyatua Bomu la kishindo na kusababisha kifo cha Daud Mwangosi.



Katika tukio la kwanza idadi ya Askari walioshiriki ni Sekisheni tatu ambapo ni askari wasiozidi thelathini. Kwa maelezo yaliyotolewa na Mwandishi wa Habari mbele ya Kamati, Bw Joseph Senga anaeleza kuwa watu walishatawanyika na hali kutulia mara baada ya Operesheni hii kukamilika na Polisi kujiandaa kuondoka kwenye eneo la tukio. Tukio la mauaji ya Daud Mwangosi lilisababishwa na kupigwa bomu la kishindo.



-Hapakuwa na uwiano wa Bomu na tukio la mauaji, kwa vile utaratibu wa matumizi ya bomu hilo unaelekeza kulenga juu usawa wa nyuzi 45 na umbali mita 80 mpaka mita 100.

-Hapakuwa na uhalali wa kutumia Bomu la Kishindo kwani lengo la ulipuaji wake ni ili watu waogope na kukimbia.

- Hapakuwepo umuhimu wa kutumia Bomu la Kishindo kwa sababu hata ingekuwa ukamataji tayari Askari Polisi wapatao sita walikuwepo eneo la tukio.



Lakini hitimisho hili nalo lina utata

Kwa misingi hiyo Kamati imeona kwamba nguvu iliyotumika mwanzo hadi kumaliza Operesheni haikuwa kubwa. Kuhusu tukio la kuuawa Bw. Daud Mwangosi na kuumizwa baadhi ya Askari Polisi halikustahili kabisa.


Vinginevyo hiyo ripoti ni nzuri sana, iko balanced na imeweka mambo yote bayana. Angekuwa ameisoma asingesababisha mivutano inayoendelea na hasa wananchi kuona kwamba Kamati imeibeba serikali

Likewise, Emmanuel Nchimbi aliisoma kabla?
 
kwa kifupi ripoti ya jaji IHEMA initia kinyaa, inasikitisha, imejigeuza msemaji wa Kamanda wa polisi mkoa Iringa.
 
that is totally lies , the police force use disproportional force , we saw them bradishing pistol on the air.
 
Hii sio ripoti ila ni collection ya stories ambazo ni biased.I doubt credibility ya hii team
 
Asante kwa ripoti lkn mhhh! mi naamini zaidi nilichokiona kwenye kipindi kilichorushwa na mlimani tv. kwa sababu nchi hii mabingwa wa kuchakachua, hivyo sina imani na ripoti hiyo, labda wanatume wangekuwa hawana uhusiano kabisa na ze gambaz ningeamini.
 
Lakini kwa polisi au kwa Nchimbi hiyo ripoti ni nzuri sana!
 
Gurudumu nimesikitishwa na conclusion yako kwamba ripoti iko balanced! Hilo zuio la mikutano ya siasa lilihusu CHADEMA peke yake au na vyama vingine? Pia unazungumziaje kwamba mkutano wa chadema haukuwa wa hadhara ulikuwa ni mkutano wa ndani, ambao hata CCM walikuwa wanaendelea na mikutano yao sehemu mbalimbali nchini? This is not a report it is rubish for Nchimbi consumption, Nchimbi was right to say the report was not for public consumption! Shame on this government.
 
Last edited by a moderator:
n00b mbona kama naona report mbili ya kamati ya Nchimbi na hiyo ya MCT?????
 
Last edited by a moderator:
Wadau tuipitie ripoti yote kuhusu kifo cha Daudi mwangosi iliyowasilishwa hapo jana na timu maalumu ya uchunguzi kwa Baraza la Habari Tanzana na kisha tuilinganishe na ripoti ya kamati ya Nchimbi. wana JF mwenye ripoti kamili ya Kamati ya Nchimbi anaombwa aiwakilishe tuijadili.

Sijapata muda wa kufanya analysis lakini report ya Nchimbi iko biased na lengo lake ni kuwasafisha polisi, serikali na ccm.

Nimesikia ITV akibabaika.

Report ya Wanahabari nayo inaubinafsi mbaya. Tangu kuuawa kwa Mwangosi wamekuwa wakionyesha kuwalaumu polisi kwa kuua mwandishi wa habari akiwa kazini.

Swali ni kwamba, kwa nini polisi wanauwa watu ovyo na kusingizia eti chanzo chadema. Chadema wasingefanya mkutano polisi wasingeua.

INALETA MAANA YOYOTE KWELI KWA POLISI KUUA MTU HATA KAMA NI MHALIFU AMBAYE HANA SILAHA, TAYARI YUKO CHINI YA UDHIBITI WAKE NA HANA UHATARISHI WOWOTE KWA USALAMA WA HAO WAKAMATAJI HATA KAMA SI MWANDISHI WA HABARI?

KWA NINI WASIMKAMATE MWANGOSI NA WOTE WANAOSHIRIKI MIKUTANO YA CHADEMA KISHA WAWAPELEKE MAHAKAMANI BADALA YA KUWAHUKUMU KIFO?

Report ya Nchimbi haijagusia mikusanyiko mingine iliyofanyika wakati huo hapa nchini ambayo si ya CHADEMA.

MAONI YA kamati yamelaumu CHADEMA ETI WAFUNDISHWE SIJUI N INI NINI hakuna hata kukemea wala kulaani mauaji ya raia wasiyo hatia katika nchi yao!.

NILIJUA TU NCHIMBI ALIPOKIMBILIA KUUNDA TUME NA KUMPELEKA YULE KIJANA POLISI MAHAKAMANI ILIKUWA NI MKAKATI WA KUTUMIA UJINGA WA WA TANZANIA KUUA SOO NA KUWALINDA WAHUSIKA WAKUU.

SERIKALI SHAME ON YOU!
 
nchimbi kachakachua ripoti ya kamati yake wenye akili timamu tumeopt kwenye ripoti ya MCT!!!!!!!!!!!
 
Judge Manento ambaye ni mkurugenzi wa tume haki za binadamu na utawala bora katika ripoti ya tume hiyo kuhusu mauaji ya Mwangosi ,tume hiyo imeeleza bila kutafuna maneno kuwa polisi walifanya ukatili mkubwa!

Haaya sasa kazi ndo imeanza!vyombo vya serikali vinapingana!
 
Tunaweza kuisoma hiyo report?JK nchi ilishamshinda naona anaogopa kurudia yale ya Zombe;Kamuhanda ilikuwa saizi yake kabisa
 
Of course.. baada ya kuwasema na hawa ila pia na caliber ya watu wenyewe; Jaji Manento ni miongoni mwa watetezi wakubwa wa haki za raia. Tusubiri waiweke hadharani halafu tuone watu wote walikuwa wanaangalia the same facts halafu wanafikia mahitimisho tofauti kabisa kama mchana na usiku. Of course.. hii ni tume ambayo imeundwa kikatiba na inalindwa kisheria na hivyo maoni yake yana uzito mkubwa zaidi kuliko ya Tume ya Uchimvi.
 
Ripoti ya Nchimbi inaonekana ni ya kupikwa. Imehoji zaidi wahusika wa Tukio kama akina Kamhanda, IGP, na ukiangalia katibu wa Kamati ni Polisi. What should we expect here???
Pili, kuna matukio kama mahojiano kati by RPC na Cdm hawajaonesha kama MCT walivyofanya. Kwa ujumla wamejichanganya zaidi. Walau repot ya MCT inatia matumaini japo ni vigumu kuitekeleza.
 
jaman mimi riport ya kumtesa ulimboka ckuipata,au bado haikutolewa? naomba aliyenayo anisaidie ili nami nifahamu aliyemteka
 
Mtafutaukweli1, ukweli unao wewe, mbona unazunguka mbuyu ndugu?
Unaonekana umekuja mwezi huu wa septemba, na unategemea kupata ukweli leo?
 
riport imejibu kile kilichoitwa hadidu za rejea, lakini haikujibu na wala kutoa mwelekeo wa kulaani na hatimaye kumfikisha mbele ya haki muuaji, sasa umefika mwakati tume ikiundwa iwe huru na si kupangiwa cha kufanya kwa kufumba eti ni" hadidu za rejea" kwa utaratibu huu tume haikuwa huru ndo maana imetoa riport ambayo haija toa ukweli wa nani alihusika na maauaji.
 
Ripoti ya Kamati ya Nchimbi--Mbona kama imeandaliwa na kitengo cha propaganda cha CCM?
 
Back
Top Bottom