Regia Mtema is No More!

Regia Mtema is No More!

Status
Not open for further replies.
Who am i to question the wills of GOD! R. I. P, our beloved and strong MP - Regia Mtema.
 
This is her last comment on facebook 19hours ago,...
alikuwa akimpongeza pacha wake Remija Mtema.

Congrats love.You have my Prayers!
,....

Regia,
Ume pigana vita vikamilifu.
Haukuangalia ulemavu wako,ulifanya kila ulilo ona linafaa sawa
na muongozo ndani ya moyo wako.

Maisha yetu hapa duniani ni maandalizi ya maisha ya baadae.
Naimani Mungu asingeruhusu uondoke kama ungekuwa hauja maliza
kazi aliyo kutuma kuifanya hapa duniani.

Ni wakati mgumu sana wanao ndugu zako,wazazi na hata marafiki pia.
Upumzike kwa amani,naamini tutaonana siku moja baada ya
hukumu ya Mungu.
 
Mungu nisamehe kwa ninachokiandika ila kuna wengi tunaowaita "Weaked one's" ungepaswa kuwachukua watu ambao hawaitendei mema Tanzania yako lakini kwa nini huyu ambaye mbele ya macho ya wengi ni "Righteous one" ndo umetuchukulia hebu tupe moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu ili tuweze kuona makusudio yako.
 
Poleni wana CDM wote popote pale mlipo,poleni wana Jf kwa sisi tuliokuwa tukimfahamu vyema Dada Regia,poleni ndugu na jamaa,lakini pia nichukue nafasi hii kuwapa pole viongozi wakuu wa CDM

Mh Dr,Slaa
Mh Mbowe
Mh Zitto
Mh Mnyika
Mh Tundulisu
na viongozi waandamizi wote wa CDM kuwa tumeondokewa na mtu ambaye alikuwa ni mpiganaji na mwenye kujitoa kwa khali ma mali.
na kumbuka mala ya mwisho ni hivi karibuni alileta thread yake kukusanya maoni na shida za Wtz
nashindwa kujizuia lakini ndivyo ilivyo CHEMA HUWA HAKIDUMU

tuwe wavumilivu ktk kipindi hiki kigumu tulichonacho

Ndugu zangu wa kilombero,paLe Ruha,kidogo basi,kihelezo,kidodi,mang'ura,kwa bibi,mkamba,ifakara,lupiro, tunasema hii ni kazi ya mungu haina makosa,tupo pamoja ktk msiba huu mzito

ee mungu hatukulaumu lakini ungetupa mda nae,kwani umemchukua kipindi tukiwa tunamhitaji mmmmh
 
Kwa nini?Watu wema na waadilifu wanakufa?Yangekufa yale mafisi ya ahadi hata 10,kwangu Regia ameniuma sana.Namfahamu tangu anasoma Kibasila sec(TEWW),maskini na ulemavu wake!!! Dah!Nimebaha sana.
 
imekuwa hivi miaka yote kuwa mtu akishatutoka kila mmoja wetu hujitahidi awezavyo kutoa sifa hata asizokuwa nazo marehemu lakini sio kwa Regia!
Tuko zaidi ya watanzania 45m lakini ni wachache sana miongoni mwetu walioweza kujitokeza hadi sasa na kuishi maisha halisi na kujieleza kwa uhalisia wao kama Regia.
Pale tulipokuwa tumeanza kuwa na matumaini ya ukombozi wa kweli hatimaye pamepata pigo!
Sijui hata jinsi ya kuuleza msiba huu!
[
QUOTE=Mr.Professional;3135264]Habari hii nimejaribu kuilazimisha kuwa uongo lakini nimeshindwa na nimeamua kukubaliana na hali halisi kwamba hatuna tena KAMANDA anayeitwa REGIA DOTTO MTEMA sisi tulimpenda ila Mungu wetu amempenda zaidi.

Hii imenifanya nikumbuke maneno ya kwenye vitabu vitakatifu kuwa " Mwanadamu ni mavumbi na mavumbini atarudi", pia " Mwanadamu hataishi katika fahari yake milele naye atakufa tu na kuiacha fahari yake"

Raha ya milele umpe Ee Bwana, na Mwanga wa milele umwangazie. Ampumzike kwa amani. Amen[/QUOTE]
 
Kwa michango hii nithubutu tu kusema inawezekana ni kweli , Basi watz, tuseme INAILAHI WAINAILAH RAJIUUN (Kwa mwenyezi Mungu sisi wote tutarejea). Ni mda tu ndo utakaosema, ila binadamu huwatunapenda kuuliza kwanini huyu na si mwingine, tuvute subra atatokea kamanda mwingine anayefanania naye. Na kwavile tumeumbwa kusahau pia, basi inatubidi tusahau. Pole TZ, CDM, wanaJF, familia (pacha wake), na wanakilombero woote.
 
...Regina tulikupenda laki Munga amekupenda zaidi,umetangulia mbele ya haki na sisi tunakufuata.Igawa umetutoka mengi ulifanya na yatabaki na-kuishimilele...Mungu tunakuomba uwape moyo wa uvumili ndugu,jamaa,marafiki,viongozi na wanachama wote wa CHADEMA...Bwana ametoa na Bwana ametwaa,jina la Bwana na lihidimiwe...
 
Regia%2BMtema.JPG
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom