Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Saa ya ukutani ya bwana khalifa iliishiwa betri kisha ikawa haifanyi kazi.Khalifa alitoa betri zilizokwisha na kuweka mpya kwenye hiyo saa,kisha ikaanza kufanya kazi.Lakini saa ya khalifa ilishapoteza majira!,khalifa hana redio,tv wala jirani yeyote wa karibu,anaishi peke yake kama jangwani.Alichofanya bwana khalifa ni kwenda kwa rafiki yake anayeishi kilometa 10 kutoka kwake ambaye pia ana saa.Alipofika kwa rafiki yake,alikaa kwa masaa 10 kisha akaanza safari kurudi kwake.Alipofika nyumbani kwake,aliweza kurekebisha muda wa saa yake.Je,aliwezaje/alitumia mbinu gani kurekebisha muda?