RC Kagera: Naagiza Wabeba Mizigo Bandari ya Bukoba walipwe, Mkurugenzi aje na fedha, asipokuja nazo nitamuweka ndani

RC Kagera: Naagiza Wabeba Mizigo Bandari ya Bukoba walipwe, Mkurugenzi aje na fedha, asipokuja nazo nitamuweka ndani

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
3,177
Reaction score
7,472
Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Fatma Mwassa ameipa siku mbili Kampuni ya IFS Consulting Limited ambayo ilipewa tenda na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ya kupakia na kushusha mizigo, kuwalipa fedha wabeba mizigo malipo yao wanayodai ya wiki Tisa katika Bandari ya Bukoba

Hatua hiyo imefikiwa baada ya mgomo uliofanywa na Wabeba Mizigo hao, jana Asubuhi Juni 23, 2025 ikidaiwa kuwa wanadai jumla ya kiasi cha Tsh Milioni 18.

Akizungumzia hali hiyo awali, Meneja IFS Consulting Limited Kagera, Godfrey Ismail amesema “Changamoto ni stahiki za Wafanyakazi wetu kudai fedha zao, tunaendelea kupambana, mpaka sasa tumefanikiwa kupata Sh Milioni 6.”

Baada ya maelekezo ya Mkuu wa Mkoa, wabeba mizigo hao wameendelea na kazi wakiisubiri, Jumatano Juni 25, 2025 kujua kitakachotokea.

Ilivyokuwa awali ~ wafanyakazi Wanaobeba mizigo Bandari ya Bukoba wafanya mgomo wakidai malipo yao

Chanzo: Azam TV
 
Mbona haja solve? Kumuweka mtu ndani kutafanya hao jamaa walipwe?
 
Sasa kama hana hela huyo mkandarasi, akifungwa ndiyo atazipata? Hela za mkandarasi zimeliwa na wale wote walioshiriki ktk mchakato wa kuanzisha, kupitisha na kuidhinisha mradi huo.
 
Back
Top Bottom