RC Abubakar Kunenge: Simu Janja na TV zinazalishwa Pwani na zipo sokoni

RC Abubakar Kunenge: Simu Janja na TV zinazalishwa Pwani na zipo sokoni

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
3,177
Reaction score
7,472

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema "Rais Samia aliagiza simu zitengenezwe Tanzania na sasa hivi simu janja zinazalishwa hapa Pwani na sasa zipo sokoni."

Akizungumza leo Julai 31, 2025, katika hafla ya uzinduzi wa Bandari Kavu ya Kwala, Kibaha mkoani Pwani, Kunenge ameeleza kuwa idadi ya viwanda katika mkoa huo imeongezeka kutoka 1,387 kabla ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan hadi kufikia viwanda 1,681, huku viwanda vikubwa vikiongezeka kutoka 59 hadi 97.

Ameongeza kuwa viwanda hivyo vimezalisha zaidi ya ajira 21,000 za moja kwa moja, na zaidi ya ajira 60,000 zisizo za moja kwa moja, huku bidhaa mbalimbali zikiendelea kuzalishwa kwa wingi.
 
Tunafanya tu assembly au tunatengeneza kabisa brand yetu. Kiwanda kinachozalisha hizo simu kinaitwaje? Na hizo simu zenyewe zinaitwaje? Bei yake ikoje?

29847463sie (764).jpeg
 
Picha na majina ya simu tafadhali
 
Toothpick mnaagiza toka china leo ndiyo mtengeneze smartphone na tusijue? Kama ni ku assemble sawa lakini siyo ku manufacture.
 
Hizi simu ufanisi wake wa kazi utakua wa mashaka mashaka kama ambavo mkuu wa mkoa alivotoa taarifa kwa mashaka mashaka...kashindwa taja aina ya simu na tv pia
 
Aache Uchawa
Simu nyingi tu zinazalishwa kibaha under licence!
Hata tv & fridge zinazalishwa kibaha mkuu,ninayotumia ni mali ya kibaha,tz.
Kwa msiofahamu mali nyingi hutoka kibaha na somewhere bunju kuja kariakoo!
Hili ni jema sana hata viatu pia na simple shoes pia!
 
Simu nyingi tu zinazalishwa kibaha under licence!
Hata tv & fridge zinazalishwa kibaha mkuu,ninayotumia ni mali ya kibaha,tz.
Kwa msiofahamu mali nyingi hutoka kibaha na somewhere bunju kuja kariakoo!
Simu gani hio
 
Simu nyingi tu zinazalishwa kibaha under licence!
Hata tv & fridge zinazalishwa kibaha mkuu,ninayotumia ni mali ya kibaha,tz.
Kwa msiofahamu mali nyingi hutoka kibaha na somewhere bunju kuja kariakoo!
Hili ni jema sana hata viatu pia na simple shoes pia!
Simu zipi hizo
 
Back
Top Bottom