Ratiba ya mapokezi ya Lema kesho Arusha!

Ratiba ya mapokezi ya Lema kesho Arusha!

Hapana Mkuu, Ninajiandaa kuelekea Abbeysinia (Ethiopia) baadae leo. Nimekumbuka chakula chao "Njera" hiyo ndio pilau yangu kwa mwaka huu shemeji.....Ila katika maandalizi ya kuupokea mwaka mpya(New Year Eve)nitakuwa nyumbani.

[QUOTE=Mwita Maranya;5278244]Mkuu Thanda utakuwepo kwenye mapokezi kesho?[/QUOTE]
 
Arusha sasa kumekucha. Palikuwa pamepoa sana baada ya Lema kuvuliwa ubunge.Mhe PM Pinda ajiandae kujibu hoja za mh Lema kuhusu mauaji ya Arusha. RC Arusha aliwahi kudai kuwa bila Lema watu wa Arusha hawamsumbui.Tulimkosa sana Mbunge wetu.Kiongozi wetu tuliyemchagua kwa kura zetu karudi.
 
Huwezi kusema haina gharama. Kuna wabunge na viongozi wa chama wanasafiri kutoka Dar mpaka Arusha. Kuna gharama za malazi na chakula. Kuna helikopta na magari, hapo kuna gharama za mafuta, services, kulipa madereva etc. Kuna gharama za vyombo vya sauti siku ya mkutano and all that. Hata kama ni pesa yao mfukoni, haina maana, kwa sababu haya yote yanafanywa kwenye jimbo ambalo hata kesho asubuhi uchaguzi ukifanyika chadema itashinda. Huoni kama ni waste of resources?

Wabunge wamejitolea kulipia magari yao na helikopta zao, malazi, service za magari, chakula na madereva wao. Wananchi wanachanga kufanikisha mkutano. Lengo ni kuhamasisha Tanzania nzima na sio jimbo la Arusha mjini peke yake. Macho na masikio ya Watanzania wengi sana kwa siku ya leo yatakuwa Arusha. Kuna kura nyingi sana zitapatikana leo nchi nzima kwa mambo yatakayofanyika jijini Arusha. We are gaining political momentum.

Waste of resources ni pale unapohonga watu wakafungue kesi za usumbufu zisizo na mbele wala nyuma. Kupoteza hela za walipa kodi kwa mahakamani kuendesha kesi ambazo kwa makusudi kabisa zimefunguliwa kujaribu kuwa keep wabunge wa CHADEMA busy wasiweze kufanya kazi yao vizuri bungeni.
 
Kuhusu mungu, dini na imani.. Elewa misingi ya kutochanganya siasa na dini. Leo hii ukiulizwa CHADEMA ni dini gani au inabudu mungu yupi, jibu ni kwamba haina dini wala mungu. Kuna wanachama wa imani tofauti na kuna wasioamini mungu.

Unaelewa kwamba sasa hivi kuna mazingira na harufu ya udini. Mfano ni majibizano na michango ya members hapa. Sasa kama CHADEMA inashutumiwa kuwa chama cha kikristu na wewe unasema "tulianza na mungu, tunamaliza na mungu" .. Hii slogan itatafsirika vipi?

Siasa na dini/mungu havichanganywi. Dini/mungu, that's your personal thing.

Mungu hana dini. Binadamu ndio tuna dini.
 
TBC 1 watarusha matangazo hayo kama walivyofanya kwa CCM na CUF? Wengine tunataka tuone kupitia kwenye luninga yetu ya Taifa..!
 
aghalabu hata mwanao nyumbani akifanya vizuri anahitaji pongezi,gharama kitu gani mbona fedha tunakufa tunaziacha
 
Hii yote itagharimu kiasi gani?

He has won the case, maisha yaendelee.

Hizi sarakasi za mapokezi na maonyesho itatofautisha vipi CHADEMA na CCM.

Nilidhania watu watashauri gharama, fedha na resource hizo zipelekwe somewhere else. Arusha tayari ngome yenu. Pelekeni hizo nguvu sehemu nyingine.

Mnawapa maadui wenu points rahisi sana. Kesho UHURU likiandika "Mbowe na Lema wachoma mabilioni ya chama kusheherekea ushindi" mtashangaa?

Washabiki wa CHADEMA wana hatari ya kukiua chama chao zaidi hata ya CCM. Kwa mfano baadhi ya washabiki wengi wanapenda slogan ya "tumeanza na mungu, tumemaliza na mungu". Kwenye siasa kuna mungu? Jifunzeni kutenganisha siasa na mungu.

Katika mazingira haya ya udini ukisema "umeanza na mungu, umemaliza na mungu" ni waislam wangapi watakua tayari kuwa wanachama? Wao si watahoji Allah yupo wapi? Wahindi nao? Wasio na dini je? Chama hakina dini, mwacheni mungu wenu huko huko. Hapa shabikieni itikadi na sera za chama.
ndugu yangu wewe huijui Arusha.hizo helkopter,magari,pikipiki ni mali ya watu binafsi!havijakodiwa na hela za chama kama wafanyavyo ccm.CDM watu hujitoa mwanzo mwisho.hawahitaji kubebwa,kula pilao,kugawiwa kanga,T.shirt,kofia wala tsh.2000/-usifananishe cdm na ccm ya J.KIKWETE.
 
karibuni Philips kushaanza kupendeza mambo mwanjamwanja!
 
Lakin ukifatilia siasa ya marekani huwa wanasiasa hupenda kusema god blees usa vile vile hata wakati wa kudai uhuru kusin mwa afrca weng walimtanguliza mungu
 
Kuhusu mungu, dini na imani.. Elewa misingi ya kutochanganya siasa na dini. Leo hii ukiulizwa CHADEMA ni dini gani au inabudu mungu yupi, jibu ni kwamba haina dini wala mungu. Kuna wanachama wa imani tofauti na kuna wasioamini mungu.

Unaelewa kwamba sasa hivi kuna mazingira na harufu ya udini. Mfano ni majibizano na michango ya members hapa. Sasa kama CHADEMA inashutumiwa kuwa chama cha kikristu na wewe unasema “tulianza na mungu, tunamaliza na mungu” .. Hii slogan itatafsirika vipi?

Siasa na dini/mungu havichanganywi. Dini/mungu, that’s your personal thing.
Acha upopompo wewe.
Wanachama wa cdm wana imani zao na ndio wanaosema hivy, siyo katiba ya chama!! tumia common sense.

Mwislamu anayekipenda Chadema ruksa kusema -Tulianza na Allah, tutamaliza na Allah! na Mhindi nae ruksa kutaja anachoamini...lakini general term ni MUNGU.!

Wewe uko overSensive na dini wewe, na watu wa aina yako ndiyo wanaovuruga nchi hii. Tuache tafsir fyongo.
 
Mkuu hapo kwenye RED, hatuwezi kumpigania MUNGU, hatuna uwezo huo, lakini MUNGU ndiye anayetupigania, sisi tu viumbe dhaifu sana kwa CCM kiasi kwamba bila MUNGU kuwa kati yetu, hatuwezi chochote.
MUNGU atakuwa nasi daima hadi hapo ukombozi wa nchi hii utakapokamilika 2015
well said mkuu
 
Ratiba ya Lema Kesho:

Mapokezi KIA kuanzia Philips saa 2:00 Asubuh

Kwenda kufungua ofisi ya Mbunge kuanzia saa 5:00 Asubuhi

Ukaguzi wa Barabara Zilizojengwa kuanzia saa 6:00 Mchana

Kusalimia akina mama waliomuombea sokoni 7:00 Mchana

Mkutano Kilombero saa 8:00 Mchana

WOOTE MNAKARIBISHWA!

Msafara utakuwa unaongozwa na Wabunge wa Chadema toka Dar es salaam na utahutubiwa na viongozi wa Kitaifa. Msafara huo pia utaongozwa na Helkopta, pikipiki, magari, baiskeli na watembea kwa miguu, maandamano yataanzia Philips hadi ofisi za Mbunge kuelekea viwanja vya kilombero!

Peeoplesssssss!

Tupo pamoja kwa sana.
 
Hiyo ratiba ya kwenda kuwasalimia akina Mama wa soko la NMC itakuwa ya Hisia kali sana, wallahi nasema kuna watu hapo watalia machozi ya damu.

Hawa akina mama kwa mamia ni watu walioteseka sana kwa shuruba za polisi na wagambo wa ccm.

Wamekimbia sana wanawake hawa, wameumizwa, wamepoteza fedha na jewellery, kisa kuwakwepa wagambo wanaowatimua huku wakiwa wamebeba vichwani bidhaa zao.

Akina mama hawa bila kujali kupoteza muda, bila kujali nini kingewatokea, bila kujali dini zao, makabila, ukanda, asili, wala umri, walikusanyika kupiga MAOMBI YA AJABU pale NMc, wakimsihi Mungu atawalaye, asimamie hukumu ya G.Lema ili isiingiliwe na maamuzi ya akili za kibinadamu.

Imagine katika mazingira kama hayo, huyo m'baba kesho anafika eneo hilo kwaajili ya KuWASALIMIA TUakina mama hao.

Ni kipengele kipengele kitakachokuwa na mvuto ajabu.

Ndg yangu hayo matukio dhidi ya wanyonge yatupe nguvu ya kuwaondea hawa wakoloni weusi
 
hongeren akina mama kwa kazi nzuri ya maombi.ama kweli mungu hutenda haki daima dumu,ar twaomba muongozwe na utulivu na hekima, jaman twendeni na singida tukashambulie ule mkoa bdo una kijani kisichokuwa na mafanikio.hasa kwa kale kafisadi kanakoibukia iramba magharibi.kabla hakajaweka mizizi pale,mana kanatuogopesha kwa wake zetu na mabinti zetu,
 
Mkuu hapo kwenye RED, hatuwezi kumpigania MUNGU, hatuna uwezo huo, lakini MUNGU ndiye anayetupigania, sisi tu viumbe dhaifu sana kwa CCM kiasi kwamba bila MUNGU kuwa kati yetu, hatuwezi chochote.
MUNGU atakuwa nasi daima hadi hapo ukombozi wa nchi hii utakapokamilika 2015

Mkuu, natumia simu tu. Ningekugongea like! Pokea hii like ya text!
 
Back
Top Bottom