Hiyo ratiba ya kwenda kuwasalimia akina Mama wa soko la NMC itakuwa ya Hisia kali sana, wallahi nasema kuna watu hapo watalia machozi ya damu.
Hawa akina mama kwa mamia ni watu walioteseka sana kwa shuruba za polisi na wagambo wa ccm.
Wamekimbia sana wanawake hawa, wameumizwa, wamepoteza fedha na jewellery, kisa kuwakwepa wagambo wanaowatimua huku wakiwa wamebeba vichwani bidhaa zao.
Akina mama hawa bila kujali kupoteza muda, bila kujali nini kingewatokea, bila kujali dini zao, makabila, ukanda, asili, wala umri, walikusanyika kupiga MAOMBI YA AJABU pale NMc, wakimsihi Mungu atawalaye, asimamie hukumu ya G.Lema ili isiingiliwe na maamuzi ya akili za kibinadamu.
Imagine katika mazingira kama hayo, huyo m'baba kesho anafika eneo hilo kwaajili ya KuWASALIMIA TUakina mama hao.
Ni kipengele kipengele kitakachokuwa na mvuto ajabu.