Hii yote itagharimu kiasi gani?
He has won the case, maisha yaendelee.
Hizi sarakasi za mapokezi na maonyesho itatofautisha vipi CHADEMA na CCM.
Nilidhania watu watashauri gharama, fedha na resource hizo zipelekwe somewhere else. Arusha tayari ngome yenu. Pelekeni hizo nguvu sehemu nyingine.
Mnawapa maadui wenu points rahisi sana. Kesho UHURU likiandika "Mbowe na Lema wachoma mabilioni ya chama kusheherekea ushindi" mtashangaa?
Washabiki wa CHADEMA wana hatari ya kukiua chama chao zaidi hata ya CCM. Kwa mfano baadhi ya washabiki wengi wanapenda slogan ya "tumeanza na mungu, tumemaliza na mungu". Kwenye siasa kuna mungu? Jifunzeni kutenganisha siasa na mungu.
Katika mazingira haya ya udini ukisema "umeanza na mungu, umemaliza na mungu" ni waislam wangapi watakua tayari kuwa wanachama? Wao si watahoji Allah yupo wapi? Wahindi nao? Wasio na dini je? Chama hakina dini, mwacheni mungu wenu huko huko. Hapa shabikieni itikadi na sera za chama.