Patriot
JF-Expert Member
- Feb 11, 2008
- 5,698
- 4,693
Nimemsikiliza waziri wa elimu akisisitiza kwamba sera mpya inatimiza matakwa ya rais. Sasa hapo ndo mwanzo wa ujinga wetu. Rais siyo mtaalamu wa elimu. Sera siyo ya rais, kwa nini sera mpya iwe inayotoa majawabu kwa rais?
Sera hii kama itapitishwa kama kawaida yetu kwa vision ndogo ya aina hii, ni sawa na kilimo cha Waziri Bashe.
Mitaala yetu haina tatizo, tatizo ni ufundishaji. HUwezi kutegemea waalimu wanaonyanyasika kukufundishia watoto wako. Pesa zote zinapelekwa kwenye siasa. Ktk kila kijiji leo hii tuna wanasiasa wengi kuliko waalimu na madaktari, halafu unategemea sera iinue elimu. Tuache hadithi za akina KIshimba Bungeni. Elimu ina misingi yake na haitrakiwi kuwa ni komedi za bungeni ndo zitunge sera na mitaala.
Nimeisoma rasimu, inasikitisha. Ni sera inayoleta makundi nchini; watakaosoma kwa Kiswahili na wale watakaosoma kwa kiingereza. Uhakika ni kwamba wao, hawa viongozi, watasomesha watoto wao kwa kiingereza. Je, nani wanamtungia elimu kwa Kiswahili?
Ni kwa nini hatukusema iwe ni Kiswahili kila mtu? Kwa sababu viongozi wetu wanaamini kiingereza kwa watoto wao ni bora zaidi. Kwa kuogopa hadithi za kisiasa wameamua kutunga mifumo miwili. Huu ni ujinga.
Sera hii kama itapitishwa kama kawaida yetu kwa vision ndogo ya aina hii, ni sawa na kilimo cha Waziri Bashe.
Mitaala yetu haina tatizo, tatizo ni ufundishaji. HUwezi kutegemea waalimu wanaonyanyasika kukufundishia watoto wako. Pesa zote zinapelekwa kwenye siasa. Ktk kila kijiji leo hii tuna wanasiasa wengi kuliko waalimu na madaktari, halafu unategemea sera iinue elimu. Tuache hadithi za akina KIshimba Bungeni. Elimu ina misingi yake na haitrakiwi kuwa ni komedi za bungeni ndo zitunge sera na mitaala.
Nimeisoma rasimu, inasikitisha. Ni sera inayoleta makundi nchini; watakaosoma kwa Kiswahili na wale watakaosoma kwa kiingereza. Uhakika ni kwamba wao, hawa viongozi, watasomesha watoto wao kwa kiingereza. Je, nani wanamtungia elimu kwa Kiswahili?
Ni kwa nini hatukusema iwe ni Kiswahili kila mtu? Kwa sababu viongozi wetu wanaamini kiingereza kwa watoto wao ni bora zaidi. Kwa kuogopa hadithi za kisiasa wameamua kutunga mifumo miwili. Huu ni ujinga.