Rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo au urembo?

Rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo au urembo?

Mbona hata ktk mambo ya msing ya kuiheshim bendera halipo kakosa wap sasa! Au kisa hajanunua yake ya ucku!
 
sasa afanyeje wakati hana hata shuka,ameona ni vyema akaitumie kulingana na ugumu wa maisha
 
huenda maisha yamembana sana kiasi cha kutokuwa na shuka ya kujifunika
 
...ujumbe ni kwamba wapo wenye dhamana kubwa ktk taifa hili lakini wamedharau hadhi ya taifa na kujali maslahi yao ya muda mfupi(kujifunika),asante kamanda ingawa upo lupango lakini wahusika wamepata ujumbe...
 
LUZILA1.jpg
 
Duh, chama pekee kinachojali watanzania na kuleta maendeleo
 
Natamani sana kampeni za uchaguzi mkuu mwakani vyama vyote vya siasa vingetumia bendera ya taifa katika kampeni za vyama vyao. Maana rais anaechaguliwa anaongoza nchi na sio chama. Tunapoingiza mambo ya chama hatutofika mbali. Pia ingefaa rais asiwe mwenyekiti katika chama chake cha siasa
 
Sijui ni sababu zipi zimekusukuma kufikia hiyo conclusion, lakini si siri tena kuwa kuna vyama ambavyo alama zake kwa sasa zimekuwa kama alama za wachawi. Viongozi wa vyama hivyo wameamua kujitambulisha kwa alama za taifa kukwepa adha wanayoipata.
 
Nchi imegeuzwa kama saccos. Unapoingia na gia ya chama hutofanya kazi za maendeleo bali kuridhisha wanachama
 
Nashangazwa sana na baadhi ya wabunifu wetu wa vazi letu la taifa.wengi wao ubunifu wao ni kwenye rangi za bendera ya taifa. Naona hii sio sawa,mimi ningeshauri tubuni vazi ambalo litakua la kipekee hapa duniani lakini lisilo na rangi za bendera ya tanzania.mfano wenzetu uk, scotland,india,nigeria,saudi arabia n.k. Mavazi yao ya taifa hayana rangi za bendera zao isipokua upekee au utofauti wa mavazi yao na mavazi ya mataifa mengine ni aina ya mitindo ya mavazi hayo.ningeshauri tutafute aina ya mavazi ya asili ya makabila yetu mawili,moja kutoka zanzibar na moja kutoka tanganyika ambayo yalikua yanavaliwa hapa nchini pekee na kuyachanganya kiubunufu, kuyatilia, maboresho na nakshi za kisasa na kulifanya hilo kuwa vazi la kitanzania. Kwa bara mfano,uvaaji wa kimasai ungeweza kuwa mfano mzuri wa ninachofikiria lakini wamasai wapo na nchi jirani hivyo kuondoa upekee ninaoufikiria.rangi za taifa zibakie kwenye vitu vingine.hata hivyo tuzingatie athari za vazi, rangi na muungano wetu.je muungano ukivunjika vazi letu litakua bado linaweza kuendelea kuwepo? Ni mchango na mawazo yangu tu. Naomba kutoa hoja.
 
Wimbo wetu wa taifa tuliiu-copy toka wimbo wa taifa wa Afrika kusini uanoitwa 'Nkosi Sikelei' uliotungwa na Enoch Sontonga mwaka 1897. Wimbo huu unafana kila kitu na wimbo wa Afrika kusini kaunzia melody mpaka maneno, tofauti yake ni kwamba wimbo wa Afrika Kusini ni mrefu kidogo kulinganisha na wa kwetu. Wale wafuatiliaji wa siasa za kimataifa wanajua hili au basi hata wasiofuatilia sana wamewahi kusikia wimbo huu katika hafla za kitaifa za Afrika Kusini kama Fainali za kombe la dunia 2010 au katika mazishi ya Mzee Nelson Mandela.

Mbaya zaidi ni kwamba wimbo huu uliwahi kutumika kama wimbo wa taifa wa Zimbabwe wakaubadilisha baada ya kipindi fulani. Lakini pia wale waliosikia wimbo wa taifa wa Zambia wanajua kwamba sehemu ya wimbo wao unafanana kabisa na wimbo wa Taifa letu. Kumbuka Zambia ni taifa kikiristo hivyo kuna maneno yanayozungumzia imani yao ila mimi nilimaanisha melody.

Kuhusu bendera, rangi zote zilizo kwenye bendera yetu ndo zilizo kwenye bendera ya South Africa isipokuwa mpangilio wa rangi hizo na inaongezeka rangi nyekundu kwa sababu ya historia ya mapambano yao ya kudai uhuru. Wakati sisi rangi za bendera yetu zimepangana, wao bendera yao imetengeneza kitu kama 'V' kwa mbele. Hivo basi hoja yangu ni kwamba tuli-copy kila kitu toka South Africa na sasa ni wakati wa kuwa na mawazo huru na kutunga wimbo wetu wa taifa na bendera yetu isyofanana na za wengine.

th
th
 
Tukiisha badili mafisadi watakamatwa, vijana watapata ajira, vijijini tutapata maji safi, tutapata umeme wa uhakika....
? kama jibu ni ndio nakuunga mkono, kama sio ,nadhani ujaribu kufikiria vitu vya msingi na vyenye uhusiano wa moja kwa moja na maisha ya kila siku ya jamii!
 
Nimekusoma vizuri, usihofu tutabadili bendera na kuweka alama ya mwezi na nyota na wimbo wa taifa utaimbwa kwa kiarabu.
 
Halafu tukishabadili wimbo wa Taifa na Bendera; itaongeza pato la Taifa (GDP) kwa asilimia ngapi?
Na mfumuko wa bei (Inflation) utapunguzwa kwa asilimia ngapi?
Vilevile deni la Taifa litapungua kwa asilimia ngapi?
Kwanini tunafikiria kuimba tu?
 
Unatumia ubongo katika kufikiri rangi zetu zinafanana na Jamaica na sio south Lakini pia sio tatizo kwani Kuna rangi mpya duniani.
 
Ili tufikie mabadiliko tunayoyalilia sote ni lazima kuanza kufikiria kubadili vitu kama hivi. Huwezi kuogopa kubadili wimbo wa taifa au bendera ya taifa ukawa na ubavu wa kubadili utawala.

Kwa hiyo Wimbo wa Taifa na Bendera kufanana na za mataifa mengine ndizo zinazotutia umasikini?
 
Back
Top Bottom