Ramadhan Special Thread

emoji287.png
emoji294.png
emoji287.png
emoji294.png




masharti ya swalah

Masharti ya swalah ni tisa:

Sharti ya kwanza: Uislamu.

Sharti ya pili: Mtu kuwa na akili.

Sharti ya tatu: Uwezo wa kupambanua.

Sharti ya nne: Kuondosha hadathi.

Sharti ya tano: Kuondosha najisi.

Sharti ya sita: Kufunika zile sehemu zisizotakiwa kuonekana (´Awrah).

Sharti ya saba: Kuingia kwa wakati.

Sharti ya nane: Kuelekea Qiblah.

Sharti ya tisa: Kunuia.

Mwandishi: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Chanzo: Duruus-ul-Muhimmah li ´Aammah al-Ummah, uk. 12
Tarjama: Wanachuoni.com

nguzo za swalah

Nguzo za swalah ni kumi na nne:

Nguzo ya kwanza: Kusimama kwa mwenye kuweza.

Nguzo ya pili: Kusema "Allaahu Akabr".

Nguzo ya tatu: Kusoma Suurah "al-Faatihah."

Nguzo ya nne: Kurukuu.

Nguzo ya tano: Kuinuka kwenye Rukuu´.

Nguzo ya sita: Kusujudu juu ya viungo saba.

Nguzo ya saba: Kutoka hapo.

Nguzo ya nane: Kukaa baina ya Sajdah mbili.

Nguzo ya tisa: Kuwa na utulivu katika nguzo zote.

Nguzo ya kumi: Kuzipangilia.

Nguzo ya kumi na moja: Tashahhud ya mwisho.

Nguzo ya kumi na mbili: Kukaa katika [Tashahhud] hiyo.

Nguzo ya kumi na tatu: Kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Nguzo ya kumi na nne: Kuleta Tasliym mbili.

Mwandishi: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Chanzo: Duruus-ul-Muhimmah li ´Aammah al-Ummah, uk. 13
Tarjama: Wanachuoni.com

mambo ya wajibu ya swalah

Mambo ya wajibu ya swalah ya ni manane:

La kwanza: Kusema "Allaahu Akbar" mbali na ile ya kwanza.

La pili: Kusema "Sami´ Allaahu li man hamidah" kwa imamu na anayeswali peke yake.

La tatu: Kusema "Rabbanaa wa lak al-Hamd". Inasemwa na wote.

La nne: Kusema "Subhaana Rabbiy al-´Adhwiym" katika Rukuu´.

La tano: Kusema "Subhaana Rabbiy´ al-A´laa" katika Sujuud.

La sita: Kusema "Rabb Ighfir liy" kati ya Sajdah mbili.

La saba na la nane: Tashahhud ya kwanza na kukaa kwayo.

Mwandishi: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Chanzo: Duruus-ul-Muhimmah li ´Aammah al-Ummah, uk. 13-14

Tarjama: Wanachuoni.com
Mkuu ukipata mda, endelea kutuletea zaidi hizi mada za swala
Mungu akulipe kheri
 
allahuma inna kaafuuu tuhibbul afwaaa faafwannaaa yaaa karyyym alfuww. haya ni maneno mtume saw alikuwa akiyataja sana ramadhan. tupunguze soga,story za vijiweni,instagram,magroup yasio na msingi, tukithirishe kuskiliza mawaidha na kujua mambo ya dini. Na pia quraaan kusoma kwa wengi wakat ndio huuu kuziba mashimp dunia si chchte akina ivan walikuwa wanacheza na madola kwenye mitandao sasa yuko maiti lets wake up brothers and sisters fill imaaan
Masha Allah. Ukumbusho mzuri sana huu na wenye manufaa.
Allah Atuwafikishe yarab.
Ameen

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
ASSALAM ALAYKUM WARAHMATULLAHI WABARAKATUH.

Ninachukua fursa hii kuwatanabahisha waislam wote waliomo jamii forum, ya kuwa tumefikiwa na mwezi mtukufu wa Ramadhani. Mwezi huu ni kwa ajili ya kufunga na kuzidi kujikurubisha kwa ALLAAH, kwa kuswali, kusoma Quran kwa wingi, kutoa swadaqa, zakkah, kuzidisha kila aina ya jambo jema ulioamrishwa na Mola wako.

Pia vilevile kuacha Yale yote ALLAAH aliyotukataza, kusema uongo, kusenganya, kuiba, kulumbana (kugombana) n.k

Na vilevile kuacha kupoteza muda kwa mambo ya upuuzi:- karata, misalsala, kulala sana, bao, muda mwingi kukaa kwenye t.v na computer, kuchezea simu n.k.

Hii fursa tulioipata ni adhiym kwa kila muislam iliyomfikia, kwa ajili ya kuomba msamaha kwa ALLAAH, na kukubaliwa toba zetu.

Kwani ALLAAH ametuahidi yoyote atakaefunga kwa imaanan na Ucha Mungu basi ALLAAH atamsamehe madhambi yake, kwa hivyo tufanyeni jitihada sana kwa kutaraji kusamehewa dhambi ZETUna muumba.

KILICHONISUKUMA KUANDIKA UZI HUU, NIMEONA KUWA KUSHAANZA KUTOKEA NA BAADHI YA THREAD AMBAZO ZIMEANZA KULETA UPOTOSHAJI JUU YA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN, (mfano kumekucha Zanzibar ) NA WATU KUANZA KULUMBANA. SISI WAISLAM TUSIJIINGIZE KABISA KATIKA MALUMBANO HAYO NA WALA TUSIZISOME KABISA THREAD HIZO KWA MAANA ZINAWEZA KUPELEKEA KUHARIBU SWAUMU ZETU NA LENGO LA KUFUNGA TUKALIKOSA.

HATUWEZI KUJUA WENYE KUFANYA HIVYO WAMETUMWA AU NI AKILI ZAO WENYEWE TUU.
TUNAMUUOMBA ALLAAH ATUJAALIE TUFUNGE SALAMA NA SWAUMU ZETU ZIWE ZENYE KULUBALIWA.
AMIYN

Hii thread si ya majibizano ni TANBIHI kwa waislam
 
Back
Top Bottom