Nyani Ngabu habari ya huko ulipo?
Kwa heshima kubwa naomba nipishane na wewe katika hilo Mimi nikiwa miongoni mwa walioumuita Kikwete "Rais was Misiba" hiyo ni dhahiri kabisa Kikwete alikuwa muhudhuriaji mkubwa wa matukio mbali mbali ya ndani na nje ya nchi yaliokuwa na umuhimu na yasiyokuwa na umuhimu Pote "alikaba nafasi". Jambo ambalo lilikuwa likiligharimu sana Taifa letu.
Back to the topic ni Kwamba Uelewe kuwa Rais ndiye Raia Namba Moja, Amiri Jeshi Mkuu na Mfariji Mkuu Wa Taifa hili, Hivyo alipaswa na anaowajibu Kuwa Faraja Kwetu RAIA katika Jambo lolote kubwa la kitaifa.
Ni jambo la ajabu na kushangaza sana Rais Kutohudhuria mambo makubwa kama Lile la Kuaga Miili ya Wale Askari waliokufa Wakiwa Katika Kutimiza Wajibu wao wa kizalendo Kule Kibiti,
Pia Kwa Mshangao huo huo Ndio unapelekea kutilia shaka "roho" yake ikoje? Yaani Msiba Mkubwa wa Watoto Waliokuwa katika Safari ya kelekea kutimiza Ndoto zao kwa Taifa lao wanapoteza uhai wao alafu mfariji hatokei Ila kuzindua Majengo na Barabara daima hutokea wala hatumi muwakilishi.
Funzo hapo ni Kuwa yeye hayo ya "uzinduzi" ni muhimu zaidi kuliko "faraja" na kutia Moyo kwa Taifa.