"Rais wa misiba"

"Rais wa misiba"

Ona sasa...mwingine huyu kimsingi anasema haoni ubaya wa Magufuli kutokwenda la kama angekuwa na uwezo wa kufufua watu.

Kwake cha muhimu zaidi ni kuangalia namna ya kuepusha ajali kama hiyo iliyotokea....

Lakini si ajabu nawe ukaitwa mkabila.....
Sasa rais hatakikusikia habari mbaya, kashasema hilo.

Mnataka kumlazimisha?

Kama hamumtaki rais wa hivyo mtoeni.

Rais mwenyewe msema ovyo, si ajabu akaja msibani na kusema maneno ya ovyo na kuzua mjadala hasi.

Sijaona Magufuli kwa roho yake ya korosho angefanya nini cha ziada kwenye msiba huo.

Ndiyo maana nikasema labda kama angekuwa ana uwezo wa kufufua watu ningeona ana umuhimuwa kuwepo.

Zaidi ni kuingiza siasa katika msiba tu. Tushaona kina Lema wanazozana na uongoziwa CCM kuweka siasa katika msiba.

Mimi mtu atakayeihoji serikali ya Magufuli inafanya nini kuhakikisha ajali hizi zinadhibitiwa nitamuona anafanya la maana kuliko anayehojikwa nini Magufuli hajaenda msibani.

Hususan kwa sababu kuna muwakilishi mkubwa sana wa serikali kaenda, makamu wa rais.

Kwa hiyo hatuwezi kusema serikali ngazi ya taifa imesusa kwenda msibani.

Kwani lazima msibani aende Magufuli? Tunajuaje kama rais na Makamu hawajagawana majukumu na Makamu kupewa jukumu la kufariji misibani wakati rais anaendelea na kazi nyingine kuhakikisha hiyo misiba haijirudii?
 
Sasa nimeelewa kwa nini kwenye kutoa maoni ya kipima joto wanataka uchague 'Ndio, Hapana au Sijui' maana hawakosi watakaokubali, watakaokataa ama wengine wao hawana la kusema.

Ahahaaaaa....umenichekesha sana aisee.

Sasa kwa taarifa yako, humu humu JF kuna watu washalalamika kwa nini hata huwa wanaweka huo uchaguzi wa 'sijui'.

Kuna watu huwa wanadai hakuna sababu ya kuweka huo uchaguzi [option] maana kwao eti jibu ni lazima liwe la 'ndiyo' au 'hapana' tu.

Binadamu ndivyo tulivyo...haturidhiki hata iweje.

Nina uhakika kabisa kama Magufuli angeenda leo kuna ambao wangelalamika kwa nini kaenda.

Kwanza tayari kuna wanaosema ni bora hajaenda...papo hapo wengine wanamlaani kwa kutokwenda.
 
Binadamu ni kiumbe changamani sana.

Huo ni ukweli ulio dhahiri ambao wala hauhitaji mtu uwe na 'kipaji maalumu' kuuona.

Hata iweje, binadamu kamwe huwa haridhiki.

Kwa kifupi, ni ndivyo tulivyo!

Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu ya yaliyotokea huko Arusha wiki ilopita na kuagwa kwa waliopoteza maisha yao kwenye hiyo ajali mapema leo hii.

Kama ilivyodhaniwa/ ilivyotarajiwa, rais Magufuli hakuwepo kwenye hiyo shughuli.

Hii si mara yake ya kwanza yeye kukosa shughuli kama hii ya leo tangia awe rais.

Watu wengi sana wanamlaumu kwa kukosekana kwake. Kwangu hizo ni lawama halali kabisa.

Naamini ingekuwa ni vyema yeye mwenyewe kuwepo kuliko kutuma mwakilishi.

Sababu za yeye kutokwenda mimi sizijui na wala sitajaribu kuanza kusadiki ni nini kilichomfanya asiende.

Ila pia bado sijasahau kipindi ambapo Jakaya Kikwete alikuwa rais na watu wengi tu [hususan humu JF] walikuwa wakimbeza kuwa eti anapenda sana kwenda misibani kuuza sura kuliko kufanya kazi.

Kuna watu walimbatiza hadi jina kuwa eti ni "rais wa misiba". Na simzushii mtu...bofya hapa usome mwenyewe!

Kikwete alibezwa, akachekwa, akaitwa kila aina ya majina kutokana na kupenda kwake kuhudhuria misiba hata ya watu wa kawaida tu wasio maarufu.

Kuna wengine walidai eti anaweka 'precedent' mbaya na kwamba eti watu watakuwa wanategemea kumwona 'rais' kwenye kila msiba utokeao.

Sasa huyu Ngosha yeye yuko tofauti. Anaonekana si mtu wa kupenda kujichanganya changanya sana na watu.

Misiba mingi tu itatokea katika utawala wake maana huo ndo uhalisia wa maisha. Watu hufa kila siku kwa sababu anuai.

Labda yeye hataki kujenga matarajio kwa watu kuwa kila msiba utokeao na yeye lazima atawepo maana vifo ni vingi mno na ukienda kwenye kifo cha huyu au vifo vya hawa basi kila afapo mtu au wafapo watu, basi na wewe lazima uwepo.

Vyovyote vile, urais ni kazi ngumu sana. Ni kazi ambayo kwa kiasi kikubwa haina shukurani.

Ufanye hili, utalaumiwa na kulaaniwa. Usifanye lile, utalaumiwa na kulaaniwa.

Chochote ufanyacho na chochote usichokifanya, ni lawama na shutuma tu.

Wakati mwingine huwa hata sielewi kwa nini watu huwa wanapenda kuwa marais......
Watu 32 ni wengi mno,wengi wakiwa wanafunzi wadogo!!Hakuna justification ya Rais kukosa msiba huu!
 
Sasa rais hatakikusikia habari mbaya, kashasema hilo.

Mnataka kumlazimisha?

Kama hamumtaki rais wa hivyo mtoeni.

Rais mwenyewe msema ovyo, si ajabu akaja msibani na kusema maneno ya ovyo na kuzua mjadala hasi.

Sijaona Magufuli kwa roho yake ya korosho angefanya nini cha ziada kwenye msiba huo.

Ndiyo maana nikasema labda kama angekuwa ana uwezo wa kufufua watu ningeona ana umuhimuwa kuwepo.

Zaidi ni kuingiza siasa katika msiba tu. Tushaona kina Lema wanazozana na uongoziwa CCM kuweka siasa katika msiba.

Mimi mtu atakayeihoji serikali ya Magufuli inafanya nini kuhakikisha ajali hizi zinadhibitiwa nitamuona anafanya la maana kuliko anayehojikwa nini Magufuli hajaenda msibani.

Hususan kwa sababu kuna muwakilishi mkubwa sana wa serikali kaenda, makamu wa rais.

Kwa hiyo hatuwezi kusema serikali ngazi ya taifa imesusa kwenda msibani.

Kwani lazima msibani aende Magufuli? Tunajuaje kama rais na Makamu hawajagawana majukumu na Makamu kupewa jukumu la kufariji misibani wakati rais anaendelea na kazi nyingine kuhakikisha hiyo misiba haijirudii?

Nakubaliana nawe.

Serikali ngazi ya taifa kweli ilikuwepo.

Na kuhusu serikali inafanya nini kupunguza hizi ajali za kizembe ambazo naamini zinaepukika hata kwangu hilo ndo la msingi zaidi.

Ila mwisho wa siku naamini kuwa, kwenye baadhi ya situations optics matter....it would have been a good thing for him to show up.
 
Binadamu ni kiumbe changamani sana.

Huo ni ukweli ulio dhahiri ambao wala hauhitaji mtu uwe na 'kipaji maalumu' kuuona.

Hata iweje, binadamu kamwe huwa haridhiki.

Kwa kifupi, ni ndivyo tulivyo!

Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu ya yaliyotokea huko Arusha wiki ilopita na kuagwa kwa waliopoteza maisha yao kwenye hiyo ajali mapema leo hii.

Kama ilivyodhaniwa/ ilivyotarajiwa, rais Magufuli hakuwepo kwenye hiyo shughuli.

Hii si mara yake ya kwanza yeye kukosa shughuli kama hii ya leo tangia awe rais.

Watu wengi sana wanamlaumu kwa kukosekana kwake. Kwangu hizo ni lawama halali kabisa.

Naamini ingekuwa ni vyema yeye mwenyewe kuwepo kuliko kutuma mwakilishi.

Sababu za yeye kutokwenda mimi sizijui na wala sitajaribu kuanza kusadiki ni nini kilichomfanya asiende.

Ila pia bado sijasahau kipindi ambapo Jakaya Kikwete alikuwa rais na watu wengi tu [hususan humu JF] walikuwa wakimbeza kuwa eti anapenda sana kwenda misibani kuuza sura kuliko kufanya kazi.

Kuna watu walimbatiza hadi jina kuwa eti ni "rais wa misiba". Na simzushii mtu...bofya hapa usome mwenyewe!

Kikwete alibezwa, akachekwa, akaitwa kila aina ya majina kutokana na kupenda kwake kuhudhuria misiba hata ya watu wa kawaida tu wasio maarufu.

Kuna wengine walidai eti anaweka 'precedent' mbaya na kwamba eti watu watakuwa wanategemea kumwona 'rais' kwenye kila msiba utokeao.

Sasa huyu Ngosha yeye yuko tofauti. Anaonekana si mtu wa kupenda kujichanganya changanya sana na watu.

Misiba mingi tu itatokea katika utawala wake maana huo ndo uhalisia wa maisha. Watu hufa kila siku kwa sababu anuai.

Labda yeye hataki kujenga matarajio kwa watu kuwa kila msiba utokeao na yeye lazima atawepo maana vifo ni vingi mno na ukienda kwenye kifo cha huyu au vifo vya hawa basi kila afapo mtu au wafapo watu, basi na wewe lazima uwepo.

Vyovyote vile, urais ni kazi ngumu sana. Ni kazi ambayo kwa kiasi kikubwa haina shukurani.

Ufanye hili, utalaumiwa na kulaaniwa. Usifanye lile, utalaumiwa na kulaaniwa.

Chochote ufanyacho na chochote usichokifanya, ni lawama na shutuma tu.

Wakati mwingine huwa hata sielewi kwa nini watu huwa wanapenda kuwa marais......
Kuwa na adabu bac usipende kulaum tu kwan makamu. Wake aliye enda hatoshi hadi liende baraza zima la viongoz kumbuka kuwa nawew pengine hujaenda na kama umeenda shida yako ilikuwa ni kwenda msibani au kuangalia walo hudhuria?
 
Watu 32 ni wengi mno,wengi wakiwa wanafunzi wadogo!!Hakuna justification ya Rais kukosa msiba huu!

Ni kweli.

Na ndiyo maana kama umenisoma vizuri na kuelewa ulichokisoma utaona nimesema kuwa ingekuwa ni vyema kama yeye mwenyewe angeenda kwenye hiyo hafla ya kuwaaga hao maiti.
 
Tatizo moja kubwa la nchi za dunia ya tatu kiujumla, na Africa hususan, ni wananchi kuwaangalia viongozi si kama vijakazi wao, bali kama waokozi wao.

Hivyo badala ya watu kuweka mkazo kuushurutisha uongozi uwasaidie kutatua matatizo, wananchi wanaangalia kiongozi awe kama baba yao aje kuwafuta machozi.

Na kiongozi asipokubali kuwa baba yao kuja kuwafuta machozi anaonekana mbaya, hata kama hakufanya hivyo kwa sababu anatafuta suluhu ya msingi ya tatizo (not that Magufuli is doing that, tomy knowledge so far).

Na kiongozi akiweza kuja kuwafuta machozi anaonekana mzuri sana, hata kama hafanyi lolote kumaliza tatizo la msingi.

Ni utamaduni wa kijinga sana, ndio huu unapelekea watu kumlilia Magufuli aende kwenye msiba kamavile Magufuli ana uwezo wa kufufua watu.
 
Kuwa na adabu bac usipende kulaum tu kwan makamu. Wake aliye enda hatoshi hadi liende baraza zima la viongoz kumbuka kuwa nawew pengine hujaenda na kama umeenda shida yako ilikuwa ni kwenda msibani au kuangalia walo hudhuria?

Hahahaaa....wenzio wanaona namtetea Magu kisa ukabila...wengine wanaona nahalalisha kukosa kwake kwenda kwa kuangalia Kikwete alikuwaje....halafu wewe nawe unaona namlaumu Magu!

Kweli watu tumetofautiana sana kiakili....
 
Nakubaliana nawe.

Serikali ngazi ya taifa kweli ilikuwepo.

Na kuhusu serikali inafanya nini kupunguza hizi ajali za kizembe ambazo naamini zinaepukika hata kwangu hilo ndo la msingi zaidi.

Ila mwisho wa siku naamini kuwa, kwenye baadhi ya situations optics matter....it would have been a good thing for him to show up.

Magufuli gubegube varuvaru hajui whats good for him, hajui whats good for his people.

Ana muelekeo wake na anaufuata huo huo kama guluguja asiye na uti wa mgongo wala ubongo anayeenda kwa reflex action tu.
 
Tatizo mojakubwa la nchi za dunia ya tatu kiujumla, na Africa hususan, ni wananchi kuwaangalia viongozi si kama vijakazi wao, bali kama waokozi wao.

Hivyo badala ya watu kuweka mkazo kuushurutisha uongozi uwasaidie kutatua matatizo, wananchi wanaangalia kiongozi awe kamababa yao aje kuwafuta machozi.

Na kiongozi asipokubali kuwa baba yao kuja kuwafuta machozi anaonekana mbaya, hata kama hakufanya hivyo kwa sababu anatafuta suluhu ya msingi ya tatizo (not that Magufuli is doing that).

Na kiongozi akiweza kuja kuwafuta machozi anaonekana mzuri sana, hata kama hafanyi lolote kumaliza tatizo la msingi.

Ni utamaduni wakijinga sana, ndio huu unapelekea watu kumliliaMagufuli aendekwenye msiba kamavile Magufuli ana uwezo wa kufufua watu.

Hahahaaa mazee....wataokuelewa hapa sidhani kama watazidi idadi ya vidole kwenye kiganja!
 
Braza njaa imekuwa kali sana huko inaonekana biashara ya box imekuwa ngumu umeanza u-Lemutuz. Kila unapotokea msiba wako watu wanaokosa kuhudhuria kwa sababu mbalimbali. Kwa vile wewe haujui sababu za Magufuli kutohudhuria ungetuliza kipago na kupiga kimya. Tatizo ni pale unapotumia hii fursa kujipendekeza na kutengeneza headline kwa manufaa yako binafsi. Nchi nzima haiwezi kuacha kufanya kazi kwa kwenda msibani na ni sahihi kabisa kwa Raisi kutuma mwakilishi ili afanye kazi nyingine. Ndio maana hakutangaza maombolezo ya kitaifa na kubabaishwa na presha zenu za mitandaoni. Sio kila mtu anahudhuria msiba, kama umetingwa unatuma salamu, ndio utamaduni wetu watanzania
 
Ni kweli.

Na ndiyo maana kama umenisoma vizuri na kuelewa ulichokisoma utaona nimesema kuwa ingekuwa ni vyema kama yeye mwenyewe angeenda kwenye hiyo hafla ya kuwaaga hao maiti.
Ila pia ukaeleza Uzuri wa yeye kutokwenda!! Ili tu asijeonekana kuwa ni rais wa misiba! Nimekupata sawia.
 
Na kweli bora hajaenda maana huenda "angechafua hali ya hewa" tena kwa kauli zenye utata.

Bado nakumbuka kauli za kule Bukoba!
 
Ila pia ukaeleza Uzuri wa yeye kutokwenda!! Ili tu asijeonekana kuwa ni rais wa misiba! Nimekupata sawia.

Unaona sasa...

Tatizo la kusoma kitu na kutokukielewa.

Hakuna hata sehemu moja niliyoelezea uzuri wa yeye kutokwenda.

Nilichofanya ni ku speculate sababu ya yeye kutokwenda.

Umeshindwa kusoma na kuelewa ulichokisoma!

Majanga.
 
Kumtetea huyo mtu inabidi uwe na akili ya mwendawazimu.....Huchelewi kusema kikwete pia alikuwa anakula rambirambi za wahanga
 
Back
Top Bottom