Rais Samia, unataka Lissu anyongwe mpaka afe?

Rais Samia, unataka Lissu anyongwe mpaka afe?

Ndugu Rais.

Huku mtaani wananchi wana shock kubwa, hawaamini kinachoendelea nchini.
Wanasema kwa mujibu wa mashitaka ambayo serikali yako imemfungulia Lissu, huenda akanyongwa mpaka kufa. Idea hiyo pekee inawapa wananchi ganzi, simanzi na kwa kweli inawafanya wakuchukie.

Na makada wa CHADEMA wanawaambia wananchi kwenye mikutano ya hadhara kuwa serikali yako inataka kumnyonga Lissu.

Kesi hii ndugu Rais, inawafanya watu wakuone kama huna moyo hivi. Tafadhali kabla ya haiba yako haijachafuka na watu kukuona mtawala katili, tafadhali ondoa hii kesi mahakamani.

Soma Pia: Tundu Lissu ashtakiwa kwa Uhaini, arudishwa rumande, kesi yake kusikilizwa Aprili 24, 2025

Tunapoelekea utaanza kuchukiwa na umma kama kipindi kile ulivyoendelea kumshikilia Mbowe gerezani, Kesi ile ilikuwa imekutoa ktk mioyo ya Watanzania sana na laiti ungeng'ang'ania kumshika Mbowe kwa muda mrefu zaidi, umma ungekuona kwa jicho negative sana. Sasa situation kama hiyo ninaiona sasa ambapo umma umeanza kukuangalia kwa jicho baya.

Ndugu Rais, Serikali yako inaongoza kwa kuwaweka wapinzani wa utawala wako jela. Ushanuweka Mbowe ndani kwa kesi ya Ugaidi, Ushamfungulia Dr Slaa, Mwabukusi na Mdude kesi ya Uhaini, na sasa Lissu serikali yako imemfungulia kesi ya uhaini. Wananchi wanasema unatumia mahakama kisiasa kupitiliza. Wanakuona kuwa huwezi kujibu hoja za wapinzani kwa hiyo badala yake unatumia msuli wa dola!.

Ndugu Rais ni kweli unaweza kumuweka Lissu jela na hata kumnyonga, lakini kiukweli hii dhana ya kumnyonga Lissu inaibua hisia nzito mno kwa wananchi huku mtaani na watu wanakuangalia vibaya sana.

Ujumbe nimekufikishia, utaamua mwenyewe serikali ifanye nini, Wananchi hawaamini kuwa mahakama inaweza kuwa huru kutenda haki kulingana na historia ya kesi hasa za hivi karibuni, kwa hiyo wananchi wanasema kuwa hii ngoma ni yako na si mahakama.

Kumnyonga Lissu kwa maoni yangu is not a good idea!.
Kwangu mimi Lissu alitakiwa kujifunza kwa Mboe,mama alipoingia madarakani katika watu waliotetewa sn alikua yeye mpk wakamtoa jela,mama alifanya uungwana sana mpk kumuita ikulu, sasa Lissu anataka TZ iwe km Sudan or DRC which it won’t happen,mbona ACT wanafanya siasa ambazo nyingi hazina drama km chadema?what special do they have which others don’t?
 
Ukweli ni kwamba, njia aliyokuwa akitumia Mtangulizi wake ilikuwa imejifunga. Yeye kaamua kutumia gharama kubwa kuhakikisha anairejesha njia ile ile. Na sasa yuko katikati ya njia kuelekea kule kule alikolenga Mtangulizi wake. Je atatoboa?? Mungu ni yule yule jana leo na kesho.
Mungu atatuamulia huu ugomvi kabla October kama alivyofanya March 12 2021
 
Lakini si walishajaribu kumuua kwa kumtwanga risasi 16, kipi kinakufanya uamini kuwa hawataki kumuua tena this time kwa kumnyonga?
Ni kweli ndani ya utawala wa awamu ya tano, alirushiwa risasi na wahuni wasiofahamika mpaka leo hii, hatuwezi sema ni nani, kwa sababu hakuna ushahidi au aliyekamatwa kuhusiana na suala hilo.
 
Kama ushahidi ni timilifu na hautaacha hata tone moja la uonevu inamfaa kunyongwa Sheria ifuate mkondo wake,lazima heshima kwa Taifa itawale,hakuna mwenye umuhimu zaidi ya Taifa
 
Kama ushahidi ni timilifu na hautaacha hata tone moja la uonevu inamfaa kunyongwa Sheria ifuate mkondo wake,lazima heshima kwa Taifa itawale,hakuna mwenye umuhimu zaidi ya Taifa
Aliyeuza Ardhi na bahari Uarabuni nini adhabu yake?
 
Heche kila akipiga nondo anamalizia na usemi "Wanataka kumnyonga Lissu"- Yaani hiyo kauli peke yake inaibua hisia nzito, simanzi na huruma ya kutisha kwa Lissu huku Samia akionekana Jitu moja katili sana
 
Huenda huo ndo mpango wake, lakini wananchi huku mtaani wanamuona ni rais katili mwenye lengo la kumnyonga Lissu
Samia ni katili sana tu. Anajificha kwenye jinsia yake, dini yake na Uzanzibari wake akiaambiwa anakosea mfano kuuza bandari, kuwafukuza Wamasai, kuuza misitu, tozo, ufisadi, mikopo ya hovyo, teuzi za hovyo, rushwa, kuua demokrasia ndani ya chama chake na kwa wapinzani wake.

Hayo anayoyafanya angekuwa Ruto, Museveni, JPM, Kagame watu wote wangepiga kelele sana hata Zitto, Mbowe. Hana tofauti na hao ila yeye hana vision yoyote, hana uzalendo wowote anautaka urais kwa ajili ya mamlaka, pesa, kutanua, kusafiri.
 
Heche kila akipiga nondo anamalizia na usemi "Wanataka kumnyonga Lissu"- Yaani hiyo kauli peke yake inaibua hisia nzito, simanzi na huruma ya kutisha kwa Lissu huku Samia akionekana Jitu moja katili sana
Baada ya uchaguzi. Chadema ikiwa hoi, haina wabunge, madiwani, ikiwa na ukata wa pesa, haina sauti bungeni.

Atasikiliza kilio chako na kukuonea huruma. Atasema anamsamehe Lissu, hatamnyonga, atamwachia huru. Nafikiri utafurahi na kumuona ni Mama mwenye huruma sana. Mapambio ya nani kama mama yataongezeka. Anajua kucheza na akili zenu.
 
Baada ya uchaguzi. Chadema ikiwa hoi, haina wabunge, madiwani, ikiwa na ukata wa pesa, haina sauti bungeni.

Atasikiliza kilio chako na kukuonea huruma. Atasema anamsamehe Lissu, hatamnyonga, atamwachia huru. Nafikiri utafurahi na kumuona ni Mama mwenye huruma sana. Anajua kucheza na akili zenu.

Kama CHADEMA ingekuwa ni mali ya Lissu hapo kweli wangekuwa wanamkomoa. Lakini ni mali ya Watanzania, kwa hiyo uhuni wowote dhidi ya CHADEMA ni sawa na Uhuni dhidi ya wananchi na huo ni Ujinga kwa mtu yeyote mwenye dhamana za kuongoza nchi kuufanya.
 
Kama CHADEMA ingekuwa ni mali ya Lissu hapo kweli wangekuwa wanamkomoa. Lakini ni mali ya Watanzania, kwa hiyo uhuni wowote dhidi ya CHADEMA ni sawa na Uhuni dhidi ya wananchi na huo ni Ujinga kwa mtu yeyote mwenye dhamana za kuongoza nchi kuufanya.
Inawezekana ni mali ya Watanzania. Lakini mbona wenye mali wapo kimya. Uhuni wamefanyiwa sana CDM kama uchaguzi wa serikali ya mitaa.

Kiongozi, anayesimamia mali yao, chama chao yupo magereza. Hakuna maandamano, mashinikizo kama hata Kenya hapo kiongozi kama Raila akionewa, Raila akifungwa ndani ya wiki moja anaachiwa au serikali ya Kenya inaanguka. Vipi hapa Tanzania?

Wengi wanaandama mitandaoni kutetea chama chao. Kenya wangekuwa mitaani.
 
Inawezekana ni mali ya Watanzania. Lakini mbona wenye mali wapo kimya. Uhuni wamefanyiwa sana CDM kama uchaguzi wa serikali ya mitaa.

Kiongozi, anayesimamia mali yao, chama chao yupo magereza. Hakuna maandamano, mashinikizo kama hata Kenya hapo kiongozi kama Raila akionewa, Raila akifungwa ndani ya wiki moja anaachiwa au serikali ya Kenya inaanguka. Vipi hapa Tanzania?

Wengi wanaandama mitandaoni kutetea chama chao. Kenya wangekuwa mitaani.
wengi wamepewa elimu mbovu kwa hiyo wapo kama vipofu
Sasa ukiona mtu anamtake advantage kipofu halafu yupo ktk mtumbwi uleule ni hatari mno huko mbeleni
usifurahie ujingaujinga kwenye nchi, unaharibu mustakbali wa vizazi vyako
 
Ndugu Rais.

Huku mtaani wananchi wana shock kubwa, hawaamini kinachoendelea nchini.
Wanasema kwa mujibu wa mashitaka ambayo serikali yako imemfungulia Lissu, huenda akanyongwa mpaka kufa. Idea hiyo pekee inawapa wananchi ganzi, simanzi na kwa kweli inawafanya wakuchukie.

Na makada wa CHADEMA wanawaambia wananchi kwenye mikutano ya hadhara kuwa serikali yako inataka kumnyonga Lissu.

Kesi hii ndugu Rais, inawafanya watu wakuone kama huna moyo hivi. Tafadhali kabla ya haiba yako haijachafuka na watu kukuona mtawala katili, tafadhali ondoa hii kesi mahakamani.

Soma Pia: Tundu Lissu ashtakiwa kwa Uhaini, arudishwa rumande, kesi yake kusikilizwa Aprili 24, 2025

Tunapoelekea utaanza kuchukiwa na umma kama kipindi kile ulivyoendelea kumshikilia Mbowe gerezani, Kesi ile ilikuwa imekutoa ktk mioyo ya Watanzania sana na laiti ungeng'ang'ania kumshika Mbowe kwa muda mrefu zaidi, umma ungekuona kwa jicho negative sana. Sasa situation kama hiyo ninaiona sasa ambapo umma umeanza kukuangalia kwa jicho baya.

Ndugu Rais, Serikali yako inaongoza kwa kuwaweka wapinzani wa utawala wako jela. Ushanuweka Mbowe ndani kwa kesi ya Ugaidi, Ushamfungulia Dr Slaa, Mwabukusi na Mdude kesi ya Uhaini, na sasa Lissu serikali yako imemfungulia kesi ya uhaini. Wananchi wanasema unatumia mahakama kisiasa kupitiliza. Wanakuona kuwa huwezi kujibu hoja za wapinzani kwa hiyo badala yake unatumia msuli wa dola!.

Ndugu Rais ni kweli unaweza kumuweka Lissu jela na hata kumnyonga, lakini kiukweli hii dhana ya kumnyonga Lissu inaibua hisia nzito mno kwa wananchi huku mtaani na watu wanakuangalia vibaya sana.

Ujumbe nimekufikishia, utaamua mwenyewe serikali ifanye nini, Wananchi hawaamini kuwa mahakama inaweza kuwa huru kutenda haki kulingana na historia ya kesi hasa za hivi karibuni, kwa hiyo wananchi wanasema kuwa hii ngoma ni yako na si mahakama.

Kumnyonga Lissu kwa maoni yangu is not a good idea!.
Mjifunze kuzoea vifo.
 
wengi wamepewa elimu mbovu kwa hiyo wapo kama vipofu
Sasa ukiona mtu anamtake advantage kipofu halafu yupo ktk mtumbwi uleule ni hatari mno huko mbeleni
usifurahie ujingaujinga kwenye nchi, unaharibu mustakbali wa vizazi vyako
Furaha ipo wapi? Una uwezo wa kusoma na kuelewa? Una akili timamu?
 
Lisu anatumika na akili kubwa kumuondolea mtia nia uhalali wake wa kutia nia!!Ili mwingine wanaemtaka atie nia na kupewa!!

Game Kali sana hii inaeezekana hasta alieshauri kituko hiki na yeye alishauriwa na hajui kwanini alishauriwa!!!
 
Lissu hawezi kunyongwa kwa shtaka la kipuuzi namna ile. Wanachofanya ni kumnyoosha tu wakitegemea pia kuua morale ya wapinzani
 
Lissu hawezi kunyongwa kwa shtaka la kipuuzi namna ile. Wanachofanya ni kumnyoosha tu wakitegemea pia kuua morale ya wapinzani

Lissu is a dead man already. Huwezi kumnyoosha mtu aliyepigwa risasi 16 na kusurvive kwa kumuweka Jela. Labda kumnyonga mpaka afe.
 
Back
Top Bottom